Tanzania emblem
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Tovuti Rasmi ya Rais

Wasifu

Mr. BENJAMIN WILLIAM MKAPA
Mr. BENJAMIN WILLIAM MKAPA
Rais Mstaafu wa Awamu ya Tatu

Hayati Benjamin William Mkapa aliongoza awamu ya tatu na ni Rais wa kwanza aliyechaguliwa katika uchaguzi ulioshirikisha vyama  vingi vya siasa tangu mfumo huo uliporejeshwa mwaka 1992. Aliingia rasmi madarakani Oktoba 1995. Mheshimiwa Mkapa alizaliwa Masasi, Mkoani Mtwara tarehe 12 Novemba, 1938. 

 

Kazi

 Mwaka 1962 aliajiriwa kama Ofisa Tawala na hatimaye Ofisa Mambo ya Nje. Kati ya mwaka 1966 na 1976 alifanya kazi katika Taasisi mbalimbali za umma. Mwaka 1976 hadi mwaka Septemba, 1995 alishika nyadhifa zifuatazo: Balozi wa Tanzania nchini Nigeria (1976; Mbunge wa Nanyumbu na Waziri wa Mambo ya Nje (1977 – 1980); Waziri wa Habari na Utamaduni (1980 – 1982); Balozi wa Tanzania nchini Canada (1984 – 1990); Waziri wa Habari na Utangazaji (1990); Waziri wa Sayansi, Teknolojia na Elimu ya Juu (1992 – Septemba 1995).

 

Elimu

Alipata elimu ya msingi na sekondari kati ya mwaka 1945 – 1956 katika shule za Lupaso, Ndanda, Kigonsera na Pugu.

Alipata shahada ya kwanza ya Lugha ya Kiingereza katika Chuo Kikuu cha Makerere, Uganda mwaka 1962, na shahada ya Uzamili ya  Masuala ya Kimataifa katika Chuo Kikuu cha Columbia, Marekani mwaka 1963

 

Nyadhifa nyengine

April 1962: Aliteuliwa Afisa Tawala Dodoma

April 1962: Afisa wa Wilaya

August 1962: Afisa Mambo ya Nje

May 1966:Mhariri Mtendaji, The Nationalist na Uhuru

April 1972: Mhariri Mtendaji, The Daily News

July 1974: Afisa Habari wa Rais

July 1976: Mhariri Mwanzilishi, Shirika la Habari Tanzania

October 1976: Balozi Nigeria

February 1977: Waziri wa Mambo ya Nje

November 1980: Waziri wa Habari na Utamaduni

April 1982: Balozi India

February 1983: Balozi Marekani

AprilL 1984: Waziri wa Mambo ya Nje

1990: Waziri wa Habari na Utangazaji

May 1992: Waziri wa Sayansi, Teknolojia na Elimu ya Juu

November 1995: Alichaguliwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania