Habari
MH. RAIS SAMIA SULUHU HASSAN AWASILI JIJINI DODOMA TAREHE 29 JUNI, 2021 AKITOKEA JIJINI DAR ES SALAAM

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan awasili Jijini Dodoma tarehe 29 Juni, 2021 akitokea Jijini Dar es Salaam ambapo anatarajia kufanya mazungumzo na Mkurugenzi wa Idara ya Afrika Bw.Abebe Aemro Selassie kutoka Shirika la Fedha Duniani (IMF) kuhusu masuala mbalimbali ikiwa ni pamoja na jinsi Shirika hilo litakavyosaidia Tanzania kukabiliana na ugonjwa wa Corona.