Tanzania emblem
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Tovuti Rasmi ya Rais

Habari

UTEUZI


Rais Jakaya Mrisho Kikwete amepokea kwa furaha na unyenyekevu uteuzi iliofanywa na Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa (UN) Bw. Ban Ki Moon kuwa Mwenyekiti wa Jopo la Ngazi ya Juu kuhusu Mwitikio wa Kimataifa wa Majanga ya Afya (High - Level Panel on Global Responses to Health Crises) .

"Ni majukumu makubwa na yenye changamoto  nyingi lakini dunia inahitaji tuwe na mikakati katika masula haya ambayo ni muhimu kwa maisha ya binadamu, hivyo hatuna budi kufanya kazi hii Kama mchango wetu kwa ajili ya maisha  ya wanadamu na dunia kwa ujumla". Rais amesema mara baada ya kutolewa kwa Tangazo hilo tarehe 2 April, 2015.

Wengine walioteuliwa katika Jopo hili ni Bw. Delos Luiz Nunes Amorim wa Brazil, Bi. Micheline Calmy-Rey wa Switzerland , Bw. Marty Natalegawa wa Indonesia, Bi. Joy Phumaphi wa Botswana na Bw. Rajiv Shah wa Marekani.

Jopo linatarajiwa kufanya kikao chake cha kwanza mapema Mwezi Mei, 2015 na linatarajiwa kuwasilisha taarifa yake kwa Katibu Mkuu wa UN mwishoni mwa Mwezi Disemba, 2015.

.........Mwisho……….

Imetolewa na;

Premi Kibanga,
Mwandishi wa Habari wa Rais Msaidizi,
Seattle - Marekani
3 Aprili, 2015