Hotuba

- May 05, 2014
SPEECH BY HIS EXCELLENCY DR. JAKAYA MRISHO KIKWETE, THE PRESIDENT OF THE UNITED REPUBLIC OF TANZANIA, AT THE OPENING OF THE INTERNATIONAL ASSOCIATION OF WOMEN J...
Soma zaidiHotuba
Hon. Mohamed Othman Chande, Chief Justice of the United Republic of Tanzania,
Hon. Madame Aloma Mariam Mukhtar, Chief Justice of the Federal Republic of Nigeria,
Hon. Dr. Asha-Rose Migiro, Minister for Constitutional and Legal Affairs;
Hon. Eusebia Munuo, President of the International Association of Women Judges, (IAWJ);
Hon. Engera Kileo, Chairperson of Tanzania Women Judges Association,
Hon. Presidents of various Courts and Tribunals Present
Hon. Judges and Magistrates;
Madame Joan Winship, Executive Director of International Association of Women Judges (IAWJ),
Members of the Diplomatic Corp;
Distinguished Guests,
Ladies and Gentlemen;
I thank your Lordship Mr. Chief Justice Mohamed Chande Othman and Madam Justice Eusebia Munuo for inviting me to join you at this auspicious occasion of gracing the 9th Biannual Conference of International Association of Women Judges. I thank the organisers for affording my dear country, Tanzania the rare opportunity of hosting this all important biennial conference for the first time. On a personal note, I sincerely appreciate the honour and priviledge of being associated with the two conferences.
Allow me at the outset, to welcome to Tanzania, all distinguished delegates who have travelled from afar. I thank you for coming, you have done us proud. As I wish you successful deliberations, I implore you to visit some of the tourist sites near Arusha. As you know this is the hub of Tanzania northern tourist circuit which is home to Mount Kilimanjaro and world renown sanctuaries like the Serengeti National Park and the Ngorongoro Crater which is the cradle of humanity. The spice Islands of Zanzibar, the ultimate paradise on the Indian Ocean is only half an hour away by plane.
I am sure you will enjoy the experience of visiting these leisure places and be enticed to come back for a longer safari and holiday experience.
Distinguished Delegates;
Ladies and Gentlemen;
This distinguished gathering of women legal luminaries from all over the world presents a perfect occasion to reflect upon important issues relating to administration of justice. I understand that, this gathering of experts from across the globe blends knowledge and experience, which is a perfect recipe for an enriched thinking and discussion. I trust that the coming five days of this Conference will generate useful discussions and ideas for the improvement of our respective legal sectors and systems, as well as the profession at large.
The Conference Topic
Distinguished Delegates;
Ladies and Gentlemen;
I have been informed that this conference has chosen to deliberate on a theme “Justice for All”. This is laudable, for, a gathering of Women Judges would definitely be concerned with matters relating to human equality in terms of equal access to justice than anybody else. This is for obvious reasons. The current social dispensation cries very loud for enhanced equality in our societies and the dispensation of justice is one such area that calls for that. It is unfortunate that, in this 21st century, we are still grappling with matters that are a hindrance to equality in accessing justice.
I am constrained to note that my country, with more than 50 years of independence is also still grappling with such matters. Let us together reflect on these issues, the efforts we have made in addressing them and the way forward. We shall definitely find that they resemble in most jurisdictions, where the majority of the delegates present here come from.
Distinguished Delegates,
Ladies and Gentlemen;
A discussion of the theme “Equal Access to Justice” will require to address issues like adequacy of laws, rules and regulations that govern administration of justice, sufficiency of manpower, infrastructure and resources to dispense justice as well as ethics and attitude of the legal staff as well as the society towards justice. Unfortunately, most of our societies have found themselves in situations which all the above matters are serious challenges for their resolve to ensure equal access to justice. To cap it all, poverty is the biggest hindrance to any effort to address the shortcomings that come across the efforts to unlock these problems.
Inadequacy of Laws
Ladies and Gentlemen;
When it comes to laws, rules and regulations, except for the developed world and countries which in one way or the other laws are home grown, which are few, the majority of our countries which emerged from colonialism have found ourselves inheriting foreign laws, rules and regulations that had to be administered in dispensing justice. Unfortunately, these laws alien as they are, are incomprehensible to the majority of the people. To make matters worse, the vexing procedural aspect born out of them has resulted in making the process of dispensing justice inordinately very slow, hence not effective to the desired standards. This has made most of our legal regimes to be seen as methods of coercing our respective societies rather than a desired tool of regulating our good lives.
To the poor, these laws are perceived as expensive tools best used by the affluent in society to oppress them, and to expropriate their properties, freedom and dignity. Unfortunately, even our customary laws which are homegrown came to be interpreted in the same way. Concerted efforts are, therefore, required to ensure that our legal system is reformed enough in order to guarantee equal access to justice.
Insufficiency Infrastructure, Manpower and Resources
Distinguished Delegates;
Ladies and Gentlemen;
To add to the inadequacy of laws, rules and regulations, there is an inherent problem of insufficiency of infrastructure, manpower and resources. Most jurisdictions emerged from colonialism with a despicable state of poverty. Hence in scaling up priorities, economic development was ruled rather higher than anything else. Second to it ranked the provision of social amenities particularly health and education. Administration of justice trailed far behind.
For quite a while the legal sector was not accorded the requisite investment. The transition from colonialism was very slow in this regard. It is not gainsaying therefore that, our respective legal machineries are characteristic of shortage in infrastructure in terms of buildings equipment, manpower and resources. Thanks to the awakening realization which came to catch up a few decades later that, economic development has a lot to do with justice in our societies. Two good examples can be made out. First, societal stability has a close relationship with the capacity to punish criminals, as this creates a stable society for a vibrant economic growth. Second, the realization that capacity to enforce contracts is necessary in order to provide a regulated and orderly interpersonal economic relationship and trust, which provide a solid basis for economic growth.
Adequate infrastructure alone without competent manpower may not bring about the desired results. Investment in manpower of all cadres in the administration of justice is critical for ensuring quality justice. I am told, the quality of justice is reflected first in professionalism in terms of excellent knowledge of the law by all players; Judges, Magistrates and other Judicial Staff on the one hand and a vibrant bar; Attorneys, Prosecutors and Advocates. Second is discipline and a sense of responsibility. Without these attributes the very root of professionalism will be defeated.
Efforts to Unlock the Shortfalls
Distinguished Delegates;
Ladies and Gentlemen;
The realization of the need to unlock bottlenecks that has befallen the legal sector, made my country, and many of our jurisdictions embark on Legal Reform Programmes aimed at ensuring efficiency in dispensation of justice taking into account the ability to access justice by the majority of the citizens from all walks in life. Through a number of programmes, country’s have embarked on reforms of the legal sector for the purpose of making our justice system accessible by the majority of the people. In my country for example, thanks to the formidable work by our old Jurist Judge Bomani and his team who between 1993 and 1996 produced the legal sector report, which formed the basis for the more ambitious legal reform strategy, that addresses among other things, challenges relating to access to justice.
Through the Law Reform Commission and BEST Project among others, a number of our legislation have been reviewed with a view to putting in place a speedy and effective civil justice system. The Commercial Court which specializes in resolution of commercial disputes has been established and has shown good progress in resolution of commercial disputes. The Labour Court has also been reformed in line with a revamped Labour Legislation. We now have a more effective labour disputes resolution system, compared to the hitherto semi executive system which was ineffective. The Land Courts and tribunals which have been established across the country from the village level to the High Court provide better access to litigants than was the case before they were established.
The criminal justice system has gone through an evolution of reform in line with the enhancement of Human Rights. I must admit though, that a lot more remains to be done in order to ensure effective penal, corrective and rehabilitative services are rendered to the society. It is my wish that forum like this one tackles difficult issues of this nature and provides practical solutions.
Institutional Rehabilitation
Ladies and Gentlemen;
Access to justice requires institutional rehabilitation of our justice system in order to instill efficiency. Our resolve to bring justice close to our people entails assurance that justice services are made available as close to the people as possible. We have resolved to build High Court Centres in every region, establish Courts of Resident Magistrates in every district and we have embarked on a momentous resolve to assign graduate lawyers at Primary Courts level. So far we have employed 300 graduate lawyers to serve in Primary Courts. The end result of this will be to ensure that eventually quality justice is accessed right from the Primary Court level to the highest level. One endeavour we have set to accomplish while in office is the building of High Court buildings in every region. We have managed to built High Court buildings in 17 regions, this year we have committed funds to build four High Courts and the remaining four will be built in the next financial year.
The institutional rehabilitation of our justice system includes reshaping of our administrative structures of the judiciary by adding up expertise in the management of the judiciary. In so doing, a legal as well as administrative framework of deploying a court administrator in the judiciary has been completed. This has added a lot of improvement, by unlocking the judicial staff and making them available for Judicial work, while Court administrators have been left to deal with administrative matters.
To ensure budgetary independence of the judiciary, the establishment of the Judiciary Fund has proved extremely useful. Now the judiciary has been more independent in the management of their finances.
Judiciary Manpower
Distinguished Participants;
Whatever investment in the justice system will only yield the desired success with deployment of adequate competent manpower. We have increased the establishment of Judges in the High Court and Court of Appeal. When we came into office in 2005 there were 45 Judges, out of whom, women were 10. Currently we have 78 Judges and 30 of them are women. I am one of those leaders who have a strong conviction in gender balance if not equality. Hence during our tenure in office we have been able to appoint the highest number of the Women Judges both of the Court of Appeal and the High Court. We have also directed those who employ judicial staff in the Lower Courts to do the same. I believe, with a good number of women judges in our high judicial offices our justice system is in good hands. Fortunately, they have not let me down. I am aware that a good number of our Regional and Zonal Registries which are manned by women judges are exemplary demonstration of dedication, hard work and output. I commend them all for the work very well done.
Legal Representation
Distinguished Delegates,
Ladies and Gentlemen;
Effective access to justice has a lot to do with legal representation. In our case, until very recently the number of advocates never exceeded a thousand. Thanks to the efforts and initiatives of the present leadership in the Judiciary, which has taken advantage of the expanded training of the legal professionals to increase enrollment of new advocates from 1,060 Advocates in 2006 to 4,184 advocates in 2013, an increase of 3,124. Still even with this number, the ratio of an advocate to the population remains to be very low. The demands for legal services in our society is very high. Many people are denied of their rights simply because of lack of legal representation, which invariably is perceived as an expensive luxury for the affluent in the society. Pro-bono schemes which are meant to assist the disadvantaged groups in society are mostly confined in urban areas leaving the majority in the rural areas unable to access such services. Unfortunately, the most vulnerable are the silent majority in the rural areas.
I am told even the legal practice in the urban areas require to be further defined in terms of specialization and organization. Until such time when retraining and organization in terms of specialization will be achieved, access to specialized justice system will remain an expensive affair for the few. Unless efforts are made to ensure that provision of legal services pro-bono to the disadvantaged majority, access to justice by all may not be achieved.
We in government have realized that these are challenges. The decision to staff courts of all ladders with graduate magistrates is meant to ensure that legal representation becomes possible in all Courts. We want to overcome the present situation which do not allow legal representation in primary courts because they are manned by non graduate judicial staff, yet they attend to the majority of our citizenry in a manner that does not accord effective access to justice.
Multisectoral Approval to Justice Dispensation
Distinguished Delegates;
Ladies and Gentlemen;
The reforms of our Justice System will not bear the desired results without involving the whole legal sector. The Criminal Justice System for example, requires that the whole system to be made effective to address not only new challenges and emerging crimes but also is compliant to human rights standards. The hounds of justice, prosecutors and prisons must be brought to the chain in order to make the system effective and accountable. This way deterrence to crime will be achieved. We are doing everything within our disposal to achieve that. There are conspicuous achievements on this score.
The modernization of Civil Justice System entails review of a number of legislation in order to weed out archaic rules and procedures that impede access to justice. The unwanted laws which are discriminatory to women and children have to be corrected and work for the accomplishment of this task is underway. It is our desire to see that our legal system is an effective and perfect tool for making all our citizen access justice notwithstanding their differences on their status in life.
Conclusion
Distinguished Participants;
Accessing justice by every person is a precious right that has to be embodied in every sphere of life. This endeavor has to progress in tandem with growth in the economic as well as social spheres. We do no longer wish to see our countries ranked down in parameters like cost of doing business indices, simply because our justice systems are dysfunctional that they cannot enforce Contracts. We do not wish to see our societies are so segmented that the rich can buy their way and the poor are driven for a ride. We need to see that every person who happen to be in this universe has guaranteed rights without regard to the status in life he or she may happen to live. We want to see that our women are respected and are held to the highest esteem they deserve. We need to groom our children to become justice minded in a society that respects justice.
Ladies and Gentlemen;
This conference is best placed to address all the overarching issues in respect of inclusion of all persons in society in addressing challenges on equal access to justice. I wish you all the best in the days you will stay here and that you spend your good time to participate in the Conference. You will, as I said earlier, find that Arusha is a very pleasant place where you can do both work and relaxation. Make use of this unique opportunity. I know you need it.
Madam President,
Distinguished Delegates,
Ladies and Gentlemen;
It is now my singular honour and pleasure to declare that this 9th Biennial of Conference International Association of Women Judges is officially opened. I wish you fruitful deliberations.
I thank you for your kind attention!
Asanteni sana.
honourable duty of our Women Judges in their efforts to reconstruct our society into an equitable one, the efforts which accord women their deserving equitable position in the society. I would be the very last person not to join my hands in adding my contribution to their efforts.

- May 02, 2014
HOTUBA YA MHESHIMIWA RAIS WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA DKT. JAKAYA MRISHO KIKWETE KWENYE KILELE CHA SIKUKUU YA WAFANYAKAZI DUNIANI, MEI MOSI 2014, DAR ES...
Soma zaidiHotuba
Kaimu Rais wa Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi Tanzania;
Bibi Northburga Maskini;
Waziri wa Kazi na Ajira, Mheshimiwa Gaudensia Mugosi Kabaka(MB);
Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu, Divisheni ya Kazi,
Mh. Regina Rweyemamu;
Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Mheshimiwa Sadiki
Meck Sadiki;
Waheshimiwa Mawaziri na Wabunge;
Mkurugenzi wa Shirika la Kazi Dunia (ILO), Kanda ya
Afrika Mashariki, Ndugu Alexio Msindo;
Viongozi mbalimbali wa Serikali mliopo hapa;
Katibu Mkuu wa Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi,
Ndugu Nicholaus Mgaya;
Ndugu Almas Maige, Mwenyekiti wa ATE;
Mkurugenzi Mtendaji, Chama cha Waajiri Tanzania (ATE),
Dr. Aggrey Mlimuka;
Mheshimiwa Abdulrahman Kinana, Katibu Mkuu wa CCM na Viongozi wa Vyama vya Siasa Mliopo;
Waheshimiwa Mabalozi;
Msajili wa Vyama vya Wafanyakazi na Waajiri, Ndugu Doroth Uiso;
Wenyeviti na Makatibu wa Vyama vya Wafanyakazi;
Viongozi wa Vyama vya Siasa;
Ndugu Wafanyakazi wenzangu;
Mabibi na Mabwana;
Shukrani
Awali ya yote naomba tuanze kwa kumshukuru Mwenyezi Mungu, mwingi wa rehema, kwa kutujalia uhai na kutuwezesha kukutana leo katika sherehe za mwaka huu za kuadhimisha siku ya wafanyakazi duniani. Aidha, natoa shukrani nyingi kwa Kaimu Rais wa TUCTA Mama Northburga Maskini na viongozi wenzako kwa heshima kubwa mliyonipa ya kuja kuungana na wafanyakazi wa Tanzania katika kuadhimisha siku hii adhimu.
Napenda kutumia fursa hii kupitia kwako Kaimu Rais wa Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi Tanzania, kutoa salamu nyingi za pongezi na mkono wa heri kwa wanachama na Viongozi wa Vyama Vyote vya Wafanyakazi katika kuadhimisha siku hii kubwa na adhimu. Nawapongeza sana Chama cha Wafanyakazi wa Taasisi za Elimu ya Juu, Sayansi, Teknolojia, Habari na Utafiti (RAAWU) kwa kuratibu vizuri maadhimisho ya mwaka huu. Nimefurahi kusikia kuwa maadhimisho ya mwaka huu yamehusisha wiki ya wafanyakazi ambako kumekuwa na maonyesho ya waajiri na wafanyakazi. Huu ni utaratibu mzuri ambao licha ya kuongeza hamasa kwa maadhimisho haya lakini pia umetoa fursa kwa wananchi wengi kujionea wenyewe mambo muhimu mnayoyafanya wafanyakazi.
Nitakuwa mwizi wa fadhila nisipowapongeza na kuwashukuru wananchi wa Mkoa wa Dar es Salaam wakiongozwa na Mkuu wa Mkoa, Mheshimiwa Saidi Meck Sadiki kwa kukubali kuwa wenyeji wa sherehe hii. Si kazi rahisi hata kidogo, hivyo wanastahili pongezi zetu kwa kufanikisha vyema shughuli hii. Tumeona jinsi uwanja ulivyofurika na maandamano yalivyofana. Usione vinaelea vimeundwa. Tafadhali pokeeni pongezi zetu sote.
Pongezi kwa Wafanyakazi Bora
Wafanyakazi Wenzangu,
Kwa mara nyingine tena katika sherehe hizi wafanyakazi bora wametambuliwa na kupewa tuzo. Mnastahili pongezi zetu sote kwa kufanya kazi kwa bidii, maarifa na nidhamu na kutambuliwa. Wahenga walisema, ”Chanda chema huvishwa pete”. Nawapongeza TUCTA na waajiri kwa kutambua umuhimu wa kutoa tuzo kwa wafanyakazi bora. Inaongeza ari ya kufanya kazi na tija kazini. Tafadhali udumisheni utaratibu huu. Kwa wale ambao hawakupata safari hii wasikate tamaa na wao siku yao yaja waongeze bidii, maarifa na nidhamu kazini ili mwakani, siku kama ya leo iwe zamu yao kupongezwa.
Risala ya Wafanyakazi
Ndugu Kaimu Rais wa TUCTA,
Wafanyakazi Wenzangu,
Nimeisikiliza kwa makini sana risala yenu iliyowasilishwa na Katibu Mkuu wa TUCTA Ndugu Nicholas Mgaya ambaye anastahili pongezi kwa kuwasilisha vizuri na kueleweka. Ni risala nzuri iliyosheheni mawazo mazuri ya kujenga. Ndani yake inayo maombi, lakini pia mapendekezo. Napenda kuwahakikishia kuwa mapendekezo yote nimeyachukua na tutakwenda kuyafanyia kazi. Baadhi ya maombi si mapya, yamerudiwa ili kuweka msisitizo. Mengine majawabu yake tunayo, nitayatolea maelezo katika hotuba yangu.
Kauli Mbiu
Wafanyakazi Wenzangu,
Nawapongeza kwa Kauli mbiu yenu isemayo, ”Utawala Bora Utumike Kuondoa Kero za Wafanyakazi”. Kauli mbiu hii ni muafaka na maridhawa kabisa. Ni ukweli usiopingika kuwa utawala bora ni jambo muhimu sana na pale ambapo upo si tu kwamba husaidia kutatua kero za wafanyakazi, bali pia huepusha mikwaruzano na migogoro kati ya wafanyakazi na waajiri.
Wafanyakazi Wenzangu,
Uzoefu unaonyesha kuwa migogoro ya wafanyakazi na waajiri hujitokeza zaidi pale ambapo kanuni za utawala bora za ushirikishwaji, uwajibikaji na uwazi hazifuatwi. Usiri usiyo wa lazima katika uamuzi, hufanya hata uamuzi mzuri kutiliwa shaka na kujenga hofu isiyostahili kuwepo. Wakati mwingine inaweza kusababisha hata uamuzi mzuri kukataliwa. Pia, ukosefu wa taarifa sahihi unaweza kusababisha wafanyakazi kutoa madai yasiyotekelezeka kwa sababu ya kuwa na matarajio makubwa mno kuliko uwezo wa mwajiri kumudu.
Tumejifunza, vilevile, kuwa utawala bora hauishii kwenye kutunga sheria na kuunda taasisi na vyombo vya usimamiaji na utekelezaji wa Sheria. Utawala bora hauna budi kuwa sehemu kamili ya utamaduni wa kazi na uhusiano ambao unapaswa kuzingatiwa na waajiri na waajiriwa. Wakati mwajiri anawajibika kuwa muwazi kwa wafanyakazi wake na kuwatimizia stahili zao kama inavyopasika, waajiriwa nao wanawajibika kumtendea haki mwajiri kwa kufanya kazi kwa bidii na kuheshimu taratibu za kazi ikiwa ni pamoja na zile zihusuzo namna ya kuwasilisha madai yao.
Waajiri na waajiriwa kudai haki zao hakuwaondolei wajibu wao kwa kila mmoja wao. Hivyo basi, kudumisha utawala bora kunawataka waajiri na wafanyakazi kuheshimu Sheria za nchi zikiwemo zile zinazotawala uhusiano na ajira sehemu za kazi. Hapa nazungumzia, Sheria ya Majadiliano katika Utumishi wa Umma ya Mwaka 2003 na Sheria ya Ajira na Mahusiano Kazini Na. 6 ya Mwaka 2004.
Ndugu Zangu;
Lazima tutambue na kukubali kuwa ufanisi sehemu za kazi hutegemea uhusiano uliopo baina ya wafanyakazi na waajiri. Kama umejengwa juu ya misingi ya kuheshimu sheria na majadiliano, mambo huwa mazuri. Vitisho vya mwajiri na migomo ya wafanyakazi si suluhisho la kuondoa kero za wafanyakazi. Kwa jumla hupunguza ufanisi. Hivyo basi, lazima tufanye kila tuwezalo kujenga uhusiano mwema kati ya waajiri na waajiriwa. Ni kichocheo kikubwa cha watu kufanya kazi kwa bidii, kuongeza tija na uzalishaji sehemu za kazi hivyo kumwongezea mwajiri kipato na uwezo wa kuboresha maslahi ya wafanyakazi.
Hali ya Uchumi
Ndugu Viongozi na Ndugu Wafanyakazi;
Mwenendo wa uchumi wetu katika mwaka 2013/2014 ni mzuri. Uchumi umeendelea kuimarika ikilinganishwa na mwaka uliopita. Ukuaji wa uchumi unategemewa kuongezeka kutoka asilimia 7.0 ya mwaka 2013 hadi asilimia 7.2 mwaka huu. Haya ni matunda ya kazi nzuri ya wafanyakazi, wakulima na wadau wengine nchini. Tunayo kila sababu ya kujipongeza kwa mafanikio haya.
Habari nyingine njema kwa wafanyakazi ni kwamba mfumuko wa bei umeteremka kutoka asilimia 9 tulipokutana mwaka jana hadi asilimia 6.3 tunapokutana leo. Azma yetu ni kutaka ubaki chini ya asilimia 10 na hasa uwe asilimia 5 au chini ya hapo ifikapo Juni, 2015. Tunahangaikia sana kushuka kwa mfumuko wa bei kwa vile unapokua juu, unasababisha hali ngumu ya maisha kwa wafanyakazi. Tukidhibiti mfumuko wa bei uongezaji wa viwango vya mishahara utakuwa na tija. Aidha, inamuwezesha hata yule mwenye mshahara mdogo kuweza kukidhi baadhi ya mahitaji yake muhimu, hivyo kumpunguzia ukali wa maisha. Kwa sababu hiyo, hatuna budi kuongeza bidii katika kukuza uchumi na kushusha mfumuko wa bei. Kwa vile hapa tulipofika sio ukomo wa uwezo wetu, naamini tunaweza kupata mafanikio makubwa zaidi tukiongeza utawala bora mahala pa kazi. Kiwango cha ukuaji wa uchumi kinaweza kuwa kikubwa zaidi na kutunufaisha sote.
Mabaraza ya Wafanyakazi
Ndugu Wafanyakazi;
Hatuwezi kuzungumzia utawala bora mahala pa kazi bila ya kuwa na ushirikishwaji wa wafanyakazi. Ushirikishwaji wa wafanyakazi, unawezekana tu pale ambapo yapo mabaraza ya kazi na yanafanya kazi. Mabaraza ya kazi ni fursa kwa wafanyakazi kuwakilisha na kujenga madaraja kati ya menejimenti na wafanyakazi. Madaraja haya hujenga mazingira ya kuwezesha madai ya wafanyakazi kufika katika menejimenti, na uamuzi kufanywa na mrejesho wa menejimenti kuwafikia wafanyakazi.
Nimepata taarifa isiyofurahisha kuwa bado zipo taasisi chache za Serikali ambazo hazijaunda mabaraza hayo. Nimeambiwa pia kwamba baadhi ya yale mabaraza yaliyoundwa hayakutani kama inavyopasa. Hata hawakutani kujadili bajeti za taasisi zao, jambo ambalo ni sharti la msingi kutekelezwa kwa kisingizio cha kukosa fedha. Madai haya hayaingii akilini hata kidogo. Mbona semina na vikao vya menejimenti vyenye posho nono hatuoni vikiachwa kufanyika?.
Napenda kuwakumbusha wakuu wa taasisi zote za umma kuwa uundwaji mabaraza ya wafanyakazi na ushirikishwaji wa mabaraza hayo katika mchakato wa Bajeti sio jambo la hiari bali ni matakwa ya kisheria. Wasiounda mabaraza na wale wasioitisha vikao vya mabaraza kujadili bajeti za taasisi zao wanavunja sheria. Hili ni jambo lisilovumilika. Nimewaagiza Waziri wa Kazi na Ajira na Katibu Mkuu Kiongozi wahakikishe kuwa Wizara zote na taasisi zote za umma zinazingatia Agizo la Rais Na. 1 la Mwaka 1970 pamoja na matakwa ya Sheria ya Ajira na Mahusiano Kazini Na.6 ya Mwaka 2004. Lazima wahakikishe kuwa mabaraza yanaundwa mapema iwezekanavyo, na zile Wizara, Idara na Taasisi zisizoitisha mabaraza yao zibanwe kufanya hivyo bila ajizi.
Umuhimu wa Vyama vya Wafanyakazi Mahali pa Kazi
Ndugu Wafanyakazi;
Jambo lingine ambalo limenisikitisha sana ni taarifa kuwa bado wapo waajiri hasa katika sekta binafsi ambao wanakaidi matakwa ya kisheria ya kuwepo kwa matawi ya vyama vya wafanyakazi mahala pa kazi. Naambiwa hata pale wafanyakazi wanapoanzisha mabaraza hayo, wale wafanyakazi wanaokuwa mstari wa mbele kudai kuwepo matawi hayo au kutetea haki za wafanyakazi wamekuwa wanapata wakati mgumu. Huishia kuhamishwa au hata kufukuzwa kazi. Aidha, wapo baadhi ya waajiri ambao wameanzisha mifumo mbadala ambayo haiko kisheria katika kukwepa kushughulikia maslahi ya wafanyakazi.
Napenda kurudia na kusisitiza kuwa kuwepo kwa matawi ya vyama vya wafanyakazi mahala pa kazi si suala la hiyari bali ni matakwa ya kisheria. Hivyo, hakuna sekta, kampuni wala mwekezaji ambaye yuko juu ya sheria hii. Ni vizui ukaeleweka kuwa hii si tu ni sheria ya nchi yetu peke yake, bali ni matokeo ya mikataba ya kimataifa na ni haki ya msingi ya wafanyakazi na utawala bora.
Ndugu Viongozi na Ndugu Wafanyakazi;
Sisi katika Serikali ni mashahidi wa manufaa ya kuwepo kwa matawi ya wafanyakazi mahala pa kazi. Uzoefu wetu umetuthibitishia kuwa pale ambapo kuna matawi ya vyama vya wafanyakazi ambayo yanatimiza majukumu yake vizuri na menejimenti inatimiza wajibu wake ipasavyo uhusiano wa kikazi huwa mzuri. Inasaidia kupunguza migogoro, kuepusha migomo na huongeza tija na ufanisi. Matawi hayo hutoa fursa ya majadiliano na mazungumzo kati ya wafanyakazi na waajiri. Si kweli hata kidogo kuwa, kuwepo kwa matawi haya hukwamisha ufanisi mahala pa kazi.
Nimemwagiza Waziri wa Kazi kuhakikisha kuwa matawi ya vyama vya wafanyakazi yanakuwepo mahala pa kazi. Pia, ahakikishe kuwa wakaguzi wanapita sehemu za kazi na kukagua utekelezaji wa sheria kuhusu kuwepo kwa matawi hayo. Wale waajiri wanaokaidi wachukuliwe hatua za kisheria bila kuoneana muhali. Aidha, nimemtaka asisite kuwachukulia hatua zipasazo za kinidhamu, wakaguzi wanaoshirikiana na waajiri kudhoofisha haki za wafanyakazi. Hawa ni watu walioshindwa kutimiza majukumu yao hivyo wasivumiliwe. Wanaipaka matope Serikali.
Wapo Wakaguzi ambao wanakwazwa na kukaa kituo kimoja kwa muda mrefu, wamezoeleka mno na wamejenga mazoea yasiyofaa kati yao na waajiri na wanashirikiana kuwakandamiza wafanyakazi. Wahamishwe. Wakati huohuo wakumbusheni kuwa kazi yao ni kusimamia sheria, kutetea haki za wafanyakazi na waajiri na kamwe sio kuwa mawakala wa kuwasaidia waajiri kukiuka sheria.
Hatua za Serikali dhidi ya Uwakala wa Ajira
Ndugu Wafanyakazi;
Nimefurahishwa sana na uamuzi wa Mheshimiwa Gaudensia Kabaka, Waziri wa Kazi na Ajira na viongozi wenzake Wizarani wa kufuta mfumo mpya ulioanzishwa wa makampuni kuajiri kupitia uwakala wa ajira. Naunga mkono uamuzi wenu wa kupiga marufuku utaratibu unaofanywa na baadhi ya Wakala Binafsi wa Huduma za Ajira nchini wa kukodisha wafanyakazi katika Makampuni. Utaratibu huu ni kinyume cha Sheria ya Huduma za Ajira Na. 9 ya 1999. Sheria ya Huduma ya Ajira inaelezea majukumu ya msingi ya Wakala Binafsi wa Huduma za Ajira kuwa ni kuwaunganisha watafuta kazi na waajiri na siyo wao kuwa waajiri na kukodisha wafanyakazi kwa makampuni.
Wakala wa Ajira kufanya mambo kinyume na matakwa ya sheria haikubaliki. Anawakosesha wafanyakazi haki zao za msingi kama vile mishahara, huduma za hifadhi ya jamii, likizo ya uzazi, matibabu, mafunzo na mengineyo. Inaondoa uwajibikaji wa moja kwa moja wa waajiri kwa wafanyakazi wao. Hili ni jambo ambalo hatuwezi kuliacha liendelee. Nimempa Waziri wa Kazi na Ajira baraka zangu zote kulishughulikia kwa nguvu zake zote na kwa umakini na ufanisi mkubwa ili tuweze kukomesha kabisa dhulma hii.
Uimarishaji wa Vyombo vya Mashauriano
Wafanyakazi wenzangu;
Jambo lingine ambalo linahitaji kupatiwa ufumbuzi katika kuimarisha uhusiano kati ya wafanyakazi na waajiri ni ufanisi wa vyombo vya mashauriano. Serikali imefanya kazi nzuri ya kuunda vyombo hivi ikiwemo Baraza la Mashauriano (LESCO). Lengo la kuunda mabaraza hayo ni kutoa fursa ya usuluhishi wa migogoro ya kikazi na maslahi ya wafanyakazi kabla ya kuiwasilisha katika mifumo ya kimahakama.
Pamoja na nia njema ya Serikali, chombo hiki kimeendelea kulalamikiwa kwamba hakitekelezi wajibu wake kwa ukamilifu. Mashauri yanayowasilishwa hayatatuliwi kwa wakati kutokana na Baraza hili kutoitisha vikao, kwa madai ya ufinyu wa bajeti. Matokeo yake, wafanyakazi aidha wanaamua kufikisha migogoro yao kwa Waziri wa Kazi, au kwenda mahakamani au kuchukua sheria mkononi. Hatua zote hizi nje ya matumizi ya Baraza la LESCO, si endelevu na hazijengi mazingira ya maridhiano kati ya waajiri na wafanyakazi. Kwa jumla zinadhoofisha utawala bora.
Nimeelekeza, kuanzia bajeti ya mwaka wa fedha 2014/2015, Wizara ihakikishe inatenga fedha za kutosha za kuwezesha Baraza la LESCO kufanya vikao vyake. Aidha, bajeti hiyo ilindwe ili kuhakikisha kuwa pesa hizo zinatumika kwa ajili ya kazi za Baraza la Mashauriano. Ni jambo linalowezekana. Nataka tuone kuwa kuanzia mwaka ujao wa fedha Baraza hili linafanya kazi yake ipasavyo. Sote tunakubaliana kuhusu umuhimu wake kuwa ni mkubwa na ipo mifano ya nchi nyingine ambazo Baraza hili hufanya kazi kwa ufanisi mkubwa.
Naamini kwamba, kwa kuwa changamoto yetu si udhaifu wa Sheria yenyewe iliyounda LESCO bali ufanisi katika utendaji tu, upatikanaji wa fedha za kutosha utawezesha Baraza hili kufanya kazi kwa ufanisi. Mwisho wa yote tutaepusha migogoro isiyo ya lazima, lakini pia tutaimarisha utawala bora kwa kujenga madaraja kati ya watumishi na waajiri pale panapojitokeza mikwaruzano.
Ushiriki wa Wafanyakazi kwenye Bodi za Mashirika
Wafanyakazi Wenzangu,
Sambamba na kulihuisha Baraza la LESCO, Serikali inalifanyia kazi suala la kushirikisha wafanyakazi katika Bodi za Mashirika ya Umma. Tunafanya hivyo kwa kutambua kuwa, Bodi za Mashirika ni vyombo muhimu vinavyofanya uamuzi wa kisera na kiuendeshaji wa mashirika. Uamuzi wake hugusa moja kwa moja maslahi ya wafanyakazi hivyo uwakilishi wao ni muhimu.
Natambua kuwa tayari yapo mashirika ambayo kwa mujibu wa Sheria ya kuanzishwa kwake, yametambua uwakilishi wa wafanyakazi katika Bodi zake. Lakini yapo mashirika mengine hayana sharti hilo katika Sheria zilizounda mashirika hayo. Manufaa na umuhimu wa kuwashirikisha wafanyakazi si mambo yanahotaji mjadala. Yapo wazi. Katika yale mashirika ambayo Bodi zake zina wajumbe kutoka vyama vya wafanyakazi, tumeona namna ambavyo mchango wa wafanyakazi umekuwa wa msaada mkubwa.
Nimeelekeza Wizara husika na Mwanasheria Mkuu wa Serikali kuchukua hatua za haraka kuandaa na kuwasilisha muswada wa Sheria Bungeni wa kulirasimisha jambo hili kwa mashirika yote ya umma. Lengo letu ni kutaka kuhakikisha kuwa, jambo hili muhimu haliwi suala la utashi tu wa Shirika husika, bali ni utaratibu rasmi wa kisheria. Naamini ushiriki wa wafanyakazi katika Bodi za Mashirika utaimarisha utawala bora na kupunguza kero za wafanyakazi mahala pa kazi.
Maslahi ya Wafanyakazi
Ndugu Kaimu Rais, Ndugu Viongozi na Ndugu Wafanyakazi;
Nafahamu kuwa hotuba yangu haitakuwa imekamilika bila kuzungumzia maslahi ya wafanyakazi. Na, wengi hasa wanasubiri kusikia nasema nini kuhusu nyongeza ya kima cha chini cha mshahara na kupungua kwa kodi ya mapato, yaani Paye As You Earn (P.A.Y.E).
Napenda kurudia kuwahakikishia kuwa mimi na wenzangu Serikalini hatuna upungufu wa dhamira ya kufanya hivyo. Tumethibitisha hivyo miaka iliyopita na tutaendelea kuwa hivyo. Leo nitapenda kuzungumzia mambo matatu: La kwanza ni kuhusu Kima cha Chini cha Mshahara. Kama tulivyoahidi mwaka jana, Serikali ilipandisha kima cha chini cha mshahara kwa watumishi wa Umma kwa asilimia 41. Kwa ongezeko hilo, kima cha chini cha watumishi wa umma kiliongezeka kutoka shilingi 170,000 hadi shilingi 240,000. Na mwaka huu nawaahidi tena kuwa tutaongeza. Najua kwamba nyongeza hii si kubwa kuliko vile ambavyo wafanyakazi na hata mimi ningependelea iwe. Kwa kweli kinachotukwaza ni mapato ya Serikali kutokuwa makubwa kumudu nyongeza kubwa ya mshahara kwa wakati. Nyongeza hii peke yake inaifanya Serikali kutumia asilimia 44.9 ya bajeti ya Serikali kulipa mishahara na asilimia 10 ya pato la taifa (GDP). Kwa vigezo vyo vyote vile kiwango hiki ni kikubwa mno hivyo ni kielelezo thabiti cha dhamira yetu njema na kujali.
Isitoshe naomba mkumbuke kuwa mwaka 2005 kima cha chini cha mshahara kilikuwa shilingi 65,000.00. Hivyo ndani ya miaka saba tumeongeza kima cha chini karibu mara nne ya ilivyokuwa na kufikia kima cha chini cha sasa. Nawaahidi mwaka huu tutaongeza tena. Kama nilivyogusia, hatuwezi kutoa nyongeza kubwa mara moja lakini, kidogo kidogo tunaweza. Na tumeweza. Naamini, miaka mitano ijayo mambo yatakuwa mazuri zaidi wakati mapato ya Serikali yatakapoongezeka sana mauzo ya gesi asilia yatakapoanza.
La pili ni Kima cha Mishahara Katika Sekta Binafsi: Kima cha chini cha mishahara katika sekta binafsi bado hakinifurahishi. Kwa upande wa sekta binafsi, mfumo wa upangaji wa kima cha chini cha mshahara unatawaliwa na Sheria ya Taasisi za Kazi Na. 7 ya Mwaka 2004. Sheria hii inaanzisha Bodi za Mishahara za kisekta ambazo zina wajibu wa kutoa mapendekezo kwa Waziri wa Kazi na Ajira kuhusu kima cha chini cha mshahara katika sekta husika. Naambiwa kuwa Bodi hizi zinapata changamoto katika utekelezaji wa majukumu yake kwa kuwa waajiri hawatoi ushirikiano wa kutosha.
Mnamo mwezi Juni, 2013, Mhe. Waziri wa Kazi na Ajira alitangaza mishahara ya kima cha chini kisekta kupitia Gazeti la Serikali Na. 196/2013 kwa sekta 12 za Madini, Afya, Kilimo, Nishati, Usafirishaji, Viwanda, Ujenzi, Ulinzi binafsi, Shule binafsi, Hoteli, Huduma za Majumbani na Mawasiliano. Taarifa ninayopata ni kuwa, sehemu kubwa ya waajiri wa sekta binafsi hawazingatii viwango hivyo. Nimemuelekeza Waziri wa Kazi awabane wsiotekeleza watekeleze Tuzo alizotoa.
Naguswa sana na kilio cha wafanyakazi katika sekta binafsi. Sisi kama Serikali hatuwezi kukwepa wajibu wa kuwasaidia. Nimeelekeza kuwepo na mkakati maalum kushughulikia jambo hili. Katika mkakati huo, nashauri utaratibu wa Utatu yaani Wafanyakazi, Waajiri na Serikali utumike kufanya tathmini na kubaini matatizo yaliyopo na kupendekeza namna bora ya kuhakikisha wafanyakazi wa sekta binafsi wanapata mishahara wanayostahili. Katika mkakati wa muda mrefu, tumekubaliana na viongozi wenu kuimarisha vyombo vya mashauriano, usimamizi na bodi za kisekta ili huko mbele ya safari visimamie kwa ukamilifu jambo hili.
Jambo la tatu ni Kodi ya Mapato kwa wafanyakazi yaani PAYE: Kumekuwepo pia na ombi la muda mrefu la kupunguza kodi inayokatwa kwenye mishahara ya wafanyakazi kuwa chini ya asilimia 10. Kama nilivyoahidi mwaka jana, hili tutaendelea kulishughulikia kadri uwezo wa Serikali utakaporuhusu. Tumeshafanya hivyo kabla, na hatuna sababu ya kutofanya hivyo huko tuendako. Tayari tumepunguza kutoka asilimia 18.5 mwaka 2007 hadi asilimia 13 hivi sasa. Maombi yenu tumeyapokea, tuachieni, tuangalie nini tunachoweza kufanya kama miaka iliyopita. Kwa jumla ni nia yetu kuendelea kufanya hivyo mwaka hadi mwaka, tunakwazwa na uwezo mdogo wa mapato ya Serikali.
Mageuzi katika Mifuko ya Kijamii
Wafanyakazi wenzangu;
Kama nilivyosema wakati wa sherehe za Mei Mosi zilizofanyika mkoani Mbeya mwaka jana, Serikali ina dhamira ya dhati ya kupanua wigo wa hifadhi ya jamii kwa wafanyakazi na kwa wananchi wote kwa ujumla. Hatua kwa hatua tutaendelea kufanya marekebisho katika Hifadhi ya Jamii nchini ili iweze kukidhi haja hiyo.
Eneo moja ambalo tumejiandaa kulitekeleza kuanzia Julai, 2014 ni kuhusu fidia kwa wafanyakazi wanaoumia au kuathirika wakiwa kazini. Wote tunafahamu kwamba tangu mwaka 2008 Serikali ilipitisha Sheria ya Fidia kwa Wafanyakazi Na. 20 ambayo inaunda Mfuko wa Fidia utakaoshughulikia malipo yaliyo bora zaidi ya fidia kwa wafanyakazi wanaoumia au kufariki au kupata maradhi yatokanayo na kazi kuliko ilivyo sasa. Mfuko huu utahudumia wafanyakazi wa sekta zote yaani sekta binafsi na ya umma na utatoa mafao bora zaidi kuliko ilivyo hivi sasa.
Tunafanya hivyo kutokana na uzoefu tulioupata wa wafanyakazi wengi hasa katika sekta binafsi kushindwa kupata fidia stahili, wakati mwingine kutokana na uchanga wa waajiri wao. Kwa kuwa na mfuko huu kutawapunguzia waajiri mzigo wa kuwalipa fidia wafanyakazi wao hasa wakati ambao hawana uwezo wa kufanya hivyo. Mfuko utawapa wafanyakazi uhakika wa kulipwa fidia yao pale watakapopata madhara mahala pa kazi. Serikali itachangia asilimia moja ya jumla ya mishahara ya wafanyakazi kila mwezi kuanzia mwezi Julai, 2014. Waajiri binafsi nao watachangia asilimia 0.5 ya jumla ya mishahara ya wafanyakazi wao.
Wafanyakazi Wenzangu;
Eneo jingine ambalo tuliahidi kulifanyia kazi ni kuhusu kuainisha mafao ya pensheni. Mchakato huu unaendelea vizuri na nafahamu kuwa Mamlaka ya Mifuko ya Hifadhi ya Jamii (SSRA) na Wadau yaani Vyama vya Wafanyakazi wanatarajiwa kukutana tarehe 5 Mei, 2014 kwa majadiliano zaidi. Kikao hicho kitajadili ulingano wa mafao yanayotolewa na Mifuko ya Hifadhi ya Jamii kwa kuweka vikokotoo bora vya Mafao ya Pensheni.
Ni vizuri kukumbushana kwamba, kuwa na vikokotoo vizuri ni jambo moja, na kuhakikisha uendelevu wa mifuko ya hifadhi ya jamii ni suala lingine. Hivyo, wakati tunaendelea na majadiliano hayo, hatuna budi pia kutoa umuhimu katika kuelimishana juu ya umuhimu na wajibu wa waajiri kuwasilisha michango ya wanachama. Mifuko ya hifadhi ya jamii inatakiwa kuhakikisha kuwa inakusanya michango ya wanachama wake na kuwekeza kwa umakini mkubwa. Wanachama wao wanatakiwa kuhakikisha kuwa michango yao inabaki katika mifuko ya hifadhi ya jamii ili ije kuwafaa wakati wa shida na maisha ya uzeeni, badala ya tabia ya sasa ya watumishi kuamua kushirikiana na waajiri kutokatwa michango hiyo, au kujitoa katika mifuko hiyo kila wanapobadilisha ajira kutoka kwa mwajiri mmoja kwenda kwa mwajiri mwingine.
Madai ya Waalimu
Wafanyakazi Wenzangu,
Serikali pia imeendelea kushughulikia madai mbalimbali ya watumishi wa umma hususan madeni ya mishahara na yasiyokuwa ya mishahara. Tumekamilisha uhakiki wa madeni kwa wafanyakazi wasiokuwa walimu. Hazina wameniarifu kuwa yatalipwa kabla ya mwaka ujao wa fedha. Kwa upande wa walimu, Serikali kwa kushirikiana na Chama cha Walimu (CWT) tumekuwa tunafanya uhakiki wa madeni ya walimu katika Halmashauri zote 147 za Tanzania Bara. Kazi imekamilika kwa Halmashauri 96 na inaendelea kwa Halmashauri 51 zilizosalia. Nimeambiwa kuwa madeni yaliyohakikiwa yameanza kulipwa. Na, kama nilivyosema kwa wafanyakazi wasiokuwa walimu ni makusudio ya Hazina kuwa madeni hayo yalipwe katika mwaka huu wa fedha.
Ni jambo la kutia faraja kwamba, katika kufanya kazi ya uhakiki wa madeni ya walimu. Serikali na Chama cha Walimu tumeweza kubaini mzizi wa fitina. Tumekubaliana kuutafutia dawa ya kuung’oa ili tatizo hili lisijirudie.
Kwa ajili hiyo, nimeelekeza Wizara na Taasisi zinazohusika hasa Wizara ya Fedha, Wizara ya Elimu na Mafunzo na Ufundi na Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, kuwachukulia hatua za kisheria na kinidhamu maofisa wa Serikali, wanaohusika na udanganyifu huu. Halikadhaika, wafanyakazi walioghushi stakabadhi nao wachukuliwe hatua za kisheria. Kwa muda mrefu, udanganyifu na hila za watumishi hawa zimechochea kutokuelewana na kutokuaminiana kati ya walimu na Serikali.
Ifike mahala sasa, walimu na Serikali tupate suluhu ya kudumu baada ya kumpata mchawi wetu. Tumekubaliana kuendelea na mfumo huu wa uhakiki wa pamoja kama msingi wa kutatua tatizo hili la muda mrefu. Huu ni mfano mzuri wa namna utawala bora unavyoweza kutatua kero za wafanyakazi kupitia ushirikishaji na uwazi.
Kuhusu muundo mpya wa Utumishi wa Walimu, habari njema ni kuwa muundo huo umekwishapitishwa na unatarajiwa kuanza kutumika tarehe 1 Julai, 2014. Suala la upandishaji wa madaraja ya walimu nalo linakwenda vizuri ambapo hadi kufikia Aprili 2014, walimu 30,236 walikuwa wamepandishwa vyeo.
Kuhusu wimbo wenu, Shemeji mshahara mdogo. Nimefuatilia nimebaini ni kweli kumekuwa na ucheleweshaji. Nimefuatilia Benki Kuu wanasema walitoa pesa mapema, lakini kumekuwepo na mkwamo mahali ambapo tutapatafuta.
Utoaji Holela wa Vibali vya Ajira kwa Wageni
Ndugu Kaimu Rais wa TUCTA;
Wafanyakazi wenzangu,
Yamekuwepo malalamiko kuwa kumekuwepo na utoaji holela wa vibali vya kazi kwa wageni kufanya kazi nchini. Naambiwa siku hizi hata zile ajira ambazo Watanzania wana ujuzi nazo hujazwa na wageni. Serikali imeyafanyia kazi malalamiko haya na kugundua kuwa udhaifu upo kwenye kuwepo kwa taasisi zaidi ya moja inayoshughulika na utoaji wa vibali kwa wageni kuishi na kufanya kazi nchini. Hali hii inatoa mwanya kwa watu wasiokuwa waaminifu kutoa vibali kwa watu wasiostahili.
Serikali imeamua kuzifanyia marekebisho sheria husika na iko mbioni kuwasilisha Bungeni Muswada wa Sheria ya Vibali vya Ajira. Nimeelekeza kuwa jitihada zifanyike ili Muswada huo uwasilishe kwenye kikao cha Bunge la Oktoba, 2014. Sheria hii sasa italiweka suala la vibali vya kazi kushughuhulikiwa na taasisi moja na hivyo kuweka udhibiti katika utoaji wa vibali hivyo.
Ndugu Wafanyakazi;
Niruhusuni nichukue fursa hii, pia, kukumbusha kuhusu umuhimu wa wafanyakazi kuheshimu na kuthamini kazi. Waswahili wana msemo “Usichezee kazi, chezea mshahara”. Yapo madai yanayojirudia kutoka kwa waajiri kuwa wafanyakazi wa Kitanzania hawathamini na kuheshimu kazi zao. Wanatuhumiwa kwa uvivu, udokozi na nidhamu ndogo. Napata taabu kukubali madai haya kuwa hii ndio sifa ya wafanyakazi wote wa Kitanzania. Leo nimetunuku tuzo kwa wafanyakazi bora na tumekuwa tunafanya hivyo kila mwaka. Kitendo hiki ni ushahidi kuwa wafanyakazi hodari wapo. Hata hivyo, siwezi kusema wavivu, wezi na watovu wa nidhamu hawapo. Lakini, sina uhakika na ukweli wa madai yanayotoa sifa mbaya na kutia doa baya kwa Wafanyakazi wa Kitanzania.
Sifa hizo hasi ndizo zinazowashawishi waajiri na hasa wawekezaji kutafuta wafanyakazi nje. Ninawaomba viongozi na wanachama wa vyama vya wafanyakazi mlitafakari suala hili kwa uzito unaostahili kwani linaelekea kuaminika. Kulikataa tatizo peke yake hakutoshi kwani hakutatui tatizo lililopo, zaidi ya kutupa faraja ya muda tu. Natoa rai kwa vyama vya wafanyakazi na Wizara ya Kazi na Ajira kulifanyia kazi jambo hili haraka.
Mchakato wa Katiba
Wafanyakazi Wenzangu,
Katika sherehe za Mei Mosi zilizofanyika mwaka jana kule Mbeya, mlitoa rai ya wafanyakazi kushirikishwa katika mchakato wa kutunga Katiba Mpya. Niliwaahidi kuwa mtashirikishwa kwa vile wafanyakazi ni sehemu kubwa sana ya jamii yetu na kundi muhimu sana katika taifa. Nimetimiza ahadi yangu wakati wa kuteua Tume ya Mabadiliko ya Katiba na Wajumbe 201 wa Bunge Maalum la Katiba. Kuna uwakilishi mkubwa wa wafanyakazi na kumfanya Ndugu Maige, Mwenyekiti wa ATE alalamikie uwakilishi mdogo wa waajiri. Kazi yangu nimemaliza, sasa iko kwa wawakilishi wenu kutumia vizuri fursa waliyopata kupigania haki na maslahi ya wafanyakazi bila ya kusahau maslahi ya Watanzania wengine. Bahati nzuri wajumbe wengi ni wafanyakazi hata kama hawakuingia Bungeni wakiwa moja kwa moja wanawakilisha wafanyakazi. Kwa hiyo ni rahisi kwa masuala ya wafanyakazi kutetewa. Hamna budi kuwasiliana nao.
Jambo muhimu kwenu kufanya ni kujipanga vizuri kwa hoja za kuwapa wawakilishi wenu kuzipigania. Msipofanya hivyo mtakuja kujikuta wawakilishi wenu wakatekwa na makundi yenye agenda na misimamo isiyoendeleza maslahi yenu. Sisemi wasijihusishe na mambo mengine yenye maslahi kwa taifa, la hasha!. Ninachosema wasifanye hayo na kuacha kusemea yenye maslahi ya wafanyakazi. Wanaweza kukosekana watu wa kuyasemea mkajutia fursa hii.
Naungana nanyi kusikitika kutokana na mienendo na kauli zisizoridhisha za baadhi ya Wajumbe wa Bunge Maalum la Katiba. Naungana nanyi pia kuwasihi watumie lugha ya staha na wazo la kutafuta majawabu kwa njia ya mashauriano itatuwezesha kumaliza tofauti za kambi. Nawasihi waliotoka Bungeni warejee pale Bunge Maalum la Katiba litakapoanza upya baada ya mapumziko ya kupisha Bunge la Jamhuri na Baraza la Wawakilishi kufanya shughuli za lazima hususan bajeti za Serikali zetu mbili.
Hitimisho
Ndugu Kaimu Rais wa TUCTA, Katibu Mkuu na Wafanyakazi Wenzangu;
Naomba nimalize kwa kurudia kuwashukuru tena kwa kunipa nafasi hii adhimu ya kujumuika nanyi tena katika sherehe za mwaka huu. Napenda kuwahakikishia, kwa mara nyingine tena, kwamba dhamira yangu binafsi, na ile ya Serikali ninayoiongoza ya kutatua changamoto zinazowakabili wafanyakazi iko palepale. Kilio chenu ni kilio changu. Tumejitahidi katika kipindi hiki kutatua matatizo ya wafanyakazi na mafanikio yake mnayaona. Nina imani kuwa tukishirikiana katika mwaka mmoja uliobakia tutaweza kutatua kero nyingi zaidi.
Mwisho, napenda kuwakumbusha kuwa, maslahi mazuri kwa wafanyakazi yana uhusiano wa moja kwa moja na kuongezeka kwa tija, uzalishaji, na pato la waajiri katika sekta binafsi na sekta za umma. Shime nawasihi muongeze juhudi ili nanyi mnufaike zaidi. Kwa upande wangu naamini kwamba neema haiko mbali sana. Tumefanikiwa kuweka misingi mizuri ya kiuchumi, tumeunda taasisi na kuweka mazingira mazuri ya kisheria na kisera. Bahati nzuri Mwenyezi Mungu ametushushia neema ya rasilimali ikiwemo gesi asilia. Vyote hivi kwa pamoja, vinatupa matumaini kuwa ndoto yetu ya kufikia nchi ya uchumi wa kati mwaka 2025 itatimia. Inawezekana Timiza Wajibu Wako.
Mungu Ibariki Afrika!
Mungu Ibariki Tanzania!
Asanteni sana kwa kunisikiliza. Nawatakia sherehe njema.

- Apr 28, 2014
HOTUBA YA MHESHIMIWA DR. JAKAYA MRISHO KIKWETE, RAIS WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA, WAKATI WA KUWEKA JIWE LA MSINGI LA UJENZI WA HOSPITALI YA CHUO KIKUU CH...
Soma zaidiHotuba
Mheshimiwa Balozi wa Jamhuri ya Korea nchini;
Mheshimiwa Dkt. Shukuru Kawambwa, Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi;
Waheshimiwa Mabalozi;
Waheshimiwa Mawaziri;
Waheshimiwa Wakuu wa Mikoa ya Pwani na Dar es Salaam,
Professa Ephata Kaaya, Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu Cha Afya na Sayansi Shirikishi, Muhimbili.
Viongozi na Watendaji wa Serikali,
Viongozi na Wanajumuia wa Chuo Kikuu cha Afya na Sayansi Shirikishi Muhimbili,
Wageni Waalikwa,
Mabibi na Mabwana;
Shukrani
Awali ya yote, napenda kukushukuru Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi kwa kunialika kuja kuweka jiwe la msingi la ujenzi wa hospitali ya kisasa ya kufundishia na kutolea huduma katika eneo hili la Kampasi mpya ya Chuo Kikuu cha Afya Sayansi Shirikishi Muhimbili, Mloganzila. Leo ni siku ya aina yake katika historia ya Chuo Kikuu cha Muhimbili na taifa kwa jumla. Kitendo hiki cha leo kinaashiria kuanza rasmi kwa kazi ya ujenzi wa Kampasi mpya ya Mloganzila ya MUHAS na ni kubwa katika uboreshaji wa huduma ya afya nchini. Shughuli hii kufanyika leo kama sehemu ya maadhimisho ya miaka 50 ya Muungano wetu ni jambo stahiki kabisa. Ujenzi huu ni moja ya kielelezo thabiti cha juhudi na mafanikio ya Serikali yetu, katika kuwapatia Watanzania huduma bora zaidi za afya.
Hali ya Sekta ya Afya Wakati Tunaungana
Wageni waalikwa, Mabibi na Mabwana;
Utoaji wa huduma bora za afya ni wajibu wa msingi wa Serikali yetu na uhai wa taifa letu. Wakati tulipoungana tarehe 26 Aprili, 1964, hali ya huduma ya afya ilikuwa duni na afya ya wananchi wetu haikuwa ya kuridhisha. Kulikuwa na hospitali chache mno, halikadhalika, vituo vya afya na zahanati zilikuwa chache sana. Iliwalazimu wananchi kutembea umbali mrefu sana kutafuta huduma za afya. Katika vituo hivyo vya kutolea huduma za afya vifaa vya uchunguzi na vifaa tiba vilikuwa haba na duni. Wataalamu wa fani mbalimbali za afya walikuwa wachache sana. Watu walikuwa wanakufa siku si zao kwa maradhi yanayoweza kuzuilika na kutibika. Umri wa wastani wa kuishi ulikuwa miaka 35. Kwa ajili hiyo, Serikali zetu zilitangaza maradhi kuwa moja ya maadui watatu wakubwa, wengine wakiwemo umaskini na ujinga.
Katika kipindi cha miaka 50 ya muungano, Serikali ya Muungano na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar zimepambana na adui maradhi kwa nguvu kubwa. Tumetoa kipaumbele cha juu katika kupanua na kuboresha huduma za afya. Hii imejidhihirisha kwa sera na mikakati mbalimbali ya afya inayotekelezwa, ukubwa wa bajeti za afya zinazotengwa, idadi ya miradi inayotekelezwa na matokeo mazuri yanayopatikana kutokana na juhudi hizo za Serikali.
Mafanikio ya Miaka 50 ya Muungano katika Sekta ya Afya
Ndugu Wananchi;
Jitihada zilizofanyika katika miaka 50 iliyopita zimewezesha kuongezeka kwa zahanati, vituo vya afya na hospitali, vifaa vya uchunguzi, vifaa tiba na wataalamu wa kada mbalimbali za afya. Kutokana na juhudi hizo, idadi ya Watanzania wanaopata huduma bora za afya katika ngazi zote imeongezeka sana na ushindi dhidi ya maradhi mengi unaonekana. Uwezo wetu wa kupambana magonjwa yanayoua watu wengi nchini umefikia mahali pazuri, na ule wa kuchunguza na kutibu maradhi yanayotulazimu kuwapeleka wagonjwa nje ya nchi unaendelea kuimarika. Kwa mfano, maambukizi ya ugonjwa wa malaria kwa watoto na akina mama wajawazito yamepungua kwa asilimia 50, na kule Zanzibar maambukizi ya malaria ni asilimia 0.3. Maambukizi ya UKIMWI yamepungua kutoka asilimia 18 mwaka 1986 hadi kufikia asilimia 5.1 hivi sasa.
Tunaendelea kuimarisha vituo vya kutoa huduma ya afya kuanzia zahanati, vituo vya afya, hospitali za wilaya, mikoa, kanda na taifa kwa majengo, vifaa tiba, vifaa vya uchunguzi na wataalamu. Katika ngazi ya taifa kwa mfano, tumepiga hatua ya kutia moyo kwa maradhi ya moyo, figo, saratani, mifupa, ubongo na mishipa ya fahamu. Kwa upande wa maradhi ya moyo tumejenga kituo cha tiba na mafunzo ya magonjwa ya moyo katika Hospitali ya Taifa Muhimbili yenye vitanda 100. Kituo hiki kinawezesha wagonjwa wa moyo wengi kupata matibabu hapa hapa nchini badala ya kupelekwa nje. Katika kipindi cha mwaka mmoja cha ufanyaji kazi wake, kituo hiki kimeweza kufanyia upasuaji wagonjwa 347, kuwawekea mashine za kuongeza nguvu kwenye moyo (pacemaker) wagonjwa 3 na mwaka huu wameanza uwekaji wa vyuma vidogo (stent) katika mishipa ya damu ya moyo ambayo imebana. Haya ni mafanikio makubwa na ya kutia moyo.
Kwa upande wa figo, hivi sasa tunatoa huduma za magonjwa ya figo katika Hospitali ya Muhimbili, Hospitali ya Kanda, Mbeya na Shule ya Tiba ya Chuo Kikuu cha Dodoma. Pale Chuo kikuu cha Dodoma pia tunajenga kituo kikubwa kitakachobobea kwenye maradhi ya figo. Lengo letu ni kwamba, kitakapokamilika chuo hiki kiweze kufanya matibabu ya kubadilisha figo (kidney transplant).
Aidha, tumeboresha taasisi ya saratani ya Ocean Road kwa mejengo, vifaa na wataalamu. Tumeongeza maradufu uwezo wa taasisi hiyo kulaza wagonjwa kutoka wagonjwa 120 mwaka 2011 hadi wagonjwa 290 hivi sasa. Halikadhalika, tumenunua mashine mpya kwa ajili ya uchunguzi na tumeongeza wataalamu waliobobea wa magonjwa ya saratani. Vilevile, tunakamilisha ujenzi wa jengo la Taasisi ya Mifupa, Ubongo na Mishipa ya Fahamu. Litakapokamilika tutaliwekea vifaa vya kisasa vya uchunguzi na tiba ili kuongeza uwezo wetu wa kukabiliana na maradhi haya.
Ujenzi wa Hospitali ya Kufundishia ya Kampasi ya Mlonganzila
Ndugu Wananchi;
Jiwe la msingi tunaloweka leo, ni mwendelezo wa juhudi hizi za Serikali za kupambana na adui maradhi. Hospitali hii itakuwa na vitanda 600, itakuwa na vifaa tiba vya kisasa kabisa kwa ajili ya uchunguzi na matibabu ya magonjwa mbalimbali yakiwemo ya mishipa ya fahamu. Ujenzi wa Hospitali ya Kampasi hii utasaidia sana kupunguza msongamano kwenye hospitali ya rufaa ya Taifa ya Muhimbili na za rufaa zilizopo nchini, ambazo hutoa huduma za utaalamu wa juu. Aidha, itasaidia kupunguza ulazima wa kupeleka wagonjwa nchi za nje kwa ajili ya matibabu. Matibabu nje ya nchi ni gharama kubwa kwa Serikali, lakini pia fursa zenyewe ni chache na wengi wengi hawapati nafasi ya kupelekwa nje kwa matibabu. Hivyo ujenzi wa hospitali hii ya Chuo Kikuu cha Muhimbili ni ishara ya wazi ya dhamira ya serikali katika kukabiliana na tatizo hili.
Hatua Zilizochukuliwa na Serikali Katika Ujenzi wa Kampasi na Hospitali ya Kufundishia
Ndugu Wananchi;
Baada ya Chuo Kikuu cha Muhimbili kutafuta eneo la kupanua huduma zake, mwaka 2006 nilifanya uamuzi wa kuwapatia eneo hili lenye ukubwa wa ekari 3,800 kwa ajili ya kujenga Kampasi mpya na hospitali ya kisasa ya kufundishia na kutolea huduma. Tulianza kutafuta fedha za ujenzi wa hospitali ya kufundishia, tukafanikiwa kupata mkopo wa riba nafuu kutoka Serikali ya Jamhuri ya Korea Kusini wenye thamani ya dola za Marekani milioni 76.5. Mkopo huo ungetosheleza kujenga jengo la hospitali hiyo pamoja na vifaa vya kisasa vya kutosheleza mahitaji ya hospitali.
Ujenzi haukuweza kuanza kwa wakati kutokana na mgogoro wa ardhi uliokuwepo katika eneo hili. Matokeo ya ucheleweshaji huo umepandisha gharama za ujenzi kwa dola za Marekani milioni 18. Maana yake ni kuwa fedha za mkopo tulizopata hazitoshi tena kukamilisha jengo hilo na kununulia vifaa kama ilivyokusudiwa. Viongozi wa Chuo Kikuu cha Muhimbili waliponijia nilikubali bila kusita kwamba Serikali itaongeza hizo dola milioni 18 zinazohitajika. Niwahakikishie kuwa tutatoa fedha hizo ili ujenzi ukamilika kwa kiwango kilichotarajiwa.
Wageni waalikwa, Mabibi na Mabwana;
Ni mategeneo ya Serikali kuwa baada ya kukamilika kwa ujenzi wa Kampasi hii, Chuo Kikuu Cha Afya na Sayansi Shirikishi, Muhimbili kitakuwa na uwezo wa kuongeza udahili wa wanafunzi wa fani mbalimbali za afya kutoka takribani wanafunzi 3,000 na kufikia wanafunzi 15,000. Hii itapunguza kwa kaisi kikubwa, kama si kumaliza kabisa uhaba mkubwa wa wataalam wa fani za afya ulioko nchini kwa sasa. Aidha, ni mategemeo yangu pia kuwa wakati ujenzi utakapokamilika idadi ya wanafunzi wa shahada za uzamili na uzamivu itaongezeka kwa kiasi kikubwa na hivyo kuongeza idadi ya wataalamu waliobobea wa fani mbalimbali za afya.
Hitimisho
Wageni waalikwa, Mabibi na Mabwana;
Kwa kumalizia, napenda kuishukuru Serikali ya Jamhuri ya Korea Kusini kwa kutupatia mkopo wa ujenzi na vifaa vya hospitali hii. Mkopo uliotolewa ni mkopo wenye riba nafuu ambao kama usingepatikana ingebidi tutumie fedha iliyopangwa kwa ajili ya miradi mingine kwenye ujenzi wa hospitali hii. Napenda kuwashukuru wananchi wa maeneo ya Kwembe na Mloganzila kwa kutoa ushirikiano katika mradi huu. Mradi huu ni moja ya kielelezo cha mafanikio ya Muungano wetu wa Miaka 50, tuutunze utakapokamilika ili utufae kwa miaka 50 mingine. Nawatakieni kila la heri katika kusherehekea miaka 50 ya Muungano wetu.
Ahsanteni sana kwa kunisikiliza.

- Apr 28, 2014
HOTUBA YA RAIS WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA, MHE. DKT. JAKAYA MRISHO KIKWETE KWENYE UFUNGUZI WA KITUO CHA UPASUAJI WA MOYO NA MAFUNZO CHA HOSPITALI YA TAI...
Soma zaidiHotuba
Mwakilishi wa Rais wa Jamhuri ya Watu wa China, Mhe. Chen Changzhi,
Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii, Mhe. Dkt. Seif S. Rashid (Mb),
Katibu Mkuu, Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii, Bw. Charles Pallangyo,
Mhe. Balozi wa Serikali ya Watu wa China,
Waheshimiwa Mabalozi waliopo hapa,
Mwenyekiti na Wajumbe wa Bodi ya Wadhamini, Hospitali ya Taifa Muhimbili,
Viongozi Wenzangu;
Wafanyakazi wa Hospitali ya Muhimbili;
Wageni Waalikwa,
Mabibi na Mabwana,
Shukrani
Nakushukuru Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii kwa kunialika kuja kushiriki nanyi katika ufunguzi wa kituo hiki muhimu cha upasuaji wa moyo na mafunzo. Nafurahi kuwa Mheshimiwa Chen Changzhi, Naibu Spika wa Bunge la China amejumuika nasi katika hafla hii. Alikuja hapa kwa sherehe za miaka 50 ya Muungano akimwakilisha Rais wa China. Tukaona tutumie fursa hiyo pia tuzindue kituo hiki muhimu kilichojengwa kwa msaada wa Serikali ya China kugharamia sehemu kubwa ya gharama. Kituo hiki kimegharimu shilingi bilioni 26.6 kati ya hizo China imetoa shilingi bilioni 16.6 na Tanzania imetoa shilingi bilioni 10.
Kituo tunachokizindua leo ni kituo cha kisasa kabisa, chenye vifaa vya hali ya juu, vinavyotumia teknolojia ya kisasa katika uchunguzi na tiba ya magonjwa ya moyo. Kupatikana kwa kituo hiki, Tanzania inapiga hatua nyingine muhimu katika kuendeleza huduma ya afya nchini. Ni ukweli usiofichika kwamba maradhi ya moyo duniani yanaongezeka. Shirika la Afya Duniani (WHO) linakadiria kuwa kwa mwaka takribani watu milioni 12 wanakufa duniani kwa maradhi haya. Hapa nchini inasemekana wagonjwa wa maradhi haya wamekuwa wanaongezeka kwa asilimia 26 kwa mwaka. Maradhi haya yameanza kuwa tatizo kubwa hapa kwetu, hivyo hatuna budi kuchukua hatua thabiti kukabiliana nayo.
Kwa sababu ya kukosa uwezo wetu wa ndani, haswa kwa wagonjwa wanaohitaji upasuaji kuwekewa wa moyo, pacemakers au stents, tumelazimika kuwapeleka nje ya nchi kwa matibabu. Ni gharama kubwa, hivyo hatuwezi kuwapeleka watu wengi wanaohitaji tiba hiyo. Matokeo yake ni wagonjwa wengi kuishi kwa mateso na hata kupoteza maisha.
Kwa nia ya kutaka kuokoa maisha ya Watanzania waliopata maradhi ya moyo, ndipo tulipowaomba ndugu zetu wa China. Wakati ule Rais wa China, Mheshimiwa Hu Jintao alitukubalia. Jimbo la Shandong ambalo ndilo limekuwa linatoa madaktari wengi kutoka China, lilikabilidhiwa jukumu la ujenzi wa kituo hiki. Kama nilivyosema, kwa ushirikiiano wa pamoja wa nchi zetu, kituo kimekamilika na kimekwishaanza kutoa huduma.
Tunapofanya uzinduzi wa kituo hiki leo, ni fursa nzuri kuwashukuru marafiki zetu wa China. Tunawashukuru kwa msaada mkubwa waliotupatia na tunawashukuru kwa heshima ya Mjumbe mzito kwenye sherehe hii. Tunashukuru pia kwamba mgeni huyu pia amekuja kumwakilisha Rais wa China, Mheshimiwa Xi Jinping na watu wa China katika sherehe za maadhimisho ya miaka 50 ya Muungano.
Mheshimiwa Waziri;
Mkurugenzi Mkuu wa Hospitali ya Taifa ya Muhimbili na
Mkuu wa Taasisi Hii;
Kituo kimekamilika sasa kazi kwetu. Tunaomba muhakikishe kuwa kituo hiki kinatimiza majukumu yake kama ilivyokusudiwa. Kwa ajili hiyo, naomba mfanye yafuatayo:
- Hakikisheni vifaa na mahitaji ya upasuaji yanapatikana wakati wote. Itakuwa haina maana kujenga jengo zuri kama hili na kufundisha mabingwa wa upasuaji wa moyo kisha wasifanye kazi waliyosomea kufanya.
- MSD ielekezwe kuhakikisha kuwa vifaa na mahitaji hayo yanapatikana wakati wote.
- Wizara, Mkurugenzi Mkuu wa Hospitali ya Taifa Muhimbili na Mkuu wa Kituo hiki hakikisheni kuwa mnatoa kipaumbele cha kwanza kwa shughuli za upasuaji katika kituo hiki. Hii ina maana ya mgao wa fedha na mipango ya kazi ya kituo.
- Waziri na Mkurugenzi Mkuu anzeni kufikiria utaratibu bora wa uandeshaji wa kituo hiki. Angalieni uwezekano wa kufanya kituo hiki kuwa taasisi inayojiendesha chini ya Hospitali ya Taifa, Muhimbili. Nazungumzia mfumo unaokaribia kufanana na Taasisi ya Mifupa. Hii itaihakikishia kituo hiki ustawi na uhai endelevu.
- Jiepusheni na kishawishi cha kugeuza wodi za taasisi hii kuwa ni wodi za wagonjwa ambao ni watu mashuhuri na wenye uwezo. Ninachoshauri, tengenezeni mpango wa kujenga jengo kama hili kwa watu hao. Nachelea tusije kujikuta, wamejaa watu wengine, wagonjwa wa moyo wakakosa nafasi.
- Naomba uongozi wa Hospitali ya Taifa Muhimbili, uongozi wa kituo na wafanyakazi kukitunza kituo hiki kwa kiwango cha juu ili kidumu na kilifae taifa letu na watu wake kwa miaka mingi ijayo. Hakikisheni kunafanyika matengenezo kwa wakati. Msifanye ajizi kwani ukarabati husababishwa na kuchelewa kufanya matengenezo. Ukifanya matengenezo kwa wakati huhitaji ukarabati. “Rehabilitation is deferred maintenance”.
Hitimisho
Ndugu Wananchi;
Nimalize kwa kutoa tena shukrani zangu za dhati kwa Serikali ya Jamhuri ya Watu wa China, Rais mstaafu Mheshimiwa Hu Jintao na Rais Xi Jinping, Serikali ya Jimbo la Shandong na Kampuni ya Uhusiano wa Kiuchumi na Kiufundi ya Kimataifa ya Shandong kwa mchango wao uliowezesha ujenzi wa Kituo hiki. Wananchi wa Tanzania wanathamini na kuienzi zawadi hii kutoka kwa wananchi wa China kwa ajili yetu. Serikali ya Tanzania itahakikisha kwamba Kituo hiki kinaendelea kutoa huduma bora kwa wagonjwa kama inavyotarajiwa.
Baada ya kusema haya sasa naomba kutamka kuwa Kituo cha Upasuaji, Tiba na Mafunzo ya Moyo kimefunguliwa rasmi.

- Apr 15, 2014
SPEECH BY H.E. JAKAYA MRISHO KIKWETE, PRESIDENT OF THE UNITED REPUBLIC OF TANZANIA, DURING THE WORLD ECONOMIC FORUMS ALIGNMENT MEETING ON DEVELOPMENT OF CENT...
Soma zaidiHotuba
Hon. Dr. Harrison Mwakyembe, Minister for Transport, United Republic of Tanzania;
Hon. Prof. Silas Lwakabamba, Minister for Infrastructure, Republic of Rwanda;
Hon. Eng. Virginie CIZA, Minister for Transport, Public Works and Equipment, Republic of Burundi;
Hon. Justin Kalumba MWANA NGONGO, Minister for Transport and Water Ways, Democratic Republic of Congo;
Hon. Eng. Abraham Byandala, Minister for Transport and Works, Republic of Uganda;
Dr. Donald Kaberuka, President of the African Development Bank;
Dr. Richard Sezibera, Secretary General of the East African Community;
Dr. Stogomena Tax, Executive Secretary of SADC;
Dr. Ibrahim A. Mayaki, President, NEPAD Agency;
Mr. Philippe Dongier, World Bank Country Director for Tanzania, Uganda and Burundi;
Distinguished Guests;
Ladies and Gentlemen;
It is a pleasure for me to welcome you all to Tanzania and Dar es Salaam. I thank the organizers for affording this rare opportunity to speak at this all important World Economic Forum Alignment Meeting on Development of the Central Corridor.
This meeting could not have been organized at a better time, than this. As a matter of fact such people of this region have been waiting for this type of action for a long time. Besides that, this meeting is part of the preparations for the World Economic Forum for Africa meeting scheduled for 7th to 9th May, 2014. The work of this meeting will therefore have a special significance to the implementation of the Priority Action Plan of Programme for Infrastructure Development in Africa (PIDA) which has its roots from the World Economic Forum in Africa held in Addis-Ababa, from 9th to 11th May, 2012.
It is gratifying to see high level participation of four important institutions among us: the EAC, SADC the AfDB, the NEPAD Agency and the World Bank. It is heartwarming indeed, to have you with us because you are critical factor on the success of the agenda at hand. We look forward to your continued involvement until we reach the objectives of this initiative.
From WEF Addis Ababa to WEF Abuja: Private Sector and
African Infrastructure Development
Distinguished Delegates;
The 2012 World Economic Forum for Africa was a turning point with regard to how we approach the question of development of infrastructure in Africa. It came to our awareness and realization that we need to bring in Private Sector in infrastructure development in Africa. Such a perspective had not been embraced before by governments in Africa, with each one trying to shoulder the cost alone.
I commend the joint-initiative of the WEF, the AfDB, the AU Commission and NEPAD (New Partnership for Africa's Development) for taking forward the agenda. As a follow up, an African Strategic Infrastructure Initiative (ASII) was formally launched in Johannesburg on the 9th of July, 2012, with the formation of the Business Working Group (BWG), a platform for African infrastructure development strategies and initiatives.
I am pleased with the work of the Business Working Group for identifying projects with high potential for short-term acceleration. I am particularly delighted with the choice of the Central Corridor in this regard. I also thank you for affording my country the honour of preparing a Wider Concept Note on the development of the Central Corridor.
Importance of the Transport Corridors
Distinguished Delegates;
The importance of transport corridors as game changers for regional growth and development need not be over-emphasized. Studies after studies have concluded that many landlocked developing countries are among the poorest in the world. It is said, out of 31 such countries, 16 are classified as least developed and half of these are in Africa.
These countries are said to be penalized annually by 1.5 percent reduction in average growth compared to coastal states by simply being landlocked. It goes without saying that: growth of landlocked countries depends on the growth of the coastal countries. That implies the ability of the coastal countries to put in place infrastructure for trade facilitation, as a pre-requisite for development of the land locked countries.
Distinguished Delegates;
The coastal states have never fallen short of good will in facilitating the landlocked countries. They have been putting in place supportive infrastructure because they too, are primary and secondary beneficiaries of such infrastructure. It is the difficulties of raising financing of these infrastructures that has been holding back coastal states particularly the Least Developed Countries, from rising to challenge effectively.
Efforts to exploit joint regional financing mechanisms has also proven unsuccessful. Experience has shown that it is easier to arrange investment for national infrastructure than for regional ones. Our experience on the ongoing construction of 11,174 kilometers of road to tarmac level serves as a good lesson. It is for this reason that, we welcome this approach of partnering with the private sector for regional infrastructure development.
Status of Central Corridors
Distinguished Delegates;
The Central Corridor is located at the strategic geographical position which makes it a natural choice as a major trade route for countries of the Eastern and Central African regions. Indeed, for many decades the Dar-es-Salaam Port, Tanzania’s roads and railways have served the neighboring countries of Uganda, Rwanda, Burundi and the Democratic Republic of Congo (DRC).
Economies of countries served by this corridor have shown strong GDP growth rates of between 4 and 8 percent. Transit demand is forecasted to increase from 2.7 million to 9.8 million tons by 2030. The Dar es Salaam port captures 14 percent of imports and exports of these countries. As a result the throughput at the port has increased from 7.4 million tons in 2007 to 13 million tons by December 2013.
The Central Corridor also enjoys one of the best roads in East Africa. The Dar es Salaam-Rusumo/Kabanga and Dar es Salaam-Mutukula (at the borders of Rwanda/Burundi and Uganda respectively) are fully paved. The presence of these routes makes the Central Corridor a competitive option for cross border trade through the Port of Dar es Salaam.
Distinguished Delegates;
Rwanda and Burundi are connected to the Port of Dar es Salaam by the Central Corridor that consists of several routes. These routes include an all-road unimodal option from Dar es Salaam to Bujumbura and Kigali. Alternatively, cargo flows along the intermodal routes made up of rail from Dar es Salaam to Isaka then trans-shipped to Kigali and Bujumbura. Rwanda and Burundi are now working together with Tanzania to extend the central railway line from Isaka to Kigali on wards to Keza – Musongati in Burundi.
The Republic of Burundi has discovered enormous deposits of nickel. The corridor is about to transport more volumes of heavy minerals within the coming two to three years. Our neighbor Burundi may in the coming 2 or 3 years start exporting between 1.5 million tons to 3 million tons of nickel concentrates a year. In the same development, we expect two nickel mines in Tanzania (Kabanga and Dutwa) to be operational in the same time span. It is likely that nickel processing would require importation of huge volumes of sulphur per annum. All these volumes are expected to pass through the Central Corridor.
Challenges Facing Central Corridor
Distinguished Delegates;
Despite the great potentials and opportunities presented by the Central Corridor, all is not rosy in terms of both effectiveness and efficiency. Transport inefficiencies in this region, have contributed to prohibitively high transport costs, and impede the region's ambition to realize its overall vision for socio-economic development.
The design capacity of the Tanzania Railway Limited (TRL) line is to move traffic of about 5million tons per year. Unfortunately, this capacity has never been achieved as the maximum capacity reached so far is only 1.4 million tons of cargo moved by train as the performance record in 2002. While there are prospects of transit cargo to double up within the coming few years, as the region braces itself to start exporting millions of tons of copper and nickel a year, the existing 2,707 kilometers Central railway, cannot in its present condition cope with the growing volume of cargo along the central corridor.
Distinguished Delegates;
It suffices to say, both our roads and the central railway line lead to the Port of Dar es salaam needs a turn around. It needs refurbishing. We still need to expand our berth capacity, modernize our cargo handling facilities as well as procedure to cope with the growing volume of throughput. We have indeed embarked on the exercise, but in a limited way by using our yearly budgetary allocations and development partners' support. Thanks to the World Bank, the AfDB and JICA. Apart from the measures we have so far taken to enhance port efficiency, reliability and security. We thank to Trade Mark East Africa, DFID and the World Bank for the continued support to improve port efficiency.
Efforts Undertaken by Tanzania to Improve the
Central Corridors
Distinguished Delegates;
Tanzania has continued to fulfill her regional responsibility to our landlocked neighbors, and international obligations under the Almaty Programme of Action. There are number of efforts we have put in place which are short and long-term plans. Our short-term plan is to rehabilitate the railway line by reinforcing its formation, strengthening its bridges, removing lighter, old, worn out rails, fasteners, sleepers and installing new heavier rails, sleepers and ballast. We have so far done almost 600 kilometers. Thanks to the World Bank and JICA.
We have continued to make available our Dar es Salaam Port as an export and import gateway for the landlocked countries of Rwanda, Burundi, Uganda, Zambia, Malawi and the DRC. Some of the initiatives which are underway includes;
a) Dredging of the Dar es Salaam port entrance channel;
b) Construction of Berths 13 and 14;
c) Strengthening and deepening of Berths 1-7;
d) Development of the Roll on – Roll off (RO-RO) Berth at the Dar port;
e) Plan to develop Kisarawe Freight Station with intention to decongest container traffic at the Dar port and development of new port at Bagamoyo among others.
The government decided to give due weight to these initiatives through mainstreaming them in the Big Results Now (BRN) Port Initiatives, with the aim to ensure their timely implementation. We have earmarked to increase throughput of the Dar es Salaam Port from the current 13 million tons per annum to about 18 million tons annually by end of 2015. Furthermore, it is targeted to reduce time taken by a truck to transport a transit container from the Dar es Salaam Port to the borders of Burundi and Rwanda to 2½ days from the current 3½ days by the end of 2015.
Distinguished Delegates;
But these short-term measures will not enable us to service a growing regional economy effectively and efficiently. The Dar es Salaam Port for example, currently handles 13 million tons of freight per year but hardly 2 percent of the freight is carried on rails, the rest is transported by trucks, drastically shortening the lifespan of most of our paved roads.
It is against this background that we came up with a long-term plan or strategy to upgrade the central line to standard gauge. Part of the line i.e. Dar es Salaam – Isaka – Keza – Kigali/Gitega – Musongati (1,591 kilometers long), is a joint project by Tanzania, Rwanda and Burundi. It is estimated to cost us a minimum of USD 4.13 billion. We have jointly done all the preliminary studies. With the completion of the detailed study recently, we are now on procurement of Transaction Advisor. Thanks to the AfDB for its support.
Tanzania and Burundi have also a bilateral arrangement to construct a 200 kilometers standard gauge railway between Uvinza in Tanzania and Musongati in Burundi expected to cost us USD 550 million.
Private Sector and Central Corridor
Distinguished delegates;
The central corridor projects I have briefly narrated cannot be successfully implemented within the context of the traditional method of financing infrastructure development. Government financing alone may not easily raise all the money required. We do not have the money nor can we easily get someone to lend us so much money. We have tried this option over the years without much success.
It is time we encouraged further private sector participation. It remains an alternative and viable option to minimize the public financing gap in infrastructure development. I have vested my hopes in this meeting which I believe will take us to the next level in terms of unlocking private sector funding, identifying cross-border regulation gaps and building private-public sector confidence.
Distinguished Delegates;
It is befitting that this alignment meeting is taking place at this point in time. We have undertaken to put in place conducive environment to facilitate private sector to join our efforts. The government has put in place the National Public-Private Partnership (PPP) Policy in 2009, in 2010 we enacted the Public-Private Partnership Act, Cap 403 and Regulations in 2011. In addition, feasibility studies have been undertaken while various identified PPP projects have been advertized for private sector to show interest. We will continue to work together with our Central Corridor member states in soliciting funds to invest in the key transport infrastructure projects along the corridor.
The Government, in partnership with the OECD and NEPAD, undertook a review of its investment policies to support the national strategy for economic reform and improve the business climate to attract more investment in key sectors, such as infrastructure and agriculture. The review was launched on 31st January, 2014 and will be used to update all investment policies; and continue with implementation of Government Roadmap on the Improvement of the Investment Climate by undertaking administrative measures with very limited cost implications while reducing hurdles of significant costs to local and foreign investors. These measures go along with automated and electronic payment systems that minimize human interference and discretionary powers.
Way Forward
Distinguished Delegates;
I am optimistic that the groundwork we have undertaken as a region for the implementation of the Central Corridor Infrastructure projects through public private sector cooperation have caught the attention of the international business community. I thank the WEF in collaboration with the AfDB, the AU Commission and NEPAD for championing this noble cause for Africa's economic development. As corridor member states with a lot to gain from improved inter and intra-regional trade, let us continue to plan, discuss, decide and implement together our infrastructure development projects. Our numbers would always attract the attention of serious investors.
Conclusion
Distinguished Delegates;
I am optimistic that our regional efforts to implement the Central Corridor Infrastructure projects through public private partnership is now at a point of take-off and definitely will bear good results in the very near future. We believe that WEF strategies under this new model of Central Corridor to be the African pilot project for accelerating investments will support the current potential infrastructure projects along the corridor to secure strategic investors soon. What I wish to share with our colleagues from the Corridor member states is to continue working together under these efforts so as to achieve the expected regional investment goals. Everything is possible if we plan, discuss, decide and implement together.
This is the opportunity for our governments to interact with other stakeholders including the private sector, with a view to coming up with a programme of action for the development of the central transport corridor.
To conclude my remarks, I have taken note of the fact that you have a rather long and demanding agenda in front of you and, for that reason, I wouldn't like to keep you any longer than necessary. It is therefore my singular honour and pleasure to wish you a very fruitful meeting and to declare that the Alignment meeting on the Central Corridor is now opened.

- Mar 21, 2014
HOTUBA YA RAIS WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA, MHESHIMIWA JAKAYA MRISHO KIKWETE, WAKATI WA KULIHUTUBIA BUNGE MAALUM LA KATIBA, TAREHE 21 MACHI, 2014, DODOM...
Soma zaidiHotuba
Mheshimiwa Samuel Sitta, Mwenyekiti wa Bunge Maalum la Katiba;
Mheshimiwa Dkt. Mohamed Gharib Bilal, Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania;
Mheshimiwa Dkt. Ali Mohamed Shein, Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi;
Mheshimiwa Mizengo Peter Pinda, Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania;
Mheshimiwa Maalim Seif Sharif Hamad, Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar;
Mheshimiwa Balozi Seif Ali Iddi, Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar
Mheshimiwa Anne Semamba Makinda; Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano;
Mheshimiwa Pandu Ameir Kificho, Spika wa Baraza la Wawakilishi na Mwenyekiti wa Muda wa Bunge Maalum la Katiba ;
Mheshimiwa Rashid Othman Chande, Jaji Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania;
Mheshimiwa Othman Makungu, Jaji Mkuu wa Zanzibar;
Viongozi Wakuu Wastaafu;
Waheshimiwa Wajumbe wa Bunge Maalum la Katiba;
Waheshimiwa Wajumbe wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba;
Wageni waalikwa;
Mabibi na Mabwana;
Pongezi
Nakushukuru sana Mheshimiwa Mwenyekiti kwa kunipa fursa ya kuja kuzungumza na Waheshimiwa Wajumbe wa Bunge letu Maalum la Katiba katika siku hii muhimu na ya kihistoria kwa nchi yetu. Nimekuja kuwatakia heri na naungana na Watanzania wenzetu wote kuwaombea baraka za Mwenyezi Mungu, ili muweze kuifanya kazi yenu kwa utulivu, hekima, umakini mkubwa na kuimaliza kwa salama na kwa mafanikio yanayoyatarajiwa na Watanzania.
Natoa pongezi nyingi kwako na kwa Makamu wako kwa kuchaguliwa kwenu kuongoza Bunge hili maalumu na la kihistoria. Ushindi mkubwa mliopata ni kielelezo tosha cha imani kubwa na matumaini waliyonayo Wajumbe wenzenu kwenu. Matumaini yao ndiyo matumaini ya Watanzania wote, kwamba mtaliongoza vizuri Bunge hili, ili liweze kutimiza kwa ufanisi mkubwa jukumu lake muhimu sana katika historia ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Mheshimiwa Mwenyekiti;
Niruhusu pia niwapongeze kwa dhati Wajumbe wote wa Bunge Maalum la Katiba kwa bahati ya aina yake waliyopata ya kutunga Katiba mpya ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Fursa hii hutokea mara chache sana katika historia ya nchi yo yote na watu wake. Mkifanikiwa kuipatia nchi yetu Katiba nzuri majina yenu yataandikwa kwa wino wa dhahabu, katika kumbukumbu za historia ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Ni matarajio ya Watanzania kuwa mtatunga Katiba itakayokubalika na wengi. Katiba inayotekelezeka. Katiba itakayoimarisha Muungano wetu kwa kuondoa changamoto zilizopo sasa. Katiba itakayoipa nchi yetu mfumo bora wa kuongoza na kuendesha mambo yetu. Katiba itakayoimarisha umoja, upendo, ushirikiano na mshikamano miongoni mwa wananchi wa Tanzania, licha ya tofauti zao za asili za upande wa Muungano na maeneo watokako, au tofauti za jinsia, rangi, kabila, dini na ufuasi wa vyama vya siasa. Katiba itakayodumisha amani, usalama na utulivu nchini. Katiba itakayostawisha zaidi demokrasia, haki za binadamu, utawala wa sheria, utawala bora na kudhibiti maovu.
Na, mwisho ingawaje siyo mwisho kwa umuhimu, Katiba itakayoweka mazingira mazuri kwa uchumi wa nchi kukua, na wananchi wengi kunufaika sawia na maendeleo yatayopatikana.
Historia ya Katiba Nchini
Mheshimiwa Mwenyekiti na Waheshimiwa Wajumbe;
Hii itakuwa mara ya tatu tangu kuzaliwa kwa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Aprili 26, 1964, kwa nchi yetu kuwa na mchakato wa kutunga Katiba mpya. Mara ya kwanza ilikuwa mwaka 1965 ilipotungwa Katiba ya Muda na mara ya pili ni mwaka 1977 ilipotungwa Katiba ya Kudumu tuliyonao sasa. Tofauti na mara mbili zilizopita, safari hii mchakato unahusisha watu wengi zaidi. Wananchi wameshiriki moja kwa moja kutoa maoni yao kwa Tume ya Mabadiliko ya Katiba, na ndio watakaofanya uamuzi wa mwisho kuhusu Katiba mpya kwa kura ya maoni. Wananchi pia walipata nafasi ya kuchagua Wajumbe wa Mabaraza ya Katiba ya Wilaya yaliyojadili Rasimu ya Kwanza ya Katiba. Pia walipata nafasi ya kutoa maoni yao kupitia Mabaraza ya Katiba ya taasisi. Katika Bunge hili wapo wananchi 201 kutoka makundi mbalimbali.
Katika mchakato wa kutunga Katiba za mwaka 1965 na 1977 kulikuwapo Tume za Kuandaa Rasimu na Bunge Maalum la Katiba kama ilivyo katika mchakato huu. Hata hivyo, kwa Katiba zilizopita Wabunge wa Bunge la Jamhuri ya Muungano pekee ndio waliounda Bunge Maalum. Safari hii Bunge Maalum linajumuisha Wabunge, Wajumbe wa Baraza la Wawakilishi na wananchi 201 wanaotoka kwenye jamii, wakiwakilisha asasi na makundi mbalimbali ya Watanzania kutoka Zanzibar na Tanzania Bara. Mchakato wa sasa utaishia kwenye kura ya maoni itakayoshirikisha wananchi wote wa Tanzania wanaoruhusiwa kupiga kura. Michakato iliyopita iliishia Bunge Maalum pekee.
Mheshimiwa Mwenyekiti;
Tangu kutungwa kwake, tarehe 25 Aprili, 1977, mpaka sasa Katiba ya Jamhuri ya Muungano ya mwaka 1977 imefanyiwa mabadiliko takriban mara 14. Mabadiliko hayo yalitokana na kufanyika au kutokea kwa mabadiliko muhimu ya kiuchumi, kisiasa na kijamii katika nyakati mbalimbali hapa nchini na katika Jumuiya ya Afrika Mashariki.
Kwa ruksa yako naomba nitaje baadhi ya mabadiliko yaliyofanywa:-
- Mabadiliko ya 1979 yaliunda Mahakama ya Rufani ya Tanzania kufuatia kufa kwa Mahakama ya Rufani ya Afrika Mashariki baada ya kuvunjika kwa Jumuiya ya Afrika Mashariki mwaka 1977.
- Mabadiliko ya mwaka 1980 yalifanyika baada ya kutungwa kwa Katiba ya Zanzibar, hivyo kulazimu Katiba hiyo kutambulika kwenye Katiba ya Jamhuri ya Muungano.
- Mabadiliko ya mwaka 1984 yaliweka utaratibu wa ukomo wa vipindi vya Urais ambao haukuwepo kabla ya hapo. Aidha, masuala ya Haki za Binadamu (Bill of Rights) yaliingizwa kwa mara ya kwanza katika Katiba. Vilevile, Mahakama ya Rufani ya Tanzania na mambo mengine ya iliyokuwa Jumuiya ya Afrika Mashariki yaliongezwa katika Orodha ya Mambo ya Muungano.
- Mwaka 1992, yalifanyika mabadiliko yaliyoanzisha Mfumo wa Vyama Vingi vya Siasa badala ya ule wa Chama kimoja uliokuwepo tangu 1965. Pia utaratibu wa uchaguzi wa Rais na Wabunge ulirekebishwa ili uendane na mfumo wa vyama vingi vya siasa. Vilevile utaratibu wa kuwa na viti maalum vya wanawake katika Bunge ulianzishwa. Wakati ule ilikuwa asilimia 15 ya Wabunge wote. Aidha, kwa mara ya kwanza katika historia ya nchi yetu Bunge lilipewa mamlaka ya kumwajibisha Rais na Waziri Mkuu kupitia kura ya kutokuwa na imani.
- Mabadiliko ya mwaka 1994 yaliweka mfumo mpya wa kumpata Makamu wa Rais kupitia Mgombea Mwenza.
- Mwaka 2000 na 2005, pamoja na mambo mengine yalifanyika mabadiliko yaliyopanua wigo wa Haki za Binadamu na kuongeza uwakilishi wa wanawake.
Umuhimu wa Mabadiliko ya Katiba
Mheshimiwa Mwenyekiti;
Kufanyika kwa mabadiliko hayo kunathibitisha utayari wa Serikali kufanya mabadiliko kila ilipoonekana inafaa kufanya hivyo. Pamoja na kufanya yote hayo na Serikali kuwa na msimamo huo, kumekuwepo na madai yaliyokuwa yanajirudia ya kutaka Katiba ya Tanzania iandikwe upya. Wako watu walioimithilisha Katiba yetu na nguo yenye viraka vingi mno kiasi kwamba ingefaa kununua mpya badala ya kuendelea kuivaa.
Madai ya kutaka Katiba mpya yalipazwa sauti baada ya kuanza kwa mfumo wa vyama vingi vya siasa. Wapo waliokuwa wanadai Katiba mpya kwa imani, eti kwamba, itawawezesha kuishinda CCM. Lakini, si hayo tu, hata katika mchakato wa Serikali zetu mbili kushughulikia kero za Muungano, imedhihirika kuwa baadhi ya changamoto zilikuwa zinahitaji mabadiliko ya Katiba ili kuzipatia ufumbuzi wa uhakika na wa kudumu.
Mheshimiwa Mwenyekiti;
Kwa kutambua ukweli huo na baada ya kushauriana na kukubaliana na viongozi wenzangu wakuu wa Chama tawala na Serikali zetu mbili wakati ule, ndipo tarehe 31 Desemba, 2010, nikatangaza dhamira ya kuanzisha mchakato wa kutunga Katiba mpya. Nilieleza siku ile kuwa katika mchakato huo tutakuwa na ushirikishwaji mpana wa wananchi wa Tanzania kwa makundi yao ya jinsia, dini, siasa na shughuli wazifanyazo kujipatia riziki na kwa maeneo wanayotoka katika pande zetu mbili za Muungano.
Mchakato wa Katiba Mpya
Mheshimiwa Mwenyekiti;
Tarehe 16 Machi, 2011 Baraza la Mawaziri liliridhia kutungwa kwa Sheria ya Mabadiliko ya Katiba ya kuliongoza taifa katika mchakato wa kutunga Katiba mpya ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Tarehe 18 Novemba, 2011 Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania lilipitisha Muswada wa Sheria ya Mabadiliko ya Katiba. Kwa mujibu wa Sheria hiyo, mchakato wa kutunga Katiba Mpya ulikuwa unaanza kwa kuunda Tume ya Mabadiliko ya Katiba. Tume hiyo imepewa jukumu la kusikiliza maoni ya wananchi mmoja mmoja na kwa makundi yao ya maslahi, taasisi zao na kupitia Mabaraza ya Katiba. Mwishowe Tume imetakiwa kutengeneza Rasimu ya Katiba mpya itakayofikishwa kwenye Bunge Maalum la Katiba kujadiliwa na Katiba mpya kutungwa. Mchakato wa Katiba utahitimishwa kwa wananchi kupiga kura ya maoni ya kuamua kama wanaikubali au kuikataa Katiba mpya.
Tarehe 6 Aprili, 2012 nilifanya uteuzi wa Wajumbe wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba na kuwaapisha tarehe 13 Aprili, 2012. Tume ilianza kazi tarehe 2 Mei, 2012 na kuikamilisha kwa mafanikio, hatua zote zilizoihusu na kukabidhi kwangu na kwa Rais wa Zanzibar, Taarifa ya Tume na Rasimu ya Katiba tarehe 30 Desemba, 2013. Kitendo cha Mwenyekiti wa Tume, Mheshimiwa Joseph Warioba kuwasilisha Rasimu hiyo mbele ya Bunge hili tukufu tarehe 18 Machi, 2014, kinahitimisha rasmi kazi ya Tume ya Mabadiliko ya Katiba. Kazi inayofuatia ni ya Bunge hili kujadili, kuamua na kutunga Katiba mpya. Baada ya hapo Katiba mpya itafikishwa kwa wananchi kwa uamuzi wa mwisho kwa njia ya kupiga kura ya NDIYO au HAPANA.
Mheshimiwa Mwenyekiti;
Rasimu ya Katiba ilichapishwa kwenye gazeti la Serikali na magazeti mengine yanayosomwa na wananchi kama ilivyoagizwa katika Kifungu cha 20(2) cha Sheria ya Mabadiliko ya Katiba. Pamoja na hayo, Taarifa ya Tume na Rasimu ya Katiba viliwekwa wazi kwenye tovuti ya Tume kwa kila mtu kusoma. Inafurahisha kuona kuwa watu wengi wameisoma Taarifa ya Tume na Rasimu ya Katiba na kumekuwa na mjadala mpana kuhusu nyaraka zote hizo muhimu. Watu wengi wametoa maoni yao na wanaendelea kufanya hivyo. Kwa maoni yangu hili ni jambo jema sana na ni kielelezo thabiti kuwa demokrasia imestawi na inazidi kuota mizizi Tanzania. Pia, kwamba, Watanzania wako huru kushiriki na kutoa maoni yao kwa mambo yanayowahusu.
Pongezi kwa Tume
Mheshimiwa Mwenyekiti;
Kwa mara nyingine tena narudia kutoa pongezi za dhati kwa Wajumbe wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba chini ya uongozi wa Mheshimiwa Jaji Joseph Warioba akisaidiwa na Mheshimiwa Jaji Augustino Ramadhani, kwa kazi kubwa na nzuri waliyofanya. Kazi yao haikuwa rahisi hasa ukizingatia ukubwa wa nchi yetu, wingi wa watu wake, utitiri wa taasisi na pigo la kumpoteza Mjumbe mwenzao muhimu Dkt. Sengondo Mvungi aliyetangulia mbele ya haki katikati ya mchakato.
Pamoja na hayo, kwa bidii kubwa Wajumbe wa Tume wameweza kutembelea mikoa yote nchini na kuwafikia watu 351,644 waliotoa maoni yao kwa mdomo na kwa maandishi. Halikadhalika, walipokea na kuchambua maoni 772,211 kutoka kwa wananchi na taasisi mbalimbali. Baada ya kupokea maoni ya wananchi, kufanya utafiti na kwa kutumia maarifa na uzoefu wao, Wajumbe wakafanya kazi ngumu, kuliko yote, ya kutengeneza Rasimu ya Katiba iliyoko mbele ya Bunge hili. Ni kweli kwamba Wajumbe hawakuweza kuwafikia wananchi wote wa Tanzania, lakini wameweza kuwafikia wananchi wengi, ambao kwa kiasi kikubwa wanawakilisha taswira na mitazamo mipana ya jamii yetu.
Baadhi ya Masuala Yaliyojitokeza Katika Mjadala wa Mapendekezo ya Tume
Mheshimiwa Mwenyekiti;
Tume imefanya kazi nzuri, yenye thamani kubwa na ya manufaa kwa taifa la Tanzania. Rasimu imeandikwa vizuri na kwa weledi wa hali juu. Tume imetoa mapendekezo ambayo kwa kiasi kikubwa yanahuisha na kuboresha Katiba ya nchi yetu, kwa namna ya pekee. Katiba inayopendekezwa, imejumuisha dhana na mambo kadhaa mapya yanayokwenda vyema na wakati tulionao na kuweka msingi mzuri kwa huko mbele tuendako. Kwa taratibu za kawaida za marekebisho ya Katiba tuliyonayo, isingekuwa rahisi kuingiza mambo mengi mapya kiasi hiki.
Wajumbe Wana Kazi Kubwa
Mheshimiwa Mwenyekiti;
Waheshimiwa Wajumbe;
Rasimu ya Katiba ni kitabu kikubwa kilichosheheni mambo mengi. Kina kurasa 106, sura 17 na ibara 271. Wajumbe wa Bunge hili mnatakiwa kusoma na kuelewa vizuri kila kilichoandikwa ili muweze kufanya uamuzi ulio sahihi. Mnawajibika kuchambua kwa kina na umakini mkubwa kila kilichomo, sura kwa sura, ibara kwa ibara, sentensi kwa sentensi na hata neno kwa neno. Hamna budi kujiridhisha kuhusu uandishi wa vifungu vya Rasimu ya Katiba na kufaa kwa dhana mbalimbali zilizoingizwa na kujengeka katika Rasimu.
Mheshimiwa Mwenyekiti;
Kile ambacho Wajumbe mtaona kinastahili kuboreshwa au kurekebishwa au kufutwa msisite kufanya hivyo ili Watanzania wapate Katiba iliyo bora. Msipofanya hivyo kuna hatari ya kupata Katiba ambayo ni ngumu kuitekeleza. Aidha, tunaweza kuwa na Katiba ambayo itanung’unikiwa na watu wengi na kusababisha madai ya kutaka ifanyiwe marekebisho muda mfupi baada ya kupitishwa. Bunge hili linao wajibu maalum wa kuzuia balaa hilo lisitokee katika nchi yetu. Ngazi mbalimbali zilizowekwa katika mchakato huu ni kama chujio la kuepusha hali hiyo isitokee. Kile ambacho hakikuonekana katika hatua moja kitaonekana katika hatua inayofuata na kurekebishwa. Nawaomba fursa mliyonayo muitumie vizuri.
Mheshimiwa Mwenyekiti;
Nimekwishaeleza kuwa moja ya jambo mnalotegemewa kufanya ninyi wenzetu mliopewa dhamana ya kutunga Katiba ya nchi yetu ni kujiridhisha na uandishi wake. Yapo maoni yaliyotolewa kuhusu uandishi ambayo naomba myatafakari na kuamua ipasavyo. Kwa mfano, kuna baadhi ya vifungu vya Katiba vinayopendekezwa vimekuwa na mambo mengi mno kuliko inavyostahili Katiba kuwa (too prescriptive). Pia kuna mawazo kwamba baadhi ya mambo hayangetakiwa kuwa katika Katiba bali yawe kwenye Sheria zinazotafsiri utekelezaji wa Katiba yenyewe.
Yako mambo yaliyotajwa kwenye Katiba ambayo yanatakiwa kuelezwa wazi kuwa mtu hatakwenda mahakamani kuidai Serikali impatie (non justiciable). Mambo yaliyotajwa kwenye Katiba ni mazuri na yanavutia, lakini lazima yaendane na uwezo wa nchi na uchumi wake kuhimili. Simaanishi kwamba tuyatoe kwenye Katiba, bali yabakie kama dhamira pale uwezo wa nchi utakaporuhusu yatekelezwe. Tusipofanya hivyo, kuna hatari ya Serikali kujikuta inalaumiwa au hata kufikishwa mahakamani kila wakati kwa madai ya jambo moja au jingine ambayo haina uwezo nayo. Ni muhimu sana mambo kama hayo muyatazame ili tusije kuwa na Katiba ambayo ni ngumu kutekeleza.
Mheshimiwa Mwenyekiti;
Yapo pia maoni kuwa baadhi ya vifungu vina upungufu katika uandishi wake, hivyo kuhitaji kufanyiwa marekebisho. Isipofanyika hivyo kunaweza kuwepo athari na nyingine zinaweza kuwa mbaya. Kwa mfano, Ibara ya 2 ya Rasimu inayotambulisha eneo na mipaka ya nchi yetu. Ibara hiyo inasomeka kuwa “Eneo la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ni eneo lote la Tanganyika likijumuisha sehemu yake ya bahari na eneo lote la Zanzibar likijumuisha sehemu yake ya bahari”.
Maelezo hayo yameacha kutambua, kwa upande wa Tanzania Bara, sehemu yetu ya maziwa na mito ambayo ni kubwa sana. Kwa nini tuache kuitaja? Je hatutoi nafasi kwa nchi tunazopakana nazo siku moja wakaja kupora sehemu zetu hizo na sisi kukosa utetezi kwa kuwa hata Katiba yetu haikuyatambua maeneo hayo kuwa ni yetu? Hili ni jambo kubwa ambalo Bunge hili lazima mlirekebishe. Wakati ndiyo huu hakuna mwingine.
Mheshimiwa Mwenyekiti;
Jambo jingine kuhusu uandishi ni mgongano kati ya pendekezo la msingi la Tume la kuwa na muundo wa Serikali tatu na majukumu ya Serikali ya Muungano ambayo kimsingi ni majukumu ya Serikali za nchi washirika. Katika Rasimu hii malengo ya taifa yameainishwa na Serikali ya Muungano inatakiwa kuhakikisha kuwa malengo hayo yanatekelezwa na itoe taarifa Bungeni. Katika mfumo wa Serikali tatu unaopendekezwa na Tume masuala yahusuyo uchumi na maendeleo ya jamii kama vile kukuza kilimo, ufugaji, uvuvi, viwanda, biashara, pembejeo, elimu, hifadhi ya jamii na kadhalika yako chini ya mamlaka ya Serikali za nchi washirika. Mamlaka ya Serikali ya Muungano ni kwa mambo saba tu yafuatayo:- Katiba na Mamlaka ya Jamhuri ya Muungano, Ulinzi na Usalama wa Jamhuri ya Muungano, Uraia na Uhamiaji, Sarafu na Benki Kuu, Mambo ya Nje, Usajili wa Vyama vya Siasa, Ushuru wa Bidhaa na Mapato yasiyo ya kodi yatokanayo na Mambo ya Muungano.
Kwa Rasimu kupendekeza muundo wa Serikali tatu na kuipa Serikali ya Muungano majukumu ambayo haina mamlaka nayo, ni kuzusha utata na migongano kati ya Serikali ya Muungano na nchi washirika. Mkichagua mfumo wa Serikali tatu, inawalazimu muyaondoe mambo hayo kwani Serikali ya Muungano haistahili kuyatekeleza na wala haina uwezo wa kuweka masharti kwa Serikali za nchi washirika kwa mambo yaliyo kwenye mamlaka ya nchi hizo. Lakini kama mtaamua tuendelee na muundo wa Serikali mbili, mambo haya mazuri yanatekelezeka na Serikali ya Muungano bila ya matatizo. Katika uandishi wa Rasimu Utumishi katika Serikali ya Muungano haumo katika Orodha ya Mambo ya Muungano. Ni lazima liwemo. Hayo ni baadhi tu ya masuala yahusuyo uandishi katika Rasimu. Naamini mkiisoma Rasimu kwa makini mnaweza kuyagundua mengineyo.
Dhana Mpya
Mheshimiwa Mwenyekiti;
Katika Rasimu kuna dhana mpya na mambo mapya kadhaa yaliyoingizwa ambayo yanabadili utaratibu wa sasa wa uendeshaji wa nchi na mambo mbalimbali. Nawaomba mfanye uchambuzi wa kina kwa kila kinachopendekezwa na kujiridhisha kuhusu kufaa kwake na manufaa yake. Fanyeni hivyo ili tujihakikishie kuwepo kwa mambo mazuri na uendeshaji mzuri wa shughuli katika taifa letu changa.
Mambo ni mengi na kwa ufinyu wa muda sitaweza kuyazungumzia yote. Niruhusuni nizungumzie baadhi ya dhana na mambo mapya yaliyomo katika Rasimu. Jambo la kwanza, kwa mfano, linahusu Ibara ya 128 (2)(d) inayoleta dhana ya “Mbunge kupoteza Ubunge iwapo atashindwa kufanya kazi za Mbunge kwa miezi sita mfululizo kutokana na maradhi au kizuizi ndani ya gereza”.
Watu hawana tatizo na Mbunge kuwa kizuizini ndani ya gereza kama amepatikana na hatia Mahakamani na kuhukumiwa kifungo. Lakini, isijekuwa yuko rumande kwa tuhuma akisubiri kesi kusikilizwa. Je akija kuonekana hana hatia na kuachiliwa? Naungana na wale wanaoshauri kuwa jambo hili lifafanuliwe vizuri na kutambua Mbunge kutiwa hatiani na kupata adhabu ya kifungo cha kipindi hicho. Ni bora ifanyike hivyo sasa ili kuondoa mikanganyiko. Hakuna haja ya kusubiri mpaka jambo hili lije kufafanuliwa baadaye kwa Sheria itakayotungwa na Bunge.
Mheshimiwa Mwenyekiti;
Kwa upande wa mtu kupoteza Ubunge kwa sababu ya “kuugua kwa miezi sita mfululizo” ni maoni ya watu wengi kuwa huu ni ukatili ambao haustahili kufanywa na Katiba. Kuugua ndiyo ubinadamu na wakati mwingine Mbunge anaweza kupata ajali akiwatumikia wananchi wa Jimbo lake. Anaweza kuugua kwa miezi sita au zaidi na kupona kabla ya kipindi chake cha Ubunge kufika mwisho. Kwa nini awekewe ukomo wa miezi sita? Katiba ya mwaka 1977 tunayotumia sasa haina sharti hilo. Watu wanauliza hoja na haja ya kuwa na sharti hili kwenye Katiba mpya ni ipi? Wanasema kwa kweli anachostahili Mbunge huyu kufanyiwa ni kuuguzwa afya yake iimarike ili aendelee kutumikia watu wake, na siyo kupoteza uongozi wake. Tusiwatie watu kishawishi cha kukatiza matibabu ili kukwepa sharti hilo. Ni vyema jambo hili mkalitazama kwa makini, na muone kama linastahili kuwepo au hapana.
Mheshimiwa Mwenyekiti;
Katika Rasimu hii imeingizwa dhana mpya ya kuweka ukomo wa vipindi vitatu kwa Wabunge. Tena mapendekezo haya hayasemi vipindi vitatu mfululizo au la!. Jambo hilo limezua mjadala motomoto katika jamii. Ni vizuri mkajiridhisha juu ya sababu za msingi na manufaa ya kufanya hivyo hapa Tanzania. Mazoea yetu na ya kwingineko duniani ni kuweka ukomo kwa Wakuu wa Nchi kwa sababu nzuri na rahisi kuzielezea. Lakini, kuwawekea ukomo Wabunge ni jambo jipya na huenda Tanzania tukawa wa kwanza. Nashawishika kuungana na wale wanaopendekeza kuwa pengine ni mapema mno kuanzisha utaratibu huo hapa kwetu.
Nachelea kuwa tutainyima nchi yetu fursa ya kupata watu wenye maarifa na uzoefu mzuri wa uongozi kwa nafasi ya Ubunge au kwa nafasi za uongozi wa Taifa bila ya sababu za msingi.
Mheshimiwa Mwenyekiti;
Jambo lingine jipya linalopendekezwa na Tume ni utaratibu wa kumuondoa Mbunge katikati ya kipindi chake cha uongozi. Kwa hoja linaonekana kuwa jambo jema lakini naomba athari zake mzitafakari vizuri. Kuna hatari ya kuanzisha misuguano kwenye Majimbo na kuwaacha Wabunge wasifanye kazi zao kwa utulivu bali wawe wanajihami dhidi ya wapinzani wao kuwatengenezea fitna za kuwatoa. Utaratibu unaopendekezwa wa Chama chake kujaza nafasi ya Mbunge inapokuwa wazi katika mazingira hayo nao unaweza kuwa ndicho kichocheo kikubwa cha vuguvugu la kumuondoa Mbunge. Walioshindwa kwenye kura ya maoni wanaweza kufanya kazi ya kuwachimba wenzao mpaka waondoke. Jipeni muda wa kupima faida na hasa thamani inayoongezwa na kuanzisha utaratibu huo. Naomba tujiridhishe kama jambo hili jipya lina tija. Hivi kupewa nafasi kila miaka mitano kurudi kwa wananchi hakutoshi kumuondoa Mbunge ambaye watu wamemchoka?
Muundo wa Muungano
Mheshimiwa Mwenyekiti;
Jambo lingine kubwa lililopendekezwa na Tume ambalo limevuta hisia za karibu watu wote nchini linahusu muundo wa Muungano wetu kuwa wa Serikali tatu badala ya mbili za sasa. Pendekezo hili limezua mjadala mkubwa tangu lilipotolewa katika Rasimu ya kwanza na kurudiwa katika Rasimu ya pili. Wakati mwingine mjadala umekuwa mkali na wa hisia kali kwa kila upande.
Kwa kweli hili ndilo jambo kubwa kuliko yote katika Rasimu kwa sababu linapendekeza kuanzishwa kwa muundo na mfumo mpya wa kuendesha nchi yetu. Hii ndiyo agenda mama ya Bunge hili ambayo kila Mtanzania anasubiri kwa hamu uamuzi wenu utakuwa upi. Ombi langu kwenu ni kuwa watulivu mnapojadili suala hili. Epukeni jazba ili mfanye uamuzi ulio sahihi. Lazima mtambue uamuzi usiokuwa sahihi kwa jambo hili una hasara kubwa. Tunaweza kupoteza kitu tulichokijenga kwa gharama kubwa kwa nusu karne iliyopita. Tanzania inaweza kuwa nchi iliyojaa migogoro na matatizo mengi ambayo hatunayo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Waheshimiwa Wajumbe;
Kama alivyoeleza Mwenyekiti wa Tume Mheshimiwa Jaji Joseph Sinde Warioba, mara kadhaa, mjadala au madai ya kutaka muundo wa Serikali tatu si jambo jipya. Ulikuwepo hata wakati wa mazungumzo ya kuunganisha nchi zetu mbili mwaka 1964. Ulikuwa kiini cha kuchafuka kwa hali ya hewa ya kisiasa Zanzibar mwaka 1984. Muundo huu uliwahi kupendekezwa na Tume ya Nyalali mwaka 1992, ndiyo hoja ya G55 mwaka 1993 na umependekezwa pia na Tume ya Jaji Kisanga ya mwaka 1998. Lakini mara zote hizo mapendekezo hayo hayakukubaliwa.
Waasisi wa taifa letu, yaani Mwalimu Julius Nyerere, aliyekuwa Rais wa Jamhuri ya Tanganyika wakati ule na Sheikh Abeid Amani Karume, aliyekuwa Rais wa Jamhuri ya Watu wa Zanzibar wakati ule, waliamua kuchagua Muungano wa Serikali mbili tulionao sasa. Walitoa sababu mbili kuu: “ni muundo unaoihakikishia Zanzibar kuwa haimezwi na Tanganyika; na pia unaiepusha Tanganyika kubeba mzigo mkubwa wa kugharamia Serikali ya Tanganyika na ile ya Muungano”.
Mheshimiwa Mwenyekiti;
Natambua kuwepo kwa rai ya kutaka Mwalimu Nyerere asitumiwe katika mjadala huu. Nionavyo mimi ni vigumu kuacha kujadili fikra za Mwalimu Nyerere na Sheikh Karume katika jambo hili. Wao ndiyo wa mwanzo kujadili na kukubaliana kuwa mfumo wa Serikali mbili ndiyo bora kwa nchi yetu. Iweje leo tunapozungumzia kuubadili, mawazo yao yawe hayafai kutumika au hata kuzungumzwa. Hivi hasa mawazo ya nani pekee ndiyo bora zaidi kutumika? Tutakuwa hatuutendei haki mjadala huu na sisi wenyewe tunaoshiriki katika mchakato huu. Rai yangu kwenu ni kuwa mzitazame hoja zote kwa marefu na mapana yake ili mpime kama zipo sababu za kuubadili muundo wa sasa wa Muungano wa Serikali mbili na kuleta wa Serikali tatu. Na, kama zipo mabadiliko hayo yaweje! Lazima mfanye uamuzi kwa utambuzi na hoja zenye mashiko. (you must make an informed decision).
Mheshimiwa Mwenyekiti;
Tume imetoa sababu mbili kubwa za kupendekeza muundo wa Serikali tatu. Sababu ya kwanza ni kwamba ndiyo matakwa ya Watanzania wengi kote Zanzibar na Tanzania Bara. Inaeleza kuwa idadi kubwa ya Watanzania waliotoa maoni, yaani asilimia 60.2 wa kutoka Zanzibar wanaunga mkono muundo wa Serikali ya Mkataba, na asilimia 61.3 wa kutoka Tanzania Bara wanaunga mkono muundo wa Serikali tatu. Sababu ya pili ni kwamba muundo huo unatoa majawabu ya uhakika na endelevu kwa changamoto za muundo wa sasa wa Serikali mbili zinazonung’unikiwa na watu wa pande zetu mbili za Muungano.
Mheshimiwa Mwenyekiti;
Sababu hizi mbili kuu zilizotolewa na Tume zimezua mjadala mkali katika jamii. Wapo wanaokubaliana na Tume na wapo wasiokubaliana nayo. Wapo wanaosema Tume imesema kweli kwamba Watanzania wengi wanaunga mkono muundo wa Serikali tatu, hivyo muundo wa Serikali tatu hauepukiki. Ndiyo matakwa ya wengi hivyo msemo wa Kiswahili usemao wengi wape uheshimiwe.
Lakini wapo wanaodai kuwa takwimu za Tume hazionyeshi ukweli huo. Wanasema kuwa taarifa ya Tume imeonesha kuwa Watanzania waliotoa maoni yao kwa Tume kwa mdomo na maandishi walikuwa 351,664. Kati yao ni wananchi 47,820 au sawa na asilimia 13.6 ndiyo waliokerwa na muundo wa Muungano hivyo wakauzungumzia. Wananchi 303,844 au sawa na asilimia 86.4 muundo wa Muungano kwao halikuwa tatizo, ndiyo maana hawakuuzungumzia kabisa. Wanahoji kuwa iweje leo asilimia 13.6 ya Watanzania wote waliotoa maoni wageuke kuwa ndiyo Watanzania walio wengi!
Mheshimiwa Mwenyekiti;
Wanasema pia, kwamba mbona Taarifa ya Tume yenyewe, kuhusu takwimu (uk. 66 na 67), inaonesha kwamba kati ya hao watu 47,820 waliotoa maoni kuhusu Muungano, ni watu 17,280 tu ambao ni sawa na asilimia 37.2 ndiyo waliotaka muundo wa Serikali tatu, asilimia 29.8 walitaka Serikali mbili, asilimia 25.3 walipendekeza Serikali ya Mkataba na asilimia 7.7 walipendekeza Serikali moja. Hii hoja ya Watanzania wengi kutaka Serikali tatu msingi wake upi?
Mheshimiwa Mwenyekiti;
Takwimu za Tume (uk. 57) zinaonyesha, vilevile kuwa Tume ilipokea maoni 772,211. Kati ya hayo asilimia 10.4 tu ndiyo yaliyozungumzia muundo wa Muungano na asilimia 88.6 hayakuzungumzia Muungano bali mambo mengine. Hivyo basi wanahoji pia kwamba kama muundo wa Muungano ungekuwa ni jambo linalowakera Watanzania wengi, lingedhihirika kwenye idadi ya watu waliotoa maoni na kwenye idadi ya maoni yaliyotolewa. Yote hayo hayakujitokeza. Waliouzungumzia Muungano walikuwa asilimia 13.6 tu ya watu wote waliotoa maoni na maoni yanayohusu Muungano yalikuwa asilimia 10.4 ya maoni yote. Hivyo basi, wanauliza “usahihi wa hoja ya Watanzania wengi kutaka Serikali tatu uko wapi?”
Changamoto za Muundo wa Serikali Mbili
Mheshimiwa Mwenyekiti na Waheshimiwa Wajumbe;
Kama nilivyokwishagusia awali, sababu ya pili ambayo Tume inatoa kuhusu kufaa kwa muundo wa Serikali tatu ni kwamba mfumo huu unajibu changamoto nyingi za muundo wa Serikali mbili. Tume imeainisha vizuri changamoto za muundo wa Serikali mbili. Kwa upande wa Zanzibar wanalalamikia kile kinachoitwa Tanzania Bara kuvaa koti la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na hivyo kutumia mamlaka ya Serikali ya Muungano kujinufaisha yenyewe. Fursa hiyo Zanzibar hainayo. Aidha, wanasema mipaka na mamlaka ya Serikali ya Muungano kwa mambo ya Muungano, na kwa mambo ya Tanzania Bara haijaainishwa vizuri ikaeleweka. Wazanzibari pia, wanazungumzia mkanganyiko kuhusu ugawanaji wa mapato, na jinsi ya kuchangia shughuli za Muungano baina ya Serikali ya Muungano na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar. Vilevile, wanalalamikia Rais wa Zanzibar kuondolewa kuwa Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano.
Aidha, kuna malalamiko kuwa orodha ya mambo ya Muungano iliyoongezwa kutoka mambo 11 mwaka 1964 mpaka 22 mwaka 1992 imepunguza uhuru wa Zanzibar kwa mambo yake ya ndani.
Mheshimiwa Mwenyekiti;
Kwa upande wa Tanzania Bara, Tume inaeleza kuwepo kwa manung’uniko kuwa Muungano wa Serikali mbili umepoteza utambulisho wa kihistoria wa Tanganyika na fursa ya watu wa upande wa Tanzania Bara kutetea maslahi yao ndani ya Muungano. Wanasema Zanzibar sasa imekuwa nchi huru; ina bendera yake, wimbo wake wa taifa na Serikali yake. Aidha, wanasema Zanzibar imebadili Katiba na kujitambulisha kama nchi na kuchukua madaraka ya Bunge la Muungano, kwa vile Sheria zinazotungwa na Bunge lazima zipelekwe kwenye Baraza la Wawakilishi kupata kibali cha kutumika Zanzibar. Wananchi wa Tanzania Bara pia wanalalamikia kutokuwa na haki ya kumiliki ardhi Zanzibar wakati wenzao wa kutoka Zanzibar wanayo haki hiyo Tanzania Bara. Na wao vilevile wananung’unikia mkanganyiko kuhusu ugawaji wa mapato na jinsi ya kuchangia gharama za uendeshaji wa shughuli za Muungano baina ya Serikali ya Muungano na Serikali ya Zanzibar. Hizi ndizo baadhi ya changamoto ambazo Tume inaona jawabu lake ili kuzitanzua ni kubadili muundo wa Muungano kuwa wa Serikali tatu badala ya mbili za sasa.
Faida za Muundo wa Serikali Tatu
Mheshimiwa Mwenyekiti;
Tume ya Mabadiliko ya Katiba imefafanua kwamba mfumo wa Serikali tatu utagawanya vizuri madaraka kati ya mamlaka tatu za Muungano. Unawezesha Washirika wa Muungano kubaki na utambulisho wao wa kihistoria na kiutamaduni na hivyo, utawezesha kuondoa hisia za Zanzibar kumezwa na Muungano. Pia unawezesha kila upande wa Tanzania kuendesha mambo yake yasiyo ya Muungano kadri wanavyoona inafaa. Vile vile unaweza ukaleta ushindani wa kimaendeleo baina ya washirika na hivyo kusaidia kukuza maendeleo ya nchi.
Faida za Muundo wa Serikali Mbili
Mheshimiwa Mwenyekiti;
Pamoja na kuainisha changamoto za muundo wa Serikali mbili na kupendekeza kuwa muundo wa Serikali tatu ndio utakaosaidia kuzitatua, Tume haikuacha kutambua manufaa na mchango muhimu uliotolewa na muundo wa Serikali mbili kwa nchi yetu. Tume inasema kuwa muundo wa Serikali mbili unapunguza gharama za uendeshaji wa shughuli za umma. Umesaidia kujenga uhusiano na ushirikiano mzuri katika nyanja mbalimbali baina ya wananchi wa pande zetu mbili za Muungano. Umezuia mkubwa kummeza mdogo; na umedumisha Muungano mpaka kuufikisha hapa ulipo tangu kuasisiwa kwake takriban miaka 50 iliyopita (1964). Aidha, umesaidia kudumisha amani, umoja na utulivu hapa nchini.
Changamoto za Muundo wa Serikali Tatu
Mheshimiwa Mwenyekiti;
Pamoja na kuelezea ubora wa muundo wa Serikali tatu kama jawabu kwa changamoto za Serikali mbili, Tume inakiri kuwa hata muundo huu nao una changamoto zake. Kwanza kabisa, Taarifa ya Tume inaeleza kuwa kutakuwa na gharama kubwa za uendeshaji wa shughuli za umma. Mheshimiwa Jaji Joseph Warioba alitutoa hofu kuhusu gharama ingawaje mwaka 1993, Mwalimu alikuwa na mawazo tofauti. Alisema kwamba: “watu …wanaodhani kuwa gharama ya Serikali yo yote kati ya hizo ingekuwa ndogo, (Waulizeni Wazanzibari) na wala gharama ya Serikali ya Shirikisho isingekuwa ndogo hata bila gharama ya mambo yasiyo ya Shirikisho”. Ni matumaini yangu kwamba katika mjadala wenu mtajipa nafasi ya kulitafakari suala hili kubwa na nyeti.
Tume imesema pia kwamba, Muundo huu, unaweza kuibua tatizo la uchangiaji wa gharama za uendeshaji wa shughuli za umma baina ya nchi washirika. Vilevile, kuna uwezekano wa kuwepo sera zinazokinzana au kutofautiana juu ya masuala ya msingi ya nchi na kuzua mgogoro kati ya washirika wa Muungano na baina ya nchi washirika na Serikali ya Muungano. Aidha, upo uwezekano mkubwa kwa muundo huu kuleta tofauti za kimaendeleo baina ya pande mbili za Muungano kutokana na kila upande kuwa na sera na mipango tofauti.
Tume pia imeelezea hatari ya muundo wa Serikali tatu kukuza hisia za utaifa (nationalistic feelings) kwa nchi washirika, hivyo kuweza kudhoofisha Muungano. Muundo huu pia unaweza kuleta misuguano (paralysis and deadklocs in decision making) katika kufanya uamuzi juu ya masuala muhimu ya kitaifa. Changamoto hizo si tu zinaweza kuwa tishio kwa ustawi wa Muungano bali pia hata uhai wake. Kwa ajili hiyo kuchagua muundo wa Serikali tatu kuna maana ya kufanya kazi ya ziada ya kuzikabili changamoto hizi ili zisiue Muungano wenyewe. Changamoto ambazo si ndogo hata kidogo.
Mheshimiwa Mwenyekiti;
Wanaounga mkono muundo wa Serikali mbili wanasema kuwa kwa mlolongo huu wa changamoto zilizoainishwa na Tume yenyewe, unadhihirisha kuwa muundo wa Serikali tatu hautapunguza matatizo ya Muungano wetu bali utayaongeza maradufu kuliko ilivyo sasa. Wanakiri kuwepo kwa changamoto katika muundo wa sasa wa Muungano. Hata hivyo, wanaamini zinaweza kushugulikiwa na kupatiwa ufumbuzi bila ya kuhitaji kuwa na Serikali ya tatu. Wanatoa mifano kadhaa ya jinsi Serikali zetu zilivyoshughulikia changamoto za Muungano katika kipindi cha uhai wake na mafanikio yaliyopatikana.
Katika kushughulikia kero za Muungano, Serikali zetu mbili ziliunda Tume ya Shelukindo mwaka 1992 na Kamati ya Pamoja ya Serikali zetu mbili mwaka 1993. Mambo mengi yaliyoainishwa katika Tume ya Shelukindo na Kamati ya Pamoja yameshughulikiwa na kupatiwa ufumbuzi. Kwa upande wa kero zilizoelezwa kwenye Tume ya Shelukindo, ilipofikia mwaka 2006 yalikuwa yamebakia mambo 13 kati ya 31. Kwa jumla, kwa kero zilizoibuliwa na Tume ya Shelukindo na Kamati ya Pamoja, hivi sasa yamesalia mambo sita tu. Kimsingi ni mambo yahusuyo maslahi ya kiuchumi na yote yapo katika hatua nzuri za kuyamaliza. Mambo hayo ni:
- Mgawanyo wa mapato:
(a) Hisa za SMZ zilizokuwa katika Bodi ya Sarafu ya Afrika Mashariki
(b) Mgawanyo wa Mapato yatokanayo na faida ya Benki Kuu.
- Utafutaji na uchimbaji mafuta na gesi asili.
- Ushirikiano wa Zanzibar na taasisi za nje.
- Ajira kwa watumishi wa Zanzibar katika taasisi za Muungano.
- Usajili wa vyombo vya moto.
- Tume ya Pamoja ya Fedha.
Mheshimiwa Mwenyekiti;
Serikali zetu mbili zimeamua kwa dhati kutumia fursa ya mchakato huu wa mabadiliko ya Katiba kuyamaliza yale yanayohitaji kuingizwa kwenye Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Mambo hayo ni matatu yafuatayo:
- Utafutaji na uchimbaji mafuta na gesi asili.
- Ushirikiano wa Zanzibar na taasisi za nje.
- Tume ya Pamoja ya Fedha.
Matatu mengine yatamalizwa kwa kutumia taratibu za kiutawala. Hali kadhalika, katika kipindi cha mpito kinachopendekezwa na Tume yaani 2015 – 2018 ni nafasi nzuri ya kushughulikia masuala yenye migongano kati ya Katiba ya Zanzibar na ile ya Jamhuri ya Muungano. Mimi naishi kwa matumaini na kwa vile tunayo dhamira njema ya kuimarisha Muungano wetu, naamini tutaweza kuziondoa tofauti zilizopo.
Orodha ya Mambo ya Muungano
Mheshimiwa Mwenyekiti;
Kuhusu orodha ya mambo ya Muungano kuwa 22 badala ya 11 ya awali, napenda kuwahakikishia kuwa Serikali ya Muungano na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar hazina kigugumizi wala upungufu wa dhamira ya kisiasa ya kuyapunguza yale yanayopunguzika. Napenda kwanza kabisa, ieleweke kuwa kilichoongeza orodha hiyo si hila za Serikali ya Muungano kutaka kupunguza madaraka ya Zanzibar kwa mambo yake ya ndani. Na, wala siyo udhaifu wa viongozi wa Zanzibar katika kutetea maslahi ya nchi yao. La hasha.
Pili, naomba ieleweke kuwa, kila kilichoongezwa katika Orodha ya Mambo ya Muungano kilikuwa na sababu inayoeleweka, inayoelezeka na iliyokubalika na pande zote mbili za Muungano. Hakuna hata jambo moja lililoingizwa kwenye Katiba kwa kificho. Taratibu stahiki za kikatiba na kisheria zilifuatwa. Hoja ziliwasilishwa Bungeni na kujadiliwa kwa uwazi na uamuzi ulifanywa na Bunge kwa kuzingatia kanuni ya theluthi mbili ya kura za kila upande wa Muungano. Kumbukumbu zipo katika Hansard za Bunge la Muungano, ambazo ziko wazi kwa kila mtu anayetaka kuzisoma asome. Nashauri mkazisome ili mpate kujua ukweli na undani wa kila kilichoongezwa na sababu za kufanya hivyo.
Mheshimiwa Mwenyekiti;
Nchi zetu mbili zilipoungana mwaka 1964 na kuzaa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, kulikuwa na mambo 11 kwenye Orodha ya Mambo ya Muungano. Mambo hayo ni haya yafuatayo:
- Katiba ya Jamhuri ya Muungano,
- Mambo ya Nje,
- Ulinzi,
- Polisi,
- Hali ya Hatari,
- Uraia,
- Uhamiaji,
- Biashara ya nje na mikopo,
- Utumishi katika Serikali ya Muungano,
- Kodi ya Mapato, Kodi ya Makampuni, Ushuru wa Forodha na Ushuru wa Bidhaa,
- Bandari, Mambo ya Anga, Posta na Simu.
Mheshimiwa Mwenyekiti;
Kati ya mwaka 1965 na 1992 mambo ya Muungano yaliongezeka kutoka 11 hadi kufikia 22, kimsingi kutokana na mambo mbalimbali yaliyotokea nchini na kwenye ukanda wetu wa Afrika Mashariki. Pande zetu mbili za Muungano zilikubaliana kuwa mambo hayo yaongezwe katika Katiba na taratibu za kisheria na Kikatiba zilifuatwa. Kwa idhini yako naomba nitoe maelezo kwa ufupi kwa yale yaliyoongezwa na kitu kilichosababisha mabadiliko hayo kufanywa.
- Jambo la kwanza kuongezwa, yaani la 12 lilikuwa ni “sarafu, mabenki na fedha za kigeni”. Hii ilifanyika tarehe 10 Juni, 1965 kufuatia kuvunjika kwa Bodi ya Sarafu ya Afrika Mashariki (East African Currency Board) mwaka 1964. Kwa ajili hiyo, kila nchi mwanachama wa Jumuiya ililazimika kuwa na sarafu yake na mipango yake ya kusimamia mambo yake ya kibenki na fedha. Serikali zetu mbili zilikubaliana masuala hayo yashughulikiwe na Serikali ya Muungano na Muswada husika wa Bunge uliidhinishwa kuwa Sheria na Mzee Abeid Amani Karume aliyekuwa akikaimu Urais tarehe 10 Juni, 1965.
- Tarehe 11 Agosti, 1967 yaliongezwa mambo yafuatayo kwenye Orodha ya Mambo ya Muungano:-
(a) Leseni za Viwanda na Takwimu, (Jambo la 13)
(b) Elimu ya Juu, (Jambo la 14)
(c) Jambo la 15 lilikuwa ni mambo yote yaliyokuwa kwenye Nyongeza ya 10 ya Mkataba wa Jumuiya ya Afrika Mashariki. Nyongeza hiyo ilikuwa na mambo 27 ambayo Serikali ya Muungano ilipewa jukumu la uratibu. Mambo hayo ni pamoja na Mahakama ya Rufani ya Afrika Mashariki, Utabiri wa Hali ya Hewa, Utafiti, Vipimo na Mizani, Huduma ya Usafiri wa Reli, Barabara, Usafiri wa Majini na kadhalika.
- Tarehe 22 Julai, 1968 “rasilimali ya mafuta, petroli na gesi asilia” iliongezwa kwenye Orodha ya Mambo ya Muungano na kuwa jambo la 16. Kimsingi Serikali ya Muungano ilipewa jukumu la kuagiza mafuta ya petroli na gesi asilia kwa ajili ya nchi nzima. Baada ya kupanga upya Orodha ya Mambo ya Muungano, suala la rasilimali ya mafuta likawa la 15.
- Tarehe 22 Novemba, 1973 Baraza la Mitihani la Taifa liliongezwa na kuwa jambo la 16. Hii ilifuatia kuvunjika kwa Baraza la Mitihani la Afrika Mashariki mwaka 1971 na hivyo nchi yetu kulazimika kuunda Baraza la Mitihani la Taifa mwaka 1973.
- Mwaka 1984 yalipofanyika mabadiliko makubwa katika Katiba ya mwaka 1977, Orodha ya Mambo ya Muungano ilipangwa upya. Mambo yaliyokuwemo kwenye Nyongeza ya 10 ya Jumuiya ya Afrika Mashariki na kuorodheshwa kama Jambo la 15 katika Orodha ya Mambo ya Muungano yalipunguzwa na kubaki matano. Mambo hayo yalipewa namba kama ifatavyo:- Usafirishaji wa Anga kuwa Jambo la 17, Utafiti kuwa la 18, Utabiri wa Hali ya Hewa kuwa la 19 na Takwimu kuwa la 20 na Mahakama ya Rufani ya Tanzania ikawa jambo la 21.
- Tarehe 17 Mei, 1992 likaongezwa jambo la “Uandikishaji wa Vyama vya Siasa” na kuwa jambo la 22. Hii ilifuatia kuanzishwa kwa Mfumo wa Vyama Vingi vya Siasa na hasa uamuzi kuwa vyama vitakuwa vya kitaifa.
Mheshimiwa Mwenyekiti;
Bila ya shaka maelezo haya yatasaidia kuelezea nini kimeongezwa na mazingira ya kuongezwa kwake ni yepi. Kulikuwepo na sababu za msingi na wala siyo hila ya namna yo yote ile iliyofanywa na mtu ye yote mwenye nia mbaya na Zanzibar. Kama tulivyoona mambo mengi yalihusu kilichokuwa kinatokea ndani ya Jumuiya ya Afrika Mashariki. Kila yalipotokea mabadiliko katika uendeshaji wa shughuli za Jumuiya ya Afrika Mashariki, huduma zilizokuwa zikitolewa na Jumuiya zilikabidhiwa Serikali ya Muungano kubeba kwa sababu ya uwezo wake mkubwa wa kiuchumi. Yale yaliyokuwa yanagusa sehemu zetu mbili za Muungano yaliingizwa katika Orodha ya Mambo ya Muungano. Mengineyo yaliachiwa kila upande kushughulikia ilivyoona inafaa. Kwa maana hii basi, mambo ambayo yalitokana na uamuzi wetu wenyewe ni mawili tu. Mambo hayo ni rasimali ya mafuta na gesi asilia (1968), na uandikishaji wa vyama vya siasa (1992).
Mheshimiwa Mwenyekiti;
Ni msimamo wa Serikali zetu mbili, tangu mwanzo mpaka leo kwamba, iwapo Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar imeshajenga uwezo wake wa kufanya baadhi ya mambo katika Orodha ya Mambo ya Muungano ipewe uhuru wa kufanya hivyo. Lililo muhimu ni kuwa zisiondolewe tunu zenyewe za Muungano wetu. Ndiyo maana, mambo kama vile bandari, takwimu, kodi ya mapato, leseni za biashara, utafiti na mengineyo, yanasimamiwa na kuendeshwa na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar pamoja na kuwemo kwenye Orodha ya Mambo ya Muungano. Imekuwa hivyo kwa miaka kadhaa sasa na imethibitika kuwa Zanzibar inayamudu. Ni makusudio yetu kutumia fursa ya mchakato huu sasa kuyaondoa rasmi mambo hayo na mengineyo tutakayokubaliana kutoka kwenye Orodha ya Mambo ya Muungano.
Rasilimali ya Mafuta na Gesi Asilia
Mheshimiwa Mwenyekiti;
Kwa ajili hiyo tumekubaliana kuliondoa suala la rasilimali ya mafuta na gesi asilia lisiwe jambo la Muungano. Jambo hili tulishakubaliana tangu wakati wa Rais Amani Abeid Karume tuliondoe na hata alipokuja Rais Shein msimamo haukubadilika. Kilichotuchelewesha kutekeleza ni kuibuka kwa fikra za kuwa na mchakato huu wa Katiba mpya. Tuliona kuwasilisha Bungeni Muswada wa Sheria wa kuondoa jambo hili katikati ya mchakato huu, ingeweza kuzua matatizo yasiyokuwa ya lazima. Tungeulizwa haraka ni ya nini tungeweza kukosa majibu.
Hatimaye wakati wake wa kulimaliza suala hili sasa umefika. Misemo ya wahenga ya “subira yavuta heri” na “kawia ufike” imetuongoza vyema tumefika mahali tunaweza kufanya hivyo. Zipo sababu mbili zilizotushawishi kuamua kuitoa rasilimali hii kwenye Orodha ya Mambo ya Muungano. Kwanza kwamba, siku hizi Serikali haiagizi mafuta. Kazi hiyo hufanywa na makampuni binafsi. Pili, kwamba, rasilimali ya mafuta na gesi yakipatikana Zanzibar ni suala la kiuchumi ambalo lipo kwenye mamlaka ya Zanzibar kama ilivyo karafuu, hiliki, mwani na kadhalika. Au kama ilivyo dhahabu, gesi, pamba, kahawa na kadhalika kwa upande wa Tanzania Bara. Hivyo, Zanzibar iachwe kumiliki rasilimali yake ya kiuchumi.
Zanzibar na Ushirikiano wa Kimataifa
Mheshimiwa Mwenyekiti;
Jambo lingine muhimu ambalo Serikali zetu mbili zimelizungumza na kukubaliana tulitafutie ufumbuzi ni kuhusu Zanzibar kupata fursa ya kujiunga na mashirika ya kimataifa, kukopa na kupata misaada kutoka nchi za nje bila kizuizi. Kwa sasa fursa hiyo ina vikwazo vya namna mbalimbali. Ni ukweli usiopingika kuwa jambo hili limechangia kwa kiasi kikubwa kujenga hisia hasi kuhusu Muungano kwa upande wa Zanzibar. Aidha, limechangia sana kuchafua hali ya hewa ya kisiasa Zanzibar kwa nyakati mbalimbali. Hata zile kauli kwamba Tanzania Bara imejificha kwenye koti la Serikali ya Muungano, na kutaka itoke ionekane ili iache kunufaika isivyostahili, zinazochangiwa sana na mazingira haya iliyonayo Zanzibar. Serikali zetu mbili zinaamini kuwa mambo haya yakipatiwa ufumbuzi tutakuwa tumeondoa kizingiti kikubwa katika ustawi wa Muungano wetu.
Mheshimiwa Mwenyekiti;
Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar tumekubaliana kuwa, tutumie fursa za mchakato huu kuyamaliza mambo haya yaishe! Bahati nzuri dhana iliyopo katika Ibara ya 65(2) ya Rasimu inatoa jawabu mwafaka kwa tatizo hili. Tukikubaliana, itaipa Zanzibar “uwezo na uhuru wa kuanzisha uhusiano na ushirikiano na jumuiya au taasisi yo yote ya kikanda na kimataifa kwa mambo yaliyo chini ya mamlaka yake kwa mujibu wa Katiba ya nchi” bila kizuizi. Ni maoni ya Serikali zetu mbili kuwa fursa hiyo inaweza kutolewa kwa Zanzibar bila ya kulazimika kuwa na muundo wa Serikali tatu. Hatuuoni ulazima huo.
Mheshimiwa Mwenyekiti;
Kwa maoni yangu kitu kingine muhimu cha kufanya ni kuongeza msukumo, utakaohakikisha kuwa Tume ya Pamoja ya Fedha inatimiza ipasavyo majukumu yake. Wanaohusika na utekelezaji wa maamuzi yake wabanwe ipasavyo kutimiza wajibu wao. Iwekwe mifumo na masharti katika sheria au Katiba ya kuwabana watekelezaji kwa ajili hiyo. Hali kadhalika ihakikishwe kuwa, Akaunti ya Pamoja inaanzishwa bila ajizi na kutumika na pande zote. Aidha, mfumo wa mawasiliano na ushirikiano baina ya Serikali zetu mbili yaani Kamati ya Pamoja ya Serikali ya Muungano na Serikali ya Mapinduzi Zanzibar, upewe nguvu ya kisheria na kama hapana budi upewe nguvu ya Kikatiba. Tukifanya hivyo tutafanikiwa kuyaweka mambo yote sawa hata bila ya kuhitaji kuunda Serikali ya tatu.
Mheshimiwa Mwenyekiti;
Waheshimiwa Wajumbe;
Katika mjadala kuhusu mapendekezo ya kuwa na muundo wa Muungano wenye Serikali tatu, wananchi wametoa maoni na mapendekezo mengi mazuri kuhusu changamoto za Serikali tatu zilizoainishwa na Tume na namna ya kuzitatua. Tena yapo maoni ya watu wanaopenda muundo wa Serikali tatu na wasiopenda muundo wa Serikali tatu. Nawaomba myatafakari kwa uzito unaostahili. Yapo mambo muhimu ya kuyatafutia ufumbuzi. Kwanza, kwa mfano ni ile hoja kwamba Serikali ya Muungano inayopendekezwa haikujengeka kwenye msingi imara. Haina nguvu yake yenyewe za kusimama. Inategemea mno ihsani ya nchi washirika. Kwa sababu hiyo inaweza kuanguka wakati wowote, na Muungano kusambaratika, iwapo itakosa ihsani ya nchi washirika. Tena inaweza kuwa hivyo hata kama ni mmoja wa washirika amefanya hivyo.
Pili, kwamba, haielekei Serikali hiyo ina chanzo cha uhakika cha mapato ya kuiwezesha kusimama yenyewe na kutekeleza majukumu yake. Ushuru wa bidhaa unaopendekezwa unatiliwa shaka kuwa hautatosheleza mahitaji. Pia, kwamba, hakuna uhakika wa fedha hizo kupatikana kwa vile, Serikali ya Muungano haina chombo chake chenyewe cha kukusanya mapato hayo. Itategemea vyombo vya nchi washirika kuikusanyia na kuipelekea. Kuna hatari ya shughuli za Serikali ya Muungano kusimama wakati wo wote au hata kusimama kabisa kwa sababu ya nchi washirika kuchelewa au kushindwa kuwasilisha makusanyo ya kutoka kwao.
Bahati mbaya Serikali ya Muungano haina uwezo wala nyenzo za kuhakikisha kuwa mapato yake yanawasilishwa. Serikali hiyo haina mamlaka ya kuzibana nchi washirika kuwasilisha au kuziwajibisha zisipofanya hivyo. Katika mazingira hayo ni rahisi kwa Serikali ya Muungano kukwama na kushindwa kutekeleza majukumu yake. Huu ni muundo ambao inakuwa ni rahisi sana kwa Muungano kuvunjika.
Mheshimiwa Mwenyekiti;
Katika Rasimu ya Katiba, Serikali ya Muungano inapewa fursa ya kukopa kama chanzo cha kujipatia mapato ya kuendesha shughuli zake. Lakini, kwa sababu ya kukosa rasilimali zake yenyewe, huenda ikawa vigumu kwa Serikali hiyo kukopesheka. Kwa jumla hii ni Serikali ambayo ukuu wake hauna nguvu iliyo thabiti, na watu wengine wanaona kama vile ukuu huo haupo kabisa. Akitokea kiongozi ye yote wa nchi washirika akatunisha misuli dhidi ya Rais wa Muungano au kupinga maamuzi ya Serikali au chombo cha Muungano, Rais na Serikali yake watakuwa hawana lo lote la kufanya. Kwa kweli uhai wa Muungano katika muundo wa Serikali tatu ni wa mashaka makubwa.
Hofu hizi kuhusu udhaifu wa Serikali ya Muungano chini ya mfumo wa Serikali tatu unaopendekezwa, zinawasumbua hata wale wanaopendelea mfumo wa Serikali tatu kuwepo. Wao wangependa iwepo Serikali ya Muungano yenye nguvu na inayoweza kusimama yenyewe kwa kujitegemea. Wanaona kilichopendekezwa hakitoi matumaini hayo. Hii ina maana kuwa lazima mawazo bora zaidi yatolewe ili kupata Serikali ya tatu yenye ukuu unaoonekana na inayoweza kusimama yenyewe bila kuwa tegemezi na egemezi kwa nchi washirika. Pia inaweza kuwa nguzo ya kutegemewa na nchi washirika. Bila ya shaka Bunge hili likiamua tufuate mfumo huo linaweza kuonyesha njia ya kuondoa hofu hizo. Kwa waumini wa Serikali mbili wanaona kuwa huu ni uthibitisho wa ubora wa muundo wa Serikali mbili.
Changamoto za Hisia za Utaifa
Mheshimiwa Mwenyekiti;
Katika kuainisha changamoto za muundo wa Serikali tatu, Tume ya Mabadiliko ya Katiba imeyataja mambo mengine mawili makubwa ambayo ningependa Waheshimiwa Wajumbe muyape tafakuri stahiki. Mambo hayo ni mosi, misuguano na mikwamo (deadlocks and paralysis) katika kujadili na kufanya uamuzi kuhusu mambo muhimu ya Muungano. Na pili, ni kuibuka kwa hisia za utaifa (nationalistic sentiments) wa zamani kwa nchi washirika. Nawaomba myatafakari kwa makini sana mambo haya, kwa sababu ya uwezo wake mkubwa wa kuhatarisha siyo tu ustawi na uhai wa Muungano, bali hata usalama wa raia na mali zao. Naona hata Tume haikuweza kupata ufumbuzi ulio mwafaka kabisa kwa changamoto hizi. Bila ya shaka katika mijadala yenu Waheshimiwa Wajumbe mnaweza kusaidia.
Mheshimiwa Mwenyekiti;
Ni lazima lifanyike kila linalowezekana kuhakikisha kuwa maamuzi hayakwami kwani yakikwama maana yake shughuli za Muungano zitakuwa zimekwama. Kama hazitakwamuliwa kwa wakati ustawi wa Muungano utaathirika. Ikishindikana kabisa kupatikana ufumbuzi Muungano unaweza kuvunjika. Kuibuka na kukua kwa hisia za utaifa (nationalistic feelings) kwa nchi washirika, yaani Utanganyika na Uzanzibari ni tishio kubwa sana kwa uhai wa Muungano. Hebu fikiria, watu walioishi pamoja kidugu na kwa kushirikiana, kama watu wamoja na raia wa nchi moja yaani Watanzania kwa miaka 50, kuja kujikuta uhusiano wao kuwa ni kati ya Watanganyika na Wazanzibari na siyo kati ya Watanznaia. Kwa mujibu wa sensa iliyopita takriban asilimia 90 ya Watanzania waliopo sasa wamezaliwa baada ya mwaka 1964. Nchi wanayoijua ni Tanzania. Litakuwa ni jambo lenye mshtuko mkubwa na athari zisizoweza kutabirika, watu hao watakapojikuta ni wageni wanaotakiwa kutengenezewa utaratibu maalum wa kusafiri na kuishi wakiwa upande wa Muungano ambao siyo kwao kwa asili. Wanakuwa wageni na fursa walizokuwa wanazipata waendapo popote haiwi rahisi tena kuzipata.
Katika mazingira hayo ni rahisi sana chuki kupandikizwa na watu waliokuwa ndugu mara moja watajikuta maadui. Aidha, watu wanaweza kujikuta wakilazimika kurudi kwao kwa asili ama kwa kufukuzwa au kwa sababu ya mazingira kuwa magumu kiasi cha kuona bora waondoke. Watu hao wanaweza kulazimika kuondoka huku wakiacha nyuma kila kitu walichokichuma maishani.
Mheshimiwa Mwenyekiti;
Changamoto hizi kubwa mbili za mfumo wa Serikali tatu ambazo Tume imeziona, ni za kweli. Si mambo ya kufikirika. Yale yaliyowakuta watu wenye asili ya Tanzania Bara ya kuchomewa moto biashara zao Zanzibar mwaka 2012 na watu wenye hisia kali za Uzanzibari, na kuwataka watu wa Bara waondoke Zanzibar, huenda yakawa madogo. Matukio ya namna hii yanaweza kutokea pande zote mbili na kusababisha maafa makubwa. Itaanza baina ya watu, baadaye itakuwa baina ya Serikali zetu mbili na kuzifikisha nchi zetu mbili zilizokuwa ndugu na rafiki, kwa nusu karne, ghafla kuwa maadui wasioombana chumvi na wasiotakiana heri. Umoja wetu utatetereka na Muungano wetu unaweza kuvunjika. Kwa nini tufike huko?
Mheshimiwa Mwenyekiti;
Sisi viongozi tuliopewa dhamana ya kuamua kwa niaba ya wananchi wetu, hatuna budi kuyapima mambo haya kwa umakini mkubwa ili tufanye uamuzi ulio sahihi. Tusije tukajutia uamuzi wetu tutakapoona watu wanafukuzana, wanauana na mali zao kuporwa. Na, tukifikia hatua hiyo Muungano kusambaratika halitakuwa jambo la ajabu.
Kwa kweli, unapoyatafakari haya, ni rahisi kuelewa kwa nini wazee wetu waasisi waliamua walivyoamua. Waliona mbali. Tusipuuze fikra zao na maono yao. Kuna hatari ya nchi yetu na watu wake kupoteza kila kitu tulichokijenga kwa miaka 50. Badala ya kujenga tunaweza kujikuta tumebomoa hata msingi katika nchi washirika. Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Nyerere mwaka 1993 alituasa kuhusu hatari hiyo: “Hamuwezi kutenda dhambi kubwa namna hiyo bila adhabu… na adhabu nyingine zimo mle mle ndani ya kitendo hazisubiri.”
Mheshimiwa Mwenyekiti;
Siku moja kiongozi mmoja wa juu wa madhehebu ya dini nchini aliniuliza: “Hivi Serikali mbili zikiwa na matatizo jawabu ni kuongeza ya tatu? Si matatizo ndiyo yatazidi? Je, matatizo yakizielemea hizo Serikali tatu si kila mtu atachukua njia yake? Mtakuwa mmepoteza kila kitu. Mimi nawashauri msichoke kutafuta majawabu kwa matatizo ya hizi mbili! Huko mnakotaka kwenda kuna hatari nyingi”.
Pengine na ushauri huu wa mtu wa Mungu nao ni vyema kuupa nafasi na kuutafakari.
Kazi Yenu Kubwa
Mheshimiwa Mwenyekiti;
Mambo ya kuyasemea ni mengi mno lakini kwa sababu ya ufinyu wa muda, nisingeweza kuyazungumzia yote. Naamini, mtayaona katika kuipitia Rasimu na kwenye majadiliano yenu. Napenda kusisitiza kwenu kuwa kazi iliyo mbele yenu ni kubwa sana. Ni kubwa kwa maana mbili. Kwanza, jukumu lenyewe la kutunga Katiba ya nchi ni zito sana. Taswira ya nchi yetu itakuwaje na itaendeshwa vipi kwa miaka mingi ijayo iko mikononi mwenu. Ipeni nchi yetu hatima njema. Pili, ni kubwa kwa maana ya uzito wa mambo ya kujadili na kuyafanyia uamuzi. Kwa ajili hiyo, ni muhimu sana kuisoma Rasimu na Taarifa ya Tume kwa makini na kuzielewa. Jipeni muda wa kutafakari kila neno, kila sentensi, na kila dhana ili muweze kufanya uamuzi ulio sahihi. Mkifanya hayo mtakuwa mmeisaidia nchi yetu na Watanzania wote kupata Katiba nzuri.
Nimefarijika sana kusikia kuwa mtajigawa kwenye Kamati 12 wakati wa kujadili Rasimu. Huu ni utaratibu mzuri kwani mkiwa katika vikundi vya watu wachache, mtakuwa na mijadala ya kina zaidi. Watu wote wanaweza kupata fursa ya kutoa maoni yao, kwa kila kifungu na kila jambo linaloibuliwa na kuzungumzwa. Kwa kufanya hivyo, mtatimiza kwa ukamilifu jukumu lenu la kutunga Katiba. Wote mtakuwa mmeshiriki kujadili kila sura na vipengele vyake vyote. Mkimaliza kazi yenu mtapokea kwa haki sifa nzuri kama Katiba itakuwa nzuri, au lawama stahiki iwapo itakuwa kinyume chake.
Pongezi kwa Mwenyekiti wa Muda
Mheshimiwa Mwenyekiti;
Nitakuwa mwizi wa fadhila kama nitamaliza hotuba yangu bila ya kutambua kazi nzuri iliyofanywa na Mheshimiwa Pandu Ameir Kificho, Spika wa Baraza la Wawakilishi, alipokuwa Mwenyekiti wa Muda wa Bunge hili. Kazi yake haikuwa rahisi hata kidogo, lakini kwa umahiri na ustadi mkubwa ameweza kufanikisha mambo kwa kiasi ambacho anastahili pongezi zetu sote. Anastahili pongezi kwa sababu yeye aliendesha Bunge hili bila ya kuwepo kwa kanuni. Tatizo hili hatakuwa nalo Mwenyekiti wa Kudumu kaka yangu Mheshimiwa Samuel Sitta.
Napenda pia kuwapongeza Waheshimiwa Wajumbe wa Bunge Maalum la Katiba kwa hatua mliyofikia. Hata hivyo, mmechukua muda mwingi katika hatua ya awali hivyo hamna budi kuongeza kasi. Naomba niwakumbushe kuwa mijadala yenu hii inafuatiliwa kwa karibu sana na Watanzania. Wamewekeza sana matarajio yao kwenu. Hamna budi, haiba na taswira ya uongozi muionyeshe wakati wote wa kuendesha mijadala yenu kwa lugha na vitendo vyenu. Wakati wa semina na mjadala wa kupitisha Kanuni za Bunge hili, baadhi ya wananchi wamekwazika sana na mwenendo wa baadhi ya Wajumbe. Hawakutegemea kuyaona matendo waliyoyaona mkifanya na kusikia maneno waliyoyasikia kutoka kwenye vinywa vya baadhi yenu.
Ni matumai
- Mar 11, 2014
SPEECH DELIVERED BY HIS EXCELLENCY DR JAKAYA MRISHO KIKWETE- PRESIDENT OF THE UNITED REPUBLIC OF TANZANIA AT HANDING OVER CEREMONY OF 11 VEHICLES DONATED BY FR...
Soma zaidiHotuba
Honourable Lazaro Nyalandu (MP), Minister for Natural Resources and Tourism;
Deputy Ambassador of European Union;
Charge d; Affairs of the Federal Republic of Germany to Tanzania;
Deputy
Permanent Secretary;
Mr. Christ of Schenk, Director for Frankfurt Zoological Society;
Members of the Diplomatic Corps and International Community;
Director of TANAPA;
Distinguished Guests;
Ladies and Gentlemen;
I welcome you all at the State House for this historic handover ceremony. I can’t find words good enough to thank the Frankfurt Zoological Society (FZS) for donating 11 vehicles in support of our ongoing anti-poaching efforts. These vehicles donated today will be used for anti poaching activities in the Selous Game Reserve, Serengeti National Park and Maswa Game Reserve.
Your passion and commitment for wildlife conservation is well known and highly appreciated in Tanzania. This is not the first time we receive support from your Organization and, I believe it is not the last time. You have been with us all along in conservation of our wildlife for almost half a century now. I want you to know that we value your support and appreciate these generous contributions.
Ladies and Gentlemen;
Poaching for meat and trophies is long standing problem in the country. But, of late poaching elephants for their ivory has reached dangerous proportions. As you are all aware, the number of elephants in Selous and Ruaha has significantly dropped from 74,416 in year 2009 to 33,084 in 2013 as a result of poaching activities. By all account, this is alarming. We have responded by scaling up our anti-poaching campaign, and the results have been so far promising. Through Operesheni Kipepeo and Operesheni Tokomeza and other interventions we have uncovered criminal networks, arrested 2,085 poachers and their accomplices in the illegal ivory trade network. We have confiscated 1,721 weapons and several catches of ammunition used by poachers. It has been a hard-won success. We need to sustain the gain because the problem remains unsolved.
As a result, in the Northern zone, we have managed to significantly reduce the number of elephant killed from six per month 2011, to zero by August 2013. Unfortunately, immediately just after the suspension of ‘Operesheni Tokomeza’ three elephant were killed in December, 2013. The statistics tell a story that, although we have won important battles in the anti-poaching campaign, we have not won the war against poaching itself. We are determined to stay the course until this war is won. Losing is not an option.
Ladies and Gentlemen;
The threat posed by poaching and illegal ivory trade to the world heritage and our economy is real. Tourism is an important sector which contributes 17 percent of the Tanzania’s GDP and employs over 300,000 people. Game Safari is an anchor of Tanzania tourism. Therefore, we take the threat of poaching very seriously. It is not lack of political will but capacity challenges that we face. We are currently faced with insufficient workforce, financial resources and anti-poaching equipment. Whatever way our friends and partners can assist us in this regard will be highly appreciated. We thank Frankfurt Zoological Society for being a leader in this regard.
The size of territory set aside for wildlife conservation is 36 percent of Tanzania territory. The total area under conservation is 159,878.02 square kilometres on which Game Reserve covers 101,313 square kilometres and Game Controlled Area covers 58,565.02 square kilometres (above the size of Bangladesh which is 143,998 square kilometres). This challenge posed by sheer size is compounded by the insufficient game and warden staff currently at 1,155 personnel, which is only 24 percent of the actual needs. The low number of staff dictates that, one person patrols about 169 square kilometres compared to the required international standard of 25 square kilometres per person. Currently, we are in the process of employing 949 wildlife management officers and we will continue to do so every year until the gap is closed in the next three to four years.
The donation we have received today is indeed timely. It has come at a time of serious need. Certainly, the challenge before us is daunting, but we have no other choice. We need to build the capacity of our wildlife division to be able to fight this war and win.
As we all know too well that, the increasing number of wildlife personnel alone will only not pay off if they do not have better equipment to enable them to respond effectively to the threat. It translates into increasing more vehicles, surveillance equipment and communication equipments among many. It requires a lot of financial investment to be able to meet capacity needs, faced with many competing needs it will take our government a long time to meet those needs. It is for this reason that we welcome the support extended by the Frankfurt Zoological Society and the Germany people. This support will go a long way towards enhancing our capacity to address poaching.
Ladies and Gentlemen;
This anti-poaching campaign cannot be won by Tanzania and affected countries alone. This is a global problem that requires a global response. It requires joint efforts from within and outside the elephant range in the country, and within and across regions.
We thank you in particular for responding to the call and we urge others to join the course. We invite other domestic and international partners to work with us to effectively address the problem of poaching and illegal wildlife trade. We must destroy the criminal networks and hold them to account. Tanzania’s wildlife is a world heritage. We are mere custodians on behalf of humanity. Therefore, protecting this heritage must be a shared responsibility. We all have a role to play. We in Tanzania are fervently determined to play our part.
Ladies and Gentlemen;
Once again I thank the Frankfurt Zoological Society for this gesture of friendship gesture. I would also like to thank Mr. Christ of Schenk, for his invaluable efforts in initiating and facilitating the process of acquisition of these vehicles. This support is a testimony for our longstanding partnership and commitment to sustainable conservation. The anti poaching crusade needs to be sustained until the lasting victory attained.
I thank you all for your attention.

Hotuba
1. Uteuzi wa Wajumbe wa Bunge la Katiba Unatawaliwa na Sheria ya Mabadiliko ya Katiba, Sura, 83 (The Constitutional Review Act, Cap 83). Sheria hii inaweka mamlaka ya uteuzi, masharti, taratibu, vigezo na mambo mengine yote yanayopaswa kuzingatiwa katika uteuzi wa Wajumbe wa Bunge la Katiba. Kwa mujibu wa Kifungu cha 22 (2A) na (2B) vigezo hivi vinajumuisha umri, jinsia, uzoefu, sifa na mahali anapotoka mjumbe husika.
2. Sheria hii inatamka aina tatu za Wajumbe wa Bunge la Katiba kama ifuatavyo:-
(i) Wabunge wote wa Bunge la Jamhuri ya Muungano;
(ii) Wajumbe wa Baraza la Wawakilishi la Zanzibar; na
(iii) Wajumbe 201 kwa mujibu wa Kifungu Na. 22(1c) cha Sheria ya Mabadiliko ya Katiba ambayo inaonyesha makundi mbalimbali 10 yanayohusika.
3. Makundi hayo ni kama ifuatavyo:-
(i) Taasisi zisizokuwa za Kiserikali (20)
(ii) Taasisi za Kidini (20)
(iii) Vyama vyote vya Siasa vyenye Usajili wa Kudumu (42);
(iv) Taasisi za Elimu (20);
(v) Watu wenye Ulemavu (20);
(vi) Vyama vya Wafanyakazi (19);
(vii) Vyama vinavyowakilisha Wafugaji (10);
(viii) Vyama vinavyowakilisha wavuvi (10);
(ix) Vyama vya Wakulima (20); na
(x) Vikundi vya Watu wenye Malengo yanayofanana (20).
4. Mchakato wa uteuzi ulianza kwa kutoa Tangazo la Mwaliko katika Gazeti la Serikali, Tangazo la Serikali Na 443 la tarehe 13 Desemba, 2013. Tangazo hilo lilitolewa kwa lugha ya Kiswahili na Kiingereza ili kuyaalika makundi yaliyotajwa kisheria kuwasilisha mapendekezo ya majina kwa ajili ya uteuzi katika Bunge laMaalum la Katiba. Aidha, Tangazo hilo la mwaliko lilitangazwa pia katika magazeti mbalimbali yanayosomwa hapa nchini. Pamoja na mambo mengine Tangazo la Mwaliko lilitamka ukomo wa muda wa Taasisi na Makundi kuwasilisha mapendekezo ya majina ya wajumbe kuwa ni tarehe 02/01/2014.
5. Mapendekezo hayo yalitakiwa kuwasilishwa kwa Katibu Mkuu Kiongozi wa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa upande wa Tanzania Bara na kwa upande wa Zanzibar, mapendekezo yalitakiwa kuwasilishwa kwa Katibu Mkuu Kiongozi wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar.
6. Kufuatia mwaliko huo, taasisi 554 kutoka Tanzania Bara na 178 kutoka Zanzibar ziliwasilisha mapendekezo yao. Mapendekezo hayo yalijumuisha majina 2,762 kwa upande wa Tanzania Bara na kwa upande wa Zanzibar mapendekezo hayo yalihusisha watu 874. Hivyo basi, taasisi na makundi mbalimbali yalipendekeza jumla ya majina 3,636. Lakini, na kinyume na Sheria, watu 118 walijipendekeza wenyewe na kufanya idadi ya majina yaliyopendekezwa kuwa 3,754.
7. Mchanganuo wa idadi ya watu walipendekezwa katika makundi mbalimbali ni kama ifuatavyo:
Na. |
Kundi/Taasisi |
Taasisi zilizoleta mapendekezo |
Idadi ya Watu Waliopendekezwa |
Idadi ya Wajumbe Wanaotakiwa |
Idadi ya Walioteuliwa |
|||
Tanzania Bara |
Zanzibar |
Tanzania Bara |
Zanzibar |
Tanzania Bara |
Zanzibar |
|||
1. |
Taasisi zisizokuwa za Kiserikali |
246 |
98 |
1,203 |
444 |
20 |
13 |
7 |
2. |
Taasisi za Kidini |
55 |
17 |
344 |
85 |
20 |
13 |
7 |
3. |
Vyama vya Siasa vyenye Usajili wa Kudumu |
21 |
14 |
129 |
69 |
42 |
28 |
14 |
4. |
Taasisi za Elimu |
9 |
9 |
84 |
46 |
20 |
13 |
7 |
5. |
Makundi ya Walemavu |
24 |
6 |
97 |
43 |
20 |
13 |
7 |
6. |
Vyama vya Wafanyakazi |
20 |
1 |
89 |
13 |
19 |
13 |
6 |
7. |
Vyama Vinavyowakilisha Wafugaji |
8 |
1 |
43 |
4 |
10 |
7 |
3 |
8. |
Vyama vinavyowakilisha Wavuvi |
7 |
3 |
45 |
12 |
10 |
7 |
3 |
9. |
Vyama vya Wakulima |
22 |
8 |
115 |
44 |
20 |
13 |
7 |
10. |
Makundi yenye Malengo Yanayofanana |
142 |
21 |
613 |
114 |
20 |
14 |
6 |
|
Mapendekezo Binafsi |
- |
- |
118 |
- |
|
|
|
|
Jumla |
672 |
178 |
2,880 |
874 |
201 |
134 |
67 |
|
Jumla Kuu |
850 |
3,754 |
|
|
|
8. Sheria ya Mabadiliko ya Katiba imeweka masharti ya kuzingatiwa katika uteuzi wa wajumbe 201 wa Bunge la Maalum la Katiba. Masharti hayo ni pamoja na wajumbe wasiopungua theluthi moja wanatakiwa kutoka Zanzibar na theluthi mbili kutoka Tanzania Bara. Kwa sababu hiyo, katika wajumbe 201, wajumbe 67 watatoka Zanzibar na wajumbe 134 watatoka Tanzania Bara. Aidha, mgawanyo wa wajumbe wanawake na wanaume unatakiwa uwe nusu kwa nusu. Pamoja na hayo, wajumbe hao wawakilishe sura ya wananchi wa Tanzania kwa ufuasi wa vyama vya siasa, dini, umri, na maeneo wanayotoka. Katika mazingira haya, zoezi la kupata wajumbe 201 halikuwa rahisi hata kidogo. Mwitikio wa makundi ulikuwa mkubwa sana ikilinganishwa na nafasi zilizopo.
9. Kama nilivyoeleza hapo awali, mapendekezo kutoka Tanzania Bara yalikuwa 2,880 wakati nafasi za wajumbe ni 134. Kwa upande wa Zanzibar, majina yaliyopendekezwa yalikuwa 874 ikilinganishwa na idadi ya wajumbe 67 wanaotakiwa kuteuliwa. Kwa nyongeza ya maelezo kuhusu uwingi wa mapendekezo, ni kwamba ukichukua taasisi zisizo za kiserikali kwa upande wa Tanzania Bara walipendekezwa watu 1,203, wakati nafasi zilizokuwa zinatakiwa kujazwa ni 13 tu. Kwa upande Zanzibar, taasisi zisizokuwa za kiserikali zilikuwa zimependekeza majina 444 ikilinganishwa na nafasi 7 tu zilizokuwa zinatakiwa kujazwa kutokana na taasisi hizi.
WAJUMBE WA BUNGE LA KATIBA
10. Rais wa Jamhuri wa Muungano wa Tanzania wakishirikiana na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mpainduzi Zanzibar wamekamilisha uteuzi wa wajumbe 201. Kabla ya kutaja orodha ya wajumbe walioteuliwa, napenda kufafanua mambo yafuatayo:
(a) Uteuzi umezingatia ushiriki wa watu wa rika zote, yaani vijana, watu wazima na wazee. Kwa ajili hiyo, wajumbe vijana yaani wenye umri wa kati miaka 22-35, ni wajumbe 35. Wajumbe wenye umri wa kati, yaani miaka 36-64, ni 145; na wajumbe wazee, yaani wenye umri wa miaka 65 na kuendelea ni 21.
(b) Sheria inataka kuwepo na uwiano sawa kwa ajumbe wanawake na wanaume. Jambo hili limezingatiwa ipasavyo, na katika orodha hii wajumbe wanawake ni 100 na wanaume 101. Kwa vile, haiwezekani kuwa na nusu mtu, ndiyo maana idadi ya wajumbe wanaume ni 101.
(c) Uwakilishi wa vyama vya siasa ambao unahitaji kila chama chenye usajili wa kudumu kiwe na wajumbe wawili umezingatiwa. Kwa kuwa kuna vyama vya siasa vyenye usajili wa kudumu 21, jumla ya wajumbe 42 wamechaguliwa kwa maana ya kuwa wajumbe wawili wameteuliwa kutoka katika kila chama.
Baada ya maelezo hayo ya utangulizi, ifuatayo ndiyo orodha ya wajumbe 201 wa Bunge Maalum la Katiba waliobahatika kuteuliwa:
TAASISI ZISIZOKUWA ZA KISERIKALI- (WAJUMBE 20) |
|
TANZANIA BARA (13) |
|
1. Magdalena Rwebangira |
2. Kingunge Ngombale Mwiru |
3. Asha D. Mtwangi |
4. Maria Sarungi Tsehai |
5. Paul Kimiti |
6. Valerie N. Msoka |
7. Fortunate Moses Kabeja |
8. Sixtus Raphael Mapunda |
9. Elizabeth Maro Minde |
10.Happiness Samson Sengi |
11. Evod Herman Mmanda |
12. Godfrey Simbeye |
13. Mary Paul Daffa |
|
TANZANIA ZANZIBAR (7) |
|
1. Idrissa Kitwana Mustafa |
2. Siti Abbas Ali |
3. Abdalla Abass Omar |
4. Salama Aboud Talib |
5. Juma Bakari Alawi |
6. Salma Hamoud Said |
7. Adila Hilali Vuai |
|
|
|
TAASISI ZA KIDINI- (WAJUMBE 20) |
|
TANZANIA BARA (13) |
|
1. Tamrina Manzi |
2. Olive Damian Luwena |
3. Shamim Khan |
4.Mchg. Ernest Kadiva |
5. Sheikh Hamid Masoud Jongo |
6. Askofu Mkuu (Mstaafu) Donald Leo Mtetemela |
7. Magdalena Songora |
8. Hamisi Ally Togwa |
9. Askofu Amos J. Muhagachi |
10. Easter Msambazi |
11. Mussa Yusuf Kundecha |
12. Respa Adam Miguma |
13. Prof. Costa Ricky Mahalu |
|
TANZANIA ZANZIBAR (7) |
|
1. Sheikh Thabit Nouman Jongo |
2. Suzana Peter Kunambi |
3. Sheikh Nassoro Mohammed Ibrahimu |
4. Fatma Mohammed Hassan |
5. Louis Majaliwa |
6. Yasmin Yusufali E. H alloo |
7.Thuwein Issa Thuwein |
|
|
|
VYAMA VYOTE VYA SIASA VYENYE USAJILI WA KUDUMU – (WAJUMBE 42) |
|
TANZANIA BARA (28) |
|
1. Hashim Rungwe Spunda |
2.Thomas Magnus Mgoli |
3. Rashid Hashim Mtuta |
4.Shamsa Mwangunga |
5. Yusuf S. Manyanga |
6. Christopher Mtikila |
7. Bertha Ng’angompata |
8. Suzan Marwa |
9. Dominick Abraham Lyamchai |
10. Mbwana Salum Kibanda |
11. Peter Kuga Mziray |
12. Isaac Manjoba Cheyo |
13. Dr. Emmanuel John Makaidi |
14. Prof. Ibrahim Haruna Lipumba |
15. Modesta Kizito Ponera |
16. Prof. Abdallah Safari |
17. Salumu Seleman Ally |
18. James Kabalo Mapalala |
19. Mary Oswald Mpangala |
20. Mwaka Lameck Mgimwa |
21. Nancy S. Mrikaria |
22. Nakazael Lukio Tenga |
23. Fahmi Nasoro Dovutwa |
24. Costantine Benjamini Akitanda |
25. Mary Moses Daudi |
26. Magdalena Likwina |
27. John Dustan Lifa Chipaka |
28. Rashid Mohamed Ligania Rai |
TANZANIA ZANZIBAR (14) |
|
1. Ally Omar Juma |
2. Vuai Ali Vuai |
3. Mwanaidi Othman Twahir |
4. Jamila Abeid Saleh |
5. Mwanamrisho Juma Ahmed |
6. Juma Hamis Faki |
7. Tatu Mabrouk Haji |
8. Fat –Hiya Zahran Salum |
9. Hussein Juma |
10. Zeudi Mvano Abdullahi |
11. Juma Ally Khatibu |
12. Haji Ambar Khamis |
13. Khadija Abdallah Ahmed |
14. Rashid Yussuf Mchenga |
TAASISI ZA ELIMU- (WAJUMBE 20) |
|
TANZANIA BARA |
|
1. Dr. Suzan Kolimba |
2. Prof. Esther Daniel Mwaikambo |
3. Dr. Natujwa Mvungi |
4. Prof. Romuald Haule |
5. Dr. Domitila A.R. Bashemera |
6. Dr. Jasmine Bendantunguka Tiisekwa |
7. Prof. Bernadeta Kilian |
8. Teddy Ladislaus Patrick |
9. Dr. Francis Michael |
10. Prof. Remmy J. Assey |
11. Dr. Tulia Ackson |
12. Dr. Ave Maria Emilius Semakafu |
13. Hamza Mustafa Njozi |
|
TANZANIA ZANZIBAR (7) |
|
1. Makame Omar Makame |
2. Fatma Hamid Saleh |
3. Dr. Aley Soud Nassor |
4. Layla Ali Salum |
5. Dkt. Mwinyi Talib Haji |
6. Zeyana Mohamed Haji |
7. Ali Ahmed Uki |
|
|
|
WATU WENYE ULEMAVU-(WAJUMBE 20) |
|
TANZANIA BARA (13) |
|
1. Zuhura Musa Lusonge |
2. Frederick Msigala |
3. Amon Anastaz Mpanju |
4. Bure Zahran |
5. Edith Aron Dosha |
6. Vincent Venance Mzena |
7. Shida Salum Mohamed |
8. Dr. Henry Mwizengwa Nyamubi. |
9. Elias Msiba Masamaki |
10. Faustina Jonathan Urassa |
11. Doroth Stephano Malelela |
12. John Josephat Ndumbaro |
13.Ernest Njama Kimaya |
|
TANZANIA ZANZIBAR (7) |
|
1. Haidar Hashim Madeweyya |
2.Alli Omar Makame |
3. Adil Mohammed Ali |
4.Mwandawa Khamis Mohammed |
5. Salim Abdalla Salim |
6 Salma Haji Saadat |
7.Mwantatu Mbarak Khamis |
|
VYAMA VYA WAFANYAKAZI-(WAJUMBE 19) |
|
TANZANIA BARA (13) |
|
1. Honorata Chitanda |
2. Dr. Angelika Semike |
3. Ezekiah Tom Oluoch |
4. Adelgunda Michael Mgaya |
5. Dotto M. Biteko |
6. Mary Gaspar Makondo |
7. Halfani Shabani Muhogo |
8. Yusufu Omari Singo |
9. Joyce Mwasha |
10. Amina Mweta |
11.Mbaraka Hussein Igangula |
12. Aina Shadrack Massawe |
13.Lucas Charles Malunde |
|
TANZANIA ZANZIBAR (6) |
|
1. Khamis Mwinyi Mohamed |
2. Jina Hassan Silima |
3. Makame Launi Makame |
4. Asmahany Juma Ali |
5. Mwatoum Khamis Othman |
6. Rihi Haji Ali |
|
|
VYAMA VINAVYOWAKILISHAWAFUGAJI-(WAJUMBE 10) |
|
TANZANIA BARA (7) |
|
1. William Tate Olenasha |
2. Makeresia Pawa |
3. Mabagda Gesura Mwataghu |
4. Doreen Maro |
5. Magret Nyaga |
6. Hamis Mnondwa |
7. Ester Milimba Juma |
|
TANZANIA ZANZIBAR (3) |
|
1. Said Abdalla Bakari |
2. Mashavu Yahya |
3. Zubeir Sufiani Mkanga |
|
|
|
VYAMA VINAVYOWAKILISHAWAVUVI –(WAJUMBE 10) |
|
TANZANIA BARA (7) |
|
1. Hawa A. Mchafu |
2. Rebecca Masato |
3. Thomas Juma Minyaro |
4. Timtoza Bagambise |
5. Tedy Malulu |
6. Rebecca Bugingo |
7. Omary S. Husseni |
|
TANZANIA ZANZIBAR (3) |
|
1.Waziri Rajab |
2. Issa Ameir Suleiman |
3. Mohamed Abdallah Ahmed |
|
VYAMA VYAWAKULIMA-(WAJUMBE 20) |
|
TANZANIA BARA (13) |
|
1. Agatha Harun Senyagwa |
2. Veronica Sophu |
3. Shaban Suleman Muyombo |
4. Catherine Gabriel Sisuti |
5. Hamisi Hassani Dambaya |
6. Suzy Samson Laizer |
7. Dr. Maselle Zingura Maziku |
8. Abdallah Mashausi |
9. Hadijah Milawo Kondo |
10. Rehema Madusa |
11. Reuben R. Matango |
12. Happy Suma |
13. Zainab Bakari Dihenga |
|
TANZANIA ZANZIBAR (7) |
|
1. Saleh Moh’d Saleh |
2. Biubwa Yahya Othman |
3. Khamis Mohammed Salum |
4. Khadija Nassor Abdi |
5. Fatma Haji Khamis |
6. Asha Makungu Othman |
7. Asya Filfil Thani |
|
|
|
WATU WENYE MALENGO YANAYOFANANA – (WAJUMBE 20) |
|
TANZANIA BARA (14) |
|
1. Dr. Christina Mnzava |
2. Paulo Christian Makonda |
3. Jesca Msambatavangu |
4. Julius Mtatiro |
5. Katherin Saruni |
6. Abdallah Majura Bulembo |
7. Hemedi Abdallah Panzi |
8. Dr. Zainab Amir Gama |
9. Hassan Mohamed Wakasuvi |
10. Paulynus Raymond Mtendah |
11. Almasi Athuman Maige |
12. Pamela Simon Massay |
13. Kajubi Diocres Mukajangwa |
14. Kadari Singo |
TANZANIA ZANZIBAR (6) |
|
1. Yussuf Omar Chunda |
2. Fatma Mussa Juma |
3. Prof. Abdul Sheriff |
4. Amina Abdulkadir Ali |
5. Shaka Hamdu Shaka |
6. Rehema Said Shamte |
Imetolewa na:
Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais,
Ikulu.
Dar es Salaam

- Feb 06, 2014
HOTUBA YA MHESHIMIWA JAKAYA MRISHO KIKWETE, RAIS WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA KWENYE KIKAO CHA BARAZA LA VYAMA VYA SIASA, UKUMBI WA MIKUTANO WA KIMATA...
Soma zaidiHotuba
Ndugu Peter Mziray, Mwenyekiti wa Baraza la Vyama vya Siasa;
Ndugu Vuai Ali Vuai, Makamu Mwenyekiti wa Baraza la Vyama vya Siasa;
Mheshimiwa Jaji Francis Mutungi, Msajili wa Vyama vya Siasa;
Ndugu Wenyeviti wa Vyama vya Siasa;
Ndugu Wajumbe wa Baraza la Vyama Siasa;
Wageni Waalikwa;
Mabibi na Mabwana;
Utangulizi
Nakushukuru ndugu Peter Mziray, Mwenyekiti wa Baraza la Vyama vya Siasa na viongozi wenzako kwa kunishirikisha kwenye kikao hiki maalum cha Baraza na kwa maelezo mazuri ya utangulizi. Tutayatafakari ya kufanyika yafanyike. Nawapongeza kwa uamuzi wenu wa busara wa kuzungumzia nafasi ya vyama vya siasa katika Bunge Maalum la kutunga Katiba. Jambo hili ni muhimu kwa uhai, maendeleo na ustawi wa nchi yetu na watu wake. Mmeonesha moyo wa uzalendo na ukomavu wa kisiasa wa hali ya juu
Tangu Baraza hili la vyama vya siasa lizinduliwe mwezi Mei, 2010, nimekuwa nikifuatilia kwa karibu shughuli zake na jinsi linavyofanya kazi. Kwa kweli nimeridhishwa na hatua mliyopiga. Ndiyo maana mliponiita sikusita kuja. Nawaahidi kuwa nitaendelea kufanya hivyo katika siku zijazo ili mradi tu nafasi iwepo.
Serikali Kuimarisha Uwanja wa Siasa
Ndugu Wajumbe;
Mtakubaliana nami kuwa Tanzania imepiga hatua kubwa katika kujenga na kuendeleza demokrasia ya vyama vingi na ushindani wa kisiasa. Kuwepo kwa vyama 21 vyenye usajili wa kudumu vilivyo huru kuendesha shughuli zao na Baraza la Vyama vya Siasa ni kielelezo tosha cha ukweli huu. Wazo la kuwa na Baraza hili liliibuka wakati wa mchakato wa kutatua mgogoro wa kisiasa wa Zanzibar uliozuka baada ya Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2000. Kamati ya Pamoja ya Mwafaka iliyokuwa na wajumbe kutoka CCM na CUF iliundwa ili kutafuta suluhu ya mgogoro ule. Mojawapo ya mambo ambayo Kamati hiyo ilipendekeza ni kuundwa kwa chombo kitachowezesha viongozi wa vyama vya siasa kukutana mara kwa mara kujadili masuala ya kisiasa ili kuepusha migogoro ya kisiasa.
Baada ya Baraza kuundwa, mwaka 2009, Serikali ikaona haja ya kupanua wigo wa ushiriki na kukifanya chombo hiki kuendesha kazi zake kwa mujibu wa Sheria. Matokeo yake Wenyeviti wa vyama vyote vya siasa wakajumuishwa kufuatia marekebisho ya Sheria ya Vyama vya Siasa yaliyofanyika mwaka 2009. Baraza la Vyama vya Siasa likatambulika kisheria na majukumu yake kuorodheshwa katika Sheria husika. Ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa ikapewa jukumu la kuratibu na kugharimia shughuli za Baraza la Vyama vya Siasa.
Mabibi na Mabwana;
Nimeamua kueleza chimbuko la Baraza la Vyama vya Siasa, ili Wajumbe wa Baraza na watu wote wanaonisikiliza wajue kwamba Baraza hili limetokeaje kuwepo na lina nafasi gani katika jamii na siasa za Tanzania. Ni chombo kilichotokana na mafunzo tuliyopata katika migogoro ya kisiasa huko nyuma. Baraza hili ndicho chombo ambacho kikitumiwa vizuri na vyama vya siasa matatizo na malalamiko yao na masuala mengine ya kisiasa yana mahali pa kujadiliwa na kupatiwa ufumbuzi. Aidha, ni jukwaa linalotoa fursa kwa vyama vya siasa kuzungumzia masuala mbalimbali yenye maslahi kwa taifa na kukubaliana kuhusu nini vyama vyenyewe vifanye au vishauri yafanyike na mamlaka husika. Ushauri unaotolewa unawasilishwa Serikalini kupitia Ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa ambayo ndio Sekretarieti ya Baraza hili.
Hakuna chombo kingine zaidi ya Baraza hili kinachowakutanisha viongozi wote wa kitaifa wa vyama vya siasa kujadili masuala ya kisiasa yenye maslahi ya kitaifa. Kwa kuzingatia nafasi yake na majukumu ya Baraza hili, nawasihi viongozi wenzangu hususan Wenyeviti wa vyama vya siasa tulipe uzito na tulitumie ipasavyo. Nawaomba tuwe tunashiriki kwa ukamilifu katika vikao na shughuli za Baraza. Natambua kwamba kwa vile Baraza linajumuisha vyama vyote hata Mwenyekiti wa Chama kidogo anaweza kuongoza Baraza inaweza kutokupendeza kwa vyama vikubwa. Si jambo la ajabu wala si jambo baya ndiyo maana na faida ya demokrasia. Wale wanaotoka vyama vikubwa wasichukie, wakifanya hivyo wanakiuka kanuni moja ya msingi ya uongozi nayo ni “kiongozi mzuri pia huwa ni mfuasi mzuri”. Hata mdogo analo la maana la kuwanufaisha wote wadogo na wakubwa. Naamini Baraza likitumika vizuri litatunufaisha wote: vyama vyote, nchi yetu na wananchi wote.
Mimi na Mheshimiwa Ali Mohamed Shein, Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi kwa nafasi zetu hatushiriki moja kwa moja katika mikutano ya Baraza hili. Pamoja na hilo bado tunalitambua, tunalithamini na tunayachukulia maamuzi ya Baraza hili kwa uzito unaostahili. Ndiyo maana Chama changu kimemteua kiongozi mzito anayenifuata kwa madaraka yaani Makamu Mwenyekiti, ndugu Philip Mangula kuwa Mjumbe wa Baraza. Kutoka Zanzibar tumemteua Naibu Katibu Mkuu wa CCM, Ndugu Vuai Ali Vuai.
Kwa kweli ingependeza sana kama viongozi wa vyama vingine nao wangetoa uzito unaostahili kwa Baraza hili. Natoa rai kwa viongozi wakuu wa vyama vya siasa, hususan wenyeviti kwa wao wenyewe kuwa Wajumbe wa Baraza hili adhimu ili kulipa uzito na hadhi stahiki. Baraza hili lilianzishwa kwa ajili yetu, kujadili masuala ya kuimarisha na kuboresha uwanja wa siasa nchini na kuweka mazingira na uwanja ulio huru na sawa. Kusudi la kutaka wenyeviti wote wa kitaifa wa vyama vya siasa wawe wajumbe wa Baraza ni kuhakikisha kuwa Baraza linakuwa na uwakilishi wa watu wenye mamlaka kamili kufanya maamuzi kwa niaba ya vyama vyao. Ni muhimu sote tuone hoja hiyo na kuitumia fursa inayotolewa na Baraza. Napenda kuwahakikishia ndugu wajumbe kuwa Serikali itaendelea kusikiliza na kuheshimu ushauri wa Baraza hili kwani ni chombo muhimu sana kwa mustakabali wa ustawi wa siasa na maendeleo ya nchi yetu.
Ndugu Wajumbe wa Baraza la Vyama vya Siasa;
Jambo lingine muhimu tunaloendelea kufanya ni kuimarisha Ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa ili iweze kumudu vyema majukumu yake. Mwaka jana (2013) niliidhinisha muundo mpya wa Ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa wenye vitengo vingi kuliko ilivyokuwa kabla ya hapo. Muundo mpya unaoongozwa na watumishi wenye taaluma nyingine mbalimbali badala ya kutegemea wanasheria peke yake. Changamoto zinaongezeka na mazingira ya kufanya kazi yanabadilika, hivyo Ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa itafaidika na kuwa na watumishi wa kada nyingine kama vile wa sosholojia, sayansi ya siasa na kadhalika.
Ili kuhakikisha ufanisi zaidi, Serikali imedhamiria kuongeza bajeti ya ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa katika mwaka ujao wa fedha. Bila ya kufanya hivyo tutakuwa hatukufanya kitu cha maana. Ofisi haitaweza kutimiza wajibu wake. Kwa kweli itakuwa ni kuwaonea kuwadai wafanye zaidi.
Ndugu Mwenyekiti na Wajumbe wa Baraza la Vyama vya Siasa;
Nimeelezwa na Msajili wa Vyama vya Siasa kuwa, jambo moja linaloikwaza ofisi yake ili waweze kutimiza ipasavyo jukumu lao la kuwa mlezi wa vyama vya siasa nchini ni mfumo wa Sheria ya Vyama vya Siasa. Nimeelezwa kuwa Sheria hii imeweka adhabu moja tu ambayo ni kukifuta Chama kinachofanya makosa yaliyoainishwa katika Sheria badala ya kutafuta taratibu za kurekebisha. Kwa maoni yake Sheria haitoi nafasi ya kutosha ya kuvilea vyama vikue, vikomae na vijiepushe na migogoro ya kisiasa ndani ya vyama na ndani ya jamii. Kwa sababu hiyo, inamfanya Msajili aonekane kuwa ni mtu wa kutoa vitisho vya kufungia vyama. Kwa maoni yake hatuna budi kuangalia sheria hiyo upya ili iweze kushughulikia changamoto hizo.
Naiona hoja ya Msajili na nampongeza sana kwa kuliona jambo hilo. Leteni mapendekezo yenu tuyatazame ili hatua zipasazo zichukuliwe. Pamoja na hayo usisubiri sheria. Mlezi hutoa ushauri na kusaidia kupata ufumbuzi wa mambo mbalimbali yanayowatatiza viongozi na wanachama wa vyama vya siasa. Usisite kututembelea mara kwa mara kuzungumza nasi na kutushauri unavyoona inafaa. Itasaidia sana wakati tunasubiri Sheria kufanyiwa marekebisho. Nafurahi kwamba kazi hiyo unaifanya. Tafadhali endelea. Pia usisite kutuita wote au mmoja mmoja unapoona inafaa kufanya hivyo.
Nimeambiwa mchakato wa kupitia upya Sheria hiyo na ile ya Gharama za Uchaguzi umeanzishwa na Ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa. Bila ya shaka marekebisho ya Sheria ya Vyama yatasaidia kuboresha uratibu wa shughuli za kisiasa hapa nchini bila kuingilia uhuru wa vyama vya siasa. Vilevile marekebisho ya Sheria ya Gharama za Uchaguzi yatasaidia kuhakikisha wananchi wetu wanachagua viongozi kwa kuzingatia uwezo wao, mwenendo na ubora wa sera za vyama vyao na si uwezo wao wa kifedha. Nimefurahi na nimefarijika sana na hatua hiyo. Ongezeni kasi ya kukamilisha zoezi hilo.
Ndugu Washiriki;
Naomba kurudia tena kusema kuwa tunafanya hayo yote ili kuimarisha demokrasia ya vyama vingi na ushindani wa kisiasa nchini. Kwetu sisi Serikalini, vyama vya siasa ni wadau muhimu wa maendeleo ya nchi yetu na watu wake. Kwa maana hiyo tunapenda vyama viwe na uwezo wa kutekeleza wajibu huo. Kinyume chake, yaani vyama vinaweza kugeuka na kuwa wakala wa kurudisha nyuma maendeleo. Hii haikubaliki, itashangaza na kusikitisha.
Mada ya Kikao
Ndugu Mwenyekiti;
Kama wote mnavyofahamu, nchi yetu ipo katika mchakato wa kuandika Katiba Mpya. Hatua inayofuatia sasa ni Bunge Maalum la Katiba kukutana na kujadili Rasimu ya Pili na kuamua ipasavyo. Kazi ya uteuzi wa Wajumbe 201 wa kuungana na Wabunge na Wawakilishi katika Bunge hilo imekamilika na kesho watatangazwa. Ilikuwa kazi ngumu sana. Watu wengi wazuri walipendekezwa hivyo hujui umchague nani na umuache nani. Kwa vile hatuwezi kuwapeleka wote basi tumewateua hao 201 na kuwaacha maelfu ya watu wazuri. Kama wote wanaofaa wangechukuliwa nchi ingenufaika sana. Lakini hatuwezi kuwa na Bunge la watu 5,000 hata China haifanyi hivyo. Ilikuwa hapana budi kuchagua baadhi yao tu. Kwa ajili hiyo nawasihi wale wote wasioteuliwa wasisononeke. Hawajapungukiwa sifa ila nafasi hazitoshi.
Ndugu Wajumbe;
Wiki iliyopita nilitembelea ukumbi wa Bunge Dodoma na kujionea mwenyewe maandalizi ya Ukumbi na vifaa unavyoendelea. Mambo yanakwenda vizuri. Nimeelezwa kuwa ifikapo tarehe 10 Februari, 2014 kila kitu kitakuwa tayari na majaribio kufanywa ya vifaa vilivyofungwa. Nimeona tujipe wiki moja baada ya hapo ili tuweze kurekebisha panapostahili. Kwa ajili hiyo nimekubaliana na Rais wa Zanzibar niangalie uwezekano wa kuliitisha Bunge Maalum tarehe 18 Februari, 2014. Tutaitangaza rasmi siku hiyo kupitia gazeti la Serikali.
Bunge la Katiba ndilo lenye mamlaka ya kutunga Katiba mpya ya nchi yetu. Hatua zote zilizopita ni za kutoa mapendekezo jukumu ambalo Tume ya Mabadiliko ya Katiba imelikamilisha vyema. Ipo Rasimu ya Katiba itakayofikishwa kwenye Bunge Maalum kujadiliwa na kufanyiwa uamuzi. Ingekuwa Bunge la kawaida au Baraza la Wawakilishi, Rasimu ya Katiba ndiyo Muswada wa Sheria utakaofikishwa Bungeni na kwenye Baraza.
Wajumbe wa Bunge hilo watambue kuwa wana dhamana isiyokuwa na mfano wake kwa nchi yetu na Watanzania wenzao kwa jumla. Wanalo jukumu la kuwapatia Katiba nzuri itakayodumu kwa zaidi ya miaka 50 ijayo. Katiba itakayoimarisha Muungano badala ya kuudhoofisha. Katiba itakayodumisha umoja, amani na utulivu nchini badala ya kuvuruga. Vilevile Katiba itakayoweka mazingira mazuri ya kisiasa, kijamii na kiuchumi na kuongeza kasi ya maendeleo ya nchi yetu na ustawi wa watu wake kwa miaka mingi ijayo. Ili haya yafanyike ni vyema Wajumbe wajue vyema kinachopendekezwa, wapambanue kinachofaa na kisichofaa, na kubwa zaidi, watangulize maslahi ya taifa mbele kuliko maslahi yao binafsi au ya makundi yao.
Ndugu Mwenyekiti na Wajumbe wa Baraza la Vyama vya Siasa;
Mabibi na Mabwana;
Vyama vya siasa vina nafasi ya pekee katika majadiliano ya Bunge Maalum la Katiba na katika mchakato mzima wa kutunga Katiba mpya. Mafanikio ya mchakato huu yatategemea sana kauli, mwenendo na matendo ya vyama vya siasa. Ukweli ni kwamba vitendo na kauli za viongozi, wanachama na wafuasi wa vyama vya siasa ndivyo vitakavyojenga au kubomoa, na ndivyo vitakavyowezesha au kukwamisha mchakato huu.
Mimi nataka vyama vijenge na kuwezesha mchakato ufanikiwe na Katiba mpya ipatikane kwa wakati tunaoutarajia sote. Yaani tufanye uchaguzi wa Serikali za Mitaa na Uchaguzi Mkuu 2015 tukiwa na Katiba Mpya. Mimi naamini kwa dhati ya moyo wangu kuwa vyama vya siasa vikiamua Katiba ipatikane, itapatikana. Hivyo basi, kama vyama vya siasa vitaamua kishirikiana kwa dhati, na kwa nia njema tutapata Katiba mpya bila kelele wala mikwaruzo. Kama vyama vya siasa vitatambua kuwa tunatengeneza jambo la kutunufaisha wote, yaani nchi yetu na watu wake na siyo maslahi binafsi ya vyama vyao itakuwa hatua kubwa ya mwanzo ya kufanya kazi ya Bunge kuwa rahisi. Pia kama vyama vitakubali kuongozwa kwa nguvu ya hoja alizotoa Mjumbe na siyo Mjumbe anatokea Chama gani au kundi gani, tutapata Katiba yenye maslahi kwa taifa letu. Tutapata Katiba itakayoridhiwa na wananchi bila ya taabu.
Ninaposema hayo sina maana kuwa vyama vya siasa au Wajumbe wanaotokana na vyama wasiende Bungeni na maoni yao au na misimamo ya vyama vyao. La hasha! Nikifiria hivyo sitakuwa mkweli kwangu mwenyewe. Nitakuwa najidanganya. Ninachosema ni kwamba, pamoja na kuwa na maoni, mwongozo na misimamo ya vyama vyenu, lazima muwe na unyumbufu wa mawazo kwa kiasi fulani ili mpate nafasi ya kusikiliza hoja za wengine zinazotofautiana na zenu, kuzivumilia na kuzikubali pale ambapo kuna mantiki. Kwa lugha ya Kiingereza natoa wito wa “flexibility”. Muungwana hukubali mawazo bora na yenye ukweli ya watu wengine. Hata wengine nao wanaweza kuwa na mawazo bora kuliko yako. Muungwana ni yule anaekiri ukweli huo na yuko tayari kupokea mawazo bora ya watu wengine hata kama watu hao hawapendi. Kama tutakwenda kwenye Bunge na azimio la kupinga kila wazo litakalosemwa na mtu fulani, hatutafikia kupata Katiba mpya. Haitawezekana.
Ndugu Mwenyekiti wa Baraza la Vyama vya Siasa;
Ndugu Wajumbe;
Mtakubaliana nami kuwa Baraza hili na hasa ninyi viongozi mliokusanyika hapa leo mnayo dhamana na jukumu la kipekee la kuipatia nchi yetu Katiba nzuri yenye maslahi kwa nchi yetu na inayojali maslahi ya watu na kukubalika na watu wote. Katiba ambayo itakapotangazwa watu waseme naam, hii ni Katiba inayojali maslahi ya nchi zetu mbili zilizoungana na kuwa nchi moja miaka 50 iliyopita. Katiba inayojali maslahi ya raia wa Tanzania ndani ya Muungano na ule upande wa Muungano anakoishi au unakotoka kwa asili yake au historia yake.
Ni kwa kutambua umuhimu huu wa vyama vya siasa ndiyo maana nilitoa wito kwa vyama vya siasa kukutana na kuzungumza miongoni mwenu. Ningependa mzungumze kuhusu namna bora ya kujadili rasimu ili mwishowe tupate Katiba nzuri. Ningependa mzungumze jinsi vyama vya siasa vitakavyoshirikiana hasa kutafuta ufumbuzi wakati majadiliano yanapokuwa magumu kwa baadhi ya mambo.
Si vyema mkadhani jawabu ni kushindana mpaka mwenye nguvu ashinde. Mnaweza kushindwa wote. Na mkishindwa, mjue sote tumeshindwa na nchi imekwama. Msikubali kuifikisha nchi hapo. Tuzidi kumuomba Mola atusaidie tusifike hapo. Lakini, Mwenyezi Mungu husaidia wanaojisaidia. Na sisi tutengeneze namna bora ya kujisaidia ili Mungu akitia mkono wake mambo yanajipa. Lililoonekana kuwa zito linakuwa jepesi kama kanda la usufi.
Ndugu Mwenyekiti wa Baraza la Vyama vya Siasa;
Nawaamini nyote mliopo hapa mnaweza kutengeneza mfumo huo na taratibu hizo. Sina majibu wala maelekezo ya mfumo huo ni upi. Nimekuja kutoa rai. Nimekuja kutoa maombi. Majibu mnayo ninyi. Mimi nasubiri jibu jema kama wanavyosubiri Watanzania wengine. Nawaomba myatafakari ninayosema na myape uzito unaostahili.
Mwisho
Narudia kuwashukuru Mwenyekiti wa Baraza la Vyama vya Siasa na Msajili wa Vyama vya Siasa, kwa kunialika kuja kuongea na viongozi wa vyama vya siasa kupitia Baraza hili. Ni matumaini yangu kuwa, miaka ishirini na mbili tangu mfumo wa vyama vingi uanzishwe tena hapa nchini kwetu mwaka 1992, vyama vya siasa vimekomaa na vinaelewa nafasi na umuhimu wake katika jamii. Hivyo basi, tutegemee matokeo mema katika mkutano wenu huu wa kihistoria na mchakato utakaozaa matunda mema katika Bunge Maalum la Katiba.
Kabla ya kumaliza napenda kurudia kuwahakikishia kuwa mimi na Serikali ninayoiongoza tutaendeleza ushirikiano wetu na Baraza. Tuko tayari kuitikia wito wa kuja kuongea nanyi wakati wowote. Baada ya kuyasema maneno yangu mengi, nawatakia kila heri katika Mkutano wenu.
Mungu Ibariki Afrika!
Mungu Ibariki Tanzania!
Ahsanteni kwa kunisikiliza.

- Feb 03, 2014
HOTUBA YA MHESHIMIWA JAKAYA MRISHO KIKWETE RAIS WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WAKATI WA SHEREHE YA KUADHIMISHA SIKU YA SHERIA NCHINI TAREHE 3 FEBRUARI, 20...
Soma zaidiHotuba
Mheshimiwa Chande Othman, Jaji Mkuu wa Tanzania;
Mheshimiwa Spika wa Bunge la Jamhuri wa Muungano
wa Tanzania;
Waheshimiwa Majaji Wakuu Wastaafu;
Mheshimiwa Dkt. Asha-Rose Migiro, Waziri wa Katiba
na Sheria;
Mheshimiwa Angella Kairuki, Naibu Waziri wa Katiba na Sheria;
Waheshimiwa Majaji wa Rufani;
Mheshimiwa Jaji Mkuu wa Zanzibar, Jaji Kiongozi na Majaji
wa Mahakama Kuu;
Waheshimiwa Mabalozi mliopo;
Rais wa Chama cha Mawakili Tanzania;
Mahakimu na Watumishi wa Mahakama;
Wageni Waalikwa Mabibi na Mabwana;
Utangulizi
Mheshimiwa Jaji Mkuu;
Nakushukuru sana Mheshimiwa Jaji Mkuu kwa kunialika kwa mara nyingine tena kuja kujumuika nanyi kwenye maadhimisho ya Siku ya Sheria Nchini na ya Mahakama kuanza kazi mwaka huu. Ni jambo la busara kuwa siku hii inaadhimishwa kila mwaka. Inatupa fursa nzuri sisi tusio wanasheria kujifunza masuala mengi yahusuyo sheria na utoaji haki nchini.
Naomba na mimi niungane na wenzangu walionitangulia kukupongeza na kukushukuru Mheshimiwa Jaji Mkuu, Waheshimiwa Majaji, Mahakimu na watumishi wote wa Mahakama kwa kazi nzuri mliyofanya mwaka jana. Nami nawatakia mafanikio mema na utendaji mzuri zaidi katika mwaka huu wa 2014.
Kaulimbiu ya Mwaka Huu
Mheshimiwa Jaji Mkuu;
Kama ilivyo kawaida yenu, kaulimbiu ya maadhimisho ya mwaka huu inayosema “Utendaji haki kwa wakati: Umuhimu wa Ushiriki wa Wadau” imebeba ujumbe mzito na muhimu kwa wadau wa utoaji haki nchini. Kwa jumla inatukumbusha kuwa ili haki iwe na maana, ni lazima ipatikane kwa wakati. Msemo wenu maarufu wa “Justice delayed is justice denied” unaelezea kwa ufasaha dhana hii. Ni ukweli usiopingika kwamba ili haki ipatikane kwa wakati, ushiriki kwa ukamilifu wa wadau wote ni jambo la lazima. Wadau hao ni pamoja na Mahakama, Ofisi ya Mwanasheria Mkuu, Polisi, TAKUKURU, Mawakili, Serikali na wengineo.
Endapo mmoja wa wadau hao atashindwa kutimiza wajibu wake ipasavyo, haki ya mtu au watu itachelewa kupatikana au itadhulumiwa. Hali hii inatokana na ule ukweli kwamba kila mdau anao wajibu maalum ambao hana budi kuutimiza. Ufanisi wa mmoja unategemea sana utendaji wa mwingine. Ni kama mwili wa binadamu ulivyo, kila kiungo kina nafasi yake, kimoja kisipofanya kazi vizuri siha ya mwili hodhoofika. Ndiyo hivyo ilivyo pia kwa mfumo wa utoaji haki. Mahakama ambapo ni kilele katika mtandao au mfumo wa utoaji haki haikamati wahalifu, haipelelezi mazingira ya utendaji kosa, haitayarishi wala haiendeshi mashtaka. Hivyo basi, kazi ya Polisi, TAKUKURU na Mkurugenzi wa Mashtaka husaidia sana kuharakisha utoaji haki, Mahakama ina uharaka wa kusikiliza kesi hasa pale ambapo upelelezi umekamilika mapema na waendesha mashtaka wako tayari, na pia, uharaka wa upatikanaji wa nakala ya hukumu ili mtu aweze kukata rufaa kwa wakati.
Mheshimiwa Jaji Mkuu;
Masuala mengi kuhusu kaulimbiu ya mwaka huu umeyaeleza vizuri pamoja na wazungumzaji waliotangulia. Jambo kubwa na muhimu ambalo limejitokeza ni kuwa ushiriki na ushirikiano wa wadau ni muhimu sana katika utoaji haki kwa wakati. Mahakama ni kilele katika mfumo wa utoaji haki nchini. Lakini, Mahakama haipelelezi, haifikishi wahalifu mahakamani, haiendeshi mashtaka. Hasikilizi mashauri na hutoa kutoa uamuzi kuhusu upande upi una haki. Hivyo, wale wapelelezi na waendesha mashtaka na wanaotetea wasipofanya kazi yao ipasavyo haki huchelewa. Hii ina maana kuwa Polisi wahakikishe wahalifu wanakamatwa, upelelezi unafanyika kwa makini na kesi zao zinapelekwa kwa Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashtaka ili zipelekwe Mahakamani.
Hivyo kwa TAKUKURU nao wahakikishe kuwa upelelezi unafanywa vizuri ili shauri linapofikishwa Mahakamani halichelewi kwa sababu ya upelelezi kutokukamilika. Mkurugenzi wa Mashtaka nae ahakikishe shauri analolipeleka limeandaliwa vizuri ili lichukue muda mfupi kusikilizwa na kuamuliwa. Weledi na uadilifu wa Polisi, TAKUKURU na DPP ni mambo ya msingi sana. Hivyo hivyo, Mawakili nao wana nafasi yao. Naambiwa kuna wakati shauri huaihirishwa kwa sababu ya wakili wa utetezi kushindwa kufika Mahakamani. Ukiacha sababu ya kuumwa lakini wakati mwingine ni kwa sababu ya kuwa na kesi mahali pengine.
Nafasi ya Mahakama
Mheshimiwa Jaji Mkuu;
Ni ukweli usiopingika kuwa Mahakama inayo nafasi ya pekee katika mfumo wa kutoa haki nchini. Nakubaliana na wale wanaouita Mhimili huu wa dola kuwa ni “The temple of Justice” kutokana na ukweli kwamba watu wanapokuja Mahakamani wanategemea kutendewa haki. Hakuna mahali pengine pa kukimbilia kutafuta haki zaidi ya Mahakamani. Wanaweza wasijue sheria za vitabuni, lakini wakajua haki yao. Hivyo, Waheshimiwa Majaji, Mahakimu na watumishi wengine wa Mahakama mnayo dhamana na wajibu mkubwa wa kusimamia sheria kwa haki. Ili haki itolewe bila upendeleo wa aina yoyote ile.
Matarajio ya wananchi ni kuwa kesi zisicheleweshwe kusikilizwa na kuamuliwa. Pale ambapo upelelezi umekamilika na mashtaka yametayarishwa vizuri kuahirishwa kusikilizwa kwa kesi huzaa manung’uniko. Pale shauri linapoamuliwa kutolewa kwa nakala ya hukumu ili anayetaka kukata rufaa afanye hivyo ni jambo la muhimu. Kinyume chake watu wanakata tamaa na kuamua kuchukua njia za mkato ambazo madhara yake ni makubwa. Wanakuwa hawana mahali pengine pa kupeleka mashtaka yao. Ndiyo maana nakubaliana na kauli yako Mheshimiwa Jaji Mkuu kwamba tusiiache misingi ya haki ikamomonyoka katika jamii yetu mpaka ukafika wakati watu wakaamini kwamba bila kutumia jambia hakuna haki. Naomba muendelee na kazi nzuri muifanyayo ili muwe kimbilio la uhakika kwa yeyote ambaye anajiona haki yake inadhulumiwa.
Mheshimiwa Jaji Mkuu;
Nimefarijika sana kusikia kwamba mmejiwekea utaratibu mzuri na misingi ya ushirikiano wa mawasiliano baina yenu na wadau wengine kwa ajili ya kuboresha utendaji wenu. Utaratibu huo utasaidia sana kuhakikisha upelelezi wa mashauri unakamilika haraka na haki inapatikana kwa wakati. Vilevile nawapongeza kwa kuelewa umuhimu wa kuhuisha sheria, kanuni na taratibu mara kwa mara ili kukidhi mahitaji ya wakati. Bila shaka hatua zote hizi zitasaidia sana kutatua changamoto ya siku nyingi ya ucheleweshwaji wa kesi.
Wajibu wa Serikali
Mheshimiwa Jaji Mkuu;
Napenda kukuhakikisha kuwa sisi Serikalini tutaendelea kutimiza wajibu wetu ili Mahakama na wadau wengine wa utoaji haki wafanye kazi ipasavyo. Kwanza tumechukua na tunaendelea kuchukua hatua kadhaa kufanya marekebisho ya sheria mbalimbali kufuatia tafiti na mapendekezo ya Tume zilizoundwa kuangalia mifumo yetu ya kutoa haki kwa lengo la kuiboresha. Kazi hiyo tunaendelea nayo. Tumeanza na kurekebisha sheria na mifumo ya utoaji haki na kuweza kutenganisha upelelezi na uendeshaji wa mashtaka.
Pili, tumeanza kuchukua hatua thabiti kuongeza bajeti ya Mahakama ili muweze kutimiza kwa ufanisi zaidi wajibu wenu. Mwaka huu wa fedha kwa mfano, tumetenga shilingi bilioni 86 kwenye Mfuko wa Mahakama na shilingi bilioni 42.7 kwa ajili ya maendeleo. Kiasi hiki ni kikubwa maradufu ukilinganisha na mwaka wa fedha uliopita ambapo zilitengwa shilingi bilioni 57 kwa shughuli zote. Pamoja na hatua hii muhimu tumejitahidi sana kuwezesha Mahakama kuongeza rasilimali watu, yaani Majaji Mahakimu na watumishi wengine. Idadi ya Majaji wa Rufani sasa imefikia 16 kutoka 9 waliokuwepo mwaka 2005, na wa Mahakama Kuu ni 69 kutoka 35 waliokuwepo mwaka 2005. Nilishakubali Majaji 20 wapya waajiriwe. Nileteeni mapendekezo niteue. Vilevile idadi ya Mahakimu imeongezeka zaidi na kufikia 672 na tayari kibali cha kuajiri wengine 300 kimeshapatikana. Hivi sasa mchakato wa ajira ya wahitimu wa sheria katika Mahakama za Mwanzo unaendelea.
Kufuatia mapendekezo ya Kamati za Jaji Mrosso na ya Jaji Lubuva, tumekamilisha mchakato wa kutenganisha shughuli za kutenda haki na utawala kwa kuanzisha nafasi ya Mtendaji Mkuu. Sasa hivi naambiwa pamekuwa na nafuu sana kwani mzigo waliokuwa nao Majaji kwenye masuala ya utawala haupo tena. Nasikitika kuwa idhini ya Muundo wa Mahakama umechelewa kuliko kawaida. Naahidi kuwa litakamilika wiki hii. Tumeendelea kuziongezea uwezo wa rasilimali fedha, vitendea kazi na nguvu kazi Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashtaka na TAKUKURU.
Mheshimiwa Jaji Mkuu;
Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali nayo pia imefanyiwa marekebisho makubwa. Shughuli za Wizara zilizokuwa zimechanganyika na zile za Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali sasa hivi zimetenganishwa. Wizara imebaki na jukumu lake la kusimamia sera na Ofisi ya Mwanasheria Mkuu inafanya shughuli za kisheria. Hatukuishia hapo. Tumefikia hatua nzuri ya kutenganisha shughuli za upelelezi na za kuendesha mashtaka. Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashtaka imebaki na majukumu yake ya kusimamia mashtaka na Polisi, TAKUKURU na wengineo wanabaki na majukumu yao ya ukamataji wa wahalifu na upelelezi. Tunafanya yote haya kuboresha mifumo ya kutoa haki nchini.
Mwisho
Mheshimiwa Jaji Mkuu;
Mabadiliko yaliyofanyika yana lengo zuri la kuboresha taratibu zetu za kutoa haki nchini. Jambo kubwa ni mabadiliko kwa jamii na watendaji wenyewe. Watoaji haki ni lazima wajipime kwa matakwa na mahitaji yao. Endeleeni kutekeleza majukumu yenu mkielewa kwamba wananchi na jamii wanawategemea katika kuhakikisha kwamba haki inatolewa kwa wakati. Wadau wa utoaji haki muendelee kutimiza wajibu wenu wa kutatua migogoro, kuwapatanisha wananchi na kuwaadhibu wahalifu ili amani na utulivu nchini mwetu idumu. Watu wawe na maelewano na waishi bila wasiwasi.
Naomba kila mmoja wetu ashiriki kikamilifu kuhakikisha lengo letu linafikiwa. Kila mmoja wetu anayo nafasi yake, hili siyo jukumu la polisi peke yao, Mwanasheria Mkuu au Jaji Mkuu. Ni jukumu la wote. Basi mwaka huu tujitahidi kufanya vizuri zaidi, kila mtu afanye hivyo mahali alipo. Bila shaka haki itapatikana kwa wakati.
Asanteni sana kwa kunisikiliza.

- Jan 22, 2014
Hotuba ya Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, wakati ufunguzi wa kongamano la viongozi wa dini kuhusu matumizi ya rasilim...
Soma zaidiHotuba
Waheshimiwa Viongozi wa Dini;
Waheshimiwa Mawaziri;
Waheshimiwa Wakuu wa Mikoa;
Ndugu Makatibu Wakuu;
Wageni Waalikwa;
Mabibi na Mabwana;
Naomba nianze kwa kumshukuru Mwenyezi Mungu, mwingi wa rehema, kwa kutujaalia uzima na kutuwezesha kukutana hapa siku ya leo kujadili matumizi ya rasilimali zetu za gesi asilia, mafuta na madini kwa amani na maendeleo ya nchi yetu. Kwa namna ya pekee nawashukuru viongozi wa dini kwa kunishirikisha kwenye Kongamano hili muhimu na la aina yake. Mmenipa heshima kubwa ambayo sikuitegemea. Asanteni sana.
Nawapongeza sana kwa uamuzi wenu wa busara wa kuandaa Kongamano hili. Mmedhihirisha kwa vitendo uhodari wenu wa kutekeleza jukumu lenu la msingi la kulea taifa letu kiroho na kushiriki kikamilifu katika masuala mengine muhimu yahusuyo maendeleo na ustawi wa Tanzania na watu wake. Ninyi ni wazalendo wa kweli. Ni matumaini yangu na ya Serikali ninayoingoza kuwa ubia wa aina hii utaimarishwa na kudumishwa kwa faida ya nchi yetu.
Najua mlianza kwa kukereketwa na athari za matumizi makubwa ya miti kwa matumizi ya nishati jambo ambalo linachangia sana kuharibika kwa mazingira duniani. Mmeishia kwenye Kongamano hili. Lina uwiano kabisa kwani tunakata miti kwa ajili ya kuni na mkaa. Tukitumia gesi itatoa huko. Ni dhamira yetu hiyo.
Ndugu Viongozi wa Dini;
Kongamano hili linafanyika katika kipindi mwafaka kabisa, kipindi ambacho ugunduzi mkubwa wa gesi tayari umefanyika na dalili za kugunduliwa zaidi zipo. Kipindi ambacho hazina ya madini mbalimbali inazidi kugunduliwa na makampuni ya utafiti yanatupa moyo kuwa mambo huenda yakawa mazuri zaidi. Pia, ni kipindi ambacho rasilimali zetu za wanyamapori na misitu zinatishiwa kutoweka. Ni kipindi ambacho wakulima na wafugaji na wafugaji na wahifadhi wa misitu na wanyamapori wanashindania ardhi ya kufanyia shughuli zao. Sasa hivi ni kipindi mwafaka kabisa kukaa chini na kutafakari jinsi gani rasilimali hizi zinaweza kulindwa na kutumika kwa manufaa ya nchi yetu na watu wake wote zikiwanufaisha kule ambako rasilimali hizo zipo na hata kule ambako hazipo.
Ni ukweli usiopingika kuwa Mwenyezi Mungu ameijalia nchi yenye utajiri mkubwa wa rasilimali za asili. Ametujaalia ardhi kubwa yenye rutuba, madini ya aina mbalimbali, misitu na mbuga za wanyama wa kila aina, hali ya hewa nzuri, bahari, maziwa makubwa, mito mingi, watu wengi na kadhalika. Rasilimali hizi, kwa tabia yake, inatakiwa zitumiwe vizuri ili kuboresha hali na maisha ya Watanzania wote sawia na kwa miaka mingi na hata milele. Vinginevyo rasilimali hizi zinaweza kugeuka kuwa chanzo cha mifarakano, magomvi na mauaji. Zinaweza kuwa balaa na kuleta maangamizi nchini badala ya kuwa baraka na neema.
Mifano ipo ya nchi mbalimbali duniani zilizojikuta zina migogoro na vita vya wenyewe kwa wenyewe kutokana na kugombania utajiri wao wa rasilimali za asili. Watu wa nchi hizo wanajuta kuwa na rasilimali ambazo zimekuwa chanzo cha kuhatarisha amani, utulivu, usalama na hata uhai wao. Kwa hapa Tanzania tunashukuru Mungu rasilimali hazijageuka kuwa balaa na tunaomba hilo lisitokee. Tangu Tanganyika ipate uhuru na Zanzibar kufanya Mapinduzi Matukufu na hatimaye nchi zetu mbili kuungana na kuwa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Serikali za awamu zote zimesimamia kwa makini rasilimali za nchi yetu ili ziwanufaishe Watanzania wote. Tumetunga sheria na sera mbalimbali kuhakikisha kuwa lengo letu hilo linatimia.
Hata hivyo, usimamizi wa sheria hizo na utekelezaji wa sera zetu nzuri umekuwa unakabiliwa na changamoto mbalimbali kwa nyakati mbalimbali. Mpaka hapa tulipofika ni umahiri wa viongozi wetu ndiyo uliotuwezesha kuzuia mambo yasiharibike na kugeuka kuwa matatizo makubwa. Tumefanikiwa kiasi chake ingawaje hatujaweza kuzuia kabisa matatizo yasitokee hapa na pale. Taarifa za kugombea rasilimali zimekuwa zinasikika na nyingine zikiwa zimesababisha watu kupoteza maisha, kujeruhiwa na mali kuharibiwa. Tutafanya nini kukomesha hali hiyo isijitokeze, ni jambo ambalo sisi kama taifa, yaani Serikali, wananchi na wadau mbalimbali, wakiwemo viongozi wa dini hatuna, budi kulizungumza na kulipatia ufumbuzi.
Ndugu Viongozi wa Dini;
Nimefarijika sana na uamuzi wenu wa kufanya mkutano huu kuzungumzia rasilimali ya mafuta na gesi. Juhudi za kutafuta mafuta na gesi imeanza tangu ukoloni, zikaendelea katika awamu zote baada ya Uhuru. Shirika la Maendeleo ya Petroli (TPDC) lilianzishwa mwaka 1969 kuongoza juhudi hizo na kusimamia sekta ya mafuta nchini kwa manufaa ya Watanzania wote. Hatujajaaliwa kupata mafuta mpaka sasa lakini tumefanikiwa kupata gesi. Ugunduzi wa kwanza wa gesi asilia ulifanyika Songosongo mwaka 1971 na baadae Msimbati, Mtwara mwaka 1982. Utafutaji na ugunduzi huo uligharimiwa na Serikali yetu na hivyo gesi hiyo ni mali ya Serikali. Baada ya ugunduzi huo makampuni binafsi yalipata shauku ya kutafuta mafuta na gesi nchini.
Mwaka 1980 ikatungwa Sheria ya Utafutaji wa Uzalishaji wa Mafuta kwa nia ya kuweka masharti na utaratibu wa makampuni kushiriki katika utafutaji na uzalishaji wa mafuta na gesi nchini. Pia unatoa mwongozo wa mgawanyo wa mapato baina ya makampuni na Serikali. Sheria hiyo imeendelea kufanyiwa maboresho kwa nyakati mbalimbali kulingana na mahitaji ya wakati husika. Kuanzia mwaka 2007 shughuli za utafutaji wa mafuta na gesi asilia ziliongezeka kwa nguvu na kasi kubwa. Juhudi hizo zilizaa matunda mwaka 2010 kwa uvumbuzi wa kwanza wa gesi katika Bahari Kuu uliofanywa na Kampuni za Orphir na British Gas. Baada ya hapo ugunduzi umeendelea hadi kufikia futi za ujazo trilioni 46.5 za rasilimali ya gesi nchini mpaka sasa. Utafiti unaendelea na matumaini ya kupata gesi zaidi yapo. Kufuatia ugunduzi huo, Tanzania sasa ni moja ya nchi zimazohesabiwa kuwa na gesi nyingi duniani na ni nchi inayovutia wawekezaji wengi katika sekta ya gesi. Kwa sababu hiyo, tukaamua kuifanyia mapitio Sheria ya Utafutaji na Uzalishaji wa Mafuta na Gesi. Mwaka 2013 tumetunga Sera ya Gesi na kurekebisha masharti ya Mkataba wa Kugawana Mapato yatokanayo na gesi (Production Sharing Agreement) na kuongeza mgao wa Serikali.
Ndugu Viongozi wa Dini;
Sera ya Gesi Asilia iliyopitishwa mwezi Oktoba, mwaka jana (2013) imeeleza wazi, tena kwa lugha nyepesi, kuwa gesi ya Tanzania ni mali ya Watanzania wote na itatumika kwa manufaa ya Watanzania wote – wa kizazi hiki na kijacho. Katika matumizi ya gesi, kipaumbele kitakuwa matumizi ya ndani. Msingi wa hoja yetu ni ule ukweli kwamba ukiuza nje gesi yote, unapata mapato peke yake lakini unakosa faida nyinginezo. Ukiitumia ndani unapata mapato na faida nyingine nyingi, kwa mfano, uzalishaji wa umeme, matumizi ya majumbani, kwenye magari na viwandani kuzalisha bidhaa mbalimbali. Hivyo basi mnapoitumia ndani gesi inakuwa kichocheo kikubwa cha maendeleo ya nchi yetu.
Vilevile tupo katika mchakato wa kuandaa sera ya kuwashirikisha zaidi Watanzania (Local Content Policy) ili wanufaike zaidi na rasilimali yao ya gesi. Kwa sasa nimewaagiza TPDC wajiandae kushiriki katika utafutaji wa gesi, uzalishaji wake mpaka inapofika sokoni. Wasiwe wagawaji vitalu tu pekee. Katika sera hiyo mpya pia tunaangalia shughuli zinazoweza kufanywa na Watanzania ili tuone njia bora ya kuwawezesha kushiriki. Kwa sasa tunadhani wanaweza kushiriki kwa urahisi katika utoaji wa huduma kwa kampuni zinazofanya utafiti na uzalishaji wa gesi na mafuta. Wapo walioanza na wanafaidika. Nia yetu ni kuona idadi yao inaongezeka.
Mabibi na Mabwana;
Tumeanza pia mchakato wa kuiboresha TPDC ishiriki katika uwekezaji kwenye sekta ya mafuta na gesi kwa niaba ya Watanzania. Katika utaratibu huo, baadaye TPDC itauza hisa zake kwenye Soko la Mitaji ili Watanzania washiriki moja ka moja katika kumiliki rasilimali hii muhimu.
Ndugu Viongozi wa Dini;
Mambo yote hayo yanafanyika ili kuhakikisha masilahi ya taifa yanalindwa na Watanzania wote wananufaika na rasilimali zao kwa usawa. Changamoto kubwa tunayoiona kuhusu ushiriki wa Watanzania kwenye utafutaji na uzalishaji wa mafuta na gesi ni uwezo mdogo wa fedha, utaalamu na teknolojia tulionao. Fedha zinazohitajika kwenye shughuli ya utafutaji mafuta na gesi, kwa mfano, ni nyingi mno na Watanzania wenzetu hawanazo na hakuna uhakika wa benki iliyo tayari kumkopesha mtu asiyekuwa nacho.
Namna nyingine ni kuwapa maeneo ili wao watafute wabia wawekeze. Lakini, mnapokuwa mnasheria inayoshirikisha ubia baina ya Serikali na mwekezaji, kuamua kuacha Serikali ili badala yake apewe Mtanzania binafsi si uamuzi rahisi sana kuufanya. Mtu binafsi ananufaika mwenyewe wakati Serikali inanufaisha wengi. Ninachokiona nafuu kufanya ni kutumia mwanya wa ushiriki wa TPDC ili tuone baadhi ya hisa ziuzwe kwa Watanzania. Hapa kunakuwa na ubia wa TPDC na wananchi upande mmoja na Serikali upande mwingine.
Jambo lingine tunalolifanya ni kuhakikisha kuwa rasilimali ya gesi inatumika vizuri, kwa manufaa ya kizazi cha sasa na vizazo vijavyo. Tutaanzisha mfuko maalum wa kuhifadhi mapato ya gesi na kuwekewa masharti ya matumizi yake. Tutatunga sheria maalum kwa ajili hiyo na tutafanya hivyo kwaka huu.
Mabibi na Mabwaba;
Kwa upande wa rasilimali ya madini mabadiliko makubwa ya kiuchumi yaliyoanza miaka 1980 katikati, Serikali ilijitoa katika uwekezaji na ikabaki kuwa mhamasishaji na kuweka mazingira mazuri ya uwekezaji. Kufuatia hali hiyo wawekezaji wengi walianza kuja kuwekeza katika maeneo mbalimbali pamoja na utafutaji na uchimbaji wa madini. Serikali ikaweka Sera (1997) na Sheria (1998) ya madini kusimamia sekta hiyo. Ni kweli mapato ya Serikali na fedha za kigeni ziliongezeka kutokana na uzalishaji wa madini. Lakini palikuwa na manung’uniko mengi kutoka kwa wananchi kuwa hawafaidiki sana na rasilimali zao.
Kamati mbalimbali ziliundwa kuangalia tatizo lipo wapi ili jawabu lake litafutwe. Nilipochaguliwa kuwa Rais wa nchi yetu mwaka 2005 niliyakuta manung’uniko hayo na kuamua tuyatafutie jawabu. Mwaka 2006 nikaunda Kamati ya Jaji Bomani ili ichambuwe mapungufu yaliyopo na kutoa mapendekezo ya hatua za kuchukua. Matokeo ya taarifa ya Kamati ile ni Sera Mpya ya Madini (2009) na Sheria Mpya ya Madini (2010). Sera na Sheria hii inalenga kuongeza faida zaidi kwa Serikali na jamii, bila kuwasahau wale wanaozunguka migodi.
Faida hizo ni pamoja na kuhimiza kampuni za uchimbaji wa madini kufungamanisha uchumi kati ya sekta ya madini na nyingine. Vilevile tumewataka waongeze nafasi ya ajira kwa Watanzania na ununuzi wa huduma na bidhaa nchini. Aidha, tumeamua Serikali iwe inapata hisa katika migodi mikubwa itakayoanzishwa siku za usoni. Ndiyo maana tunaendelea kufanya mazungumzo na kampuni zitazochimba uranium na nickel. Hatujamaliza lakini tunakwenda vizuri.
Halikadhalika, Sheria na Sera vimeweka mkazo wa kuendeleza wachimbaji wadogo ambao ni Watanzania tu. Katika kutekeleza hilo, tumeanza kutenga maeneo kwa ajili yao. Changamoto kubwa inayowakabili ni ukosefu wa mitaji, vifaa na utaalamu. Kuhusu fedha, tumeanzisha mfuko wa kuwasaidia na mwaka huu wa fedha tumewatengea jumla ya shilingi bilioni 2.5. Vile vile tunakamilisha taratibu za kuanza kuwakodisha vifaa kupitia ofisi zetu za madini za Kanda.
Jambo lingine kubwa ambalo tunajiandaa kulifanya ili kunufaisha wananchi na nchi yetu ni kutunga Sheria itakayohakikisha kuwa madini mengi yanayochimbwa nchini yanaongezewa thamani hapahapa nchini. Hatua hii itachangia sana kuongeza mapato na fursa ya ajira kwa watu wetu.
Nduvu Viongozi wa Dini;
Nimeyasema haya yote kuwaonesha kuwa Serikali haina mchezo katika usimamizi wa rasilimali zetu za asili. Tunafanya hayo kwa vile tunafahamu kuwa zinaweza kutuletea maendeleo ya haraka. Lakini pia zinaweza kusababisha nchi yetu kuingia kwenye dimbwi la migogoro inayotokana na rasilimali. Yote mawili yanaweza kutokea kutegemea tutasimamiaje na kuzitumiaje rasilimali zetu.
Jambo la muhimu ni kusaidiana kuelimisha jamii ya Watanzania namna tulivyojipanga kusimamia rasilimali zetu za gesi asilia, mafuta na madini. Waelewe kuwa utajiri huu ni mali yao na hivyo ni haki yao kunufaika nao. Wafahamu kuwa ni wajibu wao kulinda na kuzitunza rasilimali hizo ili zisipotee. Ninyi mnayo dhamana ya kuelimisha jamii waelewe nia hiyo njema ya Serikali. Pia napenda kusema kuwa siyo kweli kwamba Serikali haijali rasilimali za nchi au haitaki Watanzania wafaidike nazo; siyo kweli eti Serikali inapendelea wawekezaji wageni kuliko wazawa na hakuna mkoa au eneo linapuuzwa au kubaguliwa. Mimi na Serikali ninayoiongoza tutakua watu wa mwisho kupuuza wazawa na kupendelea wageni au kupuuza watu wa maeneo ambako rasilimali zinapatikana au hazijapatikana.
Ndugu Viongozi wa Dini;
Naomba muendelee kutekeleza jukumu lenu la msingi la kulea taifa kiroho. Mhimize waumini wenu wawe waadilifu na wazalendo. Waache kujihusisha na vitendo viovu vya wizi, ubadhilifu, matumizi mabaya ya madaraka na rushwa. Mkifanikiwa hilo, rasilimali zetu zitakuwa salama. Vile vile muendelee kuhubiri upendo miongoni mwenu, miongoni mwa waumini wenu na miongoni mwa watu wote. Watu wakumbushwe kuwa sisi wote ni viumbe wa Mungu na mbele yake sisi wote ni ndugu na inabidi kuheshimiana na kuvumiliana kwa tofauti zetu. Tukifaulu kwenye hili nchi yetu itabaki salama daima milele.
Nafahamu kuwa wapo baadhi ya watu ambao wanafanya vitendo vya kuhujumu rasilimali zetu. Wapo wanaoingia mikataba isiyozingatia maslahi ya taifa katika uvunaji wa rasilimali zetu. Wapo wengine wanaokula njama na wawekezaji ili Serikali ipunjwe mapato yake. Watu wa aina hiyo wapo katika jamii ye yote ile na sisi kuwa nao si ajabu. Napenda mfahamu kuwa Serikali inapinga vitendo vya aina yoyote vya kuhujumu rasilimali zetu. Ndiyo maana watu wa aina hiyo wanapobainika, wanachukuliwa hatua na vyombo vinavyohusika. Ninyi pia msichoke kuwafichua, wapo miongoni mwa waumini wenu.
Mabibi na Mabwana;
Kabla ya kumaliza, napenda kumshukuru Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospiter Muhongo na timu yake Wizarani kwa kushirikiana na viongozi wa dini katika jambo hili muhimu. Naamini hatua hii ya kuwapa taarifa sahihi viongozi wa dini kuhusu matumizi ya rasilimali zetu hususan gesi na madini itasaidia kuongeza uelewa wa waumini wenu na wananchi kwa jumla. Watafahamu fursa zilizopo na jinsi ya kuzitumia ili wafaidike nazo. Nakushukuru pia kwa kusimamia vizuri utekelezaji wa sera na mipango ya Serikali katika sekta ya nishati na madini. Kazi yenu nzuri inaonekana na sisi wote ni mashahidi.
Mwisho, nawashukuru viongozi wa dini kwa kunishirikisha kwenye Kongamano lenu. Naamini mkitoka hapa mtakuwa mabalozi wazuri wa kueneza ujumbe kuwa rasilimali za Watanzania zipo kwenye mikono salama. Baada ya kusema hayo, napenda kutamka kuwa Kongamano la Viongozi wa Dini kujadili matumizi ya rasilimali zetu za gesi asilia, mafuta na madini kwa amani na maendeleo ya nchi yetu limefunguliwa rasmi. Nawatakia kila la heri na mafanikio katika mwaka huu wa 2014.
Asanteni sana kwa kunisikiliza

- Jan 05, 2014
HOTUBA YA MHESHIMIWA JAKAYA MRISHO KIKWETE, RAIS WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA, WAKATI AKIPOKEA MAANDAMANO YA VIJANA WA CCM WALIOTEMBEA KUADHIMISHA MIAK...
Soma zaidiHotuba
Makamu Mwenyekiti wa CCM na Rais wa Zanzibar, Dkt. Ali Mohamed Shein na Mama Mwanamwema Shein;
Mheshimiwa Balozi Seif Ali Iddi, Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar na Bi Asha;
Wajumbe wa Kamati Kuu ya CCM;
Ndugu Vuai Ali Vuai, Naibu Katibu Mkuu wa CCM Zanzibar;
Ndugu Sadifa Juma Khamis; Mwenyekiti wa UVCCM Taifa;
Bi Mboni Mhita, Makamu Mwenyekiti Taifa;
Ndugu Sixtus Mapunda, Katibu Mkuu wa UVCCM Taifa;
Wajumbe wa Halmashauri Kuu ya Taifa ya CCM (NEC);
Waheshimiwa Mawaziri, Naibu Mawaziri, Wabunge, Wawakilishi na Viongozi wa Ngazi Mbalimbali wa Chama na Serikali;
Mabibi na Mabwana;
Ndugu Wananchi;
Nawapongeza sana viongozi wa Umoja wa Vijana kwa uamuzi wenu wa kuandaa matembezi haya ya kuadhimisha miaka 50 ya Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar. Nawashukuru kwa heshima kubwa mliyonipa ya kuja kujumuika nanyi kwenye kuhitimisha matembezi haya.
Lazima nikiri kuwa nimefurahi na kupata faraja kubwa kuona vijana wamejitokeza kwa wingi kushiriki katika matembezi haya. Tumeelezwa hapa kuwa mlianza 600 mnamaliza 1,800. Wengine wamejiunga njiani. Huu ni uthibitisho tosha kuwa UVCCM iko hai na CCM inapendwa na itadumu tofauti na dhana ya wale wasioitakia mema. Katu dua zao hazitafanikiwa. Maandamano haya ni kielelezo thabiti kuwa Jumuiya yetu na vijana wetu wanatambua wajibu wao wa kuenzi na kusimamia mambo ya msingi yahusuyo taifa letu. Miongoni mwa mambo hayo ni Mapinduzi Matukufu ya Januari 12, 1964 na Muungano wa Zanzibar na Tanganyika wa Aprili, 1964. Naomba muendelee na moyo huo wa kuhamasishana na kuelimishana kuhusu tunu za taifa ambazo zimeachwa kama urithi na viongozi na waasisi wa nchi zetu tatu za Jamhuri ya Watu wa Zanzibar, Jamhuri ya Tanganyika na Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ambao pia ndiyo waasisi wa vyama vya ASP, TANU na CCM.
Nimefurahishwa na kuunga mkono kaulimbiu ya matembezi haya inayosema “Vijana Tusirudi Nyuma Katika Kuyalinda na Kuyaenzi Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar ya mwaka 1964”. Kaulimbiu hii ni mwafaka kabisa. Hakika msirudi nyuma na wala hakuna sababu ya kufanya hivyo. Daima mbele, nyuma mwiko. Ni usaliti. Kaulimbiu hii inawakumbusha vijana jukumu lenu la msingi la kutetea malengo na madhumuni ya Mapinduzi. Pili inawafundisha kuwa umoja na mshikamano ni jambo la msingi kwani hiyo ndiyo siri ya ushindi waliopata mashujaa wetu waliokuwa na mapanga na marungu. Umoja na nguvu. Umoja ni Ushindi. Na, nguvu ya mnyonge ni umoja. Ishikilieni kamba ya umoja.
Nilipendezwa sana na taarifa kuwa wakati wa matembezi yenu watu mbalimbali wakiwemo wazee walipata nafasi ya kuzungumza nanyi kuwaelimisha kuhusu historia ya Zanzibar kabla, wakati na baada ya Mapinduzi. Bila ya shaka mmepata kuifahamu vizuri historia ya Zanzibar kabla ya mapinduzi na kwa nini waasisi walilazimika kufanya uamuzi wa kuchukua silaha kupambana na utawala uliokuwapo.
Hatuna budi kuwapongeza na kuwashukuru kwa dhati mashujaa wetu hao walioongozwa na kiongozi mkuu wa Mapinduzi Sheikh Abeid Amani Karume kwa moyo wao wa ujasiri, utayari wa kujitolea muhanga kwa faida ya wengine na upendo wao kwa nchi yao na watu wake. Walikubali kwa hiari yao wenyewe kuweka maisha yao rehani kwa ajili ya kuwatetea wanyonge waliokuwa wanadhulumiwa na kunyanyaswa katika nchi yao. Jukumu lenu vijana, ni kuiga moyo huo wa kujitolea. Mnatakiwa wakati wote muwe tayari kujitolea kwa ajili ya taifa na wananchi wake. Muwe tayari kujitolea kwa ajili ya Chama cha Mapinduzi. Muwe tayari kuenzi na kulinda ukombozi huo uliopatikana kwa jasho jingi na damu za wana Mapinduzi.
Kwenye Mapinduzi mnaenzi na kutetea malengo na madhumuni yake ya msingi ambayo ni kuwapatia wananchi wa Zanzibar uhuru wa kweli. Ule wa Desemba 10, 1963 ulikuwa wa bandia. Ulikuwa “feki”. Waingereza walifanya kiini macho. Walifanya danganya toto ambayo Mapinduzi iliiondoa ghiliba ile. Kuwakomboa watu waliokuwa wanabaguliwa na kukandamizwa pamoja na kuwaondoa wale waliokuwa wanabagua na kuwakandamiza wenzao. Ndiyo maana baada ya Mapinduzi ASP iliunda Serikali na kujenga nchi isyokuwa na ubaguzi wa rangi, kabila, dini wala eneo. Waasisi wa Mapinduzi walipinga ubaguzi wa aina zote. Naomba vijana hili mlifahamu vizuri na kulizingatia ipasavyo. Mapinduzi hayakufanywa kwa ajili ya kundi fulani teule. Jasho na damu ya mashujaa iliyomwagika ilikuwa ni kwa ajili ya kuwakomboa wananchi wote wa Zanzibar. Kudumisha msingi huo ni jambo ambalo vijana mnao wajibu wa kuutambua vizuri na kuutekeleza. Hamtegemewi kufanya kinyume chake, si sera ya ASP na wala siyo sera ya TANU na CCM iliyobeba ya TANU na ASP.
Jambo la tatu ni Umoja na mshikamano miongoni mwa Waafrika na watu wanaoonewa na kudhulumiwa kote duniani ilikuwa sera ya msingi ya Afro Shirazi Party. Sera hiyo ilitekelezwa kwa vitendo na waasisi wa ASP na Mapinduzi kwa maana kwamba Chama cha ya Afro Shirazi Party ni Chama kilichotokana na kuungana kwa vyama vya African Association na Shirazi Association. Waasisi wetu ni watu waliotambua nguvu ya umoja. Walikuwa mstari wa mbele kujenga umoja na mshikamano miongoni mwao na vyama rafiki na nchi rafiki. Kwa ajili hiyo kulikuwa na uhusiano wa karibu baina ya African Association ya Zanzibar na African Association ya Tanganyika ambayo mwaka 1954 ikawa TANU. Aidha, kulikuwa na uhusiano wa karibu kati ya ASP na TANU kabla, wakati na baada ya Mapinduzi. Hivyo haikushangaza walipounganisha nchi zao huru na Tanganyika kuunda Jamhuri ya Muungano wa Tanzania tarehe 26 Aprili, 1964.
Vilevile, watu wa nchi zetu mbili ni ndugu wa damu hivyo kuziunganisha nchi zao ni sawa na kuziunganisha familia zilizojikuta zinatenganishwa na mazingira maalum ya kihistoria hasa kutawaliwa na watu wawili mbalimbali. Waliamua kuyasahihisha mambo hayo kwa kuunganisha nchi zao. Vilevile inatupasa tukumbuke kuwa Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar ndiyo yalikuwa chachu ya Muungano wa nchi zetu mbili. Huwezi kuzungumzia Muungano bila Mapinduzi. Kama Mapinduzi yasingefanyika Muungano usingekuwepo. Muungano ni mtoto wa Mapinduzi.
Ndugu Wananchi;
Ili kuimarisha umoja, udugu na mshikamamo ulioanzishwa Aprili 26, 1964, vyama tawala vya ASP na TANU viliungana tarehe 5 Februari, 1977. Hatua hiyo iliimarisha Muungano wetu na kuupandisha hadhi kufikia daraja la juu zaidi la utangamano. Ni vyema vijana mkajua ukweli huu ili mtambue wajibu wa kuulinda Muungano wetu udumu. Pia mtambue wajibu wenu wa kuimarisha Chama cha Mapinduzi kama kiungo cha kudumisha na kuendeleza Muungano wetu. Kuna watu hawaupendi Muungano na hawaiombei mema CCM. Ni wajibu wenu kuhakikisha kuwa Muungano unadumu na CCM inazidi kuimarika na inaendelea kuongoza nchi yetu.
Ndugu Mwenyekiti wa Vijana;
Ndugu Vijana;
Ni jukumu la msingi la vijana kuhakikisha kuwa sera ya Mapinduzi Matukufu ya Januari 12, 1964 yanatekelezwa, kuenziwa na kulindwa kwa hali na mali, mchana na usiku iwe jua iwe mvua. Pia vijana mnao wajibu wa kuhakikisha Muungano wa Zanzibar na Tanganyika wa Aprili, 1964 unadumu na kustawi pamoja na uhuru wa taifa letu, umoja wa watu wake na mshikamano wa kitaifa. Mkifanya hayo vijana mtakuwa mnawaenzi kwa vitendo waasisi wa taifa letu na viongozi waliofuatia. Mtaonesha kweli mmekomaa na mko tayari kurithi uongozi wa nchi yetu na kusimamia tunu za taifa letu. Tutaondoka madarakani na hata duniani nyoyo zetu zikiwa baridi na raha tukisema hakika nchi iko kwenye mikono salama. Hayo ndiyo matamanio yetu sisi wazazi wenu na viongozi tuliopo kwenye uongozi hivi sasa.
Ndugu Vijana;
Jambo lingine muhimu kwa vijana kutambua na kufanya ni wajibu wao kushiriki kwa ukamilifu katika maendeleo yao wenyewe, kisiasa, kiuchumi na jamii yao wenyewe wanayoishi na nchi yao. Kuinua hali za maisha ya watu wa Zanzibar ni shabaha kuu ya Mapinduzi ambayo tarehe 12 Januari 2014 tutadhimisha miaka 50 ya uhai wake. Ni jambo la kusikitisha kama kijana atashindwa kutimiza wajibu wake huo. Ni jambo linalofadhaisha kwa kijana kuwa mvivu, mlevi na mhalifu. Ni hasara kwake, kwa jamii yake na nchi yetu. Vijana ndiyo nguvu kazi ya leo na kesho ya kuliletea taifa maendeleo na ndiyo urithi wa familia, jamii na taifa. Tunapenda muwe wachapakazi hodari na warithi wema ili mlihakikishie taifa maendeleo endelevu na ustawi. Vijana mlinde Mapinduzi, Muungano na mafanikio ya Zanzibar na Tanzania.
Ndugu Mwenyekiti;
Ndugu Viongozi na Ndugu Vijana;
Mwaka huu pia tunasherehekea miaka 50 ya Muungano wa Zanzibar na Tanganyika. Katika uhai wa Muungano wetu ambao hauna mfano wake Afrika tumepata mafanikio mengi. Pia kumekuwepo na changamoto kadhaa ambazo kwa nyakati tofauti hatua zimechukuliwa kuzipatia ufumbuzi. Hata hivyo, kumekuwapo changamoto zilizohusishwa na Katiba ambazo marekebisho yaliyokuwa yanafanywa yalionekana kutokuyamaliza. Kwa kutambua hayo niliamua kuanzisha mchakato wa kuitazama upya Katiba ya sasa kwa nia ya kuihuisha. Tupate Katiba itakayosaidia kuondoa changamoto zilizopo za Muungano wetu ili mambo yaende vizuri na Muungano wetu ustawi na kudumu kwa miaka 50 ijayo na kuendelea bila vikwazo.
Kama mjuavyo, kwa kushirikiana na Rais wa Zanzibar niliunda Tume ya Mabadiliko ya Katiba. Tume hiyo imekamilisha kazi yake na kutoa mapendekezo yake. Kazi iliyo mbele yetu sasa Watanzania ni kuisoma Rasimu hiyo na kutoa mawazo yetu ya kuwasaidia Wajumbe wa Bunge Maalum katika kujadili na kuamua kuhusu vipengele mbalimbali vya Rasimu ya Katiba. Ni matumaini yangu kuwa vijana mtachangamkia fursa hiyo na kutoa maoni yenu.
Napenda kulisisitiza hili la watu kutoa maoni kwa sababu baadhi ya watu wanadhani kuwa kazi ya Katiba imekamilika baada ya Rasimu ya pili. La hasha! Tume imetoa mapendekezo ambayo yanatakiwa kujadiliwa na kuamuliwa ipasavyo na Bunge la Katiba. Bunge hilo lina mamlaka ya kuamua inavyoona inafaa kwa kifungu cho chote. Itumieni vizuri fursa hii kutoa maoni yenu ili tupate Katiba itakayotupatia Muungano imara na nchi ya kidemokrasia inayozingatia na kuheshimu haki za binadamu. Katiba itupatie nchi iliyo salama, tulivu na yenye kupata maendeleo shirikishi na kunufaisha watu wote. Vijana toeni maoni bila ya hofu. Nguvu mnazo, akili mnazo na sababu mnazo. Sisi tutaendelea kuwashirikisha na kuwajengea uwezo ili mtoe mchango wenu.
Ndugu Wananchi;
Kabla ya kumaliza hotuba yangu, napenda kurudia kuwapongeza tena vijana wote walioshiriki kwenye matembezi ya kilometa 340 kuenzi Mapinduzi Matukufu yaliyotokea miaka 50 iliyopita. Kwa namna ya pekee nawashukuru wote waliochangia kwa hali na mali kufanikisha matembezi haya. Wapo wenzetu wengi waliotoa misaada mbalimbali kwa vijana wetu. Sina neno zuri la kuwashukuru zaidi ya kusema asanteni sana.
Nawatakia nyote heri ya mwaka mpya. Asanteni sana kwa kunisikiliza.

- Dec 06, 2013
Closing remarks by his excellency Jakaya Mrisho Kikwete, the President of the United Republic of Tanzania, at the Africa-France conference on new economic mod...
Soma zaidiHotuba
Your Excellency President Hollande;
Excellencies Fellow Leaders From Africa;
Mr. Pierre Moscovici, French Minister of Economy and Finance;
Ladies and Gentlemen:
I thank you Mr. President and your esteemed government for conceiving the idea of holding this meeting on a New Economic Model between Africa and France. I congratulate Minister Moscovici, heartily for organizing this meeting so well. I also thank you for affording us the opportunity to speak at this landmark event.
Excellencies;
Ladies and Gentlemen;
Africa has got all what it takes to become a prosperous continent. The prevalent poverty is a contradiction in terms. It can be made history and the continent can become the new economic powerhouse of this planet.
Africa is well endowed with natural resources such as land, minerals, oil and gas, forest and marine based resources. These are critical resources for growth and development to happen. Fortunately, most of these resources are yet to be fully utilized which means the future prospects for Africa are good.
Africa has 60 percent of the world’s uncultivated arable land. On the average many countries of Sub-Saharan Africa get good rainfall despite the stresses and strains being caused by climate change from time to time. Moreover, there are sizeable surface and ground water resources for irrigation. And, with the permissive climate for agriculture, the potential for Africa to become a dependable grain basket of this world is huge.
Excellencies;
Ladies and Gentlemen;
Eleven African countries, rank among the top ten sources for at least one major mineral in the world. Africa has 10 percent of the world’s reserves of oil. The ongoing exploration activities across Africa are bound to increase more oil and gas resources which together with wind and solar sources of energy can produce a lot of electricity for own use and export. My country Tanzania has been added on to the map as discoveries of gas have been made and several companies are continuing with exploration.
Ladies and Gentlemen;
People are another important resource that Africa has in abundance. Africa’s population is estimated to be 1.033 billion roughly 15 percent of the world’s population. There are two things worth noting about Africa’s population. First, is that Africa has a very young population, two-third of which is below the age of 25. This means there is a huge reservoir of energetic workforce and there are prospects for further growth of Africa’s population. Second, with expansion of education at all levels, the size of the educated workforce is increasing and the middle class is growing. Therefore, Africa is a dynamic source of skilled and semi skilled labor force and a growing market. On the other hand, through regional integration the African markets are being consolidated and better defined.
Excellencies;
Ladies and Gentlemen;
Fortunately, also, in most African countries economic fundamentals are right because of pursuing sound economic policies. As a result, most countries have strong macro-economic performance, making Africa’s future economic prospects to be very promising indeed. The economies of many African countries are growing at rates of around 5 percent and above. IMF forecast shows that 7 African countries will be among 10 fastest growing economies in the world during 2011 - 2015. Because of improved macro-economic environment as well as business and investment climate, foreign direct investment flows to Africa have registered significant increase in the last decade. For example, between the year 2000 and 2010 FDIs to Africa increased from US$ 27 billion to US$ 126 billion. But this is far too small. Africa needs and can absolve much more than this amount. Africa can absolve 10 times this amount and still leave a lot of potential untapped.
Excellencies;
Ladies and Gentlemen;
Democracy is taking roots as the multiparty system has become the norm rather than the exception for over two decade now. There are regular periodic elections being held in all countries. The good thing is the elections are now better organized and the people get the opportunity to elect leaders of their choice. Governance has improved tremendously. There is greater awareness and strong commitment to observe human rights and deal with corruption and other social vices.
The security situation on the continent, has improved significantly. There are by far, fewer conflicts raging in Africa, now than they were two decades or a decade ago. And, what is even more encouraging is the fact that most conflicts are managed and resolved by Africans themselves through mechanisms and initiatives of the African Union and Regional Economic Groupings. Africa’s political and governance landscape has changed for the better and things look more promising in future.
Excellencies,
Ladies and Gentlemen;
Africa needs partnership with France and other countries both in the developed and developing nations to exploit its potential. Africa needs partners with capital, technology, know-how and market to transform Africa’s potential into goods and services to increase the wealth of our nations and our people. That is why we find this meeting to be quite opportune indeed. The 800 captains of industry gathered here are the very people we are looking for. They are the appropriate answer to the longstanding question about a new model for addressing poverty and development challenges facing Africa. A model which underscores the fact that Official Development Assistance alone is not enough. Indeed, ODA has been useful in helping our nations build capacity to deal with the teething challenges impeding growth and development. We still need ODA for capacity building in areas such as education, infrastructure, social and economic services etc. We appreciate the fact that, ODA needs to be combined with investments in the productive and service sectors to make the comprehensive difference we all desire.
In this context therefore, the New Economic Model being proposed should hinge on increased investment and trade without undermining the role of ODA, where necessary. This way African nations will build own capacity and become less dependent on ODA. In other words, under the envisaged model, investment and trade have to be viewed as sustainable ways of generating needed investment resources which can make poor countries achieve growth in a more sustainable manner than being predominantly dependent on ODA.
In this regard, Africa invites FDI in the form of private investment, joint venture, or public-private partnership in infrastructure, agriculture and agro-processing, manufacturing, ICT, petrochemical industries and other potential areas deemed as potential. Africa has a huge market, a growing middle class and a rising human capital base.
Excellencies;
Ladies and Gentlemen;
France and Africa relationship has to fit in the emerging global trend marked by increasing global investment and trade inter-linkages. This calls for the need to focus more on economic and trade relationship while a certain levels of financial and technical support is maintained.
The benefits, however, are not automatic given different levels of economic and technological development. We need to take deliberate policy and administrative measures that would create conducive environment for mutual benefit. Indeed issues of market access and preferential treatment of products from Africa is essential.
Furthermore, Excellencies, our governments must encourage and support private sector to invest in each other’s country. Fortunately, this is already happening in all African nations. Besides that there are policies and frameworks in place to promote and protect private investment throughout the African continent, Tanzania included. There is no doubt that there is a lot of business potential in Africa and African governments are committed to work with the France to utilize that potentials for our mutual benefit.
Ladies and Gentlemen;
In the envisaged economic model between Africa and France, we expect France to play an important role in supporting infrastructure and human resource development in Africa, which is key to unlocking supply constraints. Africa has not been able to utilize various preferential trade opportunities offered by European Union such as “Everything But Arms” partly because of weak supply side capacity. We expect France to also support human development efforts and regional integration, both of which are key in increasing Africa’s capacity to manage the economy and expand trade and output. Let me reiterate that we in Africa are ready to work with government of France and French private sector in a win-win arrangement for mutual benefit.
Ladies and Gentlemen;
Let me conclude by once again thanking President Hollande and the Government of France for organizing this important conference which has afforded us the opportunity to exchange views on how best we can improve our economic relations in a win-win- manner. I would like to reiterate that, Africa has all that is required to make her an economic power house of the 21st Century. There are abundant resources that are yet to be exploited and the political – economic environment is permissive. Our governments and people are ready to work in partnership with France, other developed countries and international private sector like the captains of industry and business that are part of this audience. Africa is ready to do business with you to develop Africa’s potential for our mutual benefit. In the process Africa will cease to be a poor and basket case and become not only a prosperous continent but the new emerging economic power house of this century.
Thank you

- Nov 08, 2013
Hotuba ya Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, aliyotoa Bungeni kuhusu Jumuiya ya Afrika Mashariki, 7 Novemba, 2013, Dodo...
Soma zaidiHotuba
Mheshimiwa Anne Makinda, Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania;
Mheshimiwa Dkt. Mohamed Gharib Bilal, Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania;
Mheshimiwa Dkt. Ali Mohamed Shein, Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi;
Mheshimiwa Mizengo Pinda, Waziri Mkuu;
Waheshimiwa Mawaziri na Naibu Mawaziri;
Mheshimiwa Freeman Mbowe, Kiongozi wa Kambi ya Upinzani Bungeni;
Waheshimiwa Wabunge;
Mabibi na Mabwana;
Nakushukuru sana Mheshimiwa Spika kwa kukubali ombi langu na kutenga muda wenu ili niweze kuzungumza na Wabunge wa Bunge lako Tukufu kuhusu masuala muhimu kwa uhai, ustawi na maendeleo ya nchi yetu na watu wake.
Mheshimiwa Spika;
Nimeambiwa kuwa taarifa ilipotolewa kuwa ninaomba kuja kuzungumza na Waheshimiwa Wabunge, kumekuwepo na dhana mbalimbali. Wapo waliodhani kuwa nakuja kuzungumzia mchakato wa kuunda Katiba mpya na hasa matukio ya wiki chache zilizopita. Wapo waliodhani nakuja kuzungumzia “Operesheni Tokomeza”. Tena wapo waliokwenda mbali na kufikiria kuwa nakuja kuwakaripia Waheshimiwa Wabunge waliotoa maoni yao kuelezea kasoro zilizojitokeza katika utekelezaji wa Operesheni hii muhimu. Na wapo pia waliodhani ninakuja kuzungumzia ushiriki wa majeshi yetu ya Tanzania katika Jeshi la Kulinda Amani la Umoja wa Mataifa nchini Kongo.
Mheshimiwa Spika;
Hayo si makusudio yangu. Kinachonileta mbele ya Bunge lako Tukufu ni kuzungumzia Jumuiya ya Afrika Mashariki na mustakabali wa Tanzania katika Jumuiya hiyo. Lakini, kwa sababu ya umuhimu wa masuala hayo niliyoyataja na rai niliyopewa kuwa niyasemee japo kidogo. Nimeona ni vyema nifanye hivyo.
Mheshimiwa Spika;
Kuhusu mchakato wa Katiba mpya, napenda kusema kuwa tumefikia hatua nzuri katika utekelezaji wake. Kama mjuavyo Tume ya Mabadiliko ya Katiba imekamilisha, kwa mafanikio, hatua ya mwanzo ya kusikiliza maoni ya wananchi kuhusu Katiba wanayoitaka. Pia walishatoa Rasimu ya Kwanza ya Katiba na kukamilisha mchakato wa Mabaraza ya Katiba. Kinachosubiriwa kwa hamu na sisi wote, ni Rasimu ya Pili ya Katiba ambayo inatarajiwa kukamilika ifikapo tarehe 15 Desemba 2013 au kabla ya hapo.
Mheshimiwa Spika;
Kwa upande wa Bunge lako Tukufu, tunategemea kupata mambo mawili kutoka kwenu yatakayowezesha mchakato kutekelezwa vizuri katika hatua zinazofuata. Jambo la kwanza ni kutungwa kwa Sheria ya Kura ya Maoni na pili kufanyika kwa marekebisho ya nyongeza ya Sheria ya Mabadiliko ya Katiba kuhusu Bunge Maalum ili kuboresha utekelezaji wake. Baada ya Bunge kukamilisha kazi yake hiyo itafuatia uteuzi wa Wajumbe wa Bunge Maalum ili kazi ya kujadili Rasimu ya Pili ya Katiba ifanyike na kutupatia Rasimu ya Mwisho. Rasimu ambayo ikikubaliwa na wananchi katika Kura ya Maoni itakayofanyika wakati wo wote mwakani, tutakuwa tumepata Katiba Mpya. Hivi sasa katika Serikali tunaendelea kufanya tafakuri na tunachukua hatua za kuwezesha Bunge Maalum na Kura ya Maoni kufanyika kwa mafanikio.
Operesheni Tokomeza
Mheshimiwa Spika;
Napenda kuwahakikishia Waheshimiwa Wabunge wa Bunge lako Tukufu kuwa sikukasirishwa na maoni yao kuhusu madai ya kuwepo kasoro katika utekelezaji wa Operesheni Tokomeza. Shabaha ya Operesheni hii ni kuokoa maliasili za misitu na wanyamapori dhidi ya uvunaji haramu ambao umefikia kiwango kinachotishia kutoweka kwa raslimali hizo. Kwa kweli hali inatisha. Miti inakwisha na ndovu na faru wanaangamia.
Mheshimiwa Spika;
Wakati, tunapata Uhuru Tanzania ilikuwa na ndovu waliokadiriwa kuwa takribani 350,000. Lakini, kwa sababu ya ujangili uliokithiri katika miaka ya 1970 na 1980 ilipofika mwaka1989 kulikuwa na ndovu wapatao 55,000 tu. Ilipofikia hali hiyo Serikali ikaanzisha Operesheni Uhai iliyohusisha Jeshi la Ulinzi na kuongozwa na Meja Jenerali John Walden (ambaye sasa ni marehemu) kuendesha mapambano dhidi ya majangili. Kutokana na hatua hiyo na uamuzi wa Shirika linalosimamia biashara ya wanyama walioko kwenye hatari ya kutoweka (CITES) kupiga marufuku biashara ya pembe za ndovu duniani, idadi ya ndovu nchini iliongezeka na kufikia 110,000 mwaka 2009.
Tumewaomba Fankfurt Zoological Society ambao ni wabia wetu katika uhifadhi wa wanyama pori kwa miaka mingi wafanye sensa maalum ya ndovu katika Hifadhi ya Selous na kote nchini ili tujue hali halisi ikoje. Kazi hiyo inaendelea hivi sasa.
Mheshimiwa Spika;
Baada ya mwaka 2009 kumezuka wimbi jipya, tena la nguvu kubwa, la kuua ndovu na faru nchini na kwingineko katika Bara la Afrika ambako wanyama hao wapo. Idadi kubwa ya meno ya ndovu yaliyokamatwa na yanaoendelea kukamatwa nchini na kwingineko duniani inathibitisha ukweli huo. Kwa mfano, kati ya mwaka 2010 na Septemba, 2013, hapa nchini, kwa jitihada zetu vipande 3,899 vya pembe za ndovu vyenye uzito wa kilo 11,212 na vipande 22 vya pembe za ndovu zilizochakatwa zenye uzito wa kilo 3,978vilikamatwa. Aidha, katika kipindi hicho vipande 4,692 vya pembe za ndovu vilivyotokea Tanzania vyenye uzito wa kilo 17,797vilikamatwa nje ya nchi.
Mheshimiwa Spika;
Kama nilivyokwisha sema hapo awali matatizo ya kuuawa kwa wingi kwa ndovu na faru lipo pia katika nchi nyingine Afrika zenye wanyama hao. Nchi za Gabon, Kenya, Afrika ya Kusini, Jamhuri ya Afrika ya Kati, Uganda, Zimbabwe, Zambia na nyinginezo nazo zinakabiliwa na matatizo kama yetu. Tatizo limekuwa kubwa kiasi cha kuifanya Jumuiya ya Kimataifa kushtuka na kuamua kuingilia kati kwa namna mbili. Kwanza kuunga mkono juhudi za uhifadhi wa ndovu na faru katika nchi zenye wanyama hao. Na, pili, kuchukua hatua thabiti kudhibiti biashara ya meno ya ndovu duniani. Ni ukweli ulio wazi kuwa kama hakutakuwepo na wanunuzi wa meno ya ndovu na faru hakuna ndovu au faru atakayeuawa.
Mheshimiwa Spika;
Kutokana na ukweli ulivyo uamuzi wetu wa kuendesha Operesheni Tokomeza ni sahihi kabisa. Manufaa yaliyopatikana baada ya Operesheni Uhai ya mwaka 1989 yanatupa imani kuwa na safari hii pia tutafanikiwa. Tusipochukua hatua kama hii sasa ni sawa na kuwapa kibali majangili waendelee kumaliza ndovu na faru nchini. Hakika wanyama hao watakwisha. Itakuwa ni aibu kubwa kwetu na historia itatuhukumu vibaya.
Mheshimiwa Spika;
Tumeyasikia maelezo ya Wabunge kuhusu kasoro mbalimbali zilizojitokeza katika utekelezaji wa Operesheni Tokomeza. Nawaahidi kuwa tutayafanyia kazi. Serikali imeahirisha kwa muda Operesheni hii ili kujipa muda wa kurekebisha kasoro hizo na kujipanga upya. Watendaji wasiokuwa waadilifu na wale wasiokuwa waaminifu wataondolewa. Halikadhalika, kasoro za kimfumo nazo zitasahihishwa ili tutakapoanza upya Operesheni itekelezwe kwa mafanikio yaliyokusudiwa.
Mheshimiwa Spika;
Miongoni mwa mambo yaliyozungumzwa kwa uchungu ni ukamataji wa mifugo iliyokutwa kwenye mapori ya hifadhi za wanyama na vitendo vibaya walivyofanyiwa wenye mifugo na mifugo yenyewe. Narudia kusisitiza kuwa taarifa zote hizo zitafanyiwa kazi na waliohusika watachukuliwa hatua zipasazo. Pamoja na hayo, napenda kuwakumbusha ninyi watunga sheria wetu kuwa sheria ya hifadhi za wanyamapori hairuhusu mifugo kuchungwa katika maeneo ya hifadhi.
Naomba tuwakumbushe wananchi tunaowaongoza wajiepushe na kufanya hivyo. Ni uvunjifu wa Sheria za nchi. Naomba pia, wananchi waelimishwe ili wajue kuwa wakifanya hivyo na kukutwa katika maeneo hayo na mifugo yao kuna adhabu iliyotamkwa kwenye sheria. Hivyo tusiwalaumu wala kuwaona maafisa wanyamapori kuwa ni watu wabaya. Wanatekeleza Sheria iliyotungwa na Bunge hili. Pale wanapotenda visivyo tuseme, watawajibishwa ipasavyo.
Jeshi la Umoja wa Mataifa Kongo
Mheshimiwa Spika;
Mapema mwaka huu (2013) Umoja wa Mataifa uliomba nchi yetu ichangie kikosi kimoja cha wanajeshi katika Brigedi Maalum iliyoundwa na Umoja huo kuongeza nguvu ya kudhibiti waasi Mashariki ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo. Lengo la msingi ni kuiwezesha nchi hiyo kupata amani ya kudumu ambayo imekosekana kwa muda mrefu kutokana na kuibuka kwa uasi mara kwa mara.
Mheshimiwa Spika;
Tulikubali, kwani hata kabla ya kuombwa na Umoja wa Mataifa tulishakubali maombi kama hayo yaliyotolewa kwenye Mkutano wa Nchi za Maziwa Makuu. Ni miezi saba (tangu Aprili) sasa tangu wanajeshi wetu waende Kongo na wamekuwa wanatekeleza majukumu yao vizuri tena kwa weledi na nidhamu ya hali ya juu. Sifa hiyo kwa wanajeshi wetu imekuwa inatolewa na viongozi wa juu wa Umoja wa Mataifa, viongozi wa juu wa Jeshi la Umoja wa Mataifa Kongo (MONUSCO) na viongozi wa juu wa Serikali ya Kongo.
Mheshimiwa Spika;
Majeshi ya Umoja wa Mataifa hupewa majukumu na mamlaka ya namna mbili. Yapo yanayopewa jukumu la kulinda amani tu. Wanajeshi wake huwa hawapewi majukumu ya kimapigano na hata pale wanaposhambuliwa wanatakiwa kujihami tu. Kwa kawaida majeshi yenye jukumu hili hupelekwa mahali ambapo kumekuwepo na makubaliano ya kuacha mapigano. Wanapelekwa kusaidia kuona Mkataba unatekelezwa ipasavyo.
Aina ya pili ni ile ya majeshi yanayopelekwa mahali ambapo hakuna amani hivyo wanapewa jukumu la kuchukua hatua za kufanya amani ipatikane. Majeshi haya hupewa mamlaka ya kutumia nguvu ya kijeshi dhidi ya wanaosababisha amani ikosekane kama ni lazima kufanya hivyo. Maana yake ni kwamba wanayo ruhusa kuingia katika mapigano dhidi ya watu au vikundi vinavyovuruga amani. Tofauti na wenzao wa kundi la kwanza, wanajeshi wa kundi la pili wako kwenye hatari zaidi ya kupoteza maisha au kujeruhiwa kuliko wenzao ingawaje wapo wengi nao wameuawa na kujeruhiwa.
Mheshimiwa Spika;
Wanajeshi wetu wamekwenda Kongo chini ya utaratibu huu wa pili ambao unahusu kuingia kwenye mapigano dhidi ya waasi kama hapana budi kufanya hivyo. Wametekeleza majukumu yao vyema na kwa ujasiri mkubwa na weledi wa hali ya juu. Bahati mbaya tumepoteza vijana wetu watatu shupavu. Daima tutawakumbuka na tutawaenzi ipasavyo mashujaa wetu hawa. Tuzidi kuwaombea kwa Mola awape mapumziko mema. Ameen.
Wakati huo huo, Mheshimiwa Spika, napenda kutumia nafasi hii kumpongeza Rais Joseph Kabila wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo kwa mafanikio ya kihistoria waliyoyapata hivi majuzi dhidi ya waasi wa M23. Tunamtakia yeye na wananchi wa Kongo kila la heri katika kazi ngumu iliyo mbele yao ya kujenga upya eneo hilo na kujenga mahusiano mapya miongoni mwa watu wa Kongo. Pia nawapongeza sana wanajeshi wa Brigedi Maalum ya Umoja wa Mataifa kwa kazi nzuri waliyoifanya iliyowezesha mafanikio kupatikana. Wanajeshi hao ni kutoka Afrika Kusini, Tanzania na Malawi wanaoongozwa na Brigedia Jenerali James Aloisi Mwakibolwa wa JWTZ.
Jumuiya ya Afrika Mashariki
Mheshimiwa Spika;
Kama nilivyosema awali, haya mambo matatu siyo hasa makusudio yangu nilipoomba kuja kuzungumza na Waheshimiwa Wabunge wetu. Nimeyachomekea tu kwa sababu ya umuhimu wake katika jamii kwa wakati tulio nao. Jambo lililonileta hapa leo ni kuzungumzia hali ilivyo sasa katika Jumuiya ya Afrika Mashariki na nafasi ya Tanzania katika Jumuiya hiyo. Nimeona nifanye hivyo kutokana na maswali mengi ambayo Watanzania wanajiuliza kufuatia matukio ya hivi karibuni ya viongozi wa nchi tatu wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki yaani Uganda, Rwanda na Kenya kukutana bila ya ushiriki wa viongozi wa Tanzania na Burundi. Viongozi wenzangu hao wamefanya mikutano mitatu yaani: tarehe 24-25 Juni, 2013 mjini Entebbe, Uganda; tarehe 28 Agosti, 2013 mjini Mombasa, Kenya; na tarehe 28 Oktoba, 2013 mjini Kigali, Rwanda.
Mheshimiwa Spika;
Naomba kwanza niweke wazi jambo moja, kwamba nchi mbili wanachama au zaidi hazikatazwi kuwa na makubaliano ya ushirikiano katika kufanya mambo mbalimbali. Hata sisi Tanzania tunao ushirikiano wa namna hiyo na nchi zote wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki. Lakini, nchi wanachama zinatakiwa kufanya hivyo kwa yale mambo ambayo hayako kwenye shughuli za Jumuiya kwa maana kwamba hayamo katika Mkataba au Itifaki au hakuna uamuzi wa msingi uliofanywa na vikao au taasisi za Jumuiya kuyashughulikia. Pia, tunaweza kufanya hivyo kwa mambo ambayo yalishaamuliwa na Jumuiya yatekelezwe na ruhusa imetolewa kwa nchi yo yote iliyokuwa tayari kutekeleza ama peke yake au kwa kushirikiana na nchi nyingine.
Mheshimiwa Spika;
Kwa mujibu wa matamko ya pamoja (Communique) yaliyotolewa baada ya mikutano hiyo, kuna mambo yapatayomanane ya msingi yaliyoamuliwa kufanywa na nchi hizo kwa lengo la kuendeleza utengamano wa nchi hizo wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki. Mambo hayo ni haya yafuatayo:
(1) Kujenga reli ya kisasa kutoka Mombasa hadi Kampala, Kigali na Bujumbura.
(2) Ujenzi wa Bomba la Mafuta la kutoka Kenya hadi Uganda na Sudani ya Kusini.
(3) Kujenga Kiwanda cha kusafisha mafuta nchini Uganda.
(4) Kuanzisha Himaya Moja ya Ushuru wa Forodha wa Jumuiya ya Afrika Mashariki na kutekeleza vipengele vyote;
(5) Kuharakisha Shirikisho la Afrika Mashariki na kwamba itaundwa Kamati ya kuandaa rasimu ya Katiba ya Shirikisho.
(6) Kuharakisha uanzishwaji wa Visa ya pamoja ya Utalii ya Jumuiya ya Afrika Mashariki (Single East African Community Tourist Visa);
(7) Kuandaa utaratibu wa kutumia vitambulisho vya taifa kama hati ya kusafiria katika nchi zao; na
(8) Kuongeza uzalishaji na usambazaji wa umeme.
Mheshimiwa Spika;
Ni dhahiri kwamba orodha hiyo imechanganya mambo yale ambayo ni ya Jumuiya na yale yasiyo ya Jumuiya. Kwa mfano, mambo manne kati ya hayo manane hayamo kwenye masharti ya kutokufanyika bila ya kuihusisha au kupata ridhaa ya Jumuiya ya Afrika Mashariki. Jambo la kwanza ni uzalishaji na usambazaji wa umeme. Ni kweli kwamba tunao mkakati wa kuwa na akiba ya pamoja ya nguvu ya umeme (East African Power Pool). Hata hivyo, bado jukumu la kuzalisha na kusambaza umeme huo limeachiwa nchi wanachama zenyewe kuamua. Lakini, hivi ndugu zetu hawa wanao muhali kuishirikisha Tanzania katika mpango ambao kimsingi umebuniwa na Jumuiya ya Afrika Mashariki ambayo sote ni wanachama?
Jambo la pili, ni ujenzi wa kiwanda cha kusafisha mafuta nchini Uganda. Hili si suala la Jumuiya bali la nchi ya Uganda kuamua yenyewe peke yake au kwa kushirikiana na wadau wengine. Rais Yoweri Museveni alituarifu mpango huo na sote tuliupokea kwa furaha kwamba sasa tutapata mafuta karibu na nyumbani. Alitualika kushiriki katika ujenzi wake sijui sasa amebadili mawazo kwamba Tanzania siyo muhimu.
Mheshimiwa Spika;
Jambo la tatu ni ujenzi wa bomba la mafuta kutoka Kenya hadi Sudani ya Kusini na Uganda. Hili si jambo linalobanwa na masharti ya Jumuiya. Ni juu ya nchi hizi tatu kuamua kufanya ili kuwezesha mafuta yao kufika kwenye masoko. Hata hivyo, nimeambiwa kuwa Jumuiya imeshazungumzia bomba la mafuta kutoka Eldoret hadi Uganda, Rwanda na Burundi kuwa nalo lifike Tanzania kupitia upande wa Kaskazini Magharibi mwa Tanzania. Inaelekea mpango huo sasa haupo maana hatujausikia kutajwa katika ujenzi wa bomba hilo.
Mheshimiwa Spika;
Jambo la nne ni ujenzi wa reli ya kisasa kutoka Mombasa – Kampala – Kigali – Bujumbura. Hili nalo hatuna tatizo nalo. Si mradi wa Jumuiya ya Afrika Mashariki, ni jambo lililo chini ya mamlaka ya nchi wanachama husika. Hata hivyo, ni vyema kutambua ujenzi wa miundombinu ya reli, barabara na usafiri wa anga na majini kuunganisha nchi za Afrika Mashariki ni miongoni mwa mambo ya kipaumbele cha juu yanayoshughulikiwa na Jumuiya yetu. Jumuiya hutengeneza mikakati ya pamoja na ndiyo maana tuna East African Railway Masterplan, tuna East African Road Network, na tuna Lake Victoria Development Programme kwa ziwa Victoria.
Kwa ajili hiyo, nilitegemea kuwa reli ya kutoka Mombasa hadi Kigali na Juba ingekuwa na tawi linalounganisha reli hiyo na reli ya Tanzania kama ilivyo reli ya Moshi – Voi – Taveta aliyotuachia mkoloni. Tulitegemea hivyo kwa minajili ya kuunganisha soko la Afrika Mashariki ambapo naamini Tanzania ni mdau muhimu. Lakini inaelekea kwa maoni ya wenzetu hivyo sivyo.
Mheshimiwa Spika;
Lazima nikiri kuwa inashangaza na tunayo kila sababu ya kuuliza kwa nini wenzetu wameamua kufanya hivi. Kumetokea nini toka tukutane pale Arusha Aprili 28, 2013 na Juni 24, 2013 walipokutana kuamua kufanya mambo ya kujenga na kuimarisha utengamano wa Afrika Mashariki kwa kubaguana, Haijawahi kuwa hivi kabla.
Mheshimiwa Spika;
Katika mambo manne yaliyosalia ambayo yaliamuliwa na kuwekewa utaratibu wake wa utekelezaji na Jumuiya ya Afrika Mashariki mawili hatuna maneno nayo. Mambo hayo ni matumizi ya vitambulisho vya taifa kama hati ya kusafiria na Visa ya Pamoja ya Utalii kwani tuliamua kwa pamoja kuwa nchi wanachama zilizokuwa tayari waanze. Lakini, kwa upande wa kuanzishwa kwa Himaya Moja ya Ushuru wa Forodha (Single Customs Territory) na Shirikisho la Afrika Mashariki tunadhani wenzetu wamekiuka uamuzi wetu wa pamoja.
Mheshimiwa Spika;
Katika Mkutano Maalum wa 11 wa Wakuu wa Nchi wanachama uliofanyika tarehe 28 Aprili, 2012 Jijini Arusha, tulipokea na kuridhia mapendekezo ya kuanzisha Himaya Moja ya Ushuru wa Forodha (Single Customs Territory). Kwa mujibu wa mapendekezo hayo kila nchi mwanachama itasimamia shughuli zake za kiforodha na kukusanya mapato yake kama ilivyo sasa. Hata hivyo, kwa bidhaa zinazopitia nchi moja kwenda nchi nyingine mwanachama, ukaguzi na ukusanyaji wa mapato utafanyika katika kituo cha kwanza bidhaa hizo zinapoingilia. Mapato hayo yatawasilishwa kwa nchi husika baada ya kuthibitisha kuwa bidhaa zilivuka mpaka.
Mheshimiwa Spika;
Kutokana na uamuzi huo, Wakuu wa Nchi waliagiza Baraza la Mawaziri kuunda Kikosi Kazi cha kujadiliana na kuandaa utaratibu wa utekelezaji wa mfumo huo. Taarifa ya kikosi kazi inatakiwa kutolewa katika Mkutano wa 15 wa Wakuu wa Nchi utakaofanyika Kampala, Uganda tarehe 30 Novemba, 2013. Iweje leo nchi tatu wanachama ziamue peke yao kuanza kutekeleza? Wanatekeleza nini na kwa nini wafanye hivyo?
Mheshimiwa Spika;
Kuhusu Shirikisho la Kisiasa la Afrika Mashariki hadithi yake inafanana na hii ya Himaya ya Forodha. Katika Mkutano wa 14 wa Wakuu wa Nchi wanachama uliofanyika tarehe 30 Novemba, 2012, Nairobi, tulipokea taarifa ya hatua iliyofikiwa kuhusu mchakato wa kutaka kuanzishwa kwa Shirikisho. Mkutano huo uliagiza nchi wanachama kujadiliana zaidi kuhusu mpango kazi wa kufikia Shirikisho la Kisiasa na mpango wa kutekeleza mapendekezo mengine yaliyotolewa na Timu ya Wataalamu. Inategemewa kuwa Baraza la Mawaziri litawasilisha mapendekezo ya majadiliano hayo katika Mkutano wa 15 wa Wakuu wa Nchi mwezi Novemba, 2013. Iweje leo wenzetu hawa waamue kuanzisha mchakato wao wa kuharakisha Shirikisho la Afrika Mashariki.
Mheshimiwa Spika;
Kwa kweli huwa najiuliza maswali mengi na kukosa majibu kuhusu nini kinachoendelea kufanywa na viongozi wenzangu watatu na kwa nini! Nakosa majibu ya uhakika. Je wenzetu wamekosa imani na Jumuiya ya Afrika Mashariki na je wanataka kuunda yao? Je wanaichukia nchi yetu na hivyo wameamua kutufanyia vitimbi tutoke! Au sijui wanachuki na mimi! Napenda kuwahakikishia Waheshimiwa Wabunge kuwa hatuna mpango wa kutoka (kama vijana wasemavyo hatoki mtu hapa). Tupo na tutaendelea kuwepo!
Mheshimiwa Spika;
Tanzania haijafanya jambo lo lote baya dhidi ya Jumuiya au nchi yo yote mwanachama. Na ukweli ni kwamba ni mwanachama mvumilivu, mtiifu na mwaminifu kwa Jumuiya. Tunatimiza ipasavyo wajibu wetu kwa Jumuiya na kushiriki kwa ukamilifu katika ujenzi wake na utengamano ndani ya Jumuiya ya Afrika Mashariki. Sabahu ya wenzetu watatu kuamua kufanya mambo yahusuyo Jumuiya yetu peke yao kwa kweli haieleweki.
Mheshimiwa Spika;
Tunasikia eti kuwa baadhi yao walipoulizwa kwa nini wengine hatupo wakasema kuwa wao wametangulia na sisi tutakapokuwa tayari tutajiunga. Yaani wana Umoja wa Waliokuwa Tayari (Coalition of the Willing). Hivi ni nani hayuko tayari (who is not willing?) Haiwezekani watu waitane wenyewe bila ya kutualika halafu wadai kuwa wao ndiyo wako tayari na kujenga dhana kuwa sisi wasiotualika ndiyo ambao hatuko tayari. Madai hayo hayana ukweli. Ni vyema waseme ukweli. Kama walitualika tukakataa ndiyo wanaweza kusema hayo.
Mheshimiwa Spika;
Kumekuwepo na madai kutoka kwa baadhi ya wenzetu, eti kwamba Tanzania haina moyo wala dhamira ya dhati ya kuendeleza utengamano wa Afrika Mashariki. Kwa sababu hiyo inasemekana eti nchi yetu imekuwa kikwazo kwa maendeleo ya Jumuiya ya Afrika Mashariki na kwamba Tanzania tunawachelewesha wengine kupiga hatua za haraka. Wanadai kama siyo hivyo Jumuiya ya Afrika Mashariki ingekuwa mbali kwa maendeleo. Maneno hayo yamekuwa yanarudiwa au kujirudia mara nyingi kiasi cha kuwafanya baadhi ya watu wa Afrika Mashariki na hata kwingineko duniani waamini hivyo.
Mheshimiwa Spika;
Napenda kusema kwa dhati ya moyo wangu kwamba madai hayo hayana ukweli wo wote. Isitoshe hata sababu zinazotolewa kuthibitisha ukweli wake hazina mashiko. Hazifanani na ukweli kuhusu Tanzania na Watanzania walivyo. Tanzania ni muumini wa dhati wa umoja na utengamano wa nchi za Afrika Mashariki na Afrika. Tumethibitisha hivyo kwa vitendo kwa kuunganisha nchi zetu mbili huru yaani Jamhuri ya Watu wa Zanzibar na Jamhuri ya Tanganyika na kuwa taifa moja liitwalo Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Muungano wa nchi zetu mbili ndio pekee uliodumu kwa muda mrefu kuliko yote Afrika.
Mheshimiwa Spika;
Tanzania ni mwanachama mwaminifu wa Jumuiya ya Afrika Mashariki kwa maana ya kutekeleza Mkataba ulioanzisha Jumuiya hiyo, kwa Itifaki zake na maamuzi halali ya vikao na taasisi za Jumuiya. Kama lipo jambo ambalo hatujalifanya ilivyotakiwa itakuwa ni kwa sababu za msingi na siyo kwa sababu ya kupuuza Jumuiya. Tunaithamini sana Jumuiya na tumeipa kipaumbele cha juu. Hatuwezi kuhangaika kwa gharama kubwa ya muda wetu, fedha zetu na kutoa mchango wa hali na mali kuianzisha, kujenga na kuifikisha Jumuiya hapa ilipo halafu tuwe ni watu tunaoongoza kutokuipenda na kudhoofisha maendeleo na ustawi wake. Ni maneno ya kushangaza na wala hayaingii akilini. Ama kweli akutukanae hakuchagulii tusi.
Mheshimiwa Spika;
Nionavyo mimi msimamo wetu kuhusu kuharakisha Shirikisho na masuala ya ardhi, ajira, uhamiaji, pengine ndiyo yanayotuletea hisia zisizokuwa sahihi juu yetu. Mimi siamini kama kuna mengine. Hata hivyo, napata taabu kuamini kwamba kutofautiana kwa mawazo katika mambo hayo kutapelekea baadhi ya wenzetu wasipende hata kushirikiana nasi kwa mambo ambayo hayana matatizo na tumekuwa tunashirikiana vizuri.
Mheshimiwa Spika;
Tanzania imekuwa inawasihi wanachama wenzetu kuwa tujenge Jumuiya yetu hatua moja baada ya nyingine kama ilivyo kwenye Mkataba ulioanzisha Jumuiya ya Afrika Mashariki. Hatuna tatizo la kuongeza kasi ya ujenzi wa Jumuiya lakini tusivuke hatua yo yote. Tusiende kasi ya kupindukia. Mkataba unaelekeza tunaanza na Umoja wa Forodha, inafuatia Soko la Pamoja kisha Umoja wa Kifedha na hatimaye Shirikisho la Kisiasa.
Mheshimiwa Spika;
Ni kweli kabisa hatukuunga mkono kuharakisha Shirikisho la Kisasa kabla ya kukamilisha baadhi ya hatua. Na, tulifanya hivyo kwa nia njema ya kutaka Shirikisho lijengwe juu ya msingi imara. Na, msingi huo si mwingine bali utengamano wa kiuchumi kwa maana ya Umoja wa Forodha, Soko la Pamoja na Umoja wa Kifedha zilizojengeka vizuri na kufanya kazi ipasavyo na kunufaisha wanachama wote sawia.
Mheshimiwa Spika;
Lazima tutambue ukweli kuwa kunufaika kiuchumi ndicho kichocheo kikubwa cha nchi kujiunga na kuendelea kuwa mwanachama wa Jumuiya yetu. Kama mambo ya kiuchumi yakipangika vizuri na kila nchi ikanufaika sawia, unajenga msingi imara kwa Shirikisho la Kisiasa kustawi na kudumu. Kama ngazi hizi tatu za awali hazitashughulikiwa vizuri na nchi wanachama zikahisi hazinufaiki ipasavyo, Shirikisho litayumba au kuyumbishwa hivyo kudumu kwake kutakuwa kwa mashaka.
Mheshimiwa Spika;
Tanzania ni kati ya zile nchi zinazotaka ngazi zote za mchakato wa utengamano zitekelezwe moja baada ya nyingine bila kuruka hata moja. Kwa msimamo na mtazamo wetu, Shirikisho iwe ndiyo hatua ya mwisho. Na huo siyo msimamo wangu au wa Serikali peke yake, ndiyo msimamo wa Watanzania walio wengi.
Bila ya shaka sote tutakumbuka kuwa mwaka 2006 Wakuu wa Nchi Wanachama wa Jumuiya waliunda Kamati Maalum katika kila nchi kukusanya maoni ya wananchi kuhusu kuharakisha Shirikisho la Afrika Mashariki. Kwa hapa nchini Kamati hiyo iliongozwa na Profesa Samwel Wangwe na katika taarifa yake, Kamati ilieleza kuwaasilimia 74.4 ya Watanzania wanaunga mkono kuwepo kwa Shirikisho lakini ni asilimia 25.4 tu ndiyo waliunga mkono kuharakishwa kwake.
Mheshimiwa Spika;
Takwimu hizi zinaelezea ukweli kuhusu hisia za Watanzania, kuhusu kuwepo kwa Shirikisho na kasi ya utekelezaji wake. Watanzania wengi sana wanaunga mkono kuwepo kwa Shirikisho la Afrika Mashariki lakini wanataka jambo hilo lisifanywe haraka haraka. Wanataka lifanywe kwa umakini mkubwa na tuende hatua kwa hatua kama ilivyoainishwa katika Mkataba uliounda Jumuiya ya Afrika Mashariki.
Mheshimiwa Spika;
Sera na msimamo wa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania inakwenda sambamba na ile ya wananchi wa Tanzania. Ndiyo maana tumeafiki mapendekezo ya Kamati ile ya mwaka 2004iliyoongozwa na Mheshimiwa Amos Wako wakati ule akiwa Mwanasheria Mkuu wa Kenya. Kamati hiyo iliundwa kupendekeza namna ya kuharakisha utekelezaji wa mchakato wa utengamano wa Afrika Mashariki.
Mkataba wa Jumuiya ya Afrika Mashariki umetamka muda wa kutekeleza ngazi ya Umoja wa Forodha lakini uko kimya kuhusu ngazi zilizofuata. Ili kuondoa kasoro hiyo na kwa nia ya kuharakisha Shirikisho Kamati ilipewa jukumu la kutoa maoni na mapendekezo juu ya namna ya kufanya hivyo. Kamati ilifanya kazi nzuri ya kupata maoni na hisia za watu wa makundi mbalimbali katika nchi wanachama kuhusu ujenzi wa Jumuiya na utengamano.
Mheshimiwa Spika;
Kwa upande wa Tanzania kwa mfano, Kamati ya Mheshimiwa Amos Wako ilitambua hisia za Watanzania kuhusu ardhi na ajira na kupendekezwa kuwa masuala hayo yabaki kwenye mamlaka ya nchi wanachama kuamua. Kuhusu mchakato wa utengamano Kamati ilipendekeza kwanza kwamba mchakato wa ujenzi wa Umoja wa Forodha uachwe mpaka ufike ukomo wake wa miaka mitano. Baada ya hapo muda wa kutekelezwa ngazi zinazofuata unaweza kupunguzwa. Kwa mfano walipendekeza kuwa matayarisho ya kuunda Soko la Pamoja yaanze hata kabla ya mchakato wa Umoja wa Forodha kufika mwisho ili mara wakati huo ukifikiwa Soko la Pamoja linaanze. Hivyo hivyo mara baada ya ngazi hiyo kuanza matayarisho ya kuanza ngazi ya Umoja wa Kifedha yanaanza. Ngazi hiyo nayo ikianza matayarisho ya kuunda Shirikisho yanaanza. Kamati pia imetoa mapendekezo ya namna ya kufikia uamuzi kuhusu Shirikisho kwamba wananchi wa nchi wanachama wataamua kwa kura. Tukifuata mapendekezo ya Kamati ya Mheshimiwa Amos Wako na wenzake kama tufanyavyo sasa Tanzania haina matatizo nayo.
Mheshimiwa Spika;
Baada ya kazi kubwa na nzuri iliyofanywa na wana-Afrika Mashariki kuhusu ujenzi wa Jumuiya yao inasikitisha kuona vinafanyika vitendo vinavyoanzisha mivutano kuhusu mambo yaliyokwisha fanyiwa kazi na kuamuliwa. Tunapata taabu zaidi pale watu wanapobagua wenzao na wanapofanya mambo yanayopingana na Mkataba wa Jumuiya na Itifaki zake. Kwa kweli kama mwenendo huu hautabadilika sijui mambo yatakuwaje mbele ya safari.
Mheshimiwa Spika;
Nchi yetu inapenda kuona kuwa tunakuwa na Jumuiya ya Afrika Mashariki iliyo imara na iliyo endelevu. Jumuiya ambayo inaendeshwa vizuri, mambo yake ni mazuri na nchi zote wanachama na watu wake wananufaika nayo, na hivyo wanaifurahia. Tanzania haina tatizo na kuharakisha mchakato wa utengamano, lakini tunapata taabu kuruka baadhi ya hatua kabla hazijakamilika. Tunawaomba wenzetu kuwa makini katika kila hatua tunayochukua. Bila ya kufanya hivyo, Jumuiya yetu itakuwa imejengeka katika msingi dhaifu hivyo ustawi na uhai wake utakuwa na changamoto nyingi. Hatupendi ya mwaka 1977 yatokee tena.
Mheshimiwa Spika;
Napenda kuwahakikishia kuwa Tanzania itaendelea kushiriki katika shughuli za Jumuiya ya Afrika Mashariki na kuimarisha utengamano wa Afrika Mashariki kwa kuzingatia matakwa ya Mkataba wa Jumuiya ya Afrika Mashariki na Itifaki zake. Tutafanya kila tuwezalo kuhakikisha kuwa Jumuiya haidhoofiki wala kufa. Na iwapo itadhoofika au kufa kamwe hatutaki Tanzania inyooshewe kidole kuwa chanzo wala kichocheo chake. Ndiyo maana, hatutachoka kuzungumza na wenzetu kuhakikisha kuwa Jumuiya ya Afrika ya Mashariki inaendelea kustawi.
Tutaendelea kukumbushana umuhimu wa kufanya mambo yanayojenga na kuepuka yale yanayoweza kubomoa. Tutakumbushana umuhimu wa kuheshimu matakwa na masharti ya Mkataba ulioanzisha Jumuiya, Itifaki zake na maamuzi halali ya vikao rasmi na asasi za Jumuiya. Tukifanya hivyo Jumuiya ya Afrika ya Mashariki itadumu, itazidi kustawi na kunufaisha nchi wanachama na watu wake kama yalivyo malengo na madhumuni ya kuundwa kwake.
Mungu Ibariki Afrika
Mungu Ibariki Tanzania
Idumu Jumuiya ya Afrika Mashariki
Mheshimiwa Spika na
Waheshimiwa Wabunge;

- Oct 29, 2013
Hotuba ya Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwenye maadhimisho ya miaka 100 ya Kanisa Katoliki, Parokia ya Lugoba, tarehe 27 O...
Soma zaidiHotuba
Mhashamu Baba Askofu, Telesphor Mkude, Askofu wa Jimbo Katoliki la Morogoro;
Mhashamu Baba Askofu Anthony Banzi wa Jimbo Katoliki Tanga;
Wahashamu Maaskofu,
Viongozi wa Dini mliopo hapa;
Baba Paroko, Padri Constantine Luhimbo;
Mapadri, Mashemasi na Watawa;
Ndugu waumini;
Wageni waalikwa;
Mabibi na Mabwana;
Shukrani kwa Mwaliko
Niruhusuni niungane na wasemaji walionitangulia kumshukuru Mwenyezi Mungu, mwingi wa rehema, kwa kutujalia uzima na kutukutanisha hapa katika Kanisa la Msalaba Mtukuka kusherehekea Jubilei ya miaka mia moja ya Kanisa Katoliki la Lugoba. Nakushukuru sana Baba Askofu Mkude pamoja na Baba Paroko na waumini wa Parokia ya Lugoba kwa kunishirikisha katika maadhimisho haya ya kihistoria.
Nawapongeza sana waumini wa Parokia ya Lugoba kutimiza karne moja tangu ianzishwe. Hayo ni mafanikio makubwa, hivyo mnastahili kusherehekea kwa nderemo na vinubi. Nawapongeza sana kwa kuwakumbuka, kuwaenzi na kuwashukuru Padri Cornel na Padri Herman ambao ndiyo waanzilishi wa Parokia hii miaka 100 iliyopita. Hakika leo ni siku yao wao zaidi pengine kuliko sisi. Bila ya juhudi zao, moyo wao wa ujasiri, uvumilivu na kujituma huenda leo tusingekuwa hapa kufanya maadhimisho haya. Sote tumesikia kuwa mwanzoni mambo hayakuwa rahisi sana. Lakini, ni ushirikiano wa Wamisionari hao na baadhi ya wenyeji kama vile Mzee Kinogile, aliyekuwa Mtawala, Mzee Matei, Mzee Lui na wengineo ndiyo weliowezesha mambo kwenda vizuri na Parokia ikaanzishwa. Nafurahi nao pia mmewatambua na kuwaenzi.
Kwa ujumla nimefarijika sana kuona kwamba katika kusherehekea siku ya leo mnawatambua na kuwaenzi watumishi wa Mungu tangu wakati ule mpaka sasa kwa kazi kubwa waliyoifanya ya kujenga na kuimarisha kanisa kwenye Parokia hii. Kutokana na kazi yao nzuri waumini wameongezeka, huduma za kiroho zimeimarika na kwamba Kanisa limetoa mchango muhimu kwa maendeleo ya jamii katika eneo letu hili.
Ndugu waumini;
Ninyi na mimi ni shuhuda wa jinsi Kanisa Katoliki la Lugoba lilivyochangia na linavyoendelea kuchangia katika upatikanaji wa huduma za jamii kama vile elimu na afya bila ya kuwabagua watu kwa imani zao za kumuabudu Mungu. Kwa upande wa afya tumesikia zahanati zilizojengwa na Kanisa na mipango iliyopo ya kuboresha zaidi huduma zinazotolewa. Vile vile, tumesikia shule zilizojengwa na kuanzishwa na Kanisa la Lugoba. Hata mimi ni mmoja wa watu walionufaika kwani nilipata elimu ya darasa la tano hadi la nane mwaka 1962 mpaka 1965 katika shule iliyokuwa inaitwa St. John Bosco’s Lugoba Middle School iliyomilikiwa na Kanisa Katoliki Lugoba.
Kunako mwaka 1965, Serikali iliamua kuwa elimu za msingi hazitakuwa na madaraja mawili yaani ya darasa la kwanza hadi la nne (Primary School) na darasa la tano hadi la nane (Middle School) badala yake elimu ya msingi ikawa kuanzia darasa la kwanza hadi la saba. Kufuatia uamuzi huo Lugoba Middle School na Lugoba Primary School ziliunganishwa na kuwa shule ya Msingi Lugoba. Wakati madarasa tuliyosomea yanaunganishwa na shule hiyo mpya, iliyokuwa ofisi ya Walimu ikawa zahanati ya Kanisa na yaliyokuwa mabweni sasa yamekuwa madarasa ya Sekondari ya Lugoba.
Kwa kweli hatuna maneno mazuri ya kuelezea shukrani zetu kwa Kanisa Katoliki Parokia ya Lugoba kwa mchango muhimu iliyotoa kwa maendeleo ya watu wa eneo hili, Wilaya ya Bagamoyo na kwingineko nchini. Watu wengi wamefaidika na wanaendelea kunufaika. Mwenyezi Mungu azidi kuwabariki ili muendelee kuwahudumia watu katika Parokia yetu ya Lugoba na taifa kwa ujumla. Tunapenda miaka mia moja ijayo, kwa watakaokuwepo kipindi hicho, wakiri utume huo usiokifani. Na waseme “hakika wenzetu waliotangulia walikuja kufanya kazi, walikuwa watu wa kazi”.
Serikali Inathamini Mchango wa Kanisa
Mhashamu Baba Askofu Mkude;
Mabibi na Mabwana;
Napenda kuwahakikishia kuwa serikali inatambua vyema na kuthamini mambo yote mazuri yanayofanywa na Kanisa Katoliki. Kabla na hata baada ya uhuru, Kanisa limekuwa mdau muhimu na mshirika muhimu wa Serikali katika kuhudumia wananchi. Wakati mwingine unakuta huduma za jamii kama zahanati ipo mahali ambapo hata Serikali bado haijafika. Kutuunga mkono kwa namna hiyo ndiko kumechangia sana nchi yetu kupiga hatua kubwa kwenye kufikisha huduma kwa jamii nchini.
Ahadi yangu kwenu ni kuwa Serikali itaendelea kushirikiana na Kanisa Katoliki pamoja na madhehebu mengine ya dini kuboresha maisha ya Watanzania. Tutaendelea kupokea ushauri wenu na kuwashirikisha katika mambo mbalimbali yanayohusu maendeleo ya nchi yetu na watu wake. Naomba muendelee kushirikiana na Serikali katika kutoa huduma kwa wananchi. Muendelee kutumia mtandao wenu mpana uliopo nchi nzima kwa ustawi na maendeleo ya nchi yetu. Lengo letu libaki kuwa moja daima na milele. Tufanye kazi pamoja ili tufanikiwe zaidi.
Maombi kwa Viongozi wa Dini
Mhashamu Baba Askofu Mkude, Baba Paroko na viongozi wa dini mliopo;
Naomba muongeze juhudi za kuhubiri umoja na kutoa mafundisho ya kuhimiza udugu na mshikamano miungoni mwa Watanzania. Sote tunafahamu kuwa kuna baadhi ya watu wanaofanya juhudi usiku na mchana kuuvuruga upendo, umoja na mshikamano wa wananchi wa Tanzania. Kwa sasa watu hawa hawajafanikiwa lakini tuelewe kuwa hawajachoka na wala hawajaaacha. Wana sifa ya ushetani, maana shetani hachoki wala hakati tamaa katika kuwashawishi wanaadamu kutenda maovu. Na, hawa si ajabu wakathubutu tena na tena. Inatupasa na sisi pia tuwe macho. Naomba msilegeze uzi katika kuwaelimisha waumini wenu waelewe nia mbaya za watu wasioitakia mema nchi yetu, wawaepuke wala wasiwasikilize. Tudumishe upendo, umoja na mshikamano wetu. Sisi sote Mungu wetu ni mmoja kwa nini tuchukiane, tubaguane na hata tuuane kwa sababu ya kutofautiana katika kumuabudu Mungu? Wengine ni ndugu wa damu kwa nini tufarakane kwa namna ya kumsujudia Muumba wetu? Kila mtu aachwe kufuata dini anayoipenda na udugu wetu na umoja wetu kama wanadamu ubaki pale pale. Ipo hatari hata ndugu wa damu tukafarakana kwa sababu ya kuwa dini mbalimbali. Siyo sawa.
Niliwahi kusema siku za nyuma na leo narudia tena kuwa viongozi wa dini wanayo nafasi ya pekee katika kufikisha ujumbe huo kwa watu wote. Hii inatokana na ule ukweli kwamba wanasikilizwa na kuaminiwa sana na waumini wao na watu wengine pia. Wanasikilizwa na watu wengi. Waumini wakielezwa, wakaelewa na wote wakazingatia kuishi kama mafundisho ya viongozi wao, nchi yetu itabaki salama. Hakuna mtu atakayefanikiwa kutufarakanisha na kuichezea amani yetu. Hata kama ni muumini wa dini ya shetani.
Pili, naomba tuendelee kusaidiana kulea nchi yetu kimaadili. Hakuna siri kwamba kuna mmonyoko mkubwa wa maadili mema. Vitendo viovu na mambo yasiyoipendeza jamii na yasiyompendeza Mwenye Mungu yanazidi kuongezeka kwenye jamii. Mambo ambayo siku za nyuma yalikuwa nadra sana kutokea au kusikika sasa yanakuwa habari za kila siku na wakati mwingine huonekana ati ndiyo usasa. Matumizi makubwa ya dawa za kulevya, ngono, ubakaji, watoto kutokuheshimu wakubwa, wazee kutokujiheshimu, ulevi wa kupindukia, vitendo vya rushwa, uvivu, wizi na idadi kubwa ya ndoa kuvunjika ni vielelezo dhahiri vya hali mbaya ya kimaadili inayokabili jamii zetu nchini.
Kuporomoka kwa maadili ni jambo lenye athari mbaya kwa jamii na taifa kwa ujumla. Kunachangia sana kurudisha nyuma juhudi za kujiletea maendeleo ya nchi yetu na watu wake. Kunaifanya kazi ya kuondoa umaskini kuwa ngumu na kuongeza watoto wa mitaani. Kunachangia kuenea kwa maambukizi ya UKIMWI. Kunaongeza uhalifu wa aina mbalimbali nchini pamoja na mauaji.
Mimi naamini kwa dhati kuwa watu wakishika mafundisho ya dini, wakamuogopa Mwenyezi Mungu, maovu mengi yatapungua. Hayawezi kuisha kabisa lakini yatapungua sana. Ndiyo maana narejea ombi langu ninalolitoa mara kwa mara kwa viongozi wa dini zote. Tusaidiane kulea taifa letu kimaadili. Tuweke mkazo zaidi kwa vijana kwa sababu, kwanza wao ndio walengwa wakuu wa maovu yanayotendeka. Lakini pili, wao ndio taifa la leo na kesho, ndio warithi wa taifa letu. Tukiwaandaa vyema, mustakabali wa taifa letu na watu wake utakuwa kwenye mikono salama. Tukishindwa leo, tutalia na kusaga meno kesho. Taifa letu litakuwa mashakani.
Mwisho
Kwa kumalizia nawapongeza wote walioshiriki kwa namna moja ama nyingine kuandaa sherehe hizi. Kwa kweli zimefana sana na watu wote hapa ni mashahidi. Nakushukuru kwa mara nyingine tena Mhashamu Baba Askofu na Baba Paroko kwa uongozi wenu uliotukuka. Nimefurahi sana kujumuika nanyi katika maadhimisho haya. Naomba tuendelee kushirikiana kuleta maendeleo zaidi kwenye Parokia yetu na nchi yetu kwa ujumla. Tukiunganisha nguvu zetu, daima ushindi utapatikana. Naomba tuamue kuwa washindi. Tumsifu Yesu Kristu.
Asante kwa kunisikiliza.

- Oct 28, 2013
Hotuba ya Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimwia Jakaya Mrisho Kikwete wakati wa kufunga semina ya makatibu wa...
Soma zaidiHotuba
Ndugu Phillip Mangula, Makamu Mwenyakiti wa CCM;
Ndugu Abdulrahman Kinana, Katibu Mkuu wa CCM;
Ndugu Manaibu wa Katibu Mkuu;
Ndugu Makatibu wa Sekretariat Mliopo;
Ndugu Wanasemina;
Ndugu Watoa Mada;
Mabibi na Mabwana;
Nakushukuru na kukupongeza sana Katibu Mkuu kwa uamuzi wa busara wa kuwa na mafunzo haya kwa Wenyeviti wa Wilaya, Makatibu wa Wilaya na Makatibu wa Mikoa wa Chama chetu. Nafurahi kwamba mafunzo haya yamefanyika wakati muhimu katika safari yetu ya kuelekea mwaka 2015. Hivi sasa tupo takriban katikati ya safari hiyo. Naamini mafunzo haya yatasaidia kujiweka sawa katika ngwe ya pili ya kipindi cha pili cha uongozi wa Awamu ya Nne ya uongozi wa CCM katika nchi yetu. Awamu ambayo mimi ndiye kiongozi wake kwa niaba ya Chama chetu.
Ni mategemeo yangu kuwa baada ya mafunzo haya, mijadala iliyofuatia na mapendekezo mliyoyatoa mnaondoka hapa mkiwa manahodha bora zaidi wa kuongoza vyema Chama cha Mapinduzi kwenda na kufika salama katika safari yetu ya kuelekea 2015. Mnatoka kwenye mafunzo haya mkiwa na kauli mbiu moja tu kwamba “Ushindi ni Hakika mwaka 2014 na 2015”.
Lengo Kuu la Chama cha Siasa
Ndugu viongozi wenzangu;
Sote tunafahamu kwamba lengo kuu la Chama cha Mapinduzi kama ilivyo kwa vyama vyote vya siasa nchini na duniani ni kushika dola. Hivyo ndivyo Katiba ya CCM inavyotamka wazi katika Ibara ya 5 kwamba malengo na madhumuni ya CCM ni; Nanukuu “Kushinda katika uchaguzi wa Serikali Kuu na Mitaa, Tanzania Bara
na Zanzibar ili kuunda na kushika Serikali Kuu na Mitaa katika Jamhuri ya Muungano kwa upande mmoja na Zanzibar kwa upande wa pili”. Katika mazingira ya nchi yetu ni kushinda uchaguzi wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Rais wa Zanzibar, Wabunge, Wawakilishi, Madiwani na ule wa viongozi wa Serikali za Mitaa, Vijiji na Vitongoji. Hivyo pamoja na majukumu mengine mengi mliyonayo lazima mtambue kwamba hatimaye shabaha yetu kuu ni kuhakikisha kuwa wagombea wa Chama chetu wanashinda katika chaguzi hizo.
Nyie kama viongozi na watendaji wakuu wa maeneo yenu lazima mtambue kuwa chombo cha kutuongoza, kutuimarisha na kutufikisha kwenye ushindi ni Chama cha Mapinduzi. Hivyo basi, lazima Chama kiwe na nguvu ya kutosha ya kutufikisha kwenye lengo letu kuu. Hamna budi kila mnapofanya jambo mpime kama jambo hilo linakisaidia Chama chetu kuwa na nguvu za kushinda uchaguzi au la. Msifanye mambo yatakayoipunguzia CCM nguvu na yanayojenga mazingira yatakayosababisha wagombea wa CCM kushindwa na hivyo Chama chetu kushindwa. Mkifanya hivyo mtakuwa hamkisaidii Chama chetu. Wakati wote kila mmoja wetu ajiulize je hili nilifanyalo linasaidia CCM kushinda? Au kwa lugha nyingine tujiulize ni kitu gani nikifanya kinasaidia Chama cha Mapinduzi kushinda.
Uhai na Uimara wa Chama
Ndugu viongozi wenzangu;
Kwa maoni yangu kuna mambo matatu muhimu ambayo yakifanyika yatasaidia Chama cha Mapinduzi kushinda:-
(1) Uimara wa Chama;
(2) Tabia na mwenendo wa viongozi na wanachama wa CCM; na,
(3) Utendaji wa Serikali ya CCM.
Inatupasa kuhakikisha kuwa Chama chetu kinashiriki katika uchaguzi ujao wa Serikali za Mitaa na Uchaguzi Mkuu kikiwa na nguvu kubwa, hai na imara kwa kila hali toka ngazi ya shina, tawi, kata, jimbo, wilaya, mkoa hadi taifa. Siku za nyuma nilishasema kuwa Chama ni kama ulivyo mwili wa mwanadamu, uimara wake unategemea sana ukamilifu na uzima wa viungo vyake. Kikipungua kiungo kimojawapo Chama kina ulemavu na kikidhoofika chochote kinakuwa na afya mbaya. Kwa ajili hiyo basi uimara wa Chama cha Mapinduzi unategemea kuwepo kwa wanachama, viongozi, watendaji, vikao, rasilimali na jumuiya za Chama na vyote vikiwa vinafanya kazi zake ipasavyo.
Ninyi mliopo hapa yaani Wenyeviti wa Wilaya, Makatibu wa Wilaya na Makatibu wa Mikoa ndiyo mnaotegemewa zaidi kuliko mtu mwingine yeyote kuhakikisha kuwa viungo vya Chama vinakamilika na kwamba viko hai kwa maana ya kufanya kazi kama inavyotarajiwa kwa mujibu wa Katiba ya Chama cha Mapinduzi, sera na maamuzi mbalimbali.
Ndugu viongozi;
Ni matumaini yangu na nimehakikishiwa hivyo kwamba katika mafunzo haya mmepewa maarifa ya kuhakikisha kuwa Chama cha Mapinduzi kinakuwa hivyo. Mmejifunza juu ya nini mnachowajibika kufanya ili Chama chetu kiwe imara, hai na chenye nguvu. Nimeambiwa pia kuwa katika majadiliano mlipata nafasi ya kubadilishana uzoefu kutoka kwa wale waliofanikiwa na hata wale walioshindwa. Ndugu zangu mpate nini zaidi ya hayo. Mfanyiwe nini tena lililo bora zaidi kuliko hilo. Ndiyo maana sipati kigugumizi kusema kuwa sasa ninyi mmekuwa wapiganaji bora zaidi. Haya nendeni mkaoneshe umahiri wenu kwenye medani ya kujenga Chama. Nendeni mkaoneshe mtindo bora wa uongozi na utendaji. Nendeni mkakipe Chama chetu sura mpya, uhai mpya na kasi mpya ya maendeleo.
Kuingiza Wanachama
Ndugu Viongozi;
Hatuna budi kwanza kabisa kuhakikisha kwamba Chama chetu kinapata wanachama wapya wengi na kuwaimarisha waliopo. Wanachama ndiyo kielelezo cha awali cha kuwepo kwa Chama. Wingi wa wanachama ndio nguvu ya kufanya kazi ya Chama na mtaji wa uhakika wa kuanzia katika kutafuta ushindi. Hivyo basi, lazima wakati wote Chama chetu kiendelee kuingiza wanachama wapya. Tusisubiri mpaka karibu au wakati wa uchaguzi ndipo tuongeze nguvu ya kusajili wanachama wapya. Twende tukafanye kazi ndani ya umma kuwashawishi na kuwahamasisha wananchi, hususan vijana, kujiunga na Chama cha Mapinduzi. Mnapaswa kuwa na mikakati madhubuti ya kupata wanachama wapya katika maeneo yenu. Kupata wanachama wapya ni kazi ya kudumu ya Chama.
Ndugu viongozi;
Kimsingi uimara wa Chama chetu unategemea uhai wa wanachama wake. Mwanachama hai wa CCM ni yule anayelipa ada na kushiriki kwa ukamilifu katika shughuli za Chama, mojawapo ikiwa kuwashawishi watu wasiokuwa wanachama kuunga mkono CCM. Ili wanachama wawe hivyo ni wajibu wa viongozi kuwa na mikakati maalum ya kuwawezesha kufanya hivyo. Kuwatembelea mara kwa mara kuzungumza nao na kuwaelimisha mambo mbalimbali yanayohusu Chama na nchi kwa ujumla ni mbinu muhimu sana kwa ajili hiyo. Tukifanya hivyo Chama chetu kitakuwa na wanachama wengi wanaojua mambo na wenye moyo wa kukitumikia. CCM itakuwa na uwezo mkubwa wa kujiendesha na kufanya mambo yake. Kitakuwa kimeimarika zaidi. Viongozi wa Chama lazima tujenge mazoea ya kuwatembelea wanachama na kuzungumza nao. Hili ndilo jukumu la msingi na asiyefanya hivyo ameshindwa kutimiza wajibu wake.
Ndugu zangu;
Ni ukweli ulio wazi kuwa si viongozi na watendaji wengi wanaofanya hivyo. Lazima mjisahihishe. Zamani mlidai hamna magari sasa mnayo. Kwa kweli kutowatembelea wanachama ni jambo lisilokuwa na maelezo. Nilishaagiza siku za nyuma na narudia kusisitiza tena leo kuwa katika Taarifa ya kazi za Chama ya kila mwezi kila Wilaya itoe taarifa ya kuhusu viongozi kutembelea matawi na kuzungumza na wanachama. Hivyo hivyo kwa Mikoa, nao watoe taarifa ya kutembelea Wilaya zao na kuzungumza na viongozi wa Wilaya, Kata, Matawi na Mashina pamoja na kuzungumza na wanachama. Ndugu Katibu Mkuu naomba hili lazima tulidai lifanyike kwani manufaa yake kwa uhai wa Chama cha Mapinduzi hayana mfano wake.
Ndugu viongozi;
Jambo la pili muhimu kwa uhai na maendeleo ya Chama chetu ni kuwatembelea wananchi na kuzungumza nao. Ni vyema mkatambua kuwa tunapotaka kuongoza dola kwa mfumo wa vyama vingi kazi yetu kubwa ni ile ya kuwavutia watu upande wetu. Tushinde mioyo na akili zao. Tuwafanye watu waelewe sera na siasa ya Chama cha Mapinduzi, wazikubali na kutuunga mkono. Tufute maneno hasi na uongo wa wapinzani dhidi ya CCM na serikali yake. Lazima viongozi mtoke muwatembelee wananchi, mzungumze nao kuhusu Chama chetu na taifa kwa ujumla. Tumekuwa wazito sana kufanya hivyo, lazima tujirekebishe.
Utendaji wa Serikali
Ndugu viongozi na Watendaji;
Kwa vile hivi sasa CCM ndicho Chama tawala, viongozi wa Chama wanaowajibu wa namna mbili. Kwanza, kuhakikisha kuwa serikali yao inatekeleza Ilani ya Uchaguzi na pili, kuwaelezea wananchi masuala mbalimbali ya utendaji wa serikali. Viongozi wa Chama mmepewa dhamana ya kuyasimamia hayo katika maeneo yenu. Lazima mfuatilie utekelezaji wa Ilani kupitia vikao vyenu hususan Kamati za Siasa na Halmashauri Kuu za Wilaya na Mikoa. Ndiyo maana Wakuu wa Wilaya na Mikoa ni wajumbe wa vikao hivyo na hutoa taarifa ya kazi nyakati mbalimbali.
Ili muweze kufanya hivyo, lazima ninyi wenyewe mfahamu vizuri Ilani ya CCM inasema nini kuhusu Mikoa na Wilaya zenu. Pili, lazima mfahamu ahadi za wagombea wa Chama chetu na za viongozi wa Chama katika ngazi mbalimbali. Lengo ni kujua na kufuatilia utekelezaji wa ahadi hizo ili zisije zikageuka kuwa tatizo katika uchaguzi ujao. Tujue zipi zimetekelezwa, zipi hazijatekelezwa na zilizotekelezwa zimetekelezwa kwa kiwango gani. Tujue mipango iliyopo na nini kinapaswa kufanyika ili kutekeleza au kukamilisha ahadi hizo. Tukumbushane mambo ambayo hayajatekelezwa. Wakumbusheni Marais, Mawaziri, Wabunge, Wajumbe wa Baraza la Wawakilishi, Madiwani na viongozi wa Serikali za Mitaa juu ya ahadi zao walizozitoa ambazo hazijatekelezwa ili wazitekeleze au wawe na mipango thabiti ya kutekeleza.
Pia, ziambieni serikai katika ngazi zote husika kuhusu masuala mapya yaliyojitokeza ambayo wananchi wanataka tuyatekeleze. Tukiweza kuyafanya na hayo pia yatatuongezea kuaminika, kupendwa na kutuongezea uhakika wa kuchaguliwa tena. Naomba mshirikiane na viongozi wa Serikali katika maeneo yenu kutengeneza utaratibu mzuri ili masuala hayo yajulikane na kutengenezwa mkakati maalum wa kuyatekeleza.
Ndugu viongozi;
Tumieni vikao vyenu au njia nyingine za mawasiliano kuyafikisha masuala hayo na mengine. Katika vikao hivyo pia, Wakuu wa Wilaya na Mikoa wanao wajibu wa kuelezea na kufafanua masuala mbalimbali yahusuyo Serikali au Mkoa au Wilaya husika. Wajumbe waulize ili wapate maelezo ya kusaidia kujibu hoja za wananchi au wapotoshaji kwa kazi nzuri za serikali ya CCM.
Vikao
Ndugu Viongozi;
Hatuna budi kuhakikisha kuwa vikao vya Chama vinafanyika na vinaendeshwa vizuri ili viweze kutekeleza ipasavyo jukumu lake la kufuatilia utendaji wa serikali ya CCM na uendeshaji wa Chama. Lazima vikao vya Kikatiba vifanyike bila kukosa na pawepo na kalenda maalum kwa ajili hiyo. Kuwa na kalenda inayojulikana ni muhimu kwa wajumbe kwani wanashughuli zao zinazowapatia riziki hivyo wakijua mapema vikao vya Chama watajua namna bora ya kujipanga. Si vizuri taarifa ya vikao vya Kikatiba ikatolewa kwa muda mfupi kana kwamba ni vikao vya dharura.
Jambo lingine muhimu kuhusu vikao ni kuwa na agenda za maana na zilizoandaliwa vizuri. Kwa mfano, mnaweza mkaamua kila kikao kiwe na agenda ipi kuu katika Wilaya na Mkoa wenu. Mathalani mnaweza kupanga kuwa kikao cha mwezi fulani kiwe cha kupokea taarifa ya utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi, cha mwezi fulani kupokea taarifa ya uhai wa Chama na kadhalika. Mkifanya hivyo mnajipa muda wa kushughulikia masuala muhimu. Hata hivyo haizuiliwi kuzungumzia au kushughulikia masuala mengine muhimu. Ni muhimu pia kuhakikisha kuwa vikao vinaendeshwa vizuri na wajumbe wanapata nafasi ya kutoa maoni yao kwa uhuru. Kumbukumbu za vikao ziandikwe vizuri na kuhifadhiwa vizuri.
Ndugu Katibu Mkuu;
Chama lazima kiwe na utaratibu wa kuwafundisha Makatibu Tawi, Makatibu Kata, Makatibu Wasaidizi, Makatibu wa Wilaya na Mikoa kuhusu uandishi wa kumbukumbu na namna ya kuzihifadhi na kuzifanyia kazi. Lazima pia kiwe na utaratibu wa mafunzo kwa watumishi na watendaji wake wa kada mbalimbali katika ngazi zote za utumishi na utendaji. Chama kina mifumo yake na taratibu zake za kuendesha shughuli ambazo lazima zifuatwe. Ni lazima watu wafundishwe ili wazielewe na kuzifuata. Vile vile ni muhimu Chama kuwekeza katika kuwaendeleza watumishi na watendaji wake kielimu na kitaaluma. Aidha, tuwalipe maslahi mazuri.
Mali za Chama
Ndugu Viongozi na Watendaji;
Jambo lingine muhimu sana katika kuimarisha Chama ambalo naamini mmelizungumzia kwa undani ni rasilimali za Chama kwa Chama kuwa na fedha, majengo, vyombo vya usafiri na vifaa vingine vya kuendeshea shughuli zake ni jambo la kufa na kupona. Lazima tuwe na fedha za kutosha, majego mazuri ya kufanyia kazi, magari na vyombo vingine vya usafiri na vifaa mbalimbali. Lazima tuwe na mipango na mikakati dhabiti ya kuwa na rasilimali hizo na hasa fedha. Katika historia ya Chama chetu vyanzo vikuu vya fedha ni ada za wanachama, uuzaji wa vitabu na mali nyingine za Chama na michango ya hiari. Hali ilivyo sasa ni kwamba wanachama wamekuwa wazito kulipa ada, vitabu na mali za kuuza hazipo za kutosha. Na michango ya hiari haibuniwi. Kwa kweli, Chama siku hizi kinaendeshwa kwa taabu. Wilaya na Mikoa hutegemea Makao Makuu tofauti na ilivyokuwa zamani. Pale ambapo kuna wafadhili ambao ni wabunge wajumbe wa NEC wenye uwezo na wapenzi wa Chama mambo huwa mazuri. Pale ambapo hawapo kuna shida. Aghalabu baadhi ya wafadhili au wapenzi wa Chama ni watu wenye agenda zao. Ama wana tamaa za kugombea uongozi fulani hivyo wananunua kuungwa mkono au wanatafuta msaada fulani.
Mtakubaliana nami kuwa jambo hili muhimu sana kwa uhai wa Chama lakini halijapata mwelekeo mzuri. Lazima tubadilike tena tubadilike haraka vinginevyo mbele ya safari hali itakuwa mbaya zaidi. Hatuna budi kuwa wabunifu na kuongeza jitihada za kukijengea Chama uwezo wa kifedha na rasilimali katika ngazi zote. Tulishatoa maagizo kwa kila ngazi kuwa na mfuko wa uchaguzi, sijui ni wangapi wanao na wana kiasi gani. Na watu hawashtuki. Hali hii haikubaliki lazima tujirekebishe, hatujachelewa. Mtakumbuka katika Mkutano Mkuu uliopita niliagiza majengo na viwanja vyote vya Chama vipatiwe hati. Je, limekalimika?
Maadili
Ndugu viongozi na Watendaji;
Tabia na mwenendo mwema ni sifa ya msingi ya kuwa kiongozi na mtendaji wa Chama cha Mapinduzi. Kwa namna ya pekee kiongozi hutoa taswira ya CCM kwa wananchi na wanachama. Mkiwa wachapa kazi hodari, watu wenye nidhamu na waadilifu ni sifa njema kwa Chama chetu. Mkiwa tofauti na hayo ni sifa mbaya kwa CCM. Naamini haya ninayoyasema yameelezwa vizuri na kusisitizwa sana katika mafunzo haya. Naomba muwayazingatie na kuyatekeleza.
Nendeni sasa mkadhihirishe kuwa ni mfano bora kwa wanachama na wananchi tunaowaongoza. Mkifanya hivyo mtakubalika na kuungwa mkono na wanachama na jamii kwa ujumla. Na hivyo basi chama chetu kitanufaika.
Ndugu viongozi;
Si jambo jema hata kidogo kwa viongozi au watendaji wa Chama kuwa na tabia na mwenendo mbaya wanakiumiza Chama. Jiepusheni kuwa waombaji na wapokeaji wa rushwa. Epukeni kuwa mawakala na wasambazaji wa fedha chafu za wagombea wanaotaka kununua uongozi. Tukifanya hivyo tutaiharibu sana sifa ya CCM. Mtashindwa kusimamia haki na mtakigawa Chama chetu. Ninyi mnategemewa kuwa wasimamizi wa michakato ya uchaguzi lazima mtende haki na muwe waadilifu. Mkikubali kuhongwa au kuwa wakala wa mgombea mtawanyima haki baadhi ya wagombea na itakuwa vigumu kwenu kutatua malalamiko yanayotokea kwa sababu ninyi wenyewe ni sehemu ya tatizo. Isitoshe wagombea watapoteza imani kwa viongozi na watendaji wa Chama chao, jambo ambalo ni la hatari. Linalofanya watu kupata hasira na wengine kufanya uamuzi usiotarajiwa na kukiathiri Chama. Katika maeneo mengi tuliyopoteza katika uchaguzi uliopita upendeleo wa viongozi kwa wagombea ulichangia sana. Hakikisheni kasoro za chaguzi zilizopita hazijirudii tena siku za usoni. Msije mkakiingiza Chama kwenye matatizo yanayoweza kuepukika.
Ndugu viongozi na Watendaji;
Kabla ya kumaliza, ningependa kuwakumbusha kuwa Chama chetu kupitia serikali yake kimefanya mambo mengi mazuri kwa maendeleo ya nchi yetu na watu wake. Sina shaka ifikapo 2015 tutakuwa tumefanya vizuri zaidi na hivyo hatutasutwa kwa kutokuwa wakweli. Kwa ajili hiyo sioni sababu kwa nini tusifanye vizuri katika chaguzi za 2014 na 2015. Lakini, tutaweza kutokufanya vizuri iwapo tutafanya makosa katika uteuzi wa wagombea. Tukiteua watu wasiokubaliwa na jamii kwa sababu ya urafiki, ujamaa au kwa kupewa chochote binafsi zetu, jamii itatuadhibu. Anayedhani kuwa kila aliyeteuliwa na CCM atachaguliwa anajidanganya. Wakati huo umepita. Tupate wagombea wazuri tusiendekeze rushwa. Tusiwaonee au kuwadhulumu watu na kuwafanya wajenge chuki dhidi ya Chama chetu na hata kususa au kufanya matendo ya kukidhuru Chama. Tusiwasukume watu ukutani bila ya sababu acheni mambo yawe wazi, ushindi uwe wa haki ili mtu akishindwa ajue kuwa haikuwa bahati yake. Mtu mwenye upungufu aambiwe kasoro zake kama ilivyo mila na desturi ya CCM. Si vizuri mtu ajione kaonewa au kadhulumiwa na viongozi wa Chama waliopokea rushwa kutoka kwa wagombea au wanaomchukia. Nalisema hili kwa sababu habari zimezagaa za watu wanaojipanga kugombea uongozi kuwa wanahonga sana viongozi na watendaji wa CCM. Mzee Mangula analishughulikia hilo. Nawasii mjiepushe nao msije mkakutwa kuhusika, mtapata matatizo makubwa. Lazima tulinde na kudumisha heshima ya Chama chetu.
Ndugu viongozi na watendaji;
Nimalizie kwa kuwapongeza watoa mada kwa kazi nzuri waliofanya ya kutoa mafunzo kwa viongozi wetu hawa. Viongozi wenzangu tusiwaangushe wakufunzi wetu kwa kutoonesha mabadiliko katika uongozi na utendaji wetu baada ya mafunzo hayo. Nawatakia safari njema na utendaji ulio bora zaidi.
Baada ya kusema haya, natamka rasmi kwamba, semina yenu imefungwa. Asanteni kwa kunisikiliza.

- Oct 28, 2013
Speech by his excellency Dr. Jakaya Mrisho Kikwete, President of the United Republic of Tanzania during launching of the 4th Tanzania deep offshore and north l...
Soma zaidiHotuba
Honourable Professor Sospeter Muhongo, Minister for Energy and Minerals;
Mr. Michael Peter Mwanda, Chairman of the Board of Directors of Tanzania Petroleum Development Corporation (TPDC);
Mr. Yona Killagane, Managing Director of Tanzania Petroleum Development Corporation (TPDC);
Mr. Brian Horn, Representative of ION-GXT;
Mr. Stewart Walter, Representative of WesternGeco;
Distinguished Representatives from Petroleum Industry;
Invited Guests;
Ladies and Gentlemen;
I thank you, Minister Muhongo, for inviting me to officiate at this auspicious and historic occasion of launching the 4th Licensing Round for Deep Offshore blocks and Lake Tanganyika North block. I am saying this occasion is auspicious and historic because it is important and it is the first time a Licensing Round is held in Tanzania. All the other rounds took place in Europe and America. In fact, it was on my advice that this Round is being held here. It was originally planned to be held in Houston Texas.
Oil and gas exploration in Tanzania has a long and interesting history. It started in 1952 when British Petroleum (BP) and Shell International Oil Company (SHELL) were jointly awarded a concession covering the onshore coastal basins and the islands of Zanzibar, Pemba and Mafia. Extensive geological and geophysical surveys were undertaken. Four deep exploration wells were drilled. These were Pemba-5 on Pemba Island, Zanzibar-1 on Zanzibar Island, Mafia-1 on Mafia Island and Mandawa-7 in Lindi Region. Unfortunately, the mission was not successful and the two companies relinquished the concession in 1964.
Ladies and Gentlemen;
In 1969, the government decided to establish a national oil company, hence the Tanzania Petroleum Development Corporation (TPDC). It was tasked, among other functions, to spear head and coordinate all activities related to exploration of oil and gas in the country. Subsequently, the concession previously held by BP and SHELL was awarded to AGIP who were later joined by AMOCO. AGIP conducted the necessary surveys and drilled five deep exploration wells including Ras Machuisi-1, Songo Songo-1, Kisangire-1, Kisarawe-1 and Kizimbani-1. Luckily, these exploration efforts were not in vain. They revealed the presence of natural gas in Songo Songo-1 well. However, the evaluation indicated that the reserve, of around 4 Billion Standard Cubic Feet, was not of commercial quantity. In 1974, AGIP relinquished the Songo Songo licence.
Ladies and Gentlemen;
Our determination was not withered by the disappointment of previous two attempts. TPDC undertook further evaluation of the Songo Songo property by acquiring more seismic data and drilled three more wells. This extra effort and perseverance, was rewarded with the discovery of more natural gas and the new reserve estimates became 43 billion standard cubic feet.
Ladies and Gentlemen;
This new discovery then raised the interests of oil companies as a result exploration activities increased. New exploration licences were issued to SHELL in Ruvu, Selous, Mandawa and Mafia; International Energy Corporation (IEDC) in Tanga; ELF in Mafia and Nyuni; AMOCO in Lakes Tanganyika and Rukwa and TEXACO in the Ruvuma basin. These operators carried out geological and geophysical surveys and drilled a total of four exploration wells. This time round, AGIP was lucky as before. In 1982, they made another gas discovery at Mnazi Bay-1, in Mtwara. Once again, however, AGIP declared the discovery as non-commercial.
TPDC carried out seismic data acquisition onshore and offshore to promote open acreage and also drilled two exploration wells of Kimbiji-1 onshore and Tan-Can-1 offshore. Five gas appraisal wells were also drilled in the Songo Songo gas field. New reserve estimates became around 1 trillion Standard Cubic Feet (1Tcf), paving way for development. And the costs for appraising the Songo Songo gas field were around U.S. $ 100 million while costs for the two other wells were around U.S. $ 10 million.
Ladies and Gentlemen;
The exploration for oil and gas in the deep offshore Tanzania commenced in 1999. Players in the deep sea include Statoil and Exxon Mobil, BG and Ophir, Petrobras and Shell, and Dominion Oil and Gas. The first deep offshore well which became a discovery was completed in October 2010 in Block number 4. The wells drilled afterwards in the deep sea namely Jodari 1, Jodari North 1, Jodari South 1, Mzia 1, Mzia 2, Chaza 1, Pweza 1, Chewa 1, Ngisi 1, Papa 1, Zafarani 1, Zafarani 2, Lavani 1, Lavani 2 and Tangawizi 1 were all successful with the exception of Zeta 1. In this regard, we have been able to increase our natural gas reserves from 7.5 trillion standard cubic feet in 2003 to 43.1 trillion. Indeed these discoveries have transformed Tanzania into a hot spot for oil and gas exploration.
In view of the latest positive development in the oil and gas sector it became apparent that there was need to do a comprehensive review of the way we conduct the affairs of the sector. As a result of this we are in the process of putting in places a gas policy framework to ensure smooth operations of the industry. We have also reviewed the term of the Production Sharing Agreement (PSA) and we are taking concrete measures to improve investment climate in the country. As some foreign companies have confessed to me that our investment incentives are arguably among the best in the African Continent. This makes us feel good in the sense that we are as competitive as other players in the market. No wonder therefore, that we have 24 active PSA’s and 17 operators in the oil and gas industry in our dear country.
Ladies and Gentlemen;
The duty at hand for us is to ensure that there is a fair and a level playing field for operators and investors in the oil and gas industry and other sectors of the economy. This in our view will enhance further flow of foreign capital and technology in the country and intensify exploration and make more discoveries.
I wish to take this opportunity to assure all investors in the oil and gas industry and other sectors of the economy that Tanzania is ready and willing to do business with you. We are ready to facilitate your business and ensure that your investment is safe for our mutual benefits. We have the necessary institutional and regulatory frameworks in place. We will always endeavor to continue to improve the investment climate, provide efficient and effective regulatory framework and improve our infrastructure in order to reduce the costs of doing business. We intend to develop our human resource to match the requirements of the oil and gas industry. Our dream is to create a situation whereby the government, investors and the people of Tanzania will emerge as winners. There should be no loser in our envisaged set-up. In this regard, the spirit of partnership and cooperation is key.
Ladies and Gentlemen;
We all know that poorly planned petroleum operations may become an environmental hazard affecting people, land, water, plants and animals through pollution. Unfortunately, some of the negative effects of pollution are irreversible. It will be futile on our and an act of gross irresponsibility if we undertake poorly planned exploration activities that will have negative impacts to the environment. It will be adversely affect us and fortune generations. In this regard, it is important for oil and gas companies operating in Tanzania to abide by the operations guidelines and law. We want our resources to be a “blessing” not a “curse”.
While exploring and developing oil and gas resources, I urge you to seriously consider the emerging home and regional market which is growing fast. This market has a high demand of gas for power generation and industrialization. You must be aware that there is demand for gas here in Tanzania and in the region, therefore, plan to meet this demand first before considering to export to other markets elsewhere. Rest assured that the gas will not be sold at give away prices. Our ambition is to see to it that this important resource is playing an important role in promoting growth and development of our country. Let us work together towards realizing this dream.
After those many words, it is now my singular honour and pleasure to declare the historic 4th Licensing Round of the Deep Offshore and North Lake Tanganyika officially launched. I wish you all the best.
Thank you for kind attention.

- Oct 15, 2013
Hotuba ya Mheshimiwa Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwenye sherehe ya kilele cha mbio za mwenge wa uhuru, kumbukumbu ya ba...
Soma zaidiHotuba
Mheshimiwa Anne Makinda, Spika wa Bunge;
Mheshimiwa Dkt. Fenella Mukangara, Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo;
Mheshimiwa Zainab Mohamed, Waziri wa Uwezeshaji, Ustawi wa Jamii, Vijana, Wanawake na watoto - Zanzibar;
Waheshimiwa Mawaziri na Nanaibu Mawaziri;
Mheshimiwa Dkt. Christine Ishengoma, Mkuu wa Mkoa wa Iringa;
Waheshimiwa Wabunge na Wajumbe wa Baraza la Wawakilishi;
Makamu Mwenyekiti wa CCM (wa Mkoa) na Viongozi wa Vyama vya Siasa mliopo;Waheshimiwa Mabalozi na Wawakilishi wa Mashirika ya Kimataifa, Viongozi wa Serikali wa Ngazi mbalimbali za Taifa na Mkoa;
Wageni Waalikwa;
Ndugu Wananchi;
Mabibi na Mabwana;
Shukrani
Niruhusuni nianze kwa kumshukuru Mwenyezi Mungu, mwingi wa rehema, kwa kutujaalia uzima na kutuwezesha kukutana tena mwaka huu kuadhimisha Kilele cha Mbio za Mwenge wa Uhuru, kumbukumbu ya Baba wa Taifa hayati Mwalimu Julius Nyerere na Wiki ya Vijana. Namshukuru sana Mkuu wa Mkoa wa Iringa, na viongozi wenzake pamoja na wananchi wa Iringa kwa kutupokea vizuri na ukarimu wenu. Pia nawapongeza kwa kukubali kuwa wenyeji wa maadhimisho haya. Kazi ya kuandaa sherehe kubwa kama hizi siyo jambo jepesi hata kidogo. Bahati nzuri mambo yamefana sana kama tunavyoshuhudia sote. Hongereni sana.
Pongezi Wizara
Ndugu wananchi;
Niruhusuni pia nitoe pongezi nyingi kwa Mheshimiwa Dkt. Fenella Mukangara, Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo na Mheshimiwa Zainab Omary, Waziri wa Uwezeshaji, Ustawi wa Jamii, Vijana, Wanawake na Watoto wa Zanzibar kwa uongozi wao makini wa shughuli za Mbio za Mwenge. Kama tujuavyo shughuli za Mbio za Mwenge husimamiwa na Wizara zetu hizi mbili. Tunawapongeza kwa kazi nzuri waifanyayo. Ni ukweli ulio wazi kuwa kila mwaka tunashuhudia mambo yakiwa bora zaidi kuliko mwaka uliopita. Mcheza kwao hutunzwa. Hongereni sana.
Pamoja na Mawaziri napenda kuwatambua viongozi na wafanyakazi wote wa Wizara zetu mbili waliohusika na Mbio za Mwenge kwa kazi yao nzuri tunayojivunia sote. Aidha, nawapongeza Wakuu wa Mikoa na Wilaya, viongozi na watumishi wa Serikali zetu mbili na wajumbe wote wa kamati mbalimbali walioshiriki katika kuratibu Mbio za Mwenge wa Uhuru mwaka huu. Wamefanya kazi nzuri inayostahili kupongezwa na kila mmoja wetu.
Kwa namna ya pekee nawapongeza ndugu Juma Ali Sumai, kiongozi wa Mbio za Mwenge na Wakimbiza Mwenge wenzake kwa kutimiza kwa ufanisi wa hali ya juu jukumu kubwa na zito la kukimbiza Mwenge wa Uhuru nchi nzima. Nawapa pole nyingi kwa changamoto mbalimbali walizokumbana nazo katika safari ya kilomita nyingi. Kazi hiyo wameimaliza salama na leo wameukabidhi Mwenge ukiwa salama. Nawapongeza sana kwa kuufikisha ujumbe wa Mwenge kwa uhodari mkubwa.
Waheshimiwa Mawaziri;
Ndugu wananchi;
Nafurahi kusikia kuwa kama ilivyokuwa miaka iliyopita, mwaka huu watu walijitokeza kwa wingi kila mahali Mwenge wa Uhuru ulipopita. Pia nimeambiwa ujumbe wa Mwenge ulifikishwa kwa ufasaha na kwamba umepokelewa vizuri. Miradi mingi ya maendeleo imezinduliwa na kuwekewa mawe ya msingi.
Napenda kuchukua nafasi hii kuwapongeza kwa dhati kabisa wananchi wa Tanzania kwa ushiriki wao mzuri katika Mbio za Mwenge. Ushiriki wao ni kielelezo tosha cha kutambua umuhimu wa Mwenge wa Uhuru na cha moyo wa uzalendo kwa nchi yetu na kuwaenzi waasisi wa taifa letu. Kwa niaba ya Serikali nawahakikishia kuwa tutaendelea kuwahimiza viongozi wa ngazi mbalimbali kuhakikisha kuwa miradi yote iliyozinduliwa na kuwekewa mawe ya msingi wakati wa mbio za Mwenge wa Uhuru inaendelea kutekelezwa kama ilivyokusudiwa.
Kwa namna ya pekee nawapongeza waandishi na vyombo vya habari kwa kuwa nasi bega kwa bega kuhamasisha watu na kueneza ujumbe wa Mwenge. Mchango wao umesaidia sana kufanikisha malengo ya Mbio za Mwenge kwani siku zote wapotoshaji hawakosekani.
Kumbukumbu ya Baba wa Taifa
Ndugu Wananchi;
Kama mjuavyo siku ya kilele cha Mbio za Mwenge pia ni siku ya kuadhimisha kumbukumbu ya kifo cha Baba wa Taifa letu la Tanzania kilichotokea miaka 14 iliyopita. Ni siku ambayo tunawajibika kukumbuka mema mengi aliyoifanyia nchi yetu, mafundisho yake na urithi aliotuachia. Nia yetu ni kutaka watu wasimsahau kiongozi wetu huyu maalum na muhimu sana katika historia ya nchi yetu.
Miongoni mwa mambo ya kukumbuka hasa wakati huu wa Mchakato wa Katiba Mpya ni (jambo la busara kutumia muda wetu) kujikumbusha mawazo ya Mwalimu kuhusu umoja wa nchi yetu pamoja na Muungano wa Zanzibar na Tanganyika. Hotuba zake na maandishi yake kuhusu mambo hayo yana mafundisho mengi mazuri ambayo tukiyaelewa vyema na kuyazingatia yatatusaidia sana katika mjadala na ukamilishaji wa mchakato wa Katiba mpya.
Mimi naamini fikra za Mwalimu na mtazamo wake kuhusu umoja wetu na Muungano bado vina maana hata leo. Tujiepushe na kuyapuuza tusije tukawa na Katiba itakayolibomoa taifa badala ya kulijenga. Ninaposema hivyo sipendi nieleweke kuwa sitaki mabadiliko ila napenda tuwe makini katika kufanya mabadiliko. Nataka tufanye mabadiliko yatakayotupeleka mbele na siyo kuturudisha nyuma.
Ndugu wananchi;
Pamoja na kuadhimisha siku ya kifo cha Baba wa Taifa (Mwalimu Julius Nyerere), nadhani ni vyema pia tukawa tunaikumbuka siku ya kuzaliwa kwake yaani tarehe 13 Aprili (1922). Nisingependa kujiingiza katika mjadala wa siku ipi bora zaidi kwani zote ni siku muhimu katika historia ya maisha ya mwanadamu. Tofauti yake ni kuwa siku ya kuzaliwa ni ya furaha na siku ya kufa ni ya majonzi. Kama tutakubaliana tuikumbuke na siku yake ya kuzaliwa pengine siku hiyo tungeiita Nyerere Day. Tuiadhimishe siku hiyo kusheherekea maisha yake kwa kujadili kazi zake na kufanya shughuli mbalimbali kuenzi mambo mema aliyosimamia na kuifanyia nchi yetu na dunia kwa ujumla.
Kauli Mbiu ya Mbio za Mwenge wa Uhuru 2013
Ndugu Wananchi;
Kama alivyoeleza Mheshimiwa Waziri kila mwaka Mbio za Mwenge wa Uhuru huwa na ujumbe maalum unaobebwa na kauli mbiu ya mwaka huo. Mwaka huu ujumbe ulikuwa “Watanzania ni Wamoja: Tusigawanywe kwa Msingi wa Tofauti Zetu za Dini, Itikadi, Rangi na Rasilimali”. Ujumbe huu ni muafaka kabisa hasa ukikumbuka misukosuko na majaribu makubwa nchi yetu iliyopitia mwaka huu. Hivyo kutumia Mbio za Mwenge wa Uhuru kukumbushana haja na hoja za kuziba nyufa zilizoanza kujitokeza ni jambo la busara sana. Ni jambo la kuungwa mkono na kila mwananchi na hasa kila mzalendo.
Bahati nzuri upepo huo mbaya umepita na tuombe usirudi tena. Hivi sasa hali ni shwari na Watanzania tunaendelea kushirikiana vizuri bila ya kubaguana kwa dini zetu, vyama vya siasa na kadhalika kama tulivyozoea kuishi miaka yote. Waliotaka kutufarakanisha hawakufanikiwa lakini, lazima tuwe makini kwani wanaweza kujaribu tena kutugawa ama kwa yale yale au mambo mengine.
Ndugu wananchi;
Kwa kweli nafarijika sana kuona Watanzania wakiendelea kukataa ushawishi na uchochezi wa kugawanywa kwa misingi ya dini au mambo mengine. Ndugu zangu naomba tuendelee hivyo na hayo ndiyo mafundisho mema na urithi aliotuachia Baba wa Taifa tunayemkumbuka leo. Tukigawanyika, nchi yetu itavurugika na sote tutakuwa tumeharibikiwa. Dhambi kubwa ya kubaguana kwa misingi yo yote ile ni kupotea kwa amani na utulivu. Bila amani, hatuwezi kuishi kwa furaha katika nchi yetu hii nzuri. Bila amani, jamii haiwezi kujishughulisha kwa ukamilifu na shughuli za kujiletea maendeleo. Amani ikituponyoka nchi yetu itayumba na hakuna atakayebaki salama.
Napenda kuwahakikishia wananchi wenzangu wote, kuwa sisi Serikalini tutaendelea kufanya kila tuwezavyo kujenga, kulinda na kudumisha umoja na mshikamano wetu ambao ndio msingi mkuu wa kuwepo kwa amani na utulivu nchini. Tutaendelea kukemea kwa nguvu zetu na uwezo wetu wote vitendo vinavyosababisha mmomonyoko wa umoja na mshikamano wetu. Serikali haitasita kuchukua hatua za kisheria dhidi ya mtu au kikundi cha watu watakaojihusisha na vitendo vya kuvuruga amani ya nchi yetu. Naomba Watanzania wenzangu mtuelewe hivyo. Napenda kusisitiza na kuwasihi kuwa tuendelee kuaminiana, kuheshimiana na kuvumiliana pamoja na tofauti zetu.
Mapambano Dhidi ya UKIMWI
Ndugu wananchi;
Pamoja na ujumbe huu maridhawa ambao kimsingi ndiyo ujumbe mkuu wa Mbio za Mwenge tangu kuasisiwa kwake, mwaka huu wananchi waliendelea kuhimizwa kuendeleza mapambano dhidi ya ugonjwa wa UKIMWI, rushwa na dawa za kulevya. Tangu ugonjwa wa UKIMWI uingie nchini kwetu mwaka 1983, inakadiriwa kuwa zaidi ya ndugu zetu milioni 2 wamepoteza maisha kutokana na maradhi haya. Hali kadhalika zaidi ya watoto milioni 1.3 wamekuwa yatima na watu zaidi ya milioni 1.5 wanaishi na VVU hivi sasa. Bahati mbaya karibu asilimia 65 ya hao ni wanawake.
Kitaifa, takwimu zinaonesha kuwa maambukizi ya UKIMWI yanazidi kupungua kutoka asilimia saba mwaka 2005 hadi asilimia 5.7 mwaka 2010 na kufikia asilimia 5.1 mwaka 2012. Hapa Iringa napo maambukizi yamekuwa yanapungua ingawaje bado yapo juu na kwamba ni Mkoa wa pili nchini kuwa na kiwango cha juu cha maambukizi. Takwimu zinaonesha kuwa kiwango cha maambukizi Mkoa wa Iringa ni asilimia 9.1, wanaume asilimia 6.9 na wanawake asilimia 10.9. Mkoa wa Njombe ndiyo unaoongoza ukiwa na asilimia 14.8.
Kwa sababu ya maradhi haya idadi ya watoto yatima ni kubwa katika mkoa huu (inakadiriwa kuwa waliopo ni 3400). Inahuzunisha sana kusikia au kuona baadhi ya watoto hawa wamelazimika kukatisha masomo yao baada ya wazazi wao kufariki ili kuwalea wadogo zao. Kwa ajili hiyo, wamelazimika kufanya kazi zisizostahili kufanywa na watu wa umri wao. Wapo pia wazee ambao kwa umri wao wanahitaji kulelewa lakini wamebaki peke yao na wakati mwingine wanalazimika kulea watoto walioachwa na watoto wao.
Ndugu wananchi;
Nilishaagiza viongozi siku za nyuma na leo narudia tena kuwa, tuwatambue watoto yatima kisha tutengeneze mipango thabiti ya kuwasaidia. Lengo letu hapa ni kutaka tuwawezesha kupata fursa ya kukua na kuishi kama watoto wengine. Jambo moja muhimu nililolisisitiza ni kuwa tuhakikishe kuwa vijana hawa wanapata elimu ambayo ndiyo ufunguo wa maisha yao.
Ndugu wananchi;
Tuongeze ari, nguvu na kasi ya kupambana na gonjwa hili hatari. Ni kweli tunapata mafanikio lakini hayatoshi. Kiwango bado ni cha juu mno. Nawaomba viongozi wa Serikali, dini, asasi za kijamii, wanasiasa na wananchi tuendelee kuhamasisha jamii kujiepusha na ugonjwa huu. Tuwahimize watu wajitokeze kupima wajue mustakabali wao, waepuke ngono nzembe na hasa hasa wawe na subira na waaminifu kwa ndoa zao au wapenzi wao. Sisi katika Serikali tutaendelea kutimiza wajibu wetu wa kuelimisha na kuhakikisha kuwa dawa za kufubaza vijijidudu vya UKIMWI zinapatikana bure kwa waathirika waliofikia hatua ya kutumia dawa hizo.
Natoa wito kwa wananchi wa Mkoa wa Iringa kuongeza juhudi maradufu kutokana na ukweli kwamba kiwango cha maambukizi kiko juu mno. Watu waendelee kujitokeza kwa wingi kupima kwa hiari ili kujua afya zao. Katika zoezi la kupima kwa hiari hapa Iringa, watu 388,071 wamejitokeza kupima. Jambo hili ni jema sana. Napenda pia kuchukua fursa hii kuwasihi akina mama wajawazito wawe mstari wa mbele kupima VVU ili wale walioathirika waitumie ipasavyo huduma ya kuzuia maambukizi ya VVU kutoka kwa mama kwenda kwa mtoto. Huduma hii inamfanya mtoto anayezaliwa na mama aliyeathirika kuwa salama. Huduma hii ipo kote nchini na inatolewa katika hospitali zote za Serikali.
Ndugu wananchi;
Ombi langu maalum kwa wanaume, kote nchini ambao bado hawajafanyiwa tohara wajitokeze kwa wingi kufanya hivyo. Madaktari wanasema kuwa mwanaume aliyefanyiwa tohara anapunguza kwa kiasi kikubwa hatari ya kuambukizwa VVU wakati wa kujamiiana. Naomba ieleweke kuwa sisemi mtu akifanyiwa tohara hapati UKIMWI. La hasha. Ninachosema ni kwamba ukimlinganisha na yule ambaye hakufanya hivyo, uwezekano wa kuambukizwa unapungua. Wanasema asiye na tohara ana uwezekano mkubwa zaidi wa kupata michubuko ambayo hurahisisha virusi kuingia kwenye mwili wake. Narudia kusisitiza mtu akipata tohara asidhani yuko salama kabisa. Watu wote lazima wachukue tahadhari stahiki.
Ndugu wananchi;
Ombi langu la pili ni kwa watu wanaotumia dawa za kufubaza virusi vya UKIMWI wasiache kuzitumia. Wakiacha kwa sababu yo yote ile wanavipa vijidudu nafasi kujiimarisha na hivyo kuhatarisha maisha yao. Ombi langu la tatu ni kwa jamii kuendelea kuwasaidia na kuwahudumia wenzetu ambao wameathirika badala ya kuwanyanyapaa na kuwatenga. Na, muhimu zaidi tuwasaidie watoto yatima na wazee ambao wameachwa bila msaada wowote.
Nawataka viongozi wote katika ngazi mbalimbali washiriki kwa ukamilifu katika mapambano dhidi ya maradhi ya UKIMWI. Ofisi ya Waziri Mkuu, Wizara ya Afya na TACAIDS waendelee kuongoza mapambano hayo bila kuchoka. Mimi bado naamini Tanzania bila UKIMWI inawezekana iwapo tutazingatia masharti ya kuepuka ugonjwa huu na kuwahudumia ipasavyo walioathirika. Ushindi hauko mbali sana.
Mapambano dhidi ya Rushwa
Ndugu wananchi;
Mwaka huu, katika Mbio za Mwenge wa Uhuru wananchi waliendelea kukumbushwa wajibu wao katika kupambana na rushwa, kwa kauli mbiu isemayo “chukua hatua dhidi ya rushwa sasa”. Ujumbe huu unakwenda sambamba na juhudi za serikali za kupambana na rushwa nchini. Tunafahamu kuwa rushwa ni adui wa haki na kikwazo kikubwa cha maendeleo ya jamii na taifa. Nchi ikiwa imegubikwa na vitendo vya rushwa itakosa maendeleo stahiki na watu watadhulumiwa haki zao.
Hizo ndizo sababu kuu zilizoifanya serikali yetu ichukie rushwa na kuchukua hatua za kupambana na uovu huu, tangu nchi yetu ilipopata uhuru mpaka sasa. Kazi hiyo ngumu na yenye changamoto nyingi inaongozwa na Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU). Serikali imechukua na itaendelea kuchukua hatua mbalimbali za kuimarisha chombo hiki ili kiweze kutimiza majukumu yake kwa ufanisi zaidi. Matokeo yake TAKUKURU sasa ina mtandao mpana zaidi. Ina ofisi kila Mkoa na kila Wilaya, watumishi wameongezeka na vitendea kazi pia.
Nafurahi kuona kuwa mafanikio ya kutia moyo yanaendelea kupatikana ingawaje kazi iliyo mbele yetu bado ni kubwa. Sote tunasoma na kusikia kupitia vyombo vya habari taarifa za watumishi wa serikali, taasisi za umma pamoja na watu wengine wanavyokamatwa na TAKUKURU kwa kujihusisha na vitendo vya rushwa. Tangu mwaka 2006, kesi 63 zinazohusu rushwa kubwa zimefikishwa Mahakamani. Baadhi zimeisha na wahusika waliopatikana na hatia wameadhibiwa kwa mujibu wa sheria. Zipo pia tulizoshindwa, ni sawa katika nchi inayoheshimu utawala wa sheria. Nyingine zinaendelea. Vile vile juhudi za TAKUKURU zimeokoa fedha nyingi za umma. Kwa mfano, kwa kipindi cha miaka mitatu, yaani kati ya 2010 hadi 2013, zaidi ya shilingi bilioni 28 zimeokolewa ambazo zingeweza kunufaisha watu wachache wanaoendeleza vitendo vya rushwa badala ya taifa.
Naomba wananchi waendelee kutoa taarifa zitakazosaidia kuwatambua na kuwakamata watoaji na wapokeaji rushwa. Tukumbuke kuwa mafanikio katika mapambano haya hayategemei Serikali au TAKUKURU peke yake. Ni mapambano ambayo jamii ikijihusisha kwa ukamilifu ushindi mkubwa utapatikana. Yanatuhusu sote kwani tukishinda, matunda yake yatawafaidisha watu wote. Pia, napenda kutumia nafasi hii kutoa wito kwa taasisi na idara zote za serikali zinazohusika moja kwa moja katika vita dhidi ya rushwa zitimize ipasavyo wajibu wake. Aidha pakiwepo na ushirikiano mzuri na mshikamano wa dhati miongoni mwetu kwa hakika ushindi utapatikana. Tukifanya hivyo nina imani tutapata mafanikio makubwa zaidi tena kwa haraka.
Dawa za Kulevya
Ndugu Wananchi;
Tatizo la biashara na matumzi ya dawa za kulevya limeendelea kuwa moja ya changamoto kubwa zinazolikabili taifa letu. Serikali imeendelea kufanya jitihada kubwa kupambana na changamoto hiyo. Yapo mafanikio yanayopatikana lakini bado tuna kazi kubwa ya kufanya mbele yetu. Ukubwa wa kazi hiyo unaletwa na ule ukweli kwamba watu wanaohusika ni wengi na wanazidi kuongezeka kila kukicha kwa tamaa ya kupata utajiri wa haraka. Isitoshe wakati wote washiriki wake wanabuni mbinu mpya za kusafirisha, kusambaza na kuuza dawa hizo haramu. Pia ni kazi hatari kwani wapambanaji kupoteza maisha si jambo la ajabu.
Pamoja na changamoto hizo, kwa vile matumizi ya dawa za kulevya yana athari mbaya kwa watu wanaotumia na jamii kwa ujumla, Serikali haitachoka kufanya kila tuwezalo kupambana na uhalifu huu mpaka ushindi upatikane. Wakibadili mbinu na sisi tutabadili maarifa ya uchunguzi na utambuzi mpaka tuwapate. Tutawahami ipasavyo watu wanaojitolea muhanga kupambana na uovu huu. Mafanikio yanaendelea kupatikana. Kwa mfano, kuanzia Januari hadi Septemba, mwaka huu (2013) watu 2000 (wafanya biashara na watumiaji wa dawa za kulevya) wamekamatwa na aina mbalimbali ya dawa za kulevya ikiwa ni pamoja na kilo 681 za dawa hatari ya heroine, zimekamatwa.
Watu hao kama wasingekamatwa wangeendelea kuuza na kusambaza dawa za kulevya na kuathiri maelfu ya watu na hasa vijana ambao ni nguvu kazi muhimu ya taifa letu na warithi wa jamii na taifa wa kesho. Inatia uchungu sana kuona kuwa tegemeo letu hilo linaangamizwa na watu wachache wenye uroho usio na kifani wa kujipatia utajiri wa haraka, tena kwa gharama yoyote ile.
Ndugu wananchi;
Kwa niaba yenu, napenda kutumia nafasi hii kutoa pongezi zangu za dhati kwa viongozi na wafanyakazi wote wa Tume ya Kuratibu na Udhibiti wa Dawa za Kulevya na vyombo vingine vya dola kwa kazi kubwa na nzuri inayoendelea kufanyika ya kukabiliana na tatizo hili. Katika mapambano yetu tunashirikiana na nchi na taasisi za nchi mbalimbali duniani. Hivyo basi nazipongeza kwa dhati nchi na taasisi hizo rafiki kwa ushirikiano wao ambao umetusaidia kupata mafanikio haya kiasi tunayojivunia leo. Naomba ushirikiano huu uendelee kwani umetusaidia kwa namna nyingi na umekuwa wa manufaa makubwa.
Ndugu wananchi;
Nilishawahi kusema siku za nyuma kuwa ni makusudio yangu na ya serikali kuanzisha chombo chenye uwezo na nguvu kubwa zaidi ya kupambana na tatizo la dawa za kulevya nchini. Mchakato wa kuunda chombo hicho umeanza na unaendelea vizuri. Hivi sasa tunayo Tume ya Kuratibu Udhibiti wa Dawa za Kulevya. Chombo hicho kipya kitakuwa na nguvu kubwa zaidi kuliko Tume na hata kuliko kikosi kazi cha vyombo vyote vya dola nilichokiunda kuipa Tume meno.
Ndugu wananchi;
Ili juhudi hizo zifanikiwe na ushindi upatikane itategemea sana msaada, ushirikiano na ushiriki wa wananchi. Nawaomba sana ndugu zangu wananchi wenzangu mshirikiane na vyombo vya dola katika kupambana na usafirishaji, uuzaji na usambazaji wa dawa za kulevya. Baadhi yenu mnawajua watu wanaojihusisha na biashara hii haramu. Watajeni washughulikiwe ipasavyo.
Wiki ya Vijana
Ndugu wananchi;
Kama nilivyosema awali leo pia tunaadhimisha wiki ya vijana. Nimepata fursa ya kutembelea mabanda ya maonesho ya vijana ili kuona shughuli wanazozifanya. Nimefurahi na kufarijika sana na kile nilichokiona. Vijana wanafanya kazi nzuri na kwa kweli ni uamuzi wa busara kuwashirikisha katika sherehe hizi kwani wanapata fursa ya kuonesha kazi wanazozifanya katika kuboresha maisha yao na kuleta maendeleo ya taifa. Hii pia ni nafasi nzuri kwa vijana kukutana, kufahamiana na kubadilishana mawazo, ujuzi na taarifa muhimu zinazohusu maisha na maendeleo yao. Kwa kuzingatia umuhimu na faida ya maonesho haya, ni vyema kuangalia uwezekano wa maadhimisho ya Wiki ya Vijana yakafanyika katika ngazi ya Mikoa na kuhitimishwa Kitaifa kama tulivyofanya leo.
Ndugu wananchi;
Mimi na wenzangu Serikalini tunatambua na kuthamini sana nafasi na mchango wa vijana katika kuchochea maendeleo ya nchi yetu. Ndio maana Serikali inawekeza sana katika elimu na mafunzo yao. Ndiyo maana pia Serikali imeamua katika mwaka huu wa fedha kuongeza uwezo wa bajeti ya Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo ili iweze kuwahudumia vijana vizuri zaidi. Tutaendelea kuongeza bajeti hiyo ili Wizara iweze kuwaongezea vijana mitaji ya biashara kupitia Mfuko wa Taifa wa Maendeleo ya Vijana.
Nimefurahi kumsikia Mheshimiwa Waziri akiahidi hapa kwamba baadhi ya vijana walioshiriki katika maonesho niliyoyaona leo watafikiriwa kupewa mikopo kwa mujibu wa taratibu zilizowekwa. Nawasihi vijana watakaopata mikopo kupitia Mfuko huu pamoja na mifuko mingine ya uwezeshaji wahakikishe wanaitumia vizuri kwa malengo yaliyokusudiwa na kuirejesha kwa wakati ili wengine nao wapate.
Maendeleo ya Mkoa wa Iringa
Ndugu wananchi;
Jana jioni nilipokea taarifa ya maendeleo ya Mkoa wa Iringa kutoka kwa Mkuu wa Mkoa, Dokta Christine Ishengoma. Natoa pongezi nyingi kwa wananchi wa Iringa kwa juhudi zenu na mafanikio mnayoyapata katika kujiletea maendeleo. Mkoa umeendelea kuwa wa kutegemewa katika kulipatia taifa chakula hasa mahindi na sasa mwelekeo ni mzuri kwa mazao ya chai, mpunga, mboga na matunda. Nawaomba muendelee na juhudi zenu. Ongezeni maarifa na matumizi ya zana za kisasa na pembejeo za kilimo ili tija iongezeke mpate mavuno mengi zaidi. Mtatosheleza mahitaji yenu na mtapata ziada kubwa itakayotumika kwingineko nchini na hata kuuzwa nje ya nchi. Sisi katika Serikali tutaendelea kuwasaidia kwa upande wa upatikanaji wa pembejeo, zana za kilimo, masoko, huduma mbalimbali zikiwemo za ugani, fedha na kadhalika. Mkoa wa Iringa utanufaika kupitia Mpango wetu wa Matokeo Makubwa Sasa (Big Result Now) na SAGCOT.
Ndugu wananchi;
Serikali itaendelea kununua mahindi ya wakulima kupitia Wakala wa Taifa wa Hifadhi ya Chakula. Hata hivyo ni vyema nikaeleza wazi kuwa Hifadhi ya Taifa ya Chakula haitanunua mahindi yote yaliyovunwa nchini. Ukomo wetu kwa sasa ni tani 250,000 lakini tunaendelea kupanua uwezo wa maghala hadi kufikia tani 400,000 ifikapo mwaka 2015. Tayari Hifadhi ya Taifa wameshanunua tani 209,000 hivyo bado tani 41,000. Hivyo nashauri wenzetu wa sekta binafsi nao wajitokeze kununua mahindi ya wakulima.
Kwa kuwa hakuna kizuizi cha kuuza nje wanaweza kufanya hivyo wakipenda. Hata hivyo, sisi tungependa kwanza wauze hapa nchini. Naomba ieleweke kuwa hatutawauzia watu akiba yetu ya mahindi katika Hifadhi ya Taifa ya Chakula kwa ajili ya kuuza nje.
Ndugu wananchi;
Pamoja na kuendeleza kilimo katika Mkoa wa Iringa, tutaendelea kuboresha barabara, na huduma za umeme, maji, elimu na afya. Ninyi ni mashahidi kwamba utekelezaji wa ahadi ya kujenga barabara ya lami kutoka Iringa hadi Dodoma unakwenda vizuri na ukarabati wa barabara ya Morogoro – Tunduma kupitia Iringa na Mbeya umekamilika. Tunajipanga kutekeleza ahadi zetu kwa baadhi ya barabara za Mkoa huu.
Kwa upande wa umeme vijijini tunaendelea kuvipatia umeme vijiji 38 vya Mkoa huu na wakati huo huo tunajiandaa kuvipatia umeme vijiji vingine 86. Tutaendelea kuongeza upatikanaji wa maji vijijini na mijini. Aidha, tumeanza kutekeleza mkakati kabambe wa kuboresha elimu kwa shabaha ya kutoa fursa ya elimu kwa vijana wetu wengi na kuongeza kiwango cha ufaulu. Haya yote tunayafanya chini ya mkakati mpya wa kupata Matokeo Makubwa Sasa. Tutaongeza mara dufu juhudi za kuboresha huduma ya afya.
Hitimisho
Ndugu wananchi;
Kabla ya kumaliza hotuba yangu niwakumbushe Watanzania wenzangu kuwa mwaka ujao ni wa aina yake katika nchi yetu. Kwanza tunasherehekea miaka 50 ya Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar, pili, tunasherehekea miaka 50 ya Muungano. Na tatu, kama mambo yatakwenda sawa tutapata Katiba Mpya. Niwaombe Watanzania wenzangu tujiandae vyema kufanikisha mambo yetu hayo matatu ya kihistoria. Naomba nimalize kwa kuwashukuru tena wananchi na viongozi wa Mkoa wa Iringa kwa kufanikisha sherehe hii muhimu. Nawashukuru pia wadau mbalimbali ambao wamechangia kwa hali na mali kufanya sherehe hizi zifanikiwe na kufana sana kama hivi. Napenda kutumia nafasi hii pia kuwatakiwa ndugu zetu Waislamu na Watanzania wenzangu wote heri ya Sikukuu ya Idd El Hajj.
Baada ya kusema hayo sasa natamka rasmi kwamba shughuli za Mbio za Mwenge wa Uhuru, kumbukumbu ya Baba wa taifa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere na Wiki ya Vijana kwa mwaka 2013 zimefikia kilele chake.
Asante sana kwa kunisikiliza.

- Oct 09, 2013
Hotuba ya Rais Mheshimiwa Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa Wananchi, Tarehe 4 Oktoba, 2013
Soma zaidiHotuba
Ndugu Wananchi;
Namshukuru Mwenyezi Mungu, mwingi wa rehma, kwa kutujaalia uzima na kutuwezesha kumaliza mwezi Septemba salama na kuwasiliana kwa kutumia utaratibu wetu huu mzuri. Naomba radhi kuzungumza nanyi siku ya leo kwa sababu nilikuwa safari na nilirejea jioni ya tarehe 30 Septemba, 2013. Awali nilifikiria nisiseme, nisubiri mwisho wa mwezi wa Oktoba. Lakini, baada ya kupata taarifa ya yaliyojiri, nimeshauriwa na nimekubali angalau niyasemee baadhi ya mambo huenda itasaidia. Niwieni radhi nisipoyasemea baadhi ya mambo siyo kwa kuyapuuza, bali kwa kuepuka hotuba kuwa ndefu mno. Nitayatafutia mahali pengine pa kuyasemea.
Uhusiano na Rwanda
Ndugu Wananchi;
Katika hotuba yangu ya mwisho wa mwezi wa Julai, nilizungumzia hali ya uhusiano wetu na Rwanda kutokuwa mzuri na tatizo la ujambazi na wahamiaji haramu katika Mikoa ya Kigoma, Geita na Kagera. Nafurahi kusema kuwa kwa yote mawili kuna maendeleo ya kutia moyo.
Tarehe 5 Septemba, 2013, nilikutana na kuzungumza na Mheshimiwa Rais Paul Kagame waRwandamjiniKampala. Tuliitumia fursa ya ushiriki wetu katika Mkutano wa Nchi za Maziwa Makuu kuzungumzia uhusiano baina yetu na nchi zetu. Mazungumzo yalikuwa mazuri na sote tulikubaliana kuwa yaliyopita si ndwele tugange yajayo. Kwa sababu hiyo tulielewana kuwa tutengeneze mazingira yatakayosaidia kutuliza hali na kurudisha nchi zetu katika uhusiano mwema kama ilivyokuwa siku zote. Nawaomba ndugu zangu hususan wanasiasa, watumishi wa umma, wanahabari na wenye mitandao ya kijamii na blog na wananchi kwa ujumla tusaidie kuimarisha uhusiano mwema baina ya Rwanda na Tanzania na watu wake.
Majambazi na Wahamiaji Haramu
Ndugu Wananchi;
Katika hotuba hiyo pia nilisema kuwa tutachukua hatua thabiti dhidi ya majambazi na wageni wanaoishi nchini bila ya kuzingatia taratibu zinazohusika. Niliwataka majambazi wajisalimishe wao na silaha zao kwa hiari. Wale wanaoishi nchini bila ya kuwa na kibali halali wahalalishe ukaazi wao au warejee makwao. Nilitoa siku 14 kuanzia tarehe 29 Agosti, 2013 wafanye hivyo kwani baada ya hapo tungeanzisha operesheni maalum ya kushughulika na watu wa makundi yote mawili.
Ndugu Wananchi;
Kumekuwepo na mafanikio ya kutia moyo. Kwa upande wa wahamiaji wanaoishi nchini kinyume cha sheria watu wapatao 21,254 waliondoka kwa hiari. Hali kadhalika zaidi ya ng’ombe 8,000 waliondolewa na silaha 102 zilisalimishwa. Baada ya operesheni kuanza tarehe 6 Septemba, 2013 na kumalizika tarehe 20 Septemba, 2013, wahamiaji haramu 12,828 walirejeshwa makwao na watuhumiwa 279 wa unyang’anyi wa kutumia silaha walikamatwa. Aidha, mabomu 10 ya kutupa kwa mkono (offensive hand grenades), silaha 80, risasi 780 na mitambo 2 ya kutengeneza magobole vilikamatwa. Pia, ng’ombe 8,226 walikamatwa wakichungwa katika mapori ya hifadhi. Kwa upande wa mazao ya misitu, mbao 2,105 zilikamatwa pamoja na nyara mbalimbali za Serikali.
Ndugu Wananchi;
Agizo la kuwataka watu wanaoishi nchini isivyo halali wahalalishe ukaazi wao au waondoke kwa hiari au wataondolewa lilipotoshwa hasa na vyombo vya habari vya nje ya Tanzania. Walikuwa wanadai eti Tanzaniailikuwa inafukuza wakimbizi. Madai hayo si ya kweli hata kidogo. Hadi kufikia tarehe 30 Septemba, 2013 wakimbizi 68,711 walikuwepo kwenye Kambi ya Nyarugusu, Mkoani Kigoma. Hakuna mkimbizi ye yote aliyetakiwa kuondoka. Ukweli ni kwamba hakuna mtu ye yote kati ya wale watu walioondoka kwa hiari au kusaidiwa kuondoka wakati wa operesheni ambaye ni mkimbizi. Kama ingekuwa hivyo, wa kwanza kulalamika wangekuwa wenzetu wa Shirika la Wakimbizi la Umoja wa Mataifa. Bahati nzuri jambo hilo halikutokea.
Ndugu Wananchi;
Yalikuwepo pia madai kwamba tunawaonea na kuwatesa watu walioishi nchini miaka mingi. Ati iweje sasa ndiyo waambiwe kuwa siyo raia. Siku zote Serikali ilikuwa wapi? Uraia haupatikani kwa kuishi nchi ya kigeni kwa miaka mingi. Unapatikana kwa kutimiza masharti ya kuomba na kupewa uraia. Kama mtu hakufanya hivyo anabaki kuwa raia wa nchi aliyotoka au walikotoka wazazi wake. Ipo mifano ya watu mashuhuri ambao walilazimika kuachia nyadhifa zao baada ya kugundulika kuwa siyo raia. Hawakuwa wanaonewa, ndiyo matakwa ya Katiba na Sheria za nchi yetu.
Ndugu Wananchi;
Katika kutekeleza operesheni hii niliagiza kuwa wale watu ambao wameishi hapa nchini miaka mingi ambao wana nyumba, mashamba au mali mbalimbali au wameoa au kuolewa na wana watoto au hata wajukuu waelekezwe kuhalalisha ukaazi wao. Iwapo watakataa kufanya hivyo basi wasaidiwe kurejea kwao. Pia niliagiza watu wasiporwe mali zao wala kudhulumiwa. Sijapata taarifa ya kufanyika kinyume na maelekezo yangu. Lakini kama wapo watu waliotendewa tofauti, taarifa itolewe kwa Wakuu wa Wilaya na Mikoa au hata Ofisi ya Rais ili hatua zipasazo zichukuliwe. Hatutaki watu wadhulumiwe au kuonewa.
Napenda kutumia nafasi hii kumpongeza Waziri wa Ulinzi na JKT, Mheshimiwa Shamsi Vuai Nahodha na Waziri wa Mambo ya Ndani, Mheshimiwa Emmanuel Nchimbi kwa uongozi wao mzuri katika zoezi hili. Pia, nawapongeza Makamanda na askari wa JWTZ na Polisi pamoja na maafisa wa Idara ya Uhamiaji, Idara ya Mifugo, Idara ya Wanyamapori, Idara ya Misitu na Idara nyinginezo za Serikali kwa kazi kubwa na nzuri waliyofanya. Najua awamu ya kwanza imeisha tarehe 20 Septemba, 2013 na kama nilivyosema kuwa safari hii operesheni itakuwa endelevu, muda si mrefu awamu ya pili itafuata. Nawaomba waendelee kuchapa kazi kwa bidii, maarifa na nidhamu ya hali ya juu.
Ziara ya Canada na Marekani
Ndugu Wananchi;
Kati ya tarehe 17 na 28 Septemba, 2013 nilifanya ziara ya kikazi katika nchi zaCanadana Marekani. Nchini Canada nilitembelea Chuo Kikuu cha Guelph ambapo nilitunukiwa Shahada ya Heshima ya Uzamivu kwa kutambua jitihada zetu tuzifanyazo kujiletea maendeleo na mafanikio ya kutia moyo tunayoendelea kupata licha ya changamoto zinazotukabili. Katika mazungumzo yangu na uongozi wa chuo hicho wamekubali kuwa na ushirikiano wa karibu na Wizara zinazohusika na Elimu, Kilimo na Mifugo pamoja na Chuo Kikuu cha Kilimo cha Sokoine, Morogoro na Chuo Kikuu cha Dodoma. Nimewataka Mawaziri wa Wizara hizo na viongozi wa vyuo hivyo kuchangamkia fursa hiyo bila kuchelewa.
Ndugu Wananchi;
Nchini Marekani nilikutana na kuzungumza na maafisa na viongozi mbalimbali wa Serikali ya nchi hiyo wakiwemo Rais Barack Obama na baadhi ya Wabunge wa Bunge la Marekani. Mazungumzo yetu yalilenga kuimarisha ushirikiano baina ya nchi zetu na mambo yalienda vizuri. Wote walituhakikishia kuwa mambo tuliyoyazungumza na kukubaliana na Rais Barack Obama wakati wa ziara yake nchini yanaendelea kufanyiwa kazi. Miongoni mwa hayo maombi yetu ya kupatiwa vitabu milioni 2.4 vya sayansi na hisabati yamekubaliwa na utekelezaji umeanza. Upatikanaji wa vitabu hivyo utamwezesha kila mwanafunzi wa sekondari kuwa na kitabu chake.
Ndugu Wananchi;
Jambo lingine kubwa na la faraja kwetu ni kuwa mapendekezo yetu ya miradi ya umeme na barabara za vijijini za kugharamiwa na Serikali ya Marekani kupitia Shirika lao la Changamoto za Milenia yamepokelewa vizuri. Kinachosubiriwa ni miradi ipi itakubaliwa na Bodi ya MCC na kiasi gani cha fedha kitatengwa na Bunge la Marekani kwa ajili hiyo.
Tuzo ya Uhifadhi
Jambo lingine muhimu katika safari yangu ya Marekani ni kutunukiwa tuzo na “International Congressional Conservation Foundation” kwa kutambua juhudi zetu katika kuhifadhi wanyamaporina mafanikio tuliyoyapata. Licha ya changamoto mbalimbali tunazokabiliana nazo, tuzo hii imetupa moyo wa kuongeza nguvu katika jitihada tunazozifanya sasa kupambana na ujangili na matatizo mengine ya uhifadhi wa wanyama na misitu.
Ndugu Wananchi;
Kilichotupa moyo zaidi ni kauli za utayari wa kutusaidia katika mapambano hayo zilizotolewa wakati wa kupewa tuzo na katika mkutano wa mfuko wa Maendeleo wa Clinton na katika mkutano maalum wa kupambana na ujangili na biashara ya meno ya tembo duniani.
Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa
Ndugu Wananchi;
Shabaha kuu ya safari yangu ya Marekani ilikuwa kuhudhuria Mkutano wa 68 wa Umoja wa Mataifa unaoendelea jijini New York mpaka Desemba, 2013. Mada kuu ya mkutano wa mwaka huu ni kuandaa agenda ya maendeleo baada ya mwaka 2015 yaani: Post 2015 Development Agenda: Setting the Stage. Kama mtakavyokumbuka Malengo ya Milenia yaliyoamuliwa na Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa mwaka 2000, yanafikia ukomo wa utekelezaji wake mwaka 2015.
Katika Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa mwaka huu mjadala umehusu nini kifanyike baada ya mwaka 2015. Hata hivyo, mjadala huo unaanza kwa kufanya tathmini ya utekelezaji wa yale Malengo Manane ya Milenia ya mwaka 2000 umefikia wapi mpaka sasa na utafikia wapi mwaka 2015 kwa kila nchi na kwa dunia kwa ujumla. Tathmini ya jumla inaonesha kuwa kumekuwepo na jitihada kubwa ya kutekeleza malengo haya katika kila nchi. Yapo malengo ambayo utekelezaji wake umefikia shabaha hivi sasa na yapo ambayo upo uwezekano wa shabaha kufikiwa ifikapo mwaka 2015. Vile vile yapo ambayo shabaha haitafikiwa.
Ndugu Wananchi;
Kwa upande wetu, Tanzania, tumefikia shabaha katika mambo yafuatayo:
(1) Lengo la Milenia namba 2 kuhusu uandikishaji wa watoto wenye umri wa kwenda shule ya msingi;
(2) Lengo la Milenia namba 3 hasa kuhusu usawa wa kijinsia katika Shule za Msingi na Sekondari. Ukweli ni kwamba, wasichana wanaanza kuwa wengi kuliko wavulana. Hatujafikia shabaha kwa upande wa usawa wa kijinsia katika elimu ya juu na ni vigumu kulifikia ifikapo 2015. Pia hatujafikia lengo kwa upande wa usawa wa Wabunge wanawake na wanaume. Hata hivyo, kwa kutumia mchakato wa Katiba unaoendelea sasa tunaweza kufikia lengo katika uchaguzi wa 2015 iwapo tutaamua iwe hivyo;
(3) Lengo la Milenia namba 4 kuhusu kupunguza idadi ya vifo vya watoto wachanga na wale wenye umri chini ya miaka mitano;
(4) Tumefikia shabaha kwa Lengo la Milenia Namba 6 kuhusu kupunguza maambukizi ya UKIMWI; na
(5) Kwa upande wa lengo namba 7 kuhusu mazingira, tumefikia shabaha kwa upande wa upatikanaji wa maji mijini. Bado tuko nyuma kwa maji vijijini ingawaje tunaweza kufikia lengo ifikapo mwaka 2015 kama tutaendeleza uwekezaji tulioamua kufanya katika bajeti ya mwaka huu. Lakini, hatutaweza kufikia shabaha kwa upande wa usafi wa mazingira mijini na vijijini ifikapo mwaka 2015. Safari bado ndefu sana.
Ndugu Wananchi;
Malengo ya Milenia namba 1 na namba 5 ambayo bado tuko nyuma sana ya shabaha hatutafikia lengo ifikapo 2015. Tumeendelea kutekeleza lengo la Milenia namba 1 kuhusu kupunguza umaskini na njaa kwa zaidi ya nusu kutoka kiwango cha mwaka 2000. Hatua tunazochukua kuleta mageuzi katika kilimo zina lengo la kuhakikisha usalama wa chakula na kuongeza mapato ya wakulima. Mafanikio yanaanza kuonekana lakini si ya kiwango cha kutufikisha kwenye lengo ifikapo mwaka 2015. Tunao, pia, mpango wa kupanua programu ya TASAF ya Conditional Cash Transfer ili tuwafikie watu wengi maskini. Hata kama tutafanikiwa kuutekeleza mapema mpango huu utatusogeza sana mbele lakini bado tutakuwa chini ya lengo kwa upande wa kupunguza umaskini ifikapo 2015.
Ndugu Wananchi;
Kwa upande wa Lengo la Milenia namba 5, kuhusu afya ya kina mama wajawazito bado tuko nyuma katika kupunguza vifo vya kina mama wajawazito na kuongeza idadi ya wajawazito wanaojifungua chini ya uangalizi wa wataalamu wa afya. Hatutaweza kufikia shabaha ifikapo mwaka 2015. Mpango wa Maendeleo ya Afya ya Msingi (2007 – 2017) una nia ya kukabiliana na matatizo haya. Tumeongeza ujenzi wa zahanati, vituo vya afya na hospitali, tumeboresha upatikanaji wa dawa na tumepanua sana mafunzo ya madaktari, wauguzi na wakunga mambo ambayo yamesaidia kutufikisha hatua tuliyopiga mpaka sasa. Naamini juhudi zetu tukiziendeleza zitatusogeza mbele zaidi ingawaje bado tutakuwa chini ya lengo. Miaka michache ijayo, tatizo hili nalo litakuwa historia.
Ndugu Wananchi;
Lengo la Milenia namba 8 linazihusu nchi tajiri kuongeza michango yao kusaidia nchi zinazoendelea kutekeleza Malengo ya Milenia. Bahati mbayasanamataifa tajiri hayajafikia viwango wanavyotarajiwa kutoa na hata vile wanavyoahidi wenyewe kutoa katika majukwaa mbalimbali. Kama wangetimiza ahadi zao, sura ya utekelezaji wa Malengo ya Milenia ingekuwa tofauti kabisa.
Ndugu Wananchi;
Hiyo ndiyo hali ya utekelezaji wa Malengo ya Milenia hapa nchini. Hakuna nchi ye yote duniani iliyofanikiwa kutekeleza shabaha za malengo yote kwa ukamilifu. Ushauri wa viongozi wote waliozungumza ulitaka mataifa yaliyoendelea yatimize ahadi zao za kuchangia utekelezaji wa Malengo ya Milenia. Ilionekana suala la upatikanaji wa fedha halina budi kuangaliwa kwa makini sasa na baada ya mwaka 2015. Bila ya hivyo ufanisi utakuwa mdogo katika kuongeza kasi ya utekelezaji kwa pale paliposalia kufikia malengo ya 2015 na hata kwa Malengo ya baada ya mwaka 2015.
Mashambulizi ya Kigaidi ya Westgate, Nairobi
Ndugu Wananchi;
Wakati nikiwa safarini, tarehe 21 Septemba, 2013 kulitokea shambulilizi la kigaidi katika Jengo la Biashara la Westgate, huko Nairobi, Kenya. Watu 67 walipoteza maisha na zaidi ya 200 walijeruhiwa. Nilituma salamu za pole na rambirambi kwa Mheshimiwa Rais Uhuru Kenyatta na wananchi wa Kenya na kuwahakikishia kuwa tupo pamoja nao katika wakati huu wa majonzi.
Nafahamu kuwa baada ya tukio hilo watu wengi hapa nchini wameingiwa na hofu kuhusu usalama wetu. Ni hofu ya msingi kwani tarehe 8 Agosti, 1998 Ubalozi wa Marekani hapa nchini ulishambuliwa na magaidi na ndugu zetu 11 wasio na hatia walipoteza maisha.
Ndugu Wananchi;
Napenda kuwafahamisha kuwa tangu shambulio la mwaka 1998, Serikali imekuwa inajenga uwezo wa vyombo vyetu vya ulinzi na usalama kupambana na ugaidi katika nyanja mbalimbali. Tunaendelea kujiimarisha bila kusita siku hadi siku. JWTZ, Polisi na Idara ya Usalama wa Taifa wamekuwa na ushirikiano wa karibu kwa ajili hiyo. Juhudi zetu hizo ndizo zinazotufanya tuwe salama hadi sasa.
Baada ya tukio la Kenya, vyombo vyetu vya ulinzi na usalama vimeimarisha mikakati yao maradufu. Pamoja na kujizatiti kwetu huko hatuwezi kusema kuwa tukio la kigaidi halitaweza kutokea nchini. Uhakika huo hatuna kwani hata mataifa makubwa na tajiri yameshambuliwa. Kilicho muhimu ni kuendelea kuchukua tahadhari na wananchi kusaidia ili vyombo vyetu vifanikiwe zaidi.
Hali kadhalika, tumewataka watu wote wenye shughuli zinazokusanya watu wengi kama vile maduka, maofisi, mahoteli, migahawa n.k. waweke kamera za ulinzi nje na ndani ya maeneo yao. Pia waangalie uwezekano wa kuweka vifaa vya upekuzi (metal detectors and x-rays). Najua watu wanaweza kulalamikia usumbufu au gharama, lakini gharama na hasara ya kushambuliwa ni kubwa zaidi kuliko ya usumbufu huo.
Ndugu Wananchi;
Nawaomba muendelee kufanya shughuli zenu bila ya hofu ingawaje msiache kuwa makini na kuchukua tahadhari. Watu watoe taarifa kwa vyombo vya usalama wanapoona mtu au watu au kitu cha kutilia shaka. Ni muhimu kwa usalama wake, wa kila mtu, jamii na taifa. Maafisa husika wa vyombo vya ulinzi na usalama wataendelea kuelimisha umma kuhusu hatua mbalimbali za tahadhari za kuchukua. Sisi Serikalini tumejipanga kuchukua hatua zaidi kuimarisha ulinzi na usalama wa nchi yetu na watu wake.
Mchakato wa Katiba Mpya
Ndugu Wananchi;
Kamamtakavyokumbuka, Bunge lilitunga Sheria ya Mabadiliko ya Katiba Novemba, 2011. Sheria hii imeweka mchakato mzima wa kupata Katiba hiyo na kuunda taasisi zake. Mwezi Mei, 2012, Tume ya Mabadiliko ya Katiba iliundwa na imekamilisha hatua tatu muhimu katika mchakato huo. Hatua hizo ni kupokea maoni ya wananchi, kutayarisha rasimu ya kwanza ya Katiba Mpya na kupokea maoni ya Mabaraza ya Katiba ya Wilaya na ya taasisi. Hivi sasa Tume inaandaa mapendekezo ya Rasimu ya Pili ya Katiba itakayopelekwa kwenye Bunge Maalum. Baada ya tafakuri zake, Bunge Maalum litatoa rasimu ya mwisho ya Katiba ambayo itapelekwa kwa wananchi kwa ajili ya uamuzi wa mwisho kupitia kura ya maoni. Baada ya hatua hiyo, ndipo tutakapokuwa tumepata Katiba Mpya.
Ndugu Wananchi;
Baada ya Bunge la Novemba, 2011 kupitisha Sheria ya Mabadiliko ya Katiba, kulikuwepo na madai ya kutaka sheria hiyo iboreshwe kutoka vyama vyote vya siasa vikiwemo vyama vya upinzani na Chama tawala. Majadiliano yalifanyika baina ya Serikali na vyama hivyo pamoja na shirikisho la asasi za kiraia. Makubaliano yalifikiwa kuwa marekebisho yafanyike kwa awamu. Awamu ya kwanza ihusishe Tume ya Mabadiliko ya Katiba kisha hapo yafanyike marekebisho yanayohusu Bunge Maalum na mwisho Kura ya Maoni.
Kama ilivyokuwa kwa mabadiliko yaliyohusu Tume ya Mabadiliko ya Katiba, safari hii nayo vyama vya siasa vilitoa mapendekezo yao. Yalifanyika mazungumzo kati yao na Serikali na maelewano kufikiwa kuhusu maeneo ya kufanyiwa marekebisho. Serikali ilitayarisha rasimu ya Muswada na kuuwasilisha kwa wenzetu wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar.
Ndugu Wananchi;
Serikali ya Mapinduzi Zanzibar ilitoa mapendekezo yake na ushauri kwenye maeneo mawili. Kwanza kwamba uteuzi wa wajumbe wa Bunge Maalum ufanywe na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kushauriana na kuafikiana na Rais wa Zanzibar. Pili walishauri kwamba kamaBunge Maalum litashindwa kufikia maamuzi ndani ya siku 70 zilizopendekezwa, liweze kuongezwa muda hadi kufikia siku 90. Maeneo mengine ya Muswada waliafikiana nayo.
Ndugu Wananchi;
Kwa kuzingatia utaratibu wa kutunga Sheria, Serikali ilifikisha Muswada kwa Spika wa Bunge ambaye nae aliuwasilisha kwenye Kamati ya Kudumu ya Katiba, Sheria na Utawala. Kama ilivyo ada, Kamati hiyo ilifanya vikao na wadau na kupokea maoni yao kuhusu Muswada. Nimeambiwa kulikuwa na mjadala wa kina na mapendekezo mazuri yalitolewa na wadau. Kisha hapo Wajumbe wa Kamati walikaa wenyewe kujadili Muswada walikuwepo pia Wabunge ambao si Wajumbe wa Kamati walioshiriki kwa vile Kanuni zinaruhusu. Nimeambiwa pia kwamba mjadala ulikuwa mpana na wa kina zaidi. Mapendekezo kadhaa yalitolewa na Wajumbe kuhusu vifungu mbalimbali vya Muswada.
Ndugu Wananchi;
Nimefahamishwa kuwa Wabunge wa vyama vyote walichangia na kwamba baadhi ya nyakati mambo yalipokuwa ugumu mawazo mazuri ya baadhi ya Wabunge wa upinzani yalisaidia kupata ufumbuzi. Nimeambiwa pia kwamba Wajumbe wa Kamati na upande wa Serikali walikubaliana kwa maeneo mengi isipokuwa machache ambayo walikubaliana kwa pamoja wayapeleke Bungeni ili Wabunge nao wayajadili na kuyapatia ufumbuzi.
Ndugu Wananchi;
Baada ya Kamati kumaliza kazi yake, Waziri wa Katiba na Sheria, Mheshimiwa Mathias Chikawe aliwasilisha Muswada Bungeni. Akafuatiwa na Mheshimiwa Gosbert Blandes kwa niaba ya Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Katiba, Sheria na Utawala, kutoa maoni ya Kamati. Baadaye Msemaji wa Kambi ya Upinzani, Mheshimiwa Tundu Lissu alitoa maoni yake.
Ndugu Zangu;
Baada ya watu hao watatu kutoa maoni yao ilitarajiwa kuwa Wabunge wangeanza kujadili Muswada. Naambiwa mambo hayakuwa hivyo. Badala yake kukazuka malumbano baina ya Spika na baadhi ya Wabunge wa Upinzani wakitaka Muswada usijadiliwe. Ilifikia wakati hoja hiyo ikabidi iamuliwe kwa kura ambapo ilishindwa. Katika hali isiyotarajiwa, Wabunge wote wa upinzani wakatoka nje ya Bunge isipokuwa wawili. Kitendo hicho kimewanyima Wabunge wengi wa upinzani fursa ya kutetea hoja zao walizozitoa kupitia hotuba ya Msemaji wa Kambi ya Upinzani. Pia wamejinyima nafasi ya kusema mambo mengine wakati wa mjadala na Kamati ya Bunge zima.
Wabunge waliokuwepo waliendelea kuujadili Muswada na kutoa hoja na mapendekezo ya kuuboresha. Walifanya hivyo wakati wa mjadala na wakati wa kupitia kifungu kwa kifungu. Baadhi ya hoja na mapendekezo yalikubaliwa na mengine yalikataliwa. Miongoni mwa yaliyokubaliwa na Wabunge, kwa mfano, ni kuhusu elimu ya mtu atakayekuwa Mwenyekiti wa Bunge Maalum na lile la ukomo wa uhai wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba.
Ndugu Wananchi;
Kwa maoni yangu madai ya Kambi ya Upinzani yanazungumzika na hata baadhi yangeweza kukubalika kama Wabunge wake wangekuwepo Bungeni na kushiriki mchakato wote wa kujadili na kupitisha Miswada Bungeni. Bahati mbaya hawakuwepo, hivyo hapakuwepo na mtu wa kusema mawazo yao. Baada ya kupoteza fursa yao halali, kutaka kupata ufumbuzi nje ya Bunge ni jambo lisilowezekana. Haya ni masuala yanayohusu Bunge ambayo hujadiliwa na kuamuliwa Bungeni na si vinginevyo. Kuandamana nchi nzima au kuchukua hatua za kutotii sheria kama Mwenyekiti wa CHADEMA, Mheshimiwa Freeman Mbowe anavyotaka, hakutaleta mabadiliko wanayoyataka katika sheria hii. Naamini na wao wanautambua ukweli huo.
Ndugu Wananchi;
Kuna msemo wa wahenga kuwa “historia hujirudia”. Naomba hekima ziwaongoze viongozi wa CHADEMA, CUF na NCCR-Mageuzi na zituongoze sote kutumia utaratibu tulioutumia mwaka 2012. Kulipotokea mazingira kama haya pande zote zilikaa pamoja na kuzungumzia hoja moja baada ya nyingine na kukubaliana nini kifanyike na kifanyike vipi. Baada ya kuridhiana hatua zipasazo za kisheria na kanuni zilichukuliwa na kumaliza mzozo.
Ndugu Wananchi;
Kufanya kinyume cha hayo hakutaleta ufumbuzi wa mzozo huu. Tutaliingiza taifa kwenye matatizo yasiyokuwa ya lazima. Tukikataa kufanya hayo Watanzania wanayo kila sababu ya kuhoji dhamira zetu na kutilia shaka nia zetu. Watakuwa na haki ya kuuliza nia ni hii yetu sote ya kupata Katiba Mpya kwa kutumia njia za kikatiba na kisheria au tuna dhamira nyingine iliyojifisha?
Kama dhamira yetu ni kutaka kupata Katiba mpya kwa mujibu wa Katiba na Sheria, ushauri wangu na rai kwa ndugu zetu wa CHADEMA, CUF na NCCR-Maguezi ni kuwa waachane na mipango ya maandamano na kufanya ghasia. Badala yake watumie njia halali zinazotambulika kikatiba na kisheria kujenga hoja za kufanya marekebisho wanayoyaona wao yanafaa kuboresha Sheria ya Marekebisho ya Sheria ya Mabadiliko ya Katiba. Tukifanya hivyo tutakuwa tunajenga badala ya kubomoa. Tutaliponya taifa. Sisi katika Serikali tuko tayari.
Ndugu Wananchi;
Napenda pia kuzisemea baadhi ya hoja zilizotolewa na Kambi ya Upinzani. Kwanza kabisa nasema kuwa nimesikitishwa sana na madai na tuhuma za uongo eti katika uteuzi wa Tume ya Katiba sikuheshimu mapendekezo ya TEC, CCT na walemavu.
Ndugu Zangu, Watanzania Wenzangu;
Siyo tu kauli hiyo ya Mheshimiwa Tundu Lissu ni uzushi na uongo mtupu bali pia ni ya unafiki, fitina na uzandiki wa hali ya juu. Nasema hivyo kwa sababu, sipendi kuamini kuwa Mheshimiwa Mbunge amesema yale kwa kutokufahamu ukweli au kwa bahati mbaya. Amesema yale kwa makusudi mazima ya kupotosha ukweli ili pengine isaidie kujenga hoja yake ya kutaka Rais asiteue wale Wajumbe 166 wa Bunge Maalum.
Napenda ieleweke kuwa siishabikii kazi hiyo, lakini kwa kutimiza wajibu na maslahi ya taifa nikiagizwa na Sheria za nchi nitafanya. Nasema hivyo kwa sababu nafahamu ni kazi ngumu. Kama kazi ya uteuzi wa Wajumbe 30 wa Tume haikuwa rahisi hata kidogo, hii ya uteuzi wa watu 166 itakuwa ngumu zaidi. Ile ya Tume ilikuwa ngumu kwa namna mbili. Kwanza, kwamba taasisi zilizoomba na waombaji walikuwa wengi mno kuliko nafasi za kujaza yaani 15 Zanzibar na 15 Bara. Zanzibar ziliomba taasisi zaidi ya 60 na waombaji walikuwa zaidi ya 200 wakati Bara kulikuwa na taasisi zaidi ya 170 zikiwa na waombaji zaidi ya 500. Kupata watu 30 kutoka orodha kubwa kiasi hicho si mtihani mdogo. Pili kwamba tulitakiwa kuunda Tume inayoasili sura ya taifa, yaani watu wa nchi yetu kwa maeneo, vyama vya siasa, dini, wanawake, vijana, walemavu, wafanyakazi, wasomi, Wabunge, Wawakilishi, wanasheria, wafanyabiashara, wakulima, asasi za kiraia n.k.
Ndugu Wananchi;
Pamoja na changamoto hizo, lakini tulifanikiwa kuunda Tume iliyopokelewa vizuri na jamii na kufanya watu wengi hata wale ambao hawakuteuliwa wahisi kuwakilishwa. Tulifanyaje? Kwanza kabisa tulihakikisha kuwa tunapata wawakilishi wa vyama vya siasa vyenye wawakilishi Bungeni na kwenye Baraza la Wawakilishi na tunapata wawakilishi wa mashirika ya dini zetu kubwa yaani, TEC, CCT na BAKWATA. Ndiyo maana nikasema kuwa kwa Mheshimiwa Tundu Lisu kudai kuwa mapendekezo ya TEC na CCT hayakuheshimiwa ni uongo wa mchana usiokuwa na kichwa wala miguu.
Baada ya hapo ndipo tukaangalia waombaji wa makundi na taasisi nyingine. Tulijitahidi sana kupata watu ambao wanawakilisha kundi zaidi ya moja. Tulifikiria hivyo kwa sababu ni ukweli ulio wazi kuwa si kila taasisi iliyoomba itapata mwakilishi kwani hata tungependa iwe hivyo nafasi hazikuwepo. Kwa kutumia utaratibu huu makundi mengi yamepata uwakilishi kutokana na watu waliopendekezwa na makundi mengi. Tumefanya kazi kubwa sana ya kuwianisha mambo na makundi ya maslahi mbalimbali nchini.
Ndiyo maana naiona mantiki ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania akishirikiana na Rais wa Zanzibar wa kuwateua Wajumbe wa Bunge Maalum. Dhana kuwa kila kikundi kiteue chenyewe watu ingefaa sana kama kungekuwepo na nafasi za kutosha kila kundi nchini. Hilo haliwezekani, labda tuwe na Bunge Maalum lisilokuwa na ukomo wa wajumbe.
Ndugu Wananchi;
Mimi na Rais wa Zanzibar tumekuwa tunajiuliza baada ya kazi ngumu na nzuri tuliyoifanya na iliyopongezwa na wengi ya kuteua Tume ya Mabadiliko ya Katiba nini kilichoharibika sasa hata tuonekane hatuaminiki kuteua hawa 166? Kama ni kwa sababu za Mheshimiwa Tundu Lissu, nimeshasema hazina ukweli wowote. Ninapojiuliza kwa nini aseme uongo nashindwa kupata jibu linaloingia akilini. Wakati mwingine nafikiria kuwa ni hiana. Lakini nadhani ni hila za kisiasa zenye nia ya kutaka kupata watu wa kutetea maslahi ya chama chake. Kama hiyo ndiyo shabaha basi amekosea sana.
Ndugu Zangu, Watanzania Wenzangu;
Hatutengenezi Katiba ya Chama fulani bali Katiba ya nchi, Katiba ya watu wa vyama vyote na wasiokuwa na vyama ambao ndiyo wengi kuliko wote. Lazima tuongozwe na ukweli huo na tuwe na msimamo huo wakati wote. Lazima tukumbuke kuwa si watu wote wanaostahili au kuwa na sifa ambao wataomba na kupata nafasi ya kuwa Wajumbe, hivyo wale wachache watakao bahatika lazima wawasemee wote. Wanatakiwa kusikiliza na kuwakilisha mawazo ya wote hata wale wasiokuwa wa Chama chao au kundi lao.
Ndugu Wananchi;
Bahati nzuri hii ndiyo sifa kubwa iliyooneshwa na Wajumbe wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba. Wamewasimamia na kuwasemea watu wote bila ya kubagua. Natambua kuwepo kwa baadhi ya watu ambao hawafurahii msimamo huo na matokeo ya kazi yao. Watu hao kuwalaumu Wajumbe wa Tume kwa ajili hiyo ni kuwaonea na kutowatendea haki. Tunataka watakaokuwa Wajumbe wa Bunge Maalum nao waige mfano huu mzuri. Wajali maslahi mapana ya taifa letu na watu wake badala ya kujali yale ya taasisi zao au makundiyao.
Zanzibar Kutokushirikishwa
Ndugu Wanachi;
Nimeambiwa pia kuliwepo madai ya Zanzibar kutokushirikishwa ipasavyo. Nimeeleza kwa kiasi gani Serikali ya Mapinduzi Zanzibar imeshirikishwa na kutoa maoni yake yaliyojumuishwa katika Muswada. Hivyo basi napata tabu kuyaelewa madai kwamba Serikali ya Mapinduzi Zanzibar haikushirikishwa msingi wake nini! Labda kuna kitu sikuambiwa!
Nimeulizia kuhusu hoja ya Kamati kutokufanya vikao Zanzibar kusikiliza maoni ya wadau wa Zanzibar. Nimeambiwa kuwa Kanuni za Bunge hazina sharti hilo hivyo Kamati haistahili kulaumiwa. Kama hivyo, nashauri kuwa suala hili lirudishwe Bungeni ili Wabunge walizungumze na kulifanyia uamuzi muafaka. Vinginevyo watu wataendelea kulauminiana isivyostahili. Hivyo basi, kuligeuza jambo hili kuwa ni suala la kukataa Muswada au kususia vikao vya Bunge au kufanya maandamano sidhani kama ni sawa.
Ndugu Wananchi;
Nimeambiwa pia kuwa kulikuwa na hoja ya kutaka idadi ya Wajumbe wa kutoka Tanzania Bara na Zanzibar iwe sawa kama ilivyo kwenye Tume ya Mabadiliko ya Katiba. Sababu ya idadi ya Wajumbe wa Tume kuwa sawa inatokana na utaratibu wao wa kufikia uamuzi. Ni kwa maelewano ya wote (consensus) na siyo kwa kupiga kura. Ndiyo maana idadi imewekwa sawa ili sauti za pande zote zisikike sawia. Bunge Maalum lina sharti la kufanya uamuzi kwa theluthi mbili ya kura za kila upande kukubali. Bila ya hivyo hakuna uamuzi.
Hivyo basi, katika Bunge Maalum nguvu si uwingi wa kura ambazo upande fulani unaweza kupata bali ni ulinganifu sawa wa kura za kila upande peke yake. Huu ndiyo msingi unaotumika katika Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania hivi sasa kwa lengo la kulinda maslahi ya Zanzibar. Zanzibar ina Majimbo 50 ya uchaguzi na Tanzania Bara ina Majimbo 189, hivyo ukiamua kwa wingi kila wakati Wazanzibari watashindwa. Lakini, hapajakuwepo madai ya Zanzibar nao kutaka kuwa na idadi sawa ya majimbo kama Bara au kupunguza majimbo ya Bara yawe sawa na ya Zanzibar kwa sababu wingi si hoja. Msingi unaotumika ni kutoa nguvu sawa za uamuzi kwa kila upande wa Muungano wakati wa kuamua masuala ya Katiba. Hakuna mdogo wala mkubwa, wote wako sawa. Hakuna mdogo kumezwa na mkubwa. Ndiyo msingi unaopendekezwa kutumika kwenye Bunge Maalum hivyo hakuna kitakachoharibika kwa idadi ya Wajumbe kutokukulingana. Nadhani inafaa ibaki ilivyo. Lakini kama Wabunge wataamua waongeze idadi itakuwa kwa sababu nyingine siyo hii ya mfano wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba.
Ndugu Wananchi;
Katika orodha ya madai ya ndugu zetu wa upinzani lipo suala la uhai wa Tume ya Katiba. Wanataka usiishe wanapokabidhi rasimu ya pili kwa Bunge Maalum bali waendelee kuwepo mpaka mwisho wa mchakato. Nimeulizia ilikuwaje? Nimeelezwa kuwa jambo hili halitokani na mapendekezo ya Serikali wala ya Kamati ya Bunge ya Katiba, Sheria na Utawala. Limetokana na pendekezo la Mbunge katika Bunge wakati wa kupitia vifungu na kuungwa mkono na Wabunge wengi. Kwa hiyo kuilaumu Serikali si haki. Serikali inaweza kuwa mshirika katika hoja hii.
Nami naiona hoja ya Wajumbe wa Tume kuwa na wajibu wakati wa Bunge Maalum hasa wa kusaidia kufafanua mapendekezo ya Tume. Je ushiriki huo uwe vipi? Je ni Wajumbe wote au baadhi yao ni jambo linaloweza kujadiliwa.
Ndugu Wananchi;
Naomba nimalizie kwa kuwasihi viongozi wa CHADEMA, CUF na NCCR-Mageuzi kuongozwa na hekima iliyotumika wakati tulipokuwa na tatizo linalofana na hili kuhusu Sheria ya Mabadiliko ya Katiba. Mimi naamini kama iliwezekana kufanikisha mambo wakati ule inaweza kufanya hivyo hata safari hii. Itatufikisha pale tunapopataka salama salimini bila maandamano, kushupaliana au uvunjifu wa amani. Kupanga ni kuchagua, naomba sote, mmoja mmoja na kwa umoja wetu tuchague njia ya mazungumzo na maelewano kwani itaihakikishia nchi yetu amani, usalama na utulivu. Tukifanya hivyo historia itatuhukumu kwa wema.
Mungu IbarikiTanzania. Nawashukurusanakwa kunisikiliza.

- Sep 28, 2013
Hotuba ya Mheshimiwa Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika mkutano mkuu wa Umoja wa Mataifa wa 68, New York, Seotemba 27, 2...
Soma zaidiHotuba
Mr. President;
Mr. Secretary-General;
Excellencies;
Ladies and Gentlemen;
Allow me to begin by congratulating you Mr. President on your well-deserved election to steer the affairs of 68th General Assembly of our esteemed organisation. As I congratulate you, I would like to assure you of Tanzania’s support and cooperation in the discharge of your responsibilities. I also wish to acknowledge and commend your predecessor, His Excllency Vuc Jeremic for his outstanding leadership of the 67th General Assembly. A lot was achieved because of his visionary and wise leadership.
In the same vein, I would like to pay glowing tribute to our illustrious Secretary General for the excellent work he is doing for the United Nations and humanity at large.
My delegation and I, find the theme of this year’s General Assembly to be timely and very opportune. Indeed, we should start now to set the stage for the post 2015 development agenda. Hence, for the theme of this 68th General Assembly to be “Post-2015 Development Agenda: Setting the Stage” is the wisest thing to do. It affords us the opportunity to know where we are with regard to the Millennium Development Goals and decide what needs to be done to complete the unfinished business and enable us to make informed decision beyond 2015.
The Status of MDGs
Mr. President;
Millennium Development Goals framework is the best development framework ever developed to address global and national development challenges. The world has never witnessed such a coalescence of concerted efforts into a unified framework. It is heartwarming indeed to note that progress towards attaining MDGs has been made in the last 13 years. However, the progress varies from one goal to another and is highly uneven among nations and continents.
Mr. President;
Although extreme poverty has been halved at the global level, over 1.2 billion people are still trapped in extreme poverty; and an estimated 19,000 children under the age of five and around 800 women die every day mostly from preventable and curable diseases and other causes. This is totally unacceptable in the world of plenty we live in today where there is unprecedented advancement in science and technology which can be leveraged to solve almost all development challenges facing humanity. In a world which has enough food to feed everybody, nobody should go hungry or be undernourished. In a world with so much wealth, there is no reason why poverty, hunger and deprivation should ever continue to inflict pain and cause misery to many people. It is incomprehensible therefore, why the MDG’s could not be attained to the fullest.
This reality must be taken into account when we attempt to find ways to tackle unfinished business of the 2000 MDGs and design the post-2015 development agenda. Mechanism must be put in place to ensure that sources of financing will be adequate and reliable.
Mr. President;
Tanzania made significant progress in implementing the MDGs. We have already achieved the targets in four of the eight MDGs well before the set deadline of 2015. On MDG 2 we have achieved a target on universal primary education enrolment. On MDG 3 we have achieved target of parity of boys and girls in both primary and secondary schools enrolment. This is different from the past when there were more boys than girls. As a matter of fact, the trend appears to be tilting towards getting more girls than boys in the near future. We are yet to meet targets with regard to the ratio of females to males in tertiary education and in position of decision making particularly Parliament. However, it is possible to achieve the target on Parliamentarians by 2015 by taking advantage of the ongoing Constitutional review process.
We are on target with regard to reducing HIV/AIDS infection rate, the requirement of MDG 6. Similarly, we have attained MDG 4 on Child Mortality which is big achievement indeed, compared to where we were in the year 2000. But it is depressing we are not on track with regard to MDG 5 on Maternal Health. We are intensifying efforts to do better in order to improve the maternal health among Tanzania women.
With regard to MDG 7 on Environmental Sustainability we are on target with regard to drinking water for urban population. But, we are lagging behind with respect to rural water supply as well as access to improved sanitation both in rural and urban areas.
That notwithstanding, we have not relented in our pursuit of the targets in the MDGs which we are not likely to achieve by 2015. This will be the unfinished business for which we need to take action probably over and above what we are doing. We are lagging far behind with regard to MDG 1 in its four main indicators. There is not much possibility of achieving the targets despite the efforts we have been making.
We have been intensifying actions to transform and modernise our agriculture. Our aim is to increase productivity and farmers’ incomes as well as ensure food and nutrition security for themselves and the nation. Agriculture employs 75 percent of the Tanzania population and this is where the majority of poor are concentrated. Improved agriculture means less poor and hungry people. Plans are also underway to expand the conditional cash transfer programme under the Tanzania Social Action Fund supported by the World Bank. We want to increase the size of investment to benefit more vulnerable people so as to accelerate the implementation of MDG 1 in the shortest possible time.
Mr. President;
Generally, it remains my firm belief that despite some failures, MDGs have been nothing short of a remarkable success. If the developed countries provided the financing as envisaged under MDG 8 and as per the Monterrey Consensus and their own commitment in different fora of the G8 and G20, we would have implemented all the MDGs to the letter and spirit. It is in this regard we would find unrealistic any approach to the post-2015 Development agenda that does not address the critical issue of ensuring adequate financing. This is also true with regard to accelerating implementation of the MDGs in the remaining period.
We will continue to look at the United Nations for guidance and leadership in steering both processes to their successful conclusion.
The Reform of the United Nations
Mr. President;
The fact that the United Nations needs reform is a matter of little disagreement. Our collective failure to respond to this reality creates scepticism on our common resolve to strengthen an institution that is meant to serve nations and peoples. The reform we demand is long overdue. While we welcome discussions on the reform of the ECOSOC, Africa will not relent in demanding reform of the Security Council so that the continent, with the largest membership of the UN, has a permanent voice.
Global and Regional Conflict Situation
Mr. President;
Regrettably conflicts have continued to interfere in our development endeavours as they linger on in different parts of the world, from the Sahel to eastern DRC, Syria to Afghanistan, and other areas. They have caused enormous loss of innocent lives as populations continue to endure untold sufferings. The recent use of chemical weapons in Syria as confirmed by the United Nations inspections team to kill innocent people is rather distressing. We condemn such flagrant and senseless killing of innocent people including children in Syria. We commend the Secretary General and the UNSC for way they handle the matter. I believe the doors for a peaceful solution to the Syrian problem are not closed and that a military solution should be the last resort.
The Situation in the Great Lakes Region and DRC
Mr. President;
The United Republic of Tanzania regrets to see the suffering of the people of DRC as a consequence of the conflict in Eastern DRC has continued for far too long. We hope this time around the initiative of the Secretary General which resulted in the establishment of the Peace, Security and Cooperation Framework for the Great Lakes Region and DRC signed in February, 2013 will deliver lasting peace, security and development for the DRC and the Great Lakes Region. We highly commend the UN Secretary General for his vision and leadership in this regards. We welcome the choice of Her Excellency Mary Robinson, former President of Ireland as the United Nations’ Special Envoy for the Great Lakes Region. She will surely help advance the cause of peace in the region if supported by all of us in the region and the international community.
Part of the enduring problem facing the DRC is the proliferation of armed groups with varied interests. Bolder action is required to uproot these negative elements. These groups should be neutralized and disarmed. It is in this context that we welcomed MONUSCO’s expanded mandate as per resolution 2098 (2013) of the Security Council that among other things established the Force Intervention Brigade (FIB). Tanzania agreed to contribute troops to the FIB because it can help to deter belligerence and create a conducive environment for a political process to take effect. Of course the panacea to the DRC problem is political rather than military.
Tanzania’s Role in Peacekeeping
Mr. President;
Since 2007 Tanzania has become proactive in contributing troops to the United Nations Peacekeeping Operations. With over 2,500 peace keepers in Lebanon, Darfur and the Democratic Republic of Congo, we are the 6th contributor of military and police peacekeepers in Africa and 12th globally. We are partaking this noble endeavour, as members of the United Nations with the duty of advancing and upholding the ideals of our esteemed organisation.
We are satisfied that our contribution, though modest, is having a broader impact to those who have experienced the horrors of conflict. In this endeavours our peacekeepers have paid the ultimate price as was the case with the loss of we seven brave soldiers in Darfur, Sudan under UNAMID and two in Eastern DRC under MONUSCO. These are our national heroes whose sacrifices are not in vain.
The death of our peacekeepers was a grim reminder of the dangers facing peacekeepers around the world. It is disturbing that, armed groups and peace spoilers are increasingly attacking these servants of peace. We must unreservedly condemn all these attacks as there is no cause or justification for such barbaric attack which constitute a crime under international law. The UN Security Council whose primary role is the maintenance of international peace and security should be in the forefront in condemning such barbaric acts in good time.
Unilateral Sanctions and Embargo
Mr. President;
At this juncture, I wish to reiterate our call for ending unilateral economic, commercial and financial embargo against Cuba which has lasted for more than 50 years. Our call to end this unilateral embargo is not only predicated on its legality but also on humanitarian concerns particularly the negative effects of the quality of life of innocent Cubans.
We are deeply encouraged by recent developments especially of removing restrictions on family travel, cash remittances and telecommunication services. We believe this spirit will culminate into total cessation of the embargo in not to distant a future so that Cubans will be relieved of enormous economic, social and financial hardships they have endured for far too long.
Western Sahara
Mr. President;
The quest to resolve the dispute over the sovereignty of Western Sahara is also long overdue. It is high time that the United Nations took bold actions to give the people of Saharawi the opportunity to decide on their fate. It is incomprehensible why the Security Council which has been able to handle bigger security challenges cannot decide on the matter for nearly forty years now.
International Criminal Court
Excellencies;
Ladies and Gentlemen;
You will agree with me that the Rome Statute establishing the International Criminal Court (ICC) was a major milestone of the international criminal justice system. Indeed, the Court's creation as a machinery for fighting impunity was only possible with the support of Africa.
However, a decade after its entry into force, a rift has grown between the Court and the continent. The court is perceived as irresponsive to what are, in our view, legitimate concerns of African people.
It continues to ignore repeated requests and appeals by the African Union. It was sad to note that legitimate requests regarding the timing of the trials of President Uhuru Kenyatta and Deputy President William Rutto went unanswered. This attitude has become a major handicap that fails to reconcile the Court's secondary and complementary role in fighting impunity. Indeed, the Court's rigidity has proven counterproductive and stands to undermine the support it enjoys in Africa.
Terrorist Attack in Kenya
Tanzania condemns in the strongest terms possible the cowardly terrorist attack that happened last week at the Westgate Mall in Nairobi, Kenya which left at over 60 innocent people dead and hundreds others injured. I spoke and wrote to President Uhuru Kenyatta to express our sadness and dismay. I also reaffirm our solidarity with him and people of Kenya during these difficult moment and the fight against terrorism. This horrendous attack is a heart-breaking reminder of the threat that terrorism poses to humanity. Indeed none of us is completely safe from terrorism as it can happen anywhere, anytime and to anyone.
We must increase vigilance, enhance regional and global cooperation and scale up the fight against terrorism. The challenge ahead of us cannot be understated nor underestimated. The success will depend on our unity of purpose and determination. At this juncture I would like to commend His Excellency Uhuru Kenyatta, President of the Republic of Kenya for his exemplary leadership in the wake of the attack and his unshaken resolve and firm commitment to support the peace building efforts in Somalia and elsewhere. We are with Kenyan people at this time of distress and grief.
Conclusion
Mr. President;
In conclusion, I would like to stress once more that, we are passing through a time of great opportunity despite the many challenges. We must take advantage of the current scientific and technological innovations; information and communication technologies; and knowledge and lessons learned from the implementation of development programmes, including MDGs to build a world without poverty, hunger, diseases and deprivation.
A world that protects its environment and nature. It is possible to have a world without wars, conflicts and acts of terrorism. A world where human rights are respected, rule of law observed, democracy reigns and civil society is regarded as an integral part of the development endeavour. With stronger multilateralism and the United Nations leading the way and, with strong political will on the part of national leaders and the people everything is possible. We can make our world a better place for everyone to live.
I thank you for your kind attention.