Habari
MHE. RAIS SAMIA AWAAPISHA MAKATIBU TAWALA WA MIKOA

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan amewaapisha Makatibu Tawala wa Mikoa tarehe 02 Juni, 2021. Katika hafla hiyo pia amemuapisha Kapteni Mstaafu George Huruma Mkuchika kuwa Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Ikulu (Kazi Maalum). hafla ya kuwaapisha viongozi hao ilifanyika Ikulu Chamwino, Jijini Dodoma.