Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwa pamoja na Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Mambo ya Nje wa Umoja wa Falme za Kiarabu (UAE), Mhe. Abdullah Bin Zayed Al Nahyan, wakishuhudia utiaji saini wa Hati ya Makubaliano baina ya Shirikisho la Vyama vya Biashara na Viwanda vya UAE na Barazala la Taifa la Biashara kuhusu uanzishwaji wa Baraza la Pamoja la Biashara kati ya Umoja wa Falme za Kiarabu na Tanzania tarehe 05 Mei, 2025 Ikulu jijini Dar es Salaam.