Hotuba

- Jul 13, 2015
OPENING ADDRESS BY H.E. DR. JAKAYA MRISHO KIKWETE, PRESIDENT OF THE UNITED REPUBLIC OF TANZANIA TO THE 12TH FORUM OF COMMONWEALTH HEADS OF AFRICAN PUBLIC SERVIC...
Soma zaidiHotuba
Honorable Minister(s);
Chief Secretary of the Government of the United Republic of Tanzania;
Heads of African Public Service;
Distinguished Delegates;
Ladies and Gentlemen;
I thank you for the honor to warmly welcome you all to Tanzania for the 12th Forum of Commonwealth Heads of African Public Service. It is my sincere hope that your stay here though short, will be as pleasant as possible. We thank you for attending in great numbers, for it gives this meeting the weight and importance it deserves.
Theme of the Forum
Distinguished Delegates;
I congratulate the organizers for choosing a very pertinent theme for this forum: “From Good Plans to Effective Execution: Anchoring Policy Coherence, Strategy and Execution for the Higher Performance Culture in the Public Service”. You will agree with me that all governments wish to deliver better public service. However, wishes in themselves have proven not to be enough, neither do they deliver the desired outcome. Therefore, we are expected to improve on delivery and go beyond crafting good policies, strategies and plans. We are expected to improve on execution and delivery. For, the effectiveness of government is not only reflected in its ability to formulate good policies, but on its ability to execute them. And more so, the times that we are in and the increasing stakeholder’s appetite for scrutiny and demand for accountability, makes the legitimacy of the governments at stake.
The key issue all over has and will remain to be, how do we enhance and ensure government delivery? There are fundamental questions we need to ask ourselves. How can government create an impact on its policies and programmes and how can we measure that? How do we translate good policy decisions and processes into tangible results on the ground? How do we bridge the execution-gap between policy decision and delivery? What is really wrong, a policy or the implementation?
For sure, there are no readily available textbook answers. All governments are working round the clock to try to answer them based on their realities and experiences and within their competences. No wonder, public service reform has been a buzz word and at the heart of this process of modernization. Therefore, sharing experiences, lessons and learning from one another as we do at this meeting is the surest way towards answering these lingering questions of all time.
Tanzania Experience on Reforms
Distinguished delegates;
Many of our countries, particularly those in the developing world inherited, at independence, a public service designed to serve the colonial system. It was lead by foreigners, it was small with the focus on facilitating provision of essential colonial services.
The circumstances then called for immediate intervention by the newly independent government in the quest to pursue the nation building project. In the then Tanganyika and later Tanzania, for example, the civil service adopted a series of reforms which focused on building institutions and human resource capacity to respond to needs of a new nation. In our case, we pursued Africanization program aimed at replacing the foreigners inherited in the civil service, expanding rapidly the provision of basic social services and its infrastructure by bringing the services closer to the people. That led to rapid expansion of the civil service in both scope and size. At that formative stage, the focus was on the establishment of the civil service and institutions than on the delivery. That was the first generation of the civil service reforms.
There was a radical shift and departure from this in the nineties following economic crises and ensuing structural reforms. We adopted the second generation of reforms that leaned towards the free market economy. The emphasis was reducing the involvement of the government in the management of the economy, for greater efficiency and effectiveness. Let Governments govern and Private Sector do business. We adopted Civil Service Reform Program in 1991 which ran up to 1999. The Purpose was to reorientate it to serve the new political economic landscape. It resulted into downsizing the government through restructuring and cost containment.
We embarked on decentralization programs, devolution of powers to local authorities form Central Government, and establishment of executive agencies and outsourcing of non-core services. We reduced Ministries, Department and Units by 25 percent, reducing employees significantly from 355, 000 in 1992 to 264,000 by end of 1998, and some important changes in salary structures and incentive schemes. Even with such reforms, yet the government delivery and efficiency could not be fully attained. At that stage the major preoccupation was on the consolidation of the civil service by putting systems to improve operation.
In year 2000, we embarked on a serious 11 years Public Service Reform Program (PSRP). The aim was to create a new public administrative system and structures featuring standard legalized behavious, coordinated operation, fairness and transparency. The vision was such that, the public service in Tanzania would transform to an institution of excellence to play a pivotal role in achieving sustainable economic growth, prosperity and eradication of poverty.
Significant achievements have been recorded in number of areas as result of reform program. Indeed, things improved for the better. There was improved service delivery levels and access and timeliness of service delivered in certain services. Public servants remuneration increased steadily and continuously since then to date. There has been, also, an improvement in the working environment in the civil service. Such improvements were also recorded on the policy and decision making processes such as budgeting. However, this also did not answer the critical and fundamental problems of effectiveness and efficiency in terms of accountability and government delivery. The main gain was on improving processes which has impacted positively on policy and decision making process. Yet, the question about government delivery was not adequately answered.
The Big Results Now
Ladies and Gentlemen;
When I assumed office in 2005 as President of our country, I encountered the same challenge. How can I make government deliver? The first five years’ experience has taught me valuable lessons. Much as we have been changing laws, policies and introducing new institutions, there was a dire need to change the way we do things by putting more emphasis on execution and delivery.
I realized, the problems may necessarily not lie in the quality of policy making process or policies themselves, but on the mechanisms in place for implementation, monitoring and evaluation. I noticed that, much of our time we are being bogged down by processes and bureaucratic inertia. Civil servants are much more rewarded and measured by how faithful and conservative they are to processes than results. Not how much they deliver. As a result, they enjoy more gymnastics of policy making than that of execution. At the end of these long and tedious processes, it is difficult to establish the impact in terms of delivery to the public which is more interested in results than the processes.
Ladies and Gentlemen;
In year 2012, I undertook an official visit to Malaysia. My interest in that visit, was among other things to learn from the success story of Malaysia, with regard to government delivery. I wanted to know, what it is, that they do differently. I realized that, they have adopted mechanisms that helped improve government delivery.
When I got back, based on lessons learnt we crafted what we called the ‘Big Results Now” Programme. This was our programme on government delivery. We conducted seminars to my Cabinet, Permanent Secretaries and Heads of Local Government across the government to orient them on the new delivery mechanism. The Seminar was followed by a Cabinet meeting where we identified 6 priority sectors that we agreed to start with on the new model of enhancing government delivery. These sectors were agreed through a very democratic process were Education, Water, Infrastructure, Energy, Agriculture and Resource Mobilization. Later, we added the Health Sector and Business Environment.
How BRN Works
Ladies and Gentlemen;
In the BRN Programme all actors from the government, private sector, civil society, development partners and other stakeholders meet. They do an evaluation of the prevailing situation in the sector. Through thorough discussion they identify areas of strengths and weakness and agree on what needs to be done to advance and consolidate the gains made and improve on the weakness made. They also set targets and time frames and apportion role. On allocating budgetary resources the government has to give top priority to the sectors identified for priority action. I established the Presidential Delivery Bureau (PDU) in my office to track implementation of agreed targets, compile report and appraise me on the progress being made by the implementing agency concerned.
Success of the BRN
Ladies and Gentlemen;
The BRN program has worked well so far despite challenges that we face in terms of resource mobilization. It has improved system wide coherence in government in terms of focus, data, and results that can be tracked and verified. It has overall improved discipline and culture of execution within the government. The involvement of stakeholders in the formulation of goals, targets and indicators has increased public involvement, confidence and scrutiny. Has Promoted transparency and accountability for results.
Way Forward
Ladies and Gentlemen;
The future of the governments and their legitimacy will depend more on how effective they are in delivering tangible results. We must adopt measures that promote popular participation and ownership of the development agenda. We must make public service people-oriented, based on meritocracy and driven by service to the citizenry, transparency and accountability. Public service should implement its commitment on governance and public administration; mobilize budgets and manages public finances effectively. The public sector must find ways of improving the performance culture that precipitates efficiency and effectiveness of its service delivery. This means providing value for money by improving quality of service, and reducing the costs involved in providing those services.
Conclusion
Ladies and Gentlemen;
Efficient and effective government delivery remains major pre-occupation today and in future. Our experience on the implementation of the BRN convinces us that we need to continue to expand its scope by scaling up to bring on board all sectors in the near future. We believe that an effective government is the one that is able to deliver results, track them and be able to account to the general public. The days of taking comfort in processes have long gone. It is now about details, numbers, transparency, ownership and accountability. To achieve that, decision must be made on time with right information and data, and must be executed.
Tanzania is pleased to share our experience to you and equally to learn from you. I believe that the Chief Secretary will share with you more details about our BRN. We look forward, to also learning from your experiences on approaches and lessons that you use in your respective countries to enhance government delivery.
Having said that, let me wish you fruitful deliberations over the next three days. It is now my pleasure to declare the 12th Forum of Heads of Public Services of Commonwealth Africa, officially open.
I thank you!

- Jul 09, 2015
HOTUBA YA MHESHIMIWA DR. JAKAYA MRISHO KIKWETE, RAIS WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WAKATI WA KUAGANA NA BUNGE NA KULIVUNJA BUNGE LA KUMI LA JAMHURI YA MUUN...
Soma zaidiHotuba
Mheshimiwa Spika;
Tunayo kila sababu ya kumshukuru Mwenyezi Mungu mwingi wa rehma kwa kutujalia uzima na kutuwezesha kuishuhudia siku hii adhimu katika historia ya Bunge letu na nchi yetu. Hatimaye siku ya kuvunja Bunge la Kumi imewadia ili kuwezesha hatua husika za mchakato wa Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2015 ziweze kutekelezwa.
Nakushukuru sana Mheshimiwa Spika kwa kunipatia nafasi hii ya kulihutubia Bunge lako tukufu ili niweze kutimiza wajibu wangu huo wa msingi Kikatiba. Lakini, shukrani zangu kubwa ni kwa uongozi wako mahiri na shupavu. Umeliongoza Bunge vizuri. Najua haikuwa kazi rahisi. Penye wengi pana mengi. Lakini kwa uhodari mkubwa umeweza kulifikisha jahazi bandarini salama salmini. Hakika wewe ni nahodha makini na jemedari hodari, uliyethibitisha uhodari na umakini wako katika uwanja wa medani. Wewe ndiwe mwanamke wa kwanza kushika wadhifa huu wa juu kabisa katika mhimili huu wa kutunga sheria na umeidhihirishia dunia kuwa wanawake wakipewa nafasi wanaweza.
Mheshimiwa Spika;
Niruhusu pia nitoe shukrani na pongezi zangu za dhati kwa Waheshimiwa Wabunge kwa kazi kubwa na nzuri mliyoifanya. Mmetimiza ipasavyo wajibu wao wa Kikatiba wa Kutunga Sheria na kusimamia Serikali. Nawashukuru kwa ushirikiano wenu na msaada wenu. Ni ukweli ulio wazi kuwa bila ya ninyi Wabunge wetu na Bunge hili, tusingeweza kupata mafaniko na maendeleo tuliyoyapata. Mmejijengea, nyinyi wenyewe na Bunge letu heshima kubwa mbele ya wananchi. Mmeitendea haki demokrasia ya Tanzania na kuliletea heshima kubwa Bunge letu nchini, kikanda na kimataifa.
Mheshimiwa Spika;
Tarehe 30 Desemba 2005 nilipozindua Bunge la Tisa nilielezea mtazamo wangu kuhusu nchi yetu na kutaja majukumu ya msingi na vipaumbele vya Serikali ya Awamu ya Nne. Nilisema tutatekeleza wajibu wetu na vipaumbele hivyo kwa ari mpya, nguvu mpya na kasi mpya. Tarehe 16 Julai, 2010 wakati wa kuvunja Bunge hilo nilielezea mafanikio tuliyopata na changamoto zilizotukabili katika kipindi hicho. Tarehe 28 Novemba, 2010 wakati wa kuzindua Bunge hili la Kumi niliainisha vipaumbele vya Serikali ya Chama cha Mapinduzi katika kipindi changu cha pili cha uongozi wa nchi yetu na kuahidi kuvitekeleza kwa ari zaidi, nguvu zaidi na kasi zaidi. Kama ilivyo ada, leo tunafikia mwisho wa uhai wa Bunge la Kumi, naomba kutumia fursa hii kutoa mrejesho wa utekelezaji wa majukumu ya Serikali na yale mambo ambayo tuliahidi na kupanga kufanya.
Umoja, Amani na Usalama
Mheshimiwa Spika;
Niliahidi kuwa katika kipindi cha uongozi wangu nitafanya kila niwezalo kuhakikisha kuwa Tanzania inaendelea kuwa nchi moja na watu wake wanaendelea kuwa wamoja, wanaopendana na kushirikiana licha ya tofauti zao za rangi, dini, makabila, mahali watokako, na ufuasi wa vyama vya siasa. Pia, kwamba nchi yetu itaendelea kuwa yenye amani, usalama na utulivu.
Leo tunapoagana, ninyi na mimi, ni mashuhuda kuwa Tanzania na Watanzania tumebakia kuwa wamoja. Hata hivyo, katika kipindi hiki kumekuwepo na matukio ya hapa na pale madogo na makubwa, yaliyotishia umoja wa nchi yetu na watu wake. Yapo mambo yaliyopandikizwa kuleta chuki baina ya Tanzania Bara na Zanzibar, baina ya Wakristo na Waislamu na baina ya maeneo fulani ya nchi na wengine.
Bahati nzuri, msimamo thabiti wa viongozi wakuu wa Serikali zetu mbili wakisaidiwa na viongozi wengine pamoja na ushirikiano na viongozi wa dini na wa jamii na uelewa wa wananchi, vimeliwezesha taifa letu kushinda changamoto hizo na matishio yote hayo. Changamoto hizi zimethibitisha ubora wa mazungumzo. Ni kweli kabisa kwamba wanaozungumza hawagombani na wanaozungumza humaliza tofauti zao bila kugombana.
Mheshimiwa Spika;
Niruhusuni, nitumie nafasi hii kuwashukuru kwa mara nyingine viongozi wakuu wenzangu, Makamu wa Rais, Rais wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar, Waziri Mkuu, Makamu wa Kwanza wa Rais Zanzibar, Makamu wa Pili wa Rais Zanzibar, viongozi wa dini, viongozi wa jamii na wananchi wote kwa ushindi tulioupata katika kudumisha umoja wetu. Hata hivyo, tahadhari kubwa lazima iendelee kuchukuliwa kwani watu wenye nia mbaya kwa nchi yetu au na umoja wetu hawajaisha na hawajafurahi kwamba hawajafaulu. Huenda wakajaribu tena. Tunachotakiwa kufanya ni kuendelea kushikamana ili hata wakijaribu tena washindwe.
Muungano Wetu Umeimarika Zaidi
Mheshimiwa Spika;
Nafurahi kwamba namaliza kipindi changu cha uongozi tukiwa tumeweza kudumisha na kuuimarisha Muungano wetu adhimu na adimu Barani Afrika. Mtakumbuka kuwa katika hotuba yangu ya kufungua Bunge la Tisa nilisisitiza umuhimu wa viongozi wa pande zetu mbili kukutana mara kwa mara kuzungumzia ustawi wa Muungano wetu. Nafurahi kwamba jambo hili limefanyika chini ya uenyekiti wa Makamu wa Rais, akisaidiwa na Waziri Mkuu kwa upande wa Tanzania Bara na kwa upande wa Zanzibar, Waziri Kiongozi katika awamu yangu ya kwanza na Makamu wa Pili wa Rais katika awamu hii.
Mafanikio yaliyopatikana ni makubwa. Masuala mbalimbali ya zamani na mapya yamezungumzwa, yameshughulikiwa na kupatiwa ufumbuzi. Kwa mfano, hadi mwaka 2005 zilikuwa zimebakia kero 13 za Muungano zilizoainishwa na Tume ya Shelukindo, hivi sasa zimebaki kero nne. Tayari ufumbuzi wa kero moja unakamilishwa kiutawala na tatu zimeshughulikiwa kwa ukamilifu katika Katiba Inayopendekezwa. Kama kura ya maoni ingekuwa imefanyika na Katiba hiyo kupitishwa kungekuwa hakuna kiporo cha kero za Tume ya Shelukindo. Lakini kwa vile kura ya maoni haijafanyika ndiyo maana tunaendelea kuzitaja. Hata hivyo, Serikali zetu mbili zimezungumza na kukubaliana tutafute njia ya kumaliza suala la rasilimali ya mafuta na gesi. Ndiyo maana katika Muswada wa Petroli hoja ya Zanzibar kuwa na mamlaka kamili ya kusimamia uchimbaji wa mafuta na kumiliki mapato yake ilijumuishwa. Natoa shukrani nyingi kwa Bunge lako tukufu kwa kupitisha Muswada huo. Moja ya kero kubwa katika Muungano tumeimaliza.
Mpasuko wa Kisiasa Zanzibar
Mheshimiwa Spika;
Mtakumbuka kuwa nilizungumzia kusononeshwa kwangu na mpasuko wa kisiasa uliokuwepo Zanzibar wakati ule na kuelezea utayari wangu wa kusaidia kuuondoa. Kama mjuavyo mazungumzo yalifanyika ndani ya CCM na CUF na baina ya vyama hivyo na muafaka ukapatikana. Serikali ya Umoja wa Kitaifa ikaundwa na mpasuko wa kisiasa ukawa umepatiwa tiba. Matokeo ya yote hayo ni kuwa mazingira ya kisiasa na kijamii yamekuwa bora zaidi siku hizi kuliko ilivyokuwa kabla ya hapo.
Ni matumaini yangu kuwa ndugu zetu wa Zanzibar watayadumisha mafanikio haya ili waendelee kuishi kwa amani, upendo na udugu. Natambua kuwepo kwa changamoto za hapa na pale katika uendeshaji wa Serikali hiyo. Jambo linalonipa faraja ni kuwa matatizo yenyewe hayahusu muundo wa Serikali bali yanaletwa na watu kupishana kauli au kutofautiana katika uendeshaji wa baadhi ya mambo. Mimi naamini hayo ni mambo yanayoweza kumalizwa kwa wadau kukaa kitako na kuzungumza kama ilivyokuwa kabla ya muafaka.
Amani na Usalama
Mheshimiwa Spika;
Nchi yetu iko salama, mipaka iko salama kwa sababu Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania limeendelea kutimiza ipasavyo jukumu lake la kulinda uhuru na mipaka ya nchi yetu. Katika kipindi hiki tumewekeza sana katika kuliimarisha Jeshi letu kwa vifaa na zana za kisasa za kivita na mafunzo. Tumeimarisha Kamandi za Nchi Kavu, Anga na Majini. Utayari kivita wa jeshi letu ni mzuri tena wa hali ya juu. Weledi na nidhamu ya Wanajeshi wetu ni ya hali ya juu. Tumeboresha maslahi na makazi ya wanajeshi kwa kujenga nyumba mpya za kuishi. Utekelezaji wa mpango wa kuwajengea nyumba 10,000 unaendelea vizuri. Hadi hivi sasa nyumba 6,064 zinaendelea kujengwa nchi nzima na kati yake nyumba 3,096 zimekamilika. Namaliza kipindi changu cha kuwa Rais na Amiri Jeshi Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi na Usalama kwa kujiamini kwamba “Tupo vizuri”. Pamoja na hayo kazi ya utekelezaji wa Mpango wa Miaka 15 wa kuimarisha JWTZ lazima iendelezwe ili kulifikisha Jeshi letu pale tulipopakusudia.
Mheshimiwa Spika;
Katika miaka 10 hii tumefanya jitihada kubwa ya kupambana na uhalifu ili kulinda usalama wa maisha na mali za watu waishio Tanzania. Mtakumbuka kuwa mwaka 2005 na mwanzoni mwa 2006 kulikuwa na matukio mengi ya ujambazi. Niliahidi wakati wa kampeni na katika hotuba yangu Bungeni kwamba hatutawaacha majambazi waendelee kutamba. Hali ile imedhibitiwa. Ingawaje matukio ya ujambazi hayajaisha, lakini hayako kama ilivyokuwa wakati ule.
Hali kadhalika, matukio ya uhalifu wa kuwania mali yamepungua kutoka 53,268 mwaka 2005 hadi 43,808 mwaka 2014. Natoa pongezi nyingi kwa Jeshi la Polisi kwa kazi kubwa na nzuri waliyoifanya na wanayoendelea kufanya. Jambo ambalo bado hatujafanikiwa vya kutosha ni ajali za barabarani. Lazima tuendelee kuzitafutia muarobaini wake. Niruhusuni niwatambue na kuwashukuru Inspekta Jenerali (mstaafu) Omari Mahita, Inspekta Jenerali (mstaafu) Said Mwema na Inspekta Jenerali Ernest Mangu aliyepo sasa kwa uongozi wao mzuri.
Mafanikio haya ni matokeo ya uwekezaji wa Serikali katika utakelezaji wa mpango wa maboresho ya Jeshi la Polisi uliobuniwa wakati wa uongozi wa Ndugu Saidi Mwema, IGP mstaafu. Jeshi la Polisi linaendelea kuwezeshwa kwa zana, vifaa na mafunzo. Taratibu zimekamilika za kulipatia Jeshi hilo magari ya kutosha ili kuongeza ufanisi.
Pia, tumeendelea kuboresha maslahi na mazingira ya kuishi Maafisa na Askari. Kwa ajili hiyo tumekarabati baadhi ya nyumba zilizopo, tumejenga nyumba kadhaa mpya za ghorofa, za kawaida na mabweni. Mipango imekamilika ya kuwezesha ujenzi wa nyumba 10,000 ambazo zitapunguza kwa kiasi kikubwa tatizo la uhaba wa nyumba za kuishi katika Jeshi la Polisi.
Mheshimiwa Spika;
Jeshi letu la Magereza nalo limeendelea kutekeleza vizuri majukumu yake ya kulinda wafungwa na kurekebisha tabia zao. Aidha, huduma za malazi, mavazi, chakula na usafiri kwa wafungwa zimeendelea kuboreshwa. Changamoto kubwa ni msongamano wa wafungwa Magerezani. Naamini mipango ya kujenga magereza mapya na kupanua yaliyopo ikitekelezwa tatizo litaisha. Aidha, mpango wa maboresho ya Jeshi la Magereza ukikamilika na kutekelezwa, utaboresha mazingira ya kufanyia kazi na kuishi maafisa na askari, hivyo kupandisha morali wao na kuongeza ufanisi.
Jeshi la Kujenga Taifa
Mheshimiwa Spika;
Ahadi yangu ya kuanzisha upya utaratibu wa kuchukua vijana wa mujibu wa Sheria katika Jeshi la Kujenga Taifa imetimia. Mpaka hivi sasa vijana 38,200 wamekwisha hitimu mafunzo hayo wakiwemo Waheshimiwa Wabunge. Nawapongeza sana Waheshimiwa Wabunge walioshiriki kwa kuongoza kwa mfano. Imesaidia sana utaratibu huo kuanza upya bila vipingamizi. Ni matumaini yangu kuwa Wizara ya Fedha, Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa watakaa pamoja kujadili namna ya kutafuta ufumbuzi kwa changamoto zilizopo. Naamini zinaweza kumalizwa, vijana wetu wakashiriki mafunzo bila matatizo yoyote.
Utawala Bora
Mheshimiwa Spika;
Katika kipindi cha miaka kumi hii tumetekeleza dhamira yetu ya kujenga na kuimarisha utawala bora kwa sera, sheria, mifumo, taasisi na kwa rasilimali watu. Tumefanya hivyo katika maeneo yote muhimu yakiwemo yale yahusuyo haki za binadamu, demokrasia, mapambano dhidi ya rushwa, maadili ya viongozi, ukusanyaji wa mapato na nidhamu ya matumizi ya fedha za umma na mgawano wa madaraka hati ya mihimili.
Bunge la Jamhuri ya Muungano
Mheshimiwa Spika;
Serikali imetimiza ipasavyo wajibu wake kwa mhimili mkuu wa dola wa Kutunga Sheria. Tulianzisha Mfuko wa Bunge na kuongeza fedha katika bajeti ya Bunge toka shilingi bilioni 30.58 mwaka 2005/06 hadi shilingi bilioni 173.76 mwaka 2015/16. Pia tumeanzisha Mfuko wa Jimbo ili kuwawezesheni Wabunge kuchangia katika kutatua changamoto za maendeleo zinazowakabili wananchi wa majimbo yao. Bunge letu limetekeleza ipasavyo majukumu yake kupitia Kamati zake za kudumu na pale ilipolazimu Kamati teule zilizoundwa.
Katika kipindi hiki miswada 163 imepitishwa, maswali ya msingi 7,544 na ya nyongeza 22,632 yameulizwa na kujibiwa. Kamati teule 2 ziliundwa. Haya ni mafanikio makubwa kwa Bunge letu. Bunge hili limefanya kazi kubwa na kazi ya kutukuka. Michango na ushauri wake umekuwa chachu ya baadhi ya hatua na mabadiliko ya kisera, kisheria na kiutendaji yaliyofanywa na Serikali. Kwa kweli mnastahili pongezi nyingi. Huwezi kutaja mafanikio ya Serikali ya Awamu ya Nne bila kutambua mchango wa Bunge hili.
Mchakato wa Katiba
Mheshimiwa Spika;
Kama sote tujuavyo, kupitia Sheria iliyotungwa na Bunge hili, mwaka 2013 tulianzisha mchakato wa Mabadiliko ya Katiba kwa lengo la kuipatia nchi yetu Katiba mpya iliyo bora zaidi kuliko iliyopo sasa. Nafurahi kwamba mchakato huo ulituwezesha kupata Katiba Inayopendekezwa ambayo imekidhi matarajio hayo. Narudia kutoa pongezi za dhati kwa Tume ya Mabadiliko ya Katiba na Bunge Maalum la Katiba kwa kazi kubwa na nzuri waliyofanya. Hatua iliyobaki ni Kura ya Maoni ambapo sote tunasubiri maelekezo ya Tume ya Uchaguzi. Mimi naamini iwapo itapitishwa, Katiba Inayopendekezwa itaimarisha zaidi taifa letu.
Vyama vya Siasa
Mheshimiwa Spika;
Katika kipindi hiki tumeshuhudia vyama vya siasa vikiendelea kuimarika na kujijenga nchini. Idadi ya vyama vya siasa imeongezeka kutoka 18 hadi 24. Vyama vya siasa vimefanya shughuli zake kwa uhuru. Viongozi na wanachama wao wamefanya mikutano mingi na hata maandamano kote nchini. Baraza la Vyama vya Siasa na TCD vimekuwa vyombo muhimu vilivyofanya kazi nzuri ya kujenga ushirikiano miongoni mwa vyama vya siasa. Yamekuwa majukwaa muhimu ya mashauriano baina ya vyama vya siasa kwa masuala mbalimbali. Matatizo na changamoto nyingi zimeweza kupatiwa ufumbuzi. Ni matumaini yangu kuwa vyombo hivi viwili vitaendelezwa na kuimarishwa miaka ijayo.
Huu ni mwaka wa Uchaguzi, na vyama vya siasa ndiyo wahusika wakuu. Ni matumaini yangu kuwa vyama vya siasa vitaheshimu na kuzingatia maadili ya uchaguzi. Hii itasaidia kuwepo kwa utulivu na amani katika mchakato wa uchaguzi.
Uchaguzi Mkuu
Mheshimiwa Spika;
Habari kubwa hapa nchini sasa ni uchaguzi mkuu. Tayari Tume ya Uchaguzi ya Taifa (NEC) na ile ya Zanzibar (ZEC) zimekwisha tangaza tarehe 25 Oktoba, 2015 kuwa ni siku ya kufanyika uchaguzi mkuu. Maandalizi ya uchaguzi huo yanaendelea vizuri. Tume ya Taifa ya Uchaguzi inaendelea na zoezi la uandikishaji wa wapiga kura kwa mfumo mpya wa teknolojia ya Biometric Voters Register (BVR). Hadi sasa zoezi la uandikishaji limekamilika katika mikoa 13 na linaendelea katika mikoa 11 na katika mkoa wa Dar es Salaam na Zanzibar uandikishaji unategemea kuanza mwezi huu. Kwa taarifa za Tume ya Uchaguzi, tayari wamekwisha andikisha hadi sasa wapiga kura milioni 11 kati ya lengo la kuandikisha wapiga kura kati ya milioni 21 hadi 23.
Sisi katika Serikali tutaendelea kutimiza wajibu wetu wa kuiwezesha Tume kutimiza wajibu wake. Napenda kuwahakikishia kuwa kila Mtanzania mwenye haki ya kupiga kura atapata fursa ya kuandikishwa. Shime tuhimize watu wajitokeze kujiandikisha ili wasikose haki yao hiyo.
Uhuru wa Habari
Mheshimiwa Spika;
Mtakubaliana nami kuwa katika kipindi hiki uhuru wa habari na uhuru wa watu kutoa maoni yao umepanuka sana. Tanzania kuna magazeti ya kila siku 16 na kati ya hayo ya Serikali ni 2 (Daily News, Habari Leo). Pia magazeti ya kila wiki yapo 62. Aidha, kuna vituo vya redio 115 na vya televisheni 29. Serikali haifanyi uhakiki wa habari kabla ya kuchapishwa au kuandikwa. Tumeamua hivyo kwa imani yangu kwamba ustawi wa demokrasia hutegemea sana uhuru wa vyombo vya habari. Pili, kwa vile tunatambua manufaa ya vyombo vya habari kuelimisha jamii, kupambana na maovu na kuhimiza uwajibikaji.
Pamoja na hayo, hatukusita wala kuchelea kuchukua hatua pale uhuru huo ulipotumiwa vibaya na kutishia kuvuruga amani, umoja na usalama wa jamii au taifa. Au, pale ambapo Sheria za nchi zimekiukwa. Huo ni wajibu wetu wa kikatiba ambao mimi na wenzangu tuliapa kuutimiza.
Mheshimiwa Spika;
Katika kuongeza uwazi na mawasiliano na wananchi mwaka 2007 tulianzisha tovuti ya wananchi. Tovuti hiyo imeshapokea hoja 117,243 na kati ya hizo zilizohusu Serikali zilikuwa 78,258 na zote zimeshughulikiwa.
Katika kuboresha mfumo wa mawasiliano, Tanzania imeshahama kutoka mfumo wa analogia na kuingia kwenye mfumo wa digitali. Hii ni hatua kubwa muhimu kwa maendeleo ya tasnia ya habari nchini. Jambo ambalo nasikitika kuwa hatukuweza kulikamilisha ni utungaji wa Sheria ya Haki ya Upatikanaji wa Habari na Sheria ya Vyombo vya Habari. Miswada imekamilika na kusomwa mara ya kwanza hapa Bungeni lakini mchakato wake haukuweza kufika mwisho. Tunawaachia wenzetu wajao washughulike nayo katika Bunge la 11.
Vita dhidi ya Rushwa
Mheshimiwa Spika;
Vita dhidi ya rushwa ni eneo jingine ambalo tulilivalia njuga katika Awamu ya Nne. Tumepata mafanikio ya kutia moyo katika mapambano dhidi ya rushwa ingawaje kazi bado ni kubwa. Tumefanya mambo matatu. Kwanza, tumetunga Sheria Na. 11 ya mwaka 2007 ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa ambayo imeongeza nguvu ya mapambano dhidi ya uovu huu. Idadi ya makosa ya rushwa iliongezwa kutoka 4 mpaka 24 na wigo wa wakosaji pia, kwa kuhusisha watu katika sekta binafsi. Mifumo ya upelelezi na uendeshaji mashitaka nayo imeimarishwa.
Tumeunda chombo kipya TAKUKURU badala ya TAKURU ambacho kimepewa majukumu ya kuzuia na kupambana na rushwa badala ya kuzuia peke yake. TAKUKURU imepewa mamlaka zaidi katika kuongoza mapambano haya. Taasisi imeendelea kuimarishwa kwa kuipatia zana na vifaa vya kufanyia kazi pamoja na rasilimali watu na mahitaji mengine. Tumeiwezesha TAKUKURU kufungua ofisi katika Mikoa na Wilaya zote.
Mheshimiwa Spika;
Maboresho haya yamewezesha idadi ya kesi za tuhuma za rushwa zinazofikishwa mahakamani kuongezeka kutoka kesi 50 mwaka 2005 hadi 1,900 mwaka 2014. Jumla ya shilingi bilioni 87.8 ziliokolewa. Watumishi wa Serikali 97 wameachishwa kazi kwa tuhuma za rushwa na matumizi mabaya ya ofisi zao baada ya ushahidi wa kijinai kukosekana. Kwa upande wa kupambana na rushwa kwenye shughuli za uchaguzi, tumetunga Sheria ya Kudhibiti Gharama za Uchaguzi Na. 6 ya mwaka 2010 ili kutoa majibu ya kilio cha siku nyingi dhidi ya watu wanaotumia fedha kununua kura.
Mapato na Matumizi ya Fedha na Mali za Serikali
Mheshimiwa Spika;
Nilieleza katika hotuba yangu ya Kuzindua Bunge la Tisa tarehe 30 Desemba, 2005 kuwa tutatoa kipaumbele cha juu kwa ukusanyaji wa mapato ya Serikali na nidhamu ya matumizi ya Serikali. Leo miaka kumi baadae ninaona fahari tumepata mafanikio makubwa. Mapato ya Serikali yameongezeka kutoka shilingi bilioni 177.1 mwaka 2005 kwa mwezi hadi takriban shilingi bilioni 850. Hii imewezesha bajeti ya Serikali kukua kutoka trilioni 4.13 mwaka 2005/2006 hadi trilioni 22.49 mwaka 2015/2016. Isitoshe imetuwezesha kupunguza misaada na mikopo ya washirika wa maendeleo kutoka asilimia 42 ya Bajeti ya Serikali mwaka 2005 hadi asilimia 15 mwaka 2014/2015 na tumejipa lengo la kushusha zaidi hadi asilimia 8 mwaka huu wa fedha wa 2015/2016.
Mheshimiwa Spika;
Mafanikio haya yametokana hasa na kazi kubwa tuliyoifanya ya kuimarisha Mamlaka ya Mapato ambao wanastahili pongezi zetu nyingi. Bado naamini tunaweza kufanya vizuri zaidi ya hivi, kama tukiongeza udhibiti kwa mianya ya kupoteza mapato na kuimarisha zaidi TRA na mamlaka nyingine za ukusanyaji mapato ya Serikali. Bado ukusanyaji wa mapato yasiyokuwa ya kodi katika Halmashauri za Wilaya na Miji na katika Wizara, Idara zinazojitegemea na Wakala wa Serikali uko chini ya lengo. Huku kuendelee kufanyiwa kazi.
Mheshimiwa Spika;
Kwa upande wa nidhamu ya matumizi ya fedha na mali za Serikali tulielekeza nguvu zetu katika kuimarisha utaratibu wa manunuzi Serikalini na ukaguzi wa hesabu za Serikali. Kwa upande wa ununuzi wa bidhaa na huduma, tumeendelea kuimarisha Sheria na Mamlaka ya Ununuzi wa Umma ili iweze kuhakikisha kuwa kuna usimamizi thabiti wa sheria hiyo na kanuni zake. Kama mjuavyo sehemu, kubwa ya fedha za Serikali hutumiwa katika ununuzi wa bidhaa na huduma, hivyo kuwepo usimamizi mzuri ni jambo jema. Ukikosekana, wizi na rushwa hutawala.
Mheshimiwa Spika;
Kwa upande wa ukaguzi wa hesabu za Serikali, tumechukua hatua za makusudi za kuimarisha Ofisi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali. Tumetunga Sheria mpya inayoipa nguvu na uhuru zaidi Ofisi hiyo. Aidha, tumewaongezea bajeti, vitendea kazi na rasilimali watu. Ofisi 8 za Mikoa zimejengwa na 2 zinaendelea kujengwa.
Nafurahi kwamba maagizo yangu kwa viongozi na watendaji katika Serikali Kuu na Serikali za Mitaa kuhusu Taarifa ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali kupewa uzito linazingatiwa. Taarifa hizo sasa zinasomwa, zinajadiliwa na hatua kuchukuliwa kwa kasoro zilizoonekana. Kamati ya Bunge ya Hesabu za Serikali imefanya kazi nzuri. Wezi na wabadhirifu wanaobainika kuchukuliwa hatua za kisheria mara makosa yanapogundulika. Kitaifa taarifa hiyo hujadiliwa Bungeni kwa muda wa kutosha.
Mheshimiwa Spika;
Niliamua pia kuanzisha Ofisi ya Mkaguzi Mkuu wa Ndani wa Serikali na kuwaweka Wakaguzi wa Ndani wote wa Serikali Kuu na Serikali za Mitaa chini ya Mamlaka yake na kuwajibika kwake. Ofisi hii imesaidia kuhakikisha sheria na kanuni za matumizi ya fedha na mali ya umma zinaheshimiwa. Pia, katika ufuatiliaji na utekelezaji wa mapendekezo ya CAG. Uimarishaji wa ukaguzi wa ndani na ule wa CAG umesaidia kuboresha hesabu za Serikali kuwa nzuri zaidi siku hizi. Hati safi zimeongezeka na hati chafu zinazidi kupungua Serikalini. Kwa mfano katika Halmashauri za Wilaya na Miji, hati safi zimeongezeka kutoka 56 mwaka 2006 hadi 150 mwaka 2014. Hati zenye mashaka ni 13 na hakuna Hati isiyoridhisha. Kazi ya kuimarisha ukaguzi na nidhamu ya matumizi lazima iendelezwe.
Maadili ya Viongozi wa Umma
Mheshimiwa Spika;
Katika miaka 10 hii tumeimarisha mfumo wa kusimamia maadili ya viongozi. Tumefanya hivyo kwa kutambua kuwa maadili mema ni sifa ya msingi ya kiongozi na huiletea heshima Serikali. Tumeendeleza Kamati ya Maadili na kuunda Baraza la Maadili kwa mujibu wa Sheria ya Maadili ya Viongozi wa Umma namba 13 ya 1995. Tumepanua wigo na kwamba sasa mali za viongozi na familia zao hutolewa taarifa na kiongozi katika Tamko la Mali la kila mwaka. Hii inasaidia kuondoa uwezekano wa kiongozi kuficha mali kwa mgongo wa mwenza wake au mtoto.
Mheshimiwa Spika;
Kamati ya Maadili sasa si tu inapokea fomu na kuzihifadhi, bali inafanya ukaguzi wa mali za viongozi na kuzifuatilia. Kikwazo chao ni kupata rasilimali fedha. Hili litazamwe zaidi. Pale inapoonekana kuna makosa ya kimaadili wahusika hufikishwa kwenye Baraza la Maadili. Sote tumeshuhudia kazi nzuri iliyofanywa na Baraza hilo wakati wa sakata la Escrow. Bado kazi ya kuimarisha Kamati ya Maadili kwa rasilimali fedha, vitendea kazi, majengo ya ofisi na rasilimali watu haina budi kuendelezwa.
Muhimili wa Mahakama
Mheshimiwa Spika;
Katika kipindi cha miaka 10 hii tumefanya jitihada kubwa za kuimarisha mhimili wa Mahakama. Miongoni mwa mambo mengine, tumefanya mambo muhimu kwa madhumuni ya kuongeza ufanisi katika utekelezaji wa jukumu lake la msingi la utoaji haki.
Kwanza, tumetenganisha shughuli za kutoa haki na za utawala. Tumeunda Ofisi ya Mtendaji Mkuu wa Mahakama ya kushughulikia mambo ya fedha na utawala. Hivyo basi, Wasajili wa Mahakama wanabaki na jukumu la kutoa haki. Mpaka sasa mabadiliko haya yamekuwa ya manufaa makubwa kwa Mahakama kwani yameboresha utekelezaji wa majukumu katika Mahakama. Pili, tumeanzisha Mfuko wa Mahakama ambao unaipa Mahakama uhuru katika kuendesha shughuli zake. Sambamba na hilo tumeongeza bajeti ya Mahakama kutoka shilingi bilioni 36.6 mwaka 2006/07 hadi shilingi bilioni 87.6 mwaka 2014/15. Jambo linalohitaji kuboreshwa ni Hazina kutoa fedha kwa wakati ili shughuli zifanyike kama ilivyopangwa.
Mheshimiwa Spika;
Jambo la tatu, ni kwamba tumeongeza idadi ya Majaji wa Rufani, Majaji wa Mahakama Kuu, Mahakimu Wakazi na Mahakimu wa Mahakama za Mwanzo. Lengo letu ni kuongeza nguvukazi ya kusikiliza na kuamua mashauri. Kwa upande wa Mahakimu wa Mahakama za Mwanzo wameanza kuteuliwa watu wenye Shahada ya Sheria. Hivi sasa itawawezesha watu wenye mashauri katika Mahakama hizo kupata utetezi wa Mawakili. Kati ya mwaka 2005 na 2015 tumeongeza Majaji wa Rufani kutoka 8 mwaka 2005 hadi 16, na Majaji wa Mahakama Kuu kutoka 37 hadi 81 katika kipindi hicho. Hali kadhalika, tumeongeza idadi ya Majaji wanawake. Katika Mahakama ya Rufani wapo 5 na katika Mahakama Kuu wapo 32 na kufanya jumla yao kuwa 37. Hivi sasa tunao jumla ya Mahakimu Wakazi 1,266 katika ngazi zote za Mahakama. Kati ya hao 534 sawa na asilimia 35 ni wanawake. Idadi ya Majaji na Mahakimu wanawake hivi sasa ni kubwa kuliko wakati wowote uliopita.
Mheshimiwa Spika;
Kutokana na mipango mizuri iliyowekwa na Jaji Mkuu Mohamed Chande Othman Mahakama zimepiga hatua kubwa katika kupunguza mlundikano wa kesi Mahakamani. Majaji wamejiwekea malengo kwa kila Jaji asikilize na kuamua mashauri yasiyopungua 220 kwa mwaka na kila Hakimu Mkazi mashauri 250 na wale wa Mahakama ya Mwanzo mashauri 260 kwa mwaka. Kwa sababu hiyo, kuanzia Julai, 2014 hadi kufikia mwezi Machi mwaka 2015 yalifunguliwa mashauri 177,586 na Mahakama ilisikiliza na kuamua mashauri 179,962. Maana yake ni kuwa zimesikilizwa zote na nyingine zilizobakia miaka ya nyuma. Bila shaka kwa kasi hii sasa mrundikano wa kesi utabakia kuwa historia katika kipindi kifupi kijacho. Nawapongeza sana Majaji na Mahakimu kwa kazi nzuri waifanyayo.
Kwa upande wa ujenzi wa majengo ya Mahakama Kuu, wamekamilisha ujenzi wa jengo la Mahakama Kuu za Divisheni ya Kazi pamoja na majengo ya Mahakama Kuu Mikoa ya Shinyanga na Kagera. Aidha, majengo mawili ya Mahakama za Wilaya na 12 ya Mahakama za Mwanzo nayo yamekamilika. Hivi sasa, ujenzi unaendelea wa majengo ya Mahakama Kuu 9 za mikoa iliyosalia, Mahakama za Wilaya 9 na za mwanzo 25.
Maboresho ya Mfumo wa Utoaji Haki
Mheshimiwa Spika;
Jambo lingine ambalo tumefanya katika nia ya kuongeza uwajibikaji, ufanisi, na kupunguza malalamiko ya wananchi na ucheleweshaji wa mashauri ni kutenganisha kazi ya upelelezi wa makosa ya jinai na uendeshaji wa mashtaka hayo Mahakamani. Polisi waliokuwa wanafanya yote sasa watashughulikia upelelezi na ofisi ya Mkurugenzi wa Mashtaka ndiyo inayoendesha mashauri. Tayari Ofisi za Mkurugenzi wa Mashtaka zimekwishafunguliwa katika kila Mkoa na sasa tunaenda wilayani. Aidha, tumeboresha Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali kwa rasilimali watu, vitendea kazi na fedha ili kuongeza ufanisi katika utendaji wa ofisi hiyo muhimu sana. Kuna haja ya kuendelea kuongezea rasilimali fedha na vitendea kazi ili ufanisi uongezeke zaidi.
Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora
Mheshimiwa Spika;
Katika kipindi hiki, tumeimarisha Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora kwa kuiwezesha kwa nyenzo, rasilimali fedha na watu. Tume sasa inafanya kazi katika eneo lote la Jamhuri ya Muungano. Aidha, kutokana na utumiaji wa mfumo wa elektroniki malalamiko ya wananchi mengi zaidi yanafikishwa kwenye Tume na mengi yanapatiwa ufumbuzi. Kwa mfano, idadi ya malalamiko yaliyowasilishwa Tume yameongezeka kutoka 9,455 mwaka 2006 hadi 25,921 mwaka 2014 na uwezo wa Tume kushughulikia malalamiko kwa mwaka umeongezeka kutoka malalamiko 3,021 mwaka 2005 hadi malalamiko 18,501 mwaka 2014.
Utendaji Serikalini
Maeneo ya Utawala
Mheshimiwa Spika;
Kwa nia ya kusogeza huduma, mwaka 2010 tulianzisha mikoa mipya 4 ya Geita, Simiyu, Njombe na Katavi na wilaya mpya 19. Pia, tulianzisha Halmashauri 45, kata 1,432, vijiji 1,949, Mitaa 1,379 na vitongoji 8,777. Nimeamua kuanzisha mkoa mpya wa Songwe kutoka mkoa wa Mbeya na Wilaya sita kama ifuatavyo: Tanganyika mkoani Katavi, Kigamboni na Ubungo mkoani Dar es Salaam, Songwe mkoani Mbeya, Kibiti mkoani Pwani na Malinyi mkoani Morogoro. Najua tulikuwa na maombi mengi lakini kwa sasa tufanye haya.
Maslahi ya Wafanyakazi
Mheshimiwa Spika;
Serikali ya Awamu ya Nne imelipa umuhimu wa juu suala la kuboresha maslahi ya watumishi wa Serikali. Karibu kila mwaka tumekuwa tunaongeza kima cha chini cha mshahara. Kwa sababu hiyo, kima cha chini cha mshahara kimeongezeka kutoka shilingi 65,000 mwaka 2005 hadi shilingi 265,000 mwaka wa jana. Mwaka huu tumefikia shilingi 300,000. Najua bado hakikidhi mahitaji lakini ukilinganisha na tulikokuwa kipindi hiki tumeongeza sana mishahara ya wafanyakazi. Vile vile, tumeendelea kupunguza kodi ya mapato kwa mfululizo kutoka asilimia 18 mwaka 2005 hadi asilimia 11 mwaka huu. Dhamira yetu ni kutaka kutoa nafuu zaidi kwa wafanyakazi. Vile vile, tumewapandisha vyeo watumishi 233,876 na kulipa malimbikizo ya watumishi 422,348 ya kiasi cha shilingi bilioni 384.8.
Mheshimiwa Spika;
Tumetekeleza sera ya ugatuaji wa madaraka kwa wilaya jambo ambalo limelazimu kuongeza rasilimali fedha na watu kwa Halmashauri za Wilaya na Miji. Kwa ajili hiyo ruzuku kwa Halmashauri zetu imeongezeka kutoka shilingi bilioni 780 mwaka 2005/2006 hadi shillingi trilioni 4.69 mwaka 2015/2016. Aidha, tumeimarisha utumishi katika Halmashauri kwa kuajiri watumishi wengi wa kada mbalimbali.
Usawa wa kijinsia
Mheshimiwa Spika;
Mwaka 2005 niliahidi wakati wa kampeni na wakati wa kuzindua Bunge la Tisa, kuwa tutaongeza ushiriki wa wanawake katika shughuli na nyanja mbalimbali za maisha ya watu wa nchi yetu ikiwemo nafasi za maamuzi. Ninyi na mimi ni mashahidi kwamba tumetimiza ahadi hiyo. Idadi ya Wabunge wanawake imeongezeka kutoka 62 mwaka 2005 hadi 127. Hivi sasa hamsini kwa hamsini ni rasmi katika Katiba Inayopendekezwa. Kwa mara ya kwanza katika historia ya nchi yetu na Bunge letu tumepata Spika mwanamke Mheshimiwa Anne Semamba Makinda.
Wanawake wameongezeka katika ngazi zote kuu za uamuzi. Kwa mfano, tunao Mawaziri wanawake 10, Naibu Mawaziri wanawake 5, Majaji wanawake 37 na Wakuu wa Wilaya wanawake wako 53. Kwa upande wa Makatibu Wakuu, Naibu Makatibu Wakuu, Wakuu wa Mikoa, Wakurugenzi Watendaji n.k. pia wameongezeka. Katika elimu nako tuna usawa wa kijinsia kwa upande wa idadi ya wanafunzi wa kike na wa kiume katika shule za msingi na sekondari. Katika vyuo vya elimu ya juu, idadi ya wanafunzi wa kike imeongezeka kwa kasi kutoka 10,039 mwaka 2005 hadi 78,800 mwaka 2014.
Hali ya Uchumi
Mheshimiwa Spika;
Wakati ninaingia madarakani mwaka 2005 niliwaahidi Watanzania wenzangu kuwa tutafanya kila tuwezalo kujenga uchumi ulio imara na shirikishi. Hususan, nilisema nitaendeleza sera za mageuzi ya kiuchumi na kuweka misingi madhubuti ya kukuza uchumi, kuongeza ajira, kuongeza Pato la Taifa na kupunguza umaskini. Katika miaka kumi iliyopita tumeendelea kusimamia kwa kiwango kizuri sera za uchumi jumla na sera za uchumi katika ngazi ya chini zinazogusa wananchi wa kawaida.
Jitihada zetu hizo zimezaa matunda ya kutia moyo. Katika kipindi hiki, Pato la Taifa lilikua kwa wastani wa takriban asilimia 7. Nchi yetu ni miongoni mwa mataifa 10 ya Afrika na 20 duniani ambayo uchumi wake unakua kwa kasi kubwa. Pato ghafi la Taifa limeongezeka zaidi ya mara tatu kutoka shilingi trilioni 14.1 mwaka 2005 hadi kufikia trilioni 79.4 mwaka 2014. Hivyo basi, pato la wastani la Mtanzania nalo limeongezeka kutoka shilingi 441,030 mwaka 2005 hadi shilingi 1,724,416 mwaka 2014.
Mheshimiwa Spika;
Mauzo yetu ya nje yameongezeka kutoka Dola za Marekani bilioni 1.67 mwaka 2005 hadi Dola za Marekani bilioni 8.76 mwaka 2014[A1] na kutunisha akiba yetu ya fedha za kigeni na kutuwezesha kuagiza bidhaa na mahitaji ya nchi kutoka nje kwa kipindi cha miezi 4.1 kama tulivyopanga. Mfumuko wa bei ni asilimia 6.1.
Mheshimiwa Spika;
Kama mjuavyo, mwaka 2000 nchi yetu ilijiwekea Dira ya Taifa ya Maendeleo ya hadi mwaka 2025. Mwaka 2010 tulitengeneza Mpango wa Muda Mrefu (Long Term Perspective Plan) wa (2010 – 2025) wa kuongoza utekelezaji wa Dira kwa miaka 15 iliyobaki. Tuligawa utekelezaji wake katika Mipango mitatu ya Maendeleo ya Miaka Mitano kila mmoja. Tuko katika hatua za mwisho za utekelezaji wa Mpango wa Kwanza, (2011/12 – 2015/16) na kuandaa mpango wa pili (2016/17 – 2021/22).
Mpango wa Matokeo Makubwa Sasa
Mheshimiwa Spika;
Kwa madhumuni ya kuboresha utendaji wa Serikali nilianzisha Mpango wa Matokeo Makubwa Sasa (BRN). Huu ni mfumo mpya wa kupanga, kufuatilia na kusimamia utekelezaji wa malengo na shughuli za Serikali kwa nia ya kuhakikisha kuwa kilichokusudiwa kinafanyika, tena kwa wakati. Tuliamua kuanza na sekta sita za Elimu, Nishati, Kilimo, Uchukuzi, Maji na Mapato ya Serikali. Baadae sekta ya afya na uboreshaji mazingira ya uwekezaji ziliongezwa.
Katika kipindi hiki kifupi Mpango umethibitisha kuwa wenye manufaa. Mambo katika sekta zilizojumuishwa katika BRN yameanza kwenda vizuri. Changamoto yetu kubwa imekuwa ni upatikanaji wa fedha zinazohitajika kwa wakati kutoka Hazina. Kama changamoto hiyo isingekuwepo mambo yangekuwa mazuri zaidi.
Uboreshaji wa Mazingira ya Biashara na Uwekezaji
Mheshimiwa Spika;
Kwa kutambua umuhimu wa uwekezaji katika kukuza uchumi, kuzalisha ajira, kuongeza mapato na kupunguza umaskini, Serikali yetu imekuwa inachukua hatua thabiti za kutengeneza mazingira mazuri ya kuwavutia wawekezaji wa ndani na nje kuchagua Tanzania kuwa nchi inayofaa kuwekeza.
Mwaka 2010 tumetengeneza Sera na kutunga Sheria ya Ubia baina ya Sekta ya Umma na Sekta Binafsi (Public Private Partnership—PPP). Lengo letu ni kuweka mazingira mazuri kwa sekta binafsi kuvutika kushirikiana na Serikali katika shughuli za kiuchumi na maendeleo. Faida kubwa ya utaratibu huu ni kuipunguzia Serikali mzigo wa kuwekeza katika baadhi ya shughuli ambazo sekta binafsi inaweza kubeba sehemu ya gharama. Hii siyo tu inaongeza kasi ya maendeleo, bali kuiwezesha Serikali kuokoa fedha ambazo inaweza kuzitumia kwa shughuli nyingine.
Juhudi zetu za kuboresha mazingira ya uwekezaji zinaendelea kuzaa matunda mema. Kati ya 2005 na 2014, Kituo chetu cha Uwekezaji (TIC) kimesajili miradi 7,159 yenye thamani ya Dola za Marekani bilioni 154.274. Kati ya miradi hiyo asilimia 49.38 ni ya wawekezaji wa ndani, asilimia 23.41 ni wawekezaji wa kutoka nje na asilimia 27.18 ni miradi ya ubia baina ya Watanzania na wawekezaji wa kigeni. Ajira 16,000 zilipatikana. Ukuaji huu wa uwekezaji umeongeza mapato ya Serikali.
Kwa mujibu wa taarifa ya uwekezaji iliyotolewa na Shirika la Umoja wa Mataifa la Viwanda na Biashara Duniani (UNCTAD) ya mwaka 2015, Tanzania inaongoza Afrika Mashariki kwa kuvutia uwekezaji. Ilipata Dola za Marekani bilioni 2.142 sawa na asilimia 31.5 ya uwekezaji wote katika Jumuiya yetu.
Sekta za Uzalishaji
Sekta ya Kilimo
Mheshimiwa Spika;
Kuendeleza kilimo ilikuwa ni moja ya mambo tuliyoyapa kipaumbele cha juu. Shabaha yetu kuu ni kutaka kuongeza tija ili uzalishaji uongezeke, wakulima wapate mavuno mengi, masoko ya uhakika yawepo na bei iwe nzuri ili mapato yao yaongezeke na umasikini uwapungukie. Vile vile wao na taifa lijitosheleze kwa chakula.
Kwa ajili hiyo mwaka 2006 tuliasisi Programu ya miaka 7 ya Maendeleo ya Sekta ya Kilimo (Agricultural Sector Development Programme—ASDP). Katika Programu hiyo, matatizo yanayofanya tija na uzalishaji katika kilimo kuwa mdogo yalitambuliwa na kutengenezewa mpango wa kuyatatua. Serikali pia ilianzisha mikakati, programu na mipango mingine ya kuongeza msukumo katika kuleta mageuzi ya kilimo. Miongoni mwa hiyo ni mkakati wa Kilimo Kwanza, Mpango wa Kuendeleza Kilimo katika Ukanda wa Kusini mwa Tanzania (SAGCOT), Mpango wa Uwekezaji katika Sekta ya Kilimo (TAFSIP), Sera ya Umwagiliaji tuliyoitunga mwaka 2010 na Programu ya Mageuzi na Modenaizesheni ya Ushirika.
Mheshimiwa Spika;
Pamoja na hayo, tumeongeza pia bajeti ya sekta ya kilimo kutoka shilingi bilioni 233.3 mwaka 2005/06 hadi shilingi bilioni 1,084.7 mwaka 2014/15. Kuongezwa kwa bajeti kumewezesha fedha za ruzuku ya mbolea na pembejeo kuongezeka kutoka shilingi bilioni 7.5 mwaka 2005/06 hadi shilingi bilioni 299.3 mwaka 2013/14. Matrekta makubwa na madogo yameongezeka kutoka 7,491 mwaka 2005 hadi 16,412 mwaka 2014. Kwa sababu hiyo matumizi ya jembe la mkono yamepungua kutoka asilimia 70 hadi asilimia 62. Tumeongeza maafisa ugani kutoka 3,379 mwaka 2005 hadi 7,974 mwaka 2014.
Vituo vya utafiti wa kilimo tumeviongezea rasilimali fedha, watu na vitendea kazi. Aidha, tumeanza safari ya kufufua mashamba ya mbegu ya Serikali na kuhusisha sekta binafsi, Jeshi la Magereza na Jeshi la Kujenga Taifa katika kuzalisha mbegu. Aidha, tumeimarisha Wakala wa Mbegu (Agricultural Seed Agency – ASA) na kuongeza uzalishaji wa mbegu bora kutoka tani 10,477.17 mwaka 2005 hadi tani 32,340 mwaka 2014.
Mheshimiwa Spika;
Juhudi za Serikali kuendeleza kilimo zimezaa matunda mazuri. Tija katika uzalishaji wa mazao ya biashara na chakula imeongezeka. Kwa upande wa mazao ya chakula uzalishaji umeongezeka kutoka tani milioni 9.66 mwaka 2005 hadi tani milioni 16.01 mwaka 2014. Ongezeko hili limeliwezesha taifa letu kujitosheleza kwa chakula kwa asilimia 125 mwaka 2014 ikilinganishwa na asilimia 95 mwaka 2005. Uzalishaji wa mazao ya asili ya biashara umeongezeka toka tani 427,738 mwaka 2005 hadi tani 569,054 mwaka 2014 na uzalishaji wa mbegu za mafuta umeongezeka karibu ya mara 4 toka tani 1,389.9 mwaka 2005 hadi tani 5,545.6 mwaka 2014. Aidha, uzalishaji wa matunda nao umeongezeka toka tani milioni 1.2 mwaka 2005 hadi tani milioni 4.4 mwaka 2014 na maua toka tani 5,862 hadi tani 10,790.
Mheshimiwa Spika;
Upatikanaji wa masoko ya uhakika na bei nzuri kwa mazao ya wakulima bado ni changamoto. Pia kuna tatizo la upungufu wa maghala ya kuhifadhi mazao. Jitihada zinaendelea kupata mkopo au wabia wa kujenga maghala ya kisasa nchi nzima. Programu ya Mageuzi na Modenaizesheni ya Ushiriki ilianzishwa ili kutatua tatizo la masoko. Aidha, tumeanza maandalizi ya kuanzisha soko la bidhaa (Commodity Market Exchange) kwa nia hiyo hiyo. Naamini misingi mizuri tuliyoijenga pamoja na kuenea kwa SACCOS na kuanza kwa Benki ya Kilimo ikiendelezwa itatoa mchango mkubwa katika kuongeza kasi ya mapinduzi ya kilimo.
Mifugo
Mheshimiwa Spika;
Kwa upande wa mifugo, dhamira yetu ilikuwa kuanza safari ya kuleta mageuzi katika sekta hii. Safari hiyo tumeianza kupitia Programu ya Kuendeleza Sekta ya Mifugo. Changamoto zinazochangia maendeleo duni ya sekta hii zimeainishwa na kutengenezewa mkakati wa utekelezaji. Katika kipindi hiki malambo 1,008, majosho 2,364 na maabara 104 za mifugo zimejengwa. Visima virefu 101 vimechimbwa, malambo 370 na majosho 499 yamekarabatiwa katika kipindi hiki cha miaka 10.
Ukarabati na ujenzi wa majosho umeongeza idadi kutoka 2,177 mwaka 2006 hadi 3,637 mwaka 2015. Tumeongeza Maofisa Ugani kutoka 2,270 mwaka 2005 hadi 6,041 mwaka 2014. Kuhusu uhamilishaji, tumeongeza vituo kutoka kituo 1 mwaka 2005 hadi vituo 8 mwaka 2015 na kuwezesha ng’ombe 955,360 kuhamilishwa katika miaka 10 hii.
Mheshimiwa Spika;
Mazingira mazuri ya uwekezaji kwa sekta binafsi tuliyoyajenga yamewezesha viwanda vya kusindika nyama, maziwa na vyakula vya mifugo kuongezeka. Viwanda vya kusindika maziwa vimeongezeka kutoka 22 mwaka 2005 hadi 74 mwaka 2015. Viwanda vya kuzalisha vyakula vya mifugo vimeongezeka kutoka viwanda 6 mwaka 2005 hadi 80 mwaka 2015 vikiwa na uwezo wa kusindika tani milioni 1.4 za vyakula hivyo kwa mwaka. Aidha viwanda na machinjio ya kisasa 9 vimejengwa katika kipindi hiki. Usindikaji wa ngozi pia umeongezeka kutoka vipande 790,000 mwaka 2005 hadi vipande milioni 3.78 mwaka 2014. Hivi sasa kwa mfano, uzalishaji wa malisho ya mifugo (hei) umefikia marobota 957,860 ikilinganishwa na marobota 178,100 mwaka 2005.
Safari yetu ya kuanza kuondoka kwenye uchungaji kwenda kwenye ufugaji imeanza. Vijiji vingi vimeandaa mipango ya matumizi bora ya ardhi na hivyo vimetenga maeneo ya kilimo na ya ufugaji. Tuendelee kuhimiza vijiji vyetu kutekeleza mipango hiyo ili wafugaji wapate maeneo ya malisho mbali na mazao ya wakulima. Pia, tuhimize uhamilishaji kama mlango wa kuingilia kwenye kuboresha kosafu za mifugo yetu.
Uvuvi
Mheshimiwa Spika;
Wakati nazindua Bunge la Tisa tarehe 30 Desemba 2005 nilisema kuwa Serikali ya Awamu ya Nne itatoa kipaumbele kwenye kuendeleza sekta ya uvuvi. Katika kutekeleza hayo tumefanya yafuatayo. Kwanza, nimeunda Wizara mpya ya Mifugo na Uvuvi. Pili, tulifuta kodi ya zana za uvuvi ili kuwawezesha wavuvi kupata zana bora na za kisasa kwa bei nafuu zaidi. Tatu, tumeimarisha vyuo vya uvuvi na hivi sasa vina uwezo wa kudahili wanafunzi 1,215 ikilinganishwa na wanafunzi 127 mwaka 2005. Hii imetuwezesha kuongeza wagani wa uvuvi kutoka 103 mwaka 2005 hadi 540 mwaka 2014. Nne, tumeongeza sana juhudi za kupambana na uvuvi haramu ili kutunza mazingira, mazalia ya samaki na kuzuia kuvuliwa au kuuawa kwa samaki wadogo.
Tumeimarisha maabara ya Taifa ya Samaki pale Nyegezi kwa vifaa vya kisasa na wataalamu ili iende na wakati. Tano, tumeongeza msukumo wa kuhimiza ufugaji wa samaki na kuwezesha mashamba ya samaki kuongezeka kutoka 13, 011 mwaka 2005 hadi 20, 325 mwaka 2014.
Uvuvi haramu unapungua. Mapato ya sekta ya uvuvi yameongezeka kutoka shilingi bilioni 351.6 mwaka 2005 hadi shilingi trilioni 1.8 mwaka 2013. Bado tuna kazi kubwa ya kufanya katika sekta hii ili kuongeza tija na mapato ya wavuvi na taifa.
Utalii
Mheshimiwa Spika;
Kwa upande wa utalii, tumeendelea na jitihada za kuiendeleza sekta hii muhimu. Tumeongeza kutangaza vivutio vya utalii vya nchi yetu katika masoko makubwa duniani. Sekta ya utalii imekua kwa wastani wa asilimia 7.1 na imechangia asilimia 25 ya mapato ya fedha za kigeni. Idadi ya watalii imeongezeka kutoka watalii 612, 754 mwaka 2005 hadi watalii 1,140,156 mwaka 2014. Idadi ya vitanda katika mahoteli imeongezeka kutoka 15,828 hadi 21,929. Mapato pia yameongezeka kutoka Dola za Marekani milioni 823.05 mwaka 2005 hadi Dola za Marekani bilioni 2 mwaka 2014. Ajira za moja kwa moja zimeongezeka kutoka 32,673 hadi 686,130 na zisizokuwa za moja kwa moja kutoka 165,883 hadi 1,318,109. Haya ni mafanikio makubwa na ya kujivunia.
Mheshimiwa Spika;
Katika kipindi hiki tumekabiliana na tukio kubwa la ujangili wa wanyamapori hasa wa ndovu kutokana na kushamiri kwa biashara ya meno ya ndovu na bei kuwa kubwa katika nchi za Mashariki ya Mbali. Vuguvugu la ujangili lilifikia kiwango cha kutishia kumaliza ndovu nchini na dunia nzima. Tukaamua kuchukua hatua za kuidhibiti hali hiyo. Tumefanya operesheni tatu kukabiliana na tishio hili. Ya kwanza, iliendeshwa na Idara ya Wanyamapori na Misitu wakishirikiana na TANAPA na Ngorongoro Conservation Area. Hii hasa ilihusu kupambana na ujangili katika hifadhi na mapori ya Kaskazini mwa Tanzania. Mafanikio makubwa yalipatikana.
Mheshimiwa Spika;
Operesheni ya pili ni ile iliyohusisha Jeshi la Polisi katika hifadhi na sehemu nyingine za Tanzania. Operesheni Kipepeo kama ilivyoitwa nayo ilipata mafanikio. Na ya tatu, Operesheni Tokomeza iliyohusisha vyombo vyote vya ulinzi na usalama. Pamoja na changamoto zake operesheni hizi zimesaidia sana kupunguza kasi ya ujangili nchini. Matokeo yake katika sensa ya ndovu iliyofanyika mara ya mwisho, ukiacha Ruaha, hali katika hifadhi na mapori mengine ina muelekeo mzuri.
Kuundwa kwa Mamlaka ya Wanyamapori (TAWA) yenye mamlaka makubwa zaidi ya kusimamia sekta ya wanyamapori nako kutaimarisha uhifadhi na mapambano ya ujangili. Kwa mipango na program zilizopo Wizarani, naamini mambo yatakuwa mazuri zaidi muda si mrefu.
Viwanda
Mheshimiwa Spika;
Katika miaka kumi hii, sekta ya viwanda imeendelea kukua kwa kasi nzuri ya kutia moyo. Viwanda vikubwa, vya kati na vidogo vimeongezeka kutoka 11, 544 mwaka 2005 hadi viwanda 51,224 mwaka 2015. Kati ya mwaka 2005 na 2014 na miradi 751 imepewa leseni za kudumu na BRELA ya kuanzisha viwanda. Mchango wa sekta ya viwanda katika Pato la Taifa umefikia asilimia 7.3 mwaka 2014 kutoka asilimia 6.8 mwaka 2005. Mchango wa viwanda kwenye mauzo ya nje umeongezeka kutoka asilimia 9.3 mwaka 2005 hadi asilimia 23.3 mwaka 2014.
Tunategemea ukuaji mkubwa wa viwanda katika Mpango wa Pili wa maendeleo wa miaka 5 kutokana na misingi imara tuliyoijenga katika Mpango wa Kwanza. Ujenzi wa kiwanda cha chuma kule Liganga na makaa ya mawe cha Mchuchuma, unatarajiwa kuanza mwaka huu na kiwanda cha kuchakata gesi pale Lindi unatarajiwa kuanza baada ya taratibu za kuwapatia ardhi zitakapokamilika. Hivi ni viwanda vya msingi na mama ambavyo vitachochea kasi ya ukuaji wa viwanda nchini na uchumi kwa jumla.
Madini
Mheshimiwa Spika;
Sekta ya Madini ndiyo ya pili baada ya utalii kwa kuingiza fedha nyingi za kigeni. Kama nilivyoahidi, tulipitia upya sera, sheria na mikataba ya madini iliyokuwepo na kutengeneza sera na sheria mpya. Halikadhalika, tulianzisha mazungumzo na baadhi ya makampuni ambayo hatimaye yalizaa marekebisho ya mikataba yao na hivyo kuboresha maslahi ya taifa.
Kufuatia marekebisho hayo, makampuni husika ya madini yanalipa kodi ya mapato. Bila ya hivyo huenda mpaka leo yangekuwa hayajaanza kulipa kodi. Kutumika kwa Sheria mpya ya Madini, viwango vipya vya mrahaba na kupunguzwa kwa misamaha ya kodi vimeongeza mapato ya Serikali. Aidha, tuliunda Wakala wa Ukaguzi wa Madini Tanzania (TMAA) ambao umewezesha kukagua mahesabu ya migodi kuhusu uwekezaji na mauzo ya madini na kuwawezesha TRA kutoza kodi stahiki kutoka kwa makampuni hayo.
Mheshimiwa Spika;
Mabadiliko haya pamoja na kuongezeka kwa uwekezaji katika sekta hii yamewezesha mchango wa sekta ya madini katika Pato la Taifa kuongezeka kutoka asilimia 2.9 mwaka 2005 hadi kufikia asilimia 3.5 mwaka 2014. Thamani ya mauzo ya madini nje ya nchi pia imeongezeka kutoka Dola za Marekani milioni 655.5 mwaka 2005 hadi kufikia Dola za Marekani bilioni 1.794 mwezi Desemba 2014. Mambo yangekuwa mazuri zaidi kama bei ya dhahabu isingeshuka katika kipindi hiki.
Mheshimiwa Spika;
Serikali ilifanya uamuzi wa kulifufua na kuliwezesha Shirika letu la Madini (STAMICO) kuanza tena kazi ya utafutaji na uchimbaji wa madini kupitia kampuni zake tanzu. STAMICO kwa kupitia kampuni yake ya STAMIGOLD imeanza kuzalisha dhahabu na kuuza nje. Vilevile, tumejiunga na Mpango wa Uwazi wa Uvunaji wa Maliasili (EITI) ambao umesaidia sana katika kuongeza uwazi katika biashara ya madini na kusaidia katika ukusanyaji wa mapato kutoka kwenye makampuni ya madini.
Katika kipindi hiki, migodi mitatu mipya ilianzishwa nayo ni Migodi ya dhahabu wa Buzwagi (Shinyanga) na New Luika (Mbeya) na mgodi wa makaa ya mawe wa Ngaka (Ruvuma). Aidha, miradi mikubwa mingine 8 imeendelezwa na kufikia hatua ya kuanzisha mgodi ukiwemo Mradi wa Urani wa Mkuju (Ruvuma), Mradi wa Chuma Liganga na Mradi wa Makaa ya Mawe wa Mchuchuma (Njombe). Pia, ajira rasmi kwenye migodi mikubwa nchini imeongezeka kutoka waajiriwa 3,517 mwaka 2005 hadi waajiriwa 15,000 mwaka 2014. Hali kadhalika, makampuni ya madini yameongeza unununzi wa bidhaa na huduma hapa nchini (local procurement) kutoka Dola za Marekani milioni 230.41 mwaka 2005 hadi Dola za Marekani milioni 536.56 mwaka 2014.
Mheshimiwa Spika;
Katika kipindi hiki pia, tumetenga maeneo 8 kwa ajili ya wachimbaji wadogowadogo. Maeneo haya yamewezesha wachimbaji wadogo kuchimba madini bila bughudha. Aidha, Wizara imenunua mitambo miwili kwa ajili ya uchorongaji wa miamba kusaidia utafiti wa madini kwa ajili ya wachimbaji wadogo. Tumeanzisha mfuko wa kuwakopesha wachimbaji wadogo pale Wizarani ili kutoa fursa kwa wachimbaji wadogo kupata mikopo ya kuendeleza shughuli zao.
Nishati
Mheshimiwa Spika;
Wakati naanza kazi ya uongozi wa nchi yetu, Tanzania ilikuwa inakabiliwa na ukame mkubwa uliosababisha upungufu mkubwa wa chakula. Pia kulikuwa na upungufu mkubwa wa umeme kwa sababu ya mabwawa ya kuzalisha umeme kukosa maji ya kutosha. Serikali ililazimika kulisha watu zaidi ya milioni 3,776,000 na kukodisha mitambo ya kuzalisha umeme. Kwa siku za usoni tuliamua kuchukua hatua thabiti ya kuongeza uzalishaji wa umeme kwa kutumia gesi asilia na vyanzo vingine kama vile makaa ya mawe, mionzi ya jua na upepo.
Ujenzi umekamilika wa bomba la kusafirisha gesi kutoka Mtwara na Songo Songo litakaloongeza kiasi cha gesi kuja Dar es Salaam na kuwezesha uzalishaji wa megawati 3000 za umeme. Wakati huo huo kazi ya kujenga vituo vya kufua umeme inaendelea pale Kinyerezi, Dar es Salaam. Umeme huo utakidhi mahitaji ya umeme sasa na miaka kadhaa ijayo.
Mheshimiwa Spika;
Katika kipindi hiki tuliunda Wakala wa Umeme Vijijini (REA) ambao wamefanya kazi kubwa na nzuri ya kusambaza umeme kwa vijiji 5,336 kati ya vijiji 12,423 nchini. Kazi kubwa iliyofanyika vijijini inapochanganywa na ile ya mijini imeongeza idadi ya Watanzania wanaopata umeme kutoka asilimia 10 hadi asilimia 40 mwaka 2015. Uamuzi uliofanywa katika Bajeti ya mwaka huu wa kukusanya fedha kwa ajili ya umeme vijijini kupitia mafuta ya petroli, utasaidia sana kuongeza kasi ya kusambaza umeme vijijini.
Gesi Asilia
Mheshimiwa Spika;
Tumepata mafanikio katika utafutaji wa mafuta na gesi asilia. Kuanzia mwaka 2010 nchi yetu imepata bahati ya ugunduzi wa kiasi kikubwa cha gesi bahari kuu. Mpaka sasa zimegundulika futi za ujazo trilioni 47.08. Ukijumlisha na futi za ujazo trilioni 8 zilizogunduliwa takriban miaka 40 iliyopita kule Songo Songo na Msimbati jumla ya rasilimali ya gesi asilia nchini ni futi za ujazo trilioni 55.08. Kazi ya utafutaji inaendelea na wataalamu wanasema kuwa Tanzania inaweza kuwa na akiba ya futi za ujazo trilioni 200. Kiasi cha gesi kilichogunduliwa mpaka sasa ni kikubwa na kufanya Tanzania kuwa mahala papya pa kuipatia dunia nishati hii.
Gesi asilia tuliyonayo ikisimamiwa na kutumiwa vizuri itaiwezesha nchi yetu na watu wake kupata maendeleo makubwa na kuondokana na umaskini. Ni fursa ya aina yake ya kuipatia Serikali mapato makubwa na kuiwezesha kutimiza kwa uhakika majukumu yake na mipango yake. Lakini, ili hayo yaweze kufanyika hapana budi pawepo usimamizi mzuri wa hatua zote muhimu za mnyororo wa thamani: yaani utafutaji, uchimbaji, usafirishaji, uuzaji wa gesi asilia na matumizi yake nchini kama nishati na mali ghafi ya viwanda upande mmoja. Upande mwingine inategemea sana matumizi mazuri ya mapato yatokanayo na rasilimali hiyo.
Mheshimiwa Spika;
Ni kutokana na kutaka kuhakikisha kwamba mambo yanakuwa hivyo ndiyo maana tumetunga Sera ya Gesi Asilia na kuwasilisha katika Bunge hili ile Miswada miwili yaani wa Sheria ya Petroli na ule wa Matumizi ya Mapato ya Mafuta na Gesi. Nawashukuru Waheshimiwa Wabunge kwa kuipitisha Miswada hii nami nitaitia saini mara nitakapoletewa.
Usafirishaji na Uchukuzi
Barabara
Mheshimiwa Spika;
Serikali ya Awamu ya Nne, imetoa kipaumbele cha juu kwa uendelezaji wa miundombinu ya usafirishaji na uchukuzi nchini. Hii ni pamoja na barabara, reli, bandari, usafiri wa majini na usafiri wa angani. Tumeendeleza kazi ya kuongeza mtandao wa barabara za lami nchini kwa mafanikio makubwa. Karibu barabara kuu zote nchini na zile zinazounganisha mikoa zimekamilika kujengwa au kazi ya ujenzi inaendelea. Kwa sababu hiyo hivi leo kutokea po pote nchini kwenda Dar es salaam unafika siku hiyo hiyo, tofauti na ilivyokuwa zamani watu walichukua zaidi ya siku moja. Adha ya kupita Kenya na Uganda kwa watu wa Mikoa ya Ziwa tumeimaliza.
Katika mkakati wetu wa kupanua mtandao wa barabara za lami nchini, tulitambua barabara za urefu wa kilomita 11,474 za kujengwa kwa kiwango cha lami. Baadae tuliongeza barabara nyingine na kufikisha kilomita 17,742 katika mpango huo. Utekelezaji wake upo katika hatua mbalimbali. Tayari ujenzi wa kilomita 5,568 kwa upande wa barabara kuu na kilomita 535 kwa barabara za mijini umekamilika. Ujenzi wa kilomita 3,873 unaendelea. Upembuzi yakinifu na usanifu umekamilika kwa barabara za urefu wa kilometa 4,965 kinachosubiriwa ni kupatikana fedha ujenzi uanze. Baadhi ya barabara hizo zimo katika bajeti ya mwaka huu wa fedha. Barabara za urefu wa kilometa 3,336 zinafanyiwa upembuzi yakinifu na usanifu wa kina.
Mheshimiwa Spika;
Katika kipindi hiki pia, madaraja madogo 7,200 na makubwa 12 yamejengwa na mengine 16 yapo katika hatua mbalimbali za ujenzi. Miongoni mwa madaraja makubwa yaliyokamilika ni daraja la Mto Malagalasi na yanayojengwa ni daraja la Kigamboni na lile la Mto Kilombero. Madaraja haya yalikuwa miongoni mwa matano yaliyopangwa kujengwa katika Mpango wa Kwanza wa Maendeleo wa Miaka Mitano mara baada ya uhuru. Madaraja mawili yaani la Kirumi lilijengwa mwaka 1985 na la Rufiji mwaka 2003. Kwa upande wa vivuko, tumeongeza vipya 15 na kufikisha idadi ya 28 kote nchini mwaka 2014.
Mheshimiwa Spika;
Tumeongeza sana fedha katika mfuko wa barabara kutoka shilingi bilioni 73.08 mwaka 2005/06 hadi shilingi bilioni 866.63 mwaka 2015/16. Hii itasaidia katika matengenezo ya barabara za lami tulizojenga na kujenga nyingine mijini. Hali kadhalika itatumika kuimarisha barabara za udongo na changarawe wilayani na vijijini ziweze kupitika wakati wote. Katika kipindi hiki barabara za changarawe zimeongezeka kutoka kilometa 9,424 hadi kilometa 22,089.
Mheshimiwa Spika;
Katika miaka kumi hii idadi ya vyombo vya moto yaani magari, bajaji na pikipiki imeongezeka kutoka 1,696,088 mwaka 2005 hadi 3,313,254 hivi sasa. Ongezeko hili linalotokana na hali ya kiuchumi ya watu wengi kuwa nzuri limezua tatizo la msongam

- Jul 05, 2015
HOTUBA YA RAIS WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA, MHESHIMIWA JAKAYA MRISHO KIKWETE, KATIKA IBADA YA MAADHIMISHO YA JUBILEE YA MIAKA 125 YA INJILI YA KKKT DAYOS...
Soma zaidiHotuba
Mheshimiwa Baba Askofu, Dkt. Stephen Munga, Mkuu wa KKKT Dayosisi ya Kaskazini Mashariki;
Waheshimiwa Maaskofu;
Mheshimiwa Mkuu wa Mkoa wa Tanga, Magalula Said Magalula;
Waheshimiwa Wageni Wote Toka Ndani na Nje ya Tanzania;
Waheshimiwa Wana-Dayosisi na Wananchi Wote Mliopo Hapa;
Mabibi na Mabwana;
Bwana Yesu Asifiwe:
Nakushukuru sana Baba Askofu Stephen Munga kwa kunialika na kunishirikisha kwenye ibada hii ya kihistoria ya Maadhimisho ya Miaka 125 ya Injili katika Dayosisi ya Kaskazini Mashariki ya Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania. Kwa kweli ni jambo la furaha na heshima kubwa kwangu kujumuika na Maaskofu na waumini wa Kanisa hili kwa tukio hili kubwa na la kihistoria. Mwaliko wenu huu kwangu ni uthibitisho wa uhusiano mzuri uliopo baina ya KKKT na Serikali nchini. Uhusiano ambao umekuwa na manufaa makubwa kwa nchi yetu na watu wake. Uhusiano ambao umejitafsiri katika umoja, upendo, amani, na mshikamano uliopo baina ya Watanzania wa rangi zote, dini zote, makabila yote na wa popote watokako na walipo.
Maadhimisho ya Miaka 125
Mheshimiwa Baba Askofu,
Waumini Wote na Wageni Waalikwa;
Siku kama ya leo, miaka 125 iliyopita ndio siku ambayo Wamisionari wa Kijerumani wa Bethel wapoliwasili mahala hapa. Kwa maelezo yako, walipachagua hapa kuwa ni mahala pa kuwahifadhi vijana waliokombolewa kutoka utumwani. Hivyo mahala hapa paliwapa uhuru, na matumaini mapya watu ambao walikwishakata tamaa. Aidha, kutokea hapa, ndipo kazi ya injili ilipoenea na kusambaa mkoani Tanga. Kusimama na wanyonge, kuwafuta machozi na kuwatua mzigo wao, ni jambo la heri, ni jambo jema na ni jambo linalompendeza Mungu. Na huo ndiyo msingi imara wa Kanisa hili.
Huo pia ndiyo msingi ambao juu yake imejengeka kazi na wajibu wa Serikali. Sisi katika Serikali tunao wajibu wa kuwaondolea wananchi unyonge, kuwapunguzi umaskini, kuwalinda na kuwakinga dhidi ya dhuluma na uonevu na kuwajengea msingi bora wa maendeleo yao. Jitihada zetu za kuondoa umasikini, kutoa fursa za elimu, kuboresha huduma za afya na mambo mengi mengineyo tufanyayo yana malengo hayo. Jitihada za Serikali zinapounganika na zile za madhehebu ya dini tunatengeza nguvu kubwa ya kuwaondolea wananchi wetu siyo tu unyonge wa kiroho, bali pia kuwapunguzia changamoto za maendeleo zinazowakabili na kusaidia kuinua hali zao za maisha.
Mchango wa Dayosisi ya Kaskazini Mashariki
Waheshimiwa Maaskofu, Ndugu Wananchi;
Ninaposema hivyo, natambua mchango wa Dayosisi ya Kaskazini Mashariki katika kuwaletea maendeleo jamii na watu wa Mkoa wa Tanga. Mimi ni shahidi, maana nilifika kule Magamba, Lushoto mwaka jana kufungua ukumbi wa kisasa katika Chuo Kikuu cha Sebastian Kolowa (SEKOMU) kilichojengwa na Dayosisi hii. Pamoja na Chuo Kikuu, natambua mnazo shule za sekondari za Lwandai, Bangala na Dinari. Dayosisi hii inatoa pia huduma za kipekee ambazo hazipatikani kwa urahisi hapa nchini. Ninyi mna shule ya wasioona ya Irente, shule ya msingi ya watoto wenye ulemavu wa ubongo (Autism) na kituo cha kutunza wagonjwa wa akili cha Lutindi.
Kwa upande wa Afya nako mmefanya mambo makubwa. Tunawashukuru kwa hospitali teule ya Wilaya ya Kilindi (Kilindi CDH) ambayo nilishiriki kuweka jiwe la msingi na kuizindua. Aidha nawapongeza kwa Hospitali yenu ya Bumbuli kuwa Hospitali Teule ya Halmashauri ya Bumbuli. Hatua hiyo itaimarisha pia Chuo cha Waganga Wasaidizi (Clinical Officers Taining College) cha Bumbuli.
Napenda pia kupitia sherehe hii kuwashukuru ninyi wa Dayosisi ya Kaskazini Mashariki ya Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania kwa kazi yenu nzuri muifanyayo. Vile vile, nawashukuru sana kwa kuiunga mkono Serikali katika jitihada za kuwaletea maendeleo Watanzania. Nawaomba muendelee na moyo huo mwema. Namuomba Mwenyezi Mungu awaongezee pale mlipopunguza na kuendelea kuwashushia baraka tele.
Mheshimiwa Baba Askofu,
Serikali inatambua na kuthamini sana ushirikiano baina yake na madhehebu na mashirika ya dini. Ndiyo maana tumekuwa tunatengeneza mazingira mazuri kwa mashirika ya dini kuendesha shughuli zake. Tumekuwa tunatoa msamaha wa kodi, tunatoa mikopo kwa wanafunzi wa Vyuo Vikuu vyenu na kutoa ruzuku kwa ajili ya uendeshaji wa zahanati, vituo cha afya na hospitali ambazo Serikali inaingia ubia na Kanisa katika kutoa huduma kwa wananchi. Aghalabu hata pale ambapo Serikali hujenga zake utaratibu huo huachwa kuendelea. Nimetaja baadhi tu ya mambo ambayo tumekuwa tukishirikiana na kusaidiana.
Napenda kutumia nafasi hii kuwahakikishia kuwa tumekuwa tunafanya hivyo na tutaendelea kufanya hivyo kwa kutambua kuwa huduma za kijamii zitolewazo na mashirika ya dini zinawanufaisha Watanzania wote bila ubaguzi.
Maadili ya Jamii
Mheshimiwa Baba Askofu;
Ndugu Waumini na Wageni Waalikwa;
Napenda kutumia nafasi hii kuwaomba viongozi wa dini kuongeza maradufu kazi ya malezi ya jamii kimaadili. Sote ni mashahidi kuwa kuna mmomonyoko mkubwa wa maadili. Nadhani tumefika njia panda tusipofanikiwa kugeuza mwelekeo huu na kuchukua njia hiyo nyoofu tutaharibikiwa zaidi. Maadili mema ya jamii pamoja na mila na desturi zetu vinapita katika mtihani mkubwa sana hivi sasa. Vitendo vya utovu wa maadili vinaendelea kufanyika na kuchukua nafasi kubwa katika maisha ya watu siku hizi. Inaanza kutaka kujengeka dhana potofu ati kuwa ni mambo ya kawaida au ndiyo usasa. Hali hii haistahili kuachwa kuendelea kumong’onyoa misingi ya uadilifu ya jamii zetu na ya ubinadamu wetu.
Viongozi wa dini mnalo jukumu zito na nafasi maalum kwenye hili: kubwa ya kukemea na kurekebisha jamii mkianzia na waumini wenu wanaokwenda kinyume na maadili mema ya dini, jamii na nchi yetu. Hamna budi kujitahidi kuwarudisha kwenye mstari mwema na maadili mema wanakondoo mliopewa kuwachunga. Nasema hivyo kwa kutambua kuwa wengi wa watu wote isipokuwa wachache sana katika wale wanaofanya maasi na maovu ni waumini wenu na wafuasi wa dini ambazo Mungu amewapa jukumu la kuongoza. Sisi katika Serikali tuko tayari kutimiza ipasavyo wajibu wetu wa kisheria katika mapambano haya adhimu. Naomba tuendelee kushirikiana kujenga maadili mema katika jamii na nchini kote kwa manufaa ya watu wetu na nchi yetu.
Dhima ya Viongozi wa Dini na Uchaguzi Mkuu
Mheshimiwa Baba Askofu;
Waumini Wote na Wageni Waalikwa Wenzangu;
Huu ni mwaka wa uchaguzi mkuu ambao pia una umuhimu wa aina yake katika historia ya nchi yetu. Tunaiaga Awamu ya Nne na kuikaribisha Awamu ya Tano ya uongozi wa nchi yetu. Niruhusuni nitumie fursa hii kuwaomba viongozi wa dini muiombee nchi yetu ipite kipindi hiki kwa salama na amani. Uzoefu wa nchi nyingi za Afrika, chaguzi hutoa mwanya kwa uvunjifu wa amani. Haijawa hivyo kwetu, lakini haina maana kuwa tunayo kinga ya milele. Hata na sisi tunaweza kuwa kama wale iwapo yale yaliwafikisha wenzetu hapo hatutayaepuka.
Mafanikio yetu ya kuendesha uchaguzi kwa amani na usalama yametokana na tahadhari ambazo Serikali na viongozi wa dini tumekuwa tukizichukua. Tuendelee kufanya hivyo. Tusiwape mwanya wanasiasa wenye dhamira ovu kuwafarakanisha Watanzania. Tuendelee kukemea matumizi mabaya ya fedha, rushwa, hila, ghilba na hujuma katika chaguzi. Tunapaswa kufanya hivyo tena zaidi sasa, wakati wa michakato ya ndani ya vyama vya siasa na baadae wakati wa uchaguzi. Tuwakemee wanasiasa wapenda madaraka kwa gharama yoyote, ambao watataka kutumia fedha kununua ushindi au ubaguzi wa rangi, kabila, dini na kadhalika, kuwabagua wapinzani wao na kujijenga kisiasa. Nawaomba msiwasikilize wala kuwaendekeza kwani mchezo wao ni mauti yetu. Wakatalieni kwa macho makavu na kwa kweli muwanyanyapae.
Hatupaswi kukaa kimya dhidi ya watu wanaokiuka maadili na kuchochea mifarakano katika taifa letu. Hawa si watu wema watatufikisha pabaya. Hawaitakii mema nchi yetu. Kamwe tusiruhusu wachezee dini zetu ambazo ni mhimili muhimu sana wa amani yetu. Tofauti na ukabila ambao pamoja na ubaya wake, lakini unaweza kuhusisha eneo dogo, dini unahusisha nchi nzima. Hakuna mtu, dini wala eneo litakalonusurika. Tutapoteza ile sifa yetu ya kihistoria ya kuwa lulu na mfano wa amani katika Afrika. Tusikubali kumchukiza Mungu akatukasirikia na kutuadhibu kwa jambo ambalo liko ndani ya uwezo wetu kulizuia lisitokee. Kwa kweli mambo yakiharibika, hatuwezi kumlaumu mtu mwingine yeyote bali sisi wenyewe. Katu hatuwezi kusema ni mapenzi ya Mungu bali itakuwa ni makosa yetu wenyewe.
Nawaomba viongozi wa dini mlisaidie taifa letu. Limeni mraba wenu vizuri nasi tulime wetu. Msiwape nafasi viongozi wa siasa na hata wa dini kutumia majukwaa ya dini kuendeleza maslahi yao ya kisiasa na hasa kupandikiza chuki katika jamii. Tunawategemea viongozi wa dini msiwe sehemu ya makundi ya wagombea au vyama vya siasa. Mnatakiwa msiwe na upande bali muwe juu ya pande zote. Hapo ndipo mtakapofanya vizuri kazi yenu ya ulezi na kuponya taifa iwapo kutatokea matatizo.
Hatuwategemei viongozi wa dini muwapangie waumini wenu vyama au viongozi wa kuwachagua. Tunawategemea kuwahimiza na kuwakumbusha kuutumia haki na wajibu wao vizuri, muwahimize na kuwakumbusha kuwa watatakiwa kufanya mambo matatu muhimu. Kwanza, kujiandikisha, pili, kujitokeza kwenda kupiga kura na tatu kuchagua viongozi wazuri, wasiokuwa waovu, wasiofanana na uovu na kuukaribia uovu, watakaosukuma mbele gurudumu la maendeleo na kujali maslahi mapana ya jamii husika na nchi yetu.
Mheshimiwa Baba Askofu;
Ndugu Waumini, Wageni Waalikwa;
Nawaomba muendelee kuiombea nchi yetu iendelee kuwa ya amani na utulivu, watu wake wadumishe upendo na mshikamano miongoni mwao. Aidha, muuombee Uchaguzi Mkuu wa mwezi Oktoba, 2015 uwe wa salama, amani na haki ili taifa letu lipate viongozi wazuri na liendelee kuwa tulivu kabla, wakati na baada ya uchaguzi.
Hitimisho
Mheshimiwa Baba Askofu;
Kama mnavyofahamu, nakaribia kumaliza kipindi changu cha uongozi wa nchi yetu. Baada ya uchaguzi wa Oktoba, 2015 tutakuwa na Rais mwingine. Napenda kutumia fursa hii kuwaaga maana naweza nisipate fursa kama hii tena katika kipindi kilichobaki. Nawashukuru sana kwa ushirikiano mkubwa mlionipa mimi binafsi na Serikali yangu katika kipindi cha miaka kumi ya uongozi wangu. Tumeishi vizuri, tumeshirikiana na kufanikisha mambo mengi mazuri pamoja. Kwa kweli nafarijika kuwa ninapoondoka madarakani, uhusiano na ushirikiano kati ya Serikali na Kanisa la Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania ni mzuri na umeendelea kuimarika. Ndivyo nilivyoupokea kutoka kwa Rais wa Awamu ya Tatu, Mheshimiwa Benjamin William Mkapa, na ndivyo nitakavyoukabidhi kwa Rais wa Awamu ya Tano. Ningependa sana kuuona uhusiano na ushirikiano huu ukikua zaidi na zaidi, siku hadi siku kwani uhusiano wenye maslahi kwa nchi yetu na watu wake. Ni uhusiano wenye kujenga umoja, amani, upendo na mshikamano miongoni wa watu wa Taifa letu hili moja, na la watoto wa Mungu mmoja. Daima nitawakumbuka na kuthamini mchango wenu na upendo wenu kwangu.
Nawashukuru tena kwa kunialika na nawatakia maadhimisho mema ya miaka 125 ya Injili. Mungu awabariki.
Asanteni Sana, na Mungu Ibariki KKKT,
Mungu Ibariki Tanzania na Watu Wake,
Bwana Asifiwe.

- Jul 02, 2015
HOTUBA YA MHESHIMIWA DKT. JAKAYA MRISHO KIKWETE, RAIS WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WAKATI WA UFUNGUZI WA KIWANDA CHA KUZALISHA VIUADUDU VYA KUULIA VILUWIL...
Soma zaidiHotuba
Mheshimiwa Hailemariam Desalegm, Waziri Mkuu wa Ethiopia;
Mheshimiwa Mizengo Pinda, Waziri Mkuu;
Mheshimiwa Dkt. Abdala Kigoda, Waziri wa Viwanda na Biashara;
Mheshimiwa Dkt. Kebwe Stephen Kebwe, Naibu Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii;
Ndugu Lobani Gutieres Ravelo, Naibu Mkurugenzi Mkuu wa Kampuni ya LABIOFAM, Cuba;
Ndugu Joyce Phumaphi, Katibu Mtendaji wa ALMA;
Mheshimiwa Lorge Luis Lopez Tarmo, Balozi wa Cuba nchini Tanzania;
Mheshimiwa Evarist Ndikilo, Mkuu wa Mkoa wa Pwani;
Waheshimiwa Mabalozi wa Nchi za Nje na Wakuu wa Mashirika ya Kimataifa;
Wageni Waalikwa;
Wanahabari;
Mabibi na Mabwana;
Ni furaha iliyoje kwangu kuwepo hapa leo, kushuhudia uzinduzi wa Kiwanda cha Kutengeneza Viuadudu vya Kuua Viluwiluwi wa Mbu. Furaha yangu inaongezeka zaidi kwa kuwepo ugeni mkubwa wa Waziri Mkuu wa Ethiopia, Mheshimiwa Hailemariam Desalegn. Yeye ndiye Mwenyekiti wa Umoja wa Viongozi wa Afrika walio mstari wa mbele katika Mapambano Dhidi ya Malaria katika Bara la Afrika (ALMA). Kwa niaba ya Watanzania wenzangu wote namshukuru sana mgeni wetu kwa kutenga muda wake na kusafiri kutoka Ethiopia kuungana nasi siku ya leo. Ujio wako unaweka uzito mkubwa kwenye azma yetu hii ya kutokomeza Malaria katika Bara letu.
Pamoja nasi, napenda pia kuwakaribisha watu wafuatao; kwanza, Ndugu Alfred Romberto Corta, Rais wa Kampuni ya LABIOFAM ya Cuba waliotuuzia teknolojia ya kutengeneza dawa hizo. Wa pili, ni Bibi Joy Pumaphi, Katibu Mtendaji wa ALMA. Mwisho, ingawaje siyo mwisho kwa umuhimu wageni wote wengine waliopo hapa leo.
Chimbuko la Kiwanda
Wageni waalikwa;
Chimbuko la ujenzi wa kiwanda hiki ni ziara yangu niliyoifanya nchini Cuba mwezi Desemba, 2009. Katika ziara ile, mwenyeji wangu Rais Raul Castro alinipangia ratiba ya kutembelea Kiwanda cha LABIOFAM kinachomilikiwa na Serikali ya Cuba na kinachozalisha dawa za viluwiluwi vya mbu wanaosababisha malaria. Baada ya kuvutiwa na maelezo na teknolojia ile na kuhakikishiwa kuwa haina athari kwa mazingira na afya ya binadamu niliagiza mambo mawili yafanyike. Kwanza, Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii iagize dawa hizo kutoka Cuba zitumike nchini; na Pili, Shirika la Taifa la Maendeleo (NDC) lianzishe ushirikiano na Kampuni ya LABIOFAM kwa lengo la kujenga kiwanda cha aina hiyo hapa nchini.
Shukurani kwa Serikali ya Cuba
Mabibi na Mabwana;
Shukrani zangu za pekee zimuendee Mheshimiwa Raul Castro, Rais wa Jamhuri ya Kisoshalist ya Cuba, na rafiki mkubwa wa Tanzania, kwa kukubali kutuuzia teknolojia hii. Wenzetu wa Cuba wametufaa sana kwani “hawajatupa tu samaki, bali wametupa ndoano ya kuvua samaki”. Wangeliweza kabisa kwa tamaa kukataa kutuuzia teknolojia na ujuzi wao na kutaka kutuuzia dawa. Pamoja na kuwa wao si nchi tajiri hawakufanya hivyo. Wameshirikiana nasi katika ujenzi na kukubali kutupa wataaalam ambao watabakia nchini kwa miaka mitano kufundisha watu wetu na kutusaidia kwa masuala ya kiufundi na kitaalam. Tunaye pamoja nasi kiongozi na Mhandisi Mkuu aliyesimamia ujenzi huu Ndugu Alfredo R. Drespo Dorta ambaye amesafiri toka Cuba kuja kushuhudia ufunguzi wa kiwanda hiki. Huu ndio urafiki wa kweli na udugu. Nakuomba Mheshimiwa Balozi wa Cuba unifikishie shukrani zangu za dhati na za Watanzania wenzangu kwa Rais Raul Castro na kwa ndugu zetu wananchi wa Cuba.
Vita Dhidi ya Malaria
Mabibi na Mabwana;
Leo tunapiga hatua kubwa na ya aina yake katika vita yetu dhidi ya malaria hapa nchini na katika Bara la Afrika hasa nchi zilizo Kusini mwa Jangwa la Sahara. Katika Ripoti ya Malaria Duniani ya mwaka 2014 iliyotolewa na Shirika la Afya Duniani (WHO) inakadiriwa kuwa, mwaka 2013, malaria ilisababisha vifo vya watu 584,000. Kati ya vifo hivyo asilimia 90 vilitokea barani Afrika Kusini mwa Jangwa la Sahara. Bahati mbaya sana waathirika wakubwa walikuwa ni wanawake na watoto chini ya umri wa miaka 5. Inakadiriwa pia kwamba malaria inazigharimu nchi wastani wa asilimia 40 ya fedha zao za bajeti ya afya na kupunguza kasi ya ukuaji wa uchumi wa baadhi ya nchi za Afrika kwa asilimia 1.3.
Kinachosikitisha zaidi ni ule ukweli kwamba, upo uhusiano mkubwa kati ya malaria na umasikini. Bahati nzuri ugonjwa huu unazuilika na kutibika maana uliwahi kuwa tishio kubwa duniani lakini leo ni tishio zaidi Afrika. uzoefu wa nchi nyingine duniani waliofanikiwa kuzuia na kutokomeza. Unatupa matumaini kuwa na sisi tukiiga mifano yao tunaweza kuwa kama wao. Kuwekeza katika kiwanda cha aina hii kutatuwezesha kutokomeza malaria.
Hali ya Malaria Nchini
Mabibi na Mabwana;
Tangu mwanzoni mwa uongozi wangu kupambana na malaria tuliupa kipaumbele cha juu. Ndicho chanzo cha wagonjwa wengi na vifo vingi nchini. Tumekuwa tunafanya mambo makuu matatu katika kupambana na malaria; kwanza, kutumia dawa mseto kutibu wagonjwa wa malaria. Pili, kuhamasisha matumizi ya vyandarua vilivyopuliziwa dawa na tatu, kupulizia dawa inayoua mbu ndani ya nyumba. Kwa kufanya hivyo tumefanikiwa kwa kiasi kikubwa kupunguza wagonjwa na vifo vitokanavyo na malaria. Kiwango cha maambukizi nacho kimepungua kutoka asilimia 18 mwaka 2007 hadi asilimia 10 mwaka 2012. Vifo vitokanavyo na malaria kwa uzazi vimekupungua kutoka 41 kwa vizazi hai 100,000 mwaka 2004 hadi 12 kwa vizazi hai 100,000 mwaka 2014. Idadi ya wagonjwa chini ya miaka 5 imepungua kutoka wagonjwa milioni 5,372,569 mwaka 2004 hadi wagonjwa milioni 3,486,326 mwaka 2014 na vifo vya watoto wa miaka 5 kwenda chini vimepungua kutoka 7,907 mwaka 2004 hadi 4,008 mwaka 2014. Kwa ujumla idadi ya wagonjwa wote imepungua kwa asilimia 51 na vifo kwa asilimia 71 kati ya 2004 na 2014.
Kwa upande wa matumizi ya vyandarua vilivyotiwa dawa, Serikali imesambaza vyandarua 26,371,329 nchi nzima, yaani vyandarua viwili kwa kaya, kwa watoto wa umri wa chini ya miaka 5 na kina mama wajawazito. Matokeo yake, idadi ya matumizi ya vyandarua vilivyotiwa dawa imeongezeka kutoka asilimia 23 mwaka 2004 hadi asilimia 92 mwaka 2012. Kwa upande wa wajawazito kutoka asilimia 27 mwaka 2004 hadi asilimia 75. mwaka 2014. Kwa upande wa watoto wa miaka 5, idadi imeongezeka kutoka asilimia 26 mwaka 2004 hadi asilimia 72 mwaka 2014.
Mafanikio zaidi makubwa na ya kujivunia yamepatikana Zanzibar. Kiwango cha maambukizi ya malaria kimeshuka na kufikia asilimia 0.2 hivi sasa. Pamoja na kufanya yale mambo matatu ndugu zetu wa Zanzibar walipulizia na kuua viluwiluwi vya mbu waenezao malaria. Kama imewezekana Zanzibar inatufanya tuamini kuwa itawezekana na huku Bara pamoja na ukubwa wa eneo na wingi wa watu. Ni kwa sababu hiyo, tulichukulia uwekezaji huu wa kiwanda cha kuzalisha viuatilifu kuwa uwekezaji wa kimkakati katika vita dhidi ya malaria. Kwa kuwa sasa dawa hizi zitakuwa zikizalishwa nchini kwa wingi na gharama nafuu, jukumu letu sasa ni kuanzisha kampeni nchi nzima ya kupulizia maeneo yote ili kuua viluwiluwi vya mbu pale wanapozaliwa. Sasa tunatangaza vita si tu na mbu bali na viluwiluwi vyake.
Maelekezo Mahsusi
Mabibi na Mabwana;
Natoa pongezi kwa Bodi ya Shirika la Taifa la Maendeleo (NDC) kwa kusimamia vizuri ujenzi wa kiwanda hiki. Jukumu kubwa na lililo mbele yenu sasa ni kuhakikisha kiwanda hiki kinazalisha na kujiendesha kibiashara. Hatutarajii kiwanda hiki kiijiendeshe kwa hasara maana biashara yenyewe ni ya uhakika ndani na nje ya nchi yetu. Kama nilivyokwishasema hapo awali, Tanzania ni mwanachama, tena mwanachama mwanzilishi wa Umoja wa Marais wa Afrika walio katika Mapambano Dhidi ya Malaria (ALMA). Umoja huu una nchi 49 Sote kwa pamoja, tunayo dhamira ya kuondokana na malaria katika nchi zetu na tumejiwekea malengo. Uwepo hapa wa Mwenyekiti wetu Mheshimiwa Waziri Mkuu wa Ethiopia ni ushahidi huo. Shirikianeni na Wizara ya Viwanda na Biashara, Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa na Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii kutangaza bidhaa za kiwanda hiki. Tafuteni masoko barani Afrika, maana, kutokomeza malaria hakutegemei mafanikio katika nchi yetu tu, bali pia na kwa nchi nyingine katika Bara letu.
Naelekeza pia ofisi ya Waziri Mkuu, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa kukitumia kiwanda hiki katika mipango yake ya kutokomeza malaria katika Halmashauri zetu. Halmashauri zihamasishe watu wetu na kaya zilizo kwenye maneo yao ya utawala kutumia dawa zinazozalishwa na kiwanda hiki. Angalieni namna bora ya kuwezesha hilo kufanyika. Kwa kupulizia dawa hizi na kutokomeza viluwiluwi wa mbu kutang’oa mzizi wa fitina unaosababisha maambukizi na vifo vya malaria.
Hitimisho
Mabibi na Mabwana;
Kama nilivyosema awali, leo ni siku ya furaha sana kwangu kwa kukamilika kiwanda hiki na kupata fursa ya kushuhudia ufunguzi wake. Mafanikio tuliyoyapata katika kutibu malaria ni makubwa na ya kutia moyo. Hata hivyo, mafanikio hayo yasingekuwa endelelevu iwapo tusingeongeza nguvu na mkazo katika kukinga na kuzuia maambukizi. Kiwanda hiki tunachokifungua leo kitaimarisha uwezo wetu wa kukinga na kuzuia maambukizi ya malaria. Wahenga wamesema daima “kinga ni bora kuliko tiba”. Sasa tuna uhakika kuwa mapambano yetu dhidi ya malaria tumeyafikisha mahali pazuri. Nafurahi kuona leo tunatamka kwa vitendo kuwa “Malaria Haikubaliki”. Sasa natangaza kuwa kiwanda cha Kuzalisha Viuadudu vya Viluwiluwi vya Mbu kijulikanacho kama Tanzania Biotech Products Limited kimefunguliwa rasmi.
Asanteni kwa kunisikiliza!

- Jun 27, 2015
HOTUBA YA MHESHIMIWA DKT.JAKAYA MRISHO KIKWETE, RAIS WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA, KWENYE HAFLA YA KUFUNGAMAFUNZO YA UONGOZI WA JUU, KOZI NA 21/2015, CHUO...
Soma zaidiHotuba
Mheshimiwa Mathias Chikawe (Mb), Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi;
Mheshimiwa Jaji Kiongozi;
Mheshimiwa Said Mecky Sadiki, Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam na Viongozi wa Serikali mliopo;
Ndugu John Minja, Kamishna Jenerali wa Jeshi la Magereza;
Ndugu Ernest Mangu, Inspekta Jenerali wa Polisi;
Ndugu Sylvester Ambokile, Kamishna Mkuu wa Uhamiaji;
Meja Jenerali Salum Kijuu, Kamanda wa Jeshi la Nchi Kavu;
Wakuu wa Magereza wa Nchi marafiki;
Mkuu wa Chuo;
Maafisa Waandamizi wa Jeshi la Magereza;
Maafisa kutoka Vyombo vya Ulinzi na Usalama;
Viongozi mbalimbali mliopo;
Wageni Waalikwa;
Vyombo vya Habari;
Mabibi na Mabwana;
Salamu na Shukrani
Naomba nianze kwa kutoa shukrani zangu za dhati kwako Mheshimiwa Mathias Chikawe, Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi na kwa Kamishna Jenerali wa Magereza kwa kunialika na kunishirikisha kwenye hafla ya kufunga Mafunzo ya Uongozi wa Ngazi ya Juu kwa Maafisa 104 wa Jeshi la Magereza, na kuadhimisha Siku ya Magereza. Hii ni mara yangu ya kwanza kushiriki kwenye shughuli ya aina hii. Nasema Asanteni sana.
Wakuu wa Magereza kutoka Nje ya Nchi
Mheshimiwa Waziri;
Nimefurahishwa sana kuona kuwa miongoni mwa wageni waalikwa katika hafla hii, wapo pia Wakuu wa Magereza kutoka nchi rafiki za Botswana, Kenya, Namibia, Swaziland, Uganda na Zambia. Hili ni jambo jema. Ninawaomba muendelee kuudumisha ushirikiano uliopo miongoni mwenu. Mbadilishane maarifa na uzoefu katika utekelezaji wa majukumu yenu ya msingi hasa lile la kurekebisha wahalifu waweze kuwa raia wema katika nchi na jamii zao. Kwa wageni wetu nasema karibuni Tanzania na nawatakia makazi mema.
Pongezi
Mheshimiwa Waziri;
Nawapongeza sana, Kamishna Jenerali wa Magereza, Mkuu wa Chuo na wasaidizi wake, kwa maandalizi mazuri ya sherehe hizi. Hakika zimefana sana. Kwa wahitimu wa mafunzo haya, nawapongeza kwa kumaliza mafunzo yenu salama na kwa mafanikio. Gwaride lilikuwa zuri linaloashiria kwamba mmeiva barabara na kwamba mko tayari kwenda kutekeleza majukumu yenu kwa ufanisi zaidi. Ni matarajio yangu kuwa mtayazingatia yale yote mliyojifunza kwa kutekeleza majukumu yenu vizuri zaidi kuliko mlivyokuwa kabla ya kuja kozi hii. Natoa pongezi maalum kwa Mkuu wa Chuo na Wakufunzi wote kwa kazi nzuri mliyoifanya iliyotuwezesha kukusanyika hapa siku ya leo.
Jukumu la Jeshi la Magereza
Mheshimiwa Waziri;
Napenda kutumia nafasi hii adimu na adhimu kutoa pongezi maalum kwa Maafisa na Askari wa Jeshi la Magereza kwa kazi kubwa na nzuri waifanyayo katika kuimarisha usalama wa raia na jamii nzima ya Watanzania. Jeshi letu ambalo Agosti 25, mwaka kesho litasherehekea ‘Diamond Jubilee’ ya kuanzishwa kwake, kama majeshi mengine ya magereza duniani, lina jukumu la msingi la kutekeleza programu za urekebishaji wa wahalifu na kutoa ushauri wa kisera kwa Serikali juu ya uzuiaji uhalifu.
Hili ni jukumu zito na nyeti kwa kuwa linagusa maisha ya wananchi wengi na taswira ya taifa kwa ujumla. Ni matarajio ya jamii kuona kwamba wafungwa wamalizapo vifungo vyao, wanarudi kwenye jamii wakiwa raia wema. Wanakuwa wameacha matendo maovu na kuendesha maisha yao kama raia wenye mwenendo mwema na wanaotii sheria za nchi. Wanafanya shughuli zilizo halali za kuwapatia riziki zao kwa kutumia ujuzi walioupata wakati wakitumikia vifungo vyao au kabla ya hapo.
Kwa hiyo Jeshi la Magereza linapaswa kuwafundisha wafungwa stadi za maisha katika nyanja mbalimbali ili wakimaliza vifungo vyao wawe na ujuzi utakaowawezesha kuendesha maisha yao kwa kujitegemea. Jeshi letu pia lina wajibu wa kuwapa wafungwa hawa ushauri nasaha utakaowasaidia kujutia makosa yao ili waishi kama raia wema. Chombo hiki cha dola kikitimiza jukumu hili kwa ukamilifu, kitachangia kwa kiasi kikubwa katika azma ya taifa letu ya kudumisha usalama wa raia, amani na utulivu.
Kamishna Jenerali wa Magereza;
Kumalizika kwa kozi ambayo tunaifunga mafunzo yake leo kunawaongezea Maafisa 104 katika nguvu kazi yenu ya kutekeleza majukumu yenu. Hongereni sana. Pia nawapongeza wanaohitimu leo kwa kuua ndege wawili kwa jiwe moja. Mmefaulu kozi na kupanda vyeo kutoka ngazi ya Mrakibu wa Askari Magereza hadi Inspekta Msaidizi wa Magereza. Mnastahili kujipongeza na kusherehekea.
Nimefurahishwa na mpango wenu wa kuanzisha Chuo kipya cha Tanzania Correctional Training Academy. Kwa kuwa na Chuo hicho mkichanganya na Chuo cha Kiwira na hiki cha Ukonga pamoja na mafunzo ya nje, mtakuwa na wigo mpana wa kuwaongezea uwezo watumishi wa Jeshi hili. Tafadhali endeleeni na jitihada mzifanyazo katika kuboresha mafunzo ili mpate Maofisa na Askari wenye ujuzi, maarifa na weledi wa hali ya juu. Itaimarisha sana utekelezaji wa majukumu yenu.
Changamoto Mnazozikabili
Mheshimiwa Waziri;
Mimi natambua kama mnavyotambua nyinyi kuwa ili Jeshi liweze kutimiza kwa ukamilifu majukumu yake pamoja na kuwa na Maafisa na Askari waliofunzwa vizuri, lazima wapewe vitendea kazi vinavyokidhi mahitaji. Nazifahamu changamoto zenu na mahitaji yenu ambayo yakitimizwa mambo yatakuwa mazuri.
Magereza 126 yaliyopo hayatoshelezi mahitaji, hivyo kusababisha msongamano mkubwa. Yanahitajika Magereza mapya pamoja na kukarabati na kupanua yaliyopo. Huduma muhimu kwa wafungwa zinatakiwa kuboreshwa. Aidha, kuna mahitaji makubwa ya makazi, majengo ya ofisi, vyombo vya usafiri na mawasiliano na vitendea kazi mbalimbali. Chanzo kikubwa cha matatizo haya ni ufinyu wa bajeti. Kinachotengwa na kinachotolewa havikidhi haja. Ni wazi kwamba matatizo haya yamekuwa yakiathiri ufanisi katika utekelezaji wa majukumu yenu.
Kamishna Jenerali ameeleza baadhi ya jitihada ambazo mmekuwa mkichukuwa kukabiliana na changamoto hizo. Nawapongeza sana kwa ubunifu wenu uliowawezesha kufanya kazi katika mazingira hayo tete na kufanikiwa kutekeleza majukumu yenu kwa kiwango cha kuridhisha.
Naomba niwahakikishie kwamba Serikali itaendelea kufanya kila linalowezekana kutatua matatizo yanayowakabili kadri hali inavyoruhusu. Nawaomba muifanyie kazi haraka iwezekanavyo na kuikabidhi mamlaka husika Rasimu ya Sera ya Taifa ya Magereza ambayo nimeelezwa iko tayari, ili tutoe maamuzi na utekelezaji wake uanze. Kwa kufanya hivyo tutawezesha Jeshi kutekeleza mpango wa maboresho katika maeneo mbalimbali.
Shughuli za Uzalishaji Mali
Mheshimiwa Waziri;
Jeshi la Magereza linasifika si tu kwa kuzalisha bidhaa bali kwa ubora wa bidhaa zake. Natambua mnazo fursa mbalimbali ambazo mkizitumia kwa ukamilifu, mtaweza kuongeza uzalishaji wa mazao ya kilimo na mifugo, na bidhaa mbalimbali kutoka kwenye viwanda vidodo vidogo. Ninyi mna bahati ya kuwa na maeneo makubwa ambayo yanafaa kwa shughuli za viwanda, ufugaji na kilimo kikiwemo kilimo cha umwagiliaji.
Tunapoelekeza nguvu zetu kwenye mapinduzi ya kilimo kwa kuzingatia kilimo cha kisasa na cha kibiashara, Jeshi linapaswa kuwa na Mpango Mkakati unaotekelezeka kusaidia nchi yetu kufikia azma ya kujitosheleza kwa chakula na kupata malighafi za viwanda.
Mbali na ulimaji wa mazao ya chakula, Magereza sasa inabidi ielekeze nguvu zake katika kilimo cha mazao yenye thamani kama vile maua, mbegu za mafuta hususan alizeti, ufuta na karanga, mboga za aina mbalimbali na matunda. Pia fugeni samaki na nyuki. Mazao hayo yatawapatia mapato mengi yatakayo waongezea uwezo wa kutimiza majukumu yenu na kupunguza baadhi ya changamoto zenu.
Mnazo pia shughuli za viwanda vidogovidogo kama vile utengenezaji wa samani, ushonaji na ufumaji, utengenezaji wa viatu na kazi za ukarabati na ujenzi.
Naomba msiendelee kuzalisha kama zamani. Hamna budi kuwa wabunifu ili mzalishe bidhaa zinazokidhi mahitaji ya soko la sasa na la baadaye ambalo lina ushindani mkubwa. Shirika la Magereza ambalo linajishughulisha na uzalishaji katika miradi mbalimbali liwe na upeo mkubwa ili lisiishie kuzalisha kwa ajili ya soko la ndani bali hata la nje; lakini lijenge uwezo wa kuwa mwekezaji katika mipaka nje ya Tanzania. Wafungwa ambao wako katika mchakato wa kurekebishwa wapatiwe mafunzo na ujuzi kwa vitendo na inabidi wapewe mafunzo ya ziada katika stadi husika ili waendeleze ubora wa uzalishaji pindi wakiwa huru uraiani.
Maadhimisho ya Siku ya Magereza
Mheshimiwa Waziri;
Nimefurahi kusikia kwamba sambamba na shughuli za kufunga mafunzo haya, leo pia mnaadhimisha Siku ya Magereza ambapo mtakuwa mkionesha shughuli mbalimbali zinazofanywa na Jeshi la Magereza. Hii ni fursa nzuri kwenu kujitangaza kwa wananchi kuhusu kazi mnazofanya ikiwemo jukumu la urekebishaji wa wafungwa. Siku hii pia itumike kuikumbusha jamii wajibu wake wa kutimiza maadili mema ili watu watambue wajibu wao wa kutoa malezi mema tangu utoto hadi utu uzima. Kupitia maonesho hayo, jamii itajifunza kutoka kwenu lakini na ninyi muwe tayari kupokea ushauri wenye lengo la kuboresha utekelezaji wa majukumu yenu.
Katika siku kama hii, suala jingine la kutiliwa mkazo ni uzingatiaji wa Sheria, Kanuni na Taratibu katika utekelezaji wa majukumu yenu. Kumbukeni kwamba wafungwa wapo magerezani kutumikia vifungo vyao na mahabusu kusubiri hatima ya kesi zao. Kuwepo kwao ndani ya magereza hakuwaondolei utu wao zaidi ya kuwanyima uhuru tu. Wakati wote wa kutekeleza majukumu yenu, mnapaswa kuzingatia Sheria, Kanuni na Taratibu zilizopo. Kamwe msiwatendee wafungwa mambo yaliyo kinyume na haki zao kama binadamu mwingine ye yote. Wakati wote hakikisheni mnazingatia haki zao za msingi. Kwa kufanya hivyo, mtasaidia kupunguza malalamiko yasiyo ya lazima kutoka kwa wafungwa, ndugu wa wafungwa na taasisi zikiwemo zile zinazohusika na masuala ya Haki za Binadamu.
Shirikianeni na Kituo cha Uwekezaji
Mheshimiwa Waziri;
Ili kujenga uwezo wa ushindani na uwekezaji, nawashauri mtumie ipasavyo fursa hizo mlizonazo ili kuongeza uzalishaji wa mazao na bidhaa mbalimbali. Aidha, kwa kushirikiana na wadau mbalimbali kikiwemo Kituo cha Uwekezaji (TIC), tangazeni fursa za uzalishaji mlizonazo ili kuwavutia wawekezaji wenye nia njema na uwezo ili mshirikiane nao.
Ninazo taarifa kwamba mmeanzisha juhudi za kutafuta wawekezaji kwenye miradi yenu na tayari baadhi yao mmeingia nao ubia katika kuzalisha mazao ya kilimo. Vilevile nimefahamishwa kwamba mmeandaa mpango wa Jeshi kujitosheleza kwa chakula. Naomba mpango huo ufanyiwe kazi haraka na mamlaka zote zinazohusika ili tuone ni yapi tunaweza kuanza kuyatekeleza kuliongezea Jeshi uwezo katika uzalishaji.
Hitimisho
Mheshimiwa Waziri,
Kamishna Jenerali wa Magereza:
Nihitimishe hotuba yangu kwa kurudia shukrani zangu kwa jinsi mlivyoandaa hafla hii ambayo imefana sana. Nawatakia kila la kheri katika utekelezaji wa majukumu yenu. Na baada ya kusema haya, sasa natamka kwamba Mafunzo ya Uongozi wa Ngazi ya Juu kwa Maafisa Magereza Chuo Ukonga yamefungwa rasmi.
Asanteni sana kwa kunisikiliza!

- Jun 26, 2015
HOTUBA YA MHE. DKT. JAKAYA MRISHO KIKWETE, RAIS WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA KWENYE MAADHIMISHO YA KITAIFA YA SIKU YA KUPIGA VITA DAWA ZA KULEVYA DUNIANI...
Soma zaidiHotuba
Mheshimiwa Dkt. Seif Rashid, Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii;
Mheshimiwa Eng. Everist Ndikilo, Mkuu wa Mkoa wa Pwani,
Ndugu Keneth Kaseke, Kamishna wa Tume ya Kuratibu Udhibiti wa Dawa za Kulevya;
Waheshimiwa Wakuu wa Wilaya;
Viongozi na Watendaji Wakuu wa Serikali;
Viongozi wa Vyama vya Siasa wakiongozwa na Chama Tawala;
Dkt. Bwijo Bwijo, kutoka UNDP na Wawakilishi wa Jumuiya na Taasisi za Kimataifa;
Viongozi wa Dini na Asasi za Kiraia;
Wageni waalikwa;
Mabibi na Mabwana;
Ndugu wananchi;
Salamu na Shukrani
Nakushukuru sana Mheshimiwa Dkt. Seif Rashid, Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii na waandazi wa shughuli hii kwa kunialika na kunishirikisha katika Siku ya Kupiga Vita Dawa za Kulevya Duniani. Natoa pongezi nyingi kwa wananchi na viongozi wa Mkoa wa Pwani wakiongozwa na Mkuu wa Mkoa Mhe. Eng. Evarist Ndikilo kwa kukubali kuwa wenyeji wa sherehe hizi. Baada ya kuona mabango na kusikia kauli kadhaa kutoka wasanii mmejidhihirishia ni jinsi gani mlivyojitayarisha kufanikisha hafla ya leo. Nawapongeza kwa kushirikiana vyema na Tume ya Kuratibu Udhibiti wa Dawa za Kulevya na kufanikisha maadhimisho haya. Mwisho nitoe pongezi zangu kwa TAYOA kutokana na ubunifu wao mzuri wa mawasiliano miongoni mwa vijana. Hongereni sana! Hakika mambo yamefana sana.
Aidha, nawashukuru kwa zawadi nzuri ya saa ambayo itakuwa inanikumbusha wakati wa kulala na kuamka.
Kuadhimisha kupiga Vita Matumizi na Biashara
Haramu ya Dawa za Kulevya
Ndugu wananchi;
Kama alivyoeleza Mwakilishi kutoka UNDP, Dkt. Bwijo Bwijo tarehe 26 Juni ya kila mwaka ni siku maalum ya kuadhimisha kupiga vita matumizi na biashara haramu ya dawa za kulevya duniani. Maadhimisho haya hutupa fursa ya kutafakari hatua tunazopiga katika jitihada zetu za kudhibiti biashara na matumizi ya dawa za kulevya katika jamii zetu na nchi yetu kwa jumla. Katika siku hii pia, pamoja na kufanya tathmini ya mafanikio na changamoto za mapambano hayo tunapanga mikakati ya kukabiliana na changamoto zilizopo kwa ufanisi zaidi.
Tujenge Jamii, Maisha na Utu wetu bila Dawa za Kulevya.
Ndugu wananchi;
Kila mwaka maadhimisho haya yanapofanyika huwepo kauli mbiu ambayo hutoa ujumbe unaosisitiza jambo lililokusudiwa wakati huo. Kauli mbiu ya mwaka huu ya, “Tujenge jamii, maisha na utu wetu bila dawa za kulevya” inatukumbusha sote kukaa mbali na matumizi na biashara ya dawa za kulevya. Dawa za kulevya ni hatari kwa maisha ya mwanadamu, utu wake na ustawi wa jamii yake. Kauli mbiu hii inatutaka tujenge jamii, maisha na utu wetu bila kujihusisha kwa namna yoyote ile na dawa za kulevya. Dawa za kulevya hazina manufaa yo yote bali hasara tele. Mapambano haya dhidi ya biashara na matumizi ya dawa za kulevya yanamhusu kila mmoja wetu wadogo kwa wakubwa, viongozi na wananchi wa kawaida, matajiri na maskini, Serikali Kuu na Serikali za Mitaa kwani athari zake humgusa kila mmoja wetu.
Madhara ya dawa za Kulevya
Ndugu Wananchi;
Ni jambo lililo dhahiri kuwa dawa za kulevya zina madhara makubwa sana. Matumizi na biashara ya dawa za kulevya inaathiri ustawi wa binadamu. Hudhoofisha afya za watumiaji, na huchochea kuenea kwa maambukizi ya virusi vya UKIMWI, homa ya ini na mara nyingi husababisha vifo. Hali kadhalika, huchochea rushwa miongoni mwa watumishi wa umma hasa wale wanaotegemewa kuongoza mapambano dhidi yake. Kwa mujibu wa tamko la Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Kudhibiti Uhalifu na Dawa za Kulevya alilolitoa tarehe 5 Juni, 2013 kwenye Mkutano wa mwaka wa Vyombo vya Udhibiti wa Dawa za Kulevya uliofanyika Moscow, watu wapatao 200,000 hupoteza maisha kila mwaka duniani kutokana na matumizi ya dawa za kulevya. Biashara ya dawa za kulevya imeleta changamoto kubwa kwa jumuiya ya kimataifa. Kwa baadhi ya nchi, biashara hii imekuwa ni janga kubwa ambalo limesababisha kuharibika kwa mifumo ya kiutawala na kisheria, uvunjifu wa amani na usalama, kudorora kwa maendeleo ya kijamii na ya kiuchumi. Biashara hii huchochea kuwepo kwa magenge ya kihalifu yanayojihusisha na mauaji, wizi na ujambazi. Hali kadhalika, mapato yake yanafahamika kugharamia shughuli za ugaidi, usafirishaji haramu wa binadamu, biashara ya fedha haramu, biashara haramu ya silaha na uporaji wa nyara za taifa - vitendo ambavyo ni tishio kwa usalama wa dunia. Hivi basi kupiga vita biashara na matumizi ya dawa za kulevya ni vita vya haki na ni wajibu kwa kila mtu kushiriki. Lazima tushinde vita hii.
Juhudi za Mapambano Kimataifa
Ndugu wananchi;
Mataifa mengi duniani yametambua madhara ya matumizi na biashara haramu ya dawa za kulevya. Pia watu wengi wanauona umuhimu wa kufanya juhudi za pamoja ndani ya nchi, kikanda na kimataifa kukabiliana na uhalifu huu. Matokeo yake ni kuanzishwa kwa Shirika la Umoja wa Mataifa la Kudhibiti Uhalifu na Dawa za Kulevya. Pia, ni kufanyika kwa operesheni za pamoja za kupambana na biashara ya dawa za kulevya zinazofanywa na mataifa mbalimbali kikanda na kimataifa. Jambo lingine ni pamoja na kuwepo kwa mikutano ya pamoja kimataifa na kikanda kwa ajili kupanga mikakati ya pamoja.
Naungana na viongozi wenzangu wa nchi mbalimbali duniani na mashirika wa kimataifa katika mapambano haya. Nakemea vikali matumizi na biashara ya dawa za kulevya na kuwaonya wananchi wajiepushe kabisa kujihusisha nazo. Ni imani yangu kuwa, Watanzania wenzangu mtafanya kila liwezekanalo kujiepusha na kuwaepusha watu wengine hasa vijana na watoto kujihusisha na balaa hili. Watanzania wenzangu tuongozwe na kauli mbiu ya TANU wakati wa kudai uhuru na kujenga nchi inasema, “Umoja ni nguvu utengano ni udhaifu”. Na kwa sasa kauli ya CCM isemayo, ”Umoja ni Ushindi”. Hakika umoja wetu ndio utakaotuhakikishia ushindi katika mapambano haya.
Vyombo vyetu Viko Macho
Ndugu wananchi;
Naomba niwahakikishie kuwa Serikali itaendelea kutimiza wajibu wake katika mapambano dhidi ya biashara na matumizi ya dawa ya kulevya bila kuchoka na bila kigugumizi au ajizi yoyote. Lengo letu ni kudhibiti hali ili kuzuia isizidi kuwa mbaya zaidi ya ilivyo sasa na kubadili mwelekeo ili hatimaye tulikomeshe kabisa tatizo hili hapa nchini. Kwa ajili hiyo, tumekuwa tunafanya mambo makuu matatu.
Kwanza, kuimarisha vyombo vya dola vinavyoongoza mapambano dhidi ya uhalifu huo. Tunayo Tume ya Kudhibiti Dawa za Kulevya ambayo imefanya kazi kubwa ya kuelimisha jamii kujiepusha na matumizi na biashara ya dawa za kulevya. Tumeendelea kuijengea uwezo Tume hiyo pamoja na Jeshi la Polisi ambalo ndilo linalokamata wafanya biashara na watumiaji na kuwafikisha katika vyombo vya Sheria. Pamoja na hayo nikaamua kuunda Kikosi Kazi kilichojumuisha Polisi, Idara ya Usalama wa Taifa na Tume ya Kudhibiti Dawa za Kulevya. Kikosi Kazi hicho kimefanya kazi kubwa na nzuri. Kimeongeza nguvu na uwezo wa kupambana na uhalifu huu na wahalifu wanaojihusisha na biashara hii haramu na wanaotumia dawa za kulevya. Wafanya biashara wengi wadogo, wa kati na wakubwa wamekamtwa na kufikishwa kwenye vyombo vya sheria. Ukamataji wa Dawa za Kulevya nao umeongezeka sana na hivyo kunusuru taifa na hata dunia na madhara ambayo dawa hizo zingefanya. Tumezisikia takwimu zilizotolewa na Ndugu Keneth Kaseke, Kamishna wa Tume ya Kuratibu Udhibiti wa Dawa za Kulevya.
Hiki ni kiwango kikubwa cha mafanikio hivyo vyombo vinastahili pongezi nyingi kutoka kwetu sote. Takwimu hizi zinatuonesha kuwa tatizo ni kubwa hivyo lazima tuwe katika hali ya tahadhari wakati wote (saa 24 kwa siku zote saba za wiki).
Pili, ili kuongeza nguvu, mbinu na maarifa ya kupambana na uhalifu huu wa hatari na kutisha, tumetunga Sheria (mpya) ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya ya Mwaka 2015. Sheria hii imejengeka juu ya hali ilivyo sasa katika mapambano haya. Mafanikio na changamoto zilizopo imezingatiwa hivyo ni Sheria inayoimarisha mafanikio tuliyoyapata na kuyapatia ufumbuzi matatizo yaliyopo. Sheria inaunda chombo maalum cha kupambana na Dawa za Kulevya. Chombo hiki kitakuwa na nguvu kubwa zaidi ya kuratibu udhibiti wa dawa za kulevya nchini. Kimepewa mamlaka ya kupeleleza, kupekua na kukamata wafanya biashara na watumiaji wa dawa za kulevya. Nina imani kubwa kwamba chombo hiki kitasaidia sana kupunguza tatizo hili nchini. Natanguliza kuwaomba wananchi na vyombo vingine vyote vya Serikali kutoa ushirikiano wa kutosha kwa chombo hiki mara kitakapoanza kazi ili tuweze kulinusuru taifa letu na tatizo hili.
Huduma za Matibabu
Ndugu wananchi;
Kwa kuzingatia hekima na busara za usemi wa Wahenga, ”Kinga ni bora kuliko tiba”, mkakati wa kudhibiti na kupambana na dawa za kulevya unasisitiza sana kuelimisha jamii kuhusu kuepukana na kujihusisha na biashara na matumizi ya dawa za kulevya. Kwa wale waathirika wa matumizi ya dawa za kulevya, mkakati ni wa Serikali kuendeleza jitihada za kuwapatia ushauri nasaha na matibabu. Hilo ndilo jambo letu la tatu. Kwa sasa huduma hizi zinapatikana katika vitengo vya magonjwa ya akili katika hospitali za baadhi ya mikoa na wilaya hata nchini. Hata hivyo, idadi ya watumiaji wanaopata nafasi ya kupata huduma za tiba bado ni ndogo sana. Takwimu zinaonesha kuwa kuna watumiaji wa heroin wanaokadiriwa kuwa kati ya 200,000 na 425,000 nchini. Idadi ya watumiaji wa heroin wanaopata matibabu kwa kutumia tiba ya methadone mpaka kufikia Mei, 2015 ni 2,300 tu. Watu hawajitokezi kwa wingi. Tafadhalini ndugu zangu jitokezeni mpate uponyaji.
Ninaiagiza mikoa yote hasa ile yenye matatizo makubwa ya matumizi ya dawa za kulevya hususani Dar es Salaam, Tanga, Arusha, Mwanza, Mbeya, Pwani na Shinyanga kuchukua hatua thabiti za kuanzisha na kuendeleza huduma hizi. Lazima tutambue pia, kwamba hakuna Mkoa ambao uko salama, tofauti ni kiwango cha athari. Hivyo basi kila Mkoa ujiandae ipasavyo. Tahadhari kabla ya hatari. Nawataka Viongozi wa Mikoa na Wilaya kote nchini wafuatilie utekelezaji wa jambo hili. Kamati za Ulinzi na Usalama za Mikoa na Wilaya ziliweke suala la dawa za kuleya kuwa agenda ya kudumu katika vikao vyao.
Napenda kutumia nafasi hii kuwashukuru wale wote waliosaidia katika kuanzisha na kuendeleza huduma ya methadone na huduma nyingine za matibabu nchini. Niruhusuni nitoe shukrani maalum kwa Rais Barack Obama na Serikali ya Watu wa Marekani kwa msaada mkubwa wnaotupatia kwa upande wa matibabu.
Tusiharibu Taswira ya Nchi yetu
Ndugu wananchi;
Narudia kuelezea masikitiko kuhusu baadhi ya Watanzania wenzetu wanaojihusisha na biashara ya dawa za kulevya nje ya nchi. Hawa ni chachu ya kuendelea kwa tatizo hapa nchini. Pia, wanaharibu taswira nzuri ya nchi yetu kimataifa na kuhatarisha maisha yao. Zipo taarifa kuwa kati ya Januari 2012 na Desemba 2014, kwa mfano, jumla ya Watanzania 111 walikamatwa kwa kujihusisha biashara hiyo katika nchi za Brazil na China. Hii ni fedheha kubwa. Pia, naomba niwakumbushe na kuwatahadharisha kuwa baadhi ya nchi hutoa adhabu kali ikiwemo ya kifo kwa watu watakaokamatwa na kutiwa hatiani. Mfano mmoja wapo ni wa yale yaliyotokea Indonesia kati ya Januari na Aprili 2015 ilipowanyonga wasafirishaji wa dawa za kulevya 12 kutoka nchi mbalimbali zikiwemo za Afrika. Nchi hiyo ilikataa maombi ya nchi zao kutaka adhabu hiyo isitekelezwe dhidi ya raia wao.
Akitetea uamuzi wa nchi yake Mwanasheria Mkuu wa Indonesia Muhammad Prasetyo baada ya hukumu kutekelezwa alisema;
‘Tunapigana vita dhidi ya uhalifu wa kutisha wa dawa za kulevya ambao unatishia mustakabali wa taifa letu. Napenda kusema kwamba kuua si jambo jema, si jambo la kufurahisha. Lakini lazima tufanye hivyo kwa ajili ya kuliokoa taifa na hatari ya dawa za kulevya. Hatufanyi uadui na nchi ambazo raia wake walihukumiwa kifo.’
Nawaasa Watanzania wenzangu watambue ukweli huu na kuachana na biashara ya dawa za kulevya ndani na nje ya nchi yetu. Ni hatari kwao na taifa pia. Ingawa hapa nchini adhabu ya kifo haitolewi kwa kosa la kujihusisha na dawa za kulevya, Sheria ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya ya 2015 ambayo itaanza kutumika hivi karibuni inatoa adhabu kali hadi kifungo cha maisha.
Tahadhari Dhidi ya Matumizi ya Shisha
Ndugu wananchi;
Kwa masikitiko makubwa, Serikali imepokea malalamiko mengi kuhusu matumizi ya shisha nchini. Matumizi haya yameenea kwa haraka katika maeneo mengi ya starehe na huwavutia vijana wengi wa kiume na wa kike. Watumiaji wa kilevi hiki huonyesha dalili zinazofanana na za utumiaji wa dawa za kulevya. Hivyo, kuna hofu kuwa kilevi hiki kinachanganywa na dawa za kulevya. Kama hiyo ni kweli ni jambo hili ni la kusikitisha sana, halikubaliki na kwamba hatuna budi kuhakikisha kuwa haliachwi kuendelea. Nichukue nafasi hii kuziagiza mamlaka husika kufanya uchunguzi haraka iwezekanavyo ili kupata majibu yatakayosaidia kutatua tatizo hili na hatimaye kuinusuru jamii yetu.
Tusiruhusu Rushwa Ijipenyeze
Ndugu wananchi;
Mapambano dhidi ya biashara na matumizi ya dawa za kulevya si lelemama. Kuna changamoto kadhaa ikiwa ni pamoja na vishawishi vya rushwa. Vitendo vya rushwa kwa baadhi ya watendaji wasiokuwa waaminifu vinachangia sana katika kurudisha nyuma mapambano dhidi ya tatizo la dawa za kulevya. Natoa agizo kwa mamlaka husika kuhakikisha kuwa suala la rushwa linadhibitiwa kikamilifu katika mapambano haya kwa kuwachukulia hatua stahiki wote watakaobainika kujihusisha na vitendo hivyo.
Mjitokeze kwa Wingi Kujiandikisha
Ndugu wananchi;
Wote mnatambua vema kuwa mwaka huu tutakuwa na uchaguzi wa viongozi katika ngazi mbalimbali katika Taifa letu. Nawaasa wananchi wenzangu muendelee kujitokeza kwa wingi katika kujiandikisha katika Daftari la Kudumu la Mpiga Kura. Wakati wa kupiga kura utakapofika, mtumie haki yenu ya kikatiba kuchagua viongozi waadilifu ambao kwa namna yoyote ile hawajihusishi na biashara au matumizi ya dawa za kulevya. Aidha, nawaasa wazazi na walezi, viongozi wa dini, viongozi wa asasi za kijamii, watambue kuwa hivi ni vita vyetu sote. Tatizo la dawa za kulevya likiachiwa bila kudhibitiwa kwa dhati litaleta maafa makubwa kwa kizazi cha sasa na kijacho. Kwa sababu hiyo, tunao wajibu wa kupambana kila mtu kwa nafasi yake. Tuwalee watoto wetu kwa misingi ya maadili mema ili kujenga Taifa lisilokuwa na matumizi wala biashara ya dawa za kulevya. Inawezekana Timiza Wajibu wako.
Tujenge jamii, maisha na utu wetu bila dawa za kulevya
Asanteni kwa kunisikiliza.

- Jun 14, 2015
HOTUBA YA MHESHIMIWA JAKAYA MRISHO KIKWETE, RAIS WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA YA KUAGA WAKUU WA NCHI ZA UMOJA WA AFRIKA KATIKA MKUTANO WA 25 WA WAKUU WA N...
Soma zaidiHotuba
Mheshimiwa Robert Gabriel Mugabe, Rais wa Jamhuri ya Zimbabwe na Mwenyekiti wa Umoja wa Afrika;
Mheshimiwa Jacob Zuma, Rais wa Afrika Kusini, Mwenyekiti ambaye tunamshukuru sana kwa mapokezi mazuri na ukarimu wake;
Waheshimiwa Wakuu wa Nchi na Serikali;
Mheshimiwa Dkt. Nkosazana Dlamini-Zuma, Mwenyekiti wa Kamisheni ya Umoja wa Afrika;
Rais wa Palestina, Mheshimiwa Mahmoud Abbas, Katibu Mkuu wa Arab League;
Mheshimiwa Dkt. Carlos Lopes, Mkurugenzi Mtendaji wa Kamisheni ya Umoja wa Mataifa ya Afrika (UNECA);
Waheshimiwa Mawaziri;
Waheshimiwa Wageni Waalikwa;
Mabibi na Mabwana:
Shukrani
Nakushukuru sana Mheshimiwa Mwenyekiti kwa kunipa fursa hii adhimu ya kusema maneno machache na kuwaaga Waheshimiwa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Nchi Wanachama wa Umoja wa Afrika. Kuaga wenzako uliowazoea na kushirikiana nao vizuri kwa muda mrefu si jambo rahisi hata kidogo.
Mheshimiwa Mwenyekiti;
Kwangu mimi hii ni siku yenye hisia mchanganyiko, upande mmoja ni siku ya furaha kwamba nimeweza kupata bahati ya kuwaaga viongozi wenzangu na marafiki tuliofanya kazi nao kwa upendo na ushirikiano. Wapo baadhi ya wenzetu ambao hawakuweza kupata bahati hii.
Upande mwingine ni siku ya huzuni kwa sababu kuagana na watu uliowazoea na hata kufikia kuwa familia yangu katika medani ya siasa Barani Afrika ni jambo gumu kwa mwanasiasa kama mimi. Nimekuwa sehemu ya familia hii kwa takribani miaka 20 sasa. Miaka 10 nikiwa Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa wa Tanzania, na miaka 10 nikiwa Rais wa nchi yetu.
Mheshimiwa Mwenyekiti;
Nilichaguliwa kuwa Rais wa nchi yangu kwa mara ya kwanza mwaka 2005 na mara ya pili mwaka 2010. Kwa mujibu wa Katiba yetu ifikapo Oktoba, 2015, nitakuwa nimemaliza kipindi changu cha pili na cha mwisho. Uongozi wangu utakuwa umefikia ukomo na baada ya uchaguzi utakaofanyika tarehe 25 Oktoba, 2015, Tanzania itapata Rais mpya. Mimi nitajiunga na wananchi wenzangu kujenga nchi yetu.
Naisubiri siku hiyo kwa hamu. Narufahi kwamba nami nashiriki katika kudumisha mila na desturi nzuri ya Marais wa nchi yetu kuongoza kwa kipindi maalum kisha kustaafu na mwingine kuchaguliwa kidemokrasia. Utaratibu huu ulioanza wakati wa Rais wetu wa Kwanza Mwalimu Julius Nyerere, umeheshimiwa na kuendelezwa na Rais wa Pili Mheshimiwa Ali Hassan Mwinyi na Rais wa tatu Mheshimiwa Benjamin Mkapa. Mimi naudumisha.
Mchango wa Tanzania kwa Miaka 10
Waheshimiwa Wakuu wa Nchi;
Leo ninapowaaga naona fahari kwamba katika kipindi cha miaka 10 iliyopita, Tanzania imeendelea kuwa mwanachama mwaminifu na mtiifu wa Umoja wa Afrika. Tumeheshimu na kutekeleza misingi, malengo na madhumuni ya Umoja wa Afrika. Tumetekeleza kazi zote tulizopewa kufanya.
Nawashukuru kwa heshima mliyonipatia mimi na nchi yangu kushiriki na hata kuongoza baadhi ya shughuli za Umoja wa Afrika katika kipindi cha miaka kumi iliyopita. Nimewahi kuwa Mwenyekiti wa Umoja wa Afrika mwaka 2008, Mwenyekiti wa Kamati ya Wakuu wa Nchi kuhusu Mabadiliko ya Tabia Nchi (2012 – 2014), Mjumbe wa Kamati ya Uongozi ya NEPAD na Mjumbe wa Baraza la Amani na Usalama la Afrika.
Ninyi wenzangu ndiyo mnaojua zaidi kama tulitekeleza majukumu yetu kwa ufanisi wa kiasi gani. Hata hivyo napenda kuwahakikishia kuwa tulifanya kila tuwezavyo kukidhi matarajio yenu na ya Umoja wetu. Kama lipo jambo ambalo hatukulifanya vizuri ninawaomba radhi. Napenda mjue hata hivyo, kuwa haikuwa kwa makusudi, bali tulitatizwa na mambo yaliyokuwa nje ya uwezo wetu.
Miongoni mwa mambo ambayo tumeyaweka katika kumbukumbu zetu za mchango wa Tanzania kwa Umoja wa Afrika na Bara letu katika fursa mbalimbali za uongozi tulizopewa ni pamoja na yafuatayo:-
(a) Kuanzishwa kwa ushirikiano wa kiuchumi baina ya UA na India na Uturuki;
(b) Kuongoza Operesheni ya Kikosi cha Kulinda Amani cha Umoja wa Afrika kilichomuondoa Muasi Kanali Mohamed Bakar kule Anjoauni na kulinda umoja na nchi ya Comoro;
(c) Tulisimama kidete kupinga kudhalilishwa kwa viongozi wa Afrika walio madarakani na Mahakama za Nje ( Universal Jurisdiction);
(d) Tulishiriki katika kutafuta ufumbuzi wa migogoro iliyotokea Kenya na Ivory Coast;
(e) Katika kipindi chetu cha uongozi wa CAHOSCC tumeweza kufanikisha Bara letu kuwa na Climate Change Concept Paper and Climate Action Plan.
(f) Tumepata fursa ya kuwa wenyeji wa Mahakama ya Watu na Haki za Binadamu ya Umoja wa Afrika na Bodi ya Ushauri dhidi ya Rushwa ya Umoja wa Afrika.
(g) Pamoja na viongozi wengine tumeshiriki katika kuanzishwa kwa Umoja wa Viongozi wa Afrika wa Kupambana na Malaria na kuwa Mwenyekiti wake wa Kwanza.
Afrika Imepiga Hatua za Kuridhisha
Waheshimiwa Wakuu wa Nchi;
Ninapowaaga siku ya leo, nafarijika sana kuona kuwa Umoja wa Afrika unazidi kuimarika na bara letu la Afrika linazidi kusonga mbele kwa kasi kubwa katika kujiletea maendeleo ya kiuchumi na kijamii. Afrika ya leo si ile ya miaka 10 iliyopita. Ukiacha nchi au maeneo machache katika baadhi ya nchi hali ya amani na usalama barani mwetu ni ya kuridhisha sana. Demokrasia imezidi kuota mizizi na utawala bora unazidi kustawi. Vile vile muelekeo ni mzuri kwa upande wa haki za binadamu, utawala wa sheria na mapambano dhidi ya rushwa.
Katika miaka kumi hii, tumeshuhudia pia kuimarika kwa uchumi barani Afrika. Kasi ya ukuaji wa uchumi ni nzuri ambapo hivi leo nchi 6 kati ya 10 zinazokua kwa kasi zaidi duniani ziko barani Afrika. Hali kadhalika biashara baina ya nchi za Afrika inaendelea kuongezeka kutokana na kuimarika kwa Jumuiya za Kikanda.
Uwezekano wa kutimia kwa ndoto ya kuwepo kwa Jumuiya ya Uchumi ya Afrika umepata uhai mpya baada ya tukio la Sham El-Sheikh, Misri tarehe 10 Juni, 2015. Kusainiwa kwa Mkataba wa kuunda ukanda huru wa biashara unaoanzia Cape Town hadi Alexandria unaohusisha nchi 26 za Jumuiya tatu za COMESA, EAC na SADC ni jambo linalostahili pongezi ya Umoja wa Afrika. Kama Jumuiya za ECOWAS na ECCAS nazo zitaungana kuanzisha ukanda wake na baadae kuungana na ukanda huu The African Economic Community itakuwa imezaliwa kama ilivyokusudiwa katika The Lagos Plan of Action ya mwaka 1981.
Mheshimiwa Mwenyekiti;
Jambo lingine linalonipa faraja na matumaini makubwa kuhusu hatma ya Bara letu ni kule kutambuliwa kwa uwezo wa wanawake hivyo kushirikishwa na kupewa fursa stahiki za uongozi katika Serikali, taasisi za kikanda na kimataifa na biashara. Bahati nzuri wanawake wamethibitisha kuwa na uwezo sawa na wanaume na wakati mwingine hata kuzidi. Mifano ya wanawake hao ni mingi. Bahati nzuri wanawake wakipewa nafasi na kuwezeshwa wanaweza. Naomba tuendelee kuwaamini wanawake wetu na kuwapa nafasi. Mimi naamini katika mikono ya wanawake Afrika itakuwa katika mikono salama.
Afrika Bado Inayo Changamoto
Mheshimiwa Mwenyekiti;
Kwa kuelezea matumani yangu kuhusu hali ya Afrika na nchi zetu, sina maana kuwa mambo ni mazuri sana na kazi imekwisha. La hasha. Bado ipo kazi kubwa ya kufanya mbele yetu. Afrika bado ina nchi nyingi na watu wengi walio maskini sana duniani. Watu wengi wanakufa kwa maradhi yanayozuilika au kutibika, na upatikanaji wa huduma za msingi bado uko chini.
Hivyo basi, kazi ya kukuza uchumi na kupunguza umaskini lazima iendelee kupewa kipaumbele cha juu. Bado tuendelee kuimarisha utawala bora hususan tuongeze nguvu katika mapambano dhidi ya rushwa na maovu katika jamii. Tuendelee kuimarisha demokrasia, utawala wa sheria na kulinda haki za binadamu. Tuendeleze bila kuchoka, jitihada za kuzuia na kutatua migogoro Barani Afrika. Inatupotezea muda mwingi wa kufanya mambo ya maana.
Mheshimiwa Mwenyekiti;
Kila ninaposoma Agenda ya Umoja wa Afrika ya 2063 (AU Agenda 2063), na Mpango wa Miaka 10 ya Kwanza ya Utekelezaji wa Mpango huo (First Ten Year Implementation Plan of the Agenda) nafarijika kuwa tunatambua changamoto zinazotukabili pamoja na fursa na uwezo wa kuzipatia ufumbuzi. Naamini tukitekeleza kwa ukamilifu Agenda ya AU ya mwaka 2063 ile ndoto yetu ya Afrika yenye umoja na maendeleo itatimia.
Hitimisho
Mheshimiwa Mwenyekiti;
Mwisho, napenda kurudia kukushukuru kwa kunipa fursa hii ya kuagana na viongozi wenzangu. Nawashukuru nyote kwa ushirikiano mlionipa katika kipindi chote nilichokuwa nanyi ndani ya Umoja wa Afrika. Naondoka nikiwa mwenye furaha kwamba Afrika ipo katika mikono salama. Mliobaki mnatosha kulitoa Bara la Afrika hapa tulipo sasa hadi mbele zaidi kwenye neema tele.
Kwa kumalizia nawaomba mumpe mrithi wa nafasi yangu ushirikiano mkubwa kama mlionipatia mimi na hata kuzidi. Ni matumaini yangu kuwa Watanzania tutachagua kiongozi mzuri atakayeongoza vizuri nchi yetu. Kiongozi ambae ataendelea kutoa kipaumbele cha juu kwa masuala ya Afrika pamoja na uanachama na ushiriki wetu katika Umoja wa Afrika. Haya ni miongoni mwa misingi mikuu ya Sera ya Mambo ya Nje ya Tanzania tangu uhuru mpaka sasa. Mimi ninaondoka, lakini Tanzania mliyoizoea na kuijua itabaki.
Mungu Ibariki Afrika,
Mungu Ibariki Tanzania!
Asanteni kwa kunisikiliza na Kwaheri ya Kuonana!

- May 26, 2015
HOTUBA YA MHESHIMIWA RAIS WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA DKT JAKAYA MRISHO KIKWETE KATIKA UFUNGUZI WA MKUTANO MKUU WA CHAMA CHA WALIMU TANZANIA TAREHE 26 ME...
Soma zaidiHotuba
Ndugu Gratian Mukoba, Rais wa Chama cha Walimu Tanzania (CWT) na Rais wa Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi Tanzania, TUCTA;
Mhe. Shukuru Kawambwa, Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi;
Mheshimiwa Gaudencia Kabaka, Waziri wa Kazi na Ajira;
Mheshimiwa Celina Kombani, Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais – Menejimenti ya Utumishi wa Umma;
Mheshimiwa Hamis Majaliwa, Naibu Waziri – TAMISEMI;
Mheshimiwa Margaret Sitta, Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ustawi wa Jamii;
Mhe. Felix Daud Ntibenda, Mkuu wa Mkoa wa Arusha;
Ndugu Msulwa, Katibu Mkuu wa Chama cha Walimu Tanzania;
Ndugu Nicholaus Mgaya, Katibu Mkuu wa Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi Tanzania, (TUCTA);
Ndugu Ezekiel Oluoch, Naibu Katibu Mkuu wa Chama cha Walimu Tanzania;
Ndugu Wajumbe wote wa Mkutano Mkuu wa Taifa wa Chama cha Walimu Tanzania;
Mke wangu Mama Salma Kikwete;
Ndugu Walimu;
Wageni waalikwa;
Shukurani
Nakushukuru sana Rais wa Chama cha Waalimu Tanzania (CWT) Ndugu Gratian Mukoba na viongozi wenzako wa CWT kwa kunialika na kunipa heshima kubwa ya kufungua Mkutano wenu Mkuu. Nawapongeza kwa maandalizi mazuri ya mkutano. Kufanikisha mkutano wa Wajumbe 1,200 si kazi ndogo hata kidogo. Hivyo basi unapofanikiwa ni jambo linalostahili pongezi. Hongereni sana. Pia nikushukuru sana Mkuu wa Mkoa wa Arusha na wananchi wote wa Mkoa huu kwa mapokezi mazuri na kwa kukubali kuwa wenyeji wa mkutano huu. Mmekuwa wenyeji wema. Hongereni sana.
Pongezi kwa CWT
Ndugu Rais
Ndugu Waalimu;
Natoa pongezi kwa viongozi wa Chama cha Waalimu wanaomaliza muda wao kwa kazi kubwa nzuri waliyofanya na kwa mafanikio makubwa yaliyopatikana na yanayoendelea kupatikana. Mmeifanya vyema kazi ya kutetea haki na maslahi ya walimu. Tumejionea jengo kubwa na zuri la kitega uchumi lililojengwa Ilala, Dar es Salaam. Jengo hili lijulikanalo kama Mwalimu House limependezesha sana eneo la Ilala na jiji la Dar es Salaam. Kama kwamba hiyo haitoshi hivi karibuni tumepokea habari nyingine njema za kuanzishwa kwa Benki ya Waalimu itakayojulikana kama Mwalimu Bank. Mafanikio haya na mengine mengi ambayo sikuyataja, yanafanya CWT kuwa moja ya vyama vya wafanyakazi mahiri na makini nchini licha ya kuwa ndicho Chama kikubwa kuliko chote chote. Hongereni sana viongozi na wanachama wa CWT.
Risala ya Chama cha Waalimu
Ndugu Rais
Ndugu Waalimu;
Nimeisikia na kuipokea risala yenu nzuri mliyoiwasilisha kwangu muda mfupi uliopita. Nawashukuru kwa risala yenu imeainisha mafanikio, mliyopata, changamoto zinazowakabili na muhimu zaidi mmetoa ushauri muafaka kuhusu namna bora ya kuzitatua. Ni risala inayotoa fursa ya kujadiliana na kushirikiana na yenye lengo la kujenga na kuimarisha mahusiano ya pande zetu mbili. Ni risala inayoonyesha kuwepo kwa kushirikiana, kustahamiliana na kuaminiana kati ya walimu na Serikali yao. Sisi sote inatupa funzo kuwa, pale panapokuwepo na uhusiano mzuri na ushirikiano kati ya walimu na Serikali, haliharibiki jambo. Hata yale mambo ambayo pengine yalionekana magumu, tumeweza kuyatatua kwa pamoja. Hatuna budi kuendeleza hali hii ya mahusiano kati yetu siku zote.
Risala yenu pamoja na mambo mengine imeibua masuala tisa. Masuala hayo ni kuhusu madaraja ya walimu; posho ya kufundishia; madeni ya walimu; uhaba wa nyumba za walimu; utoaji wa elimu bora; mabadiliko ya mafao ya pensheni; ukaguzi wa shule; Sekta ya Elimu katika BRN; na mapungufu ya kiutendaji katika kuhudumia walimu. Mambo yote haya ni ya msingi sana na yanastahili kupatiwa majawabu muafaka. Yapo ya kisheria, ya kisera na ya kimfumo. Napenda kuwahakikishia kuwa nimeyapokea na tutayafanyia kazi mambo yote kama kawaida yetu. Kama mlivyosema katika risala yenu, baadhi ya mambo yanahitaji kukaa mezani kujadiliana na kushauriana zaidi. Tutafanya hivyo. Nitajitahidi kwa yale yanayowezekana niwe nimeyatatua kabla ya kumaliza muda wangu wa uongozi. Kwa yale ambayo yanahitaji muda mrefu, nitahakikisha kuwa kabla ya kukabidhi ofisi niwe nimeyawekea msingi mzuri ili iwe rahisi kwa Rais ajaye baada yangu kuyakamilisha.
Hatua za Serikali Kushughulikia Madai ya Waalimu
Ndugu Rais na
Ndugu Waalimu;
Kwa uchache, nitapenda kuzungumzia hatua ambazo Serikali imechukua na inazoendelea kuchukua kushughulikia madai ya waalimu. Kama mlivyoainisha katika risala yenu, Serikali ninayoingoza imefanya jitihada kubwa sana kupanua fursa za watoto wetu kupata elimu na sasa tumeelekeza nguvu zetu katika kuboresha elimu inayotolewa. Kwa ajili hiyo, tumeongeza shule za msingi kutoka 14, 257 mwaka 2005 hadi 16, 343 mwaka 2014, na kuongeza idadi ya wanafunzi kutoka milioni 7.54 hadi milioni 8.23. Shule za Sekondari, zimeongezeka kutoka 1,745 mwaka 2005 hadi 4,576 mwaka 2014 na kuongeza wanafunzi kutoka 524, 325 hadi milioni 1.8 kati ya mwaka 2005 na 2015. Hali kadhalika, idadi ya vyuo vikuu imeongezeka kutoka 26 mwaka 2005 hadi 52 mwaka 2015, na kufanya idadi ya wanafunzi kuongezeka kutoka 40, 719 hadi 200, 986 katika kipindi hiko.
Sote tunafahamu kuwa shule na elimu haikamiliki pasipo na waalimu na pasipokuwa vitabu na vifaa vya kujifunzia na kufundishia. Upanuzi huo mkubwa ulilazimu kupanua vyuo vya ualimu. Idadi ya vyuo vya ualimu vya cheti na stashahada vimeongezeka kutoka 52 mwaka 2005 hadi 126 mwaka 2015. Upanuzi huu ukiongeza na ule wa vyuo vikuu umewezesha kuongeza idadi ya waalimu wa msingi na sekondari kutoka 153, 767 mwaka 2005 hadi 301,960 mwaka 2015. Hii imewezekana kutokana pia na uamuzi wetu wa kutoa mikopo kwa wanafunzi waliochagua kusomea ualimu, na kuwahakikishia ajira pale wanapomaliza masomo yao.
Serikali imefanya jitihada pia za kuboresha maslahi ya waalimu kadri uwezo uliporuhusu. Hatukuweza kutoa nyongeza kubwa kwa wakati mmoja lakini tumeongeza mara kwa mara. Kati ya 2005 – 2015 kumekuwepo na ongezeko la kianzio cha mshahara cha Mwalimu mwenye cheti, Mwalimu mwenye Stashahada ya Ualimu na wale wenye elimu ya shahada. Watumishi wa kada nyingine za Serikali wenye elimu ya viwango hivyo, huanza na mshahara wa chini ya ule wa waalimu. Nafahamu kuwa kiwango hiki bado hakitoshi, lakini ukweli ni kuwa hakuna upungufu wa dhamira kwa upande wa serikali, ila kikwazo ni kutokuwepo na uwezo mkubwa kimapato kwa upande wa Serikali. Ukizingatia kuwa walimu ni asilimia 52.7 ya watumishi wa Serikali, hivyo, ongezeko katika mshahara wa waalimu linaleta mabadiliko makubwa sana katika bajeti ya Serikali. Kwa ajili hiyo hatukuweza kutoa nyongeza kubwa kwa wakati mmoja lakini tumeongeza mara kwa mara mpaka tumefikia hapa tulipo leo. Na katika bajeti hii tutaongeza tena. Hivyo nitawaacha mahali penye unafuu ukilinganisha na tulikotoka.
Tumeendelea pia kushughulikia kero nyingine za waalimu ikiwemo madeni na madai yenu. Deni la waalimu lililopokelewa lilikuwa shilingi bilioni 53, 185,440,406 lililohusu waalimu 70,668. Baada ya uhakiki uliofanyika kwa kuhusisha Ofisi ya Mkaguzi wa Ndani wa Serikali, jumla ya shilingi bilioni 23, 233, 654, 025 zililipwa kwa waalimu 29,243. Serikali imeshatoa ahadi ya kulipa ifikapo mwezi Agosti mwaka huu madai mengine ya waalimu 7,169 yenye jumla ya shilingi bilioni 9, 285,283,600 ambayo uhakiki wake umekamilika. Aidha, madai ya walimu 30,807 yenye jumla ya shilingi bilioni 17,346, 593, 468 hayakuweza kulipwa kutokana na kukutwa na dosari za msingi za kihasibu na kiutaratibu. Wametakiwa kurekebisha kasoro zilizoonekana.
Jambo la kururahisha katika ukaguzi na uhakiki huo wa madeni ni kule kushirikishwa kwa Chama cha Walimu. Kwa pamoja tumethibitisha palipokuwa sahihi na pasipokuwa sahihi. Inasikitisha kupata taarifa za kuwepo vitendo vya udanganyifu vinavyofanywa na baadhi ya watumishi wa Serikali na walimu vinavyochangia kuzalisha madeni bandia. Vitendo vyao hivyo ndivyo vinavyofanya madai yachukue muda mrefu kulipwa kwa kulazimika kuweko na uhakiki wa ziada. Naungana nanyi katika pendekezo lenu la kutaka watumishi hawa kuwajibishwa, maana ndio mzizi wa fitna kati ya waalimu na Serikali. Nimekwishaeleza mamlaka husika kufanya hivyo bila ajizi.
Ndugu Rais na
Ndugu Waalimu;
Tumeshughulikia lile dai kubwa la waalimu la marekebisho ya muundo wa utumishi wa waalimu (Teacher’s Service Scheme). Tumepitisha Muundo mpya wa Waalimu ambao umeanza kutumika toka Julai 1, 2014. Nimesikia kuwa utekelezaji wake haukuweza kuanza kote nchini mara moja, napenda kuwahakikishia kuwa katika mwaka ujao wa fedha tutahakikisha kuwa Waalimu wote watakuwa wamefikiwa. Sambamba na hili la Muundo, tumekwishapeleka Bungeni Muswada wa Sheria ya kuanzisha Tume ya Utumishi wa Waalimu (Teachers Service Commission) ambao tayari umesomwa kwa mara ya kwanza. Mawasiliano yanaendelea na Ofisi ya Spika ili Muswada huo ujadiliwe katika Bunge hili la Bajeti. Tunafanya hivyo pia kwa Muswada wa kuanzisha Bodi ya Taifa ya Taaluma ya Waalimu (Teachers Proffessional Board). Nimepokea maoni yenu ya kutaka uangaliwe uwezekano wa Bodi hii kuwa sehemu ya Tume ya Utumishi wa Waalimu badala ya kuwa na vyombo viwili tofauti. Hoja yenu ya kutaka kupunguza utitiri wa vyombo vinavyoshughulikia maslahi ya waalimu ina mashiko. Ushauri wenu umepokelewa, tutautafakari na kuufanyia kazi.
Napenda kuwahakikishia kuwa madai yenu mengine ikiwemo nyumba za waalimu, motisha kwa waalimu, mazingira ya kufanyia kazi, mafunzo vikokotoo vipya vya pensheni na masuala mengine mliyoibua katika risala yenu tutayashughulikia na tutawapeni taarifa. Pia nitaelekeza mamlaka zinazohusika kukutana na uongozi mpya wa Chama chenu baada ya uchaguzi mkuu wenu kuyajadili masuala hayo na kuyatafutia majawabu.
Napenda kusisitiza kwenu kwamba mimi na wenzangu Serikalini tunawathamini sana na kuwapenda waalimu kwa dhati ya mioyo yetu. Sisi tunatambua nafasi ya Mwalimu katika maendelo ya mtu binafsi na taifa kwa jumla. Hakuna badala yake. Hivyo basi tunatambua wajibu wetu wa kuwawekea mazingira mazuri ya kufanyia kazi. Tumefanya jitihada kutimiza wajibu wetu. Pale panapojitokeza matatizo yoyote si makusudio yetu. Kitendo cha makusudi na anapojulikana mtu huyo atawajibishwa ipasavyo. Wakati mwingine matatizo yanayowakuta hutokana na watu wetu kuelemewa na mzigo kutokana na ukubwa wa kada yenu katika utumishi wa umma ambapo ni asilimia 52. 7.
Kwa ukubwa huu, mnaweza kuelewa ni changamoto kiasi gani zinazojitokeza katika kushughulikia masuala yenu. Ndio sababu hatuchoki kutafuta muundo bora wa kushughulikia matatizo yenu. Ninachoomba kutoka kwenu ni uvumilivu na uelewa wenu na kuwaomba mtupime kwa dhamira yetu na utayari wetu wa kuyashughulikia madai yenu na si kwa idadi ya changamoto zinazojitokeza.
Uchaguzi Mkuu wa CWT
Ndugu Rais na
Ndugu Waalimu;
Moja ya Agenda kubwa ya Mkutano wa leo ni Uchaguzi Mkuu. Nitumie fursa hii kuwapongeza viongozi mliochaguliwa katika ngazi ya Tawi, Wilaya na Mkoa ambao kwa pamoja mmeunda Mkutano Mkuu huu. Nawapongeza kwa kuuendesha uchaguzi wa ngazi za chini vizuri maana natambua kuwa haikuwa kazi ndogo kutokana na ukubwa wa nchi yetu, na hamasa ya waalimu kisiasa.
Nawapongeza sana viongozi wote waliojitokeza kugombea nafasi za uongozi wa ngazi ya Taifa. Naamini nyote mnatosha kwa nafasi mnazoomba. Naomba mkumbuke kuwa si kila mtu aliyeomba atashinda. Nafasi si nyingi kiasi hicho. Hivyo basi, wale ambao kura hazitatosha safari hii, watumie uzoefu walioupata katika uchaguzi huu kujinoa zaidi kwa chaguzi za miaka ijayo. Haitakuwa vizuri iwapo wale ambao hawatafanikiwa kushinda, wataendeleza nongwa na kuwa chanzo cha kuvunja mshikamano mzuri mlionao katika Chama cha Walimu. Kama nilivyosema awali, sisi sote tunawaangalia waalimu kama kioo cha maadili na upevu katika jamii yetu. Naamini hamtatuangusha.
Nawapongeza na kuwashukuru sana viongozi wanaomaliza muda wao kwa ushirikiano wenu mkubwa mliotupatia sisi katika Serikali katika kipindi chenu cha uongozi. Kwa pamoja tumeweza kutatua changamoto nyingi za waalimu na kujenga madaraja kati yetu yaliyozaa mahusiano mazuri ambayo ndio msingi wa kutatua madai ya waalimu kila yalipojitokeza. Ni matumaini yetu kuwa viongozi watakaochaguliwa, wataendeleza pale mlipoishia na muhimu zaidi uhusiano mzuri na ushirikiano na Serikali. Sisi tunaahidi kuwapa kila aina ya ushirikiano unaostahili. Ni jambo lenye maslahi kwetu sote.
Hitimisho
Ndugu Rais na
Ndugu Waalimu;
Hii ni fursa yangu ya mwisho kukutana na kuzungumza na viongozi wa CWT nikiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Baada ya hapo nitakuja kumsindikiza Mwalimu mwenzenu akija mkutanoni. Hivyo, sina budi kutumia fursa hii pia kuagana nanyi na kupitia kwenu kuagana na Waalimu wote nchini. Nirudie tena kuwashukuru sana kwa mchango wenu mkubwa katika maendeleo ya elimu nchini. Kwa kweli mnajitoa sana na mnafanya kazi kubwa ambayo inaonekana na wote. Napenda kuwatia moyo kuwa msilegeze uzi bali muendelee na moyo na wito wenu huo. Nitawakumbuka sana waalimu katika maisha yangu baada ya kustaafu uongozi, kwa msaada wenu na ushirikiano wenu. Nimewapenda, ninawapenda na nitaendelea kuwapenda ‘Shemeji’ zangu.
Nawatakia Uchaguzi Mkuu na Mkutano Mkuu mwema.
Akhsanteni kwa kunisikiliza!

- May 25, 2015
HOTUBA YA MHE. DKT. JAKAYA MRISHO KIKWETE, RAIS WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA, AKIFUNGUA MKUTANO WA NNE WA MABALOZI WA TANZANIA TAREHE 25 MEI, 2015 KATIKA...
Soma zaidiHotuba
Mhe. Bernard Kamillius Membe (Mb), Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa;
Mhe. Mahadhi Juma Maalim (Mb), Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa;
Balozi Liberata Mulamula, Katibu Mkuu, Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa;
Balozi Hassan Simba Yahya, Naibu Katibu Mkuu, Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa;
Mabalozi wote;
Wakuu wa Taasisi zilizo chini ya Wizara;
Wageni waalikwa;
Mabibi na Mabwana;
Shukran na Pongezi
Nakushukuru wewe Mheshimiwa Waziri na Viongozi wenzako wa Wizara kwa kunialika kushiriki ufunguzi wa Mkutano wa Nne wa Mabalozi wa Tanzania. Mkutano huu ni wa pili katika awamu yangu na wa nne baada ya ule wa tatu uliofanyika Zanzibar, mwaka 2008. Nafarijika kuona kuwa Wizara imeendelea na utaratibu huu mzuri wa kuwakutanisha Mabalozi kujadili utekelezaji wa Sera ya Mambo ya Nje ya nchi yetu. Utaratibu huu unatoa fursa ya kujitathmini, kupeana mrejesho na kuweka malengo na mikakati mipya. Ni matumaini yangu kuwa utaratibu huu mzuri utaendelezwa na Serikali zinazofuatia.
Kauli Mbiu
Mheshimiwa Waziri;
Nimeipenda kauli mbiu ya Mkutano inayosema “Diplomasia ya Tanzania kuelekea Dira ya Taifa ya Maendeleo 2025”. Imebeba ujumbe muafaka hasa ukizingatia kuwa tuko katika hatua za mwisho za kukamilisha maandalizi ya kuanza Mpango wa Pili wa Maendeleo wa Miaka 5. Kama mjuavyo Mpango huu ni sehemu ya utekelezaji wa Mpango wa Muda Mrefu wa miaka 25 unaotekelezwa kwa Mipango mitatu ya muda wa kati wa miaka mitano kila mmoja kwa Dira ya Maendeleo ya Taifa. Shabaha kuu ya Dira hiyo ni kuifanya Tanzania kuwa nchi ya kipato cha kati ifikapo mwaka 2025.
Kama tunavyofahamu, Sera ya Mambo ya Nje ni muendelezo wa sera ya ndani, hivyo ni jambo la busara kuitana na kukumbushana nafasi na wajibu wa Wizara katika kuchangia jitihada za Serikali kufikia lengo hilo. Nimefurahishwa na mada mlizochagua na watu mliowaalika. Naamini mkutano huu utakuwa na mafanikio makubwa.
Hali ya Dunia
Waheshimiwa Mabalozi;
Sote tunafahamu kuwa tangu kuzinduliwa kwa Sera ya sasa ya Mambo ya Nje, mwaka 2004, mambo mengi yamebadilika. Hii ni kweli kwa hapa nchini na hata duniani. Mafanikio mengi yamepatikana na changamoto kubwa na ndogo zimejitokeza. Kuyumba kwa uchumi wa dunia mwaka 2002 na 2009 kumekuja na athari nyingi hususan kwa nchi maskini na zinazoendelea. Misaada ya maendeleo kutoka nchi tajiri imepungua na masoko ya bidhaa zetu kama pamba, tumbaku na dhahabu yamekuwa yanayumba. Mabadiliko ya tabianchi ni changamoto nyingine ambayo inatishia ustawi wa nchi maskini. Bado majadiliano na nchi zilizoendelea yanaendelea ili watimize wajibu wao wa kihistoria wa kutusaidia kujenga uwezo wetu wa kukabiliana na athari zake. Hivi sasa sote tumeweka matumaini yetu kwenye mkutano wa Paris, Desemba 2015 kupata mkataba ulio bora. Tusipofanikiwa itakuwa hatari kubwa. Tanzania iendelee na jitihada zake kama tulivyofanya wakati wa kuongoza Kamati ya Marais wa Umoja wa Afrika kuhusu Mabadiliko ya Tabia Nchi (CAHOSCC).
Ndugu Mabalozi;
Vitendo vya uhalifu wa kimataifa na ugaidi navyo vinazidi kushamiri duniani na kutuathiri hata sisi. Zamani tulikuwa tunasikia mambo hayo yakitokea nchi za mbali, lakini, hivi sasa nasi ni wahanga wa uhalifu huo. Mitandao ya kimataifa ya biashara ya dawa za kulevya inaangamiza vijana wetu. Hivyo basi lazima tushiriki katika mapambano dhidi ya biashara na matumizi ya dawa za kulevya. Ndovu wetu wanatishiwa kumalizwa na majangili na washirika wa mitandao ya kimataifa; na matishio ya ugaidi yanaviweka vyombo vya ulinzi na usalama kuwa katika hali ya tahadhari wakati wote. Majawabu ya changomoto hizi hayawezi kupatikana kwa juhudi za nchi moja peke yake, yanahitaji ushirikiano na jumuiya ya kimataifa. Mabalozi mnao wajibu wa kuendelea kutafuta wabiya wa kushirikiana nasi katika mpambano haya.
Utandawazi unaostawishwa na maendeleo ya sayansi na teknolojia umeleta fursa na una changamoto zake nyingi pia. Ukweli huo ndiyo iliyotufanya kutunga Sheria ya Kudhibiti Uhalifu wa Mitandaoni (Cyber Crime Act) hivi karibuni. Vilevile, Jumuiya za Kikanda zinazidi kuimarika katika kila kona ya dunia. Tanzania ni mwanachama wa EAC na SADC. Ushiriki wetu umekuwa na tija na kuleta maslahi ya kiuchumi na kibiashara. Hata hivyo hatuna budi kujituma na kujipanga vizuri zaidi ili tuweze kunufaika zaidi.
Mafanikio ya Diplomasia ya Tanzania
Waheshimiwa Mabalozi;
Pamoja na mabadiliko hayo na changamoto zake, inatia moyo kuona diplomasia ya nchi yetu imeendelea kustawi. Tanzania ina jina kubwa kikanda na kimataifa kuliko nguvu zetu za kiuchumi na kijeshi. Kwa ajili hiyo tumekuwa tunaaminiwa na kushirikishwa katika shughuli na mambo mbalimbali. Tumeendelea kuwa sauti ya watu wasio na sauti na wanyonge na kuwa kimbilio lao. Ni kwa ajili hiyo tumeaminiwa katika majukumu muhimu na Jumuiya za kikanda na kimataifa hususan AU, SADC na UN.
Jambo lingine la kujivunia sote kuhusu diplomasia yetu ni kuwa na uhusiano mzuri na nchi jirani na mashirika ya kimataifa. Nimeingia madarakani Tanzania ikiwa haina adui, na naondoka bila adui. Kwa jumla tumefanikiwa kuimarisha udugu, urafiki na ushirikiano na majirani zetu wote. Pale palipotokea upepo mbaya, tumetumia njia za kidiplomasia kuondoa tofauti zetu tukiongozwa na hekima ya wahenga kuwa: “unaweza kuchagua rafiki lakini huwezi kuchagua jirani”.
Hali kadhalika, tumepokea wageni wengi waliofanya ziara nchini ikiwemo marais wa mataifa makubwa duniani yakiwemo Marekani na China. Ziara hizo ziliitangaza nchi yetu na kufungua milango ya fursa kwa nchi yetu ya kunufaika kwa misaada ya maendeleo, biashara na vitega uchumi.
Vilevile, tumepanua wigo wa mahusiano kwa kuongeza marafiki na wabia wengine wa maendeleo. Katika kipindi cha miaka 10 nchi 6 za Brazil, Oman, Uturuki, Qatar, Umoja wa Falme za Kiarabu (UAE) na Namibia zimefungua ubalozi nchini Tanzania. Aidha, nchi 16 za Morocco, Malta, Equador, Montenegro, Azerbaijan, Bosnia na Herzegovina, Moldova, Saint Vincent na Grenadies, Fiji, Paraguay, Kosovo, Geogia, Kyrgyzstan, Visiwa vya Marshall, Visiwa vya Solomon, na Kazakhstan zimeanzisha uhusiano wa kidiplomasia na nchi yetu. Nchi yetu pia imefungua Ofisi za Ubalozi katika nchi 7 za Brazil, Uholanzi, Malaysia, Oman, Kuwait, UAE na Comoro. Kama hali itaruhusu tunatarajia kufungua Ubalozi nchini Uturuki na Algeria kabla ya kumaliza kipindi changu cha uongozi.
Mahusiano haya mapya na yale ya zamani ambayo tumeendelea kuyapalilia yamefungua fursa nyingi kwa nchi yetu na watu wetu. Mahusiano haya yametuwezesha kupata mikopo na misaada ya kimaendeleo ambayo imeziongezea Serikali zetu mbili: Serikali ya Jamhuri ya Muungano na Serikali ya Mapinduzi Zanzibar uwezo wa kutekeleza miradi ya maendeleo. Tunapojisifu leo hii kwa hatua kubwa katika kujenga miundombinu msingi ya mawasiliano, uchukuzi na nishati na upanuzi na uboreshaji mkubwa wa huduma za jamii kuna michango muhimu ya wadau wa nje. Haya ni matokeo chanya kazi yenu nzuri ya kuyajenga na kuyastawisha mahusiano mazuri na mataifa. Miradi mikubwa ya uzalishaji wa umeme, barabara, bomba la gesi, viwanja vya ndege, mkongo wa taifa ni matokeo ya mahusiano hayo. Nawashukuru sana kwa mchango wenu huo.
Maeneo mawili mapya katika Sera yetu ya Mambo ya Nje katika kipindi cha miaka 10 iliyopita ni ushirikishwaji wa Watanzania waishio ughaibuni (Diaspora) na ushiriki wa Ulinzi wa Amani (Peace-keeping Operation). Ni katika kipindi hiki tumetunga Sera ya Diaspora na kuamsha hamasa ya kuwatambua na kuwashirikisha Watanzania wenzetu waishio nje katika gurudunu la maendeleo. Hatukuweza kukidhi haya yao ya uraia pacha lakini tumefanikiwa kuwapa haki mahsusi kwenye Katiba Pendekezwa.
Tumeshiriki katika shughuli za ulinzi wa amani kule Darfur Sudan, Lebanon na DRC chini ya operesheni za Umoja wa Mataifa na Umoja wa Afrika. Aidha, tumeshiriki katika utatuzi wa migogoro katika bara la Afrika ukiwemo ule wa Comoro na kurejesha umoja wa nchi hiyo.
Mpango wa Taifa 2015 – 2020
Waheshimiwa Mabalozi,
Mafanikio niliyoyataja ni sehemu tu ya mafanikio mengi tuliyoyapata katika kutekeleza Sera yetu ya Nje. Nchi yetu iko salama na haina maadui bali marafiki duniani kote. Tumefanikisha kuvutia misaada ya maendeleo, vitega uchumi na biashara, mambo ambayo yamechangia katika jitihada za nchi yetu kukuza uchumi na kupunguza umaskini. Jukumu kubwa lililo mbele yetu ni kutumia fursa zetu kuwa na mahusiano mazuri na mataifa na mashirika ya kimataifa pamoja na ya kijiografia na maliasili yetu kujenga uwezo wetu wa kiushindani kikanda na duniani.
Mheshimiwa Waziri;
Mtakumbuka kuwa, malengo makuu ya Mpango wa Kwanza wa Maendeleo wa Miaka Mitano tunaomalizia ulilenga kuondoa vikwazo vya ukuaji wa uchumi. Shabaha yake ni:
(a) kujenga uwezo wa nchi yetu kukuza uchumi na kuondoa umaskini haraka;
(b) kujizatiti kutumia fursa zilizopo nchini kukuza mahusiano ya kiuchumi baina ya nchi yetu na nyingine katika Jumuiya za Kikanda na Kimataifa;
(c) Kukuza ajira ili kupunguza tatizo la ajira linalowakabili vijana.
Siwezi kusema tumefanikiwa kila kitu, lakini tumepiga hatua ya kuridhisha na tumeonyesha muelekeo mzuri. Hali ya uchumi kwa maana ya viashiria vya uchumi jumla, tupo mahali pazuri. Pato la Taifa limekuwa kwa wastani wa asilimia 7 na kuongezeka kutoka Dola za Kimarekani bilioni 14.4 mwaka 2005 hadi Dola za Kimarekani bilioni 43 mwaka 2015. Hivyo hivyo, pato la wastani la Watanzania nalo limeongezeka kutoka Dola za Kimarekani 375 mwaka 2005 hadi Dola za Kimarekani 944 mwaka 2014.
Katika kipindi cha muongo mzima sasa, makusanyo ya kodi yameongezeka kutoka shilingi billion 177.1 mwaka 2005 hadi shilingi bilioni 800 mwaka 2015. Tumefanikiwa kudhibiti mfumuko wa bei kutoka asilimia 18 mwaka 2011 hadi asilimia 4.5 mwaka huu. Hivi karibuni thamani ya sarafu yetu imekua inapungua dhidi ya dola ya Marekani. Hatuko peke yetu thamani ya dola ya Marekani imepanda dhidi ya sarafu zote duniani.
Katika kipindi hiki pia tumefanikiwa kuboresha miundombinu ya usafirishaji yaani upanuzi na uboreshaji wa bandari, ujenzi wa barabara na uimarishaji wa reli na uzalishaji na usambazaji wa umeme nchini. Aidha, tumerekebisha baadhi ya sheria zilizokuwa zinatukwamisha ili kuboresha mazingira ya uwekezaji. Nimefurahi kuwa katika mkutano huu wahusika watapata fursa ya kuzungumza na Mabalozi kuhusu maeneo hayo. Kwa ujumla, tumeweka msingi mzuri wa ukuaji wa maendeleo ya kiuchumi na kijamii kuelekea mwaka 2025.
Mpango wa Pili wa Maendeleo wa Miaka 5 ambao tunauanza katika mwaka wa fedha ujao, unalenga katika kuhamasisha mapinduzi ya viwanda kwa lengo la kuongeza thamani ya maliasili zetu na bidhaa za kilimo, kujenga uwezo wetu wa biashara ndani na nje ya eneo la Jumuiya ya Afrika Mashariki na kukuza ajira.
Mpango huu unalenga kujenga juu ya mafanikio ya mpango wa kwanza. Hivyo, utekelezaji wa mpango huu unahitaji sana tuvutie vitega uchumi na teknolojia za kisasa nchini kwa lengo la kuchochea mapinduzi ya viwanda vidogo, vya kati na vikubwa. Tukifanikiwa katika haya tutaweza kuitumia vizuri fursa tulizonazo na ile ya kijiografia ya kuzungukwa na soko kubwa.
Ndugu Waziri na Ndugu Mabalozi;
Nchi inawategemea ninyi kutumia nafasi mlizonazo kuvutia wawekezaji zaidi, teknolojia za kisasa na kutafuta masoko ya bidhaa zetu. Hili ni jukumu lenu la msingi katika utekelezaji wa diplomasia ya uchumi. Nawataka muwe wabunifu na makini katika kuwaunganisha wafanyabiashara wa nchini na wenzao wa nje mnakowakilisha nchi yetu.
Katika dunia ya sasa na huko tuendako, usalama na ustawi wetu utategemea zaidi uwekezaji na biashara na si misaada ya maendeleo ambayo imeendelea kuwa isiyotabirika na isiyotosha. Hamna budi sasa kuongeza msukumo kwenye kuvutia watalii, wawekezaji, kutafuta masoko na kusaidia wafanyabiashara wa Tanzania kufanya biashara nje. Ningefarijika sana kama mtajipima na kujisifu kwa uchangiaji wenu kwa uchumi na kuwawezesha wafanyabiashara wetu kujitanua kimataifa.
Zama za sasa haitoshi kujisifu kwa uhodari wa kuandika ripoti na kuhudhuria mikutano. Tujisifu pia kwa kuchangia kukuza uchumi wa nchi. Ni vizuri kujiuliza mtachangia vipi kuwezesha uchumi wetu kukua na hivyo uwezo wa Serikali kuongezeka kipato ili bajeti za balozi ziweze kuongezeka. Kila mtu ajiulize ubalozi wake umechangia nini na kiasi gani? Je, nini kifanyike ili ubalozi huo uweze kuchangia zaidi. Ni matumaini yangu kuwa mkutano huu utatafuta majawabu na maswali haya. Huo ndio mtazamo chanya wa kuelekea nchi ya uchumi wa kati mwaka 2015.
Waheshimiwa Mabalozi;
Mnatakiwa pia kutafuta wabia wapya wa maendeleo na kuimarisha ushirikiano nao. Hawa siyo wengine bali ni mashirika yasiyo ya kiserikali (NGOs) na Watanzania wenzetu waishio nje (Diaspora). Nchi zinazotoa misaada ya maendeleo hupitishia kiasi kikubwa mikononi mwa NGOs. Aidha, mifuko ya misaada ya watu binafsi Bill and Melinda Gates Foundation zinatoa michango muhimu kwa maendeleo ya kiuchumi na kijamii wakati mwingi inazidi hata ile tunayopata kutoka nchi wahisani. Bado ipo nafasi ya kuongeza ushiriki wa taasisi za namna hii kwa maendeleo yetu. Isitoshe taasisi nyingine zina ushawishi mkubwa kwa mashirika ya kimataifa, Serikali na sekta binafsi. Hivyo basi, tukiweza kuimarisha uhusiano na taasisi hizi tutafaidika katika jitihada zetu za kujiletea maendeleo.
Watanzania wanaoishi nje ya nchi nao wanaweza kutoa mchango muhimu. Mazungumzo yangu nao yanaendelea kuzaa matunda. Wengi wameonesha hamasa kubwa ya kushiriki kwenye shughuli mbalimbali za maendeleo nyumbani. Zipo nchi duniani zinazonufaika na diaspora zao na sisi inaweza kuwa hivyo. Tumeanza lakini bado tunahitaji kuongeza juhudi. Mkutano huu uje na mawazo mazuri juu ya nini kifanyike kuwafanya Watanzania walio nje wachangie zaidi ya wafanyavyo sasa. Tuangalie wenzetu hao wanafanya vipi na kuiga yale mazuri tuyafanye.
Uboreshaji wa Maslahi na Mazingira ya Kazi ya Watumishi wa Nje
Mheshimiwa Waziri;
Waheshimiwa Mabalozi,
Katika kipindi cha Awamu ya Nne tumeendelea kuboresha mazingira ya kazi ya Balozi zetu na maslahi ya watumishi wake. Nasema tumejitahidi kwa kuwa tofauti na watumishi wa kada nyingine serikalini, kada ya utumishi wa nje mahitaji yake ya kifedha ni makubwa sana. Hii ni kutokana na kuzingatia mazingira yao ya kufanyia kazi nje ya nchi yetu. Tumeendelea kuiboresha hali kadri uwezo wetu wa fedha uliporuhusu. Ninyi ni mashuhuda wa maboresho ya msingi tuliyoyafanya katika Kanuni za Watumishi wa Nje (Foreign Service Regulations). Tumerekebisha viwango vya posho ya nje (Foreign Service Allowance), posho ya wenza na ya elimu kwa watoto wa watumishi wakiwa ubalozini. Aidha, tumewapatia balozi vitendea kazi ikiwemo magari ya uwakilishi yenye hadhi na heshima inayolingana na Balozi.
Kutokana na kuanza kutengwa fedha za maendeleo, Wizara imeweza kununua na kujenga majengo ya ubalozi ambayo pia ni vitega uchumi. Tumefanya hivyo New York, Washington DC na Paris. Tunatarajia kujenga majengo ya namna hiyo Nairobi na Oman. Pamoja na ununuzi, tumeendelea na ukarabati wa majengo mengi ya Balozi zetu katika kuboresha taswira ya nchi yetu nje. Lengo letu ni siku nyingine tuachane na kupangisha majengo ya ofisi na kuishi katika Balozi zetu bali yawe mali yetu. Kwa kuwa ni vitega uchumi pia vitega uchumi na hivyo kutaziongezea Balozi mapato na uwezo wa kujiendesha bila kutegemea sana fedha kutoka nyumbani.
Vilevile, kuna haja kwa Wizara kujenga uwezo wa maafisa waliopo na watakaoajiriwa kupitia mafunzo na kupata uzoefu kwa kutenda. Ninachozungumzia hapa ni kuwa na maafisa wenye uelewa mtambuka na uwezo wa kuchambua mambo na kushiriki ipasavyo kwenye majadiliano ya kimataifa. Wasiwe wasikilizaji tu bali wawe washiriki makini wanaofahamu maslahi ya nchi na kuyalinda. Chuo cha Diplomasia kiendelezwe kwa ajili ya kuandaa wanadiplomasia wetu. Pia tuwapeleke watumishi wetu kuongeza elimu katika vyuo mbalimbali duniani. Aidha, mnapaswa sana kupanua wigo wa ujuzi wa maafisa wetu. Muwe na mchanganyiko wa taalama nje zaidi ya uhusiano wa kimataifa. Mnahitaji wataalamu wa elimu ya fani za uchumi, biashara ya kimataifa, nishati na nyinginezo.
Mheshimiwa Waziri na viongozi wenzako;
Mabalozi;
Wageni waalikwa;
Mabibi na Mabwana;
Nashiriki Mkutano huu kwa mara ya mwisho nikiwa Rais wa Nchi yetu. Hivyo, napenda kutumia nafasi hii kuwaaga rasmi. Naondoka nikiwa na kumbukumbu nzuri kwenu kwani tumefanikiwa mengi pamoja. Nakushukuru sana Mheshimiwa Waziri Bernard Membe kwa ushirikiano na msaada wako mkubwa na wenzako katika kunisaidia katika eneo langu hili kwa miaka tisa. Naelewa ugumu na uzito wa jukumu lenyewe maana name niliwahi kuwa Waziri wa Mambo ya Nje kwa miaka 10. Nakupongeza kwa jinsi ulivyoongoza vizuri Wizara hii nyeti na mafanikio mliyoweza kupata. Hii ni Wizara ambayo haikuwahi kuninyima usingizi katika kipindi cha uongozi wangu. Naondoka nikiwa na faraja kuwa Diplomasia yetu iko katika hali nzuri. Nina imani kuwa wanadiplomasia wetu watafanya Watanzania tuendelee kutembea kifua mbele. Daima mkumbuke ule msemo wetu, “Better than yesterday, Less than Tomorrow” yaani tuhakikishe tunafanya vizuri kuliko jana, ingawaje ni pungufu kuliko kile tutakachofanya kesho.
Inawezekana, timiza wajibu wako.
Asanteni sana kwa kunisikiliza!

- May 20, 2015
HOTUBA YA MHE. DKT. JAKAYA MRISHO KIKWETE, RAIS WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WAKATI WA UFUNGUZI WA MKUTANO KUHUSU UENDESHAJI WA SHUGHULI ZA SERIKALI KWA U...
Soma zaidiHotuba
Mhe. George Mkuchika (Mb), Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Ikulu, Utawala Bora;
Waheshimwa Mawaziri,
Katibu Mkuu Kiongozi;
Makatibu Wakuu;
Wakuu wa Taasisi za Serikali;
Wakuu wa Taasisi Zisizo za Serikali;
Wawakilishi wa Wabia wa Maendeleo;
Wageni Waalikwa;
Mabibi na Mabwana.
Nakushukuru Mheshimiwa George Mkuchika, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais-Utawala Bora kwa kunialika na kunishirikisha katika ufunguzi wa Mkutano wa Pili wa Kikanda wa Washirika wa Mpango wa Uendeshaji wa Shughuli za Serikali kwa Uwazi (Open Government Partnership-OGP). Pia nawashukuru waandaaji wa Mkutano huu kwa kuichagua Tanzania kuwa mwenyeji wa Mkutano wa mwaka huu. Ni heshima kubwa kwetu na kielelezo cha imani ya washirika wenzetu wa Mpango huu kwa nchi yetu.
Kwa washiriki wote nasema karibuni mkutanoni na nawatakia Mkutano wenye mafanikio. Wanaotoka nje ya Tanzania nawaambia karibuni sana kwetu. Tumefurahi kuwa nanyi na bila ya shaka wenyeji wenu watafanya kila wawezalo ukaazi wenu uwe mzuri na ushiriki wenu uwe wa mafanikio.
Nawaomba baada ya mkutano mtafute wasaa mkatembelee vivutio vya utalii ambavyo nchi yetu imejaaliwa navyo. Visiwa vya marashi ya karafuu yaani Zanzibar viko mwendo wa robo saa kwa ndege na dakika 50 kwa boti iendayo kasi. Mlima Kilimanjaro, mbuga za wanyama za Serengeti, Ngorongoro na Ziwa Manyara na Tarangire ziko saa moja kutoka hapa kwa ndege. Nendeni ili mrudi kwenu na kumbukumbu nzuri ya nchi yetu na kushawishika kuja tena kwa kipindi kirefu.
Kwa namna ya kipekee nawakaribisha wajumbe kutoka nchi za rafiki za Botswana, Nigeria, Zambia, Uganda, Zimbabwe na Ivory Coast. Nchi zao bado si wanachama wa Mpango huu, lakini ushiriki wao leo kama wasikilizaji ni sawa na ule msemo maarufu wa waswahili usemao “nyota njema huonekana asubuhi”. Bila ya shaka kuwepo kwao ni dalili njema ya uwezekano wa nchi hizi kujiunga na Mpango huu siku za karibuni. Tunawakaribisha kwa mikono miwili.
Nimefurahishwa sana na uamuzi wa kutumia lugha ya Kiswahili katika sherehe hizi za ufunguzi kwa lengo la kuwezesha umma wa Watanzania kushiriki na kufuatilia kwa urahisi kinachoendelea katika Mkutano huu. Huu ni mfano mzuri wa kutekeleza kwa vitendo moja ya nguzo muhimu ya Mpango huu ambayo ni kushirikisha wananchi. Ni jambo muhimu kwamba wananchi hawapati vikwazo katika kushiriki na kufuatilia mambo yanayowahusu kwa kutumia lugha wanayoielewa. Ningefarijika sana kama mkutano wote ungeweza kutumia lugha ya kiswahili.
Kauli Mbiu
Ndugu Washiriki;
Mabibi na Mabwana,
Kauli mbiu ya Mkutano huu yaani “Kuimarisha Uwajibikaji Kupitia Uwazi katika Uendeshaji wa Shughuli za Serikali” (Enhancing Accountability Through Open Governance) ni maridhawa kabisa. Kuendeleza uwajibikaji Serikalini ndiyo shabaha kuu ya Mpango wa Uwazi katika Serikali. Serikali kuendesha shughuli zake kwa uwazi ni jambo la msingi katika uwajibikaji. Wananchi ambao ndio walengwa na ndiyo sababu ya kuwepo kwa Serikali watatambua kwa uhakika jinsi serikali yao inavyowahudumia kama kuna uwazi. Uwazi unawawezesha watu kudai haki zao au kuwakumbusha viongozi na watendaji Serikalini kutimiza wajibu wao kwa raia wanaotakiwa kuwahudumia.
Kwa maneno mengine ushiriki wa wananchi wenye tija na uwajibikaji mzuri wa Serikali ni matokeo ya upatikanaji wa taarifa kutoka Serikalini. Taarifa hizo lazima ziwe sahihi na zipatikane kwa urahisi na uhakika. Ili iweze kuwa hivyo hapana budi kuwepo kwa uwazi. Taarifa huwaongezea wananchi uwezo wa kuhoji, kufuatilia, na kuwawajibisha viongozi wao pale wasipotimiza ipasavyo wajibu wao. Halikadhalika huwarahisishia katika mambo yanayowahusu kuchangia na kutimiza wajibu wao kama raia wa nchi yao.
Ili Serikali na jamii iweze kutekeleza ipasavyo dhana za uwajibikaji na uwazi italazimu kubadili utamaduni wetu wa uendeshaji wa mambo. Hususan, tuwe na mitazamo na fikra chanya na kuondokana na imani potofu zilizojengeka miongoni mwetu yaani Serikali, vyama vya siasa, wananchi na asasi za kiraia kuhusu uwazi na uwajibikaji. Hali kadhalika, inatupasa tuondokane na mitazamo kinzani baina yetu. Badala yake tunatazamiwa kujenga madaraja ya mawasiliano, maelewano na kuaminiana. Tunawajibika kuwa watu wamoja na wenye dhamira moja ya kuijengea nchi yetu na kuwahudumia wananchi wake. Katu hatutakiwi kuwa mahasimu. Ikiwa hivyo tutakuwa tumekosea sana. Tutakuwa tumewaangusha kupita kiasi.
Dhana ya uwazi na uwajibikaji inawahusu wadau wote yaani Serikali na asasi za kiraia ambao ndio wadau wakuu wa OGP. Tutakuwa tunakosea sana kama tutadhani kuwa dhana hizi mbili zinaihusu Serikali pekee. La hasha! Uwazi na uwajibikaji unazihusu pia asasi za kiraia. Lazima nao wawe wawazi kuhusu shughuli wazifanyazo ili jamii na watu wajue wanachokifanya kwa niaba yao, kwa ajili yao na jinsi wanavyowajibika kwao. Na kuhusu mapato na matumizi, lazima asasi za kiraia nazo ziwe wazi kuieleza jamii wamepata pesa kiasi gani, kutoka kwa nani, kwa ajili gani na jinsi walivyozitumia fedha hizo? Jamii na wananchi ambao ndiyo walengwa wa shughuli za asasi hizo wanastahili kujua kwani fedha hizo zimetolewa kwa manufaa yao na siyo ya viongozi na watendaji wa asasi za kiraia.
Tabia ya asasi za kiraia kukataa kuwa wa wazi na kuwa wakali wanapotakiwa kufanya hivyo siyo sahihi. Pia ni kinyume na misingi ya Open Government Partnership. Kutokufanya hivyo ndiko kunakozua mashaka wakati mwingine hata mizozo. Asasi za kiraia nazo lazima ziwe wazi na zitoe taarifa za shughuli ili wananchi ambao ndiyo walengwa waweze kujua kama kweli wamenufaika. Ili, pia, wananchi waweze kuhoji, kudai haki na kuwataka wahusika kuwajibika. Ni vyema ikaeleweka siku hizi sehemu kubwa ya fedha za misaada ya maendeleo hupitia asasi za kiraia hivyo kunapokosekana uwazi kupitia utoaji wa taarifa zilizo sahihi kuna hatari ya pesa za maendeleo ya wananchi kutokuwawafikia walengwa na kunufaisha watu wachache. Hivyo basi, serikali inapowakumbusha kuwa wawazi na kutoa taarifa watuelewe hivyo. Kuishutumu kuwa siyo rafiki na kuingilia asasi za kiraia si madai sahihi. Kila anayeshiriki katika Mpango wa Open Government Partnership hana budi kutambua kuwa anatakiwa kuwa muwazi na mkweli. Ndiyo itikadi na falsafa kuu.
Tanzania na OGP
Ndugu Washiriki;
Mabibi na Mabwana;
Tanzania ni mshirika wa Mpango wa OGP na ni ya pili kujiunga kutoka Afrika mara tu baada ya Mpango huu kuanzishwa mwaka 2011. Aidha, ni miongoni mwa nchi nane za Afrika (Afrika Kusini, Ghana, Liberia, Malawi, Sierra Leone, Tunisia na Tanzania) kati ya nchi 65 duniani zilizojiunga na Mpango huu ambao ni wa hiyari. Niliamua, kwa hiari yangu, Tanzania ijiunge katika Mpango huu kwa kutambua manufaa na umuhimu wa kuwepo uwazi katika uendeshaji wa shughuli za Serikali. Husaidia uwajibikaji wa Serikali. Kwa kweli, Serikali kuwajibika kwa wananchi ndiyo makusudio na uhalali wa kuwepo kwake. Uamuzi huo ni kielelezo tosha cha utayari wangu na wa Serikali ya Tanzania kuunga mkono kwetu dhana na falsafa ya uwazi na uwajibikaji katika kuendesha Serikali. Kusisitiza ukweli huo, Tanzania pia ni mwanachama wa Mpango wa Afrika wa Kujitathmini Wenyewe (APRM) na Mpango wa Uwazi katika Uvunaji wa Rasilimali (EITI).
Ndugu Washiriki;
Mimi na wenzangu katika Serikali tumefanya mengi kuhusu uwazi na uwajibikaji. Tumepanua na kuongeza mawanda ya uwazi katika shughuli za serikali, demokrasia, uhuru wa wananchi kutoa maoni yao, uhuru wa habari, haki ya kupata taarifa na ushiriki wa wananchi. Tanzania ni miongoni mwa nchi zinazoongoza Afrika na hata pengine duniani kwa kuwa na vyombo vya habari vingi. Hivi sasa kuna magazeti na majarida 825, vituo vya TV 28, radio 95 ikilinganishwa na magazeti mawili, TV moja na radio moja mwaka 1992.
Kati ya vyombo vyote hivyo Serikali ina magazeti mawili, TV moja na radio moja. Hakuna uhakiki wa habari hivyo vyombo viko huru ingawaje maadili ya uandishi husisitizwa na hakuna ajizi yanapokiukwa.
Tumeongeza pia, uwazi katika uendeshaji wa shughuli za serikali. Habari hutolewa katika tovuti za Wizara na Idara husika za Serikali kwa wote kuona. Taarifa ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) iko wazi. Mikutano ya Bunge huonyeshwa kwenye Televisheni na kwa mara ya kwanza wananchi wameshirikishwa moja kwa moja katika mchakato wa kuandika upya Katiba ya nchi yetu.
Katika kutekeleza Mpango Kazi wa OGP, kama ilivyoelezwa na Mheshimiwa Waziri wa Utawala Bora, tumekwisha tekeleza Mpango Kazi wa Kwanza (2012/2013) na sasa tunatekeleza Mpango Kazi wa Pili (2014-2016). Mipango kazi yote miwili imetayarishwa kwa kushirikisha asasi za kiraia na wadau wengine. Mafanikio yaliyopatikana katika kutekeleza Awamu ya Kwanza ya Mpango Kazi wa OGP ni pamoja na kutoa kijarida cha Bajeti ya Serikali (Citizen’s Budget) kwa lugha nyepesi ya Kiswahili na Kiingereza kwa ajili ya kutumiwa na wananchi wa kawaida ili waelewe vipaumbele vya bajeti ya Serikali; kuanzishwa kwa tovuti Kuu ya Serikali inayotoa taarifa muhimu zinazoweza kumsaidia mwananchi kupata huduma kwa urahisi; kuanzishwa kwa Tovuti ya Takwimu Huria (Open Data), inayoainisha takwimu mbalimbali. Tovuti ya “Nifanyeje” inayoweka taarifa muhimu kuhusu namna ya kupata huduma mbalimbali za umma imeanzishwa.
Ndugu Washiriki;
Mabibi na Mabwana;
Utekelezaji wa Mpango Kazi wa OGP Awamu ya Pili (2014/15 - 2015/16) umejikita katika maeneo matano ambayo ni Utungwaji wa Sheria ya Haki ya Kupata wa Habari (Access to Information), Uwazi katika upatikanaji wa takwimu za kibajeti, (Open Budget), Uwazi wa matumizi ya ardhi (Land Transparency), Uwazi katika masuala ya utafutaji na uchimbaji wa gesi, mafuta na madini (Extractive Industry Transparency) na kuanzisha tovuti ya open data kwa kuweka taarifa kuhusu afya, elimu na maji.
Tunaendelea na utekelezaji wa Mpango Kazi huu na tayari tumeshapiga hatua mbalimbali. Muswada wa Sheria wa Uhuru wa Kupata Habari tayari umeshawasilishwa Bungeni na kusomwa kwa mara ya kwanza. Ni matumaini yetu kuwa katika vikao vinavyoendelea kati ya sasa na Julai utakamilika. Vile vile, tunaendelea na utekelezaji wa mambo mengine tuliyoahidi kuyapa kipaumbele. Tunauona mkutano huu kama fursa muhimu sana ya kubadilishana uzoefu utakaotusaidia kufanya mambo yetu kwa ufanisi zaidi. Kwa ujumla wetu tutazungumza kwa uwazi shughuli zetu pamoja na mafanikio tunayopata na changamoto tunazokumbana nazo katika utekelezaji wa malengo tuliyojiwekea. Aidha, tutashauriana na kubadilishana uzoefu kuhusu kuzipatia ufumbuzi.
Ni matumaini yangu kuwa katika Mkutano huu mtatoka na Azimio la Dar es Salaam litakalosisitiza Uwazi, Uwajibikaji na Ushirikishwaji wa wananchi katika nchi zetu na Bara zima la Afrika. Ni lazima tufikishe ujumbe duniani kote kuwa ni muhimu kwa Serikali zetu kuwashirikisha wananchi na kukuza Uwazi.
Ahadi ya Serikali
Ndugu Washiriki;
Mabibi na Mabwana;
Napenda kuwahakikishia washiriki wote kuwa Tanzania itaendelea kuwa muumini wa dhati na mwanachama asiyeyumba katika Mpango huu wa OGP. Tutaendelea kushiriki kwa kuwa tunauona Mpango huu, na haswa dhana ya uwazi na uwajibikaji kuwa na manufaa makubwa kwa nchi yetu na watu wake. Hatuna sababu wala dhamira ya kurudi nyuma wala hatujutii uamuzi wetu wa kujiunga na Mpango huu, ambao kwa kweli tumejiunga kwa hiyari yetu wenyewe. Tuko imara na tayari kuendelea na safari hii kuelekea kwenye viwango vya juu vya uwazi na uwajibikaji. Tunafahamu safari hii itakuwa na changamoto zake, ndogo na kubwa kwa nyakati fulani fulani wakati wote, hata hivyo, hatutakata tama. Maadam tuna hakika na matunda mazuri huko mbele tuendako tutasonga mbele bila ya ajizi.
Ndugu Washiriki;
Tunapoangalia nyuma tulikotoka na hapa tulipo sasa tunayo kila sababu ya kujivunia hatua kubwa tuliyofikia katika kuwa na taasisi na mifumo mizuri ya kiutawala na uendeshaji zinazoakisi dhana ya uwazi na uwajibikaji. Sina budi kuwashukuru sana wadau wa ndani yaani idara na taasisi za Serikali, Bunge, vyama vya siasa, asasi za kiraia na vyombo vya habari kwa mchango wao mkubwa katika kujenga misingi na mifumo ya uwazi na uwajibikaji. Hata hivyo hatuna budi kutambua kuwa safari yetu bado ni ndefu. Hivyo hatuna budi kuongeza bidii maradufu ya sasa.
Wito wangu kwa wadau wote na washiriki wa Mpango huu, haswa taasisi za Serikali na washirika wenzetu wa asasi za kiraia ni kuwa tuendelee kushirikiana kwa karibu. Tufanye kila tuwezalo na kuimarisha uhusiano na ushirikiano baina yetu. Tujenge tabia ya kukutana mara kwa mara kuzungumzia shughuli zetu na namna ya kushirikiana. Tukifanya hivyo tutapunguza au hata kuepusha kabisa kutokuaminiana, mizozo, migongano isiyokuwa ya lazima. Kitu kilicho muhimu kwetu ni kuwa na dhamira ya dhati ya kutaka pawepo na maelewano na mashirikiano baina yetu. Kama hilo lipo mambo yatakuwa mazuri.
Nayasema haya kutokana na uzoefu tulioupata katika uhusiano wetu na asasi moja kubwa ya kiraia na kupata mafaniko makubwa. Nayo si nyingine bali Shirikisho la Wafanyakazi ambapo mikutano yetu ya mara moja au mbili kwa mwaka imesaidia sana kupata ufumbuzi wa masuala mbalimbali ya wafanyakazi. Imepunguza mizozo na misuguano, Naamini tukiwa na utaratibu kama huo na shirikisho la asasi za kiraia mambo yatakuwa mazuri.
Hata haya ya sheria ya Mitandao na Takwimu tukikaa pamoja yataisha tu. Kusema sheria mbaya haisaidii, na wengine kutishia kufuta misaada haisaidii pia. Waziri mwenye dhamana ameshasema mwenye mawazo atoe, basi pelekeni maoni. Sisi Serikali ni wasikivu sana. Tumeshafanya mabadiliko ya sheria nyingi tu. Ni vyema mtambue kuwa Serikali nayo inahitaji heshima yake. Ukitaka kuonyesha ubabe nayo itaonyesha ubabe pia. Vitisho havijengi, lakini fursa ya kuzungumza inatoa majawabu.
Nitaangalia uwezekano wa kukutana na asasi za kiraia kabla ya kumaliza kipindi changu cha uongozi ili tujenge utaratibu maalum wa mazungumzo baina ya Serikali na asasi za kiraia.
Hitimisho
Ndugu Washiriki;
Mabibi na Mabwana;
Napenda kumaliza kama nilivyoanza kwa kuwashukuru kwa uamuzi wenu wa kuchagua Tanzania kuwa mwenyeji wa Mkutano huu muhimu. Mmetupa heshima kubwa ambayo daima tutaikumbuka na kuienzi. Naamini nazungumza kwa niaba ya viongozi wenzangu wote Afrika pia, kwamba tuna matumaini makubwa na Mkutano huu kwamba utazaa matunda mema yenye manufaa kwa bara la Afrika kwa ujumla. Sisi tuko tayari kutimiza wajibu wetu, na tunatarajia kila mdau atatimiza wajibu wake. Tukumbuke kuwa, Uwazi na Uwajibikaji ni utamaduni, pia ni kama msumeno, unakata pande zote. “Inawezekana, timiza wajibu wako”.
Mungu Ibariki Afrika, Mungu Ibariki Tanzania
Ahsanteni Sana Kwa Kunisikiliza!

- May 17, 2015
STATEMENT BY H.E. JAKAYA MRISHO KIKWETE, PRESIDENT OF THE UNITED REPUBLIC OF TANZANIA ON THE OCCASION OF THE STATE BANQUET HOSTED IN HONOUR OF H.E. FILIPE JACIN...
Soma zaidiHotuba
Your Excellency Filipe Jacinto Nyusi, President of the Republic of Mozambique;
Honourable Ministers;
Your Excellencies High Commissioners and Ambassadors;
Distinguished Guests;
Ladies and Gentlemen:
On behalf of the Government and people of Tanzania, I extend to you, Mr. President and all members of your entourage, a very warm welcome to Dar-es-salaam, and to Tanzania. It is my earnest desire that you and your delegation should find your stay in our country not only pleasant, but also memorable and fruitful. Karibu Sana.
Your Excellency;
I know you are not a stranger to Tanzania. You lived here during the struggle for the liberation of Mozambique. You have been here several times after independence for various reasons and in different capacities. But this is the first time you visit us as President of your great country. The last time you came you were candidate of your Party – FRELIMO for the Presidency. Permit me to once again congratulate you on the resounding victory that you and your Party gathered in the last elections. We wish you every success.
Your Excellency;
It is comforting indeed, to note that you have chosen Tanzania to be the first country to visit since assuming leadership of your country, four months ago. We feel extremely honoured and grateful to you for affording us such a special favour.
I still recall of our first meeting in Tanga when we had a lengthy conversation on the future of the cooperation between our two countries. I remember we both made a pledge to bilateralize our two economies, to use your own words. In this case, your visit today speaks volumes about your personal commitment as well as that of your Government to see to it, that the relations between our two sisterly countries are revitalized and strengthened.
Your Excellency;
Tanzanians and Mozambicans share a lot in common. Not only are we neighbours separated by the Ruvuma River but we are also blood related brothers and sisters. Wamakonde, Wamakua, Wahiyao, Wangoni are found on both sides of the border. Our two countries and people share a lot politically, economically, socially and even culturally.
Tanzania is home to many Mozambicans just as Mozambique is home to Tanzanians. We are united by the historic bond that perhaps very few countries in Africa can compare. FRELIMO was founded here in Dar es Salaam 1962 under the progressive leadership of Eduardo Mondlane. The people of Tanzania supported the struggle for the liberation of Mozambique from inception to the day when Mozambique attained independence from the Portuguese colonists in 1975. We continued to standby our Mozambiquan brothers and sisters in the later struggle to defend the independence and sovereignty of Mozambique being threatened the RENAMO rebels. Our relations are sealed by the blood of heroes and heroins who sacrificed their lives for the cause of liberation of Mozambique. It is in their honour we aspire to strengthen and advance our bilateral relations. So far so good.
Your Excellency;
Your visit today and the fruitful official talks we held in the afternoon take our relations to another level altogether. We agreed to ease the movement of people across the border. We also agreed to increase cooperation in the fields of natural gas, education, security in our territorial waters, fight against cross-border crime including anti-poaching. We also agreed to promote trade and investments in our two countries. The onus is on us, now, to ensure that all these initiatives are fully implemented for the mutual benefits of our two countries. We in Tanzania undertake to convene the Joint Permanent Commission at the earliest possible time to follow up on what we agreed to do. I am confident we will do better this time around.
Your Excellency;
I will leave the office later this year after the General Elections in October. I will be satisfied that I leave behind a solid foundation upon which my successor will build upon to propel our relations to even greater heights. It comforts me that Mozambique has and will always be our true and most cherished friend. Having been privileged to host you as you assumed office, and learn from your ardent desire of maintaining and scale up these relations, I will leave office confident that the future of our bilateral relations are in very safe hands. I am sure, my successor shall find in Your Excellency, a brother and a friend to work with for the betterment of our countries and peoples. Forward ever backward never.
Your Excellencies;
Ladies and Gentlemen;
I would like to kindly request all of you to rise and join me for a Toast:
To the continued good health of Your Excellency Filipe Jacinto Nyusi, President of the Republic of Mozambique;
To the continued excellent relations between our two countries; and , To the good health of all of us present here tonight.
Thank you very much.
Ahsante Sana.

- May 15, 2015
HOTUBA YA RAIS WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA MHESHIMIWA DKT. JAKAYA MRISHO KIKWETE KATIKA KILELE CHA MAADHIMISHO YA PILI YA KITAIFA YA WIKI YA ELIMU TANZAN...
Soma zaidiHotuba
Mheshimiwa Dkt. Shukuru Jumanne Kawambwa (Mb), Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi;
Mheshimiwa Hawa Ghasia (Mb), Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa;
Waheshimiwa Manaibu Waziri;
Mheshimiwa Chiku Galawa; Mkuu wa Mkoa wa Dodoma;
Mheshimiwa Magreth Sitta (Mb), Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Huduma za Jamii;
Waheshimiwa Wabunge;
Balozi Ombeni Sefue, Katibu Mkuu Kiongozi;
Makatibu Wakuu na Naibu Makatibu Wakuu;
Washirika wa Maendeleo;
Wadau wa Maendeleo ya Elimu;
Viongozi wa Serikali na Mashirika ya Dini;
Walimu na Wanafunzi;
Ndugu Wanahabari;
Ndugu Wananchi;
Mabibi na Mabwana.
Shukrani
Ninayo furaha kubwa ya kuungana nanyi leo katika kuhitimisha maadhimisho haya ya pili ya kitaifa ya wiki ya elimu. Nakushukuru wewe, Mheshimiwa Waziri na viongozi wenzako wa Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi kwa kunipa heshima hii kubwa ya kushiriki maadhimisho haya.
Pia, nawashukuru na kuwapongeza kwa dhati viongozi na wananchi wa Mkoa wa Dodoma wakiongozwa na Mkuu wa Mkoa, Mheshimiwa Chiku Galawa kwa kukubali kuwa wenyeji wa maadhimisho haya kwa mara ya pili mfululizo. Vile vile, napenda kuipongeza Kamati ya Maandalizi ya Kilele cha Maadhimisho ya Pili ya Kitaifa ya Wiki ya Elimu Tanzania kwa kazi nzuri waliyofanya ya kufanikisha shughuli hii. Kwenu wote nasema hongereni sana!
Kauli Mbiu
Ndugu Waziri;
Ndugu wananchi;
Nimefurahishwa na kauli mbiu ya maadhimisho ya mwaka huu isemayo “Elimu Bora ni Haki ya Kila Mtoto kwa Maendeleo ya Taifa”. Kauli mbinu hii ni muafaka kabisa kwa kuwa kupata elimu ni moja ya haki ya msingi ya mtoto. Tena lazima apate elimu iliyo bora. Aidha kauli mbiu inaakisi kwa usahihi madhumuni na malengo ya Serikali katika hatua inazochukua kuendeleza elimu nchini. Kuwapatia Watanzania elimu bora ndiyo shabaha ya msingi ya Sera ya Elimu na Mafunzo ya Mwaka 2014 niliyoizindua mapema mwaka huu. Pia ndiyo shabaha ya Sera zilizokuwepo kabla ya hii tangu uhuru mpaka sasa. Tulichokifanya katika awamu hii ni kutoa msukumo mkubwa zaidi katika kuendeleza elimu. Kama ilivyokuwa kauli mbiu yetu ya ari Mpya, Nguvu Mpya na Ari Mpya na baadae ile ya Ari Zaidi, Nguvu Zaidi na Kasi Zaidi.
Ni ukweli ulio wazi kuwa tumepata mafanikio ya kutia moyo ingawaje bado tuna kazi kubwa ya kufanya mbele yetu. Tuliamua kuanzisha maadhimisho ya Wiki ya Elimu nchini kwa malengo mawili. Kwanza, kuelimisha Watanzania kuhusu jitihada zinazoendelea kufanyika na hatua tunazopiga katika kuboresha elimu na kuongeza fursa kwa watoto wetu na Watanzania kwa ujumla kupata elimu. Pili, kutambua na kuwatunza waliofanya vizuri katika nyanja mbalimbali za elimu.
Chanzo cha Maadhimisho ya Wiki ya Elimu
Ndugu Wananchi;
Katika kuboresha utendaji wa Serikali na kutekeleza mipango na ahadi zake tulibuni Mkakati wa Matokeo Makubwa Sasa (Big Results Now - BRN). Katika mpango huo Elimu ilikuwa miongoni mwa sekta sita za mwanzo, nyingine zikiwa maji, kilimo, nishati, miundombinu na mapato ya serikali. Baadae tumeongeza mazingira ya uwekezaji na afya.
Baada ya kufanya uchambuzi wa hali ilivyo na kutafuta ufumbuzi wa changamoto zilizopo katika elimu ilikubaliwa mambo tisa kupewa kipaumbele. Mambo hayo ni:-
(i) Upangaji wa shule kwa ubora kwa matokeo ya mtihani kitaifa kuanzia shule iliyoongoza hadi ya mwisho.
(ii) Uratibu wa utoaji wa tuzo kwa shule zilizofanya vizuri,
(iii) kuwa na kiongozi cha usimamizi wa shule,
(iv) Upimaji wa kitaifa wa stadi za kusoma, kuandika na kuhesabu,
(v) Mafunzo kwa walimu kwa stadi za kusoma, kuandika na kuhesabu,
(vi) Kujenga uwezo wa walimu na wanafunzi katika ufundishaji na ujifunzaji,
(vii) Ujenzi wa miundo mbinu muhimu ya shule; madarasa,
(viii) Utoaji ya ruzuku wa uendeshaji wa shule na,
(ix) Utoaji wa motisha kwa walimu.
Kuhusu utoaji wa tuzo naipongeza Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi kwa uamuzi wa busara kuwa tuzo hizo zitolewe kwenye kilele cha Maadhimisho ya Wiki ya elimu.
Ndugu Wananchi;
Ni matazamio yetu kuwa utoaji wa tuzo hizi utakuwa kichocheo cha kujenga ari, hamasa na tabia ya ushindani wa kitaaluma ndani ya mfumo wa Elimu. Jambo hilo litasaidia kuinua ubora na ufanisi katika ngazi zote za elimu. Ushindani wa kitaaluma utasababisha kuongezeka kwa ufanisi na uwajibikaji katika kufundisha na kujifunza na hatimaye kuendelea kuboresha uelewa wa wanafunzi na kuwafanya wawe na matokeo mazuri.
Tuzo kwa Waliofanya Vizuri katika Mitihani ya Taifa ya
Mwaka 2014 na Uandishi wa Insha za Jumuiya ya Afrika
Mashariki (EAC) na Jumuiya ya Nchi za Kusini mwa Afrika (SADC)
Ndugu wananchi;
Napenda kutumia nafasi hii kutoa pongezi nyingi kwa wale wote waliopata Tuzo. Wahenga wamesema “mcheza kwao hutunzwa”. Siku hii ya leo, jumla ya shule 20 na wanafunzi 20 waliofanya vizuri katika matokeo ya mitihani ya Taifa ya darasa la saba na kidato cha nne mwaka 2014 wamepokea zawadi na tuzo. Nazipongeza sana shule zetu hizi na wanafunzi wote hawa kwa ushindi waliopata. Aidha jumla ya shule 3,090 yaani 2,166 za msingi na 924 za sekondari zilizopata ufaulu uliotukuka na nyingine kuongeza ufaulu kwa kiwango cha juu zitapata tuzo na zawadi stahiki.
Mheshimiwa Waziri;
Ndugu wananchi;
Niruhusuni pia nitoe pongezi kwa vijana 13 walioitoa nchi yetu kimasomaso katika mashindano ya uandishi wa insha yanayoendeshwa na Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC) na Jumuiya ya Umoja wa Nchi za Kusini mwa Afrika (SADC). Hongereni Sana.
Hali kadhalika, natoa pongezi maalum kwa wale vijana watatu (3) waliopata ushindi kwa kuandika insha bora na wengine watatu (3) waliochora picha bora kuhusiana na kauli Mbiu ya maadhimisho ya mwaka 2015. Naomba Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi wakishirikiana na Ofisi ya Waziri Mkuu – Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) kuongeza wigo wa mashindano ya kitaaluma kwa wanafunzi. Naamini kufanya hivyo kutasaidia kuibua vipaji vya watoto wetu tangu wakiwa wadogo. Tusiishie hapo, nawasihi walimu, wazazi, walezi na jamii nao wahakikishe kuwa vipaji hivi vinaendelezwa.
Ndugu Wananchi;
Maadhimisho haya yanatukumbusha sote juu ya wajibu wa kila mwananchi kushiriki katika shughuli za maendeleo ya shule na ufuatiliaji wa karibu wa shughuli zote zinazofanyika shuleni kwa lengo la kumuwezesha kila mtoto kupata elimu bora. Ni ukweli ulio wazi kwamba wajibu wa kuhakikisha watoto wetu wanapata elimu bora si wa Serikali pekee, bali pia ni wa wazazi na walezi wanaoishi na watoto na jamii kwa ujumla. Daima tukumbuke kuwa watoto hawaishi Serikalini bali kwenye familia na jamii hivyo wazazi, walezi na jamii ina nafasi maalum katika maendeleo ya mtoto kwa upande wa elimu na mambo mengine maishani.
Maendeleo katika Sekta ya Elimu Nchini
Ndugu Wananchi;
Katika kipindi cha miaka kumi iliyopita tumeweza kupiga hatua kubwa katika sekta ya elimu nchini. Ninyi mliopo hapa ni wadau muhimu hivyo ni mashahidi wa mafanikio tuliyoyapata ambayo ni matokeo ya kuongezeka kwa shule, idadi ya wanafunzi, idadi ya walimu, vitabu na vifaa vya kufundishia na kujifunzia. Katika kipindi hicho, Shule za msingi zimeongezeka kutoka shule 14,257 mwaka 2005 hadi kufikia shule 16,343 mwaka 2014. Hii imefanya idadi ya wanafunzi kuongezeka kutoka milioni 7.54 hadi kufikia milioni 8.23. Kwa upande wa shule za sekondari, idadi yake imeongezeka kutoka shule 1,745 mwaka 2005 hadi kufikia shule 4,576 mwaka 2014. Hali kadhalika, idadi ya wanafunzi wa shule za sekondari imeongezeka kutoka wanafunzi 524,325 mwaka 2005 hadi kufikia wanafunzi 1,804,056 mwaka 2014.
Jumla ya walimu wote wa msingi na sekondari idadi imeongezeka kutoka 153,767 mwaka 2005 hadi 301,960 mwaka 2015. Katika kipindi hicho, vyuo vya ufundi vimeongezeka kutoka 184 mwaka 2005 hadi 744 mwaka 2015. Wanafunzi wa elimu ya ufundi nao wameongezeka kutoka 40,059 mwaka 2005 hadi 145,511 mwaka 2015. Kwa upande wa elimu ya juu, wanafunzi wa vyuo vikuu wameongezeka kutoka 40,719 mwaka 2005 hadi 200,986 mwaka 2014. Hii ni kutokana na kuongezeka kwa vyuo vikuu na vyuo vikuu vishiriki vimeongezeka kutoka 26 mwaka 2005 hadi 52 mwaka 2015. Upanuzi huu mkubwa katika udahili wa wanafunzi wa vyuo vikuu umewezekana kutokana na kuongezeka kwa bajeti ya Bodi ya Mikopo ya wanafunzi na kuruhusu wanafunzi wa vyuo vikuu vya binafsi navyo wapatiwe mikopo. Bajeti iliongezwa kutoka shilingi bilioni 56.1 mwaka 2005 hadi shilingi bilioni 345 mwaka 2015 na kunufaisha wanafunzi 98,000 mpaka sasa.
Ndugu Wananchi;
Mafanikio haya ni matokeo ya kutoa kipaumbele cha kwanza kwa elimu katika bajeti ya serikali. Leo hii bajeti ya sekta ya elimu ndiyo kubwa kuliko zote nchini ambayo sasa imefikia shilingi trilioni 3.4 ikilinganishwa na shilingi bilioni 669.5 mwaka 2005. Tumefanya hivyo kwa kutambua kwamba kuwekeza kwenye elimu ni kuwekeza kwenye uhai na maendeleo ya taifa na watu wake sasa na miaka mingi ijayo. Tusipowekeza kwenye elimu, Watanzania hawataweza kutawala mazingira na raslimali zao na kuzitumia kujiletea maendeleo. Taifa lisilowekeza katika elimu, halina nafasi huko tuendako.
Ndugu wananchi;
Ukiacha sababu hizo, jambo lingine lililotufanya tuongeze sana bejeti ya elimu ni ule ukweli kwamba, wakati Serikali ya Awamu ya Nne inaingia madarakani mwaka 2005 Tanzania ilikuwa nyuma kwa wanafunzi wa elimu ya msingi, sekondari na vyuo vikuu kuliko Kenya na Uganda. Lakini nchi yetu ndiyo kubwa kuliko nchi zote katika Jumuiya ya Afrika ya Mashariki. Takwimu zilizopo zinaonesha kuwa mwaka 2005, Tanzania ilikuwa na wanafunzi wa shule za sekondari 524,325 wakati Uganda ilikuwa na wanafunzi 728,393 na Kenya 925,341. Kwa upande wa vyuo vikuu Tanzania ilikuwa na wanafunzi 40,719, wakati Uganda ilikuwa na wanafunzi 124,313 na Kenya ilikuwa na wanafunzi 108,407.
Kwa kuwa nyuma ya wenzetu katika utoaji wa fursa ya elimu kwa vijana wetu kulituweka pagumu katika kutoa ushindani katika soko la jumuiya ya Afrika Mashariki. Wakati ule wazazi wengi walilazimika kupeleka watoto wao kusoma Uganda na Kenya. Tukafanya uamuzi wa makusudi kuongeza uwekezaji kwenye elimu ili fursa ya kupata elimu ya msingi, sekondari na chuo kikuu ziongezeke hapa hapa nchini. Kwa upande wa elimu ya msingi tulijenga shule mpya na kuongeza madarasa pale ilipohitajika. Kwa upande wa sekondari tukaanzisha mkakati wa kujenga shule ya sekondari kwa kila kata na kwa elimu ya juu tulihimiza wadau wengine kujenga vyuo vikuu na serikali kutoa mikopo ya elimu ya juu kwa wote. Sisi tulionesha mfano kwa kujenga Chuo Kikuucha Dodoma, Chuo cha Nelson Mandela na kuanzisha Chuo cha Mbeya na sasa tunajenga Chuo Kikuu cha Kilimo Butiama.
Matokeo ya uamuzi huo na hatua hizo ni kuongezeka sana kwa shule za sekondari na vyuo vikuu nchini. Kwa sababu hiyo ilipofikia mwaka 2013 hali ilikuwa tofauti kabisa. Wanafunzi katika shule za sekondari Tanzania walifikia milioni 1,804,056 na vyuo vikuu 200,986. Wenzetu wa Kenya bado wanatuzidi kwa kuwa na wanafunzi wa sekondari 2,104,300 na vyuo vikuu 324,600. Lakini, tuliweza kuipita Uganda iliyokuwa na wanafunzi wa shule za sekondari 1,362,739 na wa vyuo vikuu 140,403. Leo tuko mahala ambapo tunaweza kusema tunashindana kisawa sawa na wenzetu.
Mafanikio hayo makubwa katika sekta ya elimu hayakutokana na nguvu za Serikali peke yake. Haya ni mafanikio yaliyotokana na mchango mkubwa wa wananchi na wadau wengine. Wananchi walijitolea nguvu zao na chochote walichokuwa nacho kujenga shule za sekondari na msingi nchini kote. Aidha, huwezi kutaja mafanikio haya bila ya kutambua mchango mkubwa wa taasisi na mashirika ya dini na sekta binafsi ambao wamejenga shule za msingi na sekondari pamoja na vyuo vikuu.
Tunayo kila sababu ya kujipongeza na kujivunia matokeo haya na matunda ya kazi yetu nzuri. Wakati huo huo tunaendelea kukumbushana umuhimu wa kuendelea na kazi muhimu ya kuongeza ubora wa elimu waipatayo watoto wetu katika ngazi zote.
Suala la kuongeza ufaulu katika mitihani ya darasa la saba na kidato cha nne ni miongoni mwa malengo makuu ya Mkakati wa Matokeo Makubwa sasa. Kwa mujibu wa BRN malengo ya ufaulu kwa kidato cha nne umetakiwa uwe asilimia 60 mwaka 2013 na asilimia 80 mwaka 2014. Kiwango cha ufaulu kwa kidato cha nne hivi sasa ni asilimia 69.7. Kwa upande wa darasa la saba, malengo yalikuwa kufikia asilimia 60 mwaka 2013 na asilimia 80 mwaka 2014 mpaka sasa tumefikia asilimia 56.9.
Kwa jumla ufaulu umekuwa unaongezeka lakini bado hatujafika pale tunapopataka. Ufaulu wa wanafunzi ni kielelezo cha ubora wa elimu wanayopata. Hivyo basi, tunayo kazi kubwa ya kufanya kuinua ubora wa elimu ncini. Katika BRN kuongeza ubora wa elimu lilikuwa agenda mama na yote tunayofanya shabaha yake ni hiyo. Tunaendelea na utekelezaji wake na sina shaka kwamba tukifanikiwa kutekeleza kwa ukamilifu elimu nchini siyo tu itamfikia kila anayeistahili bali itakuwa ya ubora wa hali ya juu. Hakuna lisilowelezekana, kinachotakiwa ni kila mmoja wetu kutimiza wajibu wake.
Ndugu Wananchi;
Napenda kutumia fursa hii pia, kuzipongeza Halmashauri zote na mikoa yote kwa kuitikia wito wangu wa kujenga maabara katika shule zetu za sekondari ambazo hazina. Aidha, nawashukuru wazazi, walezi na wadau kwa kujitolea kuchangia nguvu kazi katika ujenzi wa maabara. Wasivunjwe moyo na wale wachache wanaojaribu kutukatisha tamaa. Kwa viongozi wa mikoa, Wilaya na Halmashauri, nakumbusha kwa mara ya mwisho kuwa ujenzi wa maabara zilizokuwa hazijakamilishwa uwe umekamilika ifikapo Juni 30, 2015. Nimeona nirudie hili kuweka msisitizo.
Hitimisho
Ndugu Wananchi;
Hapana shaka kuwa tuko katika njia sahihi katika azma yetu ya kuleta mapinduzi katika sekta ya elimu, na kuwaandaa vijana wetu kukabiliana na changamoto za maisha za kujiletea maendeleo yao, ya jamii wanayoishi na nchi yao. Kila mmoja na atimize wajibu wake ipasavyo. Mafanikio ya kuleta mapinduzi ya elimu yanategemea mkusanyiko wa jitihada za wanafunzi, wazazi walezi, walimu, wamiliki wa shule na vyuo ikiwemo serikali. Kila mmoja akilima mraba wake vizuri katika shamba hili kubwa, matunda yake na neema zake ni faraja kwetu. Tukifanya kinyume chake madhara yake ni hasara kwetu sote. Hivyo basi, kila mtu atambue wajibu wake katika kuhakikisha elimu inapatikana kwa watoto wetu wote na ni wa ubora ya hali ya juu. Njia nzuri ya kutimiza wajibu wako ni kuanza na shule ya msingi na sekondari iliyoko katika eneo lako na kata yako maana hakuna eneo wlala kata isiyo na shule hizo na hakuna Mtanzania asiyeishi katika kata.
Kila mmoja wetu na ajiulize, amechangia nini katika kuboresha shule ya eneo na kata yake? Amechangia nini katika kusimamia na kufuatilia mahudhurio na maendeleo ya kitaaluma ya mtoto aliyeko kwenye kaya yake? Elimu bora inawezekana na inaanza na wewe. Timiza wajibu wako.
Mungu ibariki Tanzania!
Ahsanteni Sana kwa Kunisikiliza

- May 01, 2015
HOTUBA YA RAIS WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA, MHESHIMIWA DKT. JAKAYA MRISHO KIKWETE, KWENYE KILELE CHA SIKUKUU YA WAFANYAKAZI DUNIANI, MEI MOSI, 2015 MWANZ...
Soma zaidiHotuba
Ndugu Gratian Mukoba, Rais wa Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi Tanzania (TUCTA);
Ndugu Nicholaus Mgaya, Katibu Mkuu wa Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi Tanzania (TUCTA);
Mheshimiwa Gaudentia Mugosi Kabaka, Waziri wa Kazi na Ajira;
Mheshimiwa Magesa Mulongo, Mkuu wa Mkoa wa Mwanza;
Waheshimiwa Mawaziri na Makatibu Wakuu wa Wizara;
Ndugu Alexio Musindo, Mkurugenzi Ofisi ya Shirika la Kazi Duniani (ILO) kwa nchi za Tanzania, Kenya, Rwanda na Burundi;
Ndugu Almasi Maige, Rais wa Chama cha Waajiri;
Dr. Aggrey Mlimuka, Mkurugenzi Mtendaji wa Chama cha Waajiri Tanzania (ATE);
Waheshimiwa Mabalozi;
Viongozi wa Vyama vya Wafanyakazi;
Wawakilishi wa Vyama vya Siasa;
Viongozi Waandamizi wa Serikali;
Ndugu Wananchi na Wafanyakazi Wenzagu;
Wageni Waalikwa, Mabibi na Mabwana.
Nakushukuru sana Rais wa TUCTA Ndugu Gratian Mukoba na viongozi wenzako wa vyama vya wafanyakazi kwa kunialika kuja kushiriki nanyi katika sherehe za mwaka 2015 za Mei Mosi hapa Mwanza. Aidha, natoa pongezi nyingi kwa Chama cha Wafanyakazi wa Migodi na Ujenzi Tanzania (TAMICO) ambao ndio wenyeji wetu mwaka huu kwa maandalizi mazuri ya Sherehe hizi. Hakika yamefana sana.
Sote ni mashahidi wa jinsi maandamano na maonesho ya kazi za wafanyakazi wa Tanzania yalivyopendeza. Nimesoma mengi ya mabango ya waandamanaji, napenda kuwahakikishia kuwa ujumbe umefika.
Napenda kutumia nafasi hii kuwapongeza ndugu zetu wa Mkoa wa Mwanza wakiongozwa na Mkuu wa Mkoa, Ndugu Magesa Mulongo kwa kukubali kuwa wenyeji wa maadhimisho ya sherehe hizi. Mmetupokea vizuri na kutukirimu kwa heshima kubwa. Tunajisikia tuko nyumbani.
Ndugu Rais wa TUCTA;
Kwa mara nyingine tena nakupongeza kwa kuchaguliwa kwako kuwa Rais wa TUCTA. Sisi katika Serikali tumeupokea kwa furaha uchaguzi wako. Narudia kukuhakikishia ushirikiano wangu na wa wenzangu wote katika Serikali ninayoiongoza, katika utekelezaji wa majukumu yako. Ni matumaini yetu kuwa tutashirikiana kwa ukamilifu katika kuendeleza maslahi na ustawi wa wafanyakazi wa Tanzania na nchi yetu.
Ndugu wafanyakazi;
Napenda kuchukua nafasi hii kuwapa pole kwa msiba mkubwa mlioupata wa kuondokewa na Bwana Erasto John Kihwele aliyekuwa Katibu Mkuu wa Chama cha Wafanyakazi wa Reli (TRAWU). Hakika mmepoteza kiongozi mahiri katika kujenga hoja na kupigania haki za wafanyakazi wa reli. Namkumbuka sana kwa jinsi alivyosimama kidete kutetea wafanyakazi wa TAZARA katika kikao chetu cha pamoja mwaka jana. Utetezi wake ulizaa matunda kwa kuanzishwa kwa Baraza la Wafanyakazi TAZARA. Kwa kweli sote tumepata pigo. Nawaomba muendeleze yale mazuri aliyoyasimamia. Mwenyezi Mungu ailaze roho ya Marehemu mahali pema peponi”. Ameen.
Pongezi kwa Wafanyakazi Bora
Ndugu Wafanyakazi;
Kama ilivyo ada leo tena tunawapongeza wafanyakazi wenzetu waliotekeleza vizuri majukumu yao katika maeneo yao ya kazi. Tunawapongeza kwa kazi yao njema iliyowawezesha kuibuka washindi kati ya wafanyakazi wengi walio bora. Nawapongeza na kuwasihi waendelee na ari na moyo huo wa kuchapa kazi kwa bidii, nidhamu na maarifa. Ni matumaini yangu kuwa mafanikio yao yatakuwa kichocheo kwa wengine kuongeza bidii zaidi ili waweze kufikia na hata kuzidi viwango vyao vya ubora mwakani.
Risala ya Wafanyakazi
Ndugu Rais wa TUCTA na Wafanyakazi Wenzangu;
Nimeisikiliza na kuifuatilia kwa makini sana risala ya wafanyakazi iliyowasilishwa kwa ufasaha na Katibu Mkuu wenu mahiri, Ndugu Nicholas Mgaya. Nawapongeza kwa risala nzuri iliyobeba maneno ya shukrani, changamoto, faraja na karaha za wafanyakazi. Risala yenu pia imekuwa na maoni yakinifu kuhusu namna ya kuyapatia ufumbuzi baadhi ya matatizo yaliyotajwa. Nataka kuwahakikishieni kuwa nimeisikiliza neno kwa neno na kituo kwa kituo. Nimeyasikia yale mliyosema kwa uwazi na hata yale mliyoyasema kwa mabano. Nimeyapokea, tumeyapokea na kama ilivyo kawaida yetu tutayashughulikia kwa uzito unaostahili. Baadhi yake nitayazungumzia katika hotuba yangu hii.
Kauli Mbiu
Ndugu Rais wa TUCTA;
Ndugu Wafanyakazi;
Nimefurahishwa na kauli mbiu ya Sherehe za mwaka huu isemayo “Jiandikishe, kura yako ni muhimu kwa maendeleo”. Kauli mbiu hii ni muafaka kabisa na wakati tulionao sasa. Ni kauli mbiu inayokumbusha wajibu muhimu wa kila mfanyakazi na kila Mtanzania. Kupiga kura kuchangua viongozi na, kwa ajili ya kuamua mambo muhimu kitaifa, yanayotakiwa kuamuliwa kwa Kura ya Maoni kama ilivyo Katiba Inayopendekezwa, ni haki na wajibu wa msingi wa raia. Lakini, ili mtu aweze kuitumia haki yake hiyo na kutimiza wajibu wake huo lazima awe na kitambulisho cha mpiga kura. Kitambulisho hicho hupatikana kwa kujiandikisha katika Daftari la Mpiga Kura.
Naungana nanyi kuwahimiza wafanyakazi mjitokeze kujiandikisha pale mtakapotangaziwa na Tume ya Taifa ya Uchaguzi kufanya hivyo. Ni muhimu sana kuitumia fursa hiyo vizuri kwani haitarudi itakapopita. Narudia kukumbusha kuwa watakaopiga kura mwaka huu ni wale tu wenye vitambulisho vipya vya mpiga kura. Vya zamani havitambuliki.
Ndugu wafanyakazi;
Ni ukweli usiopingika kuwa maendeleo yanategemea kuwa na Katiba nzuri na viongozi wazuri. Hivyo basi, usiipoteze fursa hii adhimu kwa ajili ya kuipigia kura Katiba Inayopendekezwa na kuchagua Rais, Mbunge, Mwakilishi na Diwani unayemuona anafaa. Hali kadhalika, ninyi mna ndugu, marafiki na kama viongozi wa kaya mnao wategemezi majumbani mwenu ambao wengine wanazo sifa za kuwa wapiga kura. Nawaomba muwakumbushe na kuwahimiza wajitokeze kujiandikisha na siku ikifika waende kupiga kura.
Ndugu Rais wa TUCTA;
Ndugu Wafanyakazi;
Hii ndiyo sherehe ya Siku ya Wafanyakazi ya mwisho kwangu kuhudhuria nikiwa Rais wa nchi yetu. Nimekuwa nanyi kwenye maadhimisho haya kila mliponialika. Katika miaka 10 ya uongozi wangu tumefanya jitihada kubwa kukuza ajira na kuinua hali za wafanyakazi nchini. Nafarijika sana kuona kuwa naondoka wakati ambapo tumefanikiwa kwa kiasi kikubwa kuyatekeleza yale tuliyopanga kufanya.
Ndugu Rais wa TUCTA;
Leo hii tukitazama tulikotoka na tulipo sasa tunaiona tofauti kubwa. Ninaposema hayo sina maana kuwa matatizo na changamoto zote za wafanyakazi zimekwisha. La hasha! Natambua pia kuwa isingelikuwa rahisi kumaliza mambo yote yanayowasibu wafanyakazi katika kipindi hiki. Tunachojivunia, ni kule kuweza kuzishughulikia kwa ufanisi changamoto za msingi za wafanyakazi. Hata hivyo ni muhimu kutambua kuwa bado tunayo kazi kubwa ya kufanya mbele yetu. Katu tusibweteke na kulevywa na mafanikio haya. Hatujafika katika safari yetu. Madamu tuko katika mwendo, tutafika.
Kuboresha Mazingira ya Kazi
Ndugu Wafanyakazi;
Kutokana na jitihada kubwa zilizofanywa na Serikali yetu tumefanikiwa kujenga taasisi, mifumo na sheria zinazoweka misingi imara ya utatuzi wa changamoto za wafanyakazi. Tumetunga Sheria na Kanuni mbalimbali kwa lengo la kulinda haki za msingi za wafanyakazi pamoja na kuweka mazingira bora ya kazi ikiwemo uhusiano kati ya waajiri na waajiriwa. Sheria na Kanuni hizi ni zile zinazohusu viwango vya kazi, hifadhi ya jamii, na ajira. Kanuni za kutekeleza Sheria ya Ajira na Mahusiano Na.6 ya 2004 zilitengenezwa na kuanza kutumika mwaka 2007.
Kuanza kutekelezwa kwa Sheria hii kumewezesha kuanzishwa na kuimarishwa kwa Taasisi mbalimbali za kazi, zikiwemo Idara ya Usimamizi Kazi na Huduma za Ukaguzi (Idara ya Kazi), Usajili wa Vyama vya Waajiri na Wafanyakazi, Mahakama ya Kazi, Tume ya Usuluhishi na Uamuzi wa Migogoro ya Kikazi (CMA), Bodi za Mshahara za Kisekta, Kamati ya Huduma Muhimu (Essential Services Committee) ya CMA na Baraza la Ushauri la Kazi, Uchumi na Jamii (LESCO). Kuwepo kwa vyombo hivi kumesaidia sana kuweka uwanja wa majadiliano kuwa sawa kati ya waajiri na waajiriwa.
Ushirikishwaji wa Wafanyakazi
Ndugu wafanyakazi;
Tangu tulipoingia madarakani katika awamu hii, tumetoa kipaumbele cha juu katika kuhakikisha kwamba ushirikishwaji wa Wafanyakazi unakuwa sehemu ya utamaduni katika sehemu za kazi. Kwa maneno mengine ni kwamba tumesisitiza utekelezaji wa matakwa ya Sheria ya Ajira na Mahusiano Kazini Na.6 ya 2004.
Juhudi zetu hizo zimezaa matunda. Tumeshuhudia Vyama vya Wafanyakazi vikiongezeka kutoka vyama vya Wafanyakazi 18 hadi 30 ambavyo vimesajiliwa ili kutetea maslahi ya Wafanyakazi. Aidha, Mashirikisho mawili (2) na Chama cha Waajiri kimoja (1) vimesajiliwa. Kwa lugha nyepesi tumewapa wafanyakazi sauti juu ya maslahi, hatima na mustakabali wao. Hata kwenye Bunge la Katiba wafanyakazi walishirikishwa kwa ukamilifu.
Mabaraza ya Wafanyakazi
Ndugu wafanyakazi;
Kwa upande wa utumishi wa umma, takwimu zinaonyesha kwamba Mabaraza ya Wafanyakazi yameundwa katika Wizara zote 26; Idara za Serikali 19; Wakala za Serikali 25 na Mamlaka za mikoa 21 na Halmashauri za Wilaya na Miji 168. Mengi ya Mabaraza hayo yamekuwa yanakutana kwa mujibu wa taratibu zilizopo. Hata hivyo zipo Idara za Serikali 4; Wakala za Serikali 7; Mikoa 5; na Mamlaka za Serikali za Mitaa 34 bado hazijaunda Mabaraza hayo kwa sababu mbalimbali.
Nimemuelekeza Waziri wa Kazi na Ajira na Katibu Mkuu Kiongozi wawabane wale wote ambao bado hawajaunda Mabaraza ya Wafanyakazi ili wafanye hivyo bila kuchelewa zaidi. Pia, kwa wote, waliounda Mabaraza na wale wote watakaounda ihakikishwe kuwa mabaraza hayo yanakutana mara mbili kwa mwaka kama Sheria inavyotaka. Kisingizio cha uhaba wa fedha hakiniingii akilini hata kidogo. Mbona sijawahi kusikia viongozi wamekosa posho za safari na vikao vyao! Hayo ni matakwa ya kisheria, na ni agizo la Rais hivyo lazima kupewa kipaumbele katika utekelezaji.
Ndugu wafanyakazi;
Jambo jingine zuri ambalo tumelifanya kwa ufanisi katika kipindi hiki ni kuwa na utaratibu wa Rais kukutana na Viongozi wa Vyama vya Wafanyakazi. Tulianza kwa kukutana mara moja baadae tukaongeza na kuwa mara mbili kwa mwaka. Japo wakati mwingine imekuwa sio rahisi sana kukutana mara mbili kwa sababu ya ratiba za Rais, lakini hatukukosa kukutana angalau mara moja.
Mimi na viongozi wa vyama vya wafanyakazi ni shahidi kwamba vikao hivi vimesaidia sana kuleta maelewano baina ya Serikali na Vyama vya Wafanyakazi na hivyo baina ya Serikali na wafanyakazi. Vikao hivi vimekuwa fursa maalum ya kuzungumzia masuala mbalimbali yanayowahusu wafanyakazi na kuyatafutia ufumbuzi. Ukweli ni kwamba matatizo mengi tumeweza kuyatatua hata yale ambayo wakati mwingine yalionekana kuwa magumu sana.
Mwaka huu tumeshakutana mara moja. Ni matumaini yangu kuwa tutapata fursa ya kukutana tena, kabla sijang’atuka. Utakuwa mkutano wa kuagana. Nitamnong’oneza Rais ajaye kuhusu manufaa ya utaratibu huu, ili ikimpendeza auendeleze. Huu ni utaratibu wa kisheria, umekuwa na manufaa makubwa sana. Kama mlivyosema, umesaidia kujenga maelewano mazuri na ushirikiano baina ya Serikali na wafanyakazi, jambo ambalo ni muhimu sana katika kuleta mustakabali mwema nchini. Naikumbuka pia ahadi yangu ya kukutana na viongozi wa Chama cha Waajiri. Nitatafuta wasaa hivi karibuni tukutane.
Usuluhishi wa Migogoro ya kikazi
Ndugu Wafanyakazi;
Katika awamu hii tumejitahidi sana kushughulikia migogoro ya kikazi kwa kupunguza muda wa mashauri kusikilizwa na hivyo kuwezesha wafanyakazi kupata haki zao kwa wakati. Kama nilivyosema awali, mwaka 2008 tulianzisha Tume ya Usuluhishi na Uamuzi (CMA) ambayo jukumu lake ni kushughulikia migogoro ya kikazi. Tangu kuanzishwa kwake Taasisi hii imefanikiwa kushughulikia migogoro ya kikazi 10,281 ambapo migogoro 6,057 imeshatolewa uamuzi. Tume imeweza kupunguza muda wa kusuluhisha na kusikiliza mashauri ya migogoro ya kazi kutoka wastani wa siku 30 hadi 12 na muda wa kuamua umepungua kutoka wastani wa siku 90 hadi 85.
Kupungua kwa muda wa mashauri kusikilizwa na kuamuliwa maana yake ni kupunguza usumbufu na madhila kwa mfanyakazi ambaye hapo awali alichelewa sana kupata haki yake. Wakati mwingine kuchelewa kupata haki kwa wakati kulitafsiriwa kama haki iliyodhulumiwa. Utaratibu huu umepunguza pia mlundikano wa kesi za masuala ya kazi mahakamani. Kasoro mlizozitaja katika risala yenu kuhusu utendaji wa CMA tutazifanyia kazi.
Usimamizi wa Ajira
Ndugu Wafanyakazi;
Kumekuwepo na malalamiko ya wafanyakazi juu ya kukithiri kwa idadi ya wageni wasio na sifa za kufanya kazi nchini ambao wanaajiriwa. Niliahidi katika hotuba yangu ya Mei Mosi mwaka jana kwamba tutatunga Sheria maalum na kuweka utaratibu wa kisheria wa kusimamia ajira za wageni nchini. Aidha, nilimwelekeza Waziri wa Kazi na Ajira akamilishe kanuni za kusimamia mawakala binafsi wa huduma za ajira.
Nafurahi kuwa ahadi yangu ile imetimia kwa kutungwa kwa Sheria ya Kuratibu Ajira za Wageni katika Bunge la Machi, 2015. Kilichobakia sasa ni Waziri wa Kazi na Ajira kutengeneza Kanuni za utekelezaji wa Sheria hiyo. Ningependa kazi hiyo ikamilike mapema ili Sheria ianze kutumika mapema iwezekanavyo.
Ndugu Wafanyakazi;
Kuhusu makampuni ya mawakala wa ajira, Serikali imekwishaweka utaratibu mzuri wa kuyatambua, kuyasajili upya na kuyatengenezea kanuni za kuongoza utendaji wao. Kwa ajili hiyo, hivi sasa Wizara inaweza kuyakagua na kujiridhisha iwapo yanafuata sheria za kazi. Tayari makampuni 96 yameshasajiliwa. Hata hivyo, ili shughuli hii iweze kufanikiwa ushirikiano wa wafanyakazi ni muhimu. Inasikitisha kusikia kuwa, wapo wafanyakazi wanaokataa kutoa taarifa za ukiukwaji wa Sheria unaofanywa na makampuni haya kwa kuogopa kupoteza ajira zao.
Napenda kuwahakikishia kuwa, Serikali itasimamia kwa nguvu zote utekelezaji wa jambo hili. Haitasita kuchukua hatua stahiki dhidi ya Mawakala watakaokiuka sheria za ajira nchini, watakapobainika kufanya hivyo. Tafadhalini timizeni wajibu wenu wa kutoa taarifa kuhusu wale wanaovunja Sheria na taratibu.
Hifadhi ya Jamii
Ndugu Wafanyakazi;
Katika kipindi cha miaka 10 ya uongozi wa Serikali ya Awamu ya Nne tumeboresha sana huduma ya hifadhi ya jamii ambayo ni moja ya haki za msingi kwa wafanyakazi. Hivi sasa tunaangalia uwezekano wa kujumuisha makundi mengine wakiwemo wakulima na wazee.
Mabadiliko ya kisheria na kisera tuliyochukua yameongeza wigo wa mafao, aina ya mafao na ongezeko la mafao kwa wafanyakazi. Takwimu zinaonyesha kwamba idadi ya Mifuko ya Hifadhi ya Jamii imeongezeka toka Mifuko 5 mwaka 2005 hadi mifuko 7 hivi sasa. Hali kadhalika, kumekuwepo na ongezeko kubwa la wanachama na wale wanaofaidika na huduma za hifadhi ya jamii hususan wafanyakazi na wategemezi wao. Idadi imeongezeka kutoka 690,000 mwaka 2005 hadi 6,400,000 mwaka 2014. Haya ni mafanikio makubwa sana.
Ndugu Rais wa TUCTA na wafanyakazi;
Habari nyingine njema ni kuwa hatimaye kile kilio chenu cha kutaka kuoanisha mafao ya mifuko ya hifadhi ya jamii kwa kuwa na kokotoo la aina moja kimepata ufumbuzi. Matokeo yake ni kwanza, kwamba mafao ya malipo ya pensheni ya mwezi sasa yameongezeka kwa asilimia 5 kutoka asilimia 67 hadi asilimia 72.5. Pili, ni kuwekwa kwa kiwango cha chini cha asilimia 40 ya mshahara hata kwa mwanachama ambaye pensheni yake ingekuwa chini ya asilimia 40 ya mshahara. Hii ina maana kuwa hakuna mwanachama wa mfuko wowote atakayepata pensheni ya chini ya asilimia 40 ya mshahara hata kama kwa masharti ya mfuko wake kabla ya uamuzi huu angestahili kupata chini ya hapo. Uamuzi huu unajenga usawa wa mafao kwa wanachama wote wa mifuko yote.
Ndugu Wafanyakazi;
Napenda kusisitiza kuwa mabadiliko haya hayataathiri wanachama wa mifuko ya PSPF na LAPF ambao waliajiriwa kabla ya kuanza kutumika kwa mfumo mpya wa ukokotoaji tulioanza tarehe 1 Julai, 2014. Najua ipo hofu fulani ambayo na hata katika mkutano wangu na viongozi wa Vyama vya Wafanyakazi ilijitokeza (na leo pia imeelezwa kwenye risala yenu). Tulikubaliana mazungumzo zaidi yafanyike kati ya TUCTA na SSRA kuhusu jambo hili. Hivyo nawaomba muwe na subira. Heri itapatikana kama walivyosema Wahenga.
Nafurahi kutoa taarifa kuwa ufumbuzi umepatikana kuhusu suala la mafao kwa wale wafanyakazi ambao wakati wa utumishi wao, kabla ya kustaafu walichangia mifuko tofauti. Hawa ni wale ambao walihama au kuhamishwa kutoka Halmashauri za Wilaya na Miji na kwenda Serikali Kuu au kinyume chake. Kwa sababu hiyo wamechangia katika mifuko tofauti. Wanapostaafu wamekuwa wanapata ugumu katika malipo na kujikuta wanapoteza haki na stahili za utumishi wao wa muda mrefu. Mwongozo wa kuunganisha michango ya wanachama waliochangia katika mfuko zaidi ya mmoja umeshatolewa na umeanza kutumika tangu tarehe 25 Aprili, 2014. Tatizo limemalizika na tayari SSRA imeshatatua malalamiko ya wanachama wapatao 11,070 waliokuwa wamekabiliwa na matatizo ya namna hii.
Mfuko wa Fidia
Ndugu Wafanyakazi;
Kile kilio cha siku nyingi cha fidia ya wafanyakazi wanaoumia kazini nacho kimefutwa machozi. Mfuko wa Fidia ya Wafanyakazi (Workers Compensation Fund) umeanzishwa kwa mujibu wa Sheria ya Fidia ya Wafanyakazi Na.20 ya mwaka 2008. Nimeshafanya uteuzi wa Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko Ndugu Masha Mshomba na Mwenyekiti wa Bodi ya Wadhamini Ndugu Emmanuel Humba. Waziri wa Kazi na Ajira ameshateua Wajumbe wa Bodi hivyo kazi imeanza. Kazi inayoendelea sasa ni kuandaa kanuni za uendeshaji wa Mfuko huo zinazotarajiwa kukamilika Juni, 2015.
Kama nilivyosema mwaka jana, Mfuko huu utachangiwa na waajiri wote yaani Serikali na wa sekta binafsi. Mfuko utaondoa ule mwanya wa baadhi ya waajiri kukwepa wajibu wa kulipa fidia pale yanapotokea madhara kwa wafanyakazi wao. Kwa hatua hii wafanyakazi sasa wana hakika ya kulipwa fidia stahiki.
Maslahi ya Wafanyakazi
Ndugu Rais wa TUCTA;
Wafanyakazi Wenzangu;
Jambo lingine ambalo tumejitahidi kufanya bila ajizi ni kuboresha maslahi ya wafanyakazi. Pamoja na changamoto tulizonazo kwa upande wa mapato na ukubwa wa majukumu ya serikali tumechukua hatua za makusudi kuongeza kima cha chini cha mishahara katika utumishi wa umma kila mwaka tangu tuingie madarakani. Kwa ajili hiyo, katika utumishi wa umma, kwa mfano, kima cha chini cha mshahara mwaka 2005 kilikuwa shilingi 65,000, mwaka 2014 kima cha chini kimeongezeka na kufikia shilingi 265,000. Ni nyongeza ya zaidi ya mara nne. Najua kwa hali ilivyo sasa ongezeko hili bado ni ndogo lakini si haba. Naahidi kuwa na mwaka huu pia tutaongeza.
Punguzo la Kodi kwa Wafanyakazi (PAYE)
Ndugu wafanyakazi;
Tumeendelea kupunguza kiwango cha kodi ya mapato kwa wafanyakazi (PAYE) mwaka hadi mwaka tangu 2005 hadi sasa. Kwa ajili hiyo, kodi hiyo iliyokuwa asilimia 18 sasa ni asilimia 12. Na mwaka huu pia tutaendelea kupunguza kodi ya mapato kwa wafanyakazi. Natambua kuwa maombi yenu ni kutaka iwe chini ya asilimia 10. Hatukuweza kufikia hapo mwaka huu lakini safari tuliyoianza na hapo tutakapofikia itabakisha padogo sana kufikia tunapopataka sote.
Ndugu Wafanyakazi;
Kama nilivyosema mwaka jana, kwa upande wa wafanyakazi katika sekta binafsi kima cha chini kinapangwa na Bodi za Mishahara za kisekta zinazoundwa na Waziri wa Kazi. Hadi kufikia mwaka 2011 tulikuwa nazo Bodi 12 ambazo zimewezesha majadiliano na waajiri wa sekta binafsi kufanyika. Matokeo yake ni kima cha chini cha mshahara kupanda kutoka shilingi 48,000 kwa mwezi hadi kati ya shilingi 100,000 na 400,000 kutegemeana na sekta. Kwa kuwa bodi hizo zinakutana kila baada ya miaka mitatu, na mara ya mwisho mishahara iliongezwa mwaka 2013 hivyo basi viwango vipya vinatarajiwa kutangazwa mwaka 2016.
Naambiwa kuwa bado wapo waajiri wasiolipa viwango hivi ambavyo vimekubaliwa kwa pamoja baina yao na wafanyakazi. Hili si jambo la kiungwana na linalonihuzunisha sana. Ndugu Almasi tusaidie tabia hii iachwe. Nazitaka mamlaka husika kutimiza ipasavyo wajibu wao wa kuhakikisha maamuzi ya Bodi yanatekelezwa. Tusikubali watu hao wakaendelea kudhulumu haki za wafanyakazi. Pendekezo la kutaka kuwepo na Bodi moja badala ya kila sekta kuwa na Bodi yake limepokelewa na litafanyiwa kazi kwa mujibu wa taratibu zilizopo.
Wakala wa Afya na Usalama Mahali pa Kazi (OSHA)
Ndugu Wafanyakazi;
Serikali yetu imetoa umuhimu mkubwa kwa uimarishaji wa afya ya wafanyakazi na usalama mahala pa kazi. Mafanikio makubwa yamepatikana. Kati ya mwaka 2010 na 2015 Wakala wa Afya na Usalama Mahala pa Kazi (OSHA) umefanya kaguzi za kawaida 26,000 na kaguzi maalumu 53,000. Hali kadhalika, wafanyakazi wapatao 435,063 wamepimwa afya zao kwa lengo la kubaini matatizo na athari wazipatazo wakati wakiwa kazini na hata baada ya kuacha kazi. Mwaka 2014, OSHA imefanya ukaguzi kwenye migodi yote nchini na kutoa maelekezo juu ya namna ya kuboresha hali katika migodi hiyo. Tutaendelea kuiimarisha OSHA ili iweze kufanya kaguzi nyingi zaidi na kwa wakati muafaka.
Marekebisho ya Miundo na Madai ya Wafanyakazi
Ndugu Wafanyakazi Wenzangu;
Katika kipindi cha miaka 10 hii, tumefanya marekebisho ya miundo ya utumishi ya kada mbalimbali za utumishi wa umma. Miundo miwili ninayopenda kuzungumzia leo ni ile ya walimu na wauguzi. Kwa upande wa walimu, muundo wa walimu umeidhinishwa na utekeleaji wake umeanza tangu Julai, 2014. Nimeambiwa kuwa utekelezaji haujaanza kote kwa wakati mmoja, lakini nimehakikishiwa kuwa wote watahamia kwenye muundo mpya katika mwaka ujao wa fedha.
Sambamba na hili la muundo, malimbikizo ya stahili za walimu yameendelea kulipwa. Mwaka huu madai ya deni la walimu yalikuwa shilingi bilioni 53,185,440,406 yanayowahusu na walimu 70,668 yalipokelewa. Uhakiki umefanyika na tayari, walimu 29,243 wamekwishalipwa jumla ya shilingi bilioni 23,233,654,025. Madai mengine ya walimu 7,169 ya jumla ya shilingi 9,285,283,600 yataanza kulipwa mwezi Agosti, 2015. Katika uhakiki uliofanywa, madai ya walimu 30,807 yenye thamani ya shilingi bilioni 17,346,593,468 yamekutwa na dosari na hivyo kurejeshwa kwenye Halmashauri na kwa wahusika kufanyiwa masahihisho. Napenda kuwahakikishia kuwa hizo zikirekebishwa malipo yatafanyika. Fanyeni hima jambo hili tulimalize.
Ndugu Rais wa TUCTA;
Tumekwishapeleka Bungeni Muswada wa Sheria ya kuanzisha Tume ya Utumishi wa Walimu (Teachers Service Commission) ambao tayari umesomwa kwa mara ya kwanza. Aidha, tunakamilisha maandalizi ya kuwasilisha Bungeni Muswada wa kuanzisha Bodi ya Taifa ya Taaluma za Walimu (National Teachers Professional Board). Yote haya yanathibitisha dhamira na utashi wetu kushughulikia masuala ya walimu na wafanyakazi kwa jumla. Shemeji zangu walimu baada ya kufanya hayo nina hakika nawaacha pazuri.
Nimefurahishwa na uamuzi wenu walimu wa kufungua Benki ya Walimu. Nawapongeza sana kwa hatua hii kubwa na ya maendeleo. Sisi katika Serikali tunaunga mkono juhudi za walimu na tunaahidi kutoa ushirikiano wa kuwezesha lengo lenu hili jema kutimia.
Ndugu Wafanyakazi;
Kwa upande wa kada ya wauguzi, mtakumbuka kuwa tulirekebisha muundo ambao umeanza kutumika tarehe 1 Julai, 2010. Tumepokea malalamiko kuwa mabadiliko hayo yameathiri baadhi ya wauguzi kwa viwango vyao vya mshahara kushuka baada ya kuanza kutumika kwa muundo mpya. Hili ni kosa ambalo halikustahili kutokea. Nimeelekeza lirekebishwe, mara moja. Nimeagiza wale ambao mishahara yao imeshushwa, warejeshewe mishahara yao ya awali na malimbikizo yao walipwe. Hali kadhalika, nafurahi kuwa yale maombi ya kutaka ianzishwe Kurugenzi ya kada ya wauguzi na wafamasiya nayo yamefanyiwa kazi. Kibali kimetolewa na Menejimenti ya Utumishi wa Umma kwa Kurugenzi hizo kuanzishwa. Kwa sasa ni kitengo.
Ndugu Wafanyakazi;
Katika kipindi hiki, tumeendelea kushughulikia na kufanikiwa kutatua kero nyingine nyingi za wafanyakazi. Kati ya mwaka 2005 na 2010, jumla ya watumishi 476,430 wamepandishwa vyeo. Aidha, kati ya mwaka 2012 na 2015, kwa mfano,jumla ya watumishi 125,372 wamelipwa malimbikizo ya jumla ya shilingi bilioni 123,141,755,959.68. Nimewaagiza ndugu zetu wa Hazina waanze kulipa madeni ya wafanyakazi wa Serikali za Mitaa yanayofikia shilingi bilioni 18,029,441,595.
Kwa kweli, mtakubaliana nami kuwa tumejishughulisha kwa kadri ya uwezo wetu kutafuta majawabu kwa kero na matatizo yanayowakabili wafanyakazi nchini. Hapajakuwako na upungufu wa dhamira upande wetu. Kwa yale ambayo hatukuweza kuyafanya ni kwa sababu ya ugumu wa tatizo lenyewe kulipatia ufumbuzi au kwa sababu ya uhaba wa pesa. Hakuna jambo ambalo hatukujaribu kulishughulikia na juhudi zinaendelea. Hata wakati huu ambapo nafikia ukingoni mwa kipindi changu cha uongozi, naendelea na nitaendelea kuyashughulikia mambo ya wafanyakazi mpaka nitakapokabidhi kijiti kwa kiongozi wetu mpya. Ninawaomba tuendelee kushirikiana mpaka wakati huo na muendelee kushirikiana na Serikali ya Awamu ya Tano kama mlivyofanya wakati wangu. Tena ningefurahi kuona ushirikiano wenu ukiwa mkubwa zaidi hata kuliko wakati wangu. Ni jambo lenye maslahi kwa pande zote: Serikali, wafanyakazi na nchi yetu.
Fursa za Ajira
Ndugu Wafanyakazi;
Serikali imeendelea kuchukua hatua za kukabiliana na tatizo la ajira nchini. Itakumbukwa kuwa katika Ilani ya Uchaguzi ya mwaka 2005 – 2010 Chama cha Mapinduzi kiliahidi ajira mpya milioni moja. Tulifanikiwa kuzalisha ajira milioni 1,271,923 ambazo ni zaidi ya lengo. Katika kipindi cha miaka mitano hii, tayari tumeshazalisha ajira milioni 1,381,621. Na hivyo kufikisha jumla ya ajira milioni 2,653,544 katika kipindi cha miaka 10. Kati ya hizo ajira 600,547 zilitokana na sekta ya umma na ajira milioni 2,052,997 zimetokana na sekta binafsi.
Pamoja na mafanikio hayo, bado tatizo la ukosefu wa ajira ni kubwa hapa nchini na hasa miongoni mwa vijana. Hivyo basi, tutaendelea na tunaendelea na utekelezaji wa mikakati na mipango ya kukuza ajira nchini. Wizara ya Kazi na Ajira ikishirikiana na Ofisi ya Taifa ya Takwimu, imefanya utafiti wa nguvu kazi nchini tangu mwezi Februari, 2014 ambao unatarajiwa kukamilika ifikapo mwezi Mei, 2015. Utafiti huu utatoa taarifa za soko la ajira nchini ikijumuisha hali halisi ya kiwango cha ukosefu wa ajira kwa vijana.
Napenda kurudia maneno niliyowahi kuyasema awali kuwa, kwa wakati wa sasa uwezo wa sekta ya umma kuajiri watu wengi si mkubwa na kwamba jawabu la ajira liko katika sekta binafsi. Azma ya Serikali ni kuendelea kujenga mazingira mazuri ya kurahisisha ukuaji wa sekta binafsi na kuvutia wawekezaji kuongeza mitaji ili kuongeza ajira. Tumefanya hivyo, na matokeo yake tumeyaona. Tutaendelea kufanya hivyo, sasa na siku zijazo.
Hitimisho
Ndugu Rais wa TUCTA;
Ndugu Wafanyakazi;
Naomba nimalize hotuba yangu kwa kurudia kuwashukuru kwa dhati Wafanyakazi wote na viongozi wote wa vyama vya wafanyakazi nchini kwa ushirikiano mlionipa katika kipindi chote cha uongozi wangu. Kimsingi ushirikiano na ushauri wenu ulikuwa wa msaada mkubwa sana kwangu na wenzangu wote katika Serikali kuhusu namna iliyo bora ya kuzikabili changamoto mbalimbali za wafanyakazi nchini. Ushirikiano wetu huo ndio uliotuwezesha kwa pamoja kuzitafutia ufumbuzi. Najua kwamba hazikuisha zote. Nawaahidi kuwa Rais ajaye nitamkabidhi orodha ya yale ambayo bado ni kiporo. Ni imani yangu kwamba mtaendelea kutoa ushirikiano kwa Serikali ya Awamu ya Tano itakayokuwapo baada ya uchaguzi mkuu wa Oktoba, 2015.
Ndugu wafanyakazi;
Narudia kuwashukuru tena kwa kunialika kwenye sherehe za mwaka huu ambazo zinanipa nafasi ya kuagana nanyi kama Rais wa Jamhuri ya Muungano Tanzania. Nawashukuru sana kwa wema wenu huo mlionifanyia. Nawatakia kila la heri katika kutimiza majukumu yenu ya ujenzi wa nchi yetu. Daima nitawakumbuka. Ninawapenda sana na nitaendelea kuwapenda.
Mungu Ibariki Afrika!
Mungu Ibariki Tanzania!
Asanteni kwa kunisikiliza.

- Apr 28, 2015
HOTUBA YA RAIS WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA NA AMIRI JESHI MKUU, MHESHIMIWA DAKTARI JAKAYA MRISHO KIKWETE, KWENYE UZINDUZI WA MELI VITA ULIOFANYIKA MAKAO...
Soma zaidiHotuba
Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa, Mheshimiwa Dkt. Hussein Ali Mwinyi (Mb);
Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Mheshimiwa Mecky Sadick;
Balozi wa Jamhuri ya Watu wa China nchini Tanzania, Mheshimiwa Lu Youging;
Katibu Mkuu Kiongozi, Balozi Ombeni Sefue;
Katibu Mkuu Wizara ya Ulinzi na JKT, Job Masima;
Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi, Jenerali Davis Mwamunyange;
Makatibu Wakuu wa Serikali Mliopo;
Mnadhimu Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi, Luteni Jenerali Samwel Ndomba;
Viongozi mbalimbali wa Serikali mliopo;
Wakuu wa Vyombo vya Ulinzi na Usalama;
Wakuu wa Kamandi za Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania;
Majenerali mliopo;
Wawakilishi kutoka Jeshi la Ukombozi la Jamhuri ya Watu wa China;
Maafisa na Wapiganaji;
Wageni Waalikwa;
Mabibi na Mabwana.
Shurani na Pongezi
Mheshimiwa Waziri wa Ulinzi;
Nakushukuru Waziri na Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi kwa kunialika kwenye hafla hii muhimu ya uzinduzi wa Meli Vita za Jeshi la Wanamaji la JWTZ. Natoa pongezi nyingi kwa CDF, Kamanda wa Navy na wanajeshi wote kwa hatua nyingine muhimu tunayopiga katika kuimarisha uwezo wa Jeshi letu kutekeleza majukumu yake kwa upande wa mpaka wetu wa majini. Kwa niaba yenu napenda kuwashukuru ndugu zetu na marafiki zetu wa Jamhuri ya Watu wa China kwa kutupa meli hizi ambazo tunazizindua leo. Ni ukweli usiofichika kuwa hatuna mshirika mkubwa kwa maendeleo ya Jeshi letu kushinda Wachina. Wamekuwa nasi tangu JWTZ lilipoanza miaka 51 iliyopita. Kwa kweli, hatuna maneno mazuri ya kuwashukuru zaidi ya kusema asanteni sana. Natoa shukrani maalum kwa kampuni ya Poly Technologies Inc. kwa ushirikiano wenu. Ni moja ya kampuni muhimu inayotupatia silaha na zana za kijeshi.
Tukio Linatuunganisha na Wananchi wa China
Maafisa na Wapiganaji;
Mabibi na Mabwana;
Kupatikana kwa MELI VITA MWITONGO na MELI VITA MSOGA kunaandika histori mpya katika kuliwezesha Jeshi letu la Wanamaji katika utendaji wake. Kama mnavyojua, Jeshi letu la Wanamaji lilianzishwa rasmi mwaka 1971 kwa msaada wa Serikali ya Jamhuri ya Watu wa China. Serikali ya China ilitoa idadi ya meli 13 na kutujengea vituo vitatu vya Rada kwa ajili ya uchunguzi wa Pwani; na kutujengea karakana na chelezo (slipway).
Pia marafiki zetu wa China wametupa wataalam mbalimbali kwa ajili ya karakana na chelezo, wametupa nafasi nyingi za mafunzo nchini kwao kwa ajili ya maofisa na askari wetu; na wametuanzishia Kombania mbili za Marine Special Forces. Hii ni pamoja na kugharamia mafunzo na vifaa vyake.
Ndugu zetu hawa wanaendelea kutupatia waalimu na wakufunzi kwa ajili ya shule yetu ya Ubaharia. Kwa ujumla, kwa mrefu Kamandi ya Navy ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania imekuwa ikipata misaada mbalimbali kutoka Jeshi la Ukombozi la Watu wa China.
Usione vinaelea vimeundwa. Haya yote ni ya udugu na urafiki baina ya nchi zetu ulioasisiwa na viongozi waasisi na mataifa yetu mawili: yaani Chairman Mao Tse Tung wa China na Julius Nyerere. Pia ni kutokana na kazi nzuri iliyofanywa na viongozi waliofuatia. Naahidi kuwa sisi Tanzania tutaenzi na kudumisha uhusiano huu wenye tija kubwa kwa nchi zetu mbili.
Meli Zimekuja muda Muafaka
Waheshimiwa Viongozi;
Mabibi na Mabwana;
Kwa mujibu wa maelezo niliyopewa, meli hizi - MELI VITA MWITONGO na MELI VITA MSOGA - zinaweza kwenda kwa kasi, zikiwa na silaha za ulinzi kwa kiwango cha kuweza kutoa ulinzi wa kutosha. Pia zinaweza kukaa baharini kwa muda mrefu na kufanya kazi kwa umbali mrefu. Uwezo mkubwa wa meli hizi kulinda maji yetu na EEZ ni hazina kwetu na faraja kubwa kwa Taifa letu. Tuendelee kuwa na ushirikiano na Serikali na Jeshi la Jamhuri ya Watu wa China ili tuzidi kuvuna zaidi kutokana na uzoefu wao.
Upatikanaji wa Meli Vita hizi umekuja wakati muafaka ambapo nchi yetu inahitaji ulinzi wa bahari wa kutosha kwa kushirikiana na majirani zetu wa Kenya, Msumbiji na mataifa mengine katika kupambana na uharamia wa baharini. Kutokana na meli hizi, eneo letu la bahari sasa litakuwa salama kwani tunaweza kulilinda kwa uhakika. Zitasaidia kuchagiza maendeleo ya kiuchumi kwa taifa letu kupitia ulinzi wa rasilimali za baharini. Kama mjuavyo, tuna samaki wengi baharini wanaoibiwa bila sisi kujua. Tuna gesi asilia ambayo ni tumaini kubwa kuitoa nchi yetu hapa tulipo na kuipeleka mbele kwenye maendeleo. Lazima rasilimali hiyo tuilinde. Namna pekee ya kuweza kuhakikisha usalama wa mipaka yetu na rasilimali za bahari ni kuwa na vifaa vya kutosha na vya kisasa, kama meli vita hizi tunazozizindua leo. Aidha, ari ya utendaji kazi kwa maafisa na askari wa Kamandi ya Navy pia itazidi kuongezeka.
Meli Zitumiwe kwa Ufanisi
Kamanda wa Navy;
Hongereni kupata zana na silaha mpya katika Kamandi yenu. Bila ya shaka itawaongezea ari ya utendaji kazi wa maafisa na askari. Kwa hiyo, napenda kutumia nafasi hii pia, kuwasihi mzitumie vizuri meli hizi, na hasa hasa mzitunze ili ziweze kutimiza majukumu yaliyokusidiwa na kwa ufanisi mkubwa. Kufanya hivyo ni kwa manufaa ya Jeshi lenyewe na kwa manufaa ya Taifa kwa ujumla, katika utendaji wenu wa shughuli za ulinzi katika maeneo yetu ya Bahari ya Hindi. Aidha, tutunze kwa umakini mkubwa vifaa na zana mbalimbali kama hizi zinazowawezesha kutekeleza majukumu yenu.
Kila fursa ya kiuchumi inapojitokeza, Serikali itaendeleza juhudi zake za kiliimarisha jeshi letu kwa kulipatia vifaa vya kisasa na kuwawezesha maafisa wake kuwa na uwezo mkubwa wa kulinda mipaka yetu. Pia tutazidi kuimarisha upatikanaji wa huduma nyingine muhimu za msingi ikiwa ni pamoja na malazi bora na mavazi nadhifu.
Hitimisho
Waheshimiwa Viongozi ;
Mabibi na Mabwana ;
Mwisho, napenda kuwapongeza Mheshimiwa Waziri wa Ulinzi na JKT, Mkuu wa Majeshi na wale wote kwa namna mbalimbali walivyotoa michango yao kufanikisha kupatikana meli hizi. Nichukue nafasi hii pia, kuwashukuru na kuwapongeza Maafisa na Askari wa Kamandi ya Navy kwa kazi nzuri wanayoifanya katika majukumu yao ya kulinda nchi yetu na hasa zinazohusiana na operesheni mbalimbali za baharini.
Aidha, nawapongeza pia wote walioshiriki katika maandalizi ya shughuli hii ya leo. Wamefanya kazi kubwa inayostahili pongezi za dhati. Tuendelee kushirikiana katika majukumu kama haya ili kuliwezesha Taifa letu kusonga mbele katika maendeleo ambayo yanategemea sana ulinzi imara.
Asanteni sana!

- Apr 13, 2015
HOTUBA YA MHE. DKT. JAKAYA MRISHO KIKWETE, RAIS WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA KWENYE MAADHIMISHO YA SIKU YA MWALIMU NYERERE (NYERERE DAY) NA UZINDUZI WA PR...
Soma zaidiHotuba
Mheshimiwa Dkt. Shukuru Kawambwa, Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi;
Mhe. Meck Said Sadick, Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam;
Mhe. Bi Sophia Mjema, Mkuu wa Wilaya ya Temeke;
Mheshimiwa Dkt. Terezya Huvisa, Kaimu Mwenyekiti wa Bodi ya Chuo;
Prof. Shadrack S. Mwakalila, Mkuu wa Chuo cha Kumbukumbu ya Mwalimu Nyerere;
Mheshimiwa Pius Msekwa, Spika Mstaafu wa Bunge la Jamhuri ya Muungano;
Waheshimiwa Mabalozi;
Ndugu Wanataaluma na Wafanyakazi Waendeshaji wa Chuo;
Ndugu Wanafunzi;
Ndugu Wanajumuiya ya Chuo;
Ndugu Wageni Waalikwa;
Mabibi na Mabwana.
Mheshimiwa Waziri wa Elimu,
Ninakushukuru sana Mheshimiwa Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi na pamoja na Mkuu wa Chuo cha Kumbukumbu ya Mwalimu Nyerere Kivukoni kwa kunialika Chuoni hapa siku ya leo. Nawapongeza kwa uamuzi wenu wa busara wa kuanzisha Programu Maalum ya Mafunzo ya Uongozi na kuizindua leo tarehe 13 Aprili, 2015 siku ya kumbukumbu ya kuzaliwa Hayati Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere miaka 93 iliyopita.
Pongezi kwa Chuo cha Kumbukumbu ya
Mwalimu Nyerere
Ndugu Wageni Waalikwa;
Nakupongeza sana Kaimu Mwenyekiti wa Bodi ya Chuo, Mkuu wa Chuo, wakufunzi na wafanyakakazi wote kwa kazi nzuri mnayoifanya na kwa mafanikio yanayoendelea kupatikana hapa Chuoni. Katika miaka 10 ya uhai wake Chuo kimekua sana. Kama alivyoeleza Mkuu wa Chuo, mmefungua tawi kule Zanzibar na sasa mnadahili wanafunzi 4,000 hapa Kivukoni na 2,400 kule Zanzibar. Aidha mnaendesha mafunzo ya ngazi za awali (foundation), cheti, stashahada na shahada hapa Kivukoni na katika Tawi la Zanzibar. Nawapongeza sana kwa upanuzi huu mkubwa.
Programu ya Uongozi na Maadili
Ndugu Mkuu wa Chuo;
Nakosa maneno mazuri ya kuelezea furaha yangu kwa uamuzi wenu wa kuanzisha Programu Maalum ya Uongozi na Maadili. Nafurahi kuwa mnafanya moja ya mambo muhimu yaliyokuwa yanafanywa na Chuo cha Kivukoni wakati ule kabla ya kuwa Chuo cha Sayansi ya Jamii cha Kivukoni na sasa Chuo cha Kumbukumbu ya Mwalimu Nyerere.
Napenda mjue kwamba hapa palikuwa hoteli iliyoitwa Ghana Hotel. Mwaka 1961, hoteli hiyo ilinunuliwa na kuanzishwa Chuo cha Kivukoni ambacho madhumuni yake ni kuwaendeleza kwa elimu na mafunzo vijana wa kiafrika ambao hawakupata elimu nzuri. Walengwa hasa walikuwa vijana waliojiunga na harakati za kudai uhuru ili waweze kujiendeleza maishani. Miongoni mwa wanufaikaji ni pamoja na hayati Kighoma Malima ambaye aliacha shule darasa la 10 na kushiriki harakati za kudai Uhuru. Alikuja Chuoni hapo akaendelezwa na baadaye kwenda Marekani kusoma zaidi na hata kufikia kuwa mchumi bingwa aliyetambulika kimataifa.
Chuo kilianza kwa kufundisha masomo ya sayansi ya jamii na walimu wake walikuwa wa kutoka nje hususan Uingereza, Canada na Marekani. Ilikuwa hivyo kwa sababu wasomi wazalendo walikuwa wachache sana. Baadaye ndipo walipoajiriwa kidogo kidogo mpaka hatimaye wazungu walipoondoka.
Baada ya Azimio la Arusha, Mwalimu Nyerere aliagiza Chuo kifundishe Azimio hilo kwa viongozi wa Chama na Serikali. Mwaka 1972 Chuo kikabadilika kabisa na kuwa cha mafunzo ya siasa na uongozi. Kwa ajili hiyo, viongozi wa ngazi mbalimbali wa Chama wakati ule, Serikali na taasisi zake wakiwemo wa vyombo vya ulinzi na usalama na mashirika ya umma walipitia Kivukoni. Walipatiwa mafunzo ya siasa, ya uongozi maadili. Mimi ni mmoja wa wanafunzi waliopitia na kuhitimu katika Chuo hiki. Lengo lilikuwa ni kuwawezesha kuwa viongozi wanaoweza kutimiza ipasavyo majukumu yao uongozi katika taifa linalojitegemea na la kijamaa. Viongozi pia ambao ni waadilifu wanaotambua na kuheshimu miiko ya uongozi. Katika mafunzo yale miiko ya uongozi kwa mujibu wa Azimio la Arusha yalikuwa yanafundishwa.
Baada ya mageuzi ya kiuchumi na ya kisiasa, na Chama cha Mapinduzi kuachana na vyuo vya siasa, kukatokea ombwe kubwa kwa upande wa mafunzo ya uongozi. Si vyema kuhoji busara ya uamuzi wa Chama lakini athari zake sote tunaziona. Kumekuwepo na kilio na manung’uniko kuhusu maadili na mienendo ya viongozi. Tumeshuhudia viongozi wakifanya matendo ya utovu wa maadili na hata kutumia lugha zisizofanana na uongozi ulio adilifu. Hivyo, uamuzi wenu huu umekuja wakati mwafaka sana. Ni uamuzi uliokuja wakati unahitajika sana.
Mkuu wa Chuo;
Mabibi na Mabwana;
Wanazuoni wamekuwa na mjadala kwa karne nyingi kuhusu uongozi na hayajakamilika. Moja ya mambo yanayowashughulisha wanazuoni ni kama viongozi huzaliwa na vipaji vya uongozi au huandaliwa kwa mafunzo kuwa viongozi. Huu ni mjadala unaoendelea hata sasa katika fani ya sayansi ya siasa. Tafiti nyingi zimeonyesha kuwa pamoja na kuwepo ushahidi kuwa wako viongozi wenye kuzaliwa na vipawa na karama za uongozi, hata hivyo, ubora wa viongozi, hata kwa wale waliozaliwa na vipawa na karama zao hutokana na mafunzo. Inaweza kuwa mafunzo darasani au kwa kuona na kwa kutenda. Bahati mbaya hatuna vyuo vya uongozi wa jamii.
Mafunzo kwa viongozi ni muhimu kwa kuwa huwapa nyenzo na ufunguo wa kuyaelewa mazingira wanayoongozea, historia na uzoefu wa eneo wanaloliongoza, watu wanaowaongoza, matarajio yao, hulka zao, changamoto zao na muhimu sana maadili na miiko ya uongozi wenyewe. Hali kadhalika, uadilifu katika uongozi, hujumuisha desturi na tabia zinazokubalika na zinazotarajiwa na jamii na wananchi kutoka kwa kiongozi. Wananchi hawamtegemei kiongozi kuwa mla rushwa, mlevi, mhuni, mwongo au asiye na uhusiano mzuri na watu.
Maadili na miiko ya uongozi vinapaswa kuzingatiwa na viongozi wote katika jamii na taifa bila ya kujali vyama vya siasa. Kiongozi asiye na uelewa huu, hupwaya katika uongozi. Maadili na miiko ya uongozi ni tunu muhimu sana kwa kiongozi yeyote. Kiongozi anapaswa awe mtu mwenye uadilifu usiotiliwa shaka utakaomfanya aaminiwe na awe na mamlaka ya kimadili (moral authority) juu ya wale anaowaongoza.
Katika miaka hii 10, tumejishughulisha sana na masuala ya maadili katika uongozi na utendaji Serikalini. Tumefanikiwa kuimarisha mifumo ya kusimamia maadili ya viongozi kwa kutunga Sheria, Kanuni na Taasisi za kufuatilia mienendo ya viongozi. Tumeimarisha Sekretariati ya Maadili ya Viongozi wa Umma kwa kuipa uwezo wa kiuchunguzi, rasilimali watu na vitendea kazi. Tumelipa meno Baraza la Maadili na tumeliona kwa mara ya kwanza likiwaita na kuwahoji viongozi wenye tuhuma za kimaadili.
Mwaka 2009 tumetunga Sheria Mpya ya Rushwa iliyoboreshwa na kuongeza nguvu kupambana na rushwa. Orodha ya makosa ya rushwa imeongezwe kutoka manne hadi 24 na Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) imeimarishwa kwa majengo, vifaa na rasilimali watu. Hivi sasa TAKUKURU iko katika wilaya zote nchini na watuhumiwa wengi wa rushwa wamefikishwa katika mahakama na fedha nyingi zimekuwa zinaokolewa.
Vilevile, tumetunga Sheria ya Matumizi ya Fedha katika Uchaguzi ili kuhakikisha kwamba maadili ya kupata viongozi wa kuchaguliwa katika taifa letu yanazingatiwa. Tutakapokamilisha Sheria ya kutenganisha shughuli za siasa na biashara tutakuwa tumepiga hatua kubwa. Tumetunga pia Sheria mpya ambayo imeimarisha Ofisi ya Mkaguzi na Mdhibti Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG). Imesaidia kuimarisha nidhamu ya matumizi ya fedha za umma na kuwabana viongozi na watumishi wa umma wanaofanya vitendo vya wizi au ubadhilifu wa fedha na mali za umma. Yote haya tumeyafanya ili kuimarisha mifumo ya kusimamia maadili ya viongozi na watendaji wetu.
Bahati nzuri katika Katiba Inayopendekezwa, Bunge Maalumu la Katiba limesisitiza na kuweka uzito unaostahili kwa maadili ya viongozi na watendaji wa umma. Ibara 28 na 29 inazungumzia maadili ya viongozi wa umma, na ibara 30 na 31 inazungumzia maadili ya watendaji wa umma. Katiba Inayopendekezwa ikipitishwa tutakuwa tumefanikiwa sana katika kuimarisha mifumo ya usimamizi wa maadili nchini. Ombwe lililoachwa na Azimio la Zanzibar kuhusu miiko ya uongozi litakuwa limepata jawabu la uhakika.
Ni ukweli usiopingika kuwa pamoja na jitihada hizo, leo hii tunayo nakisi ya maadili miongoni mwa viongozi na watendaji wa umma. Funzo tunalolipata hapa ni kuwa kukinga ni bora kuliko kutibu. Mifumo ya udhibiti pamoja na umuhimu wake, si badala ya mifumo ya kuwaandaa viongozi kimaadili. Zamani kupitia Jeshi la Kujenga Taifa (JKT) na Chuo cha Kivukoni zilikuwa sifa muhimu za kupata uteuzi wa uongozi wa siasa. Baada ya mageuzi ya kiuchumi na kisiasa na kuingia kwa mfumo wa soko huria na vyama vingi, mambo hayo hayakupewa umuhimu. JKT ikadorora, vijana wakakosa fursa ya kujengwa uzalendo. Ukichanganya na Azimio la Zanzibar lililolegeza miiko ya uongozi ya Azimio la Arusha, kumekuwa na mmong’onyoko mkubwa wa maadili miongoni mwa viongozi. Kufa kwa Chuo cha Kivukoni kumeshusha ubora wa uongozi.
Baada ya kurejesha JKT, hakika, taifa linahitaji sana programu ya aina hii tunayozindua leo ili kutuandalia viongozi wazuri, wenye mtazamo wa kitaifa na maadili mema. Nasema hivyo kwa kuwa sote ni mashuhuda wa matatizo ya maadili ya uongozi nchini.
Hatuna budi kuwaandaa viongozi wetu hasa vijana kwa mafunzo maalumu ili waje kuwa viongozi bora. Ni jambo ambalo tulikuwa tukilifanya siku za nyuma. Uzoefu unaonyesha hata katika nchi zilizoendelea wanafanya hivi. Viko vyuo maalum vinavyoandaa na kutoa viongozi wa kada mbalimbali. Katika nchi za wenzetu kuna ngazi fulani za uongozi huwezi kushika ikiwa hujafundwa katika taasisi maalumu. Kwa kuzingatia ukweli huo, ndiyo maana tumeanzisha Chuo cha Uongozi kiitwacho Uongozi Institute. Chuo hiki kinalenga kutoa mafunzo ya uongozi kwa viongozi wa Serikali. Wamekuwa wakitoa mafunzo kwa Wakuu wa Wilaya, Wakuu wa Mikoa na viongozi wengine wa ngazi mbalimbali.
Nimefurahishwa na taarifa yako kuwa kutakuwa na Kada za aina tatu katika mafunzo ya program hii yaani ngazi ya juu yenye viongozi na watendaji wa kitaifa na mkoa;ngazi ya kati itakayohusisha viongozi wa ngazi ya wilaya; na ngazi ya chini yenye viongozi wa ngazi za kijiji. Aidha, umesema yatakuwa ni mafunzo ya muda mfupi. Nakubaliana nanyi kwani si vyema kuziacha nafasi hizi wazi kwa muda mrefu. Vile vile, ni muhimu sana mafunzo haya yakaegemea pia katika vitendo na uzoefu badala ya nadharia pekee. Hii inajumuisha kuwa na wakufunzi mchanganyiko kutoka katika taaluma na wale kutoka katika uongozi na utendaji wa fani mbalimbali.
Uamuzi wenu wa kuanzisha Kibweta cha Mwalimu Nyerere kwa madhumuni ya kusimamia program ya mafunzo haya ni mzuri. Nimefurahishwa pia na uteuzi wenu wa Mheshimiwa Pius Msekwa kuwa Mwenyekiti wa Kibweta hiki. Chaguo hili ni muafaka kwani amesheheni historia, uzoefu na hazina kubwa ya uongozi. Ni imani yangu kuwa chini ya uongozi wake programu hii itafanikiwa. Sisi katika Serikali tunaahidi kuwapa kila aina ya ushirikiano mtakaohitaji. Tuleteeni mapendekezo yenu kuhusu program hii ili ifanyiwe kazi na tuanze kuleta viongozi kwa ajili ya mafunzo hayo.
Changamoto za Chuo
Mkuu wa Chuo;
Kama ulivyoeleza, kukua na kupanuka kwa Chuo hiki kumekuja na changamoto zake. Idadi ya wanafunzi inaongezeka wakati majengo ya hosteli ni finyu. Umezungumzia ujenzi wa hosteli kusimama kutokana na uhaba wa fedha. Nitawasaidia kusema. Kuhusu kupewa majengo ya TAFICO ili myabadili matumizi na kuyatumia kwa kufundishia itabidi kushauriana na wenye majengo kujua mipango yao na mahali hapo. Kama itawezekana tutawapeni taarifa. Kuhusu tatizo la mmomonyoko wa fukwe unaotokana na kuongezeka kwa bahari tutawasiliana na mamlaka husika utafiti ufanywe na ushauri wa kitaalamu utolewe.
Nikuhakikishie kuwa nimepokea changamoto zenu na ni changamoto za msingi na tutatazama moja baada ya nyingine tuone namna ya kujenga Chuo hiki kulingana na mahitaji yake ya sasa na ya siku za usoni.
Hitimisho
Mabibi na Mabwana;
Niwashukuru sana kwa kunialika katika maadhimisho ya kumbukumbu ya kuzaliwa Mwalimu Nyerere na ufunguzi wa Programu Maalum ya Uongozi na Maadili. Nimefurahi sana kujumuika na nanyi wote katika eneo hili ambalo linanikumbusha nilipokuwa nikihudhuria mafunzo katika chuo hiki. Sasa ninayo furaha kutangaza kuwa Programu Maalum ya Mafunzo ya Uongozi na Maadili imefunguliwa rasmi.
Asanteni sana kwa kunisikiliza.

- Apr 12, 2015
HOTUBA YA RAIS WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA, MHESHIMIWA JAKAYA MRISHO KIKWETE KWENYE SIKUKUU YA KUWEKWA WAKFU NA KUSIMIKWA MHASHAMU ASKOFU LIBERATUS SANGU...
Soma zaidiHotuba
Mwadhama Polycarp Kardinali Pengo;
Mhashamu Askofu Mkuu, Tarsisius Ngalalekumtwa, Rais wa Baraza la Maaskofu Tanzania;
Mheshimiwa Balozi wa Vatican, Mhashamu Askofu Mkuu Protase Rugambwa;
Mhashamu Askofu Liberatus Sangu, Askofu Mpya wa Jimbo Katoliki Shinyanga;
Wahashamu Maaskofu Wakuu na Maaskofu;
Waheshimiwa Mawaziri na Naibu Mawaziri;
Mheshimiwa Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga;
Viongozi wa Dini na Serikali Mliohudhuria;
Ndugu Waumini,Wageni Waalikwa;
Mabibi na Mabwana:
Tumsifu Yesu Kristo!
Shukrani na Pongezi
Napenda kuungana na nyote mlionitangulia kumshukuru Mwenyezi Mungu kwa rehema na baraka zake zilizotuwezesha kushiriki pamoja katika tukio hili muhimu na adhimu kwa Jimbo Katoliki Shinyanga kupata Askofu wake wa nne. Nawashukuru Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania na Jimbo Katoliki Shinyanga kwa heshima kubwa mliyonipa ya kunialika katika sherehe ya kuwekwa wakfu na kusimikwa Mhashamu Baba Askofu Liberatus Sangu kuwa Askofu wa Jimbo Katoliki Shinyanga. Hii ni heshima kubwa kwangu na kwa Serikali yetu na ni kielelezo hai cha uhusiano mzuri uliopo kati ya Kanisa Katoliki na Serikali.
Mhashamu Baba Askofu Liberatus Sangu;
Nakupongeza kwa kuteuliwa kwako na kwa leo hii kukabidhiwa rasmi dhamana ya kuwa Kiongozi Mkuu wa Jimbo Katoliki la Shinyanga. Uteuzi wako kushika wadhifa huu ni uthibitisho wa imani kubwa aliyonayo Baba Mtakatifu Francis kwako. Imani hiyo ndiyo pia waliyonayo wajumbe wa Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania, makasisi, watawa na walei wa Jimbo la Shinyanga. Sote, tumeusubiri uteuzi huu kwa hamu tangu tulipopata pigo la kuondokewa na mpendwa wetu Baba Askofu Aloysius Balina mwaka 2012.
Nakuomba utambue kuwa imani hiyo imebeba matumaini makubwa kwamba utaitenda kazi yako kwa moyo wa dhati, uadilifu na uaminifu mkubwa. Kwa kawaida matumaini ya waamini kwa kiongozi wao wa kiroho huwa makubwa na wakati mwingine huwafanya wakasahau kuwa kiongozi wa dini pia ni binadamu. Lakini wanafanya hivyo kwa nia njema na kwa sababu nzuri kwamba hakuna mwingine ila wewe. Mimi naamini kwamba kwa malezi mazuri uliyopatiwa na Kanisa lako ukichanganya na uzoevu wako wa muda mrefu wa kazi za kichungaji, uwanazuoni wako na kwa rehema za Mwenyezi Mungu utayamudu vyema majukumu yako ya kuwaongoza kondoo wa Bwana kwenye malisho mazuri ya kiroho na kimwili.
Maadili Mema
Mhashamu Baba Askofu Liberatus Sangu;
Waheshimiwa Maaskofu;
Ndugu Waumini na Wageni Waalikwa;
Malisho ya kiroho huwafanya waumini wawe wacha Mungu. Na, mcha Mungu kwa kawaida humpenda Mungu na jirani yake, huzingatia maadili mema, huwa na tabia njema na mara nyingi huwa raia mwema. Kwa ajili hiyo, viongozi wa dini kama walivyo wa Serikali wanao wajibu maalum wa kulilea taifa. Ninyi mnalea kiroho, kwa maana ya kuwafanya waumini kufuata taratibu za kiimani na sisi tunalea kidunia kwa maana ya raia kufuata taratibu za kikatiba na kisheria na maadili mema kwa mujibu wa mila na desturi za jamii na nchi yetu.
Ninyi viongozi wa dini huwalea waumini kiimani waweze kutende mema hapa duniani ili waje kupata malipo mazuri wanaporejea kwa Muumba wao. Hili la kulea kiimani likifanikiwa basi kwa kiasi kikubwa kazi ya Serikali inakuwa rahisi. Hapatakuwa na watu wanaoiba, wanaoua wenzao, wanaokata albino viungo vyao, wanaotukana wenzao, matapeli, wanaofumaniwa na kadhalika. Hivyo basi, Serikali ingepunguziwa kasi ya ikuwakamata, kuwafikisha mahakamani na kuwafunga magerezani watu wengi kama tufanyavyo sasa. Hivyo basi, mchango wenu katika kujenga maadili mema kwa jamii na watu wake ni kitu kilicho bayana. Aidha, pale tunapokuwa na jamii iliyojaa maovu, umuhimu na ukubwa wa kazi yenu unaonekana bayana. Napenda kutoa ombi maalumu kwako Baba Askofu Sangu pamoja na Maaskofu, Mapadre katika mikoa ya kanda hii kuongeza bidii katika kuelimisha jamii kuacha mauaji ya vikongwe na watu wenye ualbino. Tushirikiane na Serikali kupamba na ushirikina kitu ambacho ndicho chanzo cha mauaji haya na kukatwa viungo albino. Ninyi mnasikilizwa sana, itumieni nafasi hiyo tuondokane na aibu hii.
Mchango wa Kanisa Katika Maendeleo ya Taifa
Waheshimiwa Maaskofu;
Uhusiano kati ya Serikali na madhehebu ya dini likiwemo Kanisa Katoliki ni wa muda mrefu na ni wa kihistoria. Serikali imekuwa ikiunga mkono shughuli za Kanisa katika kutoa huduma za jamii za elimu, afya na nyinginezo zenye kuwaletea maendeleo wananchi. Mmetoa mchango mkubwa sana ambao umewanufaisha Watanzania wengi wa dini na madhehebu mbalimbali. Huduma hizi zimesaidia sana kuongeza kasi ya kuwatoa wananchi kwenye umaskini na kujiletea maendeleo. Tunawapongeza na kuwashukuru sana kwa mchango wenu mkubwa.
Haistaajabishi kuwa matumaini ya waamini wa Kanisa Katoliki, Jimbo la Shinyanga na wananchi wa Shinyanga kwa ujumla juu yako Baba Askofu Sangu siyo ya kiroho pekee. Wanatarajia kuwa chini ya uongozi wako, Kanisa Katoliki litaendelea kutoa huduma za jamii kwao. Wana matumaini hayo kwa sababu wanatambua na kuthamini manufaa makubwa wanayopata katika harakati zao za kujiletea maendeleo kutokana na kazi njema inayofanywa na Kanisa. Wanategemea utaendeleza kazi nzuri zilizofanywa na waliokutangulia na utabuni na kutekeleza miradi mingine mipya ya maendeleo katika Jimbo lako. Nami naungana nao na, sina mashaka juu ya usahihi wa imani yao hiyo kwako.
Ahadi ya Serikali
Mheshimiwa Baba Askofu;
Napenda kukuhakikishia ushirikiano wangu binafsi na ule wa Serikali ninayo iongoza katika kutekeleza majukumu yako ya kiroho na ya huduma za kiuchumi na kijamii kwa maendeleo ya wananchi wa Shinyanga. Pale utakapo ona mchango wa Serikali unahitajika, usisite kuwasiliana nasi. Na iwapo utaona kuna upungufu wo wote sema kwa viongozi wa Wilaya, Mkoa na wa kitaifa: Waziri Mkuu, Makamu wa Rais na hata kwangu. Sisi ni wasikivu. Tuite tutakuitika. Ukituambia tutakujibu kwa lile linalohitaji majibu na tutatenda kwa lile la kufanya, bora tu liwe kwenye uwezo wetu na ni wajibu wetu kufanya.
Wahashamu Maaskofu;
Sisi katika Serikali tunayo kila sababu ya kuendeleza uhusiano mzuri kati yetu na madhehebu ya dini maana kazi muifanyayo haina badala yake. Tunaamini kwa dhati kuwa, kwa pamoja tunaweza kujenga, kuimarisha na kuendeleza amani, umoja na mshikamano uliopo katika taifa letu. Hali kadhalika, tukishirikiana tutaongeza kasi ya kuwawezesha Watanzania kupata maendeleo.
Tutaendelea kutimiza wajibu wetu wa kutengeneza mazingira mazuri kwa madhehebu ya dini kutekeleza majukumu yake. Kuna mambo mawili: Jambo la kwanza ni kuhakikisha kuwa uhuru wa kuabudu unakuwapo nchini, unaheshimiwa na unatekelezwa kwa vitendo. Hii ni haki inayotambulika na Katiba yetu ya sasa na utekelezaji wake hauna kasoro. Bahati nzuri imesisitizwa na kufafanuliwa vizuri zaidi katika Katiba Inayopendekezwa.
Pili, tutaendelea kushirikiana na kusaidiana kwa upande wa shughuli zenu za huduma za kiuchumi na kijamii mzifanyazo. Tumekuwa tunatoa misamaha ya kodi kwa shughuli za madhehebu ya dini na hata kuchangia fedha za Serikali na watumishi kwa baadhi ya shughuli zenu hasa za afya na mikopo ya wanafunzi katika vyuo vikuu. Tutaendelea kufanya hivyo kwa kutambua mchango muhimu unaotolewa na huduma hizo kwa maendeleo ya nchi yetu na ustawi wa watu wake. Maombi yangu au yetu kwenu ni kuwa msiwaruhusu watu waovu wakaitumia vibaya fursa hii muhimu. Tunapopata taarifa za fursa hiyo kutumika kinyume hutusumbua sana.
Tuendako
Mwadhama Kardinali;
Waheshimiwa Maaskofu;
Wageni Waalikwa;
Wakati wote sisi viongozi wa Serikali na dini tunao wajibu wa kipekee katika uhai wa taifa letu na watu wake. Tunalo jukumu maalum la ulezi, yaani kuhakikisha watu katika nchi yetu wanaishi kwa amani, umoja, upendo na mshikamano licha ya tofauti zetu za rangi, kabila, dini, jinsia, maeneo tutokako, au ufuasi wa vyama vya siasa. Naomba tukumbuke kuwa tofauti hizi ambazo hatuna budi kuishi nazo, tusiziache zikawa nyufa za uhasama ambao siyo tu zitaligawa taifa bali zinaweza kulimong’onyoa na kulisambaratisha.
Sisi viongozi tuna wajibu wa kihistoria wa kutambua kuwa ni jukumu letu kuhakikisha kuwa hilo haliwi. Nayasema haya kwa sababu. Kwa jumla tunapita katika kipindi kisichokuwa cha kawaida, ambacho kama hatutafanikiwa kubadili mwelekeo huu kunaweza kuwepo madhara makubwa. Nawaahidi ushirikiano wangu binafsi na wa Serikali ninayoiongoza. Naomba viongozi wa dini msaidie ufa usiwe mpana zaidi. Tumieni Kamati za dini kwa mwaka kama huu wa uchaguzi ambapo baadhi ya wanasiasa na washabiki wao katika tamaa yao ya kupata madaraka hupenda kuzitumia tofauti hizi kwa maslahi yao binafsi na vyama vyao, tunaomba muwe makini zaidi. Wakati mwingine wanasiasa hufanya makusudi kuchochea uhasama kwa kutumia tofauti zetu za asili ili wapate manufaa ya kisiasa. Wao hawajali inayoweza kutokea na madhara makubwa kwa nchi yetu.
Kwa ajili hiyo, niwaombe viongozi wa dini tutumie vizuri nafasi ya uongozi mliyojaaliwa na Mwenyezi Mungu kuzuia wanasiasa wasilifikishe taifa pabaya. Watakeni waumini wenu wasiwasikilize na kufanya mambo yote yanayofarakanisha jamii bali washikilie yale yanayowaunganisha na kuleta utangamano. Na lililo muhimu kuliko yote ninalowaomba msiwape wanasiasa fursa kuingiza dini kwenye siasa au siasa kwenye dini. Tuambieni bila kigugumizi. Wasiziache dini ziwe huru kwa watu wa vyama vyote. Makanisa na Misikiti ibaki kuwa nyumba za ibada na siyo majukwaa ya siasa. Iwe mahali pa kuwaunganisha wote na viongozi wa dini wawe kimbilio lao wakati wanapogombana.
Msikubali ufuasi wa vyama vya siasa ukawafarakanisha viongozi wa dini mpaka mkapoteza dira na nafasi yenu muhimu ya uongozi wa waamini wenu. Kuchanganya dini na siasa ni hatari sana kwa usalama, amani na utulivu wa jamii na hata dini zenyewe. Si vyema wakati wa Chama cha siasa kushindwa kukawa ni kushindwa dini fulani na waumini wake au Chama na kushinda ni kwa dini nyingine na waumini wao. Wafuasi wa vyama vya siasa kugombana si jambo la ajabu. Je itakuwaje kama dini zimehusishwa na kugawanyika kidini. Ugomvi huo unakuwa na sura ya ugomvi baina ya wafuasi wa dini tofauti kwa mwamvuli wa siasa? Kuna hatari ya kuzuka vita vya kidini na nchi ikawaka moto. Kunaweza kutokea maafa yasiyotabirika sura yake na mwisho wake. Naomba viongozi wa dini mtambue wajibu wenu wa kuponya. Tuwaache waumini wawe wafuasi wa vyama vya siasa wavipendavyo. Kwa uchaguzi muwahimize waumini wenu wachague kwa busara kadri watakavyoridhishwa na sera, ilani na ahadi za vyama vya siasa na wagombea wao. Wasisitizeni kujali ubora, moyo wa uzalendo na uadilifu wa wagombea. Tukifanya hivyo tutavuka salama. Kinyume chake inaweza kuzua tatizo.
Hitimisho
Mheshimiwa Baba Askofu;
Leo ni siku ya furaha kwetu sote. Ni siku pia ya kumsifu Mwenyezi Mungu kwa neema zake na kumshukuru kwa uteuzi wako. Waumini waliofurika hapa wamekuja kwa ajili ya sherehe za kuwekwa wakfu na siyo Mkutano wa Rais. Niruhusu niishie hapa nitoe nafasi kwa kuabudu na kumtukuza Mungu wetu. Nitatafuta wasaa mwingine mwafaka wa kuzungumza na wananchi wa Shinyanga na Watanzania kwa jumla kuhusu mambo ya maendeleo.
Nikushukuru tena kwa kunialika na kwa kunipa heshima hii ya kuzungumza na viongozi wa Kanisa, waumini na wananchi. Mwenyezi Mungu na akubariki Baba Askofu na akufanyie wepesi katika majukumu yako.
Asanteni kwa kunisikiliza.

- Apr 09, 2015
WELCOMING REMARKS BY H.E. JAKAYA MRISHO KIKWETE, PRESIDENT OF THE UNITED REPUBLIC OF TANZANIA DURING SUN LEAD GROUPS VISIONING SUB GROUP MEETING ON 9TH APRIL,...
Soma zaidiHotuba
Hon. Seif Rashid, Minister for Health and Social Welfare;
Dr. Tom Arnold, Chairperson of the Sub Group Meeting and Coordinator of SUN Movement;
Members of Diplomatic Corps and Development Partners;
Invited Guests;
Ladies and Gentlemen;
I am pleased to welcome you all to Tanzania and to this SUN Lead Group’s Visioning Sub Group meeting. Tanzania is pleased to co-host this important meeting that will come up with detailed recommendations to be presented to the Lead Group for movement-wide response on the Independent Comprehensive Evaluation (ICE). This will go a long way to contribute towards having a time bound and structured process. Ultimately, the Movement wide response will help the Lead Group to prepare a report to the UN Secretary General as the contribution of the SUN Movement to improving the nutrition situation in the world.
Tanzania is proud to be among the first members of the SUN Movement which has grown to 54 countries, from the 13 countries which joined in 2014. Together we have made a difference and transformed the nutrition agenda from being a narrow health issue to a broader sustainable development matter. We have raised awareness, understanding and making the issue of nutrition a global development agenda. The growth in the number of membership of the SUN Movement is a testimony that our message has been loud enough and has reached receptive ears.
Tanzania Experience in Scaling Up Nutrition
Ladies and Gentlemen,
Our experience in scaling up nutrition convinces us that it is within our hands and means to halve global malnutrition and eventually reverse it. In my view, it requires political will, financing and coordination of response. We must invest wisely and be smarter in scaling up nutrition particularly to mothers and children. We in Tanzania, have taken bold steps to scale up investment in nutrition through our 5 Years National Nutrition Strategy (2011/12-2015/2016). These steps include:
a) Putting in place Nutrition Focal Officers in 157 out of 169 District Councils and employ Nutrition Focal Officers in 25 regions;
b) Increased food fortification plants from 6 in 2013 to 10 for wheat flour and from 3 to 10 for edible oil;
c) Increased fortification of maize flour at small and medium scale flour mills and home fortification for children aged 6-24 months from 3 to 6 regions;
d) Nearly doubled expenditure on nutrition at Council level from 18 Billion Tanzania Shillings to 33 Billion Tanzania shillings between 2010/2011 and 2012/2013;
e) Initiated a process to formulate new National Food and Nutrition Policy which will incorporate recommended structures by SUN Movement; and
f) Endorsed agricultural transformation, food fortification and consumer behavior change as 3 priorities for engaging private sector.
Achievements
Ladies and Gentlemen,
These efforts and investments have yielded encouraging results. About 20 million people have now been reached with fortified food products as a result of various interventions undertaken. The 2014 National Nutrition Survey findings shows that prevalence of stunting has decreased from 42 percent in 2010 to 34.7 percent in 2014, representing a reduction of 8 percent since 2010. Furthermore, prevalence of global acute malnutrition has been maintained below 5 percent with underweight prevalence reaching 13.4 percent in 2014 which is close to target 8 of the MDG Goal 1 of 12.5 percent in 2015. It is also important to note that, between 2010 and 2014 there has been an increase in Vitamin A supplementation for children from 6 to 59 months from 61 percent to 72 percent. With regard to deworming, coverage for children 12-59 months has increased from 50 percent to 71 percent.
This is very much a function of increased allocation of human and financial resources and improved coordination since 2011. Our experience makes me say with confidence, that big results are possible provided that the right things are done. Lot of what we have been able to achieve with only 20 percent of the planned 825 billion Tanzania shillings required for the implementation of our National Nutrition strategy. It is evident that with more resources, we can achieve far better.
Challenges
Ladies and Gentlemen;
There is still a long way to go for Tanzania to reach the MDGs objectives of the 2020 World Health Assembly targets and those of the Tanzania Development Vision 2025 with regard to nutrition. It is estimated that there are still more than 2. 7 million children under five years of age who are stunted. About 58 percent of these live in the 10 regions with inadequate key nutrition interventions.
Studies also indicate that taking 2025 as target year, the number of children who will die of stunting would be 580,687 if the status quo is maintained. This will translate into 20,376 million USD of loss of economic productivity. If averted about 120,633 children will be saved and the economic gain is estimated to be 4,759 million USD. Certainly, this is a worthy investment that Tanzania needs to make. Of course, given our limited financial resources, international collaboration and partnership with private sector will be required to achieve these targets much earlier.
Way Forward
Ladies and Gentlemen,
As we reflect and negotiate on the Post 2015 Sustainable Development Goals, we must take into account that the world still lags far behind as far as nutrition is concerned. It is important that the SUN Movement plays a part in the ongoing dialogue and negotiations of the Sustainable Development Goals (SDGs). Our experience in the SUN Movement has so far taught us that malnutrition should be approached from a standpoint of global emergency that requires global action. I am glad that this meeting will deliberate on these issues in line with the Independent Comprehensive Evaluation report and make recommendations to the Sun Movement Lead Group. In my opinion, the following could be given thorough thoughts in your deliberations:
a) The need to have in place a financing mechanism for scaling up nutrition at the Global Level in the Post 2015 Sustainable Development Goals Framework;
b) The need to have institutionalized global structures for coordination, monitoring and implementation of scaling up nutrition beyond the life of the SUN Movement to ensure sustainability of the momentum generated so far; and
c) How best to leverage Private Sector involvement and contribution in realizing the scaling up nutrition agenda given that, the benefits of investing in nutrition have far reaching impact across all sectors including the private sector.
Ladies and Gentlemen;
Let me concluded by once again thanking you for coming to Dar es Salaam. It is an honour we will always cherish. I hope you will find time at the end of this meeting to see a bit of Tanzania. I am sure you will be appetized enough to come back for a longer visit. With these many words it is now my singular honour and pleasure to wish you very successful deliberations. Good luck.

- Apr 03, 2015
AN ADDRESS BY HIS EXCELLENCY DR. JAKAYA MRISHO KIKWETE, PRESIDENT OF THE UNITED REPUBLIC OF TANZANIA AT WOODROW WILSON INTERNATIONAL CENTRE, WASHINGTON DC. USA,...
Soma zaidiHotuba
Honourable Mr. Thomas Nides, Chairman of Woodrow Wilson Centre;
Honourable Jane Harman, President and CEO of Woodrow Wilsin Centre;
Mr. Monde Muyagwa, Director, Africa Program of the Woodrow Wilson Centre;
Invited Guests;
Ladies and Gentlemen;
I thank you President Jane Harman for the invitation to speak at this prestigious and world renowned Woodrow Wilson Centre. I feel greatly honoured and privileged to have this Conversation with the distinguished audience. I will always cherish this rare opportunity. In her invitation you asked me to share my personal experience of leadership challenges as a President of the United Republic of Tanzania. Also to share my thoughts about US-Africa relations. This invitation could not have come at any better time than this. I am going to leave office after the elections in October, 2015 on completion of my mandatory two terms as President of my great country.
I must admit that I had a hard time deciding where to start and where to end especially about what and how much to say because there is too much to talk about. As such, I apologise to those who may feel I did not talk about what they would have wished me to say. Please blame that it on limited time.
Ladies and Gentlemen;
After being nominated Presidential candidate of my Party (Chama cha Mapinduzi – CCM) in May 2005 I set down to contemplate in greater depth the task ahead of me. I always reflected on the same during the campaign and after being elected President. During my maiden speech on 30th December, 2025 while opening the National Assembly, I crystallised my thoughts. I underlined six major policy tenets which will guide and define my Presidency. These were:
- Holding the country together.
- Maintain peace and political stability which is the hallmark of Tanzania.
- Promote fast socio-economic growth and development as a measure to fight poverty and accelerate development.
- Consolidate democracy and ensure good governance, rule of law and human rights.
- Undertake unrelenting fight against crime including corruption; and
- Develop good relations with all countries in the region, Africa and the world.
It is important to underscore the fact that elections are taking place in a specific context and historical timelines. Together they dictate expectations, aspirations and preferences of the voters and politics of the day. These, however, are not static, they may keep on changing every time you come close to achieving them. It gives a lesson that, leadership is all about solving puzzles, with each solution breeding another challenge or contributing to solving the other challenge.
Tanzania of 2005
Ladies and Gentlemen;
I took the country from my predecessor, President Benjamin William Mkapa, who I served under his Cabinet for 10 years as his Foreign Minister. In 2005, the country was emerging from the difficult times of Structural Adjustment Programmes (SAP) and liberalization related reforms that were so painful to our economy and people. The focus on debt repayment had a negative impact on the government’s ability to provide basic social services such as health, education and water. Less than 10 percent of primary school leavers found their way in to secondary education. The country GDP was at 14.14 billion US Dollars and per capita income was at US Dollars 375.
On the political front, with just 13 years of multiparty experience, many of our democratic and accountability institutions were at the formative stage. Opposition parties occupied less than 15 percent of the seats in the Parliament. There was a political standoff in Zanzibar after election that was threatening security and political stability in the Isles and in the entire country. That very same year Tanzania experienced unprecedented drought causing acute food shortages necessitating more than 3.776 million people to be given food support by our new government. At the same time dams at hydropower stations did not have enough water causing serious load shedding. It forced us to source power from emergence power producer which lauded our government into trouble.
Keeping the Nation Together
Ladies and Gentlemen;
Tanzania is a nation of great diversity making the task of holding the country together to top priority agenda. The people of Tanzania belong to over 120 tribes and different races although people of African descent are the overwhelming majority. They subscribe to different religions and there are many who don’t belong to any. May be they have chosen to be non-aligned or are still choosing. After the reintroduction of multiparty system in 1992, the people of Tanzania joined the various political parties. There were already signs of differences in political affiliations that could threaten the peace and stability of the nation. The United Republic of Tanzania is a new nation born on April 26, 1964 through merger of the People’s Republic of Zanzibar and the Republic of Tanganyika. Managing and balancing the differences between these two partners needed special attention. As I alluded you earlier, in Zanzibar there was a dangerous standoff between the ruling party CCM and the main opposition CUF. Because CCM was strong in Unguja Island and CUF in Pemba Island the standoff was threatening to drive a wedge between the two Islands which together formed the People’s Republic of Zanzibar.
Ensuring that the people of Tanzania celebrate their diversities but they do not split the country into hostile camps and entities is a mammoth task. Temptations of demagogue politicians to exploit social fault lines, as the means to consolidate and ascend to power is much higher. We are already seeing it happening therefore a great deal of political management is required. Fortunately, the founding fathers of Tanzania Mwalimu Julius Nyerere, the first President of Tanganyika and Tanzania and Sheikh Abeid Amani Karume the President of Zanzibar and First Vice President of Tanzania had laid strong foundation to ensure that these diversities don’t break up the country. My two predecessors His Excellency Ally Hassan Mwinyi and His Excellency Benjamin Mkapa and the successive generations of Presidents of Zanzibar have maintained the good policies. I also vowed to follow the good examples of my predecessors. So far so good.
I am proud that I have been able to continue to hold the country together despite challenges and threats. We have dealt with threats whenever they arose. I supported and contributed to political process that saw the two contending parties in Zanzibar sign a political accord in 2010. The Political Accord that contributed to peaceful elections in Zanzibar and the formation of government of National Unity between my ruling party CCM and the opposition party CUF. I have never shied away from reaching out political and to religious leaders whenever there was a need and worked with them in confronting many of the divisive tendencies. With regard to the differences, I launched the Constitutional review process to address the issues. I equally never hesitated to take resolute action against all those who use the diversity to incite chaos, civic disobedience, break laws and disrupt peace. So far so good. The country is at peace.
Economic Growth and Development
Ladies and Gentlemen;
I was elected in 2005 and 2010 on the pledge that I will deliver on the promise made by my Party in our election manifesto of “better life for every Tanzanian”. It was a pledge to change the lives of the people of Tanzania for the better. From where they were to somewhere better. This means two things. One to see people’s incomes increased, and, two to see the people of Tanzania having access to better social and economic services. Here I have in mind things like education, health care, water supply, electricity, roads, railway, aviation etc. In pursuit of these lofty goals we decided to stay the course on economic reforms started by our Second President and continued by the third President. These reforms have not been so easy since by their very nature they bite on the comfort of some sections of our people and displace others from their economic position.
It is heart-warming, indeed, that sustaining the reforms has worked well for us. Our economy has continued to register strong macro-economic performance. GDP growth has been at an average of 7 percent for the one and a half decade. Tanzania is among the 10 fastest growing economy in Africa and among 20 in the world. Our GDP now stand at 43 billion US Dollars compared to 14.4 US Dollars in 2005 and per capita GDP has increased from 375 US Dollars in 2005 to 944 US Dollars in 2014. We have succeeded to tame inflation rate from 18 percent in 2011 to 4.8 percent currently. Revenue collection has increased from Tanzania shillings 177.1 billion (96 million US Dollars) per month in 2005 to Tanzania shillings 800 billion (about 433 million US Dollars) per month in 2015. This is too little compared to demand to meet government obligations. We have accelerated the pace of poverty reduction in the last six years. Between 2000 and 2007 poverty reduction was only 2 percent and between 2007 and 2014 poverty reduction was 5.5 percent. However, the future looks even brighter for the economy and the government when the effects of the already discovered 55 tcf of natural gas begin to be felt. Certainly, government revenue position will be bolstered significantly.
Improving Social and Economic Services
Ladies and Gentlemen;
We have succeeded to scale up the provision of basic social and economic services hence increasing, Tanzania’s who have access to these important services. This contributes in a big way to the improvement of people’s lives. Allow me to give specific examples. In education for example, primary school enrolment is 98 percent and secondary school enrolment increased three and a half times from 525, 325 students in 2005 to 1.8 million students in 2014 and university enrolment increased from 40,719 in 2005 to 200,986 students in 2014. By doing so, more Tanzanian sons and daughters have access to education now than any other time. The other thing worth mentioning is that, there are more girls than boys in primary schools. There is gender parity in secondary school but in higher education there are more men than women although the number of women is increasing fast.
The number of people with access to electricity has also increased from 10 percent in 2005 to 36 percent 2014. About 5,336 villages in rural areas have access to electricity which 43 percent of the total 12,423 villages in the country. The number of people with access to clean and safe portable water have increased from 74 percent in urban areas and 53.7 percent in rural areas in 2005 to the current 86 percent and 60 percent respectively. With regard to health care, we have built more dispensaries, health centres and hospitals as a result more Tanzanians have access to better health services. This translated into reduction in under five mortality rate from 112 deaths per 1,000 in 2004/2005 to 54 deaths per 1,000 live births. Maternal mortality rate from 578 deaths per 100,000 births in 2005 to 432 deaths per 100,000 births. Malaria infections and deaths have been cut by 50 percent and HIV infection rates is down to 5.1 percent and coming further down. Immunization coverage for children and mothers is way above 90 percent. Availability of medicines has improved considerably although there are still teething challenges to overcome. Expansion in training is helping to increase the number of health professionals thus slowly but surely closing the gap.
Big Result Now (BRN)
We have recorded tremendous success on the road infrastructure. Close to 6,000km have been paved out of the 11,474 km under construction. We have set our sights on upgrading the railway network.
Consolidating Governance and Growth
Ladies and Gentlemen;
Improving governance has been a top priority agenda of my administration. We have been taking measures to promote transparency and accountability. There has been deliberate measures to build and strengthen institutions of democracy, governance, accountability and rule of law. The judiciary is independent of government interference. The Parliament is very vibrant and performs so well its oversight of government. The office of the Controller and Auditor General has been strengthened as a result financial discipline is improving. Audit reports are made public. They are debated by Parliament where proceedings are broadcast live on TV.
The fight against corruption is unrelenting. There is no undue protection of people suspected being found guilty of engaging in corrupt practices. The anti corruption law has been strengthened and the institutions responsible for Preventing and Combating Corruption (PCCB) has been strengthened. I have fulfilled my pledge of widening democratic space, and significantly improving the political environment, on which Opposition parties could grow. Further efforts have been directed in strengthening freedom of press. There are 825 newspapers, 95 radios station of which government owned are only two and 28 TV Stations. In Tanzania we have so many newspapers that one requires about 20 US Dollars to be able to buy all daily newspapers.
US-Tanzania Relations
Ladies and Gentlemen;
The relationship between the United States of America and the United Republic of Tanzania is excellent. And to say it more appropriately, they are at their best state ever. Government to government relations are strong as evidenced by two US Presidents undertaking visits to Tanzania within a span of five years. President George W. Bush visited with us in 2008 while President Barack Obama came in 2013. President Bill Clinton made an official visit in 2000 but has been to Tanzania several times after living office to follow up projects supported by his Foundation. President Bush has been there twice since leaving office. Several senior officials of our two governments have exchanged visits which have helped to strengthen our bilateral relations.
Tanzania and the United States see eye to eye on a number of global and African issues and have supported each other at international and regional fora. The US has extended a big hand of support to Tanzania’s development endeavours which has made a huge difference towards improving the lives of our people and the development of the country at large. I have in mind the good work being done by the USAID covering many aspects of the socio-economic life of the people of Tanzania. Also, programmes like PEPFER, PMI, MCC, Feed the Future and Power Africa are making phenomenon contributions to the development of Tanzania and its people.
People to people relations are also strong and getting stronger with each passing day. I believe visits like mine serves that purpose. Many private foundations, non – government organisations and individual Americans are working in Tanzania and have good relations with the people and the government of Tanzania.
Way Forward
Ladies and Gentlemen;
When I look back to 2005, when I assumed the highest office in our country, I hold no regrets, only harbour lessons. I believe my successor will carry on and learn from these lessons, so that he or she can continue from where we will have left off. One thing I am proud of is that, we have built strong foundations to guide our country in the implementation of the Tanzania Development Vision 2025 whose overarching objective is to transform the country into a middle income economy by 2025. I have in mind the Long Term Prospective Plan divided into three Five Year Development Plans. Also, I hope we will be able to have in place the policy and legislation on the management of gas economy and revenues, which are expected to flow in earnest from 2020. Ultimately, I hope we will hold free, fair, peaceful and credible elections so that I can handover the Presidency to my successor in a tranquil atmosphere. I cannot wait to see that day.
I thank you for your kind attention.

- Apr 02, 2015
SPEECH BY HIS EXCELLENCY JAKAYA MRISHO KIKWETE, PRESIDENT OF THE UNITED REPUBLIC OF TANZANIA AT THE WORLD AFFAIRS COUNCIL ON 2ND APRIL, 2015
Soma zaidiHotuba
Jacqueline Miller, President for World Affairs Council;
Excellencies;
Distinguished guests;
Ladies and Gentlemen;
I thank you Madam President for the invitation to come to your beautiful city of Seattle and for the very warm reception and gracious hospitality. I also thank you for affording me the opportunity to speak to this distinguished audience. At long last I could make it after failing to do so last year.
I have come to Seattle to know this important city, see old friends and make new ones, learn from your vast experience and successes. But, more importantly I am here to develop relation and partnership between the people of Seattle and Washington State with the people of Tanzania. Also, forge links of cooperation and partnership between Seattle’s business community and the Tanzania counterparts and Tanzania in general.
Let me begin saying that the relationship between the United States of America and the United Republic of Tanzania is excellent. And to say it more appropriately, they are at their best state ever. Government to government relations are strong as evidenced by two US Presidents undertaking state visits to Tanzania within a span of five years. President George W. Bush visited with us in 2008 while President Barack Obama came in 2013. President Bill Clinton made an official visit in 2000 but has been to Tanzania several times after living office to follow up projects supported by his Foundation. President Bush has been there twice since leaving office. Several senior officials of our two governments have exchanged visits which have helped to strengthen our bilateral relations.
Tanzania and the United States see eye to eye on a number of global and African issues and have supported each other at international and regional fora. The US has extended a big hand of support to Tanzania’s development endeavours which has made a huge difference towards improving the lives of our people and the development of the country at large. I have in mind the good work being done by the USAID covering many aspects of the socio-economic life of the people of Tanzania. Also, programmes like PEPFER, PMI, MCC, Feed the Future and Power Africa are making phenomenon contributions to the development of Tanzania and its people.
People to people relations are also strong and getting stronger with each passing day. I believe visits like mine to Seattle serves that purpose. Many private foundations, non – government organisations and individual Americans are working in Tanzania and have good relations with the people and the government of Tanzania. No wonder, some of you gathering here are among them.
Prominent citizens of Seattle, like Bill and Melinda Gates are exemplary in this regard. They have extended a lot of support in many areas of our development endeavours to buttress efforts of our government and the people of Tanzania. Their support has born positive outcomes. They are saving lives of women and children and improving the living standards of the people of Tanzania in many ways. Bill and Melinda are exceptional human beings indeed. Very wealthy people working with poor people, isn’t that amazing? Only people with big and warm hearts like them would do that. There are some rich people who blame the poor for their being poor. They are different. They empathise with them and go all the way to help them move up to the ladder. Isn’t that wonderful? Thank you so much. The people of Tanzania will always remain grateful to them and, always pray, to God Almighty, to bless them with long life, good health and even more prosperity.
Ladies and Gentlemen;
We need to do more to develop relations between US and Tanzania and between Tanzania and Seattle on the investment and trade fronts. Trade between the US and Tanzania is not worth talking about. You will agree with me that at 491 million US Dollars this is way too little. It shows that there is a lot of room to do better. The people of Tanzania like American products but they are not readily available. They also produce commodities which can be used in the US by industries and people. US investments in Tanzania stand at 4.5 billion US Dollars. This is nothing compared to what the US can do and is actually doing elsewhere in the world.
I am in Seattle today to encourage captains of industry and commerce to look at Tanzania as a destination of choice for investment and trade. For sure there are plenty of business opportunities to take advantage of and benefit from. I have brought with me responsible officials to brief Seattle businessmen on what Tanzania has to offer. Let me say generally that, opportunities abound in a wide range of sectors such as oil and gas, mining, agriculture, and agribusiness, infrastructure, manufacturing, tourism, housing, ICT and several others.
Oil and gas
On oil and gas, Tanzania and Mozambique are the latest addition to the list of global sources of natural gas. The first discovery in the deep sea started in 2010 and has never stopped ever since. So far proven deposits stand at 55 tcf. It is estimated that Tanzania has a potential of up to 200 tcf. The search for petroleum continues, but we have not been lucky yet. Indeed, exploration for oil and gas is ongoing in several blocks licensed to global companies including US companies. The fourth bidding round has just ended, but there are still a number of onshore and offshore blocks available. Not long from now, gas-based downstream activities are expected to commence, thus opening new investment opportunities. We invite interested Seattle companies to come and invest in these and other gas related activities and services.
Agriculture
There are abundant opportunities in agriculture. The country has 44 million hectares (110 million acres) of arable land of which only 25 percent is currently being utilised. The remaining 75 percent represents the potential that is yet to be exploited. Tanzania’s climatic conditions are good for all types of crops to grow including tropical and temperate crops. Rainfall is good in many parts of the country, although of recent because of the effects of climate change, rainfall reliability has become a challenge. Nonetheless, water for irrigation is available in rivers, lakes and underground. Fertile land is available throughout the country.
There are prospects in the other aspects of the agriculture value chain. I have in mind things like supply of agricultural machinery, equipment and, inputs to farmers. They need seeds, fertilizers, pesticides, herbicides, financial services, storage and marketing of their produce. There are opportunity in agro-processing and agribusiness in general. The prospects are enormous because of the ongoing transformation and modernization of smallholder farmers. There are also ample opportunities in the livestock sector as well. There is plenty of land to establish cattle ranches for beef and dairy cattle and for investing in the entire meat and milk value chain.
Energy
With only 36 percent of the population having access to electricity investment opportunities are enormous in the electricity subsector. Fortunately, Tanzania has a big potential for increasing power generation from the various sources. These include hydro, natural gas, coal, wind, solar, geothermal, bio-fuel and biomass. Work has started in earnest on reforming the power sector to unlock the present bottlenecks and give the private sector greater role in generation, transmission and distribution. This will broaden the scope of investment opportunities. Tanzania has the potential to become a power exporter in our region. Indeed, the market does exist in the East and Southern Africa regions. Those who are interested are welcome to do business with us in the power sector.
Tourism
Tourism is another sector that offers plenty of investment opportunities. It is a fast growing sector in the country. At the moment only 1.1 million tourists visit Tanzania every year. This is not much comparing to the existing potential in terms of tourist attractions: wildlife, the spice Island of Zanzibar, historic and scenic sights. The United States is an important tourist source market but I believe there can be more tourists than the current 50,000 to 70,000. I believe this number can increase ten-fold. However, we must invest more in tourism infrastructure and requisite services.
We must build more hotels, and improve services. Encourage more long haul flights to Tanzania from major tourist source markets. These are opportunity in tour operator’s business as we strive to improve their services and expand other tourism related businesses in the entire tourism value chain. The prospects in tourism and the hospitality industry as a whole are immense. I would like to use this opportunity to invite US companies to come and partner with us to develop the tourism industry in Tanzania.
Mining
There are also plenty of opportunities for investments in mining. Tanzania is blessed to have plenty of mineral resources. Some of the minerals exist in large quantities. Fortunately, also many are yet to be exploited and for those being exploited not all reserves have been depleted. Tanzania has gold, silver, copper, platinum, uranium, nickel, cobalt, kaolin, phosphates, soda ash, coal and iron ore. There are also plenty of gemstones including the rare blue stone found in Tanzania only called Tanzanite. The other good thing about mining is that the fiscal regime is like the ones you will find anywhere in the world. Investing in Tanzania is equally competitive. The responsible officials will elaborate better on these important issues.
Manufacturing
Investment opportunities in manufacturing are boundless. Tanzania has a huge raw material base from agriculture, mining, forestry, fishing and other natural resources. As a result one can establish industries to produce products from them. Moreover, industrialization is the next big thing in Tanzania’s development strategy. Also it is an important pillar of our economic reform agenda. The Tanzania Investment Centre is under specific instructions to promote investment in manufacturing. The Export Processing Zones Authority was established to drive the industrialization agenda forward. Tanzania intends to become a manufacturing and a service hub for the region to take advantage of its geographical location. Also, because of our membership of the East African Community and the Southern African Development Community when one invests in Tanzania he gets access to a market of about 300 million people. I know investors from the US can be strong partners in the manufacturing sector. I therefore, invite you to come and make full use of these opportunities which are backed with good incentives.
Service Sectors
Service sectors, in Tanzania, are growing at a very fast pace. Apart from tourism, which I have already mentioned, there are also telecommunications, banking, insurance, ICT and trade facilitation services. We welcome you to look at these opportunities and invest. They represent high paying investment opportunities where quick returns are guaranteed.
Ports and Railways
Infrastructure development is a major preoccupation of my administration and is a top priority in our economic reform agenda. In this regard, we have targeted roads, sea ports, airports, railways, power, telecommunication and water supply. So far so good. We have been doing a lot to develop these important elements of Tanzania’s infrastructure. The outcomes are visible. However, much more needs to be done and we invite the US private sector to come and join hands with us. One can come alone or in partnership with the government or with Tanzania’s private sector players. With regard to partnership, with government, there is a Public Private Partnership Law which governs such partnership. We welcome investors to access and reap the benefits it offers.
Conducive Business Environment
I spoke at length about why Seattle business people should consider Tanzania as a business destination of choice in relation to the abundant opportunities available. Let me now speak about other important things. Tanzania has a business friendly environment. We pursue sound economic policies which have engendered strong macro-economic performance. There are good incentives for investors. Investments are guaranteed by law against expropriation or nationalisation and investors are allowed to repatriate profits and dividends. We are members of MIGA and the International Centre for Settlement of Investment Disputes which further assures the investor recourse to justice in time of need. There is a sizeable skilled labour force and a growing middle class. There is political stability, democratic governance, rule of law, respect for human right and unrelenting fight against corruption. These latter attributes enhances the climate for doing business.
I, therefore, welcome you to take a serious look at Tanzania’ potentials and please come and visit with us as tourist, philanthropists and investors. The Executive Director of Tanzania Investment Centre (TIC), Director General of EPZA, the Director General of Tanzania National Parks, and the Director General of the Ngorongoro Conservative Area and the Executive Secretary of the Tanzania Private Sector Foundation. If you need any detailed account on any areas of opportunity, please make full use of them. Come One, Come All. Tanzania is ready to do business with you.
I thank you for your kind attention!

- Mar 30, 2015
KEYNOTE ADDRESS BY H.E. DR. JAKAYA MRISHO KIKWETE, PRESIDENT OF THE UNITED REPUBLIC OF TANZANIA TO THE UNITED NATIONS ECONOMIC AND SOCIAL COUNCIL, 30TH MARCH,...
Soma zaidiHotuba
Your Excellency, Mr. Stefan Lofven, Prime Minister of Sweden;
Your Excellency Mr. Peny Gladstone Christie, Prime Minister, The Commonwealth of Bahamas and Chair of CARICOM;
Your Excellency, Ambassador Vladimir Drobnjak, Vice President of ECOSOC and Chair of ECOSOC 2015 Integration segment;
Your Excellency Mr. Sam Kahamba Kutesa, President of the 69th Session of the General Assembly;
Your Excellency Mr. Jan Ealiasson, Deputy Secretary General of the United Nations;
Mr. Sharan Burrow, General Secretary, International Trade Union Conference (ITUC)
Mr. Daniel Funes de Rioja, President, International Organization of Employers (IOE);
Ladies and Gentlemen;
I thank you Mr. Vice President for the invitation and for associating me with the 2015 ECOSOC Integration Segment. I find the theme “Achieving sustainable development through employment creation and decent work” to be very opportune. Indeed, these are core issues for ensuring meaningful human development, prosperity, security and social stability within nations and in the world at large.
Mr. President;
I was happy to learn that, these important issues are now getting serious attention. I am told the Open Working Group (OWG) on Sustainable Development Goals, has included decent work and employment creation to be among the 17 goals of Sustainable Development. In the African Union’s Transformative Agenda 2063, African countries have been directed to pursue sound programmes that will create shared growth, decent jobs and economic opportunities for all.
In the Common African Position (CAP) on Post 2015 Development Agenda adopted by the Assembly of Heads of State and Government of the African Union in January, 2014, these issues were also underscored.
The Nexus Between Sustainable Development
Employment, Creation and Decent Work
Your Excellencies and Distinguished Delegates;
As we meet here today, there are, globally, 201 million people unemployed and the number is expected to increase by 80 million in the coming 4 years. This means, there is need to create additional 280 million jobs by 2019 to cater for the new entrants in the labour market. Also, we must remember that, almost half of the world’s employed people are still working in vulnerable conditions, with no guaranteed access to decent work and social protection. Unfortunately, women are the majority of such people. This is not acceptable, we must find ways of ensuring that work everywhere is decent and there is social protection.
The situation in Africa is worrisome and calls for even urgent and special attention. Statistics tell us that African countries created 37 million jobs only, over the last decade. Out of these jobs only 28 percent were qualified to be called decent jobs. At the same time, it is estimated that there are 122 million new entrants in the labour market annually in Africa. This is scaring when one considers the fact that almost 200 million people in Africa fall within the age of 15 and 24 years. It is estimated the number will double by 2045.
This means, therefore, that there will be too many unemployed people in Africa, the majority of whom will be young men and women. This is both an opportunity and a challenge. It is an opportunity in the sense that when an investor looks for employees they will be readily available provided they meet the skills he needs. But, it become a challenge if jobs cannot be found and these huge armies of unemployed youths who increase in numbers every other year, could becomes a threat to social stability and to security of the country. Some may indulge in criminal activities and cause social and security problems. Some may be recruited by bad people with ill intentions and become disruptive elements in society, nations or the world. Rebellions and terrorist groups fill their ranks and thrive from unemployed youths.
It is important, therefore that, job creation becomes a critical component of the development agenda, plans and programmes of all nations. Of course, jobs are created best when economies are growing. As such putting in place sound economic policies which will engender growth of the economy is a matter of essence. Also, it is important to note that, growth takes place where there is investment. Therefore, creating an enabling environment to attract investors to come and invest is what will actually create and deliver jobs. So developing nations, must strive to have sound economic policies as well as attractive investment climate.
The Africa Dilemma
Your Excellencies and Distinguished Delegates;
Many African countries, including mine, have registered good economic performance over the last two to three decades. Today, more than 10 African countries enjoy growth rates averaging 5 – 6 percent which is higher than the global average. Africa’s collective GDP is estimated to hit 2.6 trillion US Dollars in the next five years, making our continent one of (if not) the world’s fastest growing economic regions. However, beneath this success story lies the painful reality of high unemployment and poor working conditions in the few jobs available mostly found in the informal sector.
The truth of the matter is, the number of young men and women who enter the job market are far more than the jobs being created. I hope at this meeting we will share ideas about how African nations can tackle this problem and get advice about what we should do to attract more investments.
I would also appreciate advice and possible support about ways of assisting our young people with self employment. How to assist them to start and run a business and how to source capital. Honestly, we need special programmes and projects to address this urgent matter. Governments must play a role as well as development partners, the private sector and other interested associations. Support to programmes on self employment will surely make a difference. It makes economic and social sense. We must know that the problem of unemployment can destabilise or even topple good governments. Appropriate action in this regard is a matter of utmost agency.
Excellencies;
Much as we all agree on the need and importance of achieving sustainable development through employment creation and decent work, we must not lose sight of the realities of the world we live in. I say so, because countries on this planet are at different levels of development as a result they have different capabilities to deal with these overarching challenges of our time.
While to some countries and regions the focus is on making the available jobs decent and creating more decent jobs, we in Africa are simply struggling to create jobs first and foremost. The issue of the jobs being decent comes later. The idea here is first keep the stomach of hungry men full before talking about balanced diet. Ideally the two should be done simultaneously because jobs being decent is just as important. Decency of jobs should not be compromised. There should be clear standards and regulations which must be strictly respected. Where jobs were created first before decency being observed, it should not be allowed to remain that way. The regulators must do their job to ensure rules are followed to the letter and spirit.
Another challenge we have to contend with is that of striking the proper balance between preserving the environment on one side and promoting growth and creating jobs to meet urgent problem of unemployment on the other. This is an African and a global dilemma that needs to be addressed.
Excellencies;
It is evident that, at the current state of development, many of our countries in Africa will not deliver adequately on sustainable development through job creation and decent work. They are faced with a plethora of other challenges as such they have compelling limitations and handicaps. Mind you, Africa is home to 34 of the Lest Developed Countries in the world. African nations must, therefore, be assisted if they are to keep pace and catch up on our common goal of making extreme poverty history by 2030.
Excellencies;
Africa has demonstrated, strong desire and commitment to change its course for the better. Most African nations have undertaken socio-economic reforms which have worked well so far. On the economic front for example, pursuit of sound macro-economic policies has been responsible for the strong economic performance which Africa is being applauded for. We are, indeed, witnesses to better economic management, high economic growth rates, visible progress in the social-economic life of nations, and more people are being lifted out of poverty. However, the pace is not good enough and not deep enough. Rest assured that, we in Africa, would like to do better, faster, deeper and broader had it not been for our underdevelopment.
Africa should therefore, be assisted in the implementation of programmes and projects which will promote socio-economic growth, create jobs, increase people’s incomes, eradicate poverty and enable people to live a decent life. I believe this is the right and best thing to do by the developed countries. The waves of boat people trying to enter Europe will not end as long as long poverty and unemployment persists unabated. As long as pasture is brown in Africa and green in Europe the flow won’t stop. Help make the pasture in Africa green.
Excellencies, Ladies and Gentlemen;
Fortunately, there is, also, demonstrable progress on the governance side in Africa. There is marked improvement on the political, ethical, democracy and human rights fronts. Of course, the rate of progress varies from one country to another, but the common denominator is that things are happening for the better and steady progress is being registered in all African nations.
This is why today, we talk about Africa rising. Indeed, the continent is on the ascent. If the social, political and economic gains are sustained for another two to three decades, most of the LDCs in Africa if not all, will become middle income countries. The current lower middle income countries will become high middle income countries or be on the threshold of graduating into developed country status. Some may even become developed economies.
Tanzania’s Experience and Contribution
Your Excellencies and Distinguished Delegates;
We in Tanzania too, have set our sights on becoming a middle income country by the year 2025. This is the overarching objective of the Tanzania Development Vision 2025 launched in the year 2000. In 2010 we conceived the 15 year Long Term Perspective Plan which is divided into three medium term plans of five years each. The purpose of doing so was to guide the implementation of the objectives of the Vision in a structured manner for the remaining 15 years.
The Vision is informed and cognisant of the need for the economy to grow at a fast pace, develop human capital, increase people’s access to basic social and economic services, reduce income poverty and create a conducive environment for growth of the productive and service sectors. Also, sound environmental management policies and practices have been emphasized. Good governance, democracy, human rights and rule of law have been underscored in the Vision as well.
The implementation of the Vision and the First Five Year Development Plan is going on well and the results are encouraging. Of course, our inability to mobilise all the financial resources required to implement the various programmes and projects has been a serious encumbrance. Had we been able to mobilise all the requisite resources, I believe, Tanzania would have been better off than what we are todate.
Excellencies, Ladies and Gentlemen;
These challenges notwithstanding, significant progress has been made so far. Marco-economic indicators are on good stead. Average GDP growth has been at 7 percent for the last decade and a half. GDP per capita has increased from US Dollars 375 in 2005 to US Dollars 695 in 2013 (base year 2001). However, with 2007 as the base year GDP per capita in 2013 was US Dollars 948) which comes close to the threshold of US Dollars 1,045 that defines a middle income country. The number of people who live below the poverty line has been decreasing steadily but not at the pace I would have desired. For example, in 2000 they were 35.7 percent, 33.7 percent in 2007 and decreased further down to 28.2 percent in 2012.
We scaled up on the availability of basic social and economic services to our people. Today more Tanzanians have access to education, health care, electricity, water supply, roads, telecommunication, financial services etc. More roads are paved, these days than ever before to the extent that Tanzanians can get to any place in the country on the same day. In the past, it had to take not less than two days or more.
More young men and women have access to education from kindergarten to university. Primary school enrolment is at 98 percent and all students who pass primary school leaving examination get a place in secondary school. Between 2005 – 2014 there were 4,576 secondary schools compared to 531 that were there in 2005. The student population has increased from 524,325 in 2005 to 1,804,056 in 2014. The number of vocational training institutions has increased from 184 in 2005 to 744 in 2014 and so has the number of students getting skills training at these institutions. With regard to university education the number of students increased from 40,719 in 2005 to 200,986 todate.
We have done similar expansion with regard to health care. We have built more dispensaries, health centres and hospitals. As a result more people have access to better health services and we are witnessing reduction in numbers of people who contract and die of diseases which used to kill a lot of people. I have in mind diseases like malaria, HIV, TB and others. It is also the case with child mortality and maternal mortality although we need to do more on the latter. As a result of all these achievements on the health front life expectancy is on the increase. It is now 61 years compared to 47 two decade ago.
Transforming the Rural Economy
Your Excellencies and Distinguished Delegates;
In our quest to reduce the number of people who live below the poverty line, we decided to give special attention to agricultural reform and rural transformation. We decided to do this because the majority of the poor people live in rural areas and depend on agriculture for their livelihood. Therefore, increased productivity and production meant food security and increased incomes to farmers thus lifting many out of poverty. Improvement in the availability of basic services improves their living conditions and productive capacity.
Three initiatives are worth mentioning in this regard. The Agricultural Sector Development Programme, Kilimo Kwanza and the Southern Agriculture Growth Corridor of Tanzania. There are positive changes happening in our agriculture and rural economy. For three years now, Tanzania has enjoyed surplus food production. The challenge now is about how to increase storage and get assured market for the surplus produce. We are working on resolving those challenges. I believe current plans to establish a Commodity Exchange will help address them.
Excellencies, Ladies and Gentlemen;
These measures and achievements notwithstanding, I acknowledge much more needs to be done to see increased agricultural productivity and production through modernization of crop and animal husbandry and improving the availability of requisite support services to farmers including financial services. Implementation of the three initiatives and the establishment of the agricultural development bank will help Tanzania’s agriculture.
Excellencies;
The other important programme being undertaken by the government which will help rural transformation is rural electrification. So far 3,836 villages have been covered and the plan is to reach another 1,500 villages by June, 2015. This means, 43 percent of the 12,423 villages will be covered. Rural electrification will be a significant step in rural transformation in view of what electricity can do as a catalyst of development.
Overall, we have made encouraging progress with regard to electricity coverage in the country. In 2005 only 10 percent Tanzanians had access to electricity, in 2014 that number had increased to 36 percent compared to 32 percent for Sub-Saharan Africa. This is not bad at all but at the African and global level our coverage is too little. First we want to catch up and surpass the average Africa coverage of 43 percent. That is why electricity development is a priority programme in my government’s development agenda.
We are also taking action to expand and advance manufacturing, mining tourism, ICT, trade and other services for the sake of promoting growth and creating jobs. So far, so good and we are seeing a lot of jobs being created in these sectors.
Social Protection
Your Excellencies and Distinguished Delegation;
When we talk about sustainable development, job creation and decent work, we should also discuss social protection. In Africa, Tanzania included, social protection schemes largely cater for those who work in formal employment. In 2012 we undertook reform of the social security system to include the hardworking people in the informal sector like farmers, traders and others. It is beginning to show positive results. With the total working population estimated to be 22.5 million, and employment in the formal sector at 1.55 million, the total membership of social security schemes was at 1.95 million in 2013/2014. This means, about 400,000 new entrants have been enrolled in the Social Security Scheme from the informal sector in just two years. Therefore, we can do better if we stay the course of encouraging people in the informal sector to join social security schemes. I am confident we will succeed in this ambitious goal as well.
Informal Economy
Your Excellencies;
Ladies and Gentlemen;
The informal sector is huge and remains a major source of employment in Africa and in Tanzania. It accounts for 70 percent of employment in Sub-Saharan Africa, 80 percent of the total labour force and contributes 55 percent of the GDP. In Tanzania the contribution of the informal sector has been decreasing from 43.6 percent of the GDP in 2005 to 39.7 percent in 2010. In 2014, its contribution decreased further to 30 percent of the GDP.
It is in the best interest of the national economies in Africa and those engaged in the informal economy to have the informal sector formalised. It makes pursuit of decent work easy. It also broadens the tax base. Improvement in legal regime governing business which makes it possible for financial institutions to lend money to small and medium enterprises in the informal sector is one way of doing it. The expansion of financial services through mobile phone technology is another. It has not only promoted financial inclusion, in an unprecedented way, but also has encouraged formalization of informal business.
Excellencies;
Let me mention here that through mobile phone financial services, the number of people with access to financial services in Tanzania has increased from 17 percent in year 2012 to 43 percent in year 2013. Our financial inclusion target is to reach 50 percent by 2016. I believe we will attain it before that time. By 2014, about 10 million people were using electronic payments with transaction having reached a phenomenon one billion US Dollars per month. This is a tremendous achievement.
Conclusion
Your Excellencies and Distinguished Delegates;
I have tried to share my thoughts and our experience on job creation, decent work as means to achieve sustainable development. I believe it is achievable. If there is cooperation among all the players both in the public and private sector, together we can deliver on sustainable development, job creation and decent work. We have seen the underlying potential to achieve more if we invest more and wisely.
Let us rise to the moment.
I thank you all for listening.