Hotuba
- Feb 13, 2016
HOTUBA YA MHESHIMIWA DKT. JOHN POMBE JOSEPH MAGUFULI, RAIS WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA KWENYE MKUTANO NA WAZEE WA DAR ES SALAAM KWENYE UKUMBI WA DIAMOND...
Soma zaidiHotuba
Mheshimiwa Mzee Hemed Mkali, Mwenyekiti wa Wazee wa Mkoa wa Dar es Salaam;
Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan, Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania;
Mheshimiwa Kassim Majaliwa, Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania;
Mheshimiwa Dkt. Tulia Mwansasu, Naibu Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano;
Waheshimiwa Mawaziri mliopo;
Mheshimiwa Mecky Sadick, Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam;
Mwenyekiti wa CCM, Mkoa wa Dar es Salaam;
Waheshimiwa Viongozi wa Kamati ya Amani ya Mkoa wa Dar es Salaam;
Wazee wangu wa Mkoa wa Dar es Salaam;
Ndugu Wananchi, Mabibi na Mabwana:
Awali ya yote napenda kumshukuru Mwenyezi Mungu kwa kutukutanisha mahali hapa tukiwa salama. Aidha, napenda kukushukuru Mheshimiwa Mwenyekiti na Wazee wa Mkoa wa Dar es Salaam kwa kutukaribisha hapa ili tupate mawaidha yenu. Nina imani mawaidha yenu, hasa katika kipindi hiki ambapo tumemaliza siku mia moja tangu tumeingia madarakani, yatakuwa ni muongozo mzuri kwetu na kutupa sisi mwelekeo mzuri wa kufanya kazi kwa manufaa ya Watanzania wote.
Kabla sijaendelea, naomba pia, kupitia kwenu Wazee wa Dar es Salaam, kuwashukuru Watanzania wote, wa dini zote, wa vyama vyote, na makabila yote kwa kutuchagua kuwa viongozi wenu katika kipindi cha miaka mitano ijayo. Tuliwaahidi kipindi cha kampeni kuwa tutafanya kazi kwa bidii ili kujenga Tanzania mpya. Kwa niaba ya viongozi wenzangu, Makamu wa Rais, Waziri Mkuu, Mawaziri, Makatibu Wakuu na Manaibu Makatibu Wakuu napenda kuwahakikishia kuwa tutatimiza ahadi zetu tulizowaahidi na kamwe hatutawaangusha. Ninachoomba kutoka kwenu wazee wangu na Watanzania kwa ujumla mzidi kutuamini na kutuombea.
Mheshimiwa Mwenyekiti;
Mabibi na Mabwana;
Tangu Serikali ya Awamu ya Tano imeingia madarakani zimepita takriban siku mia moja. Mtakubaliana nami kuwa katika kipindi hicho, Serikali imechukua hatua mbalimbali za kuleta mabadiliko hapa nchini. Hatua hizo zimewagusa baadhi ya watu na kuwaumiza. Lakini napenda kuwahakikishia Watanzania wote kuwa hatua tulizozichukua na tunazoendelea kuzichukua ni za lazima kwa manufaa ya wananchi walio wengi.
Ninyi nyote mnafahamu kuwa nchi yetu hii sio masikini. Nchi yetu ina kila aina ya utajiri na neema. Tunayo ardhi ya kutosha, maji, misitu, madini nk. Kutokana na rasilimali tulizonazo, ni dhahiri kuwa hatupaswi kuwa na wanafunzi wanaokaa chini, wagonjwa kukosa vitanda, wananchi kukosa maji n.k. Lakini naomba mtambue kuwa tumefika hapa tulipo kwa sababu ya ubinafsi wa watu wachache wasio waaminifu na wabadhirifu wa rasilimali za nchi yetu. Rasilimali za nchi yetu zimekuwa zikitumiwa vibaya na watu wachache. Mifano ipo mingi, sio hapa Dar es Salaam tu bali sehemu nyingi nchini. Cha kusikitisha zaidi ni kwamba kwenye maeneo hayo wapo viongozi lakini hakuna hatua zinazochukuliwa.
Hivyo basi, napenda kuwahakikishia kuwa Serikali ya Awamu ya Tano imedhamiria kurekebisha hali hii. Hakuna mtu ambaye ametufikisha hapa tulipo atakayesalimika. Tutatumbua majipu yote na niseme tu kwa uhakika kabisa kuwa hatua hizi sio nguvu za soda bali zitakuwa ni endelevu. Ndio, ni lazima tuchukue hatua hizi.
Waasisi wa Taifa letu na ninyi wazee mkiongozwa na Baba wa Taifa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere na Mzee Abeid Amani Karume, mlipigania kupatikana kwa uhuru wa nchi yetu. Hivyo, ni jukumu letu sisi wa kizazi cha sasa kuleta maendeleo kwa taifa letu. Natoa wito kwa Watanzania wote kuendelea kuunga mkono juhudi zinazofanywa na Serikali za kutatua changamoto na kuleta maendeleo nchini mwetu.
Mheshimiwa Mwenyekiti;
Mabibi na Mabwana;
Kutokana na hatua tunazozichukua, tumeanza kupata mafanikio. Mafanikio hayo ni pamoja na kuimarisha ukusanyaji wa mapato kwa kudhibiti ukwepaji kodi. Mathalan, mwezi Novemba 2015 tulikusanya kiasi cha shilingi trilioni 1.3, mwezi Desemba 2015 shilingi trilioni 1.4 na mwezi Januari 2016 shilingi trilioni 1.06. Kabla ya hapo, wastani wa mapato yalikuwa yanakusanywa kwa mwezi ni shilingi bilioni 850. Kutokana na mapato kuongezeka, tumeanza kutekeleza miradi mbalimbali ya maendeleo na kuboresha huduma za jamii.
Tayari tumetoa kiasi cha shilingi bilioni 120 kwa ajili ya mradi wa wa umeme Kinyerezi II ambao unatekelezwa kwa ubia kati ya Serikali yetu na Japan. Serikali ya Japan inagharamia asilimia 85 ya mradi na nchi yetu ilitakiwa kuchangia asilimia 15. Serikali ya Japan ilikwisha toa kiasi cha Dola za Marekani milioni 292, hata hivyo, mradi huu ulikwama tangu mwaka 2012 kutokana na nchi yetu kushindwa kutoa mchango wa asilimia 15. Mradi huu ni muhimu na ukikamilika utaweza kuchangia takriban megawati 250 kwenye gridi ya taifa na hivyo kupunguza tatizo la umeme nchini. Utekelezaji wa mradi huu unatarajiwa kuanza wakati wowote mwezi ujao.
Sambamba na mradi huo wa umeme, hivi karibuni tunatarajia kuanza ujenzi wa miradi mbalimbali ya barabara hapa Dar es Salaam. Miradi hiyo ni pamoja na mradi wa Barabara za Juu (flyovers) ya TAZARA, ambao tutaweka jiwe la msingi mwezi Machi 2016. Miradi mingine ni pamoja na ujenzi wa Daraja kutoka Hospitali ya Aga Khan hadi Coco Beach; Barabara ya Rangi Tatu, ambayo Serikali ya Japan imekubali kufadhili, barabara ya interchange kwenye makutano ya Ubungo, ambayo Benki ya Dunia imekubali kutoa kiasi cha Dola za Marekani milioni 97. Aidha, katika kipindi hiki cha miaka mitano tunatarajia kukamilisha mradi mkubwa wa barabara ya njia sita kutoka Ubungo hadi Chalinze ambao utakuwa na flyovers saba. Sambamba na hilo, tumedhamiria kufufua shirika letu la ndege kwa kununua ndege mpya.
Mheshimiwa Mwenyekiti;
Mabibi na Mabwana;
Kuhusu uboreshaji wa huduma za jamii, Serikali imeanza kutekeleza ahadi yake ya kutoa elimu bila malipo kuanzia darasa la kwanza hadi kidato cha nne. Tunatoa kiasi cha Bilioni 18.77 kila mwezi ili kugharamia shughuli za uendeshaji, chakula cha wanafunzi wa shule za bweni, karo, fidia ya ada za mitihani na michango mingine iliyokuwepo.
Kutokana na uamuzi wa Serikali kutoa elimu bila malipo, takwimu za awali zinaonesha kuwa idadi ya uandikishaji wa wanafunzi wa darasa la kwanza mwaka huu umeongezeka maradufu. Hadi mwishoni mwa mwezi Januari, Mkoa wa Dar es Salaam pekee ulikuwa na ongezeko la wanafunzi takriban 10,129. Manispaa za Ilala na Temeke zimevuka lengo kwa kuandikisha wanafunzi wa darasa la kwanza. Ongezeko la idadi ya wanafunzi ni ishara kuwa ada na michango ilikuwa kikwazo kwa baadhi ya wazazi kuandikisha watoto wao elimu ya msingi. Hivyo, utaratibu huu wa kutoa elimu bila malipo umeleta unafuu mkubwa kwa wananchi wa kipato cha chini.
Wazee wangu wa Mkoa wa Dar es Salaam;
Mabibi na Mabwana;
Jambo lolote zuri halikosi changamoto. Hivyo, kama alivyoeleza Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam hivi punde, utekelezaji wa elimu bila malipo umesababisha changamoto kadhaa, ikiwemo upungufu wa madawati na vyumba vya madarasa. Napenda kutumia fursa hii kuwahakikishia wazee wangu wa Dar es Salaam changamoto hizi zote zilizojitokeza tutazitatua. Nawapongeza viongozi wa Mkoa wa Dar es Salaam na wananchi wengine wote waliojitolea kwa hali na mali kushirikiana na Serikali katika kutatua changamoto za utoaji wa elimu bure.
Katika kuunga mkono jitahada zinazofanywa na viongozi wa Mkoa wa Dar es Salaam, mimi na viongozi wenzangu tunaoishi hapa Dar es Salaam tumekubaliana kutoa kiasi cha shilingi milioni mia moja. Aidha, kwa mamlaka niliyo nayo ninaahidi kutoa kiasi cha shilingi bilioni mbili kwa ajili ya ujenzi wa shule hapa Dar es Salaam. Nawaagiza viongozi wa Mkoa kusimamia vizuri fedha hizo na zigawanywe kwenye wilaya zote za Mkoa wa Dar es Salaam, zikiwemo Wilaya mpya za Ubungo na Kigamboni.
Aidha, napenda kutumia fursa hii kuwahimiza viongozi wa Mikoa na Wilaya sehemu nyingine nchini kujipanga vizuri na kubuni mikakati ya kukabiliana na changamoto zilizopo. Uwezo wenu wa kukabiliana na changamoto hizi itakuwa ni kipimo tosha kufahamu kama mnatosha kwenye vyeo mnavyoshikilia. Lakini naomba kutoa angalizo kuwa, mikakati mtakayoibuni isilenge katika kuwalazimisha wananchi kuchangia. Michango iwe ya hiari kwa wale watakaoguswa.
Mheshimiwa Mwenyekiti;
Wazee wangu wa Mkoa wa Dar es Salaam;
Katika sekta ya afya, tumeimarisha utoaji huduma katika hospitali zetu kwa kuongeza upatikanaji wa madawa, kununua vifaa vya kisasa vya kuchunguza magonjwa kwenye hospitali zetu. Aidha, kwenye Hospitali ya Muhimbili tumenunua vitanda vipya. Lakini kama ilivyo kwenye sekta ya elimu, changamoto bado zipo.
Juzi nilifaya ziara ya ghafla kwenye Hospitali ya Muhimbili, hususan kwenye wodi ya akina mama ambapo nilikuta baadhi yao wakiwa wamelala chini. Kutokana na hali hiyo, nimeagiza, ikiwa ni moja ya hatua za muda mfupi, kwamba jengo lililokuwa Ofisi ya Kitengo cha Afya ya Uzazi na Mtoto litumike kwa ajili ya wodi ya kinamama. Aidha, naagiza kukamilishwa kwa haraka kwa ujenzi wa majengo mawili yaliyopo kwenye Hospitali ya Muhimbili. Moja ya majengo hayo ni lile linalojengwa na Kampuni ya Masasi Construction Co. Ltd kwa takriban miaka ishirini hivi sasa. Nimeagiza kuwa kama kinachokwamisha ujenzi ni fedha, basi zitafutwe haraka lakini kama tatizo ni mkandarasi, aondolewe mara moja.
Mheshimiwa Mwenyekiti;
Mabibi na Mabwana;
Kabla sijahitimisha hotuba yangu napenda kutumia fursa hii kueleza masuala matatu yafuatayo. Jambo la kwanza, leo mnatupima utendaji kazi wetu katika kipindi cha siku mia moja. Lakini nadhani ingekuwa vizuri zaidi kama kila mmoja wetu angejipima na kujitathimini ameifanyia nini Tanzania katika kipindi hicho. Mkulima ajipime, na vivyo hivyo kwa mfanyakazi, mfugaji, mvuvi, mfanyabiashara. Tanzania ni yetu sote hivyo kila mmoja wetu anao wajibu wa kuijenga. Binafsi naamini kama sote tutafanya kazi kwa bidii na kwa uadilifu, nchi yetu itapata maendeleo tena kwa haraka.
Hivyo basi, napenda kutumia fursa hii kutoa wito kwa viongozi katika ngazi zote Serikalini kuwahimiza wananchi kufanya kazi kwa bidii. Kwa bahati nzuri mwaka huu nchi yetu imepata mvua za kutosha hivyo sitamwelewa kiongozi ambaye baada ya kipindi cha mvua kumalizika, kulalamika kuhusu ukosefu wa chakula kwenye eneo lake. Kiongozi wa namna hiyo atakuwa amedhihirisha kuwa hatoshi kwenye nafasi anayoishikilia.
Sambamba na hilo, napenda kutumia fursa hii kuwahimiza wananchi kote nchini kulipa kodi. Hakuna nchi imeweza kuendelea hapa duniani wakati wananchi wake wanakwepa kulipa kodi. Bila kulipa kodi, mipango yote ya maendeleo na Tanzania mpya tunayoitamani itakuwa vigumu kuifikia. Niliahidi wakati wa Kampeni kuwa Serikali itatoa pensheni kwa wazee nchini, lakini azma hii nzuri itakuwa vigumu kuitekeleza endapo hatutafanya kazi kwa bidii na kulipa kodi. Hivyo, natoa wito kwa wananchi kudai risiti kila wanaponunua bidhaa mbalimbali. Kwa kufanya hivyo, mtakuwa mmeshiriki kwenye ujenzi wa nchi yetu.
Mheshimiwa Mwenyekiti;
Mabibi na Mabwana;
Jambo la pili ni kuhusu Mipango yetu ya Maendeleo ya Miaka Mitano. Azma kuu ya Serikali ya Awamu ya Tano ni kujenga uchumi wa viwanda ili kuchochea mageuzi ya kiuchumi na maendeleo ya wananchi. Viwanda tunavyolenga ni vile vinavyotumia malighafi zinazopatikana kwa wingi hapa nchini; vyenye kutumia teknolojia ya kati na nguvu kazi kubwa; na ambavyo bidhaa zake zitatumika kwa wingi hapa nchini.
Tayari tumeanza kuandaa mazingira wezeshi ya kufanikisha mipango hii yote kutekelezwa. Napenda kuwahimiza wafanyabiashara wote, hususan wafanyabiashara wa Kitanzania kutumia fursa zilizopo nchini kwa kushiriki kwenye ujenzi wa uchumi wa nchi yetu. Serikali ya awamu ya Tano itashirikiana nanyi kwa kuwa tunatambua Tanzania itajengwa na Watanzania wenyewe.
Mabibi na Mabwana;
Jambo la tatu na la mwisho linahusu kufutwa kwa matokeo ya uchaguzi wa Zanzibar. Kama mnavyofahamu, kwa mujibu wa Katiba ya Zanzibar na pia kulingana taratibu za utawala bora na wa kidemokrasia duniani kote, Tume ya Uchaguzi wa Zanzibar (ZEC) ni chombo huru. Hakuna mtu au taasisi yoyote yenye mamlaka ya kuingilia maamuzi ya ZEC. Hivi karibuni, kumekuwa na wito kutoka kwa watu mbalimbali kunitaka ningilie kati suala la uchaguzi wa Zanzibar. Mimi nimekataa kwa kuwa naheshimu sheria.
Naamini kuwa kama yupo mtu hakubaliani na maamuzi yaliyochukuliwa na ZEC, anapaswa kupeleka malalamiko yake Mahakamani ili kupata tafsiri sahihi ya sheria. Hivyo basi, narudia tena kuwa sitaingilia suala la Uchaguzi wa Zanzibar. Jukumu langu kubwa nikiwa Amiri Jeshi Mkuu ni kuhakikisha Zanzibar ipo salama na nchi yetu kwa ujumla inakuwa na amani. Nitasimamia jukumu hilo ipasavyo. Yeyote atakayefanya vitendo vya uvunjifu wa amani na usalama ajue kuwa vyombo vya ulinzi na usalama, vitamshughulikia.
Mheshimiwa Mwenyekiti;
Wahsehimiwa Viongozi mliopo;
Wazee wangu wa Mkoa wa Dar es Salaam;
Mabibi na Mabwana;
Napenda kuhitimisha hotuba yangu kwa kurudia ahadi yangu kuwa Serikali ya Awamu ya Tano imedhamira kuleta maendeleo kwa nchi yetu. Tumeazimia kutumia vizuri rasilimali tulizonazo ili kuondokana na changamoto zinazokabili nchi yetu, ikiwemo tatizo la umasikini kwa wananchi wetu. Natambua changamoto bado zipo nyingi lakini nawaahidi kuwa tutashirikiana kwa pamoja kuzitatua. Hapa Dar es Salaam pia kuna changamoto kadhaa, ikiwemo kivuko cha Kigamboni. Lakini nimefarijika kuwa Daraja la Kigamboni sasa limekamilika na litazinduliwa muda mfupi ujao.
Mwisho lakini sio kwa umuhimu, navishukuru vyombo vya ulinzi na usalama kwa kulinda mipaka yetu na kudumisha usalama wa raia na mali zao. Aidha, nawashukuru viongozi wa dini kwa kuendelea kuliombea taifa letu na hivyo kubaki katika amani. Navipongeza pia vyombo vya habari kwa kazi kubwa mnayoifanya ya kuhabarisha Watanzania kuhusu hatua mbalimbali ambazo Serikali inachukua. Hivyo ndivyo inapaswa kuwa badala ya kila wakati kujikita katika kuikosoa Serikali. Sisi tupo tayari kukosolewa na kupokea maoni yenu lakini katika kukosoa ni vyema tukakumbuka kuwa nchi hii ni yetu sote hivyo lolote litakalotokea litatuathiri sisi sote.
Mungu Wabariki Wazee wa Dar es Salaam
Mungu Ibariki Tanzania
“Ahsanteni kwa kunisikiliza”.
- Feb 08, 2016
Hotuba ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania iliyosomwa na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Kikanda na Kimataifa, Mhe. Dkt. Augus...
Soma zaidiHotuba
Honourable Dr. Suzan Kolimba, Deputy Minister for Foreign Affairs, East African, Regional and
International Cooperation,
Your Excellency Idzai Chimonyo, Ambassador of the Republic of Zimbabwe and Acting Dean of the
Diplomatic Corps,
Ambassador Ramadhan Mwinyi, Acting Permanent Secretary, Ministry of Foreign Affairs, East African, Regional and International Cooperation
Your Excellencies, Ambassadors and High Com- misioners,
Excellencies, Heads of International Organizations, Other Members of the Diplomatic Corps, Distinguished Guests,?Ladies and Gentlemen,
Welcoming Remarks
I am pleased to welcome you all to the State House this evening. I am very delighted, as it is my first time to host such an auspicious occasion as the 5th President of the United Republic of Tanzania. At the outset, I would like to thank God for his blessings throughout the year 2015, and for granting us this opportunity to meet today as we celebrate the New Year 2016.
Allow me belatedly, to extend to your Excellencies, your families, staff and leaders my warmest wishes for the New Year 2016. I know you are just back from the holiday season, in the months of December and January, I thank you for taking your time to attend this occasion. It is my great pleasure to welcome you together to the State House. Your presence here today of almost all of the envoys accredited to the United Republic of Tanzania reaffirms the good relations with your countries and the Organisations that you represent.
Excellencies, let me also convey through you my warm greetings and gratitude to your respective Heads of State and Government as well as Heads of Regional and International Organisations for the warm congratulatory messages that I have been receiving from them on my assumption of office. Although I have replied to them, through you I wish to once again reassure them of my friendship and cooperation of my Government and I look forward to continued cordial relations and partnership among our governments and citizens.On the occasion of this traditional diplomatic gathering, the President gets an opportunity to share with you some highlights of what transpired in the nation in the previous year, and to look forward on some of our priorities in the coming year. It is not yet too late in the month of February to restate our goals and marshal our energies and resources for achieving them.
Domestic Situation
Excellencies, as you all know, in October 2015 we held General Elections; and as witnessed by various observer groups, they were conducted in a fair, free and peaceful manner. The campaigns were intense, highly competitive yet peacefully conducted. There was a high voters turnout compared to previous elections with a visible participation of Women and young and new voters. Moreover, the tallying process was transparent assisted by the use of electronic means. The handing over of the administration for the fifth time in a row, was orderly and peaceful. This is a clear demonstration that Tanzania ’s democracy continues to grow and mature consistent with the unity, peace and stability of our country. At this point, I would like on behalf of the government to thank all those who supported us during the entire electoral process including the international observers who monitored the elections and affirmed its outcome on mainland Tanzania. Now that elections are over in the Mainland, it is time to work, as it was my motto during the election campaigns and now of my administration, “Its time to Work, Nothing Else” (Hapa Kazi Tu!). New governments come with new strengths, new thoughts, and new zeal and new zest. I count on your support in my efforts to transform and revi- talize the integrity of the government, respect of human rights, good performance and sustainable socio-economic change for the benefit of all Tanzanians. I should also at this forum reiterate Tanzania’s resolve to fight do- mestically and globally against international terrorism, drug and human trafficking as well as the spread of small arms and light weapons. We appeal to our partners to as- sist us especially in the areas of information sharing, ca- pacity building and technical support in these challenging areas.
Excellencies, I am sure most of you are expecting me also to speak about the difficult election outcomes in the Isles of Zanzibar. I do not have to remind you that although the United Republic of Tanzania is one country, Zanzibar has its own political system and tradition. It has its own constitution, government and an independent Electoral Commission. The Commission annulled the election results in Zanzibar following gross irregularities especially in Pemba. A new date has been set for fresh elections in accordance with the Zanzibar constitutional requirements. Dialogues has been going on since November 2015 among the main political parties without reaching a consensus on how to resolve the disputed election outcomes. The main opposition party is claiming unilateral victory from the October elections while the ruling party and other parties see the need for another round of elections.
Excellencies, in this situation, it is common political wisdom that such a political impasse or a non participation in the elections does not auger well for the peace and stability of Zanzibar. The door is still open for the dialogue on how to make the forthcoming elections free, fair and transparent according to internationally acceptable democratic practices. Refusal to participate in the elections is to reject an olive branch for compromise from the government and recipe for protracted political antagonism in the next five years. We urge, as the majority of Tanzanians do, for the opposition to validate their claims through the ballot box. There is no better way of resolving this impasse than through another round of free, fair and transparent elections. We hope all genuine friends of Zanzibar and Tanzania as a whole will support this option. Meanwhile, peace and tranquility is prevailing in Zanzibar. The peaceful status quo in Tanzania is too precious to be disturbed. It is not too late to find an agreeable solution in Zanzibar.
Excellencies, it would be remiss if I do not register my gratitudes to my predecessor, H.E. Jakaya Mrisho Kik- wete, for handing over to me a very stable country in all aspects with friends like you from all corners of the globe. Through his able leadership and of Chama cha Mapinduzi, the past five years has seen our economy growing at the average of 7 percent and we have witnessed encouraging progress in many socio economic sectors. We could not have done it by ourselves without your support. We appre- ciate your contribution. Please continue supporting and working with us particularly now that we have a very ambitious development plans for the betterment of all Tanzanians especially those lower echelons of soci- ety.
Excellencies, despite recorded achievements, we are still facing major hindrances on our way to achieving a prosperous Tanzania. Poverty, unemployment and corruption have remained to be among the major challenges confronting us. We are striving hard to over- come these challenges because we know that our vision of becoming a middle-income country by 2025 will not be reached if we do not address them compre- hensively. In our efforts to address these chal- lenges, among other things, we are working to reduce bu- reaucratic red tape and accelerate implementation of Gov- ernment’s decisions. We are also making efforts to re- duce Government spending; promote discipline, ac- countability and transparency in the Government and the public sector as a whole starting with revenue collec- tion as you have seen. We envision a corrupt free Tanzania and this can only succeed by working together at both national and international levels. We must fight both demand and supply side of corruption. On this note, I take this opportunity to appreciate and applaud the Government of the United Kingdom for taking the lead by returning the money taken corruptly from our country. It is only through such a genuine cooperation, commitment and partnership that we will be able to eliminate corruption in our countries.?
Excellencies, our emphasis in these five years is on ap- propriate industrial development. And again, to achieve this goal we are looking forward to working with you, our Development Partners, the private sector and other important stakeholders. My Government will continue to create a conducive environment for investors both from inside and outside the country. Help us to identify areas and gaps which need to be addressed in order create a more friendly investor climate in Tanzania. This will in turn accelerate economic growth of the country, reduce poverty, increase standard of living of our people and generate employment for Tanzanians, especially the youth.
Excellencies, my Government is also working to improve other key economic sectors such as education, health, agriculture, infrastructure and energy. Power generation, rural electrification and development of the central railway corridor will be among our major priorities. In terms of education, we have already embarked on providing free education for all from primary to secondary level. As I speak, we have already started to implement this and we will strive to extend it to other levels in coming years.
Excellencies, wildlife and forest conservation will receive urgent attention in the face of the alarming destruction of our wildlife and forests. We want to live up to our obliga- tion as custodians of wild heritage of our beautiful national parks and other historical and cultural attractions. Let me at this point again pay my deep condolences to the British Helicopter Pilot Roger Gower who tragically lost his life in Northern Tanzania while working with Tanzania’s authorities in the fights against illegal poaching of elephants in our national parks and game reserves. His life should not be lost in vein, I call upon all friends of Tanzania to join us in this war to save the BIG FIVE and other rare fauna and flora in the wilderness of Tanzania.
Regional Cooperation
Excellencies, my Administration will continue to build on the foundation of good relations laid down by my predecessors based on, among others, our Foreign Policy of good neighbourliness. Tanzania will continue to be committed to the regional bodies, and we will work with other members to uphold and advance the principles of the East African Community (EAC); the Southern African Development Community (SADC); the International Conference on the Great Lakes Region (ICGLR); as well as the African Union (AU). Undoubtedly, you have all been witnesses of our foreign policy being put in practice by assisting our neighbours in conflict resolutions as well as hosting refugees and asylum seekers. We will cooperate with fellow member countries to maintain peace, security, stability and development in our respective Regions.
Excellencies, now that we are embarking on industrial economy, we will endeavour to take advantage of the regional markets. My Government will intensify sensitization programmes to create awareness among the private sector and thus increase growth while stimulate production and businesses. We will continue to commit to the implementation of already concluded protocols in the region such as Free trade, Customs Union and Common Market.
Excellencies; as the current Chair of the East African Community, we have had to deal with the evolving political situation in Burundi, which is a concern not only to Tan- zania, but also to the Region, the whole continent and peace loving citizens of the world. Tanzania will continue to work closely with all stakeholders in searching for a peaceful and lasting solution to the Burundi crisis. We are of the view that in order to achieve sustainable peace and security in Burundi, inclusive dialogue is the only solution. Tanzania has reservations the use of force at this stage in dealing with the current political crisis without the consent of Burundi. We are at the same time encouraging dialogue between Burundi and the African Union because Burundi has genuine security concerns which require support from the Arican Union and the international community. It is in this spirit that we applaud the concerted efforts by H.E. Yoweri Museveni, President of the Republic of Uganda who on behalf of the East African Community is a mediator of this conflict. We are concerned that a festering political crisis in Burundi will exacerbate an already difficult economic situation in Burundi which can easily lead to institutional stress with dire security consequences in Burundi and the region as a whole. International Cooperation
Excellencies, 2015 was a very eventful year for the international community. Among other events, we celebrated 7 decades of our noble organisation the United Nations. In the same year, we also winded up the implementation of the Millennium Development Goals (MDGs) which Tanzania achieved four of them and subsequently, led to the adoption of the Agenda 2030 for Sustainable Development.
Excellencies, Tanzania will continue to participate in the United Nations and African Union peace keeping operations as her contribution to the maintenance of international and regional peace and security. Tanzania has a long history of generous hosting of Refugees long before independence. We pledge to respect this international humanitarian obligation. We appeal for equally generous international burden sharing on this issue especially as refugee hosting comes with numerous demographic, environmental, economic and social challenges to the countries of asylum like Tanzania. As you may recall, in December 2015 the global leaders adopted a historic agreement- The Paris Agreement, in Paris. This Agreement will take over from the Kyoto Protocol in 2020 and will decide the future of our Planet.
We, as Member Countries must ensure that we adhere to these agreements. There has to be a close follow-up and review mechanism of these new global Agreements and Goals so as to be sure of their successful implementation. My Government has plans in place to ensure that this takes place effectively. But we know that we cannot achieve any of these without our joint efforts, we therefore once again urge for your cooperation and necessary sup- port in these endeavours.
Conclusion
Excellencies, before I conclude, I would like to emphasise the role of women in development of the country and Tan- zania will continue to do its best so that women continue to be part and parcel of our development endeavours. We have shown this by electing our first ever-female Vice President, H.E. Mama Samia Suluhu Hassan. My Government will also continue to empower each Tanzan- ian so that no one will be left behind as pledged in the Agenda 2030 for Sustainable Development. In the same vein, every individual has to play their role in ensuring that we achieve our goals.
Your Excellencies, Ladies and Gentlemen, for the year 2016, I promise you my Government’s full cooperation and I look forward to working with you.
I thank you.
- Nov 20, 2015
Hotuba ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. John Pombe Joseph Magufuli, akifungua rasmi Bunge jipya la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, D...
Soma zaidiHotuba
Mheshimiwa Spika;
Niko hapa leo kutimiza matakwa ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Ibara ya 91 Ibara ndogo ya kwanza inayonitaka kulihutubia na kulifungua rasmi Bunge hili. Naomba nimshukuru Mwenyezi Mungu kwa kutujalia uzima na afya njema, na kutuwezesha kuwepo hapa siku ya leo. Aidha nitumie fursa hii kuwakumbuka wenzetu ambao, kwa namna na nafasi mbalimbali, walishiriki katika mchakato wa uchaguzi huu na kwa bahati mbaya walipoteza maisha yao kabla ya mchakato haujakamilika. Kwa hao wote waliotangulia mbele za haki ninamuomba Mwenyezi Mungu azirehemu roho zao na awape pumziko la amani. Nitumie nafasi hii kuwapa pole ndugu na jamaa ambao ndugu zao walifariki na wengine kupata ulemavu wakati wa mchakato wa uchaguzi huu.
Pia natoa pongezi kwako wewe Mheshimiwa Spika, Job Ndugai na Mheshimiwa Naibu Spika, Dkt. Ackson Tulia kwa kuchaguliwa kwenu kuongoza Bunge letu la 11. Waheshimiwa Wabunge wamewapa imani yao, na mimi kwa nafasi yangu nawahakikishia imani na matumaini yangu makubwa kwenu. Sina shaka Mheshimiwa Spika, chini ya uongozi wako Bunge letu limepata kiongozi mahiri, makini na mweledi.
Aidha, niwapongeze Wabunge wote kwa kuchaguliwa kuwa wabunge wa Bunge hili la 11. Aidha, nitumie nafasi hii kuwapongeza wale wote waliochaguliwa katika nafasi za udiwani katika kata mbalimbali kote nchini. Natoa pongezi hizi kwa dhati kabisa kabisa kwa sababu kuu mbili:
- Kwanza, ni kwa sababu ushindani katika uchaguzi wa mwaka huu ulikuwa ni mkubwa sana kuanzia ndani ya vyama vyetu na baadae katika Uchaguzi Mkuu uliohusisha na kushindanisha wagombea toka vyama tofauti.
- Pili, nawapongeza kwa sababu wananchi wamewapa imani na ridhaa ya kuwawakilisha katika kipindi ambacho matarajio yao kwa Awamu ya Tano ya uongozi wa nchi yetu ni makubwa sana. Watatupima kwa namna tutakavyokidhi kiu na matarajio yao. Sote tuliahidi kuwatumikia wananchi, na kutokana na utumishi wetu kwao tuweze kutatua matatizo yao mbalimbali, na kuongoza mabadiliko makubwa ya kiutendaji, usimamizi wa matumizi ya mali za umma na rasilimali za taifa, na ugawaji wa rasilimali hizo kwa haki. Mimi na Mheshimiwa Samia Suluhu, Makamu wa Rais tuliwaahidi wananchi kuwa tutawatumikia na tutahakikisha kuwa katika utumishi wetu tutawajali wananchi wote, lakini zaidi wananchi wa kawaida. Naamini wenzangu pia ndicho mlichoahidi na daima tukumbuke kuwa kazi zetu na mipango yetu yote tutakayoipanga na kuisimamia italenga katika kuwanufaisha watu wetu.
Mheshimiwa Spika;
Niwahakikishie tu wananchi kuwa mambo tuliyowaahidi tutayatekeleza. Sikusudii kurejea mambo yote niliyoahidi katika hotuba yangu hii ya leo, lakini nataka niwatoe wasiwasi kabisa kwamba tuliyoahidi tumeahidi na ahadi ni deni. Nataka Wananchi mniamini kuwa sikutoa ahadi ili tu mnipigie kura, niliahidi kuwatumikia na kuwafanyia kazi, na hicho ndicho nitakachofanya. Ni imani yangu kwamba Waheshimiwa Wabunge na Madiwani pia watafanya hivyo hivyo kama tutakavyofanya sisi.
Napenda pia kutoa shukrani zangu za dhati kabisa kwa Watanzania wote. Tulijiandikisha kwa wingi sana kwa ajili ya kupiga kura, tulishiriki na kufuatilia kwa karibu sana kampeni za uchaguzi, na tukajitokeza kwa wingi siku ya kupiga kura. Kinyume na ilivyotabiriwa na wasio tutakia mema hakuna siku iliyokuwa na utulivu mkubwa na amani kama siku ya tarehe 25 Oktoba tulivyokwenda kupiga kura. Hata baada ya matokeo kuanza kutangazwa tulionyesha utulivu mkubwa, na hata pale ambapo matokeo yalipotangazwa na yakawa sivyo baadhi yetu walivyoyatarajia bado tuliyapokea kwa hali ya utulivu na uungwana mkubwa.
Wale waliotarajia kuwa tutafarakana wameondoka wakiwa wamefadhaika sana huku wakijiuliza hivi hawa Watanzania ni Waafrika wa namna gani. Ndugu zangu Watanzania, kwa mara nyingine tena tumedhihirisha, kwetu sisi wenyewe, kwa Afrika na dunia, kwamba sisi ni kisiwa cha Amani katika bahari iliyochafuka. Tunayo haja ya kujipongeza na kujiwekea nadhiri kuwa tuaendelea kuidumisha hali hii na kuilinda amani ya nchi yetu. Ombi langu kwa vyama vya siasa, wanasiasa wa vyama vyote na viongozi wa dini ni kutimiza wajibu wetu wa kuilea amani ya nchi yetu.
Aidha, napenda niungane na ninyi pamoja na Watanzania wote kuvipongeza vyombo vyetu vya Ulinzi na Usalama (Jeshi la Wananchi Tanzania (JWTZ), Polisi, Magereza, Uhamiaji na Usalama wa Taifa pamoja na mgambo) kwa jinsi walivyoshiriki katika kuhakikisha nchi yetu inaendelea kuwa salama katika kipindi chote cha uchaguzi.
Nawapongeza pia Tume ya Taifa ya Uchaguzi kwa namna walivyosimamia zoezi zima la uchaguzi toka hatua za awali za kujiandikisha hadi siku ya kupiga kura na kutangaza matokeo. Mmetimiza wajibu wenu kwa weledi na umahiri mkubwa katika mazingira magumu na yenye changamoto nyingi. Hongereni, hongereni sana!
Mheshimiwa Spika;
Naomba kwa namna ya pekee, niwashukuru viongozi wakuu wa nchi yetu walionitangulia kwa kazi kubwa na nzuri walioifanyia nchi yetu. Natambua mchango wa Waasisi wa taifa letu, Mwalimu Nyerere na Mzee Karume kwa kujenga misingi imara wa umoja, mshikamano na amani ya nchi yetu. Mzee Mwinyi (Mzee Ruksa) kwa kuleta mabadiliko ya kiuchumi na kisiasa na kuijenga misingi yake. Mzee Mkapa (Mzee wa Ukweli na Uwazi) kwa kupanua na kuimarisha misingi ya uchumi na siasa ya nchi yetu. Mzee Kikwete (Mzee wa Maisha Bora) kwa kuendeleza misingi hiyo na kupanua fursa mbalimbali kwa wananchi kujiletea maendeleo yao. Wamefanya kazi kubwa. Nawashukuru sana na ninawatakia uzee mwema na maisha marefu ili tuzidi kuchuma busara zao.
Mhishimiwa Spika;
Tumeingia kwenye uchaguzi wamoja, tumeshindana katika kampeni tukiwa wamoja, na tumemaliza uchaguzi wetu tukiwa wamoja. Nataka niwahakikishie Waheshimiwa Wabunge na Watanzania kwa ujumla kwamba Serikali ya Awamu ya Tano itaendelea kulinda kwa nguvu na uwezo wote Tunu hizi za Umoja na Amani. Hatutakuwa na simile kwa mtu au kikundi chochote ambacho kitataka kuvuruga umoja na amani yetu kwa misingi ya udini, rangi, ukabila, vyama au ukanda.
Mheshimiwa Spika;
Wakati wa kampeni, yako maeneo yaliyojitokeza kwa kulalamikiwa sana na wananchi. Ningependa niyataje baadhi ya maeneo yaliyolalamikiwa, maeneo hayo ni pamoja na:
- Rushwa - Suala la rushwa limelalamikiwa sana takriban katika maeneo yote yanayogusa wananchi.
- TAMISEMI - Upotevu wa mapato, kushindwa kukusanya kodi, ubadhirifu, matumizi mabaya ya fedha na utekelezaji wa baadhi ya miradi chini ya viwango, wizi, uzembe, n.k.;
- Ardhi – Migogoro ya wakulima na wafugaji, viwanja, kuhodhi maeneo bila kuyaendeleza, mipango miji, kujenga maeneo ya wazi, n.k.;
- Bandari - Rushwa, wizi, ubadhirifu na urasimu;
- Maji – Kiwango cha chini cha upatikanaji wa maji safi na salama, huduma ya maji kupatikana mbali na makazi, n.k.;
- TRA - Ukwepaji kodi, rushwa, ubadhirifu, urasimu na upotevu wa mapato kwa kushindwa kukusanya kodi hasa kodi zinazotakiwa kulipwa na wafanyabishara wakubwa;
- TANESCO - Kukatika kwa umeme mara kwa mara na uwepo wa umeme wa mgao;
- Maliasili na Utalii - Ujangili ambao lazima Idara husika inashiriki, Migogoro ya mipaka kati ya vijiji na Hifadhi, Upotevu wa mapato, n.k.;
- Huduma za Afya (Hospitali) - Huduma kuwa mbali na wahitaji, Ukosefu wa madawa, hujuma kwenye vifaa vya vipimo, msongamano wa wagonjwa na tozo zisizostahili, lugha mbaya za watumishi kwa wagonjwa, uhaba wa majengo, vitendea kazi, rasilimali watu na fedha, kushindwa kukusanya mapato yanayowahusu, n.k.;
- Uhamiaji na Ajira - Kutoa hovyo hati za uraia, Vibali vya kuishi nchini kwa wageni, Kushindwa kusimamia ajira za wageni hususan kwa kazi zinazoweza kufanywa na wazawa, n.k.;
- Elimu - Uhaba wa vifaa vya kujifunzia na kufundishia, michango mingi isiyo ya lazima, malalamiko ya walimu yasiyoisha, mazingira ya kusomea ikiwa ni pamoja na majengo, Madawati, Ukosefu wa nyumba za walimu, n.k.;
- Polisi - Malalamiko ya wananchi kubambikiwa kesi, upendeleo, Madai ya askari, Ukosefu wa nyumba za askari, Ukosefu wa vitendea kazi vya kisasa, n.k.;
- Zimamoto – Kuchelewa kufika kwenye matukio, kufika kwenye matukio bila vitendea kazi kama maji, n.k.;
- Mizani – kucheleweshwa kwa magari yanayosafiri;
- Mahakama - Natambua jitihada za Mahakama katika kushughulikia swala la mrundikano wa kesi. Hata hivyo, bado kumekuwa na malalamiko mengi juu ya ucheleweshaji wa kesi.
- Madini – Wenyeji kutofaidika, Vilio vya wachimbaji wadogowadogo kutengewa maeneo ya uchimbaji na kupatiwa mikopo, kutolipa kodi stahiki, usumbufu kulipa fidia, n.k;
- Kilimo na Mifugo – Uhaba wa pembejeo za mifugo na kilimo, Tatizo la masoko, Kukopwa mazao ya wakulima, Ukosefu wa Wataalamu wa Ugani, Upungufu wa Maghala, Mabwawa, Malambo, Majosho, n.k.;
- Uvuvi – Vifaa duni na masoko, Uvuvi haramu, Uwekezaji mdogo katika Sekta ya Uvuvi hususan viwanda vya mazao ya uvuvi n.k., na hasa katika ukanda wetu wa bahari;
- Reli – Uchakavu wa miundombinu ya nchi, Kutokuwepo kwa usafiri wa uhakika wa reli, upungufu wa bandari kavu, Mizigo mingi kusafirishwa kwa barabara, n.k.;
- ATC – Shirika la Ndege lipo, Wafanyakazi wapo zaidi ya 200, na wanalipwa mishahara ila ndege ni moja (1);
- Makundi Maalum – Haki za wazee, Walemavu, Wanawake na watoto zimekuwa zikikiukwa;
- Wafanyakazi, Wasanii na Wanamichezo – Mzigo wa kodi kwa wafanyakazi, Haki na maslahi yao, n.k.;
Kero hizi tutazishughulikia kwa nguvu zetu zote. Wizara, Ofisi na Taasisi husika zijipange ipasavyo kutatua kero hizi. Nimetaja baadhi ya kero hizi ili nanyi Waheshimiwa Wabunge mzitambue na mshirikiane na Serikali na wadau wengine tuzitatue haraka.
Pamoja na kero hizo tutashughulikia pia mambo yafuatayo.
Kuimarisha Muungano
Mheshimiwa Spika;
Nilipoapa kuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, niliapa kuulinda Muungano wa nchi yetu. Hata bila kiapo, mimi ni muumini wa dhati wa Muungano wetu wa kipekee, uliounganisha nchi mbili zilizokuwa huru za Jamhuri ya Tanganyika na Jamhuri ya Watu wa Zanzibar, tena kwa hiari na kwa wino wa kalamu, na si mtutu kama miungano mingine duniani. Naamini kwa dhati ya moyo wangu kuwa Muungano wetu ndio umoja wetu, amani yetu na salama yetu. Ninayo kila sababu ya kuulinda na kuuenzi Muungano wetu adhimu na adimu. Ni azma yangu kuwaona wananchi wa Zanzibar na Bara wakifurahia matunda ya Muungano wetu badala ya kuwa kikwazo kwa ustawi wao na ustawi wa nchi yetu.
Aidha, kwa kushirikiana na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar na wadau wa siasa hususan vyama vya CUF na CCM tutahakikisha kuwa majaribu ya kisiasa yanayoikabili Zanzibar yanamalizika kwa salama na amani. Tunamuomba Mwenyezi Mungu atujalie busara na hekima tumalize kwa utulivu na amani.
Serikali nitakayoiunda itafanya kila lililo ndani ya uwezo wake kuendelea kuimarisha Muungano wetu. Nina faraja kuwa Mheshimiwa Samia Suluhu, Makamu wa Rais anao uzoefu mkubwa kutokana na nafasi yake ya awali ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais anayeshughulikia Muungano, na pia akiwa Makamu Mwenyekiti wa Bunge la Katiba. Mimi pamoja na Makamu wa Rais, Mama Samia Suluhu na Rais wa Zanzibar, Dkt. Ali Mohamed Shein tutahakikisha tunasimamia na kuimarisha Muungano wetu.
Kuimarisha Mihimili ya Serikali
Mheshimiwa Spika;
Serikali ya Awamu ya Tano itaheshimu na kuendeleza utamaduni mzuri uliojengeka nchini wa kuheshimu mihimili ya dola. Tutafanya hivyo kwa kuhakikisha kuwa mihimili yetu ya Bunge na Mahakama inapata fedha za kutosha kuendesha shughuli zake kwa uhuru kupitia Mfuko wa Bunge na Mfuko wa Mahakama. Kwa upande wa Bunge, tutahakikisha fedha za Mfuko wa Maendeleo ya Jimbo zinapatikana kwa wakati ili Waheshimiwa Wabunge mkashirikiane na wananchi wenu kusukuma maendeleo. Kwa upande wa Mahakama, tutalipa uzito mkubwa suala la uboreshaji wa Mahakama kwa kusogeza huduma za Mahakama karibu na wananchi, kuongeza kasi ya utoaji haki na kuboresha maslahi ya watumishi wa Mahakama zetu.
Mchakato wa Katiba
Mheshimiwa Spika;
Serikali yangu imepokea kiporo cha mchakato wa Katiba ambao haukuweza kukamilika katika Awamu iliyopita kutokana na kutokukamilika kwa wakati kwa zoezi la uandikishaji wapiga kura. Napenda kuwahakikishia kuwa tunatambua na kuthamini kazi kubwa ya kizalendo iliyofanywa na wananchi walioshiriki hatua ya awali ya ukusanyaji wa maoni kuhusu Katiba mpya, Tume ya Marekebisho ya Katiba na Bunge la Katiba lililotupatia Katiba Inayopendekezwa. Tutatekeleza wajibu wetu kama ulivyoainishwa katika Sheria ya Marekebisho ya Katiba.
Uchumi na Matarajio ya Wananchi
Mheshimiwa Spika;
Serikali ya Awamu ya Tano inaingia madarakani kukiwa na msingi imara wa kiuchumi uliojengwa katika Awamu inayomaliza muda wake. Uchumi wa nchi yetu umekuwa ukiimarika na kukua wastani wa asilimia 7. Katika kipindi hicho fursa mbalimbali za kiuchumi zilizopo nchini mwetu zimezidi kufunguliwa. Hii ni kutokana na jitihada zilizofanywa na Serikali za Awamu zilizopita za kujenga miundombinu ya kiuchumi kama vile barabara, uimarishaji wa bandari, uimarishaji wa reli, na ukuzaji wa sekta za mawasiliano ya simu na mitandao, ukuzaji na uongezaji wa uwezo wetu wa kuzalisha na kusambaza umeme.
Napenda kuwahakikishia kuwa tutaendeleza na kuimarisha ujenzi wa miundombinu mipya na kuiimarisha iliyopo ili kuvutia na kushawishi wawekezaji wa ndani na wa nje.
Mheshimiwa Spika;
Nasema hivi kwa sababu miongoni mwa ahadi tulizowaahidi Watanzania ni kuendeleza ujenzi wa barabara mbalimbali za kuunganisha miji yetu mikuu ya mikoa na wilaya; barabara ziendazo kwenye maeneo muhimu ya kimkakati na kiuchumi; na upanuaji wa barabara za miji kama Dar es Salaam kwa kujenga flyovers, barabara za pete (ring roads), n.k. Uboreshaji wa barabara na njia nyingine za uchukuzi na usafirishaji kuingia na kutoka Dar es Salaam ni muhimu sana kwa sababu bandari ya Dar es salaam ni lango kuu la biashara kwa nchi yetu na nchi jirani.
Mheshimiwa Spika;
Katika jitihada hizo hizo za kuboresha na kuimarisha miundombinu ya kiuchumi Serikali ya Awamu ya Tano, katika kipindi cha miaka mitano ijayo itaelekeza nguvu zake katika ujenzi wa reli mpya katika kiwango cha kimataifa (yaani standard gauge). Reli ambazo tunakusudia zianze kujengwa ni:
- Dar es Salaam – Tabora – Kigoma/Mwanza
- Uvinza – Msongati (Burundi) na Isaka – Kigali (Rwanda)
- Mtwara – Songea – Mbamba Bay na matawi ya kwenda Mchuchuma na Liganga;
- Tanga – Arusha – Musoma
- Kaliua – Mpanda – Karema
Mheshimiwa Spika;
Nchi yetu pia imejaliwa kuwa na madini na maliasili nyingi. Ugunduzi wa gesi asilia umeongeza matumaini ya watu wetu wengi juu ya uwezo wetu wa kiuchumi katika miaka ijayo. Serikali itahakikisha kwamba madini na maliasili zetu zinatumika kwa manufaa ya Taifa letu kwa kusimamia Sheria na Taratibu zilizopo. Aidha, napenda kuipongeza kwa dhati kabisa Serikali ya Rais Jakaya Mrisho Kikwete na Bunge la 10 kwa kupitisha Sheria ya Usimamizi wa Mapato ya Mafuta na Gesi yaani The Oil and Gas Revenues Management Act, 2015. Serikali yangu itasimamia utekelezaji wa sheria hiyo kwa uaminifu na umakini mkubwa.
Ujenzi wa Viwanda
Mheshimiwa Spika;
Serikali ya Awamu ya Tano itaweka mkazo mkubwa katika ujenzi wa Viwanda. Natambua kwamba sekta binafsi ndiyo muhimili mkubwa wa kujenga uchumi wa viwanda. Hatuna njia nyingine kama kweli tunataka kujenga msingi wa uchumi endelevu katika nchi yetu utakaopaisha uchumi na maisha ya watu wetu. Dira ya Maendeleo ya 2025 inatutaka tuwe nchi ya watu wenye kipato cha kati. Tunaweza tukafika huko, na dalili zipo, lakini pia tunaweza tukafika huko kitakwimu tu wakati ukweli na uhalisia wa mambo ni tofauti. Utofauti ninaouzungumzia ni pale takwimu zitakapoonyesha kwamba sisi ni nchi ya kipato cha kati wakati mapato halisi na hali za maisha ya watu wengi hazifanani na takwimu hizo. Tamaa yangu na kwa kweli jitihada za Serikali ya Awamu ya Tano, zitakuwa katika ujenzi wa uchumi wa kipato cha kati ambapo sura na maisha ya Watanzania walio wengi yafanane fanane na nchi ya kipato cha kati. Njia moja ya kutufikisha huko ni uendelezaji wa viwanda.
Mheshimiwa Spika;
Tutahakikisha suala la viwanda linasimamiwa vizuri na tunafanikiwa. Matarajio yangu ni kuwa Bunge lako Tukufu litatuunga mkono mimi na Serikali nitakayoiunda katika kufikia lengo hili.
Mheshimiwa Spika;
Kama nilivyosema wakati wa Kampeni, na nataka nirudie hapa, tutaanza na viwanda vilivyopo na kuhakikisha vinafanya kazi. Wale wote ambao walibinafsishiwa viwanda vilivyokuwa vya umma kwa makubaliano kwamba wataviendeleza niliwataka wafanye hivyo mapema. Na hapa nataka nisisitize wito wangu huo kwao. Najua huko nyuma ufuatiliaji na usimamizi wa utekelezaji wa mikataba ya aina hiyo umekuwa ukilegalega na watu wamejifanyia mambo watakavyo. Wapo walioacha kabisa uzalishaji na kufumua hata mitambo ya uzalishaji. Mimi niliahidi, na nataka niseme hapa kwa wazi kabisa, kwamba wale waliobinafsishiwa viwanda hivyo waanze kazi, waanze kazi mara moja. Wakishindwa basi tutavitwaa viwanda hivyo kwa kuzingatia sheria na taratibu za nchi na kuwapa watu wengine wenye nia ya kuviendeleza. Hatuwezi kuwa na watu wanajiita wawekezaji tunawapa viwanda vyetu halafu wanaviatamia tu. Mimi hilo sitalikubali na wala sitalivumilia. Nimeielekeza Ofisi ya Msajili wa Hazina kuanza kushughulikia suala hili mara moja. Naomba Bunge lako lituunge mkono.
Mheshimiwa Spika;
Njia ya pili ya kuendeleza viwanda ni kuhimiza na kushawishi wawekezaji kuwekeza katika maeneo mbalimbali ya nchi yetu. Kama nilivyoeleza miundombinu ya kufanya hivyo tayari ipo na baada ya muda itakuwa bora zaidi. Najua wapo watu wanaotaka kuwekeza Tanzania sasa, katika viwanda, na wamekuwepo hata miaka ya nyuma kidogo, lakini wakati mwingine sisi humu humu – tukiwemo sisi viongozi kwa kushirikiana na wafanyabiashara matapeli na laghai – tumehujumu mipango na shauku ya wawekezaji wa nanma hiyo. Pamoja na shauku na utayari wao wa kuwekeza Tanzania tumewawekea vikwazo na kuwapiga vita na hivyo kuwalazimisha kwenda kuwekeza katika nchi jirani. Sisi katika Serikali ya Awamu ya Tano tutajitahidi sana kuondoa usumbufu na urasimu wa aina hiyo na kuongeza bidii ya kuwashawishi wawekezaji wa ndani na wa nje kuja kuwekeza viwanda hapa nchini. Kwa watendaji wa Serikali watakaokwamisha jitihada za uwekezaji na ujenzi wa viwanda hapa nchini hatutawavumilia.
Mheshimiwa Spika;
Ni viwanda vya aina ipi hasa tunavyovikusudia? Sura ya kwanza ya viwanda tunavyovikusudia ni vile ambavyo sehemu kubwa ya malighafi yake itatoka ndani, hususan kweye sekta za kilimo, mifugo, uvuvi, na madini – na maliasili nyingine. Viwanda vya aina hii vitatupa fursa ya kujenga mfumo wa uzalishaji ndani ya nchi uliofungamana na kushikamana. Viwanda vya aina hii vitahitaji na kutegemea malighafi toka kwa wazalishaji wa sekta nilizozitaja, na kwa kufanya hivyo wazalishaji hao watakuwa na soko la uhakika humu humu ndani ya nchi. Sura ya pili ya viwanda hivi ni kuzalisha bidhaa ambazo zinatumiwa na watu wengi humu nchini (mass consumption) – yaani bidhaa kama vile nguo, viatu, mafuta ya kupikia, n.k. kwa hivyo viwanda hivi vitakuwa na uhakika wa soko la ndani kabla ya kufikiria soko la nje. Viwanda hivi vitatarajiwa kuzalisha ziada kwa ajili ya masoko ya nje. Yote mawili yakitokea, yaani kuzalisha kwa ajili ya soko la ndani na nje, itatuongezea akiba yetu ya fedha za kigeni na kutuwezesha kutekeleza na kuendeleza mipango mingine kwa ajili ya ustawi wa uchumi wetu. Sura ya tatu ya viwanda tunavyovikusudia ni kuzalisha ajira nyingi. Shabaha yetu ni kuwa ifikapo mwaka 2020 idadi ya ajira itokanayo na viwanda ifikie asilimia 40 ya ajira zote zitakazokuwepo nchini wakati huo.
Mheshimiwa Spika;
Nimeamua kulisema hili kwa kirefu sana kwa sababu ili tufanikiwe lazima tuelewane na tusaidiane kulisukuma kwa pamoja jambo hili.
Kilimo, Mifugo na Uvuvi
Mheshimiwa Spika;
Sekta nyingine ambazo lazima tutazitilia mkazo mkubwa na kuziendeleza ni kilimo, mifugo na uvuvi. Tutaziangalia sekta hizi kwa mtazamo wa kibiashara na viwanda kwa lengo la kuwa na viwanda vya kisasa vya kuongeza thamani mazao yatokanayo na kilimo, mifugo na uvuvi. Nchi yetu kwa kiasi kikubwa ni nchi ya kilimo, ufugaji na uvuvi. Hii inatokana na ukweli kwamba sehemu kubwa ya watu wetu wapatao asilimia 75 wanaishi vijijini na wanategemea kilimo, ufugaji na uvuvi kwa ajili ya maisha yao. Wakulima, wafugaji na wavuvi wanatumia zana na mbinu duni katika shughuli zao na wanazalisha zaidi ya asilimia 95 ya chakula chote kinacholiwa hapa nchini, na kutoa mchango wa asilimia 25 kwenye pato la taifa yaani GDP, na asilimia 30 ya mapato yetu ya fedha za kigeni. Kwa takwimu hizi chache ni wazi kwamba mchango wa sekta ya kilimo, mifugo na uvuvi katika uchumi wetu na maisha yetu ni mkubwa sana. Nichukue nafasi hii kuwapongeza na kuwashukuru wakulima, wafugaji na wavuvi wote wa Tanzania kwa mchango wao mkubwa katika maisha yetu na uchumi wa nchi yetu. Nataka kuahidi kwao sitawaangusha.
Mheshimiwa Spika;
Pamoja na umuhimu wa kilimo, mifugo na uvuvi katika uchumi wetu wakulima, wafugaji na wavuvi wetu wengi bado ni watu maskini. Mapato yao yako chini na wanaishi maisha duni. Lengo letu ni kuuimarisha sekta hizi ili ziweze kutoa mchango mkubwa zaidi katika uchumi wa nchi lakini pia ziweze kuwanufaisha wakulima, wafugaji na wavuvi katika kuyabadili maisha yao. Tukiweza kuboresha sekta hizi vijana wengi zaidi watavutiwa kujiunga nazo na hivyo kupunguza tatizo la upatikanaji wa ajira. Nataka niwahakikishie wakulima, wafugaji na wavuvi wetu kwamba ahadi zetu kwao tutahakikisha zinatekelezwa. Serikali ya Awamu ya Tano itazisimamia kwa dhati ahadi hizo ili kuhakikisha kwamba kilimo, ufugaji na uvuvi unakuwa wa kisasa zaidi na wenye tija. Baadhi ya mambo tuliyowaahidi kuyatekeleza ni pamoja na haya yafuatayo:
- Kuwapatia mafunzo ya kilimo, ufugaji na uvuvi wa kisasa ikiwa pamoja na ufugaji wa samaki,
- Kuwapatia pembejeo,
- Kuwapatia zana za kisasa za kilimo, ufugaji na uvuvi,
- Kuwapatia wataalamu wa ugani,
- Kuwawezesha kupata masoko ya uhakika ya mazao yao,
- Kuwapatia mikopo, na kwa hili Benki ya Kilimo itasaidia sana kufikia lengo hili,
- Kuondoa ushuru, kodi na kero mbalimbali za mazao ya kilimo, mifugo na uvuvi zinazosababisha bei ya mazao hayo kuwa chini (mfano. Kahawa, kule Kagera ina kodi 26 ambazo husababisha wananchi kuuza kahawa yao Uganda ambako bei iko juu, tutapunguza kama sio kuondoa kabisa ushuru hizo ili wakulima wapate bei nzuri. Tutafanya hivyo pia kwa mazao mengine kama mahindi, chai, pamba, korosho, mkonge, ngozi, nyama, maziwa, samaki, n.k.),
- Kuwahakikishia umiliki wa ardhi na kuwaondolea usumbufu wa wao kuondolewa kwenye ardhi zao kupisha wawekezaji,
- Kuhakikisha kwamba migogoro ya ardhi baina ya wakulima na wafugaji tunaitatua na kuikomesha kwa kuhakikisha kuwa vyanzo vya msingi vya migogoro hiyo tunaviondosha haraka,
- 10. Kuhakikisha kwamba tatizo la wavuvi kuvamiwa na majambazi na uvuvi haramu linashughulikiwa kikamilifu.
Tatizo la Umaskini na Ajira
Mheshimiwa Spika;
Nimezungumzia umuhimu wa kuendeleza viwanda, kilimo, mifugo na uvuvi kwa sababu ya matatizo makubwa mawili yanayoikabili nchi yetu kwa sasa. Kwanza, ni tatizo la UMASIKINI na pili ni tatizo la AJIRA. Ni kweli uchumi wetu umekuwa ukikua kwa kasi ya kuridhisha, lakini kasi hiyo haijawiana na kasi ya kuondoa umasikini na uzalishaji wa ajira za kutosha kwa vijana wetu wanaoingia kwenye soko la ajira kila mwaka.
Mheshimiwa Spika;
Kwa mujibu wa takwimu zilizopo zaidi ya asilimia 28.2 ya Watanzania ni maskini. Na kwamba kwa namna na kadri uchumi wetu unavyokuwa pengo baina ya matajiri (walionacho) na maskini (wasionacho) linazidi kukua. Tukiendelea hivi tunavyoendelea sasa hatutakuwa tunaitakia mema nchi yetu kwa sababu mgawanyiko mkubwa wa kimapato na tofauti kubwa za kimaisha baina ya matajiri na maskini ukiachiwa uendelee na kuzidi kukua utachochea chuki na uhasama baina ya walionacho na wasionacho. Lazima tujizatiti na kutumia akili, maarifa na nguvu zetu zote kukabiliana na kuibadilisha hali hii. Kwanza, lazima tushughulike na UMASIKINI wa watu wetu. Na njia moja kama nilivyokwisha eleza ni uendelezaji wa sekta ya viwanda na uboreshaji wa sekta za kilimo, mifugo na uvuvi.
Mheshimiwa Spika;
Tatizo la pili ni AJIRA. Kama nilivyokwisha kugusia, ukuaji wa uchumi wetu haujaenda sambamba na kasi ya watu wanaoingia kwenye soko la ajira kila mwaka. Tatizo la ajira ni kwa vijana wote waliosoma viwango mbalimbali vya elimu na wasio na ujuzi. Hii inamaana kwamba sekta zinazochangia kukua kwa uchumi wa nchi yetu sizo zinazozalisha ajira kwa wingi. Ndio maana ya kuweka msisitizo kwenye sekta ya viwanda hasa vile vinavyoajiri watu wengi, na sekta ya kilimo, uvuvi na mifugo ambavyo ndio mwajiri mkubwa hivi sasa.
Mheshimiwa Spika;
Pamoja na kuweka msisitizo katika Viwanda, Kilimo, Mifugo na Uvuvi hatuna budi kuwawezesha vijana wetu kuanzisha shughuli mbalimbali za uzalishaji kwa viwango mbalimbali. Ili hili liwezekane, na sisi tutalifanya, linahitaji mambo mawili makubwa.
Kwanza, kuwaandaa vijana wetu vizuri kielimu na kiujuzi. Hatuna budi kuweka mkazo katika viwango vya ubora vya elimu na stadi za kazi wanazopata vijana wetu. Nalisema hili kwa sababu hatuwezi kuzungumzia uendelezaji wa viwanda ikiwa hatujaandaa vijana wenye uwezo, ujuzi, na stadi za kufanya kazi hizo kwa ubora na ufanisi wa hali ya juu; hatuwezi kutaka kuwekeza katika viwanda vya nguo au samani ikiwa hatuna wahandisi wa mitambo wazuri, wabunifu wa zuri na wenye viwango vinavyotakiwa na kukubalika. Aidha hatuwezi kuwa na vijana wenye uthubutu wa kuanzisha shughuli za uzalishaji kama hawana elimu na maarifa ya kubuni miradi na kuiendeleza. Kwa hivyo tutaelekeza nguvu zetu katika kuhakikisha kuwa shule na vyuo vyetu katika ngazi mbalimbali vinafundisha na kutoa vijana wenye viwango vya hali ya juu vya elimu, maarifa, ujuzi na ufundi.
Mheshimiwa Spika;
Pili, ni suala la uwezeshaji wa vijana hasa wale watakaotaka kujiajiri. Katika kutekeleza lengo hili Serikali ya Awamu ya Tano itachukua na kutekeleza hatua mbalimbali ikiwemo:
- Kuwawezesha vijana wanaohitimu Elimu ya Juu na Vyuo vya Ufundi kupata mitaji ya kuwasaidia kuanzisha makampuni yao kulingana na fani walizosomea;
- Kuwawezesha vijana kuanzisha SACCOS zao na kupitia SACCOS hizo kuwawezesha kupata mikopo;
- Kuwawezesha vijana wajasiriamali kujiunga na Mifuko ya Hifadhi ya Jamii ili waweze kupata mikopo na kunufaika na mafao mengine katika mifuko hiyo.
Mheshimiwa Spika;
Tatu, ni kuzitambua na kuziheshimu kazi na shughuli mbalimbali zinazofanywa na makundi mbalimbali ya kinamama na vijana. Hapa namaanisha shughuli za kina Mama lishe, wachuuzi mbalimbali, Machinga, waendesha Boda Boda na Maguta, na vijana wa kike na wa kiume wanaojitafutia kazi mbalimbali halali za kujipatia mapato kwa ajili ya kuendesha maisha yao, n.k. Shughuli za makundi haya zinatusaidia sana katika kupunguza makundi ya vijana wetu ambao wangekaa tu na kuzurura zurura ovyo bila shughuli ya kufanya. Na kwa kuwa kwa sasa uwezo wetu wa kuwapatia ajira tofauti ni mdogo ni jukumu letu kuwasaidia na kuwawezesha kufanya shughuli zao kwa utilivu bila bugudha. Niliahidi, na nataka nirudie hapa, kwamba Serikali ya Awamu ya Tano ikishirikiana na Halmashauri zetu, pamoja na Wakuu wa Mikoa na Wilaya itaweka mipango na taratibu nzuri na rafiki kwa aina ya shughuli ambazo baadhi nimezigusia. Aidha, ushuru usio wa lazima na wenye usumbufu kwa wafanyabiashara wadogo wadogo utokanao na shughuli nilizozitaja tutauondoa. Tunaamini ikiwa tutaweza kuongeza ukusanyaji mapato, na kuziba mianya ya wakwepaji wakubwa wa kodi ambao huipotezea Serikali mabilioni ya fedha tutakuwa hatuna sababu ya kufukuzana na kina mama na vijana mitaani. Viongozi na watendaji wa Serikali na hasa wa Halmashauri watenge maeneo kwa ajili ya wafanyabishara wadogo na waandae mipango ya kupunguza ushuru usio wa lazima.
Afya
Mheshimiwa Spika;
Dhamira ya kujenga uchumi wa kisasa na suala la kupambana na umasikini linakwenda sambamba na kuwa na wananchi wenye afya bora. Kwa kutambua ukweli huu na mahitaji ya huduma bora za wananchi wetu Serikali ya Awamu ya Tano itahakikisha kwamba wananchi wanapata huduma bora za afya kwa kufanya baadhi ya mambo yafuatayo:
- Kwanza, kuimarisha huduma za afya pale zilipo na kuanzisha pale ambapo hazipo. Lengo ni kuhakisha kwamba kila kijiji kinakuwa na Zahanati, kila Kata inakuwa na Kituo cha Afya, kila wilaya inakuwa na Hospitali, na kila Mkoa unakuwa na hospitali ya Rufaa.
- Pili, tutaimarisha na kuboresha huduma za afya kwa kuongeza utaalamu katika Nyanja za afya kwa kuwapatia mafunzo watumishi wake ndani na nje ya nchi; kwa kuzipatia vifaa bora na vya kisasa hospitali, vituo vya afya na zahanati zetu. Lengo la kufanya hivyo ni kuwezesha upatikanaji wa huduma mahsusi hapa hapa nchini na hivyo kutolazimika kupeleka watu wetu kutibiwa nchi za nje.
- Tatu, tutaongeza bajeti ya dawa na kuboresha mfumo wa upatikanaji ili kuhakikisha dawa zinapatikana katika hospitali, vituo vya afya na zahanati zetu. Aidha, tutahamasisha wananchi wajiunge na Bima ya Afya.
Elimu
Mheshimiwa Spika;
Natambua juhudi kubwa zimefanyika katika upanuzi wa elimu ya awali, msingi, sekondari na vyuo vikuu. Serikali ya Awamu ya Tano itajielekeza katika kuongeza ubora wa elimu inayotolewa ikiwa pamoja na na kuongeza mkazo katika masomo ya sayansi. Aidha, tutahakikisha kwamba vifaa vya kufundishia na kujifunzia vinapatikana ikiwa ni pamoja na maabara, vitabu, madawati, n.k. Tutahakikisha kuanzia Januari mwakani elimu kuanzia darasa la kwanza hadi kidato cha nne inatolewa bure, kama tulivyoahidi kwenye kampeni. Tutahakikisha kwamba wanafunzi wengi zaidi wa elimu ya juu wanapata mikopo kwa wakati. Tutashughulikia maslahi na kero za walimu wa ngazi zote ikiwa ni pamoja na kujenga nyumba za walimu vijijini na kuiunga mkono Benki ya walimu ili iweze kuwanufaisha zaidi.
Maji
Mheshimiwa Spika;
Wakati wa kampeni nimekutana na malalamiko mengi sana ya ukosefu wa maji. Serikali ya Awamu ya Tano itahakikisha kwamba inaongeza kiwango cha upatikanaji wa maji kufikia asilimia 85 kwa maeneo ya vijijini na asilimia 95 kwa maeneo ya mijini ifikapo 2020. Tutakamilisha miradi iliyokwishaanza na kuanzisha miradi mipya mikubwa na midogo ya maji kutoka katika mito, maziwa na vyanzo vingine vya uhakika vya maji ikiwa pamoja na kuvuna maji ya mvua. Tunataka tuwatue akina mama ndoo kichwani. Tunatambua umaskini hauwezi kuondoka nchini kama wananchi hawapati maji safi na salama.
Umeme
Mheshimiwa Spika;
Suala la upatikanaji wa umeme limeendelea kuwa tatizo katika nchi yetu pamoja na jitihada kubwa zilizofanywa na Serikali zilizopita. Hatuwezi kuzungumzia suala la kujenga viwanda wakati umeme hautoshi. Serikali yangu itahakikisha kwamba umeme unapatikana wa kutosha na wa uhakika. Tutakamilisha miradi ya umeme iliyopo na kujenga mingine mingi mipya ili wananchi wengi zaidi wanufaike na nishati ya umeme na viwanda vingi zaidi vidogo vidogo, vya kati na vikubwa vianzishwe.
Madawa ya Kulevya
Mheshimiwa Spika;
Madawa ya kulevya yamekuwa ni janga kubwa kwa taifa letu na kundi linaloathirika zaidi ni vijana wa kiume na kike. Familia nyingi zimeathirika na nguvu kazi ya taifa imepotea. Tutaushughulikia mtandao huo hususan wafanyabiashara wakubwa wanaojihusisha na madawa ya kulevya bila ajizi.
Mheshimiwa Spika;
Masuala mengine tutakayoyawekea mkazo katika utawala wa Awamu ya Tano ambayo ninaamini yatasaidia katika kujenga uchumi wetu ni pamoja na masuala ya Utalii, Mawasiliano, Madini, Ardhi na Makazi, Ujenzi na Miundombinu, Bandari, Barabara, Ulinzi na Usalama, utunzaji wa mazingira, Vijana, Wanawake, Watu wenye Ulemavu na Ualbino, Wazee, Wafanyakazi, Wasanii na Wanamichezo, wanahabari, wafanyabiashara, wawekezaji, wajasiriamali, sekta binafsi, n.k. Utekelezaji wa masuala haya umefafanuliwa vizuri katika Ilani ya CCM ya mwaka 2015. Tutayatekeleza ipasavyo.
Mapambano Dhidi ya Rushwa na Ufisadi
Mheshimiwa Spika;
Jambo moja nililolisemea kwa nguvu kubwa wakati wa kampeni ni mapambano dhidi ya rushwa na ufisadi. Sikufanya hivyo kwa sababu nilitaka tu kuwarubuni wananchi ili wanipe kura zao na kunifanya kuwa Rais wao. Nililiongea jambo hili kwa dhati kabisa, na nilichokisema na kuwaahidi wananchi ndicho hasa nilichokikusudia.
Mheshimiwa Spika;
Wananchi wanachukia sana rushwa na ufisadi, na wamechoshwa na vitendo hivyo. Mimi pia ninachukia rushwa na ufisadi. Sifurahishwi kabisa na vitendo vya rushwa na ufisadi vinavyoendelea hapa nchini. Vitendo vya rushwa na ufisadi vinawanyima haki wananchi na kuitia hasara serikali kwa mamilioni ya fedha ambazo zingeweza kutumika kwa ajili ya kujenga miradi ya maendeleo kwa ajili ya watu wetu.
Mheshimiwa Spika;
Chama changu, Chama cha Mapinduzi, kimejengwa katika misingi ya kukataa rushwa na ufisadi. Ndio maana moja ya Imani kuu za CCM ni ile isemayo: “Rushwa ni adui wa haki, sitatoa wala kupokea rushwa”
Kwa Mtanzania mwaminifu kwa imani yake hatakuwa na kigugumizi katika kuwa mstari wa mbele katika kupambana na rushwa na ufisadi.
Mheshimiwa Spika;
Mmoja wa waasisi wa Taifa letu, Baba wa Taifa, Hayati Mwalimu Julius Kambarage Nyerere, aliwahi kuifananisha rushwa na ufisadi ‘Kama Adui Mkubwa wa Watu’. Akiongea Bungeni Mei 1960, Mwalimu Nyerere alisema yafuatayo kuhusu rushwa:
“Rushwa [na ufisadi] havina budi kushughulikiwa bila huruma kwa sababu naamini wakati wa Amani rushwa na ufisadi ni adui mkubwa kwa ustawi wa watu kuliko vita.”
Mheshimiwa Spika;
Haya ni maneno makali ya mtu na kiongozi aliyeichukia na kuikemea rushwa katika maisha yake yote ya uongozi. Ni maneno yanayotukumbusha tu nini kinaweza kikatutokea kama taifa endapo tutaendekeza rushwa na ufisadi. Chuki za wananchi dhidi ya rushwa na ufisadi ni dhahiri, wamechoka kabisa, wamechoka sana, hawako tayari kuvumilia upuuzi wa serikali itayoonea haya rushwa na kulea mafisadi.
Mheshimiwa Spika;
Mimi nimewaahidi wananchi, na nataka niirejee ahadi yangu kwao mbele ya Bunge lako tukufu, kwamba nitapambana na rushwa na ufisadi bila kigugumizi na bila haya yoyote. Dawa ya jipu ni kulitumbua, na mimi nimejipa kazi ya kuwa mtumbua jipu. Najua kutumbua jipu kuna maumivu lakini bahati mbaya halina dawa nyingine. Hivyo ninaomba Waheshimiwa Wabunge na Watanzania wote mniombee na muniunge mkono wakati natumbua majipu haya.
Mheshimiwa Spika;
Ninafahamu ugumu wa vita niliyoamua kuipigana. Nasema nafahamu ugumu na changamoto zake kwa sababu wanaojihusisha na rushwa sio watu wadogo wadogo. Vitendo vya rushwa na ufisadi vyenye madhara makubwa kwa nchi na ustawi wa nchi yetu hutendwa na watu wenye dhamana kubwa za uongozi na utumishi ambazo wamezipata kutokana na ridhaa ya watu. Kwa hivyo ili niweze kufanikiwa lazima nipate ushirikiano mkubwa toka kwa Bunge lako tukufu na vyombo vingine vilivyopo na vyenye majukumu ya kupambana na vitendo hivi.
Aidha, tutashinda vita hii endapo wananchi pia watatuunga mkono. Sina mashaka kuwa kwa vile wao, kwa wingi wao, wanachukia rushwa na ufisadi, watakuwa tayari kutoa ushirikiano wao katika mapambano haya dhidi ya rushwa na ufisadi.
Mheshimiwa Spika;
Katika kushugulikia tatizo hili nimeahidi kuunda mahakama ya Rushwa na Ufisadi. Ni matumaini yangu vyombo husika katika jambo hili havitanikwamisha.
Aidha, nataka niahidi mbele ya Bunge lako tukufu kwamba, kiongozi yeyote wa kuteuliwa, ambaye mimi nitakuwa nimemteua kwa mamlaka niliyonayo kikatiba, na ninayo mamlaka ya kumwajibisha, pindi tu nikibaini na kujiridhisha kuwa anajihusisha na vitendo vya rushwa na ufisadi nitamtimua mara moja. Baada ya mimi kuchukua hatua hizo hatua na taratibu zingine za kisheria zitafuata.
Mheshimiwa Spika;
Ninachotaka kusema ni kuwa Serikali yangu itafuatilia kwa karibu mienendo ya viongozi na watendaji wake ili kubaini kwa haraka nani anajihusisha na vitendo vya rushwa na ufisadi. Na tukishajiridhisha hatutasubiri, tutachukua hatua. Ni imani yangu wengine pia katika ngazi mbalimbali mtafanya hivyo. Kwa sababu bila kufanya hivyo rushwa na ufisadi vitazoeleka na kuwa wimbo unaoburudisha badala ya kuudhi na kukera.
Muundo wa Serikali na Utumishi
Mheshimiwa Spika;
Nilipokuwa nazunguka na kuzungumza na wananchi wakati wa Kampeni za Uchaguzi, niliahidi kuwa nitaunda serikali ndogo ya wachapa kazi.
Aidha, niliahidi pia kuunda serikali ambayo itawatumikia watu na hasa wananchi wa kawaida. Serikali nitakayounda, nataka iwe inawahudumia wananchi kwa haraka na sio kuwasumbua sumbua na kuwazungusha. Natoa rai kwa watumishi wa serikali, hasa ambao ni wazembe na wavivu, kujiandaa. Wamevumiliwa kwa muda mrefu sasa basi. Kwa sababu watumishi wa aina hiyo hawatavumuliwa katika serikali nitakayoiongoza. Lugha za “hiyo ni changamoto tutaishughulikia”, au “Mchakato unaendeela” hazitavumiliwa katika Serikali ya Awamu ya Tano. Mimi nataka watu wa Kazi Tu. Hatuwezi kulea watu ambao wanalipwa mishahara lakini hawafanyi kazi wanazotakiwa kufanya, au wamegeuza ofisi za umma kuwa ni mahala pa kuchuma bila kufanya kazi.
Mheshimiwa Spika;
Pamoja na kuwataka watumishi wa Serikali kufanya kazi hatuna budi kuyaangalia na kuboresha mishahara na maslahi yao na mazingira yao ya kufanyia kazi kwa kuwapatia vitendea kazi bora na vya kisasa. Na jambo moja tutakalolitekeleza ni kuangalia namna ya kupunguza kodi ya mapato katika mishahara ya wafanyakazi yaani PAYE. Pia tutajitahidi kuwatambua na kuwapa motisha wafanya kazi wachapa kazi.
Kuongeza Mapato na Kupunguza Matumizi ya Serikali
Mheshimiwa Spika;
Kwa zaidi ya miaka mitatu sasa ukusanyaji wa mapato umekuwa chini ya makadirio kwa sababu mbalimbali. Serikali ya Awamu ya Tano itaongeza nguvu katika upanuzi wa wigo wa kodi na kuongeza ufanisi katika ukusanyaji wa mapato. Tutahakikisha kwamba kila mtu anayestahili kulipa kodi analipa kodi stahiki. Hatutasita kumchukulia hatua mtu yoyote atakaye kwepa kulipa kodi. Tunawaomba wananchi mhakikishe mnapewa risiti kila mnaponunua bidhaa au huduma. Kodi ni kitu muhimu lazima kila mtu anayestahili kulipa kodi alipe.
Aidha, tutahakikisha kwamba kila senti inayoongezeka katika mapato ya Serikali inaelekezwa katika kutoa huduma bora zaidi kwa wananchi. Tutaziba mianya ya upotevu wa fedha za Serikali ambayo inaipunguzia Serikali uwezo wake wa kuwahudumia wananchi.
Mheshimiwa Spika;
Nitataja baadhi tu ya maeneo ambayo tutayasimamia kwa lengo la kupunguza matumizi yasiyo ya lazima na kuziba mianya ya uvujaji wa fedha za Serikali:
Kwanza, safari zote zisizo za lazima nje ya nchi Serikalini tutazidhibiti na badala yake tutawatumia mabalozi wetu kutuwakilisha kwenye mikutano ya aina hiyo. Na pale inapolazimu kiongozi au mtumishi mwandamizi kusafiri tutahakikisa kwamba haandamani na msururu wa watu wengi ambao hawana umuhimu wala shughuli za kufanya katika safari hizo.
Katika kusisitiza hili napenda niwape takwimu za fedha zilizotumika ndani ya Serikali, Mashirika ya Umma na Taasisi nyingine za Serikali kwa safari za nje kati ya mwaka 2013/14 na 2014//2015. Jumla ya shilingi bilioni 356.324 zilitumika kwa ajili ya safari za nje kama ifuatavyo:
- Tiketi za ndege (Air ticket) zilitumia shilingi bilioni 183.160;
- Mafunzo nje ya nchi (Training Foreign) zilitumia shilingi bilioni 68.612;
- Posho za kujikimu (Per Diem Foreign) zilitumia shilingi bilioni 104.552;
Wizara na Taasisi zinazoongoza kwa matumizi ya safari za nje ni pamoja na Bunge, Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikano wa Kimataifa, Wizara ya Fedha, Ofisi ya Waziri Mkuu, Ofisi ya Taifa ya Ukaguzi wa Hesabu za Serikali (NAOT), Wizara ya Mambo ya Ndani, n.k.
Hizi fedha zingeweza kutumika vizuri kuboresha huduma za wananchi wa maisha ya chini, kama afya, maji, elimu, umeme n.k. Mfano; fedha hizi zingetosha kutengeneza kilometa 400 za barabara za lami, tujiulize zingeweza kutengeneza zahanati ngapi?, nyumba za walimu ngapi?, madawati mangapi? n.k. Hivyo tunapodhibiti safari za nje tunawaomba Waheshimiwa Wabunge na Watanzania wote mtuelewe na mtuunge mkono.
Pili, tutahakikisha tunadhibiti safari na ziara za mafunzo nje ya nchi zinazogharamiwa na serikali ambayo yanapatikana hapa nchini.
Tatu, tutadhibiti warsha, semina, makongamano, na matamasha ambayo kwa kweli yanatumia fedha nyingi tu za serikali lakini hayana tija na wala hayaongezi ufanisi katika utekelezaji na usimamizi wa sera na mipango ya Serikali.
Nne, tutasimamia kwa ukamilifu Sheria ya Manunuzi ya Umma ili kuhakikisha kwamba mianya yote ya fedha za umma inayotokana na usimamizi hafifu tunaiziba. Ni matarajio yangu kutakapoleta Mswada wa Marekebisho ya Sheria ya Manunuzi ya Umma Waheshimiwa Wabunge mtatuunga mkono.
Tano, tutasimamia na kudhibiti ukiukwaji wa maagizo na maelekezo mbalimbali yaliyokwisha kutolewa na Serikali siku za nyuma kuhusu ununuzi wa bidhaa kama samani kwa ajili ya matumizi ya Serikali. Samani zote kwa ajili ya matumizi ya Serikali zinatakiwa ziwe zile zinazozalishwa hapa hapa nchini.
Sita, Serikali ya Awamu ya Tano itasimamia kwa karibu na kuthibiti ununuzi wa magari ya gharama kwa ajili ya Viongozi na Watumishi waandamizi wa Serikali; na
Saba, tutaendelea kuchunguza na kudhibiti matumizi ya Serikali na Taasisi zake zote yasiyo na tija kwa uchumi wa taifa letu.
Mheshimiwa Spika;
Kwa ajili hiyo, vipaumbele vya Serikali ninayotarajia kuiunda vitakuwa ni: kupunguza urasimu ili kuongeza kasi ya utekelezaji wa maamuzi na miradi ya Serikali; kubana matumizi kwa kupunguza yale ambayo kutokana na hali yetu ya uchumi kwa sasa yanaweza kuepukika; na kurejesha nidhamu ya Serikali na utumishi wa umma kwa kuongeza uwazi na uwajibikaji.
Tutatekeleza vipaumbele hivyo kwa kufanya pamoja na mambo mengine kupunguza ukubwa wa Baraza la Mawaziri; kuongeza usimamizi katika ukusanyaji wa mapato ya kodi na maduhuli ya Serikali kwa kuziba mianya ya ukwepaji kodi, tutahakikisha kwamba wale wote wanaotakiwa kulipa kodi wanalipa ipasavyo. Tutaongeza nidhamu ya matumizi ya Serikali ili kuhakikisha fedha zinazookolewa zinakwenda kwenye miradi ya maendeleo; na kusimamia sheria, kanuni na taratibu za uwajibikaji wa viongozi na watumishi wa umma ili wawajibike kwa wananchi ambao ndio wateja na waajiri wakuu wa watumishi wa umma. Serikali ya Awamu ya Tano itaendelea kubainisha maeneo mengine ya matumizi yasiyo ya lazima ambayo yanaigharimu Serikali fedha nyingi na kuyadhibiti. Aidha, nitoe wito kwa Watanzania wote kila mmoja wetu afanye kazi iwe shambani, ofisini, kiwandani, sokoni, n.k. Badala ya tabia ya sasa iliyoanza kujengeka kwa Watanzania kutokupenda kufanya kazi na hivyo kupoteza muda mwingi vijiweni, muda ambao ungetumika kufanya kazi ndiyo maana kauli mbiu yangu ni HAPA KAZI TU!
Mambo ya Nje na Ushirikiano wa
Kikanda na Kimataifa
Mheshimiwa Spika;
Nchi yetu imepata mafanikio makubwa katika Nyanja ya diplomasia na ushirikiano wa kimataifa katika awamu zilizotangulia za uongozi. Serikali yangu itaendeleza sifa hiyo kwa kujenga juu ya msingi imara uliowekwa na awamu zilizotangulia na awamu ya nne chini ya Rais Mstaafu Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete. Tutaendelea kuwa waumini na tutaendeleza sera ya ujirani mwema na nchi zinazotuzunguka kwa lengo la ustawi wa watu wetu na maslahi mapana ya nchi yetu. Tutaendelea kuwa waaminifu wa utangamano wa Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC) na daima tutatekeleza wajibu wetu kwa mujibu wa Mkataba wa Uanzishwaji wa Jumuiya ya Afrika Mashariki, itifaki zake na maamuzi ya vikao vya nchi wanachama. Tutaendelea kutekeleza matakwa ya Mkataba huu wa kujenga utengamano wetu hatua kwa hatua.
Mheshimiwa Spika;
Tanzania itaendelea kuwa mwanachama mwaminifu wa Jumuiya ya Maendeleo ya Kusini mwa Afrika (SADC) na kuendelea kushirikiana kwa karibu na nchi wanachama ambao tunauhusiano wa kihistoria na kidugu. Tutaendelea kuamini katika Umoja wa Afrika (AU) na azma ya ndoto ya waasisi wetu ya kuunganisha bara la Afrika. Tutaendelea pia kushiriki kikamilifu katika Jumuiya ya Nchi za Maziwa Makuu (ICGLR) na kushirikiana na nchi wenzetu wanachama kutafuta majawabu ya kudumu ya amani, usalama na maendeleo katika eneo la maziwa makuu.
Tutaendeleza na kustawisha mahusiano na marafiki zetu wote Magharibi, Mashariki ya Mbali na Mashariki ya Kati kwa lengo la kushirikiana kwa maslahi ya nchi zetu na watu wetu. Tutapenda kutumia fursa nzuri ya mahusiano yetu mazuri kisiasa kukuza mahusiano yetu ya uchumi kwa kutumia diplomasia ya uchumi. Tutafanya hivyo pia kwa ushirikiano wa kimataifa kwa kuendeleza mahusiano yetu na Umoja wa Mataifa (UN) na taasisi zake, Jumuiya ya Madola, Benki ya Dunia, Shirika la Fedha Duniani (IMF) na Benki ya Maendeleo ya Afrika (AfDB), n.k.
Aidha, tutazitaka Balozi zetu zionyeshe matunda yanayolingana na thamani ya fedha tunazowapelekea hususan katika kuvutia uwekezaji, biashara, utalii na mchango wao katika ukuzaji wa sekta ya viwanda. Tunataka kuona diplomasia yetu na Sera yetu ya nje ikijibu changamoto zetu za ndani za ajira, miundombinu, masoko ya mazao ya wakulima, viwanda n.k.
Hitimisho
Mheshimiwa Spika;
Naomba kabla ya kuhitimisha nitoe wito kwa Waheshimiwa Wabunge, Bunge hili linalo nafasi ya kuweka historia ya kuwa kitu kimoja na kuweka masilahi ya Taifa mbele. Kama kuna kitu ambacho wananchi wanachukia ni lugha za vijembe, mipasho, na ushabiki wa vyama bungeni. Kwanza, tukumbuke wote bila kujali itikadi za vyama vyetu sisi ni kitu kimoja; na pili tumechaguliwa kuwawakilisha wenzetu. Baada ya miaka mitano kila mmoja atarudi kwenye jimbo lake kuomba kura na huko atapimwa kwa maendeleo aliyopeleka.
Tusimame pamoja, Tanzania ni yetu sote tutangulize masilahi ya nchi mbele, na kwa mara ya kwanza Watanzania waone Bunge tofauti na sio Bunge la kuzomea, kutoka nje, kutukanana, mipasho, n.k. Tunaitwa Waheshimiwa kwa heshima ya dhamana tuliyopewa na Bunge hili Tukufu, tutunze heshima hiyo ili tuzidi kuheshimiwa.
Aidha, napenda kusisitiza kuwa kazi iliyoko mbele yetu ni kubwa. Matarajio na matumaini ya Watanzania waliotuchagua na kutupa ridhaa ya kuwaongoza katika kipindi cha miaka mitano ijayo ni makubwa. Wanachotaka kuona ni nchi yetu kupiga hatua kubwa za maendeleo zitakazojibu matumaini yao na kutatua shida na kero zao. Nyie na mimi, baada ya miaka mitano toka sasa, tutapimwa kwa namna tutakavyokuwa tumetekeleza mambo ambayo tumewaahidi Watanzania wenzetu. Mimi nina amini kabisa kwa ushirikiano wetu na kwa kufanya kazi kwa bidii na ubunifu tutaweza kuzitimiza ndoto za Watanzania wenzetu.
Mheshimiwa Spika;
Sasa natamka kwamba nimelifungua rasmi Bunge la 11 la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Asanteni kwa kunisikiliza!
Mungu libariki Bunge letu na Wabunge wake!
Mungu Ibariki Afrika!
Mungu Ibariki Tanzania!
Ahsanteni kwa kunisikiliza
- Oct 22, 2015
Hotuba ya Mhe. Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika hafla ya kuagana na watumishi wa Umma tarehe 22 Oktoba, 2015
Soma zaidiHotuba
Mhe. Mohamed Othman Chande, Jaji Mkuu wa Jamhuri ya
Muungano wa Tanzania;
Balozi Ombeni Y. Sefue, Katibu Mkuu Kiongozi wa Jamhuri ya
Muungano wa Tanzania;
Ndugu Makatibu Wakuu na Makatibu Tawala wa Mikoa;
Wakuu wa Vyombo vya Ulinzi na Usalama,
Ndugu Wenyeviti wa Bodi wa Taasisi Mbalimbali;
Ndugu Watendaji Wakuu wa Taasisi Mbalimbali;
Ndugu Wenyeviti wa Vyama vya Wafanyakazi;
Ndugu Watumishi Wote.
Shukrani
Nakosa maneno ya kutosha ya kubeba na kuelezea furaha yangu ya kujumuika nanyi leo kwa wingi wenu kwenye hafla hii ya kuniaga. Mmenigusa sana kwa ishara hii ya upendo mliyoionyesha kwangu. Si jambo la kawaida kwa Rais kuagwa na watumishi wa umma, wala si jambo la lazima. Hii ni ishara kuwa tumeishi vizuri na tunaachana vizuri. Nawashukuru sana kwa zawadi mlizonipatia, maana pia mmenipatia katika kuzichagua zawadi zenyewe. Zitanifaa sana katika maisha ya ustaafu.
Nakushukuru sana Katibu Mkuu Kiongozi na viongozi wenzako kwa kuandaa hafla hii na kwa maneno yako ya kunikaribisha kuzungumza. Umeeleza kwa ufasaha yale mambo ambayo kwa pamoja tumeweza kuyafanikisha katika utumishi wa umma, na yale ambayo hatukuweza kuyakamilisha lakini tumeyafikisha mahala penye muelekeo wenye matumaini ya kukamilika siku zijazo.
Nawashukuru sana watumishi wa umma kwa risala yenu nzuri. Nimeisikiliza kwa umakini mkubwa na nimeipokea kwa mikono miwili. Ndani ya risala yenu yako maombi, ushauri na mapendekezo. Napenda kuwahakikishia kuwa nimeyapokea na nitayajumuisha katika Taarifa yangu ya Makabidhiano (Hand Over Notes) nitakayomkabidhi Rais ajaye ili ayazingatie na kuyapatia majawabu.
Shukrani kwa Watumishi wa Umma
Mabibi na Mabwana;
Nitakuwa mchoyo wa shukrani nisipowashukuru na kuwapongeza sana watumishi wa umma kote nchini kwa kazi kubwa mliyoifanya katika kipindi cha miaka 10 ya awamu ya nne. Ni uungwana kukiri kuwa, mafanikio na sifa ninazozipata, zimechangiwa kwa kiasi kikubwa na jitihada zenu. Jukumu langu kama Rais, ilikuwa ni kutoa uongozi na maelekezo wa nini kifanyike. Ninyi kwa kiasi kikubwa ndio mlioshauri, mliotafsiri na mliotekeleza maagizo na maelekezo niliyowapatia ambayo imezaa matokeo tunayojivunia nayo. Nawashukuru na kuwapongeza sana kwa kujitoa kwenu na kutekeleza kwenu wajibu wenu kwangu kama kiongozi mkuu na wajibu wenu kwa taifa.
Umuhimu wa Utumishi wa Umma
Mabibi na Mabwana;
Umuhimu wa Watumishi wa Umma katika nchi yetu ni jambo lisilohitaji mjadala, ingawa ni jambo linalopaswa kusemwa ili lieleweke vizuri. Kumekuwepo na uelewa finyu juu ya umuhimu wenu na mchango wenu mkubwa katika ujenzi wa taifa letu. Ipo haja ya kuendelea kuelimisha umma na wanasiasa kuwa ninyi ni chombo cha umma, kwa ajili ya umma na mnautumikia umma wote mkiongozwa na uweledi, uzalendo na viapo vyenu kwa taifa. Serikali za Vyama zinapita, ninyi mnaendelea kuwepo ndio maana masharti yenu ya ajira ni masharti ya kudumu na pensheni.
Mafanikio ya Kujivunia
Mabibi na Mabwana;
Katika miaka 10 iliyopita, ukiachilia mbali mafanikio makubwa ya kiuchumi na kijamii, kumekuwepo na mafanikio makubwa ndani ya utumishi wa umma. Awamu ya nne imejenga juu ya msingi mzuri ulioachwa na awamu zilizotangulia na kuboresha zaidi maslahi na utendaji kazi wa utumishi wa umma.
Mtakubaliana nami kuwa tumepiga hatua za kuridhisha katika kuongeza ufanisi serikalini kwa kuboresha mifumo ya utendaji na ufuatiliaji wa kazi za serikali, ushirikishwaji wa watumishi katika maamuzi na uendeshaji wa serikali na uendelezaji wa maslahi ya watumishi wa umma. Kwa upande wa uboreshaji wa mifumo ya kazi tumefanya yafuatayo:
a) Kuanzishwa kwa mfumo wa Matokeo Makubwa Sasa (BRN). Mfumo huu wa usimamizi na ufuatiliaji umeongeza uwazi na ufanisi kwa kushirikisha wadau wote katika sekta husika;
b) Kuanzishwa kwa Serikali Mtandao (e-government) ambapo tumewezesha kuanzishwa kwa Mfumo wa Ajira kwa Njia ya Kielektroniki (e-Recruitment), mfumo shirikishi wa utoaji wa huduma za serikali kwa njia ya simu za mkononi; ukusanyaji wa maduhuli kwa njia ya mtandao; na tovuti ya wananchi kwa ajili ya kupokea maoni ya wananchi;
c) Kuanzishwa kwa Mfumo wa Taarifa Shirikishi za Kiutumishi na Mishahara mwaka 2012 ambao umewezesha ufanisi katika uhifadhi na uchakataji wa Taarifa za kiutumishi na mishahara ya Watumishi. Mfumo huu umetuwezesha pia kubaini Watumishi hewa.
d) Kupitia Sheria ya Majadiliano ya Pamoja katika Utumishi wa Umma Sura ya 105, tuliunda Baraza Kuu la Wafanyakazi katika Utumishi wa Umma, Baraza la Majadiliano ya Pamoja ya Kisekta (Sekta ya Utumishi Serikalini, Sekta ya Elimu, Sekta ya Afya na Sekta ya Serikali za Mitaa).Tulianzisha pia Tume ya Usuluhishi na Uamuzi (CMA) kwa lengo kutatua migogoro ya kazi.
Mafanikio haya katika uboreshaji wa mifumo ya kazi, umewezesha pia uboreshwaji wa maslahi ya watumishi wa umma. Katika eneo hili ningependa kutaja kwa uchache yafuatayo:
a) Kuundwa kwa Tume ya Kuboresha Maslahi ya Watumishi wa Umma mwaka 2006 ambayo mapendekezo yake yaliwezesha kuhuishwa kwa Sera ya Malipo ya Mishahara na Motisha katika Utumishi wa Umma ya mwaka 2010, na kuundwa kwa Bodi ya Mishahara na Maslahi katika Utumishi wa Umma mwaka 2012.
b) Kupandishwa kwa kima cha chini cha mshahara mwaka hadi mwaka kutoka shilingi 65,000 kwa mwezi mwaka 2005/2006 hadi shilingi 300,000 mwaka 2015/16 (ongezeko la mara 5). Wakati huo huo kushusha Kodi ya Mapato (PAYE) kutoka asilimia 18 mwaka 2005/2006 hadi asilimia 11 mwaka 2015/16.
c) Kutolewa kwa Waraka wa Watumishi wa Serikali Na. 3 wa mwaka 2011 unaowawezesha Watumishi wa umma kukopa fedha taslimu za kununulia samani, vyombo vya usafiri au matengenezo ya vyombo vya usafiri. Kutokana na ufinyu wa bajeti, Serikali pia imeweka utaratibu wa mabenki na taasisi za fedha kukopesha Watumishi wa umma.
d) Kuboresha mfumo wa Bima ya Afya kwa Watumishi wa Umma kwa kuondoa madaraja katika utoaji wa huduma. Aidha, tumepitia upya na kuboresha mafao ya kustaafu ya watumishi wa umma. Naipongeza sana Mamlaka ya Mifuko ya Hifadhi ya Jamii (SSRA) kwa kazi nzuri waliyoifanya katika eneo hili. Nafahamu kuwa bado yapo masuala machache ambayo yako mezani kwa majadiliano.
Mabibi na Mabwana;
Ninachoweza kusema ni kuwa, jitihada hizi kwa pamoja zimefanya Utumishi wa Umma kuwa ni mahala pazuri pa kufanya kazi na kimbilio hata la wafanyakazi walioko katika sekta binafsi. Ni ukweli ulio wazi kuwa, watumishi wa umma wanaopokea kima cha chini cha mshahara wana nafuu kimaisha kuliko wale wa sekta nyingine. Natambua bado tunahitaji kuboresha zaidi katika eneo hili. Mimi binafsi, nimetumia madaraka yangu ya urais kuhakikisha kuwa nyongeza na nafuu inapatikana kila mwaka kwa watumishi wa ngazi za chini wa Serikali. Naamini Rais ajaye aye atafanya hivyo, muhimu tu mchague vizuri.
Pamoja na ukweli kuwa jitihada hizi hazijatatua changamoto zote zilizopo, kilicho wazi ni kuwa tumeweka msingi imara wa kuzipatia majawabu ya uhakika changamoto za utumishi wa umma. Ni bahati mbaya kwamba dhamira yetu njema imekuwa ikielemewa na uwezo mdogo wa mapato ya Serikali. Utatuzi wa changamoto nyingi unategemea sana upatikanaji wa fedha za kutosha jambo ambalo halina jawabu la mkato. Tunapaswa tuendelee kufanya kazi kwa bidii, kuongeza tija, ukusanyaji wa maduhuli ili hatimaye tujenge uwezo wa serikali kutoa maslahi mazuri zaidi kwa watumishi wa umma.
Mambo Mengine ya Kujivunia
Mabibi na Mabwana;
Mambo Mengine ninayojivunia ninapoagana nanyi ni kule kuwapa nafasi za uongozi wanawake na vijana; na kuimarisha ushirikiano na sekta binafsi. Tuliingiza katika Kipengele cha 12 (4) cha Kanuni za Utumishi wa Umma za 2013 kisemacho, “Inapotokea mwanamke na mwanaume wametimiza vigezo sawa kwa kulingana, basi kipaumbele atapewa mwanamke”. Kila zilipotokea fursa za uteuzi sikuacha kuwateua wanawake katika nafasi za juu zikiwemo za Makatibu Mkuu, Naibu Makatibu Mkuu na Wakuu wa Taasisi za Serikali. Tulifanya hivyo kwa nia njema ya kurekebisha kasoro za kihistoria zilizowanyima wanawake fursa za uongozi ndani ya Utumishi wa Umma.
Nimeteua pia vijana wengi katika utumishi wa umma kadiri fursa ya kufanya hivyo ilipojitokeza. Lengo kubwa ilikuwa ni kuandaa na kuwalea vijana walioonyesha ari kuwa viongozi wa baadae. Utumishi wa Umma lazima utambue vipaji mbalimbali na kuviendeleza na si kuvizima. Nimefanya hivyo pia kwa kuteua vijana kutoka sekta binafsi na kuwaingiza serikalini. Lengo langu ni kuleta serikalini changamoto mpya na mitazamo mipya ya utendaji kazi.
Mabibi na Mabwana;
Tulipo sasa na huko tuendako, tunapaswa kujenga uelewa wa kufaya kazi kwa ushirikano na sekta binafsi ambayo ni muhimili muhimu wa ujenzi wa nchi ya uchumi wa kati. Ndio sababu, nimejitahidi kuileta sekta binafsi karibu na kuwashirikisha na hivyo kuwafanya kuwa sehemu ya suluhisho badala ya wao kuwa sehemu ya tatizo. Tumewashirikisha katika uundaji wa maabara za BRN na tumefanya hivyo pia kupitia Baraza la Taifa la Biashara (TNBC) na kwa kuweka Sheria ya Ubia kati ya Sekta Binafsi na Sekta ya Umma (PPP). Sasa tunawashirikisha katika mapambano dhidi ya rushwa ambako sasa nao watasaini Hati za Uadilifu kama zile zitakazosainiwana viongozi wa umma na watumishi wa umma. Haya ni mambo ambayo nitafurahi kuona mkiyaendeleza.
Changamoto Mpya kwa Sekta ya Umma
Mabibi na Mabwana;
Utumishi wa Umma wa leo unapita katika kipindi chenye changamoto tofauti na huko tulikotoka. Mabadiliko katika mazingira ya kidunia, kisiasa na rika/demografia (demography) yanaathiri sana utamaduni na utendaji kazi katika utumishi wa umma. Wadau wa serikali wameongezeka na madai yao yamepanuka sawia. Kumekuwepo na mahitaji makubwa ya ufanisi, uwazi na uwajibikaji katika maamuzi ya serikali, mapato na matumizi ya serikali na ushirikishwaji wa wananchi na sekta binafsi katika maamuzi na shughuli za serikali.
Hamna budi kujitazama upya na kuchukua hatua za kufanya maboresho na mageuzi kuendana na mazingira mapya. Ukiritimba usio na lazima, usiri usio na lazima na uhafidhina katika uendeshaji wa mambo hauna nafasi tena sasa na huko tuendako. CAG ametusaidia sana kuona mapungufu yetu. Nawapongeza kwa kuzifanyia kazi Taarifa zake kiasi cha yeye kukiri hivyo katika Taarifa ya CAG ya Ukaguzi ya mwaka ulioishia 30 Juni, 2014. Tumejitahidi kuondokana na hati chafu, sasa ongezeni juhudi kuondokana na hati zenye mashaka.
Mabibi na Mabwana;
Mnapaswa pia kuangalia namna mpya ya kuboresha mfumo wa mawasiliano wa serikali na umma. Awamu ya nne tumefanya mambo mengi makubwa lakini tumekuwa wazito katika kuyaelezea kwa kile tulichojizoesha kuwa ‘Chema chajiuza, kibaya chajitembeza’. Nawakumbusha kwamba zama hizo zimepita na hazitarudi tena. Kufanya mambo mazuri ni jambo moja, na kujulikana kwa mambo hayo mazuri ni jambo lingine, ambalo ndio muhimu zaidi. Hili ni jambo la kulifanyia kazi huko tuendako.
Wosia
Mabibi na Mabwana;
Nimesema mengi, lakini ningependa nimalizie kwa kuwakumbusha machache ambayo naona yana umuhimu wa kipekee kwa ustawi na uhai wa utumishi wa umma. Kwanza, nawaomba sana muheshimu viapo vyenu. Pili, zingatieni miiko na maadili ya utumishi wa umma ambayo ndio msingi na uhai wa utumishi wa umma. Hakuna serikali duniani isiyo na miiko au usiri wa masuala nyeti ya uendeshaji wa serikali. Uvujaji wa siri ni kielelezo kikubwa cha kuporomoka kwa maadili ya utumishi wa umma popote duniani. Mkifika hapo, maana yenyewe ya kuwa na serikali inakuwa ni kama haipo. Tatu, mtii sheria, kanuni na taratibu za utumishi wenu ili kuleta ufanisi na kuondoa migogoro na manung’uniko yasiyokuwa ya lazima.
Hitimisho
Mabibi na Mabwana;
Namalizia kwa kuwashukuru tena kwa hafla hii mliyoniandalia na zawadi mlizonipatia. Kwa nama ya kipekee, Nawashukuru Makatibu Wakuu Viongozi niliofanya nao kazi Mheshimiwa Balozi Marten Lumbanga, Mheshimiwa Philemon Luhanjo na Mheshimiwa Balozi Ombeni Sefue. Nawashukuru pia Makatibu Wakuu, Naibu Makatibu Wakuu, Makatibu Tawala wa Mikoa na Wilaya, Makamishna, Mabalozi, Wakurugenzi, Wakuu wa Taasisi na Mashirika ya Serikali na watumishi wote wa umma kwa mchango wenu mkubwa ulioniwezesha kutimiza wajibu wangu kwa watanzania kwa mafanikio makubwa.
Nafurahi kuwa, niliupokea utumishi wa umma kutoka kwa Rais wa awamu ya tatu, Mheshimiwa Benjamin William Mkapa ukiwa imara na katika hali nzuri. Nafarijika kwamba nitamkabidhi Rais ajaye utumishi wa umma ulio katika hali nzuri zaidi ya kuweza kumsaidia kutekeleza malengo yake na Ilani ya uchaguzi ya Chama chake. Nitapenda sana awe mwana CCM maana naamini mnamjua na hampatapa tabu ya kuendana nae na kutekeleza Ilani ya CCM ambayo ndio iliyo bora katika uchaguzi mkuu huu.
Nachowaomba, mpeni Rais mpya ushirikiano wenu kama au hata zaidi ya ule mlionipatia mimi. Muwe tayari kumsoma na kumuelewa matakwa yake, aina yake ya ufanyaji kazi na kasi yake. Msije mkasema, ‘Rais Kikwete alikuwa hafanyagi hivi”. Kumbukeni ule msemo wa Mzee wetu Rais Ali Hassan Mwinyi kuwa ‘Kila Zama na Kitabu Chake’. Nawatakia kila la kheri katika utumishi wenu. Nawaaga rasmi, kwaherini!
Mungu Ibariki Afrika,
Mungu Ibariki Tanzania.
Asanteni kwa kunisikiliza!
- Oct 16, 2015
Hotuba ya Mheshimiwa Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, kwenye uzinduzi rasmi wa ujenzi wa Bandari ya Bagamoyo, viwanja vya...
Soma zaidiHotuba
Mheshimiwa Mizengo Peter Pinda, Waziri Mkuu,
Mheshimiwa Dkt. Ahmed Mohammed Al Furaisi, Waziri wa Mawasiliano na Uchukuzi wa Oman;
Waheshimiwa Mawaziri wa Jamuhuri ya Muungano
wa Tanzania mliopo;
Mheshimiwa Eng. Evarist Ndikilo, Mkuu wa
Mkoa wa Pwani;
Waheshimiwa Wakuu wa Mikoa mliopo;
Dkt. Florens Turuka, Katibu Mkuu, Ofisi ya Waziri Mkuu na Mwenyekiti wa Kamati ya Pamoja ya Utatu, Mradi wa Eneo Maalum la Kiuchumi Bagamoyo;
Makatibu Wakuu mliopo;
Dkt. Hu Jianhua, Makamu wa Rais wa China
Merchants Group;
Mheshimiwa Abdulsalam Al Murshidi, Afisa Mtendaji
Mkuu wa SGRF;
Col. Joseph Simbakalia, Mtendaji Mkuu wa EPZA;
Ndugu Awadhi Masawe, Mkuu wa Mamlaka ya Bandari;
Mheshimiwa Dkt. Lv Youqing, Balozi wa China
Nchini Tanzania;
Mheshimiwa Sheikh Saud Al Ruqaishi, Balozi wa Oman
Nchini Tanzania;
Waheshimiwa Mabalozi mliopo;
Watendaji Wakuu wa Taasisi mliopo;
Mheshimiwa Majid Hemed Mwanga, Mkuu wa
Wilaya ya Bagamoyo;
Waheshimiwa Wakuu wa Wilaya mliopo;
Wageni Waalikwa;
Mabibi na Mabwana.
Ni furaha na heshima kubwa kwangu kushiriki katika tuko hili la kihistoria la kuweka jiwe la msingi la ujenzi wa bandari mpya na wa Eneo Maalum la Kiuchumi (Special Economic Zone) hapa Mbegani karibu na mji wa Bagamoyo. Nawashukuru sana wajumbe wa Kamati ya Utatu, chini ya Mwenyekiti wake Dkt. Florence Turuka, Katibu Mkuu, Ofisi ya Waziri Mkuu kwa kazi nzuri mliyoifanya kuwezesha mradi huu mkubwa na wa aina yake kuanza kutekelezwa. Pia tunawapongeza kwa maandalizi ya sherehe hizi. Kama mjuavyo, mradi huu unatekelezwa kwa ubia wa mashirika ya nchi tatu za China, Oman na Tanzania.
Kwa namna ya kipekee napenda kutumia nafasi hii kuwakaribisha wawakilishi wa Serikali ya Jamhuri ya Watu wa China na Kampuni ya China Merchants Holdings International Ltd (CMHI) na wa Serikali ya Oman na Shirika lao la State General Reserve Fund (SGRF) katika uzinduzi huu. Kufika kwenu kunatupa faraja kubwa sana na kuashiria mwanzo mzuri na mwisho mwema wa utekelezaji wa Mradi wa Eneo Maalum la Kiuchumi na Bandari la Bagamoyo.
Salamu za Rambirambi
Wageni Waalikwa,
Mabibi na Mabwana;
Mwanzoni uzinduzi wa mradi huu ulikuwa ufanyike jana, lakini tukalazimika kuahirisha hadi leo hii kutokana na kuingiliana na shughuli za mazishi ya marehemu Dkt. Abdallah Omari Kigoda, aliyekuwa Waziri wa Viwanda na Biashara aliyefariki dunia tarehe 12 Oktoba, 2015. Katika hali ya kawaida, marehemu Mheshimiwa Kigoda angekuwa nasi hapa leo hii kwani Wizara yake ndiyo inayohusika na uendelezaji wa eneo maalum la kiuchumi. Alishiriki kwa ukamilifu katika hatua zote za matayarisho ya mradi huu. Nasikitika kuwa hakuweza kuishuhudia siku hii ya leo. Mchango wake utakumbukwa daima.
Chimbuko la Mradi wa Bandani ya Bagamoyo
Wageni Waalikwa,
Mabibi na Mabwana;
Wahenga wanasema usione vinaelea, vimeundwa. Napenda kumtambua muasisi wa mradi huu Mheshimiwa Mizengo Pinda, Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Alipokuwa ziarani nchini China Oktoba, 2013 ndipo alipokutana na Serikali ya China na Kampuni ya China Merchant Holdings na kubuni wazo la kuwa na mradi huu. Alipokuja kunisimulia kuhusu wazo la kuwa na mradi huu, lazima nikiri kuwa nilipata taabu kuamini kwa vile ni mkubwa mno. Mradi wa Dola bilioni 10, kweli unawezekana? Lakini alifanikiwa kunifanya niamini. Nikakubali.
Baadaye wakaja wajumbe wa China Merchant Holdings kunielezea na wakati wa ziara ya Rais wa China nchini makubaliano ya ushirikiano wa ujenzi wa miradi hii yakatiwa saini. Hapo ndipo hofu ikanitoka. Baadaye nikapokea ujumbe kutoka Serikali ya Oman kuniambia kuwa na nchi yao inajiunga katika utekelezaji wa mradi huu ndipo nikaamini zaidi kuwa huu ni mradi muhimu na kwamba utawezekana. Nilipotembelea China mwaka Oktoba, 2014 kule Shenzhen makubaliano ya kuijumuisha SGRF yakatiwa saini hivyo kuliongeza rasmi Shirika la Oman katika mradi.
Baada ya hapo ndipo maandalizi yakapata kasi kubwa. Wenzetu wa China na Oman wamekuwa na msukumo mkubwa wa kutaka kuanza na kuna nyakati nadhani walikuwa wanahisi kama vile upande wetu unachelewa. Hata wiki iliyopita Waziri wa Mambo ya Nje wa Oman alinipigia simu kuelezea wasiwasi wake kwa nini uzinduzi umecheleweshwa. Nikamhakikishia kuwa hakuna mabadiliko.
Bahati nzuri miradi yote miwili katika mradi mkubwa wa Eneo Maalum la Kiuchumi la Bagamoyo ni sehemu ya miradi ya kimkakati kitaifa. Kwa mfano, Mradi wa Bandari ya Bagamoyo ni kati ya miradi iliyoainishwa na Mamlaka ya Bandari Tanzania (TPA) kama mradi wa kipaumbele kwenye Mpango Kabambe wa Miaka 20 wa Kuendeleza Bandari Nchini (Tanzania Ports Master Plan 2008-2028). Mradi wa Ujenzi wa Bandari ya Bagamoyo ulianishwa baada ya uchambuzi kuonesha kwamba Bandari ya Dar es Salaam itafikia ukomo wa upanuzi wake baada ya miaka michache ijayo.
Sambamba na mpango wa TPA, Mamlaka ya Uzalishaji Bidhaa kwa Mauzo ya Nje (EPZA) nayo ilikuwa na mpango mkakati wa kuanzisha eneo la kujenga viwanda vya kuzalisha bidhaa za kuuza nje ya nchi hapa hapa. EPZA ilianisha eneo la Hekta 9,800 kwa ajili ya ujenzi wa Mji wa Viwanda Wilayani Bagamoyo ikijumuisha eneo la Hekta 800 kwa ajili ya Ujenzi wa Bandari mpya ya kisasa. Aidha, zitajengwa barabara na reli kuiunganisha bandari hiyo na barabara na reli nchini.
Wageni Waalikwa,
Mabibi na Mabwana;
Utekelezaji wa miradi hii miwili ulihitaji mtaji mkubwa kwa maana ya rasilimali fedha na teknolojia ya kisasa ambavyo kwetu ingetuchukua muda mrefu kupata. Hii ilitulazimu kutafuta marafiki wenye ujuzi, uzoefu na uwezo wa kutekeleza miradi ya aina hii. Kama nilivyokwisha eleza, Waziri Mkuu alilipatia ufumbuzi suala hili alipotembelea China. Lilikamilika wakati wa ziara ya Mheshimiwa Xi Jinping Rais wa China alipofanya ziara hapa nchini mwaka 2013, tuliposhuhudia utiaji saini wa Mkataba wa Ushirikiano wa Kimkakati (Framework Agreement on Strategic Partnership).
Kama nilivyokwisha dokeza, rafiki zetu wa Serikali ya Oman nao wakajiunga kwenye Mradi huu kupitia Mfuko maalum wa Uwekezaji wa Serikali ya Oman (SGRF). Kitendo hicho kimeupa mradi uwezo mkubwa wa kutekelezwa. Kwa kweli kilichochelewesha mradi kuanza ni pamoja na kutaka kuwa makini katika mazungumzo ; na kukawia kwetu kukamilisha fidia na uhamishaji wa wananchi wanaopisha mradi.
Fidia kwa Wananchi
Wageni Waalikwa,
Mabibi na Mabwana;
Taarifa kutoka Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari Tanzania zinaonesha kuwa asilimia 94.1 ya Wananchi wanaodai fidia wamelipwa. Jumla ya Wananchi 2,211 ndio watakaopisha mradi huu na kati ya hao, 2,081 wamelipwa fidia. Eneo mbadala la makazi lenye ukubwa wa hekta 296 limepatikana katika eneo la Kidagoni. Taratibu za kupima na upatikanaji wa hati zinaendelea kufanywa na Mamlaka husika.
Hata hivyo, zipo taarifa za manung’uniko za watu kutolipwa fidia inayostahili kwa ardhi yao na mazao yao. Nataka jambo hili lihakikiwe vizuri ili wananchi walipwe stahili zao. Serikali haiwezi kudhulumu wananchi wake. Kikosi kazi maalum kiundwe kwa ajili hiyo. Ofisi ya Waziri Mkuu iongoze na kazi ifanyike mara moja ili tusichelewe zaidi.
Shabaha ya Serikali ni kuhakikisha kwamba Wananchi wanaopisha mradi wanakuwa na hali bora zaidi ikilinganishwa na hali yao kabla ya mradi. Tunategemea pia kuwa wananchi hao hao ndio watanufaika na miradi hii moja kwa moja ikiwa ni ajira na shughuli za kibiashara.
Mafanikio ya Sera za Uchumi Jumla na Uwekezaji
Wageni Waalikwa,
Mabibi na Mabwana;
Utekelezaji wa mradi huu wa ni matokeo ya Sera zetu rafiki za uchumi jumla na uwekezaji zinazochochea ukuaji wa uchumi na kuvutia uwekezaji mkubwa. Kutungwa kwa Sera na Sheria kuhusu ubia kati ya serikali na sekta binafsi (Public Private Partnership) ndiko kulikotufikisha hapa. Hatua hizo pamoja na uwekezaji mkubwa tuliofanya kwenye miundombinu, nishati na huduma kumeweka mazingira mazuri ya kuvutia uwekezaji nchini. Ndio maana marafiki zetu wa China na Oman wameweza kuamua kuwekeza mradi huu mkubwa wenye thamani ya dola za kimarekani milioni 10 hapa nchini.
Safari ya Kuelekea Uchumi wa Viwanda
Mabibi na Mabwana;
Uzinduzi wa mradi huu ambao ujenzi wake unakadiriwa kuchukua miaka 3 kukamilika, unafanyika wakati ambapo nchi yetu inaanza safari ya ujenzi wa uchumi wa viwanda ambao ni daraja la kutufikisha kwenye nchi ya uchumi wa kati ifikapo mwaka 2025. Kama mnavyofahamu, kuanzia mwaka wa fedha 2016 - 2020, Serikali itaanza kutekeleza Mpango wa Pili wa Miaka 5 wa Maendeleo unaojikita katika kuchochea mapinduzi ya viwanda.
Habari njema zaidi ni kuwa, Tanzania ni moja ya nchi tatu zilizochaguliwa na China barani Afrika katika mpango wake wa kuendeleza viwanda barani Afrika unaotarajiwa kuanza mwaka 2016-2018. Nchi nyingine zilizochaguliwa ni Msumbiji na Ethiopia. Hivyo, utekelezaji wa mradi huu umeanza wakati muafaka kabisa. Pia Bandari itafaidika na fursa ya kuwepo kwa soko kubwa la mizigo kufuatia ujenzi wa reli mpya ya upana wa kimataifa unaotarajiwa kuanza wakati wowote kutokea sasa.
Mradi wa Eneo Maalum la Uchumi Bagamoyo
Wageni Waalikwa,
Mabibi na Mabwana;
Mradi huu wa Eneo Maalum la Uchumi utaigeuza Bagamoyo kuwa Jiji la Viwanda (Industrial City) ambapo Eneo Maalum la Viwanda (Portside Industrial Zone) lenye ukubwa wa Hekta 1,700 lina uwezo wa kujengwa viwanda zaidi ya 1,000. Bandari ya Bagamoyo itatuwezesha kuitumia vyema fursa yetu ya kijiografia na kuongeza ushindani wa kiuchumi katika ukanda wa Afrika Mashariki na Kusini. Bandari ya Bagamoyo itaifanya Tanzania kuwa lango kuu la biashara ya kimataifa na kuwa kichocheo cha mageuzi ya kiuchumi kwa Tanzania na nchi nyingine za Ukanda wa Mashariki, Kati na Kusini mwa Afrika.
Tafiti mbalimbali za Mwenendo wa Uchumi wa Dunia na Biashara za Kimataifa zinaonesha kwamba kwa miaka ijayo zaidi ya asilimia 60 ya biashara ya kimataifa itakuwa kwenye Bahari Kuu ya Hindi. Hivyo, Bandari ya Bagamoyo inakuja wakati muafaka kwa kuzingatia kwamba Bandari ya Dar es Salaam itafikia ukomo wake wa upanuzi miaka michache tu ijayo. Ule umaarufu wa Bagamoyo uliovuma kati ya karne ya 14 na 15 utarudi tena. Historia inajirudia lakini kwa sifa njema.
Wageni Waalikwa;
Mabibi na Mabwana;
Kwa sasa hivi uwezo wa kuhudumia mizigo katika bandari zetu tatu yaani Dar es Salaam, Tanga na Mtwara ni tani milioni 11.49 na kontena 600,000. Jumla ya wafanyakazi wa kudumu 3,240 wameajiriwa na vibarua kwa kazi za kutwa ni wastani wa 1,520. Kama ilivyoelezwa bandari hii ya Bagamoyo tunayoizindua leo ujenzi wake unategemea kuongeza uwezo wa kuhudumia mizigo kwa tani 600,000 na makasha 1,000,000 (Tani milioni 6). Inategemewa kuajiri wafanyakazi wapatao 1,000. Haya yote yamepangwa kutokea katika awamu ya kwanza inayoishia mwaka 2030. Uwezo wetu utaongezeka na kufikia tani 12.09 milioni na makasha 1,600,000.
Uendelezaji wa Bandari Zilizopo
Mabibi na Mabwana;
Serikali inaendelea pia kuchukua hatua za kuongeza uwezo wa bandari zetu katika upande wa kuhudumia mizigo na makasha kufikia kiwango cha juu kabisa katika miaka mitano ijayo. Hatua tunazochukua kwa kushirikiana na wadau kadhaa wa maendeleo na kwa kutumia pesa zetu wenyewe zinategemea kuongeza uwezo wetu kufikia takribani tani milioni 65 katika kipindi cha miaka mitano ijayo. Kwa Dar es Salaam pekee tutaruka mara 3 ya uwezo uliopo sasa hivi. Lakini pia kwa Mtwara tunategemea kuongeza tani 500,000 na makasha 300,000 baada ya maegesho manne yanayotegemewa kujengwa kukamilika. Vilevile ile jeti ya Dangote itakuwa na uwezo wa kuhudumia tani milioni 4.
Ushindani wa Bandari Nyingine
Wageni waalikwa;
Mabibi na Mabwana;
Ujenzi wa bandari hii na upanuzi wa bandari zetu tatu za Mtwara, Dar es Slaaam na Tanga utakapokamilika utaiweka nchi yetu kwenye nafasi nzuri ya ushindani mkubwa katika mwambao wa Afrika Mashariki ikizingatiwa kuwa tofauti na wenzetu, jiografia imetupendelea sisi zaidi kwa kupakana na nchi nyingi zisizo na bandari.
Wito kwa Watanzania
Mabibi na Mabwana;
Wito wangu kwa Watanzania ni kufanya mambo makubwa mawili. Kwanza, kudumisha amani na utulivu maana uwekezaji wote huu na utakaokuja baada ya kukamilika miradi hii kunategemea sana utulivu na amani ya nchi yetu. Hii itategemea pia na namna tutakavyochagua katika uchaguzi mkuu huu. Tuchague Chama na kiongozi ambaye hatavuruga utulivu wetu na ule wa Sera zetu za uchumi. Pili, tujiandae kuitumia fursa nyingi zitakazokuja kwa sababu ya uwekezaji katika Eneo Maalum la Kiuchumi la Babamoyo. Tujiandae kuwa washiriki na wadau kikweli kweli. Sekta binafsi nchini ichangamkie fursa za kuwekeza kwenye miradi ya viwanda na huduma kwa viwanda vitakavyowekezwa hapa. Pia kutajengwa mji mkubwa hivyo mjiandae kwa ujenzi wa majengo ya ofisi na makazi yatakayohitajika. Wananchi hamna budi kujiendeleza kwa elimu na stadi za kazi ili muweze kupata ajira na kuanzisha shughuli zitakazonufaika na kuwepo kwa bandari na mji wa viwanda, biashara na huduma nyinginezo.
Ahadi ya Serikali
Mabibi na Mabwana;
Serikali inaahidi kutekeleza wajibu wake kama ulivyo kwenye mkataba wa uwekezaji huu. Tutaendelea na azma yetu ya kuleta miundombinu katika eneo hili kuwezesha ujenzi wa bandari na viwanda kwenda kwa pamoja na kukamilika kwa wakati. Milango yetu iko wazi na tutafanya kila lililo ndani ya uwezo wetu kufanikisha mradi huu kwa wakati. Pale itakapobidi tutashirikiana na wabia wetu kuona uwezekano wa kugharamia ujenzi wa miundo mbinu kwa ubia. Sekta binafsi inakaribishwa katika uendelezaji wa mradi chini ya utaratibu wa Public Private Partnership (PPP).
Hitimisho
Wageni Waalikwa;
Mabibi na Mabwana;
Napenda kuwashukuru tena wabia wetu wa kutoka China na Oman katika utekelezaji wa Mradi. Ni matumaini yangu kwamba utekelezaji wa mradi utazingatia mgawanyo wa majukumu wenye tija kwa pande zote. Ni matarajio yangu pia kwamba utekelezaji wa Mradi utachangia kwa kiasi kikubwa kukuza uhusiano wa kidugu, kidiplomasia na wa kihistoria uliodumu kwa miaka mingi kati ya Tanzania, Jamhuri ya Watu wa China na Oman. Nastaafu kwa amani na furaha kuwa kwa kuanza kwa miradi ya kusafirisha gesi asilia, uzalishaji wa umeme kwa kutumia gesi asilia, ujenzi wa bandari ya eneo maalum la kiuchumi la Bagamoyo, mradi ya makaa ya mawe wa Mchuchuma na mradi wa chuma kule Liganga na miradi kadhaa ya miundombinu ya barabara, reli na viwanja vya ndege, ninaiacha nchi katika hatua ya kuwa tayari kupaa kuelekea kwenye uchumi wa kati.
Baada ya kusema maneno hayo mengi, sasa natamka kuwa ujenzi wa bandari ya Bagamoyo na ukanda maalum wa kiuchumi umezinduliwa rasmi.
Asanteni sana kwa Kunisikiliza.
- Oct 14, 2015
Hotuba ya Mheshimiwa Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, kwenye sherehe ya kilele cha mbio za Mwenge wa Uhuru, kumbukumbu ya Ba...
Soma zaidiHotuba
Mheshimiwa Dkt. Fenella Mukangara, Waziri wa Habari,
Vijana, Michezo, Utamaduni na Michezo;
Mheshimiwa Zainabu Omar Mohamedi, Waziri wa Uwezeshaji, Ustawi wa Jamii, Vijana Wanawake na Watoto – Zanzibar;
Mheshimiwa Chiku Gallawa, Mkuu wa Mkoa wa Dodoma;
Waheshimiwa Mawaziri na Naibu Mawaziri;
Waheshimiwa Wabunge na Wajumbe wa
Baraza la Wawakilishi;
Ndugu Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Dodoma;
Waheshimiwa Wakuu wa Mikoa Kutoka Tanzania
Bara na Zanzibar;
Makatibu Wakuu Kutoka Wizara Mbalimbli Tanzania
Bara na Zanzibar;
Waheshimiwa Mabalozi na Wawakilishi wa Mashirika
ya Kimataifa;
Waheshimiwa Viongozi wa Vyama Mbalimbali vya Siasa;
Viongozi Wetu wa Kiroho Kutoka Katika Madhehebu
Mbalimbali;
Vijana Wetu;
Ndugu Wananchi;
Mabibi na Mabwana;
Nawashukuru Mawaziri wetu Mheshimiwa Fenella Mukangara wa Serikali ya Muungano na Mheshimiwa Zainabu Omari Mohamed wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar kwa kunialika kuja kushiriki katika sherehe za mwaka huu za kilele cha Mbio za Mwenge wa Uhuru. Napenda pia kutumia nafasi hii kumpongeza na kumshukuru Mheshimiwa Chiku Galawa, Mkuu wa Mkoa wa Dodoma na viongozi wenzake na wananchi wote wa Dodoma kwa kukubali kuwa mwenyeji wa sherehe hizi na kwa maandalizi mazuri. Tunawashukuru kwa mapokezi mazuri na kwa ukarimu wenu mkubwa.
Pongezi kwa Wizara na Wananchi
Pia, nawapongeza Mawaziri, Makatibu Wakuu, viongozi waandamizi na maafisa wa ngazi mbalimbali wa Wizara zetu hizi mbili husika kwa kazi kubwa na nzuri waliyofanya ya kuandaa na kusimamia utekelezaji wa programu ya Mbio za Mwenge wa Uhuru mwaka 2015. Kwa namna ya kipekee pia napenda kuwatambua, kuwashukuru na kuwapongeza Wakuu wa Mikoa, Wakuu wa Wilaya, Wakurugenzi, Watendaji wa Halmashauri na viongozi wa Majimbo, Kata, Shehiya, Vijiji na Mitaa kote nchini kwa kuziwezesha Mbio za Mwenge mwaka huu kufanyika kwa usalama katika maeneo yao.
Nawapongeza na kuwashukuru wananchi wote kwa jinsi walivyoupokea na kuukimbiza Mwenge katika maeneo yao. Nafarijika kuona hamasa ya wananchi juu ya Mwenge iko juu sana na kuwanyima wale wote wenye fikra hasi kuhusu Mwenge. Mwaka huu, Mwenge umekagua, kuzindua na kuweka mawe ya msingi kwa miradi yenye thamani ya shilingi bilioni 463.5. Haya ni baadhi tu ya manufaa ya Mwenge wa Uhuru.
Pongezi kwa Wakimbiza Mwenge
Ndugu wananchi;
Nawapongeza kwa namna ya pekee vijana wetu waliokimbiza Mwenge wa Uhuru kitaifa chini ya uongozi mahiri na makini wa Ndugu Juma Khatibu Chum. Nawapongeza kwa kazi kubwa na nzuri ya kukimbiza Mwenge kwa siku 168 kupitia Mikoa yote, Wilaya zote, Vijiji vingi na mitaa mingi kote nchini. Jukumu hili ni zito na lina changamoto nyingi. Linahitaji watu wenye moyo wa uvumilivu, ustahamilivu na kuwa tayari kujitoa na kulitumikia taifa. Kwa uzalendo wenu na mapenzi kwa nchi yenu hamkukata tamaa na kuweza kumaliza mbio hizi na kuufikisha Mwenge mikononi mwangu salama salmini. Napenda kuwahakikishia kuwa tumeona uongozi ndani yenu na uzalendo mkubwa. Majina yenu yatabaki katika historia ya nchi yetu.
Nawashukuru pia, kwa Risala yenu na kwa kunikabidhi Kitabu kikubwa chenye Risala za Utii za wananchi wa Tanzania. Tutazisoma zote na tutayafanyia kazi yale yenye kuhitaji hatua za kuchukua.
Umuhimu wa Mwenge katika Taifa letu
Ndugu Wananchi;
Umuhimu wa Mwenge wa Uhuru katika Taifa letu ni jambo linalolopaswa kurudiwa kuelezwa mara kwa mara bila kuchoka. Hatupaswi kubweteka maana kazi ya ujenzi wa moyo wa uzalendo na mapenzi ya raia kwa taifa lao haina ukomo. Kama nchi kubwa ambazo zimejitawala kwa zaidi ya karne moja zinaendelea na kazi hiyo seuze sisi nchi yenye umri wa nusu karne?
Ndugu wananchi;
Mwenge wa Uhuru uliwashwa kwa mara ya kwanza tarehe 9 Desemba, 1961 kwenye kilele cha mlima Kilimanjaro kutimiza ahadi ya Hayati Baba wa Taifa Mwalimu Julius Nyerere wakati wa kudai uhuru wa Tanganyika kwamba: “Sisi tunataka kuwasha Mwenge na kuuweka juu ya mlima Kilimanjaro, umulike hata nje ya mipaka yetu, ulete tumaini pale ambapo hakuna matumaini, upendo mahali palipo na chuki na heshima palipojaa dharau”.
Baada ya Uhuru ndipo utaratibu wa Mbio za Mwenge wa Uhuru ulipoanzishwa na kuendelea hadi sasa. Kimsingi mbio hizo zimeendelea kueneza ujumbe wa amani, umoja, mshikamano, utu na moyo wa uzalendo na kujitolea miongoni mwa Watanzania. Mambo hayo yamekuwa Tunu zinazolitambulisha nchi Tanzania na watu wake.
Ni mambo yasiyokuwa na chama wala itikadi. Sote yanatuhusu, kutugusa na kutunufaisha. Pamoja na kusema tunu hizo kila mwaka kumekuwepo na ujumbe maalum unaoakisiwa katika kauli mbiu. Mwaka huu kwa mfano kauli mbiu ni “tumia haki yako ya kidemokrasia na kupiga kura katika uchaguzi wa mwaka huu 2015”. Mtakubaliana nami kuwa ni ujumbe muafaka. Aidha katika Mbio za mwaka huu pia Mwenge hueneza ujumbe kuhusu mapambano dhidi ya UKIMWI, malaria, dawa za kulevya na rushwa. Masuala hayo yamekuwa yanazungumzwa kwa miaka kadhaa sasa kwa sababu ya umuhimu wake, bado yapo na kwamba mapambano yanastahili kuendelea dhidi ya changamoto hizo. Haya ni masuala ya kutafakari tunaposherehekea Mwenge wa Uhuru, kutafakari maisha na wosia wa Hayati Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere na kuamua juu ya mwelekeo na hatma ya nchi yetu kupitia sanduku la kura katika uchaguzi mkuu ujao.
Kumbukumbu ya Baba wa Taifa
Ndugu Wananchi;
Kama mjuavyo, katika siku ya leo, sambamba na sherehe za kumaliza Mbio za Mwenge wa Uhuru, ni siku ya kumbukumbu ya maisha ya Baba yetu wa Taifa, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere aliyeaga dunia siku kama ya leo miaka kumi na sita iliyopita. Hivyo leo ni siku ya kusherehekea maisha yake na kujikumbusha mchango wake na urithi uliotuachia kama taifa na kama Watanzania. Hayati Baba wa Taifa alikuwa ni mwalimu wetu. Katika maisha yake ya uongozi hata baada ya uongozi ameendelea kuwa alama ya ushujaa, umoja wetu, uadilifu na uongozi uliotukuka. Jambo linalotia faraja ni kuwa, sote tunakubaliana kuwa Mwalimu Nyerere ndio kipimo cha uongozi bora katika nchi yetu.
Bahati nzuri, kumbukumbu ya Mwalimu Julius Kambarage Nyerere mwaka huu inaadhimishwa siku 10 tu kabla ya Uchaguzi Mkuu wa Rais na Wabunge, Wawakilishi na Madiwani nchini kwetu. Hivyo ni wakati muafaka sana kutafakari kwa wosia wake kuhusu uongozi na uchaguzi katika nchi yetu.
Baba wa Taifa Mwalimu Nyerere ametuachia wosia muhimu kuhusu watu wanaofaa kuchaguliwa kuongoza nchi yetu katika hotuba zake na maandishi yake mbalimbali. Kimsingi alitutaka Watanzania tutambue kuwa hatima ya nchi yetu inategemea aina ya viongozi tulionao. Alisisitiza umuhimu wa kuwa na viongozi watakaojenga umoja wa taifa letu na uadilifu. Kwa ajili hiyo alituusia kuchagua viongozi watakaodumisha Muungano wetu na kuwawezesha Watanzania kuishi pamoja kidugu wakiwa na mshikamano na ushirikiano licha ya tofauti zao za dini, rangi, kabila au mahali watokako. Alisisitza sana uadilifu wa viongozi kwa ajili hiyo alituasa bila kumung’unya maneno kuwaogopa kama ukoma watu wanaotaka kwenda Ikulu kwa kutumia agenda za utanganyika na uzanzibari, udini, ukabila, ubaguzi wa rangi na kwa kutumia rushwa.
Ndugu zangu, Watanzania wenzangu;
Leo hii baada ya zaidi ya wiki sita za kampeni za uchaguzi na zinapoingia katika siku 10 za mwisho tumeshapata nafasi za kuwasikiliza watu wanaoomba kutuongoza na vyama vyao. Bila ya shaka tunawatambua nani ni nani? Naomba tuutumie Uchaguzi Mkuu huu kumuenzi Baba wa Taifa kwa vitendo kwa kuwakataa viongozi ambao wamekiuka wosia wake. Badala yake tuwachague viongozi watakaosaidia kuziba zile nyufa kuu nne za taifa letu alizozizungumzia kabla ya uchaguzi wa mwaka 1995. Kwa kufanya hivyo, tutakuwa si tu tumemuenzi bali tumejinusuru sisi wenyewe na nchi yetu dhidi ya laana na majuto yanayoweza kutupata tukiupuuzia wosia wake. Wapo wagombea wanaodiriki kuomba kuchaguliwa kwa sababu ya kuwa dini fulani au madhehebu fulani. Wapo wapiga debe wa mgombea fulani waliothubutu kuomba watu wa kabila fulani kumpigania na kumpigia kura mgombea fulani ati kwamba wanamaslahi na mgombea huyo. Hatuchagui mgombea wa kunufaisha kabila bali Watanzania wote. Wapo wagombea ambao wameshindwa kukemea rushwa je tunawaelewaje? Wako tayari kupambana na rushwa? Hapana. Bila ya shaka wao ni sehemu ya tatizo. Bila ya shaka pia wao wanatumia rushwa kupata uongozi. Tarehe 25 Oktoba, 2015 tuwakatae.Watu wa aina hii ni balaa na janga. Tuliepushe taifa na watu wa aina hiyo.
Uchaguzi Mkuu
Ndugu wananchi;
Jukumu lililo mbele yetu sote tuliojiandikisha ni kujitokeza bila ya kukosa kupiga kura tarehe 25 Oktoba, 2015 tukiwa na vitambulisho vyetu vya mpiga kura mkononi. Bila ya hivyo hutapiga kura yako. Napenda kutumia nafasi hii kuwakumbusha kutunza vitambulisho vyenu kwani bila kuwa navyo hutapiga kura. Nasikitishwa sana na taarifa kuwa wapo watu wanaouza vitambulisho vyao. Natamani habari hiyo iwe ni uvumi tu. Lakini kama ni kweli nawashangaa sana watu hao. Kwa nini ukubali kupoteza haki yako ya msingi ya kuchagua kiongozi wako umtakae? Nawashangaa zaidi wale wanaonunua. Hivi hiyo ndiyo maana ya kudumisha demokrasia huko? Naomba wajue kuwa wanatenda kosa la jinai. Vyombo vya dola vinawasaka watakapopatikana watafikishwa mbele vya vyombo vya sheria. Na hili litawahusu wote waliouza na kununua. Kipengele cha 2.3.1 (e) kinasema; “kila chama cha siasa kinachoshiriki katika uchaguzi kina wajibu wa kufuata na kutekeleza maamuzi na maelekezo ya Tume”.
Amani na Usalama wakati wa Uchaguzi Mkuu
Ndugu wananchi;
Napenda kuwakumbusha kuwa zoezi la uchaguzi linasimamiwa kwa mujibu wa Katiba na Sheria za nchi ambazo zinaelekeza kuwa Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) na Tume ya Uchaguzi ya Zanzibar (ZEC) ndizo pekee zenye mamlaka ya kuendesha na kusimamia uchaguzi. Nawaomba ndugu zangu tuheshimu kauli na maelekezo ya tume hizo. Hivi karibuni baadhi ya viongozi wa vyama vya upinzani wametoa maelekezo kwa wafuasi wao kutaka wakishapiga kura wakae mita mia kulinda kura zao. Tume ya Uchaguzi imetoa tamko kwamba kufanya hivyo ni kinyume cha sheria. Wameeleza kwa usahihi kabisa kwamba wanaosimamia na kulinda kura za wagombea na vyama vyao kwa mujibu wa sheria ni mawakala wa wagombea na si mtu mwingine yeyote. Wao wapo ndani ya vyumba vya kupigia kura kwa ajili hiyo. Hivyo basi wafuasi wa vyama vya siasa msikubali kuchuuzwa na viongozi wenu kwa kuwaambia msiondoke vituoni kwa madai ya kulinda kura zenu. Kwanza mnazilindaje, kura zinazopigwa na kuhesabiwa ndani ya chumba cha kupigia kura.
Hapana shaka wenzetu wana dhamira mbaya na wanachotaka ni kuhamasisha uvunjifu wa sheria. Wana lao jambo lenye shari ndani yake. Hebu tujiulize, hivi ikiwa wapiga kura 22,751,292 wa bara na 503,193 wa Zanzibar watabaki kituoni kulinda kura za vyama vyao, je patatosha?
Narudia kusisitiza: Unailindaje kura yako ukiwa umbali wa mita mia moja wakati kura zinapigwa na kuhesabiwa ndani ya vituo vya kupigia kura? Mlinzi wa uhakika wa kura ni wakala wa Chama chake aliyeko ndani ya chumba cha Kupigia Kura. Tume imeshaelekeza kuwa aliyekwishapiga kura aondoke kituoni, naomba agizo hilo liheshimiwe. Anayekaidi hatavumiliwa, hatua za kisheria zitachukuliwa dhidi yake bila ya kusita. Msilazimishe Serikali kufanya yale ambayo yasiyopendeza. Lakini hapana budi na kwa maslahi ya taifa hatutoacha kutimiza wajibu wetu.
Ndugu Wananchi;
Hizo ni njama za kuleta vurugu na kutaka kuwazuia watu wengine kupiga kura. Nataka kuwahakikishia kuwa njama zao na nia yao ovu zimeshajulikana na katu hazitofanikiwa. Sisi kwa upande wetu wa vyombo vya ulinzi na usalama tumejipanga vizuri kuhakikisha kuwa agizo la Tume linatekelezwa kwa ukamilifu. Wale wanaotaka kufanya fujo watadhibitiwa ipasavyo bila ajizi wala kuonewa muhali. Upo usalama na ulinzi wa kutosha kuhakikisha kuwa kila mmoja mwenye sifa ya kupiga kura atapiga kura bila ya bughudha. Wale wenye nia ya kufanya fujo na kukaidi maelekezo halali wana hiyari ama ya kutiii sheria na taratibu au kukabiliana na mkono wa sheria kwa nguvu ile ile watakayoitumia wao. Kamwe hatutaruhusu, demokrasia kutekwa nyara. Kamwe hatutawapa nafasi ya kuivuruga nchi yetu. Wahalifu hawana kinga.
Mapambano dhidi ya UKIMWI
Ndugu Wananchi;
Ujumbe wa Mwenge umeendelea kusisitiza mapambano dhidi ya UKIMWI. Mwaka huu, kauli mbiu ni “Vijana wa leo na UKIMWI- Wazazi Tuwajibike”. Ni ujumbe unaokumbusha wajibu wa wazazi na walezi katika vita dhidi ya maambukizi mapya. Katika kipindi cha miaka 10 ya uongozi wangu, tumepata mafanikio ya kutia moyo katika vita dhidi ya UKIMWI.
Maambukizi ya VVU/UKIMWI yamepungua kutoka asilimia 7 mwaka 2007 hadi asilimia 5.1 mwaka 2012. Tumeongeza uwezo wetu wa kupima na kutambua virusi vya UKIMWI ambapo leo tuna vituo vya upimaji wa hiyari na ushauri nasaha (VCT) 2,929 ikilinganishwa na 96 mwaka 2005. Watu waliopima VVU/UKIWMI kuanzia 2005 mpaka sasa wamefikia 25,048,908. Hali kadhalika idadi ya wanaofaidika na huduma ya dawa za kufubaza (ARVs) nayo imeongezeka kutoka 16,167 mwaka 2005 hadi 1,904,000 mwaka 2015. Huduma ya kuzuia maambukizi ya mama kwenda kwa mtoto imeongezeka kutoka vituo 544 mwaka 2005 hadi 5,361 mwaka 2015.
Ndugu wananchi;
Mafanikio haya hayatupi sababu ya kubweteka maana maambukizi mapya bado yapo na yanaathiri zaidi vijana na hasa vijana wa kike. Inakadiriwa kuwa tunao wagonjwa wa UKIMWI milioni 1.4 nchini. Wito wa ujumbe huu wa mwaka huu ni kuwakumbusha wazazi na walezi wajibu wenu. Mnapaswa kuvunja ukimya na kuzungumza na vijana wenu kuhusu hatari inayonyemelea ujana wao, kuwaelemisha juu ya kujitunza na kuepuka mitego ya maisha inayoweza kuwaingiza katika tatizo hili. Huu ni wajibu ambao hamna mtu mwingine wa kumkasimisha, maana vijana wetu wanaishi katika kaya zenu.
Vita dhidi ya Malaria
Ndugu Wananchi;
Tuliendesha Mapambano dhidi ya malaria kwa nguvu kubwa na mafanikio ya kutia moyo katika miaka 10 ya uongozi wangu. Nafurahi kuwa kutokana na jitihada zetu tulizofanya na hatua tulizochukua zikiwemo usambazaji wa vyandarua vyenye dawa; kupulizia dawa ukoko majumbani na matumizi ya dawa mseto tumeweza kupunguza maambukizi ya malaria kutoka asilimia 18 mwaka 2007 hadi asilimia 10 mwaka 2012, na vifo vitokanavyo na malaria kutoka watu 41 kwa vizazi hai 100,000 mwaka 2004 hadi watu 12 kwa vizazi hai 100,000 mwaka 2014. Kwa upande wa Zanzibar, kutokana na jitihada kama hizo, haswa ila ya kupulizia mazalia ya mbu, wameweza kutokomeza malaria ambako sasa kiwango cha maambukizi ni asilimia 0.2.
Ndugu wananchi;
Jambo muhimu tulilofanya ambalo litatupa ushindi wa kudumu dhidi ya malaria ni kujengwa kwa Kiwanda cha Kutengeneza Madawa ya Viuadudu pale Kibaha. Kiwanda hiki kitazalisha madawa ya kupulizia kwenye mazalia ya mbu na hasa kuua viluviluvi vya mbu. Tutang’oa mzizi wa fitina wa malaria kwani hatimae mbu hawatakuwepo.
Vita Dhidi ya Dawa za Kulevya
Ndugu Wananchi;
Tunaendelea kupata mafanikio katika mapambano dhidi ya dawa za kulevya. Haya ni mapambano makali ambayo hatuna budi kupambana kweli kweli mpaka tushinde. Dawa hizi za kulevya zinaathiri zaidi vijana wetu na kudhoofisha nguvu kazi muhimu ya taifa la leo na kesho. Aidha, ni kichocheo kikubwa cha vitendo vya uhalifu.
Ndugu wananchi;
Bahati nzuri, tofauti na ilivyokuwa huko nyuma, sasa walioathirika na dawa za kulevya wanaweza kupata matibabu na kupona. Nafurahishwa na kauli mbiu ya Mwenge mwaka huu isemayo, “Uteja wa Dawa za Kulevya Unazuilika na Kutibika; Chukua Hatua”. Inahamasisha watumiaji wa dawa za kulevya kuchukua hatua na kupata tiba. Hali kadhalika, inakumbusha wajibu wetu sote kuwasaidia wale walioathirika kwa kuhakikisha kuwa wanapata ushauri nasaha na tiba ambazo zinatolewa katika vituo vya serikali tena bila gharama yoyote.
Serikali imeendelea kutoa huduma katika vitengo vya afya ya akili vilivyopo Mirembe na Lutindi. Vitengo kama hivi vimeanzishwa pia katika hospitali Muhimbili, Mwananyamala na Temeke. Sasa tunajenga Kituo cha Matibabu cha kisasa cha Waathirika Madawa ya Kulevya hapa Itega, Dodoma ambacho kitakuwa kituo kikubwa kuliko vyote nchini. Kutokana na juhudi hizi, nchi yetu imekuwa nchi ya kwanza Kusini mwa jangwa la Sahara kuanzisha huduma hii kwenye mfumo wa afya ya jamii (public health).
Ndugu wananchi;
Upande wa pili wa mapambano dhidi ya biashara ya dawa za kulevya yaliendelea kwa nguvu. Huku nako tumepata mafanikio ya kutia moyo. Kati ya mwaka 2010 mpaka 2014 jumla ya kesi za dawa za kulevya 40,930 zilitolewa taarifa polisi. Kati yake kesi 22,167 zilifikishwa Mahakamani, kesi 18,763 zinaendelea kufanyiwa uchunguzi na kesi 1,082 zimekamilika. Kati ya mwaka 2005 na 2014 tumefanikiwa kukamata watuhumiwa 1,704 wa cocaine, wahutumiwa 2,149 wa heroine na watuhumiwa 5,462 wa mirungi. Mafanikio makubwa kuliko yote ni yale kukamatwa kwa kilo 211 za heroine mkoani Lindi mwaka 2012 kikiwa ni kiasi kikubwa zaidi kuwahi kukamatwa Barani Afrika.
Ndugu Wananchi;
Tumekwenda mbali zaidi kukabiliana na mtandao wa uuzaji na usafirishaji wa dawa za kulevya. Naweza kusema kuwa tumewadhibiti kwa kiasi kikubwa mtandao huu na sasa wamebanwa kweli kweli. Tumeongeza uwezo wetu wa kupambana na biashara ya madawa ya kulevya kwa kuipitia upya na kuibadili Sheria ya Kudhibiti Biashara ya Dawa za Kulevya ya mwaka 1995 na kutunga Sheria mpya ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya Namba 5 ya mwaka 2015, iliyoanza kutumika rasmi tarehe 15 Septemba, 2015. Sheria hiyo pamoja na kuongeza makali ya adhabu ya makosa ya madawa ya kulevya, imeanzisha Mamlaka mpya yenye uwezo wa kupeleleza, kupekua na kukamata watuhumiwa wa dawa za kulevya. Awali, Tume kwa muundo wake, ilitegemea zaidi ushirikiano wa Polisi na mamlaka nyingine kutekeleza wajibu wake. Serikali itaendelea kuiwezesha Mamlaka hii kufanya kazi yake ipasavyo. Tunachoomba kutoka kwenu ni ushirikiano wenu. Vita hii tutashinda.
Mapambano Dhidi ya Rushwa
Ndugu Wananchi;
Tumeendelea na mapambano dhidi ya rushwa na mafanikio yameendelea kupatikana katika kipindi cha miaka 10. Hatua za kisera na kisheria tulizochukua ikiwemo kubadilisha Sheria iliyokuwapo ya Kupambana na Rushwa, kuongeza idadi ya makosa kutoka 4 hadi 24, kujenga uwezo wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) kwa mafunzo, rasilimali watu na vitendea kazi kwa pamoja zimeongeza kasi ya kupambana na rushwa. Katika kipindi cha miaka 10, zimefunguliwa kesi 2,185 Mahakamani, watuhumiwa 611 wametiwa hatiani na fedha kiasi cha shilingi bilioni 93, 410,572, 117 kimeokolewa na kesi 658 zinaendelea Mahakamani.
Nafurahi kuwa nimejenga msingi mzuri wa vita dhidi ya rushwa. Sina mashaka kuwa katika awamu ijayo vita hii itashika kasi zaidi hasa ikiwa mgombea wa Chama changu atashinda kwani amezungumzia kupambana na rushwa na kuahidi kuunda Mahakama Maalum ya Rushwa. Sina mashaka kuwa, uchaguzi huu tutachagua wale wagombea wanaozungumza lugha ya kupambana na rushwa kwa maneno, nyuso zao na vitendo. Viongozi wasioionea rushwa haya. Hii ndio siri ya kuikabili rushwa. Inawezekana, timiza wajibu wako tarehe 25 Oktoba, 2015.
Wiki ya Vijana
Ndugu Wananchi;
Nimepata fursa ya kutembelea mabanda ya maonyesho ya shughuli za vijana katika viwanja vya barafu. Nimeguswa sana na ubunifu wao na ari yao ya kujikwamua kwa kujiajiri badala ya kungoja kuajiriwa. Mahitaji yao makubwa ni kuwezeshwa tu ili waweze kupanua shughuli zao na kuajiri vijana wenzao.
Katika kipindi cha miaka 10 iliyopita tumejitahidi kutoa fursa kwa vijana na kuchochea maendeleo yao kupitia Mfuko wa Maendeleo ya Vijana. Mwaka 2005 Mfuko huu ulikuwa na kiasi cha shilingi milioni 100,000,000 mwaka 2005 na sasa bajeti yake imefikia shilingi bilioni 6,000,000,000 na umefaidisha vijana 10,241. Mwaka jana katika sherehe za Mwenge kule Tabora, nilizikumbusha Halmashauri zote za Wilaya na Miji kutekeleza kwa ukamilifu agizo la kutenga asilimia 10 ya mapato yao kwa mwaka kwa ajili ya shughuli za maendeleo ya Vijana na Wanawake. Nafurahi kuwa zimejitahidi kufanya hivyo na mwaka huu wa fedha zilitengwa kiasi cha shilingi bilioni 1.5 kwa ajili ya mfuko huo. Natambua kuwa mahitaji ya fedha yameongezeka sana kutokana na mwamko ulioko sasa. Nina imani serikali ijayo italipa jambo hili kipaumbele zaidi. Muhimu vijana msikilize wagombea na vyama vyao kwa makini kisha mfanye maamuzi sahihi.
Hitimisho
Ndugu Wananchi;
Sherehe hizi za Mwenge ndizo zitakuwa sherehe za mwisho kwangu kushiriki nikiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Nafurahi kuwa katika kipindi chote cha uongozi wangu, Mwenge wa uhuru umeendelea kuwa na mafanikio na kuleta nuru zaidi, mshikamano zaidi matumaini zaidi na maendeleo zaidi kote ulikopita. Ninapoondoka rai yangu kwenu ni kuwa namna moja ya kumuenzi Baba wa Taifa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere, ni kuudumisha Mwenge huu wa Uhuru ambao aliuasisi yeye mwenyewe.
Nitumie pia fursa hii kuwasisitiza tena kujitokeza kupiga kura ili kuchagua viongozi mnaowataka. Narudia kuwahakikishia kwa mara nyingine tena usalama katika kipindi chote cha uchaguzi. Kila mmoja na atimize wajibu wake wa kulinda amani ya nchi yetu katika kipindi hiki.
Nawatakia kila la kheri katika shughuli zenu za kila siku.
Mungu Ibariki Tanzania!
Mungu Ibariki Afrika!
Ahsanteni sana kwa kunisikiliza.
- Oct 13, 2015
Hotuba ya Mheshimiwa Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, wakati wa ufunguzi wa kituo cha kufua Umeme cha Kinyerezi 1, tarehe 1...
Soma zaidiHotuba
Mheshimiwa George Boniface Simbachawene, Waziri wa
Nishati na Madini,
Dkt. Mighanda Manyahi, Mwenyekiti wa Bodi ya
Wakurugenzi wa TANESCO,
Mhandisi Felchesmi Mramba, Mkurugenzi Mtendaji wa
TANESCO,
Ndugu Wageni Waalikwa,
Mabibi na Mabwana.
Nawashukuru Mheshimiwa Waziri na uongozi wa TANESCO kwa kunialikana na kunishirikisha katika hafla hii muhimu ya uzinduzi wa Kituo cha Kufua Umeme cha Kinyerezi I. Natoa pongezi nyingi kwa TANESCO kwa kukamilisha mtambo huu mkubwa wa kufua umeme kwa kutumia gesi asilia nchini. Kuzinduliwa kwa kituo hiki baada ya uzinduzi wa kituo cha kuchakata gesi asilia kule Madimba, Mtwara, juzi tarehe 11 Oktoba, 2015, ndiyo uthibitisho wa kukamilika kwa uwekezaji mkubwa tulioufanya wa kujenga bomba la gesi kutoka Mtwara na Songosongo hadi Dar es Salaam.
Nilipokuja hapa 8 Novemba, 2012 wakati wa kuweka jiwe la msingi la ujenzi wa bomba la gesi asilia nilieleza kwamba, uamuzi wa kujenga bomba hilo lenye gharama kubwa uliotokana na matatizo ya uhaba mkubwa wa umeme tuliyopata mwaka 2006 na 2007. Chanzo chake kilikuwa mabwawa kukosa maji ya kutosha kwa sababu ya ukame mkali. Tuliridhika kuwa umeme wa nguvu ya maji hauaminiki hivyo tuelekeze nguvu kwenye vyanzo vingine vya nishati. Hali imejirudia.
Kama mlivyosema, kwa kawaida tunaingiza katika gridi ya taifa kiasi cha megawati 561 kutoka vyanzo vya maji. Lakini, kwa sasa vyanzo hivyo vinatoa MW 105 tu na kufanya upungufu wa Megawati zaidi ya 456. Kwa ajili hiyo mmelazimika kufunga mitambo ya bwawa la Mtera na mabwawa mengine ya Kidatu, Kihansi, Nyumba ya Mungu na New Pangani Falls yapo hatarini kufungwa kwani maji ni kidogo sana. Yapo kwenye kiwango kisichozidi mita moja juu ya viwango kinachoruhusiwa kuendesha mitambo ya kufua umeme.
Siku ile nilielekeza kuwa wakati bomba likiendelea kujengwa, kazi ya ujenzi wa vituo vya kufua umeme kwa kutumia gesi nao ufanyike. Shabaha yangu ilikuwa kwamba wakati bomba likifika Dar es Salaam mitambo ya kuzalisha umeme iwe inawashwa na umeme unapatikana majumbani, viwandani, maofisini na sehemu nyinginezo.
Ninafurahi kuona mmetekeleza maagizo yale na leo ninazindua mradi wa kufua umeme wenye uwezo wa hadi MW 150. Hata hivyo, bado ni chini ya matarajio yetu ya kuzalisha takribani MW 900 na ushei hapa Kinyerezi kama mlivyosema wenyewe. Kama mjuavyo katika Mpango wa Kwanza wa Maendeleo wa Miaka Mitano inatakiwa ifikapo mwaka 2015/16 Tanzania iwe na umeme wa MW 2780. Hivi sasa tunao uwezo wa kuzalisha MW 1490 na kuacha pengo la MW 1390. Hivyo basi kama hapa Kinyerezi tungepata hizo MW 900 na kuongeza umeme unaotarajiwa kuzalishwa pale Somanga Fungu na kwingineko tungefikisha lengo. Leo tunapata MW 150 hivyo bado MW 750 ambazo sijui zitapatikana lini?
Mheshimiwa Waziri;
Mwenyetiki wa Bodi;
Mkurugenzi Mtendaji;
Mimi kama walivyo Watanzania wengine tungependa kupata majibu ya uhakika kuhusu jambo hili muhimu kwa ustawi wa nchi yetu na watu wake. Nini kilichotufanya hivi sasa tusiwe na vituo vingine vya kufua umeme zaidi ya hii?. Au kwa nini hatuoni ujenzi wa vituo vingine ukiwa unaendelea. Jambo gani linalowatatiza? Nani anayewachelewesha? Kama halipo na kama hayupo je tatizo liko kwenu TANESCO. Waingereza wamesema: “Procrastination is an enemy of development”. Kwamba kuchelewa kufanya uamuzi ni adui wa maendeleo.
Mnaona sasa athari za kuchelewa kuamua? Ni hali ya wasiwasi tuliyonayo sasa kuhusu upatikanaji wa umeme. Naomba Bodi ya TANESCO ikae kwa dharura leo muizungumze hali hii na mtengeneze mpaka wa haraka wa kujenga vituo vingine. Ningependa kesho kutwa mnipe maelezo. Tukutane tarehe 16 Oktoba, 2015. Waziri endelea na kampeni. Bodi, Katibu Mkuu na Kamishina wa Nishati wanatosha.
Kama tungeongeza kasi ya ujenzi wa mitambo tusingekuwa na hofu tuliyonayo sasa.
Mheshimiwa Waziri;
Upatikanaji wa umeme nchini ni jambo ambalo tumelipa kipaumbele cha juu kwa sababu ya kutambua kuwa umeme ni kichocheo kikubwa cha kuleta maendeleo. Kwa ajili hiyo, tumefanya uamuzi wa kuongeza uzalishaji na usambazaji wa umeme nchini. Ujenzi wa bomba la gesi na uendelezaji wa miradi ya makaa ya mawe ya Mchuchuma na Kiwira ina lengo la kuongeza uzalishaji wa umeme. Katika kipindi hiki kupitia miradi mbalimbali pamoja na ile inayotekelezwa na Wakala wa Umeme Vijijini (REA) kazi kubwa ya kusambaza umeme mijini na vijijini imefanyika. Kwa kipindi hiki Watanzania wanaoweza kupata umeme wameongezeka kutoka asilimia 10 mwaka 2005 hadi asilimia 40 mwaka 2015. Tumeunganisha umeme kwa vijiji 5,336 kati ya vijiji 12,423 nchi nzima. Hali kadhalika miji mikuu ya Wilaya 13 zimeweza kupatiwa umeme. Miji hiyo imepatiwa umeme wa gridi ya Taifa au miradi ya jenereta za kutumia mafuta.
Mabibi na mabwana;
Nchi za Afrika bado zina uwezo mdogo sana wa uzalishaji wa umeme ukilinganisha na nchi zenye viwanda na uchumi mkubwa. Takwimu za uzalishaji umeme duniani za mwaka 2013 zilizotolewa na Macro Economy Meter, zinaonyesha kuwa uwezo wa Dunia ni MW 5,250,000. Nchi tano kubwa zinazalisha kiasi cha asilimia 55.3 ya uwezo wa dunia. Nchi hizo ni China MW 1,146,000, Marekani MW 1,039,000, Japan MW 287,000, Russia MW 223,100, na India MW 208,100.
Kwa upande wa Bara la Afrika, Afrika Kusini ndiyo inayoongoza ikiwa na MW 44, 260, ikifuatiwa na Misri MW 26,910, Algeria MW 11,330, Libya MW 6,766, Morocco MW 6,620, na Nigeria MW 5,600. Jumla ya uwezo wa nchi hizi kubwa barani Afrika ni MW 101,786 tu ambapo haufikii hata nusu ya uwezo wa India. Kwa Afrika Mashariki uwezo wetu bado mdogo sana, Kenya inazalisha MW 2,295, Tanzania MW 1,498, Uganda MW 850 na Rwanda MW 110.
Hali hii inatuonyesha kuwa bado tuna kazi kubwa ya kufanya na safari ni ndefu mpaka tufikie kukidhi mahitaji yetu ya umeme. Kwa nchi yetu ambayo imebahatika kuwa na vyanzo vingi vya kuzalisha umeme hii ni fursa ya aina yake ya kuzalisha umeme mwingi na kuwapatia majirani. Kenya na Rwanda wanapenda kununua umeme kutoka kwetu. Tena ni maombi ya siku nyingi na nimeshawaambia. Sijui ni nini kinachofanya muwe wazito wa kuamua kutumia fursa hiyo. Tafadhalini amkeni na mchangamkie fursa hizo.
Mabibi na Mabwana;
Nawapongeza tena TANESCO na Wizara ya Nishati na Madini kwa kukamilisha mradi huu wa kituo cha kufua umeme wa gesi. Ni matumaini yangu na ya Watanzania kuwa mtakamilisha, mapema iwezekanavyo kazi ya kuingiza MW 80 zilizobakia ili mgao upungue makali yake. Ongezeni kasi ili pengo lililopo mlizibe mapema iwezekanavyo. Shirikianeni na mamlaka husika ili tupate ufumbuzi wa kudumu wa tatizo la umeme nchini. Mimi naamini kila mtu akitekeleza ipasavyo wajibu wake na mkishirikiana tatizo la umeme litakuwa historia muda si mrefu.
Sasa ninayo furaha kubwa kutangaza kuwa Mtambo wa Kufua Umeme kwa Kutumia Gesi Asilia hapa Kinyerezi, Maarufu kwa jina la Kinyerezi 1, Umezinduliwa Rasmi!
Ahsanteni sana!
- Oct 10, 2015
Hotuba ya Mheshimiwa Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, kwenye uzinduzi wa Miundombinu ya kusafisha na kusafirisha Gesi asil...
Soma zaidiHotuba
Mheshimiwa George B. Simbachawene, Waziri wa Nishati na Madini,
Waheshimiwa Mawaziri,
Mheshimiwa Halima Dendego, Mkuu wa Mkoa wa Mtwara,
Waheshimiwa, Wakuu wa Mikoa ya Lindi, Pwani na Dar es Salaam,
Mheshimiwa Balozi wa China Nchini Tanzania,
Waheshimiwa Viongozi kutoka Jamhuri ya Watu waChina, CNPC, EXIM Bank na CPTDC,
Viongozi wa Kata ya Madimba na Vijiji vya jirani,
Waandishi wa Habari,
Wageni Waalikwa,
Mabibi na Mabwana!
Leo ni siku ya furaha tele. Hayawi hayawi yamekuwa. Hatimaye mradi umekamilika. Mradi huu una umuhimu wa aina yake. Unatuhakikishia kumaliza tatizo la uhaba wa umeme. Umeme wa maji sasa haukidhi haja tunategemea vyanzo vingine. Gesi asilia kikiwa chanzo kimojawapo. Mungu ametujalia gesi nyingi. Tuna wajibu wa kuitoa aridhini na kuisafirisha gesi.
Tunayo kila sababu ya kumshukuru Mwenyezi Mungu, mwingi wa rehema, kwa kutujaalia uzima na kutuwezesha kuishuhudia siku hii adhimu katika historia ya nchi yetu na hasa katika masuala ya uendelezaji wa sekta ndogo ya mafuta na gesi asilia. Kama mnavyofahamu utafutaji wa mafuta na gesi asilia hapa nchini ulianza mwanzoni mwa miaka ya 1950 na hatimaye Gesi Asilia iligunduliwa huko kisiwani Songo Songo mwaka 1974 na baadaye hapa Mnazi Bay mwaka 1982. Ugunduzi huu ulifanywa na Kampuni ya Agip ya Italia ambayo ilikuwa na Mkataba na Serikali ya Tanzania kuhusu Utafutaji wa mafuta.
Ndugu Wananchi,
Ugunduzi wa rasilimali kama hii unakuwa na tija pale inapotolewa ardhini na kutumika ipasavyo, na hivyo kuchangia kuleta maendeleo ya Taifa. Miaka ya 1970, rafiki zetu wa Italia walipoigundua gesi hii waliondoka na kuiacha kwa sababu za kibiashara kwa madai kuwa kiasi cha gesi kilichogunduliwa kilikuwa ni kidogo. Pamoja na madai hayo, Serikali yetu haikukata tamaa. Kwa mujibu wa Sheria ya Utafutaji na Uzalishaji wa Mafuta ya Mwaka 1980, Serikali ililipatia Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania (TPDC) jukumu la kuendeleza utafiti na utafutaji rasilimali hii kwenye maeneo yaliyoachwa na Kampuni hiyo kutoka Italia.
Matokeo ya shughuli za TPDC yakawa ni ugunduzi zaidi kwa kuchimba visima vya uendelezaji huko Songo Songo na baadaye Mnazi Bay. Matumizi ya gesi asilia ya Songo Songo yalianza Oktoba, 2004 na ya Mnazi Bay yalianza Mwaka 2006. Juhudi zaidi za utafiti zimekuwa zikifanywa na TPDC katika maeneo mbalimbali yakiwemo yale ya Bahari Kuu. Kuanzia Mwaka 2010 hadi sasa, umefanyika ugunduzi wa gesi nyingi baharini na hadi kufikia mwezi Juni, 2015 jumla ya kiasi cha gesi kilichogunduliwa kilifikia takriban futi za ujazo Trilioni 55.24 (Gas Initially in Place). Kiasi hiki kinajumuisha gesi iliyogunduliwa baharini na nchi kavu.
Ndugu Wananchi,
Kama mnavyofahamu, kihistoria ufuaji wa umeme nchini umekuwa ukitegemea kwa kiasi kikubwa, maporomoko ya maji kwenye mito ya Ruaha, Kihansi, Pangani na mingineyo. Kuanzia miaka ya 1990, Mito hii iliathirika na ukame hivyo kutoweza kukidhi mahitaji ya kufua umeme na kupelekea nchi yetu kutegemea umeme unaozalishwa kwa kutumia mafuta mazito na gesi kwa kiasi kidogo. Taifa lilitumia fedha nyingi sana kugharamia mafuta hayo mazito.
Changamoto ya kutumia gesi asilia ya kutosha kwa kuzalisha umeme ilikuwa ni udogo wa miundombinu iliyokuwepo, kwani baada ya miaka minne tu tangu ianze kutumika, mitambo ya Songo Songo ilikuwa haikidhi mahitaji ya kusafisha na kusafirisha gesi. Ili kutatua tatizo hilo, Serikali iliona ni busara kujenga mitambo na bomba jingine kubwa zaidi ili liweze kukidhi mahitaji yetu ya sasa na ya baadaye. Leo ninayofuraha kuzindua mitambo hii ikiwa ni miaka miwili tangu nilipoweka jiwe la msingi kwa ujenzi wa Miundombinu hii na ile ya kufua umeme pale Kinyerezi, Dar es Salaam. Na nimeambiwa kuwa leo hii ninapofanya uzinduzi tayari gesi imeishaanza kuchakatwa, kusafishwa na kusafirishwa kwenda Dar es Salaam ambako umeme umeanza kufuliwa. Kitendo hicho kitakuwa ni ukombozi mkubwa kwa taifa. Kukamilika kwa miundombinu hiyo na kuanza uzalishaji wa umeme kwa kutumia gesi ni hatua kubwa sana ya maendeleo kwa nchi yetu. Tumeanza safari ya uchumi wa gesi kwa uhakika. Wale wote waliokuwa wanabeza na kutilia shaka mipango na juhudi za serikali kwa hakika sasa wamepatwa na aibu. Hatua hii italeta mapinduzi makubwa katika shughuli za uzalishaji mali na upatikanaji wa huduma muhimu za kijamii.
Ndugu Wananchi,
Miundombinu hii imejengwa kwa ushirikiano wa Serikali yetu na Serikali ya Jamhuri ya Watu wa China. Napenda kuishukuru sana Serikali ya China kwa mchango wake katika kufanikisha mradi huu. Kuna usemi usemao ‘Akufaaye kwa dhiki ndiye rafiki’ au kwa lugha ya wenzetu Waingereza wanasema‘A Friend in need is a Friend indeed’.
Ndugu zetu wa China wamekuwa na ushirikiano wa kidugu na Tanzania kwa muda mrefu, kuanzia enzi za ukombozi wa Bara letu la Afrika toka kwa Wakoloni. Wametusaidia katika mambo mengi ya maendeleo ikiwemo ujenzi wa Reli ya TAZARA, ujenzi wa viwanda vya nguo, kutupatia nafasi za elimu katika nyanja mbalimbali na mambo mengine mengi ambayo siwezi kutaja na kuyamaliza kwa wakati huu. Kwa kifupi nasema asante sana kwa wananchi wa China na Serikali yao kwa kuendeleza ushirikiano nasi ikiwa ni pamoja na kukubali kushirikiana nasi kujenga miundombinu hii muhimu tunayo ifungua leo. Kama mtakumbuka, baadhi ya marafiki zetu walipinga zoezi hili lakini China ilisimama kidete kulitetea na kuruhusu taasisi zake kutoa mikopo nafuu na Kampuni zake kujenga miundombinu hii kwa bei nafuu ikilinganishwa na gharama za ujenzi wa miundombinu kama hii kwingineko duniani.
Ndugu Wananchi,
Napenda kuwashukuru na kuwapongeza wenzetu wa Mikoa ya Lindi na Mtwara ambako gesi asilia iligundulika, wameonesha ushirikiano mkubwa licha ya kusumbuliwa na shughuli za mfumo mzima wa utafutaji, uchimbaji na hata ujenzi wa bomba. Wamekuwa wavumilivu na wenye subira katika kuunganishiwa umeme utokanao na gesi asilia au kunufaika na matumizi ya gesi yenyewe majumbani au kwenye viwanda linakopita bomba. Waswahili husema: Mvumilivu hula mbivu.Wataalamu wetu wanatueleza kuwa katika bomba hili pamewekwa matoleo ya gesi (viunganishi) katika maeneo mbali mbali ilikukidhi haja ya kuendeleza maeneo hayo kwa kutumia gesi hii. Pamoja na matumizi ya gesi majumbani, maendeleo makubwa yataletwa na mapato yatakayotokana na ajira zitakazopatikana kwenye viwanda kwa wananchi kutokana na kutoa huduma zinazohitajika katika shughuli za uendelezaji gesi asilia na malipo ya kodi ya huduma yatakayolipwa na Kampuni kwa Serikali za Mitaa ambayo kwa pamoja vitafanya uchumi wa maeneo husika kukua.
Napenda pia niwapongeze ndugu zetu wa Mikoa ya Pwani na Dar es Salaam ambako bomba la mwanzo na la sasa yanapita. Wamekuwa walinzi na watunzaji wa miundombinu hiyo muhimu kwa niaba yetu sote. Kwa ajili hiyo napenda kutumia fursa hii kuwasihi kuendelea na moyo huo.
Aidha,natumia fursa hii kutoa rai kwa wananchi wote, na hasa wale wa Mikoa ya kusini, kuitunza na kuithamini miundombinu hii, na muwe tayari kutoa taarifa kwenye vyombo vya ulinzi na usalama endapo vitaonekana viashiria vyovyote vya hujuma kwenye miundombinu hii.
Ndugu Wananchi,
Kipekee nampongeza sana Mkandarasi China Petroleum and Technology Development Corporation (CPTDC) pamoja na kampuni ilizozihusisha China yaani Petroleum Pipeline Bureau (CPP) kwa ujenzi wa Bomba na China Petroleum Engineers (CPE), kwa ujenzi wa Mitambo ya Kuchakata gesi asili, kwa utaalamu na umahiri wa hali ya juu, pamoja na kujitahidi kuukamilisha mradi kwa muda uliopangwa. Vilevile napenda kumpongeza Mshauri, Kampuni ya Worley Persons ya Jamhuri ya Afrika ya Kusini, ambaye amesimamia vema utekelezaji wa mradi hadi kukamilika kwake.
Ndugu wananchi,
Nimeona pia ni vyema kutumia fursa hii kutoa tahadhari kwa kauli za matumaini zinazotolewa na watu wa kada mbalimbali kufuatia ugunduzi huu; hususani matamshi ya kuwa sasa Tanzania si masikini tena, au kuwa kila mwananchi atajazwa mapesa au sasa tumeukata; ama wadau wengine wanashauri eti sasa tuache kwanza shughuli za utafutaji. Ndugu zangu, ni vizuri tukaelewa kuwa pamoja na ugunduzi huu mkubwa wa gesi, itachukuwa muda wa takribani miaka 10 kwa nchi kuanza kufaidi mapato yatokanayo na gesi hii, hasa ile inayopatikana kwenye kina kirefu cha bahari. Kwa sasa gesi tunayotumia ni ile iliyogundulika nchi kavu na matumizi yake makubwa ni kwa ajili ya uzalishaji wa umeme na uendeshaji wa mitambo mbalimbali ikiwemo viwanda vya hapa nchini. Kwa hiyo ni vema pamoja na shughuli za kuendeleza gesi tukafanya kazi zinazotuzunguka kwa bidii kwenye sekta nyingine muhimu. Ni wazi kwamba ili uchumi wa gesi uwe na manufaa ni lazima uhusishe shughuli za sekta nyingine.
Ndugu Wananchi,
Hivi karibuni Serikali imepitisha nyenzo muhimu katika usimamiaji wa sekta ndogo ya mafuta na gesi kwa manufaa ya taifa. Ili kuhakikisha kwamba rasilimali hiyo inatumika ipasavyo, Serikali imepitisha Sera ya Gesi Asilia, Sera ya Petroli, Sera ya Usimamizi wa Mapato yatokanayo na shughuli za Mafuta na Gesi na Sera ya ushirikishwaji wa Wazawa. Baada ya Bunge kupitisha Sheria ya Petroli ya 2015, Sheria ya Usimamizi wa Mapato yatokanayo na shughuli za Mafuta na Gesi pamoja na Sheria ya Uwajibikaji na Uwazi kwenye Sekta ya Uziduaji, tarehe 04/08/2015 nilisaini sheria hizi pale Dar es Salaam. Sheria hizo zitaanza kutumika baada ya Mawaziri husika kutengeneza Kanuni zinazotakiwa.Waziri wa Nishati na Madini atatengeneza Kanuni za Sheria ya Mafuta na Gesi na Waziri wa Fedha atatengeneza Kanuni za sheria ya Usimamizi wa Mapato yatokanayo na shughuli za Mafuta na Gesi.
Pamoja na mambo mengine mazuri, sheria hizo zimeliboresha zaidi Shirika letu la Maendeleo ya Petroli (TPDC) kwa kulipa hadhi ya kuwa Shirika la Taifa la Mafuta (National Oil Company). Lakini vile vile sheria imeanzisha Mamlaka ya Udhibiti wa Mkondo wa Juu (PURA)na kuiachia EWURA mamlaka ya kisheria ya kusimamia na kudhibiti Shughuli za Mkondo wa Kati na wa Chini. Kwa mabadiliko hayo TPDC sasa inabaki na majukumu ya kibiashara na hivyo kufanya kazi kibiashara zaidi na kuendelea kukua na hatimaye lifanane na Mashirika mengine makubwa ya kimataifa ya mafuta na gesi kama vile Statoil, Sonangol, Petronas na Petrobras na mengineyo.
Pia nitumie fursa hii kuwahakikishia wananchi kuwa kuwepo kwa Sera na Sheria madhubuti na kukamilika kwa miundombinu kutaboresha usimamizi wa raslimali hiyo na si vinginevyo. Napenda niwatoe hofu kwa wale wanaoambiwa kuwa Sera na Sheria hizo hazitaleta mageuzi katika sekta hii kama watu kadhaa wanavyojaribu kupotosha. Hiyo siyo kweli. Serikali ina nia ya dhati kabisa katika kulinda na kuendeleza raslimali zake kwa manufaa ya taifa.
Ndugu Wananchi,
Napenda kuipongeza TPDC kwa kazi kubwa ambayo imeifanya katika kutimiza majukumu iliyopewa na Serikali ya Utafutaji na Uzalishaji wa Mafuta/Gesi. Matunda yake ni kama haya tunayoyaona leo. Mtakumbuka kwenye nyakati za misukosuko kama vile vita ya Kagera, TPDC walitoa mchango mkubwa kuhakikisha mafuta yapo nchini. Kwa wakati huu mnalojukumu la kusimamia mfumo mzima wa gesi asilia. Serikali haina budi kuhakikisha TPDC mnafanikisha utafutaji na Uendelezaji wa mafuta/gesi kwa kushiriki kikamilifu kwenye utafutaji (Upstream); kusimamia miundombinu ya usafishaji, uchakataji na usafirishaji (midstream), kama mradi tunaozindua leo hii, pamoja na usambazaji (Downstream).
Nimalizie kwa kusema kuwa tukio hili la uzinduzi wa miundombinu hii linanipa furaha sana kwa sababu ni ushahidi mojawapo ya kazi kubwa tulizozifanya kwa kushirikiana nanyi wananchi nikiwa Kiongozi mkuu wa nchi. Kazi tuliyoianza tunaimaliza vizuri! Kwa hakika ni zawadi mojawapo kubwa kwangu ya kustaafu.
Baada ya kusema hayo machache napenda sasa nitamke rasmi kuwa Mitambo ya Usafishaji gesi asilia ya Mtwara na Songo Songo pamoja na Bomba la kusafirisha Gesi hadi Dar es Salaam imezinduliwa.
MUNGU, IBARIKI TANZANIA NA WATU WAKE!
Ahsanteni Sana!
- Oct 06, 2015
ADDRESS BY H.E. JAKAYA MRISHO KIKWETE, THE PRESIDENT OF THE UNITED REPUBLIC OF TANZANIA, TO THE PARLIAMENT OF REPUBLIC OF KENYA, NAIROBI-KENYA 06TH OCTOBER, 2...
Soma zaidiHotuba
His Excellency Honourable Uhuru Muigai Kenyatta,
the President of Republic of Kenya;
Honourable Justin Muturi, Speaker of the National
General Assembly;
Honourable Ekwe Ethuro, Speaker of the Senate;
Honourable Members of the Parliament;
Honourable Senetors;
Honourable Ministers;
Invited Guests;
Ladies and Gentlemen.
I thank you Honourable Speaker for availing me with this rare opportunity to address this esteemed Parliament of Kenya. It is an honour and a privilege I will always remember. You have availed me this opportunity at a very opportune moment indeed. Three weeks from office as directed by the constitution of my dear country. So to me, this is an opportunity to bid farewell to this House and through you to my brothers and sisters of the Republic of Kenya.
When H.E. President Uhuru Kenyatta invited me to visit his great county. I did not hesitate to accept the invitation. This was because of the importance of Kenya in Tanzania’s foreign policy. Kenya is a very important neighbour of ours. Kenya is a great friend of Tanzania and an ally. Our political and diplomatic relations are strong. We see eye to eye on many bilateral, regional, continental and global issues.
We have been working together very well and support each other at regional, continental and global fora.
We have also supported each other at the bilateral level as well. To me and to Tanzania, Kenya’s problems are our problems.
It is in this spirit that during 2007 and 2008 crisis I did not wait to be invited, I came to lend a helping hand. Fortunately, God was kind enough to the people of Kenya, you were able to navigate safely out of the crisis. It is in the same spirit also we have not only grieved with our Kenyan brothers and sisters whenever there was a terrorist attack, but we have supported Kenya’s efforts in fighting terrorism. Our Intelligence services and Police Forces have been working closely. They have been sharing intelligence and arrested suspected terrorists who flee to Tanzania after committing crimes in Kenya. We never hesitated to send them back to Kenya to face justice.
The Purpose of the Visit
Honourable Speaker;
We also have robust and longstanding cooperation in the fight against narcotic drugs and cross border crime. This way, we have been able to deal with criminal gangs operating in our two countries. Recently, we have began to develop cooperation in fighting poaching and illegal trade in wildlife. This cooperation has worked well for our two countries. What is required of us going forward is to strengthen and advance this cooperation. Lets make it clear to criminals that if they cause trouble in any of our countries there is nowhere to hide and nowhere to run to.
Honourable Speaker;
On the social-economic front there has been vibrant cooperation as well. Our two countries have been undertaking joint infrastructure projects. Take for example, the Althi-River-Namanga-Arusha road which was completed in 2012. Currently, we are now doing the Mwatate – Taveta – Holili – Moshi- Arusha road. As you know, my first function in my visit to Kenya this time was at Taveta, where together with President Uhuru Kenyatta we inaugurated the construction of this road on the Kenyan side. We are working on a suitable date to do the same on the Tanzanian side.
Other important infrastructure projects are in energy. In the electricity subsector we have been doing two things. One, whenever one of our countries has electricity and the other doesn’t, the people on the other side of the border are connected. This is what we have done at Namanga where power from Kenya has been extended to Namanga and Longido on the Tanzanian side. We did the same between Sirari (Tanzania) and Isbania Kenya. Secondly, we are building a power transmission line from Tanzania to Namanga where the Tanzania electricity grid will be connected to the Kenyan grid. This way power from Tanzania will be made available to Kenya and vice versa. Our two countries are discussing how to extend the gas pipeline from Tanzania to Kenya so as to enable Kenya produce more electricity from a cost effective source.
Honourable Speaker;
On investment and trade our two countries have been able to develop strong bonds of cooperation. For us in Tanzania, Kenya is not a competitor but a strategic partner. Kenya ranks 5th in the Top Ten list of countries with the largest investments in Tanzania. Kenya comes after only United Kingdom, United States, China and India. Actually, in that Top Ten List, there are only two African countries namely Kenya and South Africa, on which Kenya is the leader. Kenya’s investments in Tanzania account for 518 projects with the total value of 1,685.47 million USD and have created about 55,762 jobs.
Kenya is Tanzania’s largest trading in East Africa. Trade between our two countries is growing fast and in the last five years there was a 40 percent increase.
Tanzania’s exports to Kenya have increased from 179.3 million USD in 2009 to 227.1 million USD in 2013 and imports have increased from 301.5 million USD to 333.6 million USD in 2013. I am told trade between our two countries account for over 80percent of trade in East Africa. It demonstrates in no uncertain terms how much our two countries contribute to the East African integration agenda. Also its how important it is for our two countries to forge closer and stronger cooperation in investment and trade.
As a matter of fact, what we have accomplished now is simply a tip of an iceberg in relation to what we can do together. This morning when speaking at the Kenya-Tanzania Business Forum I assured the Kenyan business men and women that Tanzania is ready to do more business. We can absorb more investments and opportunities are plenty in oil and gas, energy, mining, transport, agribusiness, manufacturing, ICT, health care, education and many more. Moreover, the business environment is both conducive and permissive. Investments are safe. No nationalisation, and it is allowed to repatriate profits and dividend.
Tanzania and EAC
Honourable Speaker;
To us in Tanzania, regional integration is a matter of both principle and policy. We have always remained believers in African Unity and the East African economic and political integration. We hold strong belief that, a divided East Africa will not be able to claim its rightful place and compete effective in the regional and global marketplace, therefore, that Tanzania commitment to the East African integration and its flagship the East African Communities. We will do everything within our power to see the East African integration agenda is implemented to the letter and spirit. It is pleasing to note that the same understanding is shared by you our brothers and sisters in Kenya.
Conclusion
Honourable Speaker;
I will leave office fully satisfied I leave behind strong bonds of friendship and cooperation between of two countries and two people. I would like to assure you that Tanzania’s policy towards Kenya will remain the same even after I have left office. If anything there will be stronger and closer cooperation in the coming years.
I know there is a lot of anxiety and speculation about what will happen after the elections. Have no worries have peace. I don’t see any change or shift of policy. And, if the candidate of my party wins that is completely assured. I am not only hopefully but confident that he will emerge victorious. By the way he sends his greetings to you all. He has asked me to assure you that if elected President he will strengthen and advance our bilateral relations to the greatest heights possible.
With these many words, I thank you once again Honourable Speaker and Members of this House for your kind attention, and for the honour given to me to address and bid farewell to this Assembly.
Ahsante sana!
- Oct 06, 2015
KEYNOTE ADDRESS BY HIS EXCELLENCY JAKAYA MRISHO KIKWETE, PRESIDENT OF THE UNITED REPUBLIC OF TANZANIA, AT THE KENYA - TANZANIA BUSINESS FORUM IN NAIROBI, KENY...
Soma zaidiHotuba
Ladies and Gentlemen;
I thank you President Uhuru Kenyatta for including this meeting in my itinerary and for what you have just said emphasizing the importance of promoting business relations between our two countries. I thank Mr. Kiprono Kittony the Chairman of the Kenya Chamber of Commerce and Industry for organising this important forum. It will surely go a long way towards strengthening the overall relations between our two countries.
Doing Business in Tanzania
Ladies and Gentlemen;
We are gathered here this morning to discuss issues of bread and butter: Kenya – Tanzania investment and business opportunities and relationships. Honestly, I don’t know what to tell you about the business opportunities in Tanzania or the business environment in Tanzania because some of you, if not many, are already doing business in Tanzania. Our records show that Kenya is the fifth largest investor in Tanzania and the leading in Africa followed by South Africa. There are 518 investment projects from Kenya worth USD1,685.49 million, employing 55,762 Tanzanians.
Manufacturing accounts for 45 percent of the total value of Kenya’s investment while real estate accounts for 13 percent, tourism 12 percent and transport and logistics 11 percent. The remaining 19 percent is distributed in small portions among other sectors.
With regard to trade between our two countries, records show that we have been doing very well. Kenya’s exports to Tanzania increased from USD 301.5 million in 2009 to USD 333.6 million in 2013. During the same period Tanzania’s exports increased from USD 179.3 million in 2009 to USD227.1 million in 2013. I am told at this level of trade volume that our two countries account for nearly 90 percent of intra East African trade. This demonstrates in empirical terms how much our two countries need each other and how significant we are in the East African integration agenda.
Mr. President;
Ladies and Gentlemen;
Let me state clearly and loudly that our two countries can do better than what we are doing at the moment. Tanzania can absorb more investment from Kenya sell more and vice versa. There are, in Tanzania, plenty of opportunities in oil and gas, energy manufacturing, agriculture, mining, tourism, real estate, transport, ICT, hearth care, education and several others which you may know better than me. Our two countries enjoy cordial relations which is good for business. Also, we are members of the East African Community one of whose main objectives is to promote trade and investments between member states. The EAC arrangements under the Customs Union, the Common Market and Monetary Union have opened the borders, for trade which is constantly making life easy for business in the East African region.
Since the socio–economic reforms which began in the mid 1980’s, Tanzania has been pursuing sound economic policies. As a result, there is strong macro-economic performance and stability for over two decades now. On the average Tanzania’s economy grow at around 7 percent over the last decade and we expect a 7.3 percent growth this year. The GDP has trebled from USD 14.1billion in 2005 to USD 49.1 billion in 2014. And so, has the GDP per capita from USD 375 in 2005 to USD 1,066 in 2014. The population of Tanzania is estimated to be around 48 million with a sizeable and a growing middle class. With more than 50 percent of the people below the age of 30 who have better access to primary and tertiary education there is an assured labour force and a market. Moreover, Tanzania’s membership of SADC and Kenya’s membership of COMESA, gives the Kenyan investor an extended market beyond the East African Community and COMESA. I gather only 4 of the 14 SADC member states are in COMESA.
Mr. President;
Ladies and Gentlemen;
As we all know, Tanzania has enjoyed peace and stability since independence. We are a vibrant democracy and committed to advancing good governance, rule of law and human rights. The fight against corruption, terrorism, narcotic drugs, and other vices in society is unrelenting. We espouse friendly business policies and investments are safe. No more nationalization and investors are allowed to repatriate profits and dividends. The government stands ready to take more measures to improve the business environment. We are doing exactly that and more. There is regular consultation between the government and private sector under the auspices of the Tanzania National Business Council which I chair. This has proven to be very useful. Issues are discussed openly freely discussed and solutions found.
Conclusion
Mr. President;
Ladies and Gentlemen;
I could go on and on since I have a lot to say, but allow me to conclude by expressing my sincere gratitude to the business community in Kenya for being valuable partners. I believe the discussions here today will further encourage Kenyan private sector to do more business with Tanzania. I whole heartedly welcome you to do so. Tanzania is more than ready to do business with you.
Please come one, come all.
Thank you very much, Asanteni sana.
- Sep 29, 2015
STATEMENT BY HIS EXCELLENCY DR. JAKAYA MRISHO KIKWETE, PRESIDENT OF THE UNITED REPUBLIC OF TANZANIA, AT THE GENERAL DEBATE OF THE SEVENTIETH SESSION OF THE UNIT...
Soma zaidiHotuba
Your Excellency, Mr. Mogens Lykketoft, President of the General Assembly;
Your Excellency, Mr. Ban Ki-moon, United Nations Secretary-General;
Excellencies Heads of State and Government;
Distinguished Delegates;
Ladies and Gentlemen;
I join those who spoke before me in congratulating you, on your well-deserved election to preside over the 70th Session of the General Assembly. Your election is a fitting tribute to your distinguished political career, having served as a Finance Minister, Foreign Minister and recently as Speaker of the Danish Parliament. It is also a reflection of the high regard this august Assembly has for your great country, Denmark. I would like to assure you of my country’s full support and cooperation in discharging your duties and responsibilities.
Mr. President;
I wish to pay glowing tribute to your predecessor Hon. Sam Kahamba Kutesa, Minister for Foreign Affairs of the Republic of Uganda for the outstanding manner in which he steered the affairs of the sixty-ninth session of the Assembly. Indeed, this great son of the African soil has done us proud. A deserving word of appreciation also goes to our illustrious Secretary-General His Excellency Ban Ki Moon and his staff, for their dedicated service and efforts in promoting the ideals and principles of the Charter of the United Nations.
Mr. President;
I also commend you, your predecessor and the Secretary General for the excellent work which has culminated into the adoption of the Post 2015 Development Agenda and the 17 Sustainable Development Goals (SDGs) with their 169 targets. We sincerely hope that there will be reliable mechanisms of ensuring availability of means of implementation and follow-up. It was failure to have such mechanisms which was responsible for the short falls in the implementation of the MDGs.
Mr. President;
My delegation welcomes the theme designated for this general debate, namely “The United Nations at 70: the road ahead for peace, security and human rights”. Indeed, at 70 years the United Nations has not only withstood the test of time but has evolved and become a stronger organization. I am glad we all agree that a lot has been achieved in the past 7 decades. Equally, we agreed that not everything that the founding fathers envisaged the UN would do has been done satisfactorily.
The United Nations has succeeded to prevent another world war but challenges of preserving world peace and security remain. Interstate and intrastate conflicts and wars are many and on the increase. Terrorism has become a serious global threat. There are still too many people who live under conditions of abject poverty, squalor and depravation in a world of unprecedented wealth.
The Partnership Between UN and Regional Organization
Mr. President;
Unlike 70 years ago, today there is better understanding, cooperation and partnership between countries and organizations in preserving peace and security. It is easier today for the world to come together for a course of peace than it was before.
As a matter of fact most of the conflicts we are witnessing today are being handled, first and foremost, by regional and sub-regional organizations. The UN, therefore, must seek to forge strategic partnership with these organizations. By taking advantage of the knowledge these organizations have of the history and nature of the crises, the key players and culture of the people, it would be easier to manage and resolve the conflicts. Where and when appropriate, the United Nations should invest in strengthening the capacity of these organizations and their member states, in anticipating, detecting, preventing, managing and resolving conflicts. I am of the view that this capacity is urgently needed in Africa.
The Security Council Reform
Mr. President;
We highly commend the President of the Sixty-ninth session of the General Assembly and the Chair of the Intergovernmental Negotiations (IGN) on reform of the Security Council, for efforts made. It is the wish of member states to see an acceleration of the negatiation process during this 70th Session. For the UN Security Council to remain what it was 70 years ago is incomprehensible and, to say, the least, unacceptable. It is high time the demands of the majority of the membership of the United Nations are heard and heeded too.
We must be mindful of the fact that the credibility of the UN depends on a more agile, representative and responsive Security Council. Let all of us muster political will and accomplish this long overdue task, for the sake of our Organization. In the mean time we must continue to support the Revitalization of the work of the General Assembly.
Peace Keeping Operation
Mr. President;
Peace keeping operations remain one of the most dependable instruments of promoting world peace and security. I believe it will remain so for many years to come. I am told there are about 125,000 men and women deployed in 16 peacekeeping missions across the world. Tanzania is proud to have contributed 1,322 of these gallant people who often times serve under challenging conditions. Sometimes they are compelled to serve in places where there is little or no peace to keep. Tanzania stands ready to contribute more whenever requested to do so.
Combating Terrorism
Mr. President;
We can not talk about security challenges of today without mentioning terrorism. This is the security challenge that the United Nations and the entire international community must remain vigilant in the coming decade. While reiterating our strongest condemnation of terrorism, in all its forms and manifestations, we believe there is an urgent need to bolster efforts at all levels for fighting the scourge. Collectively, we must aspire to improve our preparedness, collaboration and response to the threat we face.
Global Epidemics
Mr. President;
The Ebola outbreak in West Africa last year is a stark reminder of how dangerous epidemics can be and how vulnerable we are as nations and people. More than 11,000 people lost their lives including citizens of the US and Spain and about 28,000 were infected. The economies of Liberia, Guinea and Sierra Leone were devastated. Economic activities and services almost ground to a halt thus causing gigantic losses to the economies of the three countries. The World Bank estimates that they lost about USD 2.2 billion of their GDP as a result. There were about 7,000 children who lost their parents and about half a million people who became food insecure. More than 5 million children lost valuable schooling and skills-development time. It requires mammoth recovery efforts to get these economies and societies back to where they were before the outbreak. Unfortunately, many countries in Africa also, suffered irrespective of how far a country is from the three affected countries. The tourist industry has been affected the most.
Mr. President;
The biggest lesson from the handling of this Ebola outbreak in West Africa is that the world needs to be better prepared to prevent and respond to epidemics in future. This was not the case unfortunately. It is in this regard that, we should all commend the Secretary General for the wise decision he took of establishing a High Level Panel on Global Health Crises to come up with recommendations about how the world can respond better to public health emergencies of global concern in future.
I was given the honour of chairing the panel. It is premature for me to report anything substantive now to this august Assembly. We will complete our work in December, 2015 and I am sure our report will be brought before this Assembly for information and action. We look forward to your support.
US/Cuba Relations
Mr. President;
Tanzania welcomes the historic and momentous decision taken by the United States of America and the Republic of Cuba to restore diplomatic relations and reopen embassies of the two countries in Washington D.C. and Havana. We join the people of Cuba and the United States in celebrating this landmark achievement.
We commend President Barack Obama and President Raul Castro for their bold and courageous leadership. The two leaders and countries have proved to all of us, the power of dialogue in finding solutions, even to deep rooted difference and long standing conflicts. We extend best wishes to our US and Cuban friends as they open a new chapter in their bilateral relations. We hope and appeal to the United States to lift the economic embargo which has condemned the people of Cuba to untold socio-economic hardships, poverty and misery for the last 50 years.
Palestine
Mr. President;
In the same vein, it is our wish that Israel and Palestine would resume the dialogue so that their long standing conflict can be resolved peacefully. It is high time the pain and suffering endured by the people of Palestine over the many decades was put to an end. Also, it is about time the people of Israel lived peacefully and harmoniously with their neighbours.
It is regrettable that we are celebrating seventy years of the founding of the United Nations this conflict remains unresolved. Tanzania subscribes and supports the two states solution, with the state of Israel and a sovereign, contiguous and viable state of Palestine living side by side, in peace, security, harmony, mutual recognition, trust and cooperation. We believe it is possible and achievable. We must double our efforts.
The Question of Western Sahara
Mr. President;
Another outstanding matter which this organisation has to ensure that it does not continue to be left unresolved is the issue of Western Sahara. The lack of movement on the side of the United Nations to implement its decisions on the matter is both regrettable and incomprehensible. The people of Saharawi have waited for far too long to get the opportunity to determine their fate and future. Let this esteemed Organisation of ours muster political will and pluck up courage to do what it had long decided to do. At seventy years the United Nations is old enough and has accumulated a lot of wisdom and experience to put this matter to rest. Please do it.
A Farewell Message
Mr. President;
On September 20th, 2006, I stood on this very podium, for the first time and addressed this august Assembly as the newly elected fourth President of my dear country: the United Republic of Tanzania. Today, I am standing here to bid farewell to you all as I am about to leave office at the completion of my two term mandate, as provided for in the Tanzania Constitution.
I thank all of you for the invaluable support and cooperation extended to me, my administration and my country in the past ten years that we have worked together. Kindly be assured that I will always value each and every one’s contribution. I feel proud to have had the opportunity to work with all of you in promoting the ideals of the United Nations and contributed to the pursuit of world peace, security, stability and development.
As I take leave of you, I would like to assure you that Tanzania shall remain a faithful member and an unwavering supporter of the United Nations’ Organisation. I am confident that you will find in my successor, a likeable and dependable friend and ally. Please accord him or her the necessary support and cooperation in fulfilling his or her duties and responsibilities.
Conclusion
Mr. President;
The road ahead for peace, security and development remains challenging but worthy the journey. It requires our renewed resolve and reaffirmation of our commitment to the ideals, values and principles laid down by the founding fathers of the United Nations seven decades ago in San Francisco. All nations, individually and collectively, should endeavour to promote them as we have been doing in the last seventy years. It can be done, play your part.
I thank you.
- Sep 04, 2015
SPEECH BY HIS EXCELLENCY DR. JAKAYA MRISHO KIKWETE, THE PRESIDENT OF THE UNITED REPUBLIC OF TANZANIA DURING OPENING OF AFRICA OPEN DATA CONFERENCE HELD AT JUL...
Soma zaidiHotuba
Honorable Saada Mkuya, Minister for Finance;
Honorable Mathias Chikawe, Minister for Home Affairs;
Honorable Celina Kombani, Minister for
Public Service Management;
Ambassador Ombeni Sefue, Chief Secretary;
Your Excellencies Ambassadors;
Permanent Secretaries, Deputy Permanent Secretaries;
World Band Country Director for Tanzania,
Uganda, and Burundi;
Head of International Organizations based in Tanzania;
Representatives from CSO and Private Sector;
The Media;
Members from Mass Media;
Distinguished Delegates;
Ladies and Gentlemen.
I am pleased to get the opportunity to grace the first ever Open Data Africa Conference in the history of our dear continent. The fact that it’s the first ever, conference signifies the dawn of a new era in Africa’s transformation towards knowledge based development. It gives me great pride that my country has been chosen to host this first conference. To us, it is a gesture of acknowledgment and appreciation for the strides we are making to embrace openness in governance through open data. I thank the organizers for the trust you have reposed on my country. In a special way, I thank the World Bank for partnering with us in the preparations of this conference.
I thank you Honourable Mathias Chikawe, Minister for Home Affairs for your introductory remarks. I commend you and your team for the excellent facilitation of this conference. Please continue to do the good work so that all delegations stay happy and the conference concludes successfully. I am told delegates come from governments, civil society, academia and business from 30 countries in Africa and development partners. Such a good response reflects the growing interest on open data agenda across the continent. It goes without saying that, this conference will spur more interest and make future conferences be even more successful.
Theme of the Conference
Ladies and gentlemen;
I commend the organizers for choosing a very opportune theme for this conference namely “Developing Africa Through Open Data”. I totally subscribe to the idea that data is an important tool for development. No successful and meaningful development will take place without the use of data. Data assists us with the diagnosis of the social and economic challenges, informs policy choices and decisions and helps us with monitoring and evaluation of progress and impact. Much as data does not in itself, change the world, it is also true however that it makes change possible.
Information technology has revolutionalized the way we collect, use and make sense of data. I has made data open. The impact of open data has been immense in all walks of life. There is hardly anyone today who has not benefited directly or indirectly from data being open. Open data has freed science, spurred innovations and making collaboration across countries and continent in solving global challenges possible. It has brought together the researchers, policy makers, financiers, private sector and civil society across the world to work together to find solutions to world’s challenges in a manner that has never been seen before.
Africa has not been spared by this development. As a matter of fact we have no choice but to join everybody else on this planet. We cannot honestly speak of developing Africa today without improving on ways we source, process and make use of data. More importantly, we must transform ways we manage data by increasingly making public data open and shared. In that way we will enable decision makers to make informed decisions. We will also empower the public to use data to hold the public officials accountable. In that way we will enhance good governance and take Africa to the next level.
Challenges of Open Data in Africa
Ladies and gentlemen;
One teething challenge you will find across African governments today is the lack of quality data. This has made planning, policy making and policy execution become a challenge. As a result, a number of policies and interventions have failed to produce intended impact. It has all been a source of wastage of valuable resources and loss of opportunities to solve development challenges.
It is evident, therefore, that there exist in Africa a disturbing relationship between underdevelopment and underutilization of quality data (and the vice versa). In many cases, this has been a function of lack of capacity on the part of responsible government institutions to collect, process and store data. In many of our countries, budgetary constraints, poor infrastructure and lack of qualified human capital have been responsible for this sad state of affairs. At times also administrative and policy oversight or shortsightened on the importance of data are to blame. In some ways legal and institutional systems have played a part in restricting access and sharing of data within and among various institutions.
There is a need, therefore, for African governments to explore ways and means to promote open data in their countries. There is need to undertake requisite reforms in some aspects of governance to support open data. Open Data strives best where there is transparency, rule of law, and freedom of expression to mention but a few. There is a need also to strengthen national institutions responsible for data management such as bureau of statistics so that stakeholder’s demand for credible, reliable and timely data can be met.
Open Data Beyond Governments
Ladies and gentlemen;
It gives me much comfort that this Conference will discuss among many issues the role of the private sector in the open data agenda. You should consider including the civil society as well. For quite a long time, the issue of openness of data was seen as a matter of the government and public institutions alone. The private sector and civil society organizations are not only consumers of data but also important sources of data. It is about time that the demand for transparency on the side of the private sector is also heard and honoured. As governments making their data open such as revenues and expenditures; the private sector too has a share of responsibility to open their data as well, regarding revenues, tax payments and profits.
qualified human capital have been responsible for this sad state of affairs. At times also administrative and policy oversight or shortsightened on the importance of data are to blame. In some ways legal and institutional systems have played a part in restricting access and sharing of data within and among various institutions.
There is a need, therefore, for African governments to explore ways and means to promote open data in their countries. There is need to undertake requisite reforms in some aspects of governance to support open data. Open Data strives best where there is transparency, rule of law, and freedom of expression to mention but a few. There is a need also to strengthen national institutions responsible for data management such as bureau of statistics so that stakeholder’s demand for credible, reliable and timely data can be met.
has always been about where to strike a balance between the two. It must be understood that open data does not and should not mean absolute freedom to produce, access and publish data. I subscribe to the view that, open data should not in any way jeopardize national security rather it should enhance it. It is my considerable opinion that data relating to national security issues should not be made public for obvious reasons.
Approaches to open data must, therefore, answer the following important questions: To whom the data is opened to? Which data should be made open? Why should data be open? When should data be open? And how should data be made open? Indeed, open data and data sovereignty can co-exist, and should co-exist. It is up to us to strike that delicate balance to avoid unnecessary contradictions. It requires the understanding and cooperation of all stakeholders.
Tanzania’s Experience with Open Data
Ladies and gentlemen;
Tanzania embraces open data and sees in it an opportunity to consolidate and entrench democracy and good governance. We have taken measures and initiatives to promote transparency and accountability through open data. For that reasons we voluntarily joined international initiatives geared to promote open data, transparency and accountability such as Open Government Partnership (OGP), Extractive Industry Transparency Initiative (EITI) and African Peer Review Mechanism (APRM).
We publish citizens’ budget to enhance public understanding of the government budget, and reports of the Controller and Auditor General (CAG) are published and made public for every Tanzanian to see. They are also debated in Parliament. As you know Parliament sessions are broadcast live on television. Over and above that, in line with our commitment to OGP, we have put in place a government portal with information and guidance about: how one can get public services; acts and legislation; regulations; policies; speeches and other important government information.
In our resolve to improve government’s service delivery, we introduced the famous ‘Big Results Now’ model. This is a system of improving on the way we decide on priority areas of action, monitor, implementation and enhance accountability on the part of ministries, government agencies and officials. In this regard we chose water; energy; transport; agriculture; education; resource mobilization; health and strengthening of the business environment as key priorities. Through this system government implementing agencies act in an open manner, made data open thus empowering the public to be informed and able to track the progress and put the duty bearers to task. Therefore open data has been an embedded part of the BRN process with the data in those priority areas being made public.
Our experience has taught us that, open data must be backed and supported with a facilitative legal regime to guarantee access and effective use of the open data. For that reason, we have enacted the Statistics Act of 2015 that has empowered the National Bureau of Statistics (NBS) as a sole autonomous body, with powers to direct Ministerial Departments and Agencies to adhere to the principles and standard of production of quality data. To complement the open data, we have initiated a process to enact the Freedom of Information Act, on which the draft has already been presented to Parliament.
Tanzania’s Commitment
Ladies and gentlemen;
Tanzania shall continue to support and live up to her commitment on open data. In January 2015, we endorsed the Guidelines for Open Data in Tanzania. The guidelines serve as a tool for Ministries, Government Departments and Agencies to provide data to the Open Data Government Portal. We are also in the process of coming up with the Open Data Policy that will put in place procedures for identifying government open data, institutional framework for open data management, establish one window where the public can access to data, and put in place procedures of uploading and updating data. This way we will enhance for public access to government data in a friendly manner that allows the use and re-use of data for socio-economic development. Ultimately our intention is to enact an Open Data Act.
These and many other steps we have taken speak volumes about our resolve to uphold open data. For us, open data is the way to go if we are to transform our country from Least Developed Country to a Middle Income Country, and ultimately to become an advanced economy. We are looking at the future of open data in Tanzania with much optimism. There is no reason or intentions of back tracking. You can count on us.
Conclusion
Ladies and gentlemen;
There is no doubt that Africa needs to embrace open data in her development agenda. It is an idea whose time has come. It is the way to go about achieving Africa’s Vision 2063 of “an integrated, prosperous and peaceful Africa, driven by its own citizens and representing a dynamic force in global arena”. Indeed, the road towards achieving open data will not be without difficulties or challenges. However, it is the best way forward to a better Africa. Africa where democracy, good governments and development reign. I believe the rewards of open data far outweigh the costs.
I vest a lot of hope on this Conference. I believe it will provide a useful platform for African governments, private sector and civil society to create an understanding on how best we can approach open data in the African context. I am glad that, this conference will be the beginning of annual African Open Data Conferences in future. Tanzania pledges support and participation in the coming future conferences for they provide an avenue to share experiences and best practices. With these many words, I therefore wish you successful discussions and deliberations.
I now declare the first African Open Data Conference officially open.
I thank you all for listening!
Asanteni sana!
- Sep 02, 2015
SPEECH BY H.E. DR. JAKAYA MRISHO KIKWETE, PRESIDENT OF THE UNITED REPUBLIC OF TANZANIA TO THE 8TH TANZANIA NATIONAL BUSINESS COUNCIL MEETING HELD ON 2nd SEPTEMB...
Soma zaidiHotuba
Honourable Ministers;
Amb. Ombeni Sefue, Chief Secretary, and Chairman of the Executive Committee of the Tanzania National Business Council;
Mr. Abdulhamid Yahya Mzee, Chief Secretary of Zanzibar;
Dr. Reginald Mengi, Chairman of Tanzania Private Sector Foundation
and Co-chair of Tanzania National Business Council
Executive Committee;
Distinguished Members of the Tanzania National
Business Council;
Limited Guests;
Ladies and Gentlemen;
I welcome you all to the 8th Meeting of the Tanzania National Business Council (TBNC). I thank you for responding in good numbers to my invitation. It speaks volume about the importance and commitment you have vested in this Council.
I regret that we could not meet as schedule in 2014 for apparent reasons. Apart from the exigencies of office on my part, it was bought to my understanding that the three task forces formed at the 7th meeting that of Improving Business Environment; Tourism; and Economic Empowerment requested more time to complete the assignment given onto them. I agreed with the view that there will be more value to meet when we have a solid agenda to deliberate upon. This meeting today therefore, will dwell on examining progress, results and impact rather than concept and processes had we met last year as earlier planned.
I congratulate you Ambassador Ombeni Sefue, Chairman of the Executive Committee and your team for the excellent follow-up work and the preparations for today’s meeting. I commend you on your wise decision to invite other stakeholders as observers beyond the TNBC membership in this meeting. I am told the invitees include our development partners, non-government organizations, multinational institutions and the companies and most importantly the informal sector. It is a good idea to bring on board anyone whose contribution matters in improving our dialogue and enhancing our performance.
Theme of the Year
The choice of the theme of this year “Enhancing Business Environment for Sustainable Growth” is of significant importance in reminding us of the task ahead of us. It amplifies the call for improving business environment to contribute towards sustainable development. It admits in first place that it is business that will contribute to development, and eventually check out poverty. It also reminds us that for business to play its role there must be in place a conducive business environment. And, it is government’s role to put in place such an environment through better governance, facilitative policies, regulations and laws. Certainly, government and business needs one another to ensure that conducive business environment and sustainable growth. This is the rationale for government and private sector to have a structured dialogue like the one we have today.
Agenda of the Meeting
Ladies and Gentlemen;
The agenda of the meeting today is to carry out an evaluation of the status of the implementation of the deliberations of the 7th TNBC meeting held in December 2013. In doing so, we shall highlight milestone we have recorded, challenges endured and proposing a way forward. We shall see by ourselves, how far we have gone in enhancing business environment and unlocking potentials in the natural resources subsector.
I am informed that TNBC, PDB and Tourism Working Group have jointly carried out the evaluation on how to improve earnings from natural resources and improving business environment. I am also told that TPSF have carried out an evaluation of effectiveness of these dialogues for the last five years.
With regard to Local Content, which was part of the 7th TNBC meeting, I am glad that we have made encouraging progress. The draft Local Content Policy for oil and gas industry is in place. The draft has benefited from the inputs made by the TPSF and other stakeholders. Given the broadness of the subject and a need for further dialogue and consultation this agenda remains in progress for the forthcoming Business Council meeting.
State of Our Economy
Ladies and Gentlemen;
There is no doubt today that our economy is growing fast. There are dozens of review and reports to attest that. Numbers tell it better. For a decade Tanzania economy has been growing at an average rate of 7 percent per annum. The inflation has been maintained at single digit between 4-6 percent. Our GDP trebled from 14.4 billion USD from 2005 to 49.2 billion USD in 2015, and, as a result, per capita GDP has also increased nearly three-fold from 375 UDS in 2005 to 1,066 USD in 2014. It is important to note that, with the current per capita of 1,066 USD we are just short of 30 USD to attain the middle income status which starts at 1,096 USD. This rosy outlook however does not give us reason to be complacent. Our target remains to become a Middle Income Country with per capita income of at least 3,000 USD by 2025. We also need to do more and better to ensure that growth benefits all equitably. At 28.2 percent these are still too many people who live below the poverty line. This means we still have a long ground ahead to cover to make growth inclusive and eradicate poverty.
The macroeconomic gains we attained are a function of the contribution of the partnership between government and the private sector. And by extension, they are the product of the dialogue that has taken place through this esteemed council. It is important that I mention few which are:
- The inclusion of Business Environment in the key sectors of the BRN initiative.
- Kilimo Kwanza Initiative that has resulted into the increased agriculture output, the introduction of the SAGCOT initiative and the recent establishment of the Tanzania Agriculture Development Bank;
- Land reforms covering mortgage financing for accessing finance for real estate development and Unit title for promotion of provision of decent housing.
- Promotion of Public Private Partnership with the objective of drawing private sector resources into economic and social infrastructure development of the country.
Members of the Business Community;
Ladies and Gentlemen;
I would like to reiterate continued government’s commitment in addressing challenges that negatively impacts on business environment. We have demonstrated our unwavering commitment by adding Business Environment within the BRN priorities. We are committed to implementing the six key areas identified by the stakeholders in the laboratory namely:
- Realigning Regulations and Institutions;
- Access to Land, and Security of Tenure;
- Taxation, Multiplicity of Levies and Fees
- Curbing Corruption
- Labor Law and skills set
- Contract Enforcement, Law and order
I am pleased that we have taken measures to implement these recommendations. Some have already been addressed or are in the process of being addressed. These include review of our labor laws with regard to issuance of work permits; enhancement of the judiciary’s capability to address issues related to backlog of cases and the duration of handling of cases; introducing name and shame program and the integrity pledges for private sector, government officials and political leaders to add value to the fight against a corruption. The list is quite long, and the feedback will be tabled and discussed in today’s meeting.
A call for Private Sector
It is my plea that we should continue to work together as partners than as foes or adversaries. In my opinion the best way to go is to explore ways of having the dialogue rather than resorting to a blame game. I say so because in essence business environment reflects a state of relations between government and private sector. If the two see eye to eye, enjoy mutual confidence and trust, there comes no reasons of having in place too many restrictive rules and regulations. Therefore, the surest way to improve the business environment is first to improve our working relations. Let each one of us honour each obligation responsibly and live up to the other partners’ expectation. Let us uphold dialogue, engage constructively and work with one spirit with one common objective as a nation. If we are to achieve that, I believe we will have done half the work towards achieving sustainable development for our dear country and respective business undertakings.
Conclusion
Ladies and Gentlemen;
As you are aware, my term of office will come to an end after the elections on 25th October, 2015. This, therefore, will be my last National Business Council to chair as President of our dear country. I would like to use this opportunity to bid farewell to you. I sincerely thank you for your contribution and support to my administration. We take pride in economic growth because of your tremendous efforts. My team and I, in government simply put in place policies and measures which were facilitative. It is you who were the prime movers and shakers of our economic success story.
As I leave the office, I ask you to continue to support the new administration as you did during my time. As a matter of fact strive to do more. I have all reasons to believe that the coming President shall build on the foundation we have built together. Also he shall see to it that the many agreed programs that are in the process at the moment are implementing to the letter and spirit. One thing I am sure, there will be no back tracking on the role of private sector in the Tanzanian economy.
With these many words allow me now to declare the 8th TNBC Meeting Open.
Thank you all for your attention.
“Asanteni sana”
- Aug 27, 2015
HOTUBA YA MHE. DKT. JAKAYA MRISHO KIKWETE, RAIS WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA, KATIKA UFUNGUZI WA MKUTANO WA NNE KATI YA OWM-TAMISEMI, BODI YA MFUKO WA BAR...
Soma zaidiHotuba
Mhe. Hawa Abdulrahman Ghasia, Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu TAMISEMI;
Mheshimiwa Kassim Majaliwa, Naibu Waziri TAMISEMI;
Mhe. Daud Felix Ntibenda, Mkuu wa Mkoa wa Arusha;
Waheshimiwa Wakuu wa Mikoa na Wilaya;
Bw. Jumanne Sagini, Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu TAMISEMI;
Naibu Makatibu Wakuu mliopo pamoja na Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Rais, Zanzibar;
Makatibu Tawala wa Mikoa;
Wakurugenzi wa Halmashauri zote nchini;
Dkt. James Wanyancha, Mwenyekiti wa Bodi ya Mfuko wa Barabara;
Wajumbe wa Bodi ya Mfuko wa Barabara;
Meneja wa Mfuko wa Barabara, Bw. Joseph Haule;
Wageni Waalikwa;
Mabibi na Mabwana;
Utangulizi
Naomba kupitia kwako Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu-TAMISEMI, Mheshimiwa Hawa Ghasia nimshukuru Mheshimiwa Mizengo Pinda, Waziri Mkuu kwa kunialika kuja kushiriki kwenye ufunguzi wa mkutano huu muhimu. Nakupongeza wewe binafsi na viongozi wenzako Wizarani kwa maandalizi mazuri na kwa uamuzi wenu wa busara kuitisha mkutano huu muhimu unaojumuisha wadau wa barabara za Mamlaka ya Serikali za Mitaa. Nimekubali kuja kufungua mkutano huu pamoja na kuwepo kwa shughuli nyingi zinazonikabili siku hizi kutokana na kutambua na kuthamini umuhimu wa mkutano huu katika kusukuma mbele gurudumu la maendeleo ya Taifa letu.
Umuhimu wa Mkutano wa Wadau
Ndugu washiriki;
Ni ukweli uliodhahiri kwamba barabara zilizo chini ya Mamlaka ya Serikali za Mitaa zina mchango mkubwa kwa ukuaji na ustawi wa uchumi wetu. Maana ili kusukuma maendeleo vijijini, hatuna budi kuunganisha Vijiji, Wilaya na Mikoa kwa mtandao wa barabara zinazowezesha vijiji vyote maeneo yote mijini na vijiji kufikika kwa urahisi wakati wote. Bila ya kuwa na barabara zinazopitika kwa uhakika wakati wa majira ya mvua na kiangazi zilizopo katika maeneo yaliyoko chini ya Serikali za Mitaa, uwekezaji mkubwa tunaoufanya kujenga mtandao wa barabara za Taifa na mikoa zinazohudumiwa na Wakala wa Barabara (TANROADS) unapoteza maana. Kwa lugha rahisi, barabara hizi zinategemeana.
Ninafurahi kuwa wadau wote muhimu wameshirikishwa katika mkutano huu. Nimejulishwa kuwa OWM-TAMISEMI, Wizara ya Ujenzi, Makatibu Tawala wa Mikoa na Wahandisi wa Sekretarieti za Mikoa; Wakurugenzi na Wahandisi wa Mamlaka za Serikali za Mitaa, pamoja na wadau wengine mmehudhuria. Ni vyema sana kukaa pamoja ili mzungumze lugha moja maana pamoja na kuwa chini ya mamlaka tofauti, barabara hizi zinamhudumia mteja mmoja yule yule anayehudumiwa na wote yaani mwananchi. Mbele ya jicho la mwananchi, barabara zote ni za Serikali. Haelewi kwa nini ubora wa barabara zinazosimamiwa na Halmashauri utofautiane. Isitoshe, hata pale ambapo Halmashauri ndio iliyojenga barabara isiyo na kiwango, lawama ya mwananchi huenda kwa Serikali nzima kwa ujumla. Hivyo, mnao wajibu wa kukutana na kufanya tathmini za pamoja kama mfanyavyo katika mkutano huu.
Mafanikio katika Barabara za Serikali za
Mitaa kwa Miaka 10
Ndugu Washiriki;
Leo hii, hali ya barabara zilizo chini ya Serikali za Mitaa imekuwa bora zaidi ya ilivyokuwa miaka 10 iliyopita. Hatua tulizopiga, pamoja na mambo mengine zimetokana na maamuzi ya kisera ya kufungua fursa za uchumi vijijini na wilayani. Kwa ajili hiyo tumetenga fedha nyingi zaidi kwa ajili ya ujenzi na ukarabati wa barabara na kuimarisha usimamizi wa miradi ya barabara kuu. Tumeongeza fedha za matengenezo ya barabara, kwa zaidi ya mara 10 kutoka shilingi bilioni 23.8 mwaka 2005/2006 hadi shilingi bilioni 257.7.
Mtandao wa barabara za lami katika Halmashauri umeongezeka kutoka kilomita 790 mwaka 2005/2006 hadi kilomita 1,326 hivi sasa na barabara za changarawe zimeongezeka kutoka kilomita 13,000 mwaka 2005/2006 hadi kilomita 22,089 hivi sasa. Lakini hayo yote yamewezekana kutokana na kuongezeka kwa idadi ya Wahandisi waliosajiliwa (“Registered Engineers’’) kwenye sekta ya barabara katika Halmashauri hivi sasa ni 137 ulinganisha na 70 wa mwaka 2010.
Ili kuimarisha usimamizi na ufuatiliaji wa kazi za barabara kwenye Wizara ya Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa nimeridhia kukipandisha hadhi Kitengo cha Miundombinu kuwa Idara kamili. Idara hiyo ina sehemu tatu ambazo ni Miundombinu Mijini, Miundombinu Vijijini na Utafiti na Mipango.
Aidha Sekretarieti za Mikoa na Halmashauri zote nchini zikiwamo Halmashauri mpya zimekwishapatiwa magari ya usimamizi wa kazi za barabara. Kwa wale waliopatiwa magari muda mrefu uliopita na magari hayo kuanza kuchakaa, utaratibu utafanyika ili waweze kupatiwa magari mapya.
Utekelezaji wa Kazi za Barabara katika Halmashauri
Ndugu Washiriki;
Taarifa za utekelezaji za kila mwisho wa mwaka zinaonyesha kuwa Halmashauri nyingi zimepiga hatua nzuri katika usimamizi na matumizi ya fedha za Mfuko wa Barabara. Nafurahi kusikia kuwa uwezo wa kutumia fedha za Mfuko wa Barabara umeongezeka. Pia kwamba, Sheria ya Manunuzi ya Umma inaeleweka vizuri zaidi na kuzingatiwa. Hali kadhalika, uwezo wa usimamizi wa ubora wa kazi za barabara nao umeongezeka.
Ni jambo la faraja kwamba Halmashauri nyingi nchini zimejenga uwezo wa kusanifu na kusimamia ujenzi na miradi mikubwa ya madaraja. Niruhusuni nitoe mifano michache ya Halmashauri zenye miradi iliyotekelezwa kwa namna hiyo. Halmashauri ya Wilaya ya Morogoro (daraja la Gizigizi), Bariadi (daraja la Gibishi), Kilosa (daraja la Berega), Rufiji (daraja la Mohoro), Kyela (daraja la Kyela), Manisapaa ya Tabora (daraja la Igombe) na Manispaa Arusha (Daraja la Themi). Napenda kuwapongeza wahandisi waliowezesha Halmashauri kwa kuwezesha kusanifu na usimamia ujenzi wa madaraja hayo muhimu.
Ndugu Washiriki;
Napenda pia kuipongeza Bodi ya Mfuko wa Barabara kwa kuanza mchakato wa kutafuta Mtaalam Mshauri wa kufanya uhakiki wa mtandao wa barabara za Serikali Kuu na za Mamlaka za Serikali za Mitaa. Zoezi hili litatupatia takwimu sahihi zitakazotuwezesha kuandaa mpango mzuri wa kuhudumia barabara hizo. Barabara hizi zikiimarishwa kwa kiwango kizuri pamoja na kuweza kupitika majira yote ya mwaka zitasaidia watu kufika kwa uhakika katika maeneo ya uzalishaji mali, masoko na ya utoaji huduma za maisha.
Changamoto Mbalimbali katika Usimamizi wa Barabara
Ndugu Washiriki;
Najua zipo changamoto zinazokabili Mamlaka za Serikali za Mitaa kama vile upungufu wa wataalam wa ujenzi, uchache wa vifaa vya kupimia ubora wa kazi, uhaba na uchakavu wa baadhi ya vyombo vya uchukuzi kwa ajili ya magari ya usimamizi, upungufu wa fedha za ujenzi na ukarabati wa barabara na madaraja na fedha za matengenezo kutokidhi mahitaji. Serikali inazitambua changamoto hizi na imekuwa inazifanyia kazi kadri rasilimali zinaporuhusu. Ninyi ni mashahidi wa namna Serikali yetu ilivyotoa kipaumbele kwenye kazi za barabara.
Ndugu Washiriki;
Zipo pia changamoto za usimamizi zitokanazo na upungufu katika ngazi ya Mkoa na Wizara hizo ni pamoja na hizi zifuatazo:
a) Ucheleweshaji wa utekelezaji wa kazi za ujenzi wa barabara kwa visingizio mbalimbali vitokanavyo na mipangilio mibovu;
b) Kazi za barabara kufanyika kwa viwango duni zikilinganishwa na viwango vya mikataba husika;
c) Kuteua wakandarasi wa kazi za barabara kwa upendeleo kinyume na matakwa ya sheria ya manunuzi na hivyo kupata wakandarasi wasio na uwezo;
d) Kuwepo kwa tuhuma za rushwa katika utoaji wa kazi za barabara;
e) Kuwepo kwa mgongano wa maslahi kwa baadhi ya wataalam na viongozi wa Halmashauri katika usimamizi wa kazi za barabara;
f) Usimamizi duni wa kazi za ujenzi na matengenezo ya barabara;
g) Kupotea kwa nyaraka muhimu zinazohusiana na ujenzi na matengenezo ya barabara.
Ndugu Washiriki;
Majawabu ya changamoto hizo yako ndani ya mamlaka na uwezo wenu kuyatatua, maana yanatendeka machoni penu na katika taasisi zenu mnazosimamia. Ninawakumbusha na kuwasisitizia Viongozi na Watendaji wote wa Halmashauri kutimiza wajibu wenu. Wajibu huo ndio sababu ya ninyi kuwemo kwenye nafasi za uongozi na utendaji mlizonazo. Kama hamtekelezi wajibu huu, je ni yupi mwingine zaidi ya nyie ambaye ni muhimu zaidi kuutekeleza? Nampongeza sana Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni, Ndugu Paul Makonda kwa kuonyesha uthubutu na uongozi. Nimefurahi kuwa Taarifa ya Kamati iliyoundwa na Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni itajadiliwa katika mkutano huu. Kwa ujumla mkutano huu ni fursa ya ninyi kujitathimini, kujifunza na kujipanga upya.
Wadau wa Maendeleo
Ndugu washiriki;
Mafanikio ya juhudi za Serikali vimetokana pia na kuungwa mkono na wadau mbalimbali wa maendeleo. Sina budi kuwatambua na kuwashukuru wadau wafuatao kwa mchango wao muhimu kwa Serikali ya Uingereza kupitia Shirika lake la Maendeleo (DFID) kwa kusaidia katika Programu ya Uboreshaji wa Barabara Vijijini. Serikali ya Marekani kupitia shirika lake la USAID hasa programu ya Feed the Future, Serikali ya Japan kupitia shirika lake la JICA kwa “Rural Roads System Development” na Jumuia ya Ulaya (EU) kupitia ‘’European Development Fund - Capacity Building to LGAs’’ kwa lengo la kuboresha barabara za vijijini Iringa na Ruvuma. Aidha tunawashukuru Benki ya Dunia na Benki ya Maendeleo ya Afrika kutokana na michango yao katika kuboresha barabara kwenye maeneo mbalimbali ya nchi yetu ikiwa ni pamoja na madaraja na kujenga uwezo wa watalaam wetu.
Hitimisho
Ndugu washiriki;
Napenda kuhitimisha hotuba yangu kwa kuwatakia majadiliano mema na mrudipo kazini mkatekeleze vyema majukumu yenu. Hakikisheni pia kwamba katika kutimiza wajibu wenu mnaheshimu na kuzingatia Sheria, Kanuni na Taratibu zilizowekwa. Lengo letu la kutaka tupate matokeo makubwa linategemea sana ushirikiano wenu wa pamoja na mchango wa kila mmoja wenu kwa nafasi yake katika kutekeleza majukumu na wajibu wake vizuri na kwa wakati.
Mheshimiwa Waziri;
Ndugu washiriki;
Hii ni mara yangu ya mwisho kukutana nanyi kabla ya kustaafu kazi ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Napenda kutumia fursa hii kuwashukuru sana kwa mchango wenu, uliowezesha Awamu yangu ya uongozi kuwa na mafanikio makubwa kwenye sekta ya barabara kama ilivyo kwa nyinginezo. Sifa ninazopata katika sekta hii zimetokana na mchango wenu ninyi mliopo na wale mnaowaongoza ambao hawapo hapa. Nawashukuru kipekee Waziri Hawa Ghasia wa TAMISEMI na Waziri wa Ujenzi, Dkt. John Pombe Magufuli kwa uongozi wenu mzuri.
Nastaafu nikiwa na matumaini makubwa kuwa hatutarudi nyuma kwa mafanikio tuliyoyapata katika sekta ya barabara bali tukisonga mbele zaidi. Tumeweka msingi imara hivyo sitegemei kwamba viongozi wajao hawataona umuhimu wa kulisukuma mbele gurudumu la ujenzi na uimarishaji wa barabara nchini. Tena basi, kama Watanzania watamchagua mgombea wa CCM Mheshimiwa John Pombe Magufuli kuwa Rais wa nchi yetu nina uhakika tutapata maendeleo zaidi katika sekta ya barabara kwani yeye I mmoja wa wadau wakubwa wa sekta hii. Mimi namtakia kila la kheri na Mwenyezi Mungu amsaidie. Inshallah Mwenyezi Mungu atapokea dua zetu.
Baada ya kusema hayo, sasa natamka kwa furaha kubwa kwamba Mkutano Nne wa Wadau wa Mfuko wa Barabara za Serikali za Mitaa umefunguliwa rasmi.
Asanteni kwa Kunisikiliza.
- Aug 25, 2015
SPEECH BY H.E. DR JAKAYA MRISHO KIKWETE, PRESIDENT OF THE UNITED REPUBLIC OF TANZANIA ON EAST AFRICA MAGISTRATES AND JUDGES ASSOCIATION, ANNUAL CONFERENCE AND G...
Soma zaidiHotuba
THEME: Enhancing Public Trust and Confidence in the Judiciary: Judicial Accountability, Court Performance and Management Systems
Justice Edward Rutakangwa, Representative of the Chief Justice of Tanzania;
Hon. Bart Kalunebe, Chief Justices of Uganda;
Hon. Justice Omar Makungu, Chief Justice of Zanzibar;
Hon. Nkwirunziza, Vice President of East Africa Court of Justice;
Hon. Ignus Kitusi, President of the Judges and Magistrate Association of Tanzania (JMAT);
Hon. Judges and Magistrates from our Jurisdictions;
Hon. President of the East Africa Magistrates and Judges Association;
Distinguished representative of the Common Wealth Magistrates and Judges Association and other Professional Associations;
Hon. Regional Commissioner for Mwanza Region;
Distinguished delegates;
Invited guests;
Ladies and gentlemen;
It is a pleasure and an honour for me to join you and officiate the opening ceremony of the 2015 Annual Conference and General Meeting of the East Africa Magistrates and Judges Association (EAMJA). I feel privileged to have had the opportunity to do this twice in 5 years. As you may recall the last time was at the 8th Annual Conference on 19th May, 2010 in Arusha.
Tribute to EAMJA
Ladies and Gentlemen;
I Commend the EAMJA for the outstanding achievements recorded in the past 15 years of its existence. You have all along remained consistent and persistent to your vision and mission. The fact you have been able to meet regularly in the past 15 years, is in itself, a testimony of the strength and vibrancy of your association. It is not surprising therefore that you have increased your membership from 3 to 4 countries.
This Association is playing an important role in advancing the East African Community’s integration agenda. Despite your observer status in the East Africa Community, the impact of your work is beyond observing. You have gone a step further to integrate judges and magistrate in the region over and beyond the inter-governmental structures within the Community. I commend you for always being ahead of the political leadership. I see in the work of this Association an important building block being erected which will make it easier for EAC member states to integrate their legal systems at a later stage of integration. Indeed, the dream reflected in the theme of your first conference in 2001 titled “Towards Harmonization of the Administration of Justice in East Africa” looks possible.
Theme of the Conference
Ladies and Gentlemen;
This year’s theme “Enhancing Public Trust and Confidence in the Judiciary: Judicial Accountability, Court Performance and Management Systems” resonates well with the realities of the day. You will agree with me that the demand for better governance is on the rise. There is mounting public pressure on accountability and transparency in public service. The Judiciary has not been spared. People’s expectations on the judiciary are equally on the rise, and at times too overwhelming or overbearing given the capability challenges facing our Courts.
I sincerely commend you for choosing such a pertinent theme. It addresses the perennial complaints of our people which threaten loss of trust and confidence in our Judiciaries. One other important thing the East Africa region needs besides economic cooperation and integration are judiciaries that observe somewhat similar standards with regards to lifespan of cases, commercial case rules of practice and procedures, punishment of offenders and compensation to victims of crime etc.
Much as I understand that it may take us sometime more before we achieve harmonized laws or a common appellate court, I believe there are things which always form a common denominator that when put in place or done the feeling of relief will be felt across the region. For instance, it is good for an East African to be able to predict the duration of litigation in our Courts, the level of ethics and competence of Judicial and non-Judicial officers.
When I looked at the program of this Conference, it gave me a course of satisfaction. I am informed, that there will be discussion on Measuring Court Performance and Case Management System, Women’s Right to inheritance and strategies of addressing case delays. I have been made to understand that blue prints for measuring court performance are hard to come by but the fact that you have included such a topic in your program reassures some of us that Judges and Magistrates have now taken upon themselves the leading role to measure their performance.
I think I can speak with confidence that no Chief Justice wants to head a Judiciary whose judges and magistrates can choose to work or not to. We may go on to ask, is it not good for the people of East Africa to have courts that have performance standards? Is it not better for our people if these standards were Regional but at the same time benchmarking on international standards?
Our judiciaries have no choice if they are to remain relevant and enjoy public trust. What is the use of a judiciary or a court-of law if the people who are the primary clients do not rely on it in pursuit of justice? It is not uncommon in our countries, to see people resort to mob justice and other barbaric ways to settle disputes. Indeed, such acts impact negatively in our quest to promote judiciary, peace and security but what do we make of it? It is heartwarming indeed, to note that the judiciary in Tanzania has responded in a fashionable manner by introducing benchmarks and targets to ensure timely and quality delivery of justice.
Efforts of Enhancing Public Confidence and Trust in Tanzania
Ladies and Gentlemen;
It is true that the judiciary has the primary responsibility to respond to public demands for accountability and trust. However, Judiciary cannot achieve it alone, since the question of justice and access to justice involves equally the Executive and the Parliament. As we know, the Judiciary is only to interprets laws encted by Parliament. It is Parliament which makes laws that promotes access to justice. Therefore, for the Judiciary to be seen to deliver justice, it must first and foremost use laws which in themselves are seen and perceived to be just.
The share of the Executive in supporting the Judiciary to win public trust and confidence is equally unequivocal. It is the Executive that has a role to ensure the Judiciary get the requisitive finances, manpower and infrastructure to be able to meet public demands for timely and quality justice. I say so having in mind that at times, the delays of cases may be a function of limited capacity than indifference and incompetence of the Judges and magistrates.
The Role of the Executive
Ladies and Gentlemen;
My administration has taken a number of measures in the past 10 years to enhance the Court’s ability to respond to the challenges of maintaining public trust and confidence through increased accountability, improved performance and management systems. I understand that this August Assembly will receive country presentations. Therefore, you will be presented with our Tanzania’s experience. It suffices therefore, to mention that my government made the following interventions.
i. To put in a place the Judiciary Fund in year 2011 with the idea of giving the judiciary increased ability to plan and execute its program. We are yet to perfect the new systems of financing the judiciary, but there has been a significant increase in budgetary allocations. For example the judiciary budget has increased from 36.6 billion Tanzania Shillings in 2005 to 88.9 billion Shillings in 2015. But we need to do more.
ii. To address the issue of manpower by increasing number of Judges, Magistrates and staff of the court. The number of the Judges for the Referral Court has increased from 9 in 2005 to 16 in 2015, High court Judges from 35 in 2005 to 94 in 2015 and Resident Magistrates from 151 in 2005 to 677 in 2015.
iii. The other significant thing has been the sharp increases in the number of women Judges and Magistrates. There are now 41 women judges in both Referral Court and High Court, compared to 8 in 2005. Such affirmative action has had some significant impact on winning public confidence and trust, and increasing sensitivity to women’s rights on issues such as land and inheritance.
iv. Improve the remuneration packages for the Judges and Magistrates by enacting the Judges Remuneration Act No. 4 of 2007 to provide incentive for Judges and Magistrates to perform their noble duties judiciously.
v. Development of the court infrastructure by embarking on a comprehensive program to build more Primary Courts, Resident Magistrates Courts and High Courts. According to this program we build High Courts in every region for the same purpose to enable people to have access to court close to where they live.
Ladies and Gentlemen;
As a result of collaborative efforts, the Judiciary has been able to register remarkable improvements in its performance of our Judiciary. The Chief Justice Othman Chande and his team came with the plan reminiscence of the governments “Big Result Now” (BRN), a mechanism adopted by the government to ensure effective government delivery. In Judiciary’s BRN, they have set a benchmark for every Judge to handle at least 220 cases per year and Resident Magistrates 250 cases per year and 260 cases for primary court magistrates. They have also set a target of a period of 2 years for a case to stay at the Court. They also undertook to deal with the huge backlog of cases with remarkable success. So far 50 percent of such cases have been cleared in the past two years. Likewise, I am told they have rolled out new Management Information System (MIS) which enable the Chief Justice to track and know how many cases have been registered, how many files closed and how many files each Judge has from his desk.
I am amply encouraged by the progress made and being made. I look to the future of our judiciary with a great sense of optionism. The future is very promising indeed.
Conclusion
Ladies and Gentlemen;
This Assembly offers a unique opportunity to learn from each other’s experience and best practices. I find it important that you find ways and means of forging closer for collaboration. Such collaboration will go a long way towards bringing closer our judicial systems as we walk towards deeper East Africa integration and hopefully the Federation. I dream to see your Association rise to the occasion and take our Community to greater heights. I encourage you to keep up the good work.
As earlier said, this will be my second EAMJA Assembly to officiate. This is also the last to officiate as the President of the United Republic of Tanzania. I will leave office after the elections in October 2015. This is therefore, an opportunity for me to bid you farewell. I will go to my retirement happily that I played my part in promoting access promoting East African integration and increased the quality of Justice for Tanzanians.
With these many words, I declare this Assembly and conference officially opened.
I thank you for your kind attention
- Aug 21, 2015
SPEECH BY HIS EXCELLENCY DR. JAKAYA MRISHO KIKWETE, PRESIDENT OF THE UNITED REPUBLIC OF TANZANIA, AT THE SADC LAWYERS' ASSOCIATION ANNUAL CONFERENCE AND GENERAL...
Soma zaidiHotuba
The President of the SADC Lawyers’ Association, Mr Gilberto Caldeira Correia;
The President of the Tanganyika Law Society, Mr Charles Rwechungura;
The Chairperson of the Commission for Human Rights and Good Governance in Tanzania, Hon Tom Bahame Nyanduga;
The Director of Jurisdiction, Complimentarily and Cooperation Division of the International Criminal Court, Mr Phakiso Mochochoko;
The Legal Council and Director of Legal Affairs for the African Union, Professor Vincent Nmehielle;
Presidents of the Law Societies and Bar Associations here present;
Distinguished ladies and gentlemen, all protocol is observed;
It is an honour and a pleasure for me to join you and grace the 16th Annual Conference and General Meeting (AGM) of the SADC Lawyers' Association. I welcome to Tanzania and to Dar-es-Salaam all delegates from other SADC member states in particular. I trust that you have been received well and that your hosts are taking good care of you.
Tribute to Tanganyika Law Society
Ladies and Gentlemen;
I equally commend the Tanganyika Law Society for hosting this Annual General Meeting. I congratulate you on assuming this very important responsibility and discharging it so well. It’s an honour and a pride for Tanzania. If there is any way you think we in Government can be useful don’t hesitate to let us know.
Appreciation to the SADC Lawyers
Association (SADCLA)
Ladies and Gentlemen;
It is fair to give credit where it is due. The SADC Lawyers Association deserves praise for its success in integrating lawyers and bar associations in the region. Congratulations on a job very well done. Since its establishment in 1999, the Association has been able to expand its membership to all the 15 member countries of SADC. Congratulations on remaining faithful to your mission of upholding and defending the rule of law without fear or favour.
Indeed, this is what we mean by regional integration. For me, there is no better way of promoting regional integration in SADC, than to see sons and daughters, institutions and nations in the SADC region, coming together in their sameness and diversity under the banner of a single profession like what the SADC Lawyers Association has done. These are important building blocks of our development endeavours. I wish other professional bodies could emulate your good example.
I am of the opinion that, such people to people contact is what precipitates and drives the integration agenda. The SADCLA will go a long way towards facilitating cross boarder legal practices when we reach the common market stage. I appreciate the fact that you have started to match and be ahead of experts and politicians. We should learn from you.
Theme for the SADCLA Assembly
Distinguished Guests;
I commend the organisers for choosing a very pertinent theme of your meeting: “Using the law to strengthen good governance practices and to facilitate social, economic and political transformation in the SADC Regions” It rhymes well with what is being done in SADC at present. As you might be aware, at the 34th SADC Summit that was held in Zimbabwe in 2014 we agreed to focus on industrialisation in the SADC region through the development of a regional industrialisation strategy. Therefore, this theme is very befitting, timely and relevant to take us forward.
You will agree with me that, the importance of the law in social, economic and political transformation needs no further emphasis. History is full of ample examples and cases which attest to such a causal relationship. Indeed, the level of sophistication of society can be reflected in the level of development of the laws and the legal systems. Laws give life to policies and create an environment and platform on which social, economic and political transformation can take place. Laws give legitimacy, confer obligations, duties and responsibilities, harmonize roles and functions of different players and administer fairness and justice.
Laws are important in attracting investment, raising investor confidence and assuring investors on the predictability of the policy environment which is a critical pre-requisite for the growth of investment. Legal instruments such as Avoidance of Double Taxation, Protection of Investments, Mechanisms for Settlement of Disputes, Environment Protection, Labour regimes and the like must be in place for a country or region to be an investment destination of choice for investors.
More importantly, there should be harmonization of legal and fiscal regimes across the region so as to avoid unfair competition among players. It suffices to say that laws are an important instrument for the realization of SADC industrialization program. It is incumbent upon you, our lawyers, to advise governments and other state holders with regard to how best should our region approach such a transformation. This makes your gathering here in Dar es Salaam and the outcome of your deliberations to be of special interest to all of us.
Importance of Law on Tanzania Transformation
Ladies and Gentlemen;
The importance of law in realizing social, economic and political transformation has been as well captioned in Tanzania’s transformation agenda. Tanzania is implementing three 5 years development plans with the ultimate goal of enabling our country realize the Development Vision of becoming a middle income country by 2025.
The success of implementation of development plans demand changes in the way we do business inside the government. There is a need to improve government’s delivery and ability to track and account for the results so as to ensure effectiveness in implementation. For that reason, we instituted a mechanism and tagged it “Big Result Now (BRN)”, borrowing a leaf from the Malaysian model. One of the things we have embarked on doing, in this regard was to address problems of doing business in Tanzania.
We initiated what we called a Business Environment Laboratory where all stakeholders in the business fraternity met and held open and in depth discussions on the challenges facing the business environment. The teething issues were identified and solutions were proposed.
The laws of the land as well as legal and fiscal regimes were identified as among stumbling blocks to the growth of business in Tanzania. Issues of enforcement of contracts, conflicting laws and regulations and delay in adjudication of cases in the Courts of Law were also identified as constraints to business. The report of the Lab has resulted in the ongoing legal reform to free encumbrances in doing business.
Role of SADCLA
Ladies and Gentlemen;
I have been made to understand that one of the objectives of the SADC Lawyers’ Association at its formation was the protection and promotion of the rights of vulnerable and marginalised people in the region, including women and children. I wish to seize this opportunity to congratulate you on this decision and urge you not to lose sight of such an important founding principles. In holding such tenets close to your hearts, as lawyers, you will also draw yourselves close to the hearts of the ordinary people in society who look up to you for protection, advise and assistance. The development and implementation of lawyer led legal aid and pro bono models through the law societies are therefore important in ensuring that lawyers have in place structured ways of providing legal services to those in need in our society.
SADCLA and SADC Tribunal
Ladies and Gentlemen,
I am also aware that lawyers in the region have had a disagreement with SADC leaders regarding the decision to suspend the SADC Tribunal on 18th August, 2010, and the eventual decision by the 32nd SADC Summit on August 2012 to make the Tribunal an intestate court and therefore inaccessible to the citizens of SADC. I am also aware that the Tanganyika Law Society and the Law Society of South Africa have taken this disagreement before the Courts of Law in their respective countries for adjudication.
I am of the view, however, that whilst the Court processes are ongoing, the SADCLA could explore the possibility of reaching out to regional governments and have constructive engagements over the issue. I say so, fully cognisant of the fact that, this matter is not only legal but also political. Therefore, all possible avenues should be sought. A more holistic approach may be the wisest thing to do.
Africa and the ICC
Ladies and Gentlemen;
I am glad also you have included, in your programme, a discussion on international criminal justice and the place of Africa in such discourses. It is common knowledge, that the Africa Union and many African leaders have not been the best of friends and partners of the International Criminal Court (ICC). There are strong feelings that African leaders are being unduly targeted while the same is not being done to leaders who commit similar or even worse crimes in other parts of the World. The Court looks selective and discriminatory, in the eyes of African leaders hence the movement to ask African Nations to withdrawal membership of the ICC. If is yet to succeed but the sustained campaign may. We look forward with great anticipation to the outcome of your discussions on the matter.
Conclusion
Ladies and Gentlemen;
This is the last time I will ever have an opportunity to address this august Association as President of my dear country, the United Republic of Tanzania. After the General Election scheduled for 25th October, 2015, Tanzania will have a new leader and I will join H.E. Ali Hassan Mwinyi and H.E. Benjamin William Mkapa in the list of retired Presidents. This Assembly, therefore, presents me with the rare opportunity to bid farewell to you all. As I leave office, I feel proud that the future of SADC is very promising indeed. I am amply satisfied to have had the opportunity to make my humble contribution to this wonderful organization. Let all of us continue to play our part of the bargain to promote and advance the agenda for integration to the highest level possible.
Learned brothers and sisters, with these many words, it is now my singular honour and pleasure to declare the 16th Annual Conference and General Meeting of the SADC Lawyers’ Association officially opened. Long live SADC, long live SADCLA!
Ahsanteni sana!
- Aug 14, 2015
HOTUBA YA RAIS WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA, MHESHIMIWA JAKAYA MRISHO KIKWETE, AKIZINDUA HATI ZA AHADI YA UADILIFU KWA VIONGOZI, WATUMISHI WA UMMA NA SEK...
Soma zaidiHotuba
Mheshimiwa George Huruma Mkuchika, Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Utawala Bora;
Ndugu Sofia Mjema, Kaimu Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam;
Mheshimiwa Balozi Ombeni Yohana Sefue, Katibu Mkuu Kiongozi;
Makatibu Wakuu Mliopo;
Ndugu Tixon Nzunda, Kaimu Kamishna wa Maadili;
Ndugu Ali Mfuruki, Mwenyekiti wa CEO’s Roundtable;
Bw. Omari Issa, Afisa Mtendaji Mkuu, PDB;
Bw. Frank Kanyusi, Afisa Mtendaji Mkuu, BRELA;
Viongozi wa Vyama vya Siasa;
Viongozi wa Serikali;
Viongozi wa Dini;
Wawakilishi wa Sekta Binafsi;
Wageni Waalikwa;
Mabibi na Mabwana;
Nakushukuru sana Mheshimiwa George Huruma Mkuchika kwa kunialika katika tukio hili muhimu la kuzindua Hati za Ahadi ya Uadilifu kwa Viongozi wa Umma, Watumishi wa Umma na Sekta Binafsi. Namshukuru pia Ndugu Tixon Nzunda anayemuwakilisha, Mheshimiwa Jaji Salome Suzette Kaganda, Kamishna wa Tume ya Maadili kwa maelezo yake ya utangulizi kuhusu Hati za Ahadi tunazozindua leo. Napongeza wewe, na ofisi yako kwa maandalizi mazuri ya shughuli hii.
Kuzinduliwa kwa Hati za Uadilifu leo ni hatua kubwa, muhimu na ya kihistoria katika safari yetu ya kuboresha na kuhuisha mifumo ya uadilifu iliyopo ili iweze kwenda sambamba na mazingira na nyakati tulizonazo. Kama mnavyofahamu, jitihada hizi za kujenga misingi na mifumo ya uadilifu zimeanza mara baada ya kupata uhuru. Kwa ajili hiyo napenda kutambua Sheria ya Maadili ya Taifa 1962, Tume ya Kudumu ya Uchunguzi 1965, iliainisha Miiko ya Viongozi kwa mujibu wa Azimio la Arusha 1967, Sheria ya Kamati ya Utekelezaji wa Miiko ya Uongozi Na. 6 ya 1973 ambayo baadaye ilibadilishwa kuwa Tume kwa Sheria Na. 5 ya 1987, Sheria ya Kuzuia Rushwa Na. 16 ya 1971, Sheria ya Maadili ya Viongozi wa Umma Na. 13 ya 1995 na Maboresho katika Sekta ya Umma na Mamlaka za Serikali za Mitaa.
Umuhimu wa Maadili Katika Taifa
Mheshimiwa Waziri na Wageni Waalikwa;
Maadili ya Taifa ni moja ya tunu muhimu zinazolitambulisha Taifa na kutofautisha Taifa moja na lingine. Maadili mema ni kichocheo kikubwa cha maendeleo ya taifa, hujenga umoja, amani, upendo, uvumilivu na mshikamano katika Taifa. Maadili huchora mstari kati ya mema na maovu, mambo yanayovumilika na yasiyovumilika, yanayositirika na mambo yasiyositirika. Hivyo maadili ni nyenzo muhimu sana katika ujenzi wa taifa na huepusha taifa kuingia katika mifarakano na migogoro.
Leo hii nchi yetu inajipambanua kuwa nchi yenye amani kwa sababu ya kazi kubwa ya ujenzi wa maadili iliyofanywa tokea uhuru na kutujengea mshikamano, kuvumiliana na kuheshimiana. Si kweli hata kidogo kuwa sisi Watanzania tumezaliwa na vinasaba vya amani au kinga dhidi ya machafuko. Amani na umoja wetu ni zao la kulinda na kuheshimu maadili yetu. Hivyo hatuna budi nasi kuyalinda kwa uwezo wetu wote.
Chimbuko la Hati za Maadili
Mheshimiwa Waziri na Wageni Waalikwa;
Kwa muda mrefu kumekuwepo na changamoto kubwa katika kupambana na rushwa kama moja ya tatizo kubwa la utovu wa uadilifu nchini. Tumechukua hatua kadhaa ikiwemo kutengenezwa kwa Mkakati wa Mapambano Dhidi ya Rushwa na mabadiliko katika Sheria ambayo yalipelekea kuanzishwa kwa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) badala ya iliyokuwa Taasisi ya Kupambana na Rushwa (TAKUKURU). Tumepata mafanikio makubwa na ya kutia moyo ingawa bado zipo changamoto na manung’uniko ambayo hatuwezi kuyapuuza.
Kwa madhumuni ya kuyaongezea mapambano haya nguvu na kasi, tukaamua Mpango wa Mapambano dhidi ya Rushwa uingizwe katika Mpango wa Matokeo Makubwa Sasa (BRN) ili kutoa msukumo wa pekee katika utekelezaji wake. Ahadi ya Uadilifu ni moja ya maeneo 12 iliyo katika Mpango wa Mapambano dhidi ya Rushwa chini ya Mpango wa Tekeleza sasa kwa Matokeo Makubwa (BRN). Maeneo mengine ni yafuatayo:
- i. Kuimarisha mwamko na uelewa kuhusu mapambano dhidi ya rushwa;
- ii. Kuwaumbua wala rushwa (name and shame);
- iii. Kuandaa Mtaala wa Maadili katika ngazi zote za elimu;
- iv. Kutoa taarifa kwa njia ya mtandao;
- v. Kuchukua hatua kali za kisheria dhidi ya wala rushwa;
- vi. Kulinda watoa taarifa na mashahidi wa vitendo vya rushwa;
- vii. Kuboresha, kuhuisha na kuweko uwiano wa maslahi katika sekta ya umma;
- viii. Kupunguza mlundikano wa kesi Mahakamani;
- ix. Matumizi ya mtandao katika manunuzi ya umma;
- x. Kuimarisha mfumo wa taarifa, ufuatiliaji na tathmini; na
- xi. Kuhakikisha utoaji wa huduma kwa wakati kwa njia ya Mkataba wa Huduma kwa Mteja.
Ahadi za Uadilifu
Mheshimiwa Waziri na Wageni Waalikwa;
Hati za Ahadi za Uadilifu tunazozindua leo hii ni za aina tatu. Kuna Hati ya Ahadi ya Uadilifu kwa Viongozi wa Umma; Hati ya Ahadi ya Uadilifu ya Watumishi wa Umma; na Hati ya Ahadi ya Uadilifu ya Sekta Binafsi. Kwa upande wa Sekta ya Umma, Hati hizi zitasimamiwa na Menejimenti ya Utumishi wa Umma kupitia Waraka maalum utakaotoa mwongozo wa utekelezaji wa mpango huu. Kwa upande wa sekta binafsi, Hati za Uadilifu zitasainiwa kati ya makampuni binafsi na Wakala wa Usajili wa Biashara na Leseni (BRELA).
Kuwepo kwa Hati za Uadilifu kunaimarisha sana mapambano ya kisheria dhidi ya rushwa na makosa mengine ya kiuadilifu. Hati za Uadilifu zinachochea utashi wa wale waliosaini hati hizo kuishi na kuenenda katika misingi ya uadilifu. Inatoa fursa kwa kujipima na kujitathimini wenyewe tofauti na mifumo ya kisheria ambayo msisitizo wake ni kutoa adhabu mara baada ya kitendo kutokea. Hati ya Uadilifu inachochea ile hali ya nadhiri ya mtu kumsuta na hivyo kumfanya atii bila shuruti. Huu ni mwanzo mzuri katika kujenga utamaduni wa kuheshimu maadili badala ya watu kushinikizwa kuyafuata maadili bila kuyaamini maadili yenyewe.
Nawapongeza pia kwa uamuzi mzuri wa kufanya tathmini kila baada ya miaka mitatu kuona namna ambavyo mfumo huu utakuwa ukifanya kazi. Ufuatiliaji ni muhimu sana ili kufanya Hati za Maadili kuwa na maana. Vinginevyo, kusaini Hati ya Maadili kunaweza kuchukuliwa kama utekelezaji wa matakwa ya mwajiri au Serikali na sio wajibu na ahadi ya kuishi na kukienzi kiapo chenyewe. Mimi naamini huu ni mwanzo mzuri sana katika safari ya kujenga uadilifu nchini.
Wito kwa Sekta Binafsi
Mheshimiwa Waziri na Wageni Waalikwa;
Uwepo wa Hati za Uadilifu kwa sekta binafsi ni hatua ya kimapinduzi katika ujenzi wa utamaduni mpya wa uwajibikaji. Kwa muda mrefu jitihada za kujenga uadilifu na kupambana na rushwa umekuwa ukilenga sekta ya umma pekee. Ni ukweli ulio wazi kuwa, rushwa katika sekta ya umma haifanywi na watumishi wa sekta ya umma pekee. Maana ili watumishi wa umma wapokee rushwa, lazima pawepo na mtu wa sekta binafsi anayetoa. Wapo wanaotoa kwa kuombwa lakini pia wapo wanaotoa bila kuombwa ili kushawishi wapate nao upendeleo kwa tenda. Kwa minajili hiyo, kutoshiriki kwa sekta binafsi katika mapambano dhidi ya rushwa hupunguza kasi na nguvu ya mapambano hayo. Nafurahi kuwa sasa sekta binafsi nayo imeamua kuwa sehemu ya suluhisho badala ya kuwa sehemu ya tatizo.
Ninaposema hivyo, simaanishi kuwa watu wote au makampuni yote katika sekta binafsi yanashiriki vitendo vilivyo kinyume na maadili ikiwemo rushwa. Natambua kuwa hata kabla ya kubuniwa kwa Hati za Uadilifu, tayari zilikuwepo kampuni ambazo zilishajiwekea hati za uadilifu zenye kuhusisha maadili kama uwazi katika ulipaji kodi, kutoshiriki katika rushwa na utii wa Sheria na kanuni za kuendesha biashara zao. Makampuni haya yamekuwa wahanga wakubwa kutokana na kuwepo kwa makampuni mengine ambayo hayafuati maadili hayo. Matokeo yake imekuwa ni gharama sana kwa makampuni kufuata misingi ya uadilifu kuliko kutoifuata. Hawa ndio wamekuwa wakinung’unika sana juu ya kuwepo kwa mazingira yasiyoridhisha ya kufanya biashara.
Ninafurahi kuwa kumekuwa na uungwaji mkono wa mfumo huu wa Hati ya Uadilifu miongoni mwa wadau wa sekta binafsi. Leo hii tumeshuhudia Mwenyekiti wa CEO’s Roundtable akitia saini Hati za Uadilifu akiwakilisha makampuni yapatayo 100 yaliyoonyesha utayari. Natambua kuwa wako wale ambao hawajafurahia sana utaratibu huu na wangependa usifanikiwe. Nawasihi nao wajifunze kutoka kwa wenzao na wawe tayari kubadilika. Kushiriki kwa wenzao ni kielelezo kuwa inawezekana kufanya biashara kwa kufuata maadili na ukapata faida. Tena kadiri wote watakapoingia katika utaratibu huu, uwanja wa kufanya biashara utakuwa sawia zaidi na kumfanya kila mmoja kunufaika kuliko ilivyo sasa.
Ahadi ya Serikali
Mheshimiwa Waziri na Wageni Waalikwa;
Serikali itaendelea kuimarisha utendaji Serikalini na kupambana na maovu katika jamii, hususan rushwa na utovu wa maadili. Tutaendelea kuchukua hatua thabiti za kuzuia viongozi na watumishi wa umma kutumia nafasi zao kujitajirisha, kujilimbikizia mali na kujipatia manufaa binafsi isiyo halali. Tuko tayari kutunga Sheria mpya, kurekebisha zile zilizopo na kujenga mifumo mizuri ya usimamizi wa uadilifu, uwajibikaji, uwazi na mapambano dhidi ya rushwa.
Tumeiishi dhamira yetu hiyo kwa vitendo kwa kuwezesha kutungwa kwa Sheria mpya ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa, Sheria ya Kudhibiti Gharama za Uchaguzi, Sheria ya Ukaguzi wa Umma na hivi karibuni Sheria ya Kulinda Watoa Taarifa na Mashahidi. Pia, Serikali yetu ni mwanachama wa Mpango wa Afrika wa Kujitathimini Kiutawala Bora (APRM) na Mpango wa Uendeshaji Serikali kwa Uwazi (OGP) ambayo yote kwa pamoja inasisitiza uadilifu katika uendeshaji wa shughuli za Serikali.
Serikali inaahidi kuiwezesha Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma kwa Rasilimali fedha ili iweze kuutangaza mpango huu vyema na kujenga uelewa mpana wa wadau wote muhimu katika mapambano dhidi ya rushwa. Tunaahidi kutekeleza sehemu ya wajibu wetu kwa kusimamia vyema na kuhakikisha Hati za Uadilifu kwa Viongozi wa Umma na zile za Watumishi wa Serikali zinasainiwa, na wanaozisaini wanaziishi na kuzizingatia katika kutekeleza wajibu wao. Tutahakikisha pia tunashirikiana na sekta binafsi katika kutekeleza mpango huu. Azma yetu kwa siku za usoni ni kutoa kipaumbele katika zabuni zitolewazo na Serikali kwa yale makampuni ambayo yanashiriki katika mpango huu, kama tufanyavyo sasa kwa kutoa zabuni kwa makampuni yenye hati ya mlipa kodi na mashine za EFD.
Hitimisho
Mheshimiwa Waziri na Wageni Waalikwa;
Ni matarajio yangu kwamba Viongozi wa Umma, Watumishi wote wa Umma na Makampuni yaliyosajiliwa Tanzania yatasaini Hati ya Ahadi ya Uadilifu na kuwasilisha kwa Mamlaka inayohusika na kusimamia utekelezaji wake ndani ya Taasisi zao ikiwa ni ishara ya kuonesha utayari wao wa kukuza uadilifu na kupambana na vitendo vya rushwa.
Nawasihi wadau wote muendelee kuunganisha nguvu mliyoionesha katika maabara ya BRN na uandaaji wa Ahadi ya Uadilifu katika kukuza uadilifu nchini. Aidha, ninawaomba wananchi wote kushirikiana na Serikali katika kufichua vitendo vya rushwa na utovu wa maadili, pia kufuatilia utekelezaji wa ahadi zilizotolewa na Viongozi, Watumishi wa Umma na Sekta Binafsi.
Nimalize kwa kusema kuwa mapambano dhidi ya utovu wa maadili na rushwa katika Serikali na sekta binafsi ni jambo linalohitajika kuwa endelevu, wakati wote tuwe makini na wabunifu ili kuendeleza mapambano hayo. Mpango huu tunaouzindua leo ni utekelezaji thabiti wa dhamira hiyo njema.
Kwa maneno hayo mengi, sasa niko tayari kuzindua Hati za Ahadi ya Uadilifu ambazo zitakuwa nyenzo muhimu katika Kampeni ya Kitaifa ya Maadili na Mapambano dhidi ya Rushwa.
Nawashukuru kwa Kunisikiliza
- Aug 08, 2015
HOTUBA YA MHESHIMIWA DKT. JAKAYA MRISHO KIKWETE, RAIS WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA, SIKU YA KILELE CHA MAADHIMISHO YA SIKUKUU YA WAKULIMA (NANE NANE) KAT...
Soma zaidiHotuba
Mhe. Stephen M. Wasira, Waziri wa Kilimo Chakula na Ushirika;
Mhe. Dkt. Titus Kamani, Waziri wa Maendeleo ya Mifugo na Uvuvi;
Waheshimiwa Mawaziri wote mliopo hapa;
Mhe. Mwantumu Mahiza, Mkuu wa Mkoa wa Lindi na mwenyeji wetu;
Wakuu wa Mikoa mliopo;
Ndg. Engelbert Moyo, Mwenyekiti TASO Taifa;
Ndg. Wakulima, Wafugaji, Wavuvi na Wanaushirika;
Wageni Waalikwa;
Mabibi na Mabwana;
Nawashukuru Mheshimiwa Waziri Stephen Masato Wassira na Eng. Engelbert Moyo, Mwenyekiti wa TASO kwa kunialika na kunishirikisha katika maadhimisho ya mwaka huu ya Nane Nane yanayofanyika Kitaifa hapa Lindi. Aidha, nakushukuru Mheshimiwa Mwantumu Mhiza, Mkuu wa Mkoa wa Lindi na wananchi wa Lindi kwa mapokezi mazuri na ukarimu wenu. Hali kadhalika nakupongeza wewe na Mheshimiwa Halima Dendegu, Mkuu wa Mkoa wa Mtwara kwa kukubali kuwa wenyeji wa maadhimisho haya kwa mwaka wa pili mfululizo.
Pia nawapongeza kwa kushirikiana vizuri na Chama cha (TASO) kwa maandalizi mazuri ya maadhimisho haya. Nimetembelea mabanda ya maonyesho na kuridhika kuwa yamefana. Pamoja na hayo bado kuna kazi kubwa ya kufanya ili kuboresha miundombinu ya hapa uwanjani na kufanya kuwa mazuri zaidi.
Kwa ujumla nafurahi kuona maonyesho haya yakizidi kustawi mwaka hadi mwaka tangu yalipoanzishwa mwaka 1993. Linalofurahisha zaidi ni kile kitendo cha kuongezeka kwa idadi ya viwanja na Kanda za Maonesho kutoka tatu mwaka 2005 hadi tano hivi sasa kuna. Kanda ya Ziwa (Mwanza), Kanda ya Kati (Dodoma), Kanda ya Mashariki (Morogoro), Kanda ya Kaskazini (Arusha), Kanda ya Nyanda za Juu Kusini (Mbeya) na Kanda ya Kusini hapa Lindi.
Hali kadhalika nawapongeza TASO kwa utaratibu wenu mzuri wa kuchagua Kanda moja kufanya maadhimisho ya Kitaifa na Kanda nyingine kufanya maonyesho ya Kikanda. Uendelezeni utaratibu huu kwani ni kichocheo kizuri cha maendeleo ya kilimo na ufugaji nchini.
Kauli Mbiu
Mheshimiwa Waziri, Mwenyekiti wa TASO na
Ndugu Wananch;
Nimefurahishwa pia na chaguo lenu la kauli mbiu ya Maadhimisho haya ambayo ni “Matokeo Makubwa Sasa - Tuchague Viongozi Bora kwa Maendeleo ya Kilimo na Ufugaji”. Kaulimbiu hii, imezingatia shughuli kubwa tuliyonayo mwaka huu ya kuchagua Rais, Wabunge na Madiwani watakaoliongoza Taifa kwa miaka mitano (5) ijayo. Nakubaliana nanyi kuwa tuwe makini katika kuchagua na hasa tupate viongozi ambao watatuwezesha kupata mafanikio makubwa katika kilimo chetu na ufugaji wetu pamoja na mambo mengineyo makubwa na madogo nchini.
Nakubaliana nanyi, vilevile kuwa kuna kila sababu ya kukamilisha miradi na hatua ambazo tumezichukua chini ya Mpango wa Matokeo Makubwa Sasa katika Kilimo. Kukamilika kwa kazi hiyo na kupata matokeo hayo kutainua sana hali ya kilimo na ufugaji nchini. Ni ukweli usiopingika kuwa tukiwa na viongozi wazuri mambo yetu yatakuwa mazuri na tukiwa na viongozi wasiokuwa wazuri mambo yatatuharibikia.
Hivyo basi, ndugu zangu ni muhimu sana kuitumia vizuri fursa hii adimu na adhimu. Tutunze shahada zetu za kupigia kura, tujitokeze kwenye kampeni za vyama, kusikiliza Sera na Ilani za vyama kama zitakavyonadiwa na wagombea na hatimaye kujitokeza kwa wingi kufanya uamuzi sahihi tarehe 25 Oktoba, 2015 kupitia kura zetu. Kura yako ina maana na thamani kubwa kwako, nchi yetu na watu wake.
Hali ya Sekta ya Kilimo
Ndugu Wananchi;
Katika kipindi chote cha miaka 10 ya uongozi wangu sekta ya kilimo inayojumuisha ukulima, ufugaji na uvuvi, imeendelea kuwa sekta kiongozi. Inaongoza katika kutoa ajira na tegemeo la maisha kwa asilimia 75 ya Watanzania wanaoishi Vijijini. Kilimo kinachangia asilimia 25 ya Pato la Taifa na asilimia 34 ya fedha za kigeni. Kinatupatia chakula na malighafi ya viwanda vyetu.
Bahati nzuri kwa upande wa chakula tumeongeza kiwango cha kujitegemea kutoka asilimia 95 mwaka 2005 hadi asilimia 125 mwaka 2014. Kutokana na umuhimu huo Serikali imekuwa ikitoa kipaumbele cha juu katika kuendeleza kilimo kwa lengo kuu la kuongeza tija na uzalishaji. Upatikanaji wa masoko ya uhakika na bei nzuri kwa wakulima hivyo kuongeza mapato na kupunguza umaskini.
Ni bahati ya kipekee kwangu kwamba sherehe hizi zinafanyika wakati nami nakamilisha Awamu yangu ya Uongozi wa nchi yetu. Hivyo ni fursa nzuri ya kutoa mrejesho wa kile tulichoahidi kufanya kuhusu kilimo na kile tulichotekeleza. Katika hotuba yangu ya kufungua Bunge tarehe 30 Desemba, 2005, niliahidi kuwa Serikali ya Awamu ya Nne itachukua hatua madhubuti kuboresha kilimo na kuanza safari ya Mapinduzi ya Kijani. Kwa ajili hiyo tulikamilisha mchakato wa kutayarisha Programu ya miaka 7 ya Maendeleo ya Sekta ya Kilimo (Agriculture Sector Development Programme - ASDP). Katika Programu hiyo, matatizo yanayofanya tija na uzalishaji katika kilimo kuwa mdogo yalitambuliwa na kutengenezewa mpango wa kuyatatua. Serikali pia ilianzisha mikakati, programu na mipango mingine ya kuongeza msukumo katika kuleta magaeuzi ya kilimo. Miongoni mwa hayo ni mkakati wa Kilimo Kwanza, Mpango wa Kuendeleza Kilimo katika Ukanda wa Kusini mwa Tanzania (SAGCOT), Mpango wa Uwekezaji katika Sekta ya Kilimo (TAFSIP), Sera ya Umwagiliaji ya mwaka 2010 na Programu ya Mageuzi na Modenaizesheni ya Ushirika na mpango wa "Matokeo Makubwa Sasa".
Utekelezaji wa mipango na programu hizo umekuwa na matokeo mazuri. Hatua ya kwanza muhimu ilikuwa kuongezeka fedha kwanye bajeti ya Sekta ya Kilimo kutoka shilingi bilioni 233.3 mwaka 2005/2006 hadi kufikia shilingi bilioni 1,084.7 mwaka 2014/2015. Kutokana na ongezeko hilo tumeweza kufanya mambo mengi yanayoihusu Serikali. Kwa mfano, fedha za ruzuku ya mbolea na pembejeo zimeongezeka kutoka shilingi bilioni 7.5 mwaka 2005/2006 hadi kufikia shilingi bilioni 299.3 mwaka 2013/2014. Maana yake ni kuwa, wakulima wengi zaidi wananufaika kuliko ilivyokuwa zamani. Shughuli za utafiti zimeendelea kuimarishwa pamoja na huduma za ugani na miundombinu ya masoko imejengwa. Kiashiria kingine ni kule kuongezeka kwa matumizi ya zana za kisasa, kwa mfano, uingizaji wa matrekta makubwa na madogo umeongezeka na kuongeza idadi kutoka 7,491 mwaka 2005/2006 hadi 16,412 mwaka 2013/2014. Hali hiyo imepunguza matumizi ya jembe la mkono kutoka asilimia 70 hadi asilimia 62, matumizi ya wanyamakazi nayo yameongezeka kutoka asilimia 20 hadi 24, na matumizi ya trekta kuongezeka kutoka asilimia 10 hadi asilimia 14. Aidha, eneo linalotumika kwa kilimo cha umwagiliaji limeongezeka kutoka hekta 264,388 mwaka 2005 hadi hekta 461,326 mwaka 2015.
Matokeo ya juhudi zetu hizo ni kuongezeka kwa uzalishaji wa mazao ya chakula na biashara. Uzalishaji wa chakula umeongezeka kutoka tani 9.66 mwaka 2005 hadi tani 16.01 Mwaka 2015 na kutufanya tuweze kujitosheleza kwa chakula kwa asilimia 125 ikilinganishwa na asilimia 95 mwaka 2015. Leo hii hatuna tena tishio la usalama wa chakula kama ilivyokuwa miaka 10 iliyopita. Hivi sasa kwa wakulima wa mpunga na mahindi tatizo siyo uzalishaji tena, bali ni masoko na uhifadhi wa mazao. Uzalishaji wa mazao ya biashara nao umeongezeka kutoka tani 427,738 hadi tani 569,054 na hivyo kuchangia katika kuongezeka mapato ya fedha za kigeni.[A1]
Kwa upande wa mifugo, dhamira ya Serikali imekua ni kuleta mageuzi katika Sekta hii, kupitia ASDP na baadae tukatayarisha programu maalum ya kuendeleza sekta ya mifugo. Katika Programu na Mpango huo tumeainisha changamoto zinazosababisha maendeleo duni katika sekta ya mifugo na kutengenezewa Mpango wa utekelezaji kwa upande wa mifugo ujulikanao kama Mpango wa Modenaizesheni ya Mifugo niliouzindua hivi karibuni. Mafanikio yaliyopatikana katika kipindi cha miaka 10 ni kuongezeka kwa idadi na ubora wa mifugo: ng’ombe, mbuzi, kondoo, kuku na nguruwe. Haya ni matunda ya kuendelea kuimarika kwa huduma za ugani na nyinginezo kwa mfano, ujenzi wa malambo mapya 1,008, majosho 2,364 na maabara 104 za mifugo. Visima virefu 101 vimechimbwa na malambo 370 na majosho 499 yamekarabatiwa katika kipindi hicho pia.
Kutokana na ukarabati wa majosho ya zamani na ujenzi wa majosho mapya, idadi ya majosho imeongezeka kutoka 2,177 mwaka 2005/2006 hadi 3,637 mwaka 2014/2015. Maofisa Ugani wa mifugo wameongezeka, kutoka 2,270 mwaka 2004/2005 hadi 6,041 mwaka 2014. Kuhusu uhamilishaji, vituo vimeongezeka kutoka kituo 1 mwaka 2005 hadi vituo 8 mwaka 2015 na kuwezesha ng’ombe 955,360 kuhamilishwa.
Ndugu Wananchi,
Mazingira mazuri ya uwekezaji yamewezesha sekta binafsi kuwekeza katika uanzishaji wa viwanda vya kusindika nyama, maziwa na vyakula vya mifugo. Kwa ajili hiyo, viwanda vya kusindika maziwa vimeongezeka kutoka 22 mwaka 2005/2006 hadi 74 mwaka 2014/2015. Viwanda vya kuzalisha chakula cha mifugo vimeongezeka kutoka viwanda 6 mwaka 2005 hadi 80 mwaka 2014/2015 vikiwa na uwezo wa kusindika tani milioni 1.4 za chakula cha mifugo kwa mwaka. Uzalishaji wa malisho ya mifugo nao umefikia marobota 957,860 ikilinganishwa na marobota 178,100 mwaka 2005. Aidha viwanda na machinjio ya kisasa 9 yamejengwa katika kipindi hiki. Usindikaji wa ngozi pia umeongezeka kutoka vipande 790,000 mwaka 2005 hadi vipande milioni 3.78 mwaka 2014.
Kama nilivyosema tarehe 20 Julai, 2015 nilizindua Mpango wa Modenaizesheni ya Mifugo wa Mwaka 2015 hadi 2021. Chini ya mpango huu, sasa tumedhamiria na kuweka mkakati wa kuufanya ufugaji kuwa wa kisasa. Mimi naamini kuwa safari ya kutoka kwenye uchungaji kuelekea kwenye ufugaji wa kisasa sasa imepata dira ya uhakika.
Uvuvi
Ndugu wananch;
Katika kupindi hiki pia tumetoa msukumo mkubwa katika kuendeleza uvuvi nchini. Tumefanya mambo kadhaa: Kwanza, niliunda Wizara mpya ya Mifugo na Uvuvi. Pili, tulifuta kodi ya zana za uvuvi ili kuwawezesha wavuvi kupata zana bora na za kisasa kwa bei nafuu zaidi. Tatu, tumeimarisha vyuo vya uvuvi na hivi sasa vina uwezo wa kudahili wanafunzi 1,215 ikilinganishwa na wanafunzi 127 mwaka 2005/2006. Hii imetuwezesha kuongeza maafisa ugani wa uvuvi kutoka 103 mwaka 2005 hadi 540 mwaka 2014. Nne, tumeongeza sana juhudi za kupambana na uvuvi haramu ili kutunza mazingira, mazalia ya samaki na kuzuia kuvuliwa au kuuawa kwa samaki wadogo.
Hali kadhalika, tumeimarisha Maabara ya Taifa ya Samaki pale Nyegezi ili kuwa na vifaa vya kisasa na wataalamu ili twende na wakati. Vilevile, tumeongeza msukumo wa kuhimiza ufugaji wa samaki na kuwezesha mashamba ya samaki kuongezeka kutoka 13,011 mwaka 2005/2006 hadi 20,325 mwaka 2013/2014.
Jambo moja la kujipongeza ni kuwa mapato ya sekta ya uvuvi yameongezeka kutoka shilingi bilioni 351.6 mwaka 2005/2006 hadi shilingi trilioni 1.8 mwaka 2013/2014. Mapato hayo yamechangia kuinua hali ya maisha ya watu wanaojihusisha na uvuvi. Bado tuna kazi kubwa ya kufanya katika sekta hii ili kuongeza tija na mapato ya wavuvi na Taifa kwa ujumla.
Lakini kazi kubwa zaidi ni ile ya kupambana na uvuvi haramu wa kutumia baruti na nyavu zisizofaa kama vile makokoro na nyingine. Pia tusiharibu mazalia ya samaki, kwa ukanda wa Pwani tuhifadhi mikoko na matumbawe. Lazima tufanye hivyo vinginevyo baada ya muda si mrefu shughuli ya uvuvi itatoweka. Tayari wenzetu wa Ziwa Victoria wameanza kuonja joto la jiwe. Samaki wamepungua sana na watu wengi wamepoteza ajira. Hivyo tunapohimiza kuacha uvuvi haramu si jambo la masihara hata kidogo.
Changamoto katika Sekta ya Kilimo
Ndugu wananchi;
Mafanikio katika kutekeleza miradi na mipango ya kukuza kilimo yamekuja na changamoto zake mpya. Wakati naingia madarakani kulikuwa na uhaba mkubwa wa chakula na ukame. Serikali ililazimika kutoa chakula cha msaada kwa zaidi ya watu milioni 3.7. Leo tunazalisha ziada ya tani milioni 5 ambayo imetuletea changamoto mpya ya uhaba wa maghala ya kuhifadhi chakula pamoja na kukosekana kwa masoko ya uhakika na bei nzuri kwa mazao ya wakulima. Jitihada zinaendelea kupitia Mpango wa Matokeo Makubwa Sasa za kujenga maghala ya kisasa nchi nzima ili kuongeza uwezo wa kuhifadhi nafaka kutoka tani 250,000 hadi tani 400,000.
Aidha, mpango wa kuwaunganisha wakulima na masoko kupitia mfumo wa Soko la Bidhaa (Commodity Exchange) umefikia mahali pazuri. Baraza la Mawaziri limekwisharidhia, na muswada wa sheria ya uanzishaji wa soko hilo litakalokuwa chini ya Mamlaka ya Masoko ya Mitaji na Dhamana ulishapitishwa na Bunge, nami nimesha idhinisha kuwa sheria. Kilichobaki sasa ni uanzishwaji wa soko hilo.
Jambo lingine ambalo limekuwa ni changamoto kwa wakulima ni upatikanaji wa fedha na mitaji kwa ajili ya kuendeleza shughuli za kilimo, kuongeza tija na uzalishaji. Serikali imefanya jitihada ya kuhimiza uanzishaji wa asasi ndogo za fedha (Micro-finance) zipo za Serikali na zisizokuwa za Serikali na tulihimiza uimarishaji wa Vyama vya Ushirika wa Nyama vya Akiba na Mikopo (SACCOS) ambavyo vimesaidia sana wakulima kupata mikopo. Hata hivyo, asasi hizi hazijaweza kuwa za msaada mkubwa kwa sababu ya uwezo mdogo na raslimali. Pia SACCOS nazo kwa kutegemea michango ya wakulima maskini kumezinyima uwezo wa kumsaidia kwa dhati mkulima aondokane na umaskini. Bahati mbaya mabenki ya biashara yamekuwa yakisita kukopesha na kuwekeza kwenye kilimo kutokana na kuhofia kupata hasara. Changamoto ya wakulima kukosa vyazo vinavyotosheleza mahitaji ya fedha na mitaji imechangia sana ukuaji mdogo wa sekta ya kilimo.
Benki ya Maendeleo ya Kilimo
Ndugu Wananchi;
Nafurahi kuwa leo hii nitafungua Benki ya Maendeleo ya Kilimo ambayo nilizindua ofisi zake jana jijini Dar es Salaam. Kufunguliwa kwa Benki hii ni mwanzo mpya katika safari yetu ya kuelekea kweye kilimo cha kisasa. Maana, zile hatua tulizochukua za kuongeza matumizi ya zana za kisasa, mbegu na mbolea bora na utafiti pekee haviwezi kutuletea mapinduzi ya kilimo bila ya uwekezaji. Nasema hivi kwa kuwa uzoefu wa nchi zilizofanikiwa katika mapinduzi ya kilimo kama wenzetu wa India, Vietnam, China na Brazil, mapinduzi yao yalichochewa sana na uwepo wa benki mahsusi za kilimo za kuwezesha uwekezaji kwenye sekta hii.
Benki yetu hii tumeianza na mtaji wa shilingi bilioni 60 na lengo letu ni kufikisha mtaji wa bilioni 800 katika kipindi cha miaka 8 kwa uwekezaji wa shilingi bilioni 100 kila mwaka. Tofauti na benki za biashara, benki hii shughuli yake ni mahsusi yaani kilimo. Lengo lake kuwakopesha wakulima na vikundi vya wakulima kwa ajili ya kuendeleza shughuli zao za kilimo kwa masharti nafuu na rafiki yanayozingatia uhalisia na mazingira ya shughuli za kilimo. Aidha, Benki hii itafadhili miradi ya kilimo na ile inayochochea kilimo katika mnyororo wa thamani wa kilimo.
Kwa kuanzia Benki hii haitapokea amana na haitakuwa na matawi. Itatumia mabenki ya biashara yaliyopo kuwafikia wakulima kwa masharti mahsusi ya Benki ya Maendeleo ya Kilimo. Vilevile, itaziwezesha Benki za biashara kukopesha wakulima kwa kuwekeza katika mabenki hayo. Katika muda wa kati itafungua ofisi sita za kanda kwa lengo la kusogeza huduma kwa wananchi. Aidha, miradi katika mnyororo wa thamani wa uzalishaji katika maeneo 10 ya sekta ya kilimo ndio yatakayokuwa ya kipaumbele. Maeneo hayo ni 10 ni Mahindi, Mchele, Miwa, Mbegu za mafuta, Kilimo cha Matunda, Maua na mbogamboga, Ng’ombe wa maziwa na nyama, ufugaji wa Kuku wa Kienyeji, Ufugaji wa Samaki na Ufugaji wa Nyuki. Huo ni mwanzo mzuri.
Ahadi ya serikali ni kuhakikisha kuwa Benki hii inapata mtaji wa kutosha na kuweza kuwafikia wakulima wengi. Tumeipatia Bodi ya Wakurugenzi ya watu mahiri na waliobobea wakiongozwa na Mwenyekiti Mama Rosemary Kujirwila, ambaye awali alikuwa Kamishna wa Umoja wa Afrika wa Masuala ya Maendeleo vijijini. Sina mashaka hata kidogo kuwa kilimo chetu sasa tumekiwekea muelekeo mzuri wa Mapinduzi ya Kijani. Tunataka tuanze safari ya kufanya kilimo kuwa biashara na sio cha kujikimu. Lazima tukione kilimo kuwa ni kazi na ni shughuli ya kibiashara na kamwe siyo shughuli ya watu waliokosa kazi na fursa ya kwenda mjini.
Ndugu wananchi;
Wito wangu kwa wadau wa sekta ya kilimo ni kuelekeza nguvu zetu katika kutekeleza mkakati wa Mpango wa Matokeo Makubwa Sasa katika sekta ya kilimo. Kila mdau na atekeleze ule wajibu unaoangukia katika mamlaka yake ili kuondoa changamoto na vikwazo vilivyoainishwa kwamba vinaathiri ukuaji wa sekta ya kilimo. Nasema hivyo kwa kutambua kuwa, kuwakopesha wakulima ni jambo moja, kuwawezesha kupata faida na kuweza kufanya marejesho ya mkopo ni jambo jingine. Mikopo na uwekezaji utakuwa na maana tu ikiwa kutakuwa na mazingira wezeshi ya kumfanya mkulima kuwekeza, kuvuna na kuuza kwa uhakika.
Kuagana na Wananchi wa Mkoa wa Lindi
Ndugu Wananchi,
Napenda kutumia pia fursa hii kuagana na wananchi na Mkoa wa Lindi.
Nawashukuru kwa kunichagua kwa kura nyingi mwaka 2005 na mwaka 2010. Kama nilivyoahidi katika Ilani zote mbii za CCM tumetimiza kwa asilimia 90 na kupata mafanikio makubwa. Yapo madeni machache ambayo tutayamalizia. Mheshimiwa Mkuu wa Mkoa ameeleza kwa kina tuliyoyafanya na mafanikko tuliyoyapata. Kwa uchache, tumemaliza ujenzi wa barabara ya Dar-Kibiti-Lindi yenye urefu wa kilometa 508 kwa kiwango cha lami. Jana nimezindua kipande kilichokuwa kimebakia cha Ndundu-Somanga cha kilometa 60. Sasa safari ya Dar es Salaam – Lindi imekuwa fupi, na mabasi ya Luxury sasa yanakuja Lindi. Tumejenga kilometa 5 za barabara za lami katika mji wa Nachingwea, kilomita 3 Liwale, kilomita 2 Ruangwa na kilomita 11.7 Lindi Manispaa.
Hali ya uchumi wa Lindi kwa ujumla imekua na kuimarika. Pato la mkazi limeongezeka kutoka shilingi 385,378 mwaka 2005 hadi shilingi 1,127,104 mwaka 2013. Uzalishaji wa mazao ya chakula umeongezeka kutoka tani 112,848 mwaka 2005 hadi 192,893 mwaka 2014. Mazao ya biashara kutoka tani 17,621 hadi tani 45,521 mwaka huu. Upatikanaji wa pembejeo kutoka tani 2,341 hadi tani 2,816. Haya ni mafanikio ya kutia moyo sana.
Kwa upande wa huduma za jamii nako kuna maendeleo makubwa. Umeme sasa unapatikana katika vijiji 231 (asilimia 45) mwaka huu ikilinganishwa na vijiji 52 mwaka 2005. Kubwa zaidi ni upande wa elimu. Shule za Sekondari zimeongezeka kutoka 43 hadi 115 ambapo saa kila Kata ina shule ya sekondari. Maabara zimeongezeka kutoka 20 mwaka 2005 hadi 134 mwaka huu. Tumeongeza hosteli kutoka 19 mwaka 2005 hadi 81 mwaka 2015. Hizi ni habari njema kwa watoto wa kike, maana sasa wasichana wanapata nafasi ya uhakika ya kupata masomo kwa kuwa wako hosteli. Aidha, katika kipindi hiki tumefanikiwa pia kujenga hapa Lindi Chuo chaUfundi Stadi (VETA).
Huduma za Afya zimeboreka, vifo vya akinamama wajawazito na watoto vimepungua, maambukizi ya malaria imepungua kutoka asilimia 35.5 mwaka 2008 hadi asilimia 26 mwaka 2012. Tumekamilisha pia mradi wa maji wa Masasi unaohudumia Mji wa Masasi na Nachingwea na Vijiji vinavopitiwa na bomba hilo. Aidha, tutakapo kamilisha mradi wa maji wa Ng’apa tatizo la maji katika Mji wa Lindi litapungua kwa kiasi kikubwa. Tumepata pia mafanikio kwenye maeneo mengi kama yalivyoelezwa na Mkuu wa Mkoa. Itoshe tu kusema nawashukuru sana na nitawakumbuka daima kwa upendo na ukarimu wenu kwangu na ushirikiano kwa Serikali yangu. Nawaaga nikiwa na furaha kuwa tunaagana vizuri. Mie hapa mwenyeji, mtaniona mara kwa mara nikija kukaa hapa baada ya kustaafu.
Hitimisho
Ndugu Wananchi,
Kwa kumalizia, haya ni maadhimisho ya Nane Nane ya mwisho ninayoshiriki nikiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kabla sijamaliza Awamu yangu ya uongozi. Napenda kuwashukuru sana wakulima, wafugaji na wavuvi wa Tanzania kwa kuunga mkono juhudi za Serikali ninayoiongoza katika kukuza kilimo. Ukweli ni kuwa mliolima, mliofuga na mliovua na kutuhakikishia usalama wa chakula ni ninyi. Sisi tulitunga tu sera, sheria na kuwawekea mazingira wezeshi. Nawashukuru sana kwa kujitoa kwenu na ninafurahi kuwa kwa pamoja katika kipindi hiki tumeweza kupiga hatua kubwa. Leo hii kilimo chetu si kama kilivyokuwa miaka 10 iliyopita kama takwimu zinavyoonyesha. Leo kilimo kimeanza kuvutia sekta binafsi na sasa kinavutia vijana wasomi.
Ninakwenda kupumzika nikiwa na amani kuwa ninawaacha pazuri zaidi kuliko nilipowakuta. Nafarijika kuwa hata yale ambayo sikukamilisha na yale mapya yaliyoibuka, nayo tumeyawekea mikakati na muelekeo wenye uhakika wa kutatulika. Nawaomba mumpe Rais ajaye upendo na ushirikiano zaidi ya ule mlionipatia mimi. Sasa natamka kuwa, “BENKI YA MAENDELEO YA KILIMO TANZANIA “TADB” IMEZINDULIWA RASMI LEO TAREHE 8 MWEZI WA 8 MWAKA 2015” na MAADHIMISHO YA 22 YA SHEREHE ZA SIKUKUU YA WAKULIMA NANE NANE KWA MWAKA 2015 YAMEFUNGWA RASMI.
Asanteni kwa Kunisikiliza
[A1]Ni kwa mujibu wa economic survey, angalizo: takwimu zimewekwa kwenye dola milioni na sio dola bilioni
- Aug 06, 2015
HOTUBA YA MHESHIMIWA JAKAYA MRISHO KIKWETE, RAIS WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA KATIKA HAFLA YA KUAGANA NA MAHAKAMA YA TANZANIA TAREHE 6 AGOSTI, 2015
Soma zaidiHotuba
Mheshimiwa Jaji Mkuu,
Mheshimiwa Waziri wa Katiba na Sheria,
Mheshimiwa Mwanasheria Mkuu wa Serikali,
Mheshimiwa Jaji Kiongozi,
Waheshimiwa Majaji na Mahakimu,
Ndugu Viongozi na Watumishi wa Mahakama,
Wageni Waalikwa,
Mabibi na Mabwana,
Nilipokutana nanyi katika kuadhimisha Siku ya Sheria Nchini tarehe 04 Februari, 2015 nilitumia fursa ile kuwaaga. Hata hivyo mkasema haitoshi, mmetafuta wasaa wa ninyi kuniaga. Nakushukuru Mheshimiwa Mohamed Chande Othuman, Jaji Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Majaji wa Mahakama ya Rufani, Majaji wa Mahakama Kuu, Wasajili, Mahakimu Wakazi, Mahakimu Watendaji na Wafanyakazi wote wa Mahakama kwa heshima hii kubwa mliyonipa. Nikiri kuwa ni jambo ambalo sikulitegemea, lakini nimeguswa sana na upendo wenu huu mkubwa mlionionyesha. Nimefarijika sana. Ni kielelezo kuwa tumeishi vizuri, tumeheshimiana na kushirikiana kwa maslahi mapana ya wananchi wa Taifa letu. Huu ni ushirikiano ambao hauna budi kuuendelezwa na kudumishwa katika Awamu ya Tano na zote zijazo.
Mheshimiwa Jaji Mkuu,
Katika hotuba yako umeongelea mafanikio ya Mahakama yaliyopatikana katika kipindi hiki cha Awamu ya Nne. Umenipongeza mimi kwa mafanikio hayo. Mimi naamini mafanikio haya yametokana na juhudi zetu za pamoja, maana bila ya mchango wenu na mipango yenu, sisi katika Serikali tusingeweza peke yetu kuyafanikisha. Kutokana na kujipanga kwenu vizuri, kazi yetu kwa upande wa Serikali imekuwa rahisi sana.
Umuhimu na Nafasi ya Mahakama
Mheshimiwa Jaji Mkuu,
Nafasi na umuhimu wa Mahakama katika jamii na Taifa ni jambo lisilohitaji mjadala. Tunu za amani, utulivu na umoja ambazo nchi yetu inasifiwa duniani zina mchango muhimu wa Mahakama. Ni ukweli usiopingika kuwa kama watu wanadhulumiwa haki zao za msingi na hawana matumaini ya kuzipata katika mifumo ya kawaida au rasmi ya utoaji haki kuna hatari ya amani kuvurugika. Kishawishi cha watu kuchukua Sheria mikononi mwao hujitokeza. Kwa maneno mengine huchochea uvunjifu wa Sheria na hali ikikithiri amani huweza kuathirika. Ipo mifano ya hapa nchini na kwingineko duniani.
Kwa kutambua ukweli huo suala la utoaji wa haki ni jambo ambalo nililipa kipaumbele cha juu. Kwa ajili hiyo mwanzoni kabisa nilipoanza kazi ya uongozi wa nchi yetu nilitembelea Mhimili wa Mahakama. Nilikutana na kuzungumza na Jaji Mkuu Banarbas Samata na Majaji wa Rufaa na Mahakama Kuu. Ziara yangu ile ilinipatia ufahamu mkubwa kuhusu hali ilivyokua katika Mhimili huu wa dola wenye dhamana na jukumu muhimu la utoaji wa haki nchini. Niliweza kujua mafaniko na changamoto za Mahakama. Nilitambua upungufu mkubwa wa nguvu kazi, uhaba wa vitendea kazi, bajeti finyu na masuala ya maslahi ya Majaji, Mahakimu na Watumishi wengine wa Mahakama. Niliahidi kuzifanyia kazi kwani changamoto hizo zinapunguza ufanisi wa kazi, mashauri kuchelewa kusikilizwa, na kumalizwa na kujitokeza kwa tuhuma za rushwa. Napata faraja moyoni mwangu kuwa leo tunapoagana tumepiga hatua kubwa katika kuzipatia ufumbuzi changamoto hizo. Ni ukweli usiopingika kuwa Mahakama ilivyo leo sivyo ilivyokuwa mwaka 2005. Hali ni bora zaidi sasa.
Rasilimali watu
Mheshimiwa Jaji Mkuu,
Kwa upande wa upungufu wa nguvu kazi, kama ulivyosema kwenye hotuba yako, wakati tunaingia madarakani, Mahakama yetu ilikuwa na Majaji wachache sana ukilinganisha na mahitaji. Kwa upande wa Mahakama ya Rufani, tulikuwa na majaji tisa (9) tu, huku tukiwa na majaji 37 wa Mahakama Kuu. Idadi hii ilikuwa ni ndogo sana ikilinganishwa na wingi wa mashauri yaliyokuwa yamerundikana mahakamani nchi nzima. Lakini hadi leo tunapoagana leo idadi ya Majaji wa Rufani imeongezeka kutoka 9 hadi 16 wakati ile ya Majaji wa Mahakama Kuu imeongezeka kutoka 35 hadi 94.
Jitihada zetu hazikuishia hapo. Tuliajiri pia Mahakimu wa kada mbalimbali. Hadi kufikia mwaka huu, idadi ya Mahakimu Wakazi pekee imefikia 677 ikilinganishwa na Mahakimu Wakazi 151 waliokuwepo mwaka 2005. Mbali na Mahakimu Wakazi, pia wameajiriwa Mahakimu wengine wa kada mbalimbali kulingana na mahitaji. Vile vile, watumishi wa kada mbalimbali wameajiriwa na kuongeza idadi ya watumishi wa ngazi na kada mbalimbali kutoka 4,972 mwaka 2005 hadi kufikia 6,052 mwaka 2015.
Ni katika kipindi hiki pia zimeanzishwa kada nyingine muhimu, yaani watendaji wa Mahakama pamoja na Wasaidizi wa Sheria wa Majaji chini ya Sheria ya Uendeshaji wa Mahakama. Hii imewaondolea Majaji na Mahakimu majukumu ya kiutawala na fedha na kuwaacha washughulike na jukumu lao la msingi la utoaji wa haki. Sasa tunaye Mtendaji Mkuu wa Mahakama, Mtendaji wa Mahakama Kuu, pamoja na watendaji wengine wa ngazi mbalimbali.
Kwa hatua hizo tulizochukua, naweza kusema kwa kujiamini kuwa tumeongeza sana uwezo wa rasilimali watu. Pia tumewapunguzia Majaji na Mahakimu mzigo wa kesi kutokana na sasa kuwa wengi, lakini muhimu zaidi imetusaidia kuharakisha utoaji haki kwa wananchi.
Bajeti ya Mahakama
Mheshimiwa Jaji Mkuu,
Tulilitazama suala la bajeti ya Mahakama na kuamua kufanya mambo mawili ili kuiongezea Mahakama uwezo wa kutimiza majukumu yake. Kwanza, kwamba kila mwaka tuliongeza fedha kwa utaratibu wa kawaida. Pili, tukafanya uamuzi wa kimapinduzi wa kutekeleza matakwa ya Katiba kwa kuanzisha Mfuko wa Mahakama kwa kutunga Sheria ya Uendeshaji Mahakama Namba 4 ya Mwaka 2011. Mfumo huu siyo tu unaongeza bajeti bali pia unaipa Mahakama uhuru wa kufanya mambo yake. Aidha, inaondoa ile dhana ya kuuona Mhimili wa Mahakama kama Idara ya Serikali.
Kutokana na hatua hizi bajeti ya Mahakama iliongezeka kutoka shilingi bilioni 36.6 mwaka 2005 hadi shilingi bilioni 57.8 mwaka 2012/2013 kwa mujibu wa nyongeza za kawaida. Hili ni ongezeko la zaidi ya asilimia 66 ndani ya kipindi kifupi cha tangu mwaka 2012/2013. Mwaka huu wa fedha bajeti hiyo imefikia shilingi bilioni 88.9 kufuatia ongezeko kubwa baada ya kuanzishwa kwa Mfumo wa Mahakama. Kwa jumla hii ni ongezeko la zaidi ya asilimia 136 ikilinganishwa na bajeti ya mwaka 2005/2006.
Pamoja na nyongeza hii inayoonekana kuwa ni kubwa sana lakini natambua kuwa bado ni kidogo kuliko mahitaji halisi ya Mahakama. Mtakubaliana nami kuwa imeleta ahueni kubwa na kuiwezesha Mahakama kuboresha utekekelezaji wa majukumu yake. Halikadhalika Mahakama sasa imeanza kutekeleza miradi ya maendeleo kama ujenzi wa ofisi za Mahakama. Nina imani Rais ajaye na Serikali ijayo itahakikisha kuwa fedha zinaongezeka zaidi na Hazina inatoa fedha zote zilizopangwa katika bajeti. Tena zinatolewa kwa wakati.
Uboreshaji wa Maslahi ya Majaji, Mahakimu
na Watumishi wa Mahakama
Mheshimiwa Jaji Mkuu,
Katika kipindi hiki tumechukua hatua za maksudi za kuboresha maslahi ya Majaji. Mwaka 2007 tukatunga Sheria ya Majaji (Judges Remuneration Act) yaani Sheria Namba 4 ya mwaka 2007. Chini ya Sheria hii, maslahi ya majaji yameboreshwa na tunaamini hiki ni kichocheo cha waheshimiwa majaji kufanya kazi kwa bidii zaidi, kwa weledi zaidi na kwa ufanisi zaidi. Lakini pia chini ya Sheria hii mafao ya majaji baada ya kustaafu yamewekwa vizuri zaidi. Nafikiri hili ni muhimu sana kwamba Majaji wasifanye kazi wakihofu juu ya hatma yao baada ya kazi kutokana na unyeti wa kazi yao ambayo kwa kweli inawazuia kuwa na vyanzo vingine vya mapato.
Hatukuishia kwa Majaji tu, mwaka 2007 mishahara ya Mahakimu iliboreshwa. Mipango iko mbioni kuhakikisha pia kwamba watumishi wengine wa kada mbalimbali za Mahakama nao maslahi yao yanaboreshwa. Haya yote tumeyafanya ili kuwawezesha Majaji na Mahakimu kutimiza wajibu wao pasipo kuwiwa na mtihani wa tamaa.
Miundombinu na vitendea kazi
Mheshimiwa Jaji Mkuu,
Kwa muda mrefu suala la miundombinu hususan majengo ya Mahakama imekuwa ni tatizo. Kuna upungufu mkubwa na kusababisha watu kusafiri masafa marefu kufuata huduma hususan Mahakama za Mwanzo na Mahakama Kuu. Kwa upande wa Mahakama za Mwanzo nyingi zina majengo duni na yasiyofaa. Katika baadhi ya maeneo nimewahi kuambiwa kwamba Majaji Wafawidhi walitoa maelekezo ya kufunga Mahakama hizo kutokana na kuwa katika hali mbaya sana na hata kuhatarisha maisha ya watumishi wa Mahakama pamoja na wateja wa Mahakama. Kwa bahati mbaya Mahakama za namna hiyo zilikuwepo hata hapa Dar es Salaam ambako tunasema ni uso wa nchi.
Hili nalo tukaliwekea nia na mkakati wa kuondokana nalo. Kati ya mwaka 2006 hadi sasa tumeweza kujenga Mahakama Kuu 2 za kisasa kabisa katika mikoa ya Kagera na Shinyanga na Mahakama Kuu Divisheni ya Kazi 1. Vilevile zimejengwa Mahakama mpya ya Mkoa 1 (Babati), za Wilaya 2 (Mafia na Kisarawe), na Mahakama za Mwanzo 12. Mahakama za Mwanzo tulizojenga zimesaidia kurejesha imani ya Watanzania kwa Mahakama.
Mbali na majengo ya Mahakama, tumeweza kujenga nyumba za kisasa kwa ajili ya Mahakimu. Nafahamu suala la kujenga nyumba za kuishi ni endelevu na katika eneo hili bado tuna deni kubwa. Hili pia naamini Mheshimiwa Jaji Mkuu pamoja na Mtendaji Mkuu mtaendelea kulifanyia kazi kwa kushirikiana na Serikali.
Matumizi ya TEHAMA
Mheshimiwa Jaji Mkuu,
Ulimwengu wa sasa ni ulimwengu wa Tehama. Nawapongeza kuwa katika hili Mahakama nanyi hamkubaki nyuma. Inatia moyo kuona kwamba taratibu mnabadili mfumo wa uandishi na utunzaji wa kumbukumbu za mwenendo wa kesi na nyinginezo na kutumia mfumo wa Tehama. Inafurahisha kusikia kwamba kwa sasa takwimu za mashauri ya nchi nzima zinapatikana kwenye mtandao. Lakini pia tumeambiwa kwamba sasa Mheshimiwa Jaji Mkuu anapata taarifa za mashauri yote yaliyofunguliwa, yaliyoisha na yaliyobaki kwa mwezi kwa kupitia njia ya mtandao. Hali kadhalika, anaweza kufahamu kila Jaji na Hakimu amesikiliza mashauri mangapi kwa mwezi na kwa mwaka kwa njia ya mtandao.
Hili si jambo dogo kwa Mahakama zetu. Lazima tukiri kuwa tumepiga hatua kubwa ya kujivunia. Uhifadhi wa zamani wa kumbukumbu za Mahakama ni jambo ambalo kwa muda mrefu limesababisha usumbufu na malalamiko kwa wananchi. Aidha, eneo hili linatajwa kuwa kichaka cha vitendo vya rushwa. Nafurahi kuwa tanaanza kuondokana na yale maelezo ya “jalada halionekani”. Mimi naamini, tunaweza kufanya zaidi kwa kutumia pia mifumo ya simu katika malipo Mahakamani, na kuwezesha wananchi kuuliza na kujua tarehe za mashauri yao bila kuwalazimu kuja kufuatilia taarifa hizo Mahakamani. Maana, ile ‘nenda-rudi’ nayo inaleta usumbufu usio wa lazima kwa wananchi.
Uboreshaji wa Utendaji Katika Mahakama
Mheshimiwa Jaji Mkuu,
Katika hotuba yako Mheshimiwa Jaji Mkuu, umeonesha jinsi ambavyo idadi ya mashauri yanayoisha imekuwa ikiongezeka mwaka hadi mwaka toka mwaka 2006 hadi sasa. Nimefurahishwa zaidi na mkakati uliowekwa na Mahakama wa kila Jaji na Hakimu kumaliza idadi maalum ya mashauri kwa mwaka. Pia, nawapongeza kwa kuamua kuwa muda wa shauri kukaa mahakamani usizidi miaka miwili. Mkakati wenu wa kuyamaliza mashauri yaliyokaa Mahakamani kwa muda mrefu unaelekea kuzaa matunda. Taarifa kwamba mmeyapunguza mashauri hayo kwa zaidi ya asilimia 50 yaani kutoka mashauri 6,887 mwaka 2012 hadi mashauri 3,632 mwaka 2014 ni za kutia moyo. Kwa hili mnastahili pongezi zetu nyingi. Tunawaomba muendelee hivyo kwani kwa kujiwekea malengo, inawapa urahisi wa kujipima ninyi wenyewe, na wananchi kuwapima pia. Huo ndio uwajibikaji.
Wajibu wa Mahakama katika Uchaguzi
Mheshimiwa Jaji Mkuu,
Nchi yetu sasa inaelekea katika Uchaguzi Mkuu kuchagua Rais, Wabunge na Madiwani. Tunategemea kama ilivyo ada yetu utakuwa uchaguzi huru, wa haki na wa amani. Lakini ‘penye wengi pana mengi’. Kama ilivyokuwa katika chaguzi zilizopita, wakati mwingine yanajitokeza mashauri mbalimbali mara uchaguzi unapoisha. Siku za nyuma mashauri haya yalikuwa yanachukua muda mrefu na baadhi kudumu toka uchaguzi mmoja hadi mwingine. Hali hii ilibadilika uchaguzi uliopita. Mashauri ya uchaguzi yalipewa kipaumbele yakaweza kuisha mapema na hivyo wananchi kujua hatima ya waliowachagua. Ni ombi letu kwamba utaratibu huu uendelee ili mashauri yote, kama yatakuwepo, yaishe ndani ya muda mfupi iwezekanavyo na haki iweze kupatikana.
Mwisho
Mheshimiwa Jaji Mkuu,
Napenda kuhitimisha kwa kukushukuru kwa mara nyingine kwa uamuzi wenu wa kuandaa hafla ya kuagana. Nawashukuru sana kwa ushirikano mlionipatia mimi na wenzangu Serikalini na zaidi kwa mafaniko ambayo sote tumeyapata. Kupitia kwako, nawashukuru waheshimiwa Majaji wa Mahakama ya Rufani na Mahakama Kuu, Mtendaji Mkuu, Msajili Mkuu, Mahakimu ngazi malimbali, watendaji na watumishi wa Mahakama. Daima nitakumbuka wema na upendo wenu mkubwa mlionionyesha. Lakini kubwa zaidi nitawakumbuka kwa uchapa kazi wenu na moyo wenu wa uzalendo.
Safari bado ni ndefu, muhimu ni kuwa tumeshaianza, na hivyo kuifupisha. Awamu itakayokuja wataanzia pafupi zaidi kuliko pale tulipoanzia sisi wa Awamu ya Nne. Ninaondoka nikiwa na furaha na amani moyoni kuwa nauacha Mhimili wa Mahakama mahali pazuri zaidi ya nilipowakuta mwaka 2005. Hata hivyo bado kuna kazi kubwa ya kufanya mbele yetu mpaka tufike pale tunapopataka sote tufike. Tukiendelea na kasi hii sina shaka kabisa kwamba tutafika tunapopataka katika miaka mitano ijayo.
Nawatakia kila la kheli na mafanikio makubwa siku za usoni. Kwaherini.
Mungu ibariki Tanzania
- Aug 03, 2015
HOTUBA YA MHESHIMIWA DKT. JAKAYA MRISHO KIKWETE, RAIS WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA KWENYE UFUNGUZI WA MAADHIMISHO YA WIKI YA NENDA KWA USALAMA BARABARANI...
Soma zaidiHotuba
Mwenyekiti wa Baraza la Taifa la Usalama Barabarani (T) na Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mh. Pereira Silima,
Mhe. Ummy Mwalimu, Naibu Waziri Katiba na Sheria,
Mhe. Magalula Said Magalula, Mkuu wa Mkoa wa Tanga,
Wakuu wa Wilaya ya Tanga,
Kamishna Chadiel Chagonja, anayemwakilisha Inspekta Jenerali wa Polisi,
Waheshimiwa Wabunge,
Mhe. Henry Shekiffu Mwenyekiti wa CCM Mkoa,
Ndugu Mohammed Mpinga Katibu Mtendaji wa Baraza la Taifa Usalama Barabarani (T) na Kamanda wa Kikosi cha Usalama Barabarani (T)
Mwenyekiti wa Kamati ya Usalama Barabarani (M) Tanga,
Wajumbe wa Baraza la Taifa la Usalama Barabarani (T),
Wageni waalikwa,
Wanahabari,
Mabibi na Mabwana,
Asalaam Aleikum, Amani ya Mungu iwe juu yenu.
Ndugu Wananchi,
Nakushukuru sana Mheshimiwa Naibu Waziri, Pereira Silima na viongozi wa Baraza la Taifa la Usalama Barabarani kwa kunialika kwenye Maadhimisho ya Wiki ya Nenda kwa Usalama Barabarani ambayo mwaka huu yanafanyika kitaifa hapa Mkoani Tanga. Pia nakushukuru Mheshimiwa Mkuu wa Mkoa, na kupitia kwako nawashukuru wananchi wa Mkoa wa Tanga kwa mapokezi mazuri na ukarimu wenu. Lakini sishangai kwani hii ndiyo sifa ya watu wa Tanga. Nawashukuru pia kwa kujitokeza kwenu kwa wingi katika uzinduzi huu wa Wiki ya Nenda kwa Usalama Barabarani.
Ndugu zangu wa Tanga,
Nalipongeza Baraza la Taifa la Usalama Barabarani kwa maandalizi mazuri na kufanikisha maadhimisho haya. Ujumbe mliyouchagua kwa maadhimisho ya mwaka huu yaani ”ENDESHA SALAMA – OKOA MAISHA, TUZINGATIE SHERIA ZA USALAMA BARABARANI” ni muafaka kabisa. Ni ukweli usiopingika kuwa ajali nyingi za barabarani zinatokea kutokana na uzembe na kupuuza sheria za usalama barabarani. Takwimu zinaonyesha kuwa asilimia 56 ya ajali za barabarani hapa nchini hutokana na uzembe na ukosefu wa umakini wa madereva. Hivyo, basi kama madereva wataendesha kwa kufuata sheria za usalama barabarani ajali zinazotokea nchini zitapungua sana. Maana yake, tutaokoa maisha ya watanzania wengi kwa kuwaepusha na vifo na ulemavu.
Gharama za Ajali za Barabarani
Ndugu Wananchi,
Ajali za barabarani zimeendelea kugharimu maisha ya watu wengi, ustawi wa kaya nyingi na uchumi kwa ujumla. Kinachosikitisha ni kuwa sehemu kubwa ya ajali hizi zinaepukika ikiwa sheria za usalama barabarani na tahadhari zingechukuliwa na madereva wa vyombo vya usafiri na watumiaji wa barabara. Wakati mwengine hata ile dhana ya kuwa ‘ajali haina kinga’ inapoteza mantiki. Maana, ajali kwa asili yake ni tukio lisilozuilika na lisilobashirika kama lilivyo janga lingine lolote.
Hali ya Usalama Barabarani
Ndugu wananchi,
Takwimu za ajali za barabarani zinazotolewa na Jeshi la Polisi zinaonyesha kuwa, kwa miaka takribani mitano iliyopita yaani kuanzia mwaka 2010 hadi Desemba 2014, watu 19,264 wamepoteza maisha. Mwaka jana pekee watu 3,534 wamepokeza maisha, idadi ambayo ni karibu sawa na watoto wote (4,008) waliofariki kwa malaria nchini mwaka 2014. Aidha, katika mchanganuo huo, watembea kwa miguu ndio kundi lililoongoza kwa vifo vya ajali ambapo watu 6,013 walifariki dunia wakifuatiwa na abiria ambapo watu 5,708 walipoteza maisha. Watu wengine 3,825 walifariki kwa ajali za pikipiki, wapanda baiskeli 2,148, wasukuma mikokoteni 217 na madereva wa magari 1,383.
Mbali na wale waliopoteza maisha, kumekuwepo pia na majeruhi 96,788, ambapo majeruhi 19,155 ni watembea kwa miguu, 42,300 abiria wa magari, wapanda pikipiki 21,236, wapanda baiskeli 6,389, madereva 6,938 na wasukuma mikokoteni 770. Kwa vigezo vyovyote vile vya kitakwimu, idadi hii ni kubwa sana na haipaswi kuendelea hivi.
Naambiwa katika kipindi cha miezi sita (6) ya Mwaka huu (Januari - Juni 2015) pekee yake zimekwisha tokea ajali 4,079 zilizosababisha vifo vya watu 1,747 na kujeruhi watu 4,826. Ajali za pikipiki pekee ni 1,352 zilizosababisha vifo vya watu 473 na kujeruhi 1,275. Ni vizuri Watanzania mkasema imetosha. Hasara kwa taifa ni kubwa mno.
Ndugu Wananchi,
Kama nilivyosema awali, nyingi ya ajali hizi zingeweza kuepukika. Nasema hivyo kwa kuwa stadi zinaonyesha kuwa vyanzo vikubwa vya ajali vifuatavyo ndio vinavyochangia sehemu kubwa ya ajali zinazotokea nchini. Vyanzo hivi ni:
- i. Kuendesha kwa mwendo wa kasi kupita kiasi,
- ii. Kuyapita magari ya mbele yao bila ya kuchukua tahadhari,
- iii. Kuendesha magari mabovu barabarani,
- iv. Kutoheshimu alama na michoro ya barabarani,
- v. Kuendesha vyombo vya moto bila kupata mafunzo na bila leseni,
- vi. Kubeba abiria zaidi ya mmoja kwenye Pikipiki,
- vii. Kuendesha gari/pikipiki dereva akiwa amekunywa au ametumia kilevi (viroba),
- viii. Kuzidisha mizigo au abiria kwenye vyombo vya usafiri,
Kwa vile haya hayazingatiwi haishangazi kwa nini ajali ni nyingi na utetezi wa ‘ajali haina kinga’ unapoteza maana.
Wajibu wa Wadau Katika Kudhibiti Ajali
za Barabarani
Ndugu Wananchi,
Kuzuia na kudhibiti ajali za barabarani ni jambo linalotegemea wajibu wa kila mmoja wetu. Serikali, ina wajibu wa kuhakikisha kuwa kunakuwepo na miundombinu mizuri na sheria za usalama wa barabarani inasimamiwa ipasavyo. Kikosi cha Polisi wa Usalama Barabarani kinapaswa kusimamia utekelezaji wa sheria za usalama barabarani kwa ukamilifu, bila ajizi, uzembe wala rushwa. Wamiliki wa vyombo vya kusafirisha abiria na mizigo wanapaswa kuhakikisha kuwa wakati wote vyombo vyao viko katika hali nzuri ya kusafiri barabarani. Lazima viwe vinakidhi vigezo na viwango vya usalama ili visihatarishe maisha ya watu na mali inayobebwa. Vivyo hivyo, na hasa madereva wanapaswa kutii sheria, kuzingatia alama za barabarani na kutambua dhamana kubwa waliyonayo ya kubeba roho za watu na mali.
Mara nyingi, abiria wanajisahau kuwa na wao wanao wajibu muhimu katika kuzuia ajali za barabarani. Hawana budi kuchukua tahadhari kwa mambo matatu. Kwanza, kutokukubali kupakiwa wengi zaidi ya uwezo wa chombo cha usafiri. Pili kutokukubali kuendeshwa kwa mwendo wa kasi kupita kiasi. Na, tatu watoe taarifa kwa askari wa usalama barabarani pale ambapo dereva anaonyesha dalili za kukiuka kwa makusudi sheria na kanuni za usalama barabarani. Wasikubali wala kuwaogopa madereva wanaohatarisha maisha yao wakati wamelipa nauli. Watu wamekata tiketi kwa lengo la kufikishwa wanapokwenda, kwa usalama na siyo kwenda kuzimu. Mkumbuke kuwa unyonge wenu ni mauti yenu. Ikiwa kila mmoja atatimiza wajibu wake katika mnyororo huu wa wajibu, tutaweza kuepusha ajali nyingi na hivyo, kuokoa maisha ya watu, kuwanusuru watu wasipate vilema na kuokoa mali zisiharibiwe.
Hatua za Kuchukua
Ndugu Wananchi, mabibi na mabwana,
Hatuna budi kubadilika namna tunavyoliangalia suala la usalama barabarani. Tusilichukulie suala la usalama barabarani kama ni jukumu la Kikosi cha Usalama Barabarani peke yake. Tunapaswa kubadilisha mitazamo yetu na kuliona suala hili kuwa ni letu sote. Hivyo inatulazimu sote kila mmoja na kwa umoja wetu kuchukua hatua kwa kadri ya uwezo wetu katika kukabiliana na tatizo hili. Kwa ajili hiyo, nataka Baraza la Taifa la Usalama Barabarani kufanya yafuatayo:
- i. Kuelekeza nguvu zetu katika kudhibiti vyanzo vikuu vya ajali na kusababisha vifo, majeruhi na uharibifu wa mali. Mambo hayo nilishayataja lakini nisisitize mambo matano; ambayo ni mwendo kasi, ulevi, kutovaa kofia ngumu (helmet), kutofunga mkanda, na vifaa vya kuwalinda watoto wadogo wakiwa ndani ya gari (Child Restrain),
- ii. Kuanzisha mfumo wa kuweka alama kwenye leseni za udereva (points system) ili kuwaondoa madereva wanaokithiri kwa kukiuka sheria na kuwafungia kuendesha vyombo vya usafiri wale watakaoonyesha usugu,
- iii. Kupendekeza marekebisho ya Sheria na Kanuni za usalama barabarani ili ziendane na wakati na kutilia maanani namna ya kudhibiti wimbi la ajali za barabarani. Hii ni pamoja na kufunga kamera katika barabara kuu ili kufuatilia mienendo ya madereva wa masafa marefu barabarani,
- iv. Kikosi cha Usalama Barabarani kiongeze nguvu katika kudhibiti ajali za barabarani. Pamoja na mkazo unaowekwa kwenye kukusanya faini, tufanye hivyo pia kwenye kudhibiti ajali. Tuwachukulie hatua wale askari wachache wanaoendekeza vitendo vya rushwa. Hali kadhalika uanzishwe mfumo wa ulipaji faini kwa njia ya benki na simu ili kuondoa vishawishi vya rushwa,
- v. Kutoa elimu ya kuhamasisha umma juu ya usalama barabarani kwa watumiaji wa barabara na katika shule zetu za msingi na sekondari,
- vi. Wamiliki wa mabasi na magari ya mizigo washirikishwe katika mkakati wa kudhibiti wimbi la ajali za barabarani, na wasimamiwe kutimiza wajibu wao kwa madereva,
- Shirika la Viwango Tanzania (TBS) liongeze uwezo wa kukagua mara kwa mara viwango vya matairi, vipuri na mabodi ya mabasi nchini,
- Wakala wa barabara nchini (TANROADS) ihakikishe kuwa alama za barabarani pamoja na michoro stahiki inakuwepo barabarani wakati wote,
- ix. Mfumo wa ukaguzi wa magari kwa lazima (Mandatory Vehicle Inspection) uanze kutumika. Isiwe tena hiari ili kuhakikisha usalama wa magari yanayotumika katika barabara zetu. Msiishie tu kuuza stika za ukaguzi wa magari.
- x. Kutoa msukumo maalum kwa shughuli za utafiti wa suala la usalama barabarani ili kupata majawabu ya kisayansi na kimfumo ya namna ya kulipunguza tatizo la ajali za barabarani kutoka kiwango cha sasa. Natambua tayari Chuo Kikuu cha Dar es Salaam na Taasisi ya Teknolojia (DIT) wanafanya tafiti hizi, shirikianeni nao kwa ukamilifu.
Hitimisho
Ndugu Wananchi,
Mimi naamini tukiamua na kuchukua hatua zinazostahili kwa uthabiti tutaweza kupunguza idadi ya ajali za barabarani na kubaki zile tu ambazo kweli ni za bahati mbaya. Tutaokoa maisha ya watu wengi, tutapunguza idadi ya yatima, na kupunguza idadi ya walemavu. Haya yanawezekana kwani iko mifano ya kuwezekana kwenye nchi za wenzetu. Tuwe tayari kujifunza na kuiga kutoka kwao.
Niruhusuni nimalize kwa kusisitiza kuwa kila mmoja wetu dereva, abiria, watembea kwa miguu, wamiliki wa vyombo vya usafiri anapaswa kutimiza wajibu wake kwa kuchukua hatua zinazostahili kuchukuliwa. Mimi naamini kila mtu akichukua kinga na tahadhari, hakutakuwepo na ajali zitokanazo na uzembe. Zitabaki zile tu zisizoepukika. Lazima tufanye kila lililo ndani ya uwezo wetu kukabiliana na tatizo hili.
Inawezekana, timiza wajibu wako. Sasa natangaza kuwa maadhimisho ya Wiki ya Nenda kwa Usalama Barabarani mwaka 2015 yamefunguliwa rasmi.
Ahsanteni kwa kunisikiliza.




