Tanzania emblem
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Tovuti Rasmi ya Rais

Habari

Uteuzi


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli amemteua Rais Mstaafu wa awamu ya nne wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete kuwa Mkuu wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (Chancellor of the University of Dar es salaam).

Rais Mstaafu Kikwete anachukua nafasi hiyo, iliyoachwa wazi na Marehemu Balozi Fulgence Kazaura aliyefariki dunia Februari, 2014.

Taarifa iliyotolewa na Katibu Mkuu Kiongozi Balozi Ombeni Sefue Ikulu Jijini    Dar es Salaam, imeeleza kuwa uteuzi huo umeanza tarehe 17 Januari, 2016.

 

Gerson Msigwa

Kaimu Mkurugenzi wa Mawasiliano, IKULU.

Dar es salaam.

21 Januari, 2016.